tz2015
JF-Expert Member
- Jun 23, 2014
- 982
- 447
Ukiunganisha hizo semi za Sitta hapo kwenye red utagundua,Makonda hayupo peke yake,Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.
Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.
Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.
Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.
Nyuma yake ipo nguvu kubwa kama iliyokuwa nyuma ya Nape wakati wa kampeni ya kuvua gamba,
Kinacholeta matumaini ni kuwa Kampeni ya nape iligonga mwamba na hii itagonga mwamba pia, maana msimamizi au mchochezi ni mmoja.Na hapa Warioba atashinda Damu ya Sengondo imetosha hatuhitaji kuona damu nyingine ya mjumbe wa tume ya katiba ikimwagwa juu ya ardhi ya Tz maana ni laana kwa nchi.