Sitta: Warioba amejitakia mwenyewe

Sitta: Warioba amejitakia mwenyewe

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.

Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.

Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.

Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.

Dah kazi ipo. Mungu wetu ni mwaminifu sana halali. Kama hajatoa huku wakati wa mvua atatoa wakati wa jua, kama cyo masika basi wakati wa kiangazi. Tusubiri tu kipindi kitafika. Kama wanaweza kuutendea mti ulio mbichi namna hii; je kwa mti mkavy itakuwaje? Mjomba Six usihukumu maana hao hao waliomsubu Warioba ndiyo haohao watakao kuchinja muda ukifika. Yetu ni macho. Mungu ibariki Tanzania
 
Kwa maelezo yake Sitta, inawezekana kabisa kuwa ndiye aliyemtuma, kugharamia na kuratibu mpango wa Makonda!

hilo sio la kuuliza makonda baba yake mlezi ni samweli sita ninamfahamu in and out so yeye ndio aliyemtuma
 
Membe amemuhaidi 6 uwaziri mkuu, uroho wa madaraka wafunika hekima zake
 
Mheshimiwa Sitta yuko sahihi kabisa nami namuunga mkono kwa asilimia mia...Warioba anatakiwa awaachie watanzania wataamua wenyewe lakini huku kuhangaika kwake na kujidai yeye ndiye aliyekaa na Mwalimu kuliko watanzania wote kutamuumbua siku si nyingi

Hivi nieleze kuna tofauti gani na wana ccm mbalimbali ambao kila kukicha wanapanda majukwaani na kuwaambia wananchi waikubali katiba iliyopendekweza kwa sababu ni 'nzuri'? Kwani Warioba, au mtu mwingine yeyote yule haruhusiwi kusema kuwa katiba iliyopendekezwa si nzuri?

Jambo ambalo limejitokeza ni kwamba bado katiba iliyopendekezwa haijatolewa kwa wananchi. Badala yake sisi wananchi tunashinikizwa tuikubali hiyo katiba. Ni vyema basi, wakajitokeza watu wenye kuielewa katiba, pamoja na mchakato wake wote, kuelimisha wananchi. Si vyema kuwaburuza wananchi wakubali kitu ambacho hawakielewi vizuri, hasa katiba ambayo itaathiri maisha yao kwa miaka mingi ijayo.
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.

Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.

Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.

Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.

wakati.mwingine.kunyamaza ni hekima kuliko kuongea.sita sijui yamemkuta nini au ni mgonjwa? maana anajiporomosha kutoka kuheshimiwa kwa kasi kubwa sana.kwa kutumia vibaya ulimi.
 
Sitta kwanza aombe msamaha kwa kuwakashifu maaskofu ndipo azungumzie ya Mheshimiwa Warioba ambaye ni Makamu wa Raisi na Waziri Mkuu mstaafu. Sitta akumbuke kuwa alijadili rasimu mwenyewe, akaipigia kura mwenyewe, akahesabu kura mwenyewe, akatangaza matokeo mwenyewe, akajipongeza mwenyewe, akajitekenya mwenyewe, akacheka mwenyewe na akaserebuka kwenye ukumbi wa bunge mwenyewe. Kwa hiyo hatuiamini hiyo katiba pendekezwa kwani haina misingi ya maoni ya wananchi. Mhe Warioba ana haki ya kutufafanulia tofauti kati ya rasimu na katiba pendekezwa ya CCM.
 
Laana gani ya viongozi wa dini hivi viongozi wa dini wakizungumzia suala la kisiasa linatokana na maandiko matakatifu? Wewe ndio uliochanganyikiwa kwa maana hujui yapi ya mungu na yapi ya kidunia.tena unatisha kwa sababu kiongozi wa dini anaweza kutembea na mkeo ukaogopa kumkemea kwa sababu unaogopa laana hahahahaha


Waambie WATUMBAFU hawa! WAUAJI WAKIJIVIKA KANZU NA VIBARAGHASHIA WAKAJIITA MASHEHE WAO WATAWAKUBALI PIA!

 
Kumbe mtu akiongea kitu usichokipenda ukamvamia hapohapo na kumpiga ni akili na kujitambua kwa mtanzania wa sasa! Basi yaliyotokea jana ni kionjo tu tusubiri movie lenyewe
 
Hivi nieleze kuna tofauti gani na wana ccm mbalimbali ambao kila kukicha wanapanda majukwaani na kuwaambia wananchi waikubali katiba iliyopendekweza kwa sababu ni 'nzuri'? Kwani Warioba, au mtu mwingine yeyote yule haruhusiwi kusema kuwa katiba iliyopendekezwa si nzuri?

Jambo ambalo limejitokeza ni kwamba bado katiba iliyopendekezwa haijatolewa kwa wananchi bado. Badala yake sisi wananchi tunashinikizwa tuikubali hiyo katiba. Ni vtema basi, wakajitokeza watu wenye kuielewa katiba, pamoja na mchakato wake wote, kuelimisha wananchi. Si vyema kuwaburuza wananchi wakubali kitu ambacho hawakielewi vizuri, hasa katiba ambayo itaathiri maisha yao kwa miaka mingi ijayo.


Kweli kabisa mkuu, lakini mzee Warioba aache kabisa, kama anavyowaambia wenzie, kujifichaficha nyuma ya MWALIMU!
Nani kawateua Warioba, na Butiku, kufanya kazi ya 'PRIESTHOOD IN MWALIMU NYERERE'S TEMPLE'? HAWAWEZI KABISA KUONGEA WAO KAMA WAO! KILA KITU MWALIMU MWALIMU MWALIMU!
WATU SASA TUNACHOKA KURUDISHWA NYUMA KIFIKRA NA KUGANDISHWA MIAKA YA SITINI NA SABINI! HEBU TUSONGE MBELE!
 
Kweli kabisa mkuu, lakini mzee Warioba aache kabisa, kama anavyowaambia wenzie, kujifichaficha nyuma ya MWALIMU!
Nani kawateua Warioba, na Butiku, kufanya kazi ya 'PRIESTHOOD IN MWALIMU NYERERE'S TEMPLE'? HAWAWEZI KABISA KUONGEA WAO KAMA WAO! KILA KITU MWALIMU MWALIMU MWALIMU!
WATU SASA TUNACHOKA KURUDISHWA NYUMA KIFIKRA NA KUGANDISHWA MIAKA YA SITINI NA SABINI! HEBU TUSONGE MBELE!

Kitu pekee unchotakiwa uelewe ni kwamba Waryoba ni Kiongozi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere hivyo anawajibu wa kuwakumbusha Watanzania Mazuri ya Nyerere kuliko taasisi yoyote ile.
 
Kumbe mtu akiongea kitu usichokipenda ukamvamia hapohapo na kumpiga ni akili na kujitambua kwa mtanzania wa sasa! Basi yaliyotokea jana ni kionjo tu tusubiri movie lenyewe


MSIPINDISHE UKWELI MAANA KILA MTU ALIONA!
Waliopigwa ni wachache waliokuwa na maoni mbadala kwenye 'concentration of Warioba fanatics'!
Waliopigwa ni wale wanaounga mkono katiba pendekezwa! Na, kuficha maovu, jamaa zetu 'wanaotoa habari bila upendeleo' waliamua kuzima kamera zao ili 'uhuni utendeke' nyuma ya mapazia.
ASIYETOA DEMOKRASIA NA ASIPEWE DEMOKRASIA, MAANA HERI LAWAMA KULIKO FEDHEHA!
 
Huyu Mzee ashachanganyikiwa kabisa, laana ya viongozi wa dini ishaanza kumvuruga

😂😂😂😂 we jamaaaa umechekesha


Kwa ujumla mzee Sitta ubongo wake kwa sasa umechakachuliwa 😕😕😕
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.

Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.

Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.

Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.

Waziri mzima wa JMT ana condone Mtanzania kufanyiwa FUJO! Tena mtanzania huyo wa calibre ya Warioba former PM of URT?!

Nimeamini nchi hii hatuna viongozi bali VIKARAGOSI fulani!
 
Kilichomkuta jana Warioba ni msiba wa kujitakia

Lizaboni ifikilie mara mbili hiyo kauli yako walio nyuma ya walioba ni wengi na wengine wapo ndani ya ccm sasa mnaharalisha zomea zomea katika kila mikutano yenu maccm mjipange vizuri hatutakubali kama watanzania wapenda amani jaji walioba afedheheshwe namna ile na hii inaonyesha viongozi wetu waliostaafu hawa huru kutoa maoni yao yatakayo enda kinyume na selikali ya ccm leo kwa walioba na kesho hao waliopo madarakani kwa sasa mambo yaliyotokea jana ni aibu kwa ccm na serikali yake na ni lazima makonda,aron na kundi lao wote wachukuliwe hatua kali na waseme ni nanialiwatuma hii nchi ni yetuwote naomba vyombo vya usalama fanyieni kazi hili jambo linaweza kuleta shida hapo baadaye vinginevyo naanza kuona heshima kwa viongozi wetu inaanza kupotea.
 
"Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote".

Dunia ina mambo mengi sana ya kufurahisha,kusikitisha na Kushangaza...Hivi haya Maneno ya Sitta kwenye Red ni kweli yeye amesema Sitta? ni kitu gani ambacho Warioba alifanya kibaya? sasa naanza kuhamini kuwa huu ni mpango na umepangwa na utaendelea kutekelezwa popote atakapokuwepo Warioba ikiwa ni njia ya kumnyamazisha.

Kweli ukistajabu ya Musa utaona ya firauni
 
Kwa majibu haya ya samweli sitta,bhasi amefadhili uharamia huu kupitia paul makonda.
 
Back
Top Bottom