ngorope
JF-Expert Member
- Jul 15, 2011
- 1,112
- 243
Ungetimiza vigezo ungekuwa na walinzi mle ndani na vijana wenu wasingeandaa fujo ili wawasingizie UVCCM..Hakuna jazba ya CCM kwani mjadala ulikuwa bado kuanza..Ingekuwa mjadala umeanza baada ya Warioba kumaliza kumzushia Nyerere na fujo ikafuata ndiyo ungesema jazba lakini vijana wenu waliowapiga wale waliobeba mabango na kuwarushia viti ndio walikuwa na jazba
Upeo mdogo kwako mjadala kuanza ni maswali na majibu pole, je mabango yenu yalikuwa sehemu ya mjadala au ndo kutumika pasipo welewa? nadhani mngengoja kipindi cha maswali ili nyie mnaojiona kuwa mmeisoma na kuielewa katiba pendekezwa muwaelimishe wenzenu nao waielewe ila kwa vijana niliowaona pale na mabango nina hakika wengi wao hawawezi hata kusema kifungu kimoja cha katiba pendekezwa kinasema nini kwa kuwa hawajaisoma. Nilichoona pale ni ushabiki na jazba za kiuanafunzi kama zile za migomo chuoni