Sitta: Warioba amejitakia mwenyewe

Sitta: Warioba amejitakia mwenyewe

Ungetimiza vigezo ungekuwa na walinzi mle ndani na vijana wenu wasingeandaa fujo ili wawasingizie UVCCM..Hakuna jazba ya CCM kwani mjadala ulikuwa bado kuanza..Ingekuwa mjadala umeanza baada ya Warioba kumaliza kumzushia Nyerere na fujo ikafuata ndiyo ungesema jazba lakini vijana wenu waliowapiga wale waliobeba mabango na kuwarushia viti ndio walikuwa na jazba

Upeo mdogo kwako mjadala kuanza ni maswali na majibu pole, je mabango yenu yalikuwa sehemu ya mjadala au ndo kutumika pasipo welewa? nadhani mngengoja kipindi cha maswali ili nyie mnaojiona kuwa mmeisoma na kuielewa katiba pendekezwa muwaelimishe wenzenu nao waielewe ila kwa vijana niliowaona pale na mabango nina hakika wengi wao hawawezi hata kusema kifungu kimoja cha katiba pendekezwa kinasema nini kwa kuwa hawajaisoma. Nilichoona pale ni ushabiki na jazba za kiuanafunzi kama zile za migomo chuoni
 
kweli wewe bongolala....akili mgando unayo wewe na ndio maana umejitambulisha kama bongolala..mjadala wa uwazi una kanuni zake lakini sio kushikilia tu kuwa kile alichoandika yeye ndiyo sahihi. Kulikuwa na vichwa zaidi ya 450 pale bungeni na vingi vilikuwa vimebobea katika sheria sasa mbona warioba hataki kukubali kuwa sauti ya wengi ni sauti ya Mungu???

Matusi ni kipimo cha weledi mdogo wa kujadili na kujenga hoja swali umesema mjadala wa uwazi una kanuni zake ni zipi hizo? kubeba mabango kama tuko kwenye maandamano ni sehemu ya kanuni za mjadala? kwa nini wasitoe maoni yao kwa kuueleza welewa wao katiba pendekezwa au wote walikuwa bubu? hii inadhihirisha kuwa wametumika kubeba ujumbe wa walio nyuma yao
 
Uzushi mwingine huo..Warioba anatetea maoni gani ya wananchi?? yale ya serikali ya mkataba yapo? yale ya mabaraza ya kata yapo? yale ya wakulima na wafugaji yapo?? au unaota ndoto ya mchana..Warioba aliondoa maoni ya wananchi wengi akaweka maoni ya kikundi cha wachache..Zanzibar wengi walitaka serikali ya mkataba hakuiweka...tanzania bara ukiondoa kigoma na sehemu ya shinyanga na moshi sehemu zilizobaki wote walitaka serikali mbili na wengine hawakujadili kabisa muundo wa muungano...sasa hayo maoni ya wananchi ni yapi???Rais muungwana anaokoa kwanza fedha za umma halafu anawashitaki wahalifu na ndicho alichofanya Mheshimiwa Rais kwanza kuwaomba warejeshe na walirejesha tukaokoa mabilioni kadhaa na bado tukawashtaki na kuwafunga wengine..Wangeshtakiwa hivihivi wangeweza kutorosha hizo fedha nje ya nchi na wao wakakimbilia uhamishoni...Serikali haijajaza wezi wa kuku magerezani, tembelea upate takwimu, waliojaa ni majambazi ya kutumia silaha, wauzaji wa dawa za kulevya, wauaji, wahujumu uchumi na wahaini....UONGO WAKO HAUNA MASHIKO..JARIBU TENA BAADAYE

Shetani kasoro mkia
 
Kati ya hao ni wangapi walishawahi kuwa mawaziri wakuu? Kati ya hao wenye uwezo kuliko Mzee Warioba, ni wangapi walikuwa wenyeviti wa tume ile?

Wewe ni mpumbavu tena juha la kwanza.

Ungekuwa wewe ungekaa kimya kwa kuwa huna akli na ni marehemu badokuzikwa tu.

Kwa nini usinyamaze usubiri sanda na kupelekwa kaburini? Mbona unapiga kelele za kijinga hapa?

Pumbavu kweli kweli.

Umeshakunywa gongo sasa unaharisha Tu.Dr. Salim Ahmed Salim hakuwahi kuwa waziri mkuu mbona yupo kimya kwani haoni.? Vijana wa chadema ndio tabia yenu kuropoka Na kutoa matusi Kama viongozi wenu nimewazoea.
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.

Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.

Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.

Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.

Huyu Mzee ashachanganyikiwa kabisa, laana ya viongozi wa dini ishaanza kumvuruga

6 Ataokota makopo tu na bado
 
Warioba anatakiwa ajiunge na chama au kundi la jamii linalotambulika ili awashawishi wananchi wapige kura ya hapana lakini asitumie hoja kwamba yale aliyoyaweka yeye ndiyo yalikuwa sahihi na yaliyowekwa na bunge sio sahihi. na asiwadanganye wananchi kuhusu maadili na kumwajibisha mbunge kwani angezingatia gharama na muda angeelewa kuwa kama maoni yake yangekubalika basi yule anayeshindwa kazi yake inakuwa kumtengenezea fitina yule aliyeshinda hivyo hakutakuwa na shughuli za maendeleo zaidi ya kunyang'anyana madaraka. Mshauri Warioba asajili chama kwani ni yeye aliyeandika kwenye katiba kuwa chama cha siasa ndicho kitaelimisha raia kuhusu uraia.

Kwa kuwa ninyi CCM mmezoea kuhonga wapiga kura basi kila wakati mnaogopa kivuli cha rushwa na takrima yenu. kwa nini uanze kuhofia mizengwe kama unafanya kazi ambayo wananchi wanaikubali?
 
Huyu kijana makonda inabidi taifa limfadhili aende kwenye mashindano ya bondia kimataifa.
 
Mbona hujajibu yote? Wewe ni juha tu, hujui maana wala faida ya taarifa sahihi. Unataka wanyamaze ili iwe nini? Pumbafu kweli kweli. Kama wewe ni bendera fuata upepo na akili zako kama ulishawahi kuwa nazo, ulizipa likizo isiyo malipo ni wewe na hao wajinga wenzio wasiojua thamani ya elimu.

Kwanza CHaDEMA imeingiaje hapa ? Nani kakuambiwa wanaotetea maslahi ya taifa ni Chadema tu? Au unadhani CDM wako peke yao? Mwehu kweli kweli.


Umeshakunywa gongo sasa unaharisha Tu.Dr. Salim Ahmed Salim hakuwahi kuwa waziri mkuu mbona yupo kimya kwani haoni.? Vijana wa chadema ndio tabia yenu kuropoka Na kutoa matusi Kama viongozi wenu nimewazoea.
 
Mheshimiwa Sitta yuko sahihi kabisa nami namuunga mkono kwa asilimia mia...Warioba anatakiwa awaachie watanzania wataamua wenyewe lakini huku kuhangaika kwake na kujidai yeye ndiye aliyekaa na Mwalimu kuliko watanzania wote kutamuumbua siku si nyingi

Cha kufanya hapa, ni jino kwa jino. Kama red bridged wapo, wafanye hiyo kazi. Naamini kama Makonda jana angekuwa Musoma, kilikuwa kifo chake. Kule hawataki upumbavu kabisa. Daa wajinga na wapumbavu ni wengi, wanakalia maneno tu vitendo hakuna, sijui kwanini, shit!
 
Umeshakunywa gongo sasa unaharisha Tu.Dr. Salim Ahmed Salim hakuwahi kuwa waziri mkuu mbona yupo kimya kwani haoni.? Vijana wa chadema ndio tabia yenu kuropoka Na kutoa matusi Kama viongozi wenu nimewazoea.
Sasa kama yeye amehalalisha hujuma, basi na wengine wakubali tu? Isitoshe, yeye CCM ilishasema, si mtanzania, ni mtu wa Omani hivo haimuhusu ndo maana yuko kimya. Au hii kitu umesahau mkuu kuwa mlimtoa kwenye kugombea urais kwa kigezo hicho? "Fikiri kwanza kabla ya kuandika'
 
Sita ni mmoja kati ya wapumbavu niliowahi kuwasikia katika nchi hii!
 
Sita ajitokeze yeye aone hasira za UMMA zilivyo! Sita umejipa aibu ktk uzee wako hadi siku ya kiyama chako! Kibaya zaidi hata wapakwa mafuta unawatukana! Uzee wako ni hasara sana na majuto!:shetani:
 
Huyu ndiye kiongozi mwadilifu. Sina hakika na maana ya kauli ya Sitta kuwa watazia wa leo siyo wajinga kama inasadifu hali halisi ya matumizi ya neno hilo. Kinsingi mimi naona amelitumia vibaya, kati watu ambao hawakujitabua tangu mchakato wa katiba ulipo aza naweza kusema ni Sitta. Moja ya watu ambao awali nilidhani ni wazalendo na wenye uwezo wa kuliokoa taifa ni Sitta, kitendo chake cha kukubali kutegwa na uenyekiti wa Bunge la Katiba na kuingia huo mtego bila kujua kuwa nafasi hiyo alipewa ili kumharibia heshima aliyokuwa nayo mbele ya umma ilidhihirisha kuwa uwezo wake ni mdogo kuliko ambavyo niliamini awali. Hivyo sishangai sana kusikia tena sita akitoa kauli za ajabu kama hii
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samwel Sitta amesema kilichomkuta aliyekuwa Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba jana ni sawa na kujitakia mwenyewe.

Akihojiwa muda mfupi uliopita na Redio Voice of Tabora kuhusu maoni yake kwa vurugu kubwa iliyoongozwa na Paul Makonda jana, Mzee Sitta amesema kimsingi wananchi walio wengi wanaunga mkono Katiba pendekezwa.

Mzee Sitta amesema Jaji Warioba anapaswa kutulia kwani akiendelea anaweza kuaibishwa kuliko aliyofanyiwa jana pale Ubungo blue pearl.

Mzee Sitta amemtaka Warioba awaachie wananchi Katiba pendekezwa waamue wenyewe kwa njia ya kura.Sitta ameendelea kusema watanzania wa sasa siyo wajinga na wakikuona unawadanganya watakuvamia hapohapo.Amedai uelewa wa wananchi kwa sasa ni mkubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Alipoulizwa swali kuhusu Uvumi kwamba yeye ndiye anamfadhili na kumtuma Paul Makonda kupambana na yeyote anayempinga Mzee Sitta amecheka na kusema hatajibu hilo swali.
 
th
 
Huyu Mzee zamani nilikuwa namuona ana akili kumbe ni mwendawazimu kabisa

Na sasa ndio tunazidi kugundua kuna kitu kwenye hii katiba,kwa nini mpaka watu wagombane ??
 
Huyu Mzee zamani nilikuwa namuona ana akili kumbe ni mwendawazimu kabisa

Na sasa ndio tunazidi kugundua kuna kitu kwenye hii katiba,kwa nini mpaka watu wagombane ??

yahani hauelewi kabisa??!!
 
Mheshimiwa Sitta yuko sahihi kabisa nami namuunga mkono kwa asilimia mia...Warioba anatakiwa awaachie watanzania wataamua wenyewe lakini huku kuhangaika kwake na kujidai yeye ndiye aliyekaa na Mwalimu kuliko watanzania wote kutamuumbua siku si nyingi

Aha, kama j.k alivyowaachia wananchi waamue sio? Mtavuna mlicho na mnachopanda definitely only time will tell
 
Naomba tusilaumu sana hizi kauli za magamba, tuerejee kwenye ule utaratibu alioueleza Mhe. Jaji Warioba, wa mchakato mzima wa kupitisha hii katiba. Kwa hizi kauli zao inaelekea wameshapanga matokeo ya hii pendekezwa

Kwa anayekumbuka utaratibu mzima atukumbushe kwenye uzi mpya tafadhali
 
Back
Top Bottom