Siungi mkono mgomo wa madaktari...

Siungi mkono mgomo wa madaktari...

ULAANIWE WEWE NA FAMILIA YAKO!
Kuna umuhimu gani Daktari kuwepo kazini wakati hakuna facilities za kufanyia kazi? ata kama daktari atakuwepo kazini kama hakuna madawa na nyenzo za kufanyia kazi hao wagonjwa wataponaje? wameshatoa ufafanuzi kwamba si maslahi tu lakini mazingira ya kufanyia kazi lazima yaboreshwe ili tuweze kupata huduma bora!. HIVYO WEWE UMELAANIWA KWA KUTOYAJUA HAYO!
 
Wewe ni kuku mwoga
Sisi ni mwewe
Dua lako halitupati
Asilani twakwambia

Huna mbawa za kuruka
Miguu mizito kwa miolo
Kisu ni halali yako
Ewe wa kufugwa

Ubongo wako wa kuku
Macho yako 20/30
Mtama ulikuponza
Ukakubali kufugwa
jiande Sifulia lachemka
Misuli yako ifanywe supu

Umenona makalio
Wewe wadhani ni tunu
Fukuto walitamani
uonyeshwapo kisu macho pima
woga wa nini kuku?
Dezo inakuponza

Dua lako la kikuku
litmpataje Mwewe ngangari?






Wakuu JF.
Waweza kuwa mwepesi kushabikia mgomo wa madaktari kwa sababu kuu zifuatazo:

  1. Unaichukia serikali iliyoko madarakani, hivyo unashabikia mgomo wa madaktari kwa kuwa unahisi wanaishikisha adabu serikali hiyo.
  2. U mzima wa afya, wewe pamoja na familia yako yote hivyo kwa muda huu, huhitaji huduma yoyote kutoka kwa madaktari hawa wanaogoma.
  3. Una pesa za kutosha kwamba hata ukiumwa leo hii, unao uwezo wa kwenda kutibiwa Aga Khan, AAR, Regency etc bila bughudha wala shida yoyote.

Napenda niwakumbushe watanzania wenzangu kwamba maisha magumu kwa nchi hii hayapo kwa madaktari tu, nina uhakika yapo makundi ambayo yanamaisha magumu zaidi ya madaktari, wapo walimu, wapo polisi, wapo wakulima ambao ndio wengi zaidi ya wengine, na kubwa zaidi watanzania ambao hawana ajira/kazi maalum ni kundi kubwa zaidi ya makundi yote niliyotaja, na ndio wenye maisha magumu zaidi kuliko wengineo licha ya kwamba katika kundi hili pia wamo wasomi ambao wamemaliza kwenye vyuo vikuu lakini hawana hata uhakika wa mlo mmoja au pesa ya ku print CV.

Tuachane na ushabiki, roho ya mtu akishakufa hairudi hata kama hayo madai ya Madaktari yatatekelezwa, wananchi tusikubali wanasiasa watuingize kwenye siasa zao kwa kutumia mgomo wa madaktari, by the way I hate CCM kwa sababu ndio iliyotufikisha hapa tulipo kwa kushindwa ku plan vyema jinsi ya kulilea taifa la Tanzania na Watanzania, but kwa hili la Madaktari kugoma siungi mkono hata asilimia 1, hao akina Mzee Mwanakijiji et al wanaounga mkono madaktari kugoma yatupasa tutambue kwamba hawaishi Tanzania na hawajui shida wanazokutana watanzania wa kawaida kwa mgomo huu wa madaktari.

Nahitimisha kwa kulaani wote waliohusika kujaribu kumuua Dr. Ulimboka.

Na pia kama viongozi wetu wangekuwa na hekima za kutosha, wasingeruhusu kauli kama LIWALO NA LIWE kutoka vinywani mwaol.

God Bless Tanzania, God bless Tanzanians.
 
Upunguf wa dam au anemia na ukosef wa lishe au malnutrition ndo umesabisha sana kupungua kwa uwezo wa kufikiri miongon mwa watanzania weng,usitegemee aliyekutwa na matatizo hayo ktk ukuaji wake awe na uwezo mkubwa wa kufikiri! Sikutegemea kama naweza kuwasikia watu wanapinga mgomo wa madaktari kwa kuangalia sababu za kugoma.jaman ondoen woga madai ya madaktari ni ya msingi tusiingize siasa,hata mungu pia hapend mtu apate matatizo yanayosababishwa na uzembe.
 
wanagoma na mwisho wa mwezi wanaenda na ATM kudraw Bank fedha zetu walipa kodi huku wagonjwa wetu wanakufa hospitali. hii ni halali? kwanini waendelee kulipwa mwezi huu? kwanini serikali haigomi kuwalipa kwa kususa kwao? hawatendi haki hata kidogo.
 
[h=6]madaktari.
Washenzi kabisa.
Pengine hawana dini ni 'makafiri'.
Mmepewa fani muhimu sana kwa maisha yetu kama wanadamu.
Mnapogoma kwa sababu ya madai yenu kwa serikali, hamtutendei haki watanzania, hasa sisi wa kipato duni tunaojazana kwenye hospitali zenu zenye huduma mbofu mbofu.
Eti mnagoma kuishinikiza serikali, hao wakubwa waa swrikalini wana uwezo wa kutibiwa popote hata kama msingekupo ninyi.

Kuna wapumbavu wengine wanalishabikia hili suala kisiasa, acheni hizo.

Fikiria kama wewe ndo ungekuwa pale na mgonjwa wako mahututi halafu unambiwa kuna mgomo..

Uzalendo unahitajika!

Mbona enzi ya mwalimu hakukuwa upuuzi huu?

Eti migomo inatokea wakati huu ambao wenye taaluma hiyo tunashudia wakiishi maisha ya kifahari.[/h]
 
KWA HIYO UNAONA NI VYEMA WATANZANIA MASKINI WAFE KWA SABABU UMEDANGANYWA KWAMBA WANADAI MAZINGIRA BORA?

ULIFUATILIA MADAI YAO KWENYE KIKAO CHAO NA J.K

POLE SANA KAMA UNASHINDWA HATA KUFIKIRI NA KUJUA ATHARI ZA MGOMO HUU ZINAENDA KWA AKINA NANI.

Pole sana bwana kakulwa.

Acha uoga na uvivu wa kufikiri pamoja na ushabiki wa CCM; KamaSerikali haina hela inapata wapi za kuwalipa Wabunge na kujaza migari yao inayofanya kazi ya kutanua mjini mafuta? Wote tunalalamika rushwa mahospitali ya serikali kwa sababu maslahi ya madaktari ni finyu leo wanataka kuondokana na hii hali wewe unawaona wauaji? Kapime akile zako haziko sawa na U-TOP Thinker Fake wako
 
Kachangia kama mchangiaji yeyote yule.Ni haki yake ya kikatiba ya kutoa maoni na kusikilizwa,kama hujaona point wengine wameona.Labda wewe ni Dr.ndio maana una uchungu sana na yeye anaona wote sawa labda yupo katika kundi la tatu(unemployed).
 
Kila mtu analaumu serikali kwa kila kitu, kila mtu anataka malipo mazuri na makubwa, inapokuja wakati wa kulipa kodi kila mtu hayuko tayari kulipa kodi. Tunanyoshea mikono wengine eti ndo walipe.

Tunaitaji kuongelea mambo haya bila ushabiki na mind ya vyama.
 
Ulaaniwe wewe!!!
If you have nothing to write please dont write it here, thanks

Yaelekea wewe ni miongoni mwa mafisadi wachache mnaotafuna Nchi hii wenye uwezo wa Kwenda kutibiwa Nje ya Nchi
 
Wanadai mishahara mikubwa kuliko walimu, polisi, watumishi wengine wa umma kwakuwa wao ni bora sana!!

Hilo la mazingira danganya toto tu hata walipoenda kwa rais hawakulisema.

Acha kupotosha uma ww,ww unaona mazingira wanayofanyia kazi ni mazuri au unaongea tu?,ss ulitaka wawadaie na wengine,km wenyewe wameridhika je?..nao wachukue hatua kivyao
 
ni kweli wengi wanachuki na serikali na kugoma kwa madaktari wanaona ni kuishikisha adabu hiyo serikali,lakini si kweli wanaoshikishwa adabu ni sisi walalahoi.Si vema kushabikia ujinga huu watu wanakufa na kupata maumivu wewe unaona sawa.
 
thanx lord,ulimboka anaendelea vzr!God is in control!ndo maana jaribio la kutaka kumuua limeshindikana,shame on u,mlidhani kila mtu mwepesi,ulimboka aliaga kwao!
 
Huwezi kulaaniwa kama unaunga mkono mgomo ukiwa na valid reasons!
 
ni kweli wengi wanachuki na serikali na kugoma kwa madaktari wanaona ni kuishikisha adabu hiyo serikali,lakini si kweli wanaoshikishwa adabu ni sisi walalahoi.Si vema kushabikia ujinga huu watu wanakufa na kupata maumivu wewe unaona sawa.
Mlala hoi unatibiwa regency na Apollo? sema uko hapa unapalilia kitumbua chako kisiingie mchanga. Nenda kwenye hospitali ukutane na dawa za kutuliza maumivu badala ya kukutibu. Mlalahoi hajui hata keyboard inafananaje siyo wewe mkuu wangu. Acha kabisa, nimeshuhudia na naendelea kushuhudia kutoka kwa mke wangu alivyonahuruma hadi kamshahara kake kanaishia kusaidia wagonjwa ambao hawaewezi hata kununua sindano au wembe au pamba za kusafishia. Ni zaidi ya hayo unayofikiria mkuu.
 
laiti ungelijua wanachodai madaktari ungekuwa wa kwanza kuwaunga mkono
mojawapo la dai la madaktari. mazingira mazuri ya kazi na vitendea kazi vya kutosha ikiwa ni wagonjwa kutolala chini au wawiliwawili na kuwepo na dawa za kutosha.

tatizo tunaongozwa na roho za woga.


MAZINGIRA MAZURI ILI WAPELEKE DAWA KUUZA PRIVATE HOSPITAL NA KUFUNGUA HOSPTAL MPYA NA MADUKA YAO YA DAWA; KUMUONA SHILING 10000, DAWA UNANUNUA KWENYE DUKA LAKE. ANAPEWA COMMISSION REGENCY/HINDU MANDARI AKUPELEKE INDIA WKT ANAJUA UTAKUFA ILI APATE 10% NA KUKUONGEZEA GHARAMA BURE AKIJUA MAKUSUDI UTAPONA ; HII WAANZISHE FANI YA MEDICAL BUSSINESS ADMN au MSYRGICAL WITH ACCOUNTANCY; WAPO KIBIASHARA ZAIDI
 
Ulaaniwe kwanza wewe mwenye akili FINYU kama funza, Madaktari waendelee na mgomo hadi suruhu ipatikane.
 
Back
Top Bottom