Sitta kukutana na kardinali Pengo na Mufti Simba

Sitta kukutana na kardinali Pengo na Mufti Simba

Samuel-Sita-April8-2014.jpg
Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Samuel Sitta Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, leo anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam. Kadhalika, Sitta atakutana na Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban bin Simba, makao makuu ya Baraza la Kiislamu Tanzania (Bakwata), yaliyopo Kinondoni. Tangazo fupi lililotolewa kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari (Maelezo), jana lilisema kuwa kiongozi huyo wa Bunge atakutana na Kardinali Pengo leo saa 3:00 asubuhi na kisha atakutana na Mufti Simba saa 6:00 mchana. Tangazo hilo fupi halikufafanua nia hasa ya kiongozi huyo kukutana na viongozi hao wa dini. "Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba anatarajia kukutana na Kardinali Pengo saa 3:OO asubuhi St. Joseph na baadaye saa 6:00 mchana Kinondoni kukutana na Mufti bin Simba. Mikutano itafanyika jijini Dar es salaam," lilieleza tango hilo fupi. Hata hivyo, pamoja na kwamba tangazo hilo halikuweka bayana nia ya Sitta kukutana na Mufti pamoja na Kardinali Pengo; wadadisi wa masuala ya kisiasa wameeleza kuwa mwenendo wa Bunge la Katiba hasa mivutano isiyokwisha inayoendelea kwenye vikao bungeni itakuwa ajenda kuu ya kuwafuata viongozi hao. Tangu kuanza kwa Bunge Maalum la Katiba, kumekuwa na mivutano isiyokwisha kuanzia ile ya kura ya siri au ya wazi, iliyoibuka wakati wa kupitisha Kanuni za Bunge hilo kiasi cha kuafikiana kwamba kura zote mbili zitumike wakati wa upitishaji wa vifungu mbalimbali vya rasimu ya Katiba. Kadhalika, suala la kupitisha kifungu cha rasimu kwa theluthi mbili ya kura za wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika pamoja na muundo wa serikali; ni masuala ambayo bado yanaleta mvutano mkubwa bungeni. Mivutano hiyo imezaa makundi ndani ya Bunge; kundi moja likiundwa kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambalo linatetea muundo wa serikali tatu kwenye Katiba ijayo na lingine likijiita Tanzania Kwanza, linalotetea muundo wa serikali mbili. Kundi la Ukawa linaundwa na wajumbe wa upinzani na kundi la Tanzania Kwanza linaundwa na wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na yamekuwa yakilumbana ndani na nje ya Bunge, kiasi cha kuyumbisha kiti cha Mwenyekiti. CHANZO: NIPASHE
Kosa kafanya mwenyewe kinyume na kanunu walizojitungia kwamba!; aanze kufungua ile hadhara JK kisha Jaji Warioba aje amalizie Sauti ya Wenye nchi! Hao hawatamsaidia bali anaendeleza uzoefu wake wa kukosea! Ni heri angepata ushauri wa Mtikila!
 
Mi sielewi 6 anasali wapi...nahisi si Mkatoliki wala Mwislamu...kwa hiyo kwenda kwa Mufti na Kardinali maandamu gazeti lenyewe hawajajua anaenda kuongelea nini, wamfuate tu mara akimaliza wamuulize kaongea nini huko. Yawezekana anataka kubadili dini anaendaa kutaka kujua aelekee wapi, ili mara tu baada ya Bunge hili la katiba awe kama Tonny Blair atangaze anaelekea kwa Mufti au kwa Pengo...si vema tukamhukumu kabla hatujajua nini kimempeleka huko. Na kama ni masuala ya mbili, tatu au moja napo atakuwa kaenda kuwaona kama ambavyo huenda wajumbe wa Warioba au Warioba mwenyewe alionana nao...na tutayasikia. Ushauri wangu kwa wanaJF ni kuwa tusijaribu kuchanganya mambo ya dini na ya siasa maana huwa si wanandugu sana ila moja ni kumpa mwelekeo mwanasiasa anayepotea au anayepotoka kimaadili na si katika kanuni za siasa. Kwa akina Pengo na Simba angalieni msiingilie mihimili mitatu isiyo ndani ya kanuni za swala tano au kipingi cha kwaresma. Napita tu....!
 
Wakatoliki sio wapumbavu kama wewe unaezani kutotoa dhaka na sadaka ni kumkomoa Pengo. kwa uandishi huu nakuomba sana ukatubu ndugu yangu la sivyo unaweza kupata matatizo makubwa au mtafute mchungaji wako akushauri juu ya ujumbe huu wa kujiandaa kukwamisha injili.

mpu.mbavu mwenyewe! Unajua role yangu katika kanisa katoliki au unabwabwaja tu. Hii tayari ni damge kwa kanisa jimbo la Dar na kama hatjirekebisha ataona mavuno mwaka huu km ataambulia kitu!
 
Ukiwa kiongozi mwenye heshima kubwa jitahidi kuwa wamwisho kutoa msimamo wako ili siku za mbele uaminike na pande zote
 
Mungu kakupa mwili lakini kakunyima akili! kama pengo sio mwanasiasa mbona anakubali kuburuzwa na wanasiasa?
Ndiyo raha ya JF. Wewe kweli ni wa kumwambia Moshi hana akili? Unamfahamu?! Kwenye maandishi yake, ni kipi kinachokushawishi kwamba hana akili!
 
Amri zilitolewa kuwalenga shabaha walokusudiwa kwa kauli zilizosikikika “Piga Yule”, “ Piga shaba”, “yule piga shaba”… (rejea mkanda wa mauaji ya mwembechai wa ITV).

Silaha za moto zikarindima, Waislamu wanne (4) wakauawa pale pale na maiti zao zikaburuzwa na kutupiwa ndani ya gari la Polisi kama mizoga.

Mamia ya Waislamu wakiwemo wanawake zaidi ya mia mbili walijeruhiwa na kuwekwa mahabusu.

Baada tu ya mauaji ya Mwembechai, mkutano mkuu wa chama tawala, CCM, mwenyekiti wake akiwa Benjamini Mkapa, ambaye pia alikuwa Rais wa nchi, uliipongeza serikali kwa hatua iliyochukua Mwembechai.

Pia kiongozi Mkuu wa kanisa Katoliki, Polycarp Kadinali Pengo, aliunga mkono mauaji yale ya Waislamu akidai kuwa, askari wale walikuwa na haki ya kuwapiga risasi za moto kwa kuwa nao walikuwa wakiwatupia mawe.

Akajaribu kuhalalisha kwa kurejea kisa cha Nabii Daud kuwa jiwe nalo linaua kama Daud (a.s) alivyomuua mfalme Jalut kwa jiwe


Malizia story, BAKWATA walichukua hatua gani baada ya Mkapa kupongeza?
 
Udhalimu ni kwa unavyoona wewe lakini sio wote wanaoona udhalimu kwa wengine ni poa tu , ndo maana nikasemaje mawazo ya wengi yapite na si kama oja zako za kuhamasisha watu wasitoe sadaka ili kanisa lihahe, kisa pengo ana urafiki na ccm
 
Kuna habari katika gazeti la Nipashe kwamba leo Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Samweli Sita anakwenda kukutana na viongozi wa dini: Pengo na Mufti kwa nyakati tofauti.

pamoja na kwamba maudhui ya kikao chao hayajulikani bado lakini inaonekana ni kuhusu swala la serikali mbili au tatu linalolisumbua BMK.

kwanza kuna urafiki wa ghafla umeibuka kati ya Pengo na serikali na CCM. Hasa baada ya Pengo kuonesha kuunga mkono msimamo wa serikali mbili kinyume na maoni ya Baraza la maaskofu katoliki waliopendekeza serikali tatu.

Tumezoea mara zote kumuona muadhama akisimama mara nyingi upande wa wanyonge (wananchi) kuwateteta na ikafika mahali akadai anapewa vitisho ili anyamaze lakini akasema hata kama vyombo vyote vya habari ( Hat nyie wa Tumaini Media) vitakataa kuyaandika yale yalio kweli basi yeye hatanyamaza kusema. Ilifika mahali kukawa na kurushiana maneno kati ya serikali na kanisa kwa sababu ya kanisa kukemea uovu wa serikali kwa nguvu. Ilifika mahali wakaambiwa wavue majoho waingie kwenye ulingo wa siasa! Kisa kanisa kuikosoa serikali na chama chake.

lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida pengo ametengeneza urafiki mkubwa na serikali na chama tawala kiasi kwamba siku hizi hatumsikii tena akitoa yale maneno yake mazito ya kiunabii kuionya serikali. Zaidi sana ameungana na chama tawala kutetea maoni yao binafsi na kupingana na ukweli wa hali halisi na maoni ya wananchi wengi.

Kiongozi mkubwa kama pengo ndiye mtu anayetakiwa asimame kati kam arbitrattor wakati mabo yamekwenda kombo na pande mbili zinashindwa kukubaliana. lakini ameamua kuchukua upande katika yanayobishaniwa! Kwa hiyo leo hatuna tena wa kututetea wanyonge. CCM wanaweza kuamua kufanya wanavyotaka kwa sababu viongozi wa dini wanaowaogopa sana walishawaweka sawa. Hakuan asiyejua kwamba Mufti Simba ni CCM dam na analipwa na serikali.

Onyo: Sisi wkatoliki tunamtahadharisha tu kardinali Pengo kwamba kama amekubali kuungana na watawala kuwakandamiza wananchi wanyonge basi na ahakikishe anashikana nao kweli kweli kwa sababu tutaendesha kampeni kubwa katika makanisa yote ya Dar ili wagome kutoa sadaka ya mavuno ambayo ndiyo chanzo kikuu cha mapato ya kanisa. Serikali uliyoamua kuwa nayo upande mmoja basi na wakugharimie gharama za kuendesha jimbo na mapadri wako. Tunataka kanisa libaki katika nafasi yake ya kuteteta wanyinge na kusimamia haki na wala sio kukaa upande wa watawala.

Tumsifu Yesu Kristo.

wewe na wakatoliki wapi mtagoma?? sema wewe utagoma siyo wakatoliki wote Nyerere alikuwa mkatoliki kindaki ndaki Mkapa naye hivyo hivyo Pinda na wengine kibao una uhakika wote watagoma kama wewe
 
Viongozi makini huenda kimyakimya. Viongozi wetu hamsomeki kabisa. Ni wazi kuwa Pengo atatoa maoni na msimamo wake na si kwa niaba ya Kanisa Katoliki. Habari Maelezo njooni na kilichozungumzwa ili muone upepo utakavyoharibika.
 
Pengo asilete za kuleta kanisa linapaswa kusubiri kuambiwa umma umeamua nini chondechonde lisijiingize kwenye serikali mbili au tatu.
 
Hao viongozi wa dini wana maslahi binafsi.Hakuna hata mmoja aliyechukua maoni yetu ktk nyumba za ibada hivyo HAWANA UHALALI WA KUKUTANA NA SITTA JUU YA KATIBA

Viongozi wa dini??!! Nimemwona nikaona mmmmh, hii ni kali! By the way Mufti sera zake zinafahamika, sawa na Cardinal. Nilitarajia angekutana na viongozi wa dini wenye FIKRA HURU pia kama SHURA YA MAIMAM, WAKUU WA PENTEKOSTE, KKKT, MABOHORA,WABAHA'I,KAKOBE. Hii ingeondoa dhana ya kuwa mh Sitta amekuwa too selective kwa kukutana na viongozi wa mrengo uleule!
 
Simjadili Mufti Simba kwasababu hanihusu lakini kama ni Pengo anataka kuongea naye nini wakati ameisha weka msimamo wake wazi kwamba ni muumini wa Muungano kama ulivyo? Na tusisahau Pengo ni kada wa CCM.
 
wewe na wakatoliki wapi mtagoma?? sema wewe utagoma siyo wakatoliki wote Nyerere alikuwa mkatoliki kindaki ndaki Mkapa naye hivyo hivyo Pinda na wengine kibao una uhakika wote watagoma kama wewe

Unadhani Wakatoliki ni misukule kama wewe? Hii ndio tatizo la kupata nafasi za uongozi wa Kanisa kwa nguvu ya giza na umafia. Hope umenielewa!
 
Pengo asipokuwa makini Kanisa Katoliki litapasuka mapande. Katiba mpya ilijadiliwa sana kwenye Jumuiya na watu wameshatoa maoni yao. Kujaribu kugeuza mambo kipindi hiki kutazua balaa.

safari hii bora Klayini yeye kasema serikali mbili zimeshindwa tujaribu moja.amekwepa tatu huu ndiyo ukomavu
 
Kuna habari katika gazeti la Nipashe kwamba leo Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba Samweli Sita anakwenda kukutana na viongozi wa dini: Pengo na Mufti kwa nyakati tofauti.

pamoja na kwamba maudhui ya kikao chao hayajulikani bado lakini inaonekana ni kuhusu swala la serikali mbili au tatu linalolisumbua BMK.

kwanza kuna urafiki wa ghafla umeibuka kati ya Pengo na serikali na CCM. Hasa baada ya Pengo kuonesha kuunga mkono msimamo wa serikali mbili kinyume na maoni ya Baraza la maaskofu katoliki waliopendekeza serikali tatu.

Tumezoea mara zote kumuona muadhama akisimama mara nyingi upande wa wanyonge (wananchi) kuwateteta na ikafika mahali akadai anapewa vitisho ili anyamaze lakini akasema hata kama vyombo vyote vya habari ( Hat nyie wa Tumaini Media) vitakataa kuyaandika yale yalio kweli basi yeye hatanyamaza kusema. Ilifika mahali kukawa na kurushiana maneno kati ya serikali na kanisa kwa sababu ya kanisa kukemea uovu wa serikali kwa nguvu. Ilifika mahali wakaambiwa wavue majoho waingie kwenye ulingo wa siasa! Kisa kanisa kuikosoa serikali na chama chake.

lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida pengo ametengeneza urafiki mkubwa na serikali na chama tawala kiasi kwamba siku hizi hatumsikii tena akitoa yale maneno yake mazito ya kiunabii kuionya serikali. Zaidi sana ameungana na chama tawala kutetea maoni yao binafsi na kupingana na ukweli wa hali halisi na maoni ya wananchi wengi.

Kiongozi mkubwa kama pengo ndiye mtu anayetakiwa asimame kati kam arbitrattor wakati mabo yamekwenda kombo na pande mbili zinashindwa kukubaliana. lakini ameamua kuchukua upande katika yanayobishaniwa! Kwa hiyo leo hatuna tena wa kututetea wanyonge. CCM wanaweza kuamua kufanya wanavyotaka kwa sababu viongozi wa dini wanaowaogopa sana walishawaweka sawa. Hakuan asiyejua kwamba Mufti Simba ni CCM dam na analipwa na serikali.

Onyo: Sisi wkatoliki tunamtahadharisha tu kardinali Pengo kwamba kama amekubali kuungana na watawala kuwakandamiza wananchi wanyonge basi na ahakikishe anashikana nao kweli kweli kwa sababu tutaendesha kampeni kubwa katika makanisa yote ya Dar ili wagome kutoa sadaka ya mavuno ambayo ndiyo chanzo kikuu cha mapato ya kanisa. Serikali uliyoamua kuwa nayo upande mmoja basi na wakugharimie gharama za kuendesha jimbo na mapadri wako. Tunataka kanisa libaki katika nafasi yake ya kuteteta wanyinge na kusimamia haki na wala sio kukaa upande wa watawala.

Tumsifu Yesu Kristo.

Kumbe sheikh Mkuu analipwa na serikali; Kwani yeye ni mtumishi wa serikali? Je pengo nae halipwi na hao hao? Nimewahi muona sheikh Mkuu kwenye shangingi lenye number stk mara nyingi.Duuuuh only in tz
 
Hawa waku wa dini, wanasiasa si wa kuwaamini tena inafaa tuirudishe nchi mikononi mwetu
 
Afadhali Pengo anajua kusoma ....Shekhe Mkuu hajui kusoma wala kuandika.....sijui itakuaje!
 
Back
Top Bottom