Ikumbukwe ziara hii imefanyika wiki kadhaa baada ya Mwenyekiti wa Ccm taifa (Kikwete) na timu ya mawaziri kumaliza ziara yao hapa!
Wakati wa ziara ya Kiwete watu walisombwa kwa marori na kulazimisha shule kufunguliwa j,mos na j,pili ili kuongeza idadi kwenye mikutano.
Ziara ya Mbowe watu walikodi magari wenyewe kutoka vijijini mbali kufuata mikutano. Mkutano mmoja tu wa Karagwe taarifa niliyopewa na katibu wa jimbo hilo leo, ni kuwa watu waliosaini karatasi za maoni ya chama kuhusu katiba ni 5,811 kwenye mkutano mmoja.
Wanawake sasa wanakuja mstari wa mbele kwenye mabadiliko, nilishuhudia akina mama na wasichana wakianguka wakijaribu kuwagusa tu viongozi wakati wanaingia na kutoka kwenye mikutano. Kwenye mkutano wa Karagwe wasichana ndio waliongoza kwa kuvaa skafu na kofia za Chadema.
Misenyi watu walifunga bara bara ya Mtukula - Bukoba kwa masaa kadhaa kutokana na wingi wa watu. Lakini badala ya wasafiri kukasilika na wao walijiunga kusikiliza hotuba za viongozi!
Katika mkutano wa Kyerwa mama mmoja wa makamo aliangua kilio ndege ilipopaa huku akisema anaogopa wanaweza kupata ajari "Hawa watoto Mungu wangu sijui kama watazunguka nchi nzima na kuimaliza salama na hiyo ndege yao, tuwaombee sana" alisikika akisema mama huyo huku akitokwa na machozi.
Mikutano ilifanyika asubuhi au mchana, lakini watu walijaa huku wakichomwa na jua kwa muda mrefu. Wazee wengi walijitokeza kwenye hali kama hiyo na kusema kero zao wakiamini Chadema pekee ndiyo itawasemea kero zao.
Sijui hayo yote ni kwa nini, ni mpango wa Mungu? wananchi wamechoka utawala uliopo? ni mvuto wa viongozi wa Chadema? Hali hii itaendelea mpaka 2015? Kwa nini juhudi za kuichafua Chadema zinashindwa na watu ndo wanaongeza mapenzi kwake?