Sitta kukutana na kardinali Pengo na Mufti Simba

kbm

JF-Expert Member
Oct 5, 2012
5,222
1,670
Samuel-Sita-April8-2014.jpg

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Samuel Sitta

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, leo anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam.

Kadhalika, Sitta atakutana na Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban bin Simba, makao makuu ya Baraza la Kiislamu Tanzania (Bakwata), yaliyopo Kinondoni.

Tangazo fupi lililotolewa kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari (Maelezo), jana lilisema kuwa kiongozi huyo wa Bunge atakutana na Kardinali Pengo leo saa 3:00 asubuhi na kisha atakutana na Mufti Simba saa 6:00 mchana.

Tangazo hilo fupi halikufafanua nia hasa ya kiongozi huyo kukutana na viongozi hao wa dini.

"Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba anatarajia kukutana na Kardinali Pengo saa 3:OO asubuhi St. Joseph na baadaye saa 6:00 mchana Kinondoni kukutana na Mufti bin Simba. Mikutano itafanyika jijini Dar es salaam," lilieleza tango hilo fupi.

Hata hivyo, pamoja na kwamba tangazo hilo halikuweka bayana nia ya Sitta kukutana na Mufti pamoja na Kardinali Pengo; wadadisi wa masuala ya kisiasa wameeleza kuwa mwenendo wa Bunge la Katiba hasa mivutano isiyokwisha inayoendelea kwenye vikao bungeni itakuwa ajenda kuu ya kuwafuata viongozi hao.

Tangu kuanza kwa Bunge Maalum la Katiba, kumekuwa na mivutano isiyokwisha kuanzia ile ya kura ya siri au ya wazi, iliyoibuka wakati wa kupitisha Kanuni za Bunge hilo kiasi cha kuafikiana kwamba kura zote mbili zitumike wakati wa upitishaji wa vifungu mbalimbali vya rasimu ya Katiba.

Kadhalika, suala la kupitisha kifungu cha rasimu kwa theluthi mbili ya kura za wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika pamoja na muundo wa serikali; ni masuala ambayo bado yanaleta mvutano mkubwa bungeni.

Mivutano hiyo imezaa makundi ndani ya Bunge; kundi moja likiundwa kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambalo linatetea muundo wa serikali tatu kwenye Katiba ijayo na lingine likijiita Tanzania Kwanza, linalotetea muundo wa serikali mbili.

Kundi la Ukawa linaundwa na wajumbe wa upinzani na kundi la Tanzania Kwanza linaundwa na wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na yamekuwa yakilumbana ndani na nje ya Bunge, kiasi cha kuyumbisha kiti cha Mwenyekiti.



CHANZO: NIPASHE

===========
Up DATES
===========
9th April 2014

BUNGE LA KATIBA:Sitta awatwisha mzigo Pengo, Mufti Simba

Polycarp-Kardinali-Pengo-April9-2014.jpg

Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhadhama Polycarp Kardinali Pengo,akiagana Sitta.



Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, jana alikutana kwa nyakati tofauti na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, na Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu, Issa bin Shaaban Simba, kwa lengo la kuwaeleza lilipotokea Bunge hilo, lilipo na linakotaka kwenda.
Sitta, ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, alimtembelea Kardinali Pengo katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph na Mufti Simba, Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kuwatembelea viongozi hao, Sitta alisema lengo la ziara yake ni kuwaeleza mambo hayo, pia kuwaomba kuwa na maombi ya kuliombea Bunge hilo na mchakato huo kwa jumla.
KAULI ZA PENGO, SIMBA
Kwa mujibu wa Sitta, Mufti alishukuru kwa ugeni huo na kujua linaloendelea kwenye mchakato huo.
¡°Kama kiongozi mkuu ndani ya jamii hapaswi kuyapapasa masuala ya mchakato wa Katiba mpya ndiyo maana nimekuja kumueleza kwa undani na kupata ushauri wake¡-kubwa zaidi ni maombi yao ili mambo yawe mepesi na tuweze kumaliza mchakato salama na kupata Katiba bora,¡±alisema.
Kardinali Pengo alisema ameridhishwa na mchakato huo na anaendelea kuliombea Bunge ili umalizike salama.
Aidha, Sitta alisema ataendelea na ziara yake kwa makundi mengine kama ya vijana; asasi za kiraia na taasisi nyingine za kidini, ili kuwajulisha kinachoendelea kwenye Bunge kuliko kuwaacha wakipata taarifa kupitia vyombo vya habari pekee.
Hata hivyo, alitumia nafasi hiyo kuwaomba wajumbe wa Bunge hilo kuacha kulumbana kuhusu muundo wa serikali mbili au tatu bali wajikite katika kujadili kupata Katiba yenye Taasisi imara zenye kusimamia nchi katika misingi ya sheria na maadili.
Mwenyekiti huyo alisema tatizo kubwa kwa sasa maadili yameporomoka hivyo Katiba mpya ndiyo itakayosaidia kutengeneza sheria zenye meno ili kuwabana watumishi wa serikali wasio na maadili mazuri.
¡°Lazima Katiba mpya iwe na sheria kali ili kuondokana na watumishi wababaishaji, lazima nchi iende kwa maadili,¡± alisisitiza Sitta.
Bunge Maalum la Katiba lilianza Februari 18, mwaka huu, kwa wajumbe kuchagua Mwenyekiti wa muda, kujadili Rasimu ya Kanuni kwa siku 21 na baadaye kumchagua Mwenyekiti na Makamu wa kudumu, Samia Suluhu.
Baada ya uchaguzi huo kanuni zilianza kufanyakazi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, kuwasilisha Rasimu ya Katiba Bungeni na Rais Kikwete hufungua rasmi.
Aidha, kwa takribani wiki moja sasa, Bunge hilo limegawanyika kwenye Kamati 12 zenye jukumu la kujadili Rasimu ya Katiba, huku kukiwa na kamati za kitaalam tano.


CHANZO: NIPASHE
 
Mr 6 kama lengo ni kuzungumza na vion?gozi wa dini usiwatenge na wale wa makundi mengine! au kwa kuwa hao wameshaonyesha msimamo wa sirikali 2?
 
Kuna habari katika gazeti la Nipashe kwamba leo Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Samweli Sita anakwenda kukutana na viongozi wa dini: Pengo na Mufti kwa nyakati tofauti.

pamoja na kwamba maudhui ya kikao chao hayajulikani bado lakini inaonekana ni kuhusu swala la serikali mbili au tatu linalolisumbua BMK.

kwanza kuna urafiki wa ghafla umeibuka kati ya Pengo na serikali na CCM. Hasa baada ya Pengo kuonesha kuunga mkono msimamo wa serikali mbili kinyume na maoni ya Baraza la maaskofu katoliki waliopendekeza serikali tatu.

Tumezoea mara zote kumuona muadhama akisimama mara nyingi upande wa wanyonge (wananchi) kuwateteta na ikafika mahali akadai anapewa vitisho ili anyamaze lakini akasema hata kama vyombo vyote vya habari ( Hat nyie wa Tumaini Media) vitakataa kuyaandika yale yalio kweli basi yeye hatanyamaza kusema. Ilifika mahali kukawa na kurushiana maneno kati ya serikali na kanisa kwa sababu ya kanisa kukemea uovu wa serikali kwa nguvu. Ilifika mahali wakaambiwa wavue majoho waingie kwenye ulingo wa siasa! Kisa kanisa kuikosoa serikali na chama chake.

lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida pengo ametengeneza urafiki mkubwa na serikali na chama tawala kiasi kwamba siku hizi hatumsikii tena akitoa yale maneno yake mazito ya kiunabii kuionya serikali. Zaidi sana ameungana na chama tawala kutetea maoni yao binafsi na kupingana na ukweli wa hali halisi na maoni ya wananchi wengi.

Kiongozi mkubwa kama pengo ndiye mtu anayetakiwa asimame kati kam arbitrattor wakati mabo yamekwenda kombo na pande mbili zinashindwa kukubaliana. lakini ameamua kuchukua upande katika yanayobishaniwa! Kwa hiyo leo hatuna tena wa kututetea wanyonge. CCM wanaweza kuamua kufanya wanavyotaka kwa sababu viongozi wa dini wanaowaogopa sana walishawaweka sawa. Hakuan asiyejua kwamba Mufti Simba ni CCM dam na analipwa na serikali.

Onyo: Sisi wkatoliki tunamtahadharisha tu kardinali Pengo kwamba kama amekubali kuungana na watawala kuwakandamiza wananchi wanyonge basi na ahakikishe anashikana nao kweli kweli kwa sababu tutaendesha kampeni kubwa katika makanisa yote ya Dar ili wagome kutoa sadaka ya mavuno ambayo ndiyo chanzo kikuu cha mapato ya kanisa. Serikali uliyoamua kuwa nayo upande mmoja basi na wakugharimie gharama za kuendesha jimbo na mapadri wako. Tunataka kanisa libaki katika nafasi yake ya kuteteta wanyinge na kusimamia haki na wala sio kukaa upande wa watawala.

Tumsifu Yesu Kristo.
 
Onyo: Sisi wkatoliki tunamtahadharisha tu kardinali Pengo kwamba kama amekubali kuungana na watawala kuwakandamiza wananchi wanyonge basi na ahakikishe anashikana nao kweli kweli kwa sababu tutaendesha kampeni kubwa katika makanisa yote ya Dar ili wagome kutoa sadaka ya mavuno ambayo ndiyo chanzo kikuu cha mapato ya kanisa. Serikali uliyoamua kuwa nayo upande mmoja basi na wakugharimie gharama za kuendesha jimbo na mapadri wako. Tunataka kanisa libaki katika nafasi yake ya kuteteta wanyinge na kusimamia haki na wala sio kukaa upande wa watawala.

Tumsifu Yesu Kristo.

Mkuu hili la kuwawekea vikwazo vya kiuchumi watumishi sio jema. Mwacheni Pengo awe huru kwa kile anachokiamini, mpingeni kwa hoja, na kama ni kweli wananchi wengi wana msimamo tofauti litadhihirika hilo kwenye kupiga kura.
 
Acha mkwara utagoma peke yako,kama unatoa sadaka au mavuno kwa lengo hilo,huo ni unafiki mbaya Sana.
 
Sielewi hasa lengo lake nini kama sio uzushi tu!! Wananchi tayari walishatoa maoni yao na rasimu ikakamilika, sasa hii mikutano ya nini tena kwa watu waliokwisha tamka kuwa wanaunga mkono serikali mbili? Sitta fanya kazi achana na mbwela mbwela za CCM..
 
Hao viongozi wa dini wana maslahi binafsi.Hakuna hata mmoja aliyechukua maoni yetu ktk nyumba za ibada hivyo HAWANA UHALALI WA KUKUTANA NA SITTA JUU YA KATIBA
 
Ndiyo tunalitegemeza kanisa ili lisimamie na kuisema haki ili lisije kuhongwa na wenye uchu wa madaraka. Kumbuka hwa viongozi wa kanisa ni binadami na wanatamaa ya fedha pia!
 
Acha woga wewe....pengo jembe langu naliaminia...hapa ndio linapata nafasi ya kumweleza ukweli mgumu kumeza kuwa "mkichakachuwa maoni ya wananchi waliyompatia warioba mujuwe siku wanapiga kura za maoni tutawatuma wawamwage na kikinuka tutakuwa upande wao"....pengo hatishiwi nyau na yeye huwa hana kauli ya mwisho zaidi ya ile ya baraza la maaskofu....yeye ana-endorse tuu maamuzi ya baraza.

Pia nilitaka kujua...hivi sita akishamaliza kuongea na viongozi wa dini..atarudi pia kuongea na wananchi???....pia inamaaana hawaamini kama warioba alikusanya maoni mpaka ya viongozi wa din?..mbona kama wanakosea njia ya kupita...walitakiwa waje kwetu tupige kura ya muundo tunaoutaka kisha katiba draft iundwe then ikajadiliwe bunge maalumu la katiba.......

Hapa ni mwendo wa tatu bomba au moja imara muda wa mbili legelege ushapita...50 years of sovereignty unrest umetosha.
 
wewe hujamsikia pengo akitetea serikali mbili? Au u mgeni hapa Samaria?
 
Mr 6 ujue damu itamwagika kama wamini kukutana na ccm wanzio ndio suluhisho kama maoni yetu sisi wananchi hayata sikilizwa namini kitanuka
 
Muadhama anapaswa kuangalia maslahi ya taifa sio yawatu wachache wenye tamaa kama wewe
 
Acha woga wewe....pengo jembe langu naliaminia...hapa ndio linapata nafasi ya kumweleza ukweli mgumu kumeza kuwa "mkichakachuwa maoni ya wananchi waliyompatia warioba mujuwe siku wanapiga kura za maoni tutawatuma wawamwage na kikinuka tutakuwa upande wao"....pengo hatishiwi nyau na yeye huwa hana kauli ya mwisho zaidi ya ile ya baraza la maaskofu....yeye ana-endorse tuu maamuzi ya baraza.

Pia nilitaka kujua...hivi sita akishamaliza kuongea na viongozi wa dini..atarudi pia kuongea na wananchi???....pia inamaaana hawaamini kama warioba alikusanya maoni mpaka ya viongozi wa din?..mbona kama wanakosea njia ya kupita...walitakiwa waje kwetu tupige kura ya muundo tunaoutaka kisha katiba draft iundwe then ikajadiliwe bunge maalumu la katiba.......

Hapa ni mwendo wa tatu bomba au moja imara muda wa mbili legelege ushapita...50 years of sovereignty unrest umetosha.

mbona hajawaita waganga wa kienyeji.sita fix tu
 
Hatma ya Taifa letu ipo mikononi mwa Mungu na wala sio CCM au dini fulani...
 
Kuna habari katika gazeti la Nipashe kwamba leo Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Samweli Sita anakwenda kukutana na viongozi wa dini: Pengo na Mufti kwa nyakati tofauti.

pamoja na kwamba maudhui ya kikao chao hayajulikani bado lakini inaonekana ni kuhusu swala la serikali mbili au tatu linalolisumbua BMK.

kwanza kuna urafiki wa ghafla umeibuka kati ya Pengo na serikali na CCM. Hasa baada ya Pengo kuonesha kuunga mkono msimamo wa serikali mbili kinyume na maoni ya Baraza la maaskofu katoliki waliopendekeza serikali tatu.

Tumezoea mara zote kumuona muadhama akisimama mara nyingi upande wa wanyonge (wananchi) kuwateteta na ikafika mahali akadai anapewa vitisho ili anyamaze lakini akasema hata kama vyombo vyote vya habari ( Hat nyie wa Tumaini Media) vitakataa kuyaandika yale yalio kweli basi yeye hatanyamaza kusema. Ilifika mahali kukawa na kurushiana maneno kati ya serikali na kanisa kwa sababu ya kanisa kukemea uovu wa serikali kwa nguvu. Ilifika mahali wakaambiwa wavue majoho waingie kwenye ulingo wa siasa! Kisa kanisa kuikosoa serikali na chama chake.

lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida pengo ametengeneza urafiki mkubwa na serikali na chama tawala kiasi kwamba siku hizi hatumsikii tena akitoa yale maneno yake mazito ya kiunabii kuionya serikali. Zaidi sana ameungana na chama tawala kutetea maoni yao binafsi na kupingana na ukweli wa hali halisi na maoni ya wananchi wengi.

Kiongozi mkubwa kama pengo ndiye mtu anayetakiwa asimame kati kam arbitrattor wakati mabo yamekwenda kombo na pande mbili zinashindwa kukubaliana. lakini ameamua kuchukua upande katika yanayobishaniwa! Kwa hiyo leo hatuna tena wa kututetea wanyonge. CCM wanaweza kuamua kufanya wanavyotaka kwa sababu viongozi wa dini wanaowaogopa sana walishawaweka sawa. Hakuan asiyejua kwamba Mufti Simba ni CCM dam na analipwa na serikali.

Onyo: Sisi wkatoliki tunamtahadharisha tu kardinali Pengo kwamba kama amekubali kuungana na watawala kuwakandamiza wananchi wanyonge basi na ahakikishe anashikana nao kweli kweli kwa sababu tutaendesha kampeni kubwa katika makanisa yote ya Dar ili wagome kutoa sadaka ya mavuno ambayo ndiyo chanzo kikuu cha mapato ya kanisa. Serikali uliyoamua kuwa nayo upande mmoja basi na wakugharimie gharama za kuendesha jimbo na mapadri wako. Tunataka kanisa libaki katika nafasi yake ya kuteteta wanyinge na kusimamia haki na wala sio kukaa upande wa watawala.

Tumsifu Yesu Kristo.

...mimi tu! kukuletea habari.
 
Wakatoliki sio wapumbavu kama wewe unaezani kutotoa dhaka na sadaka ni kumkomoa Pengo. kwa uandishi huu nakuomba sana ukatubu ndugu yangu la sivyo unaweza kupata matatizo makubwa au mtafute mchungaji wako akushauri juu ya ujumbe huu wa kujiandaa kukwamisha injili.
 
Nani kakuchagua mcfm40 kuwa msemaji wa Wakatoliki? Jisemee mwenyewe, na usidanganye kuwa unawasemea Wakatoliki.

Muadhama Kardinali Pengo ni kiongozi wa kidini, lakini pia ni Mtanzania. Anayo haki ya kutoa maoni yake binafsi juu ya muundo wa serikali anaoona unafaa. Hajasema Kanisa Katoliki linataka serikali mbili. Ni yeye angependa serikali mbili. Msimamo wa Baraza la Maaskofu Katoliki unatolewa na Rais wake.

Kutoa zaka na sadaka si jambo la kisiasa. Kama huelewi hivyo basi wewe unaweza kuwa Mkatoliki feki.

Leave us alone. Usithubutu kumshambulia kiongozi wetu wa kiroho. Sio mwanasiasa yule.
 
Kwanza kabisa Sitta anakutana na watu ambao hawana nguvu ya kusema kwa niamba ya makundi yao.Kwa upande wa wakristo chombo kikuu chao ni umoja wa wakristo nchini( ambao ni umoja wa madhehebu yote ya kikristo) mwenyekiti wake ni Kalekekuntwa, ambaye ni askofu wa Iringa.Pili kwa mufti upande wa waislam wengi wamekuwa kama vile hawamtambu na kujikuta wakianzisha msururu wa taasisi nyingine nyingi hivyo sidhani kama maoni yao yataakisi maoni ya taifa.

Pili anawapa kazi ngumu sana viongozi hao wa dini kutoa mustakabali wa kisiasa maana wao sio wanasiasa.
 
Back
Top Bottom