Waliyofanya fujo si wanachi ni vijana wanotumwa na mafisadi,kwanini ilipotajwa kuwa na Akunti nje ndo mambo yalibadirika.kama wangeona hoja za Mzee Warioba ni za upotoshaji na wao wangetafuta jukwaa lakupinga yote aliyo yafafanua.Kumvunjia heshima Mzee wetu ni laana itakayopiga wengi.Tunataka Raisi azungumze kuhusu hili.
Daniel alikuwa kiongozi wa kidini na mwanasiasa, Jesus alikuwa nabii na mkosoaji mkuu wa serikali hata wakati mwingine alimwita mfalme "MBWEHA", yohana alifika mahali akamkosoa mfalme kuoa mke wa kaka yake.Laana gani ya viongozi wa dini hivi viongozi wa dini wakizungumzia suala la kisiasa linatokana na maandiko matakatifu? Wewe ndio uliochanganyikiwa kwa maana hujui yapi ya mungu na yapi ya kidunia.tena unatisha kwa sababu kiongozi wa dini anaweza kutembea na mkeo ukaogopa kumkemea kwa sababu unaogopa laana hahahahaha
sawa umeeleweka Paulo Makonda, ila laana ya Maaskofu inakusubiri, Paulo mwenyewe alitubu na kuongoka, vipi wewe?Kilichomkuta jana Warioba ni msiba wa kujitakia
Maneno mengiiiii, pointi hakuna hata moja kwa uliyo ya andika.
ukishangaa ya Musa utayaona ya huyu Firauni!!!!Huyu sista ni hajielewi, hakuna hata mmoja aliyewakataza kuandaa midahalo kwa ajili ya katiba yao ya CCM, na wao waende wakaandae hiyo midahalo ya kwao, aache kuwafanya watanzania mbumbuzi
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.
Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.
Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.
Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.
Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.