Sitta kukutana na kardinali Pengo na Mufti Simba

Sitta kukutana na kardinali Pengo na Mufti Simba

Kweli viongozi wana play role kubwa sana katika utulivu wa nchi... lakini kwa sasa hawakupaswa kushirikishwa baada ya rasimu ya pili kuwasilishwa... hawa wataharibu hali ya hewa soon asipoangalia...

Hawa viongozi wa dini lazima kwanza watambue sitta ndiyo chanzo cha haya yote tangu alipochakachua kanuni hadi uchaguzi wA WENYEVITI WA KAMATI.Tayari kagundua ni machweo sasa anatafuta pa kutokea.Akumbuke Lema alimpa ushauri wa bure akapuuza.Alinywe mwenyewe
 
Kweli viongozi wana play role kubwa sana katika utulivu wa nchi... lakini kwa sasa hawakupaswa kushirikishwa baada ya rasimu ya pili kuwasilishwa... hawa wataharibu hali ya hewa soon asipoangalia...

You are Genious! Very big mistake.Tayari amejenga tension isiyokuwa na ulazima.
 
mie ninachoona viongozi wa dini wawe makini mambo ya kutoa matamko then alafu mtu anasema ni maoni binafsi yanaweza kuwagharimu baadae mfano kuhusu msimamo wa Pengo kama unapingana na baraza la maaskofu sasa yeye yuko kundi gan anaweza kujenga mahusiano yasio mazuri na baraza pasipo kujua.kwa upande wa wananchi unaweza kujenga matabaka ya kutokukuamini kwa kile unachosimamia mfano kama Pengo anaona serikali mbili zinafaa na huku wauumini wake wengi wao wanasema serikali tatu na pengine ndo maana baraza la maaskofu limekuja na pendekezo la serikali tatu kutokana na kuona waumini wanaonaje linaweza kumshushia heshima yake.
Ni bora viongozi wa dini waachie wajumbe wa katiba kuliko kujiingiza katika malumbano na wanasiasa na wananchi walikuwa na nafasi ya kukutana na Warioba sasa waepuke kuanza kujenga matabaka
 
Nani kakuchagua mcfm40 kuwa msemaji wa Wakatoliki? Jisemee mwenyewe, na usidanganye kuwa unawasemea Wakatoliki.

Muadhama Kardinali Pengo ni kiongozi wa kidini, lakini pia ni Mtanzania. Anayo haki ya kutoa maoni yake binafsi juu ya muundo wa serikali anaoona unafaa. Hajasema Kanisa Katoliki linataka serikali mbili. Ni yeye angependa serikali mbili. Msimamo wa Baraza la Maaskofu Katoliki unatolewa na Rais wake.

Kutoa zaka na sadaka si jambo la kisiasa. Kama huelewi hivyo basi wewe unaweza kuwa Mkatoliki feki.

Leave us alone. Usithubutu kumshambulia kiongozi wetu wa kiroho. Sio mwanasiasa yule.

Mungu kakupa mwili lakini kakunyima akili! kama pengo sio mwanasiasa mbona anakubali kuburuzwa na wanasiasa?
 
Waumini wa kanisa Catholic wamekua kwa mara zote wakiwa heshimu sana viongozi wao wa dini hata awe katekista anaheshimika sana kwa waumuni wake
Kwa upande wa Mwadhama baba askofu Pengo anapaswa ajitathimini kotokana na siku za hivi karibuni kuonekana akipingana wazi na misimamo ya pamoja ya kanisa hasa ktk utungaji wa katiba moya.

Nikweli hatujui kuwa wanaenda kuzungumza nini juu ya mchakato huu adhimu wa KATIBA Lakini nyendo za viongozi hao wawili ktk suala hili zimekuwa zikizua maswali kutoka kwa waamini wa pande zote za dini hasa ikizingatia tayara Pengo sijui kwa upande wa waislam amekiri hadharani kwamba yeye ni muumini wa serikali mbili jambo ambalo halijapendekezwa na wananchi

Itakua ni ngumu sana kutenganisha hofu ya wananchi juu ya viongozi hawa ktk muundo wa serikali ktk rasimu ya katiba Je hawatatoa misimamo yao kwa niaba ya taasisi wanazoziongoza, ni jambo la kusubiri

Binafsi mabadiliko yoyote katika uenfeshaji wa vikao vya bunge kuanzia sasa nitalichukulia kwa jicho la tatu na kwakweli siwezi kulitenganisha na kikao hiki kinacho kaliwa leo tusubiri.

BACK TANGANYIKA
 
Samuel-Sita-April8-2014.jpg

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Samuel Sitta

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, leo anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam.

Kadhalika, Sitta atakutana na Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban bin Simba, makao makuu ya Baraza la Kiislamu Tanzania (Bakwata), yaliyopo Kinondoni.

Tangazo fupi lililotolewa kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari (Maelezo), jana lilisema kuwa kiongozi huyo wa Bunge atakutana na Kardinali Pengo leo saa 3:00 asubuhi na kisha atakutana na Mufti Simba saa 6:00 mchana.

Tangazo hilo fupi halikufafanua nia hasa ya kiongozi huyo kukutana na viongozi hao wa dini.

"Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba anatarajia kukutana na Kardinali Pengo saa 3:OO asubuhi St. Joseph na baadaye saa 6:00 mchana Kinondoni kukutana na Mufti bin Simba. Mikutano itafanyika jijini Dar es salaam," lilieleza tango hilo fupi.

Hata hivyo, pamoja na kwamba tangazo hilo halikuweka bayana nia ya Sitta kukutana na Mufti pamoja na Kardinali Pengo; wadadisi wa masuala ya kisiasa wameeleza kuwa mwenendo wa Bunge la Katiba hasa mivutano isiyokwisha inayoendelea kwenye vikao bungeni itakuwa ajenda kuu ya kuwafuata viongozi hao.

Tangu kuanza kwa Bunge Maalum la Katiba, kumekuwa na mivutano isiyokwisha kuanzia ile ya kura ya siri au ya wazi, iliyoibuka wakati wa kupitisha Kanuni za Bunge hilo kiasi cha kuafikiana kwamba kura zote mbili zitumike wakati wa upitishaji wa vifungu mbalimbali vya rasimu ya Katiba.

Kadhalika, suala la kupitisha kifungu cha rasimu kwa theluthi mbili ya kura za wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika pamoja na muundo wa serikali; ni masuala ambayo bado yanaleta mvutano mkubwa bungeni.

Mivutano hiyo imezaa makundi ndani ya Bunge; kundi moja likiundwa kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambalo linatetea muundo wa serikali tatu kwenye Katiba ijayo na lingine likijiita Tanzania Kwanza, linalotetea muundo wa serikali mbili.

Kundi la Ukawa linaundwa na wajumbe wa upinzani na kundi la Tanzania Kwanza linaundwa na wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na yamekuwa yakilumbana ndani na nje ya Bunge, kiasi cha kuyumbisha kiti cha Mwenyekiti.



CHANZO: NIPASHE

Amri zilitolewa kuwalenga shabaha walokusudiwa kwa kauli zilizosikikika "Piga Yule", " Piga shaba", "yule piga shaba"… (rejea mkanda wa mauaji ya mwembechai wa ITV).

Silaha za moto zikarindima, Waislamu wanne (4) wakauawa pale pale na maiti zao zikaburuzwa na kutupiwa ndani ya gari la Polisi kama mizoga.

Mamia ya Waislamu wakiwemo wanawake zaidi ya mia mbili walijeruhiwa na kuwekwa mahabusu.

Baada tu ya mauaji ya Mwembechai, mkutano mkuu wa chama tawala, CCM, mwenyekiti wake akiwa Benjamini Mkapa, ambaye pia alikuwa Rais wa nchi, uliipongeza serikali kwa hatua iliyochukua Mwembechai.

Pia kiongozi Mkuu wa kanisa Katoliki, Polycarp Kadinali Pengo, aliunga mkono mauaji yale ya Waislamu akidai kuwa, askari wale walikuwa na haki ya kuwapiga risasi za moto kwa kuwa nao walikuwa wakiwatupia mawe.

Akajaribu kuhalalisha kwa kurejea kisa cha Nabii Daud kuwa jiwe nalo linaua kama Daud (a.s) alivyomuua mfalme Jalut kwa jiwe


 
jamani kama nia ni kukutana na viongozi wa dini kwan viongozi wa dini ni hao tu?

wakatoliki ndio wengi...magamba yakiwashika watakuwa wameshika sehemu muhimu sana ambayo itawawezesha kutimiza azma yao ovu dhidi ya wananchi.
 
Samuel-Sita-April8-2014.jpg

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,Samuel Sitta

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, leo anatarajiwa kukutana na Kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini, Muadhama Polycarp Kardinali Pengo, katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph, jijini Dar es Salaam.

Kadhalika, Sitta atakutana na Mufti wa Tanzania, Sheikh Shaaban bin Simba, makao makuu ya Baraza la Kiislamu Tanzania (Bakwata), yaliyopo Kinondoni.

Tangazo fupi lililotolewa kwa vyombo vya habari na Idara ya Habari (Maelezo), jana lilisema kuwa kiongozi huyo wa Bunge atakutana na Kardinali Pengo leo saa 3:00 asubuhi na kisha atakutana na Mufti Simba saa 6:00 mchana.

Tangazo hilo fupi halikufafanua nia hasa ya kiongozi huyo kukutana na viongozi hao wa dini.

"Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba anatarajia kukutana na Kardinali Pengo saa 3:OO asubuhi St. Joseph na baadaye saa 6:00 mchana Kinondoni kukutana na Mufti bin Simba. Mikutano itafanyika jijini Dar es salaam," lilieleza tango hilo fupi.

Hata hivyo, pamoja na kwamba tangazo hilo halikuweka bayana nia ya Sitta kukutana na Mufti pamoja na Kardinali Pengo; wadadisi wa masuala ya kisiasa wameeleza kuwa mwenendo wa Bunge la Katiba hasa mivutano isiyokwisha inayoendelea kwenye vikao bungeni itakuwa ajenda kuu ya kuwafuata viongozi hao.

Tangu kuanza kwa Bunge Maalum la Katiba, kumekuwa na mivutano isiyokwisha kuanzia ile ya kura ya siri au ya wazi, iliyoibuka wakati wa kupitisha Kanuni za Bunge hilo kiasi cha kuafikiana kwamba kura zote mbili zitumike wakati wa upitishaji wa vifungu mbalimbali vya rasimu ya Katiba.

Kadhalika, suala la kupitisha kifungu cha rasimu kwa theluthi mbili ya kura za wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika pamoja na muundo wa serikali; ni masuala ambayo bado yanaleta mvutano mkubwa bungeni.

Mivutano hiyo imezaa makundi ndani ya Bunge; kundi moja likiundwa kama Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambalo linatetea muundo wa serikali tatu kwenye Katiba ijayo na lingine likijiita Tanzania Kwanza, linalotetea muundo wa serikali mbili.

Kundi la Ukawa linaundwa na wajumbe wa upinzani na kundi la Tanzania Kwanza linaundwa na wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM); na yamekuwa yakilumbana ndani na nje ya Bunge, kiasi cha kuyumbisha kiti cha Mwenyekiti.



CHANZO: NIPASHE

WAPENTECOSTE sijui kama bado hata kukumbukwa kama wanakumbukwa..
 
Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya upum.bavu walio nao watanzania na viongozi wao wa dini!Kuna watu hata ukiwaambia walambe kinyesi watalamba tu ili mradi liwe ni agizo la kiongozi wa dini kwa hiyo unajisumbua bure tu mkuu kutoa tahadhari

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums

hakika! na hili hasa ndilo TATIZO linalorudisha nyuma maendeleo ya nchi hii.
 
Mr. 6 ukimaliza kufanya mkutano na hao nenda kwa;

Waprotestanti

Wapentekoste,

Waanglikana ,

Walutheri,

Wasabato

Waorthodoksi

Wamormoni

Mashahidi wa Yehova

Wahindu

Wausikh

Baha'i, n.k.

Hao wengine wote vijaragosi tu. Katoliki ndiyo kila ki2 bhana!
 
wakatoliki ndio wengi...magamba yakiwashika watakuwa wameshika sehemu muhimu sana ambayo itawawezesha kutimiza azma yao ovu dhidi ya wananchi.

Pengo asipokuwa makini Kanisa Katoliki litapasuka mapande. Katiba mpya ilijadiliwa sana kwenye Jumuiya na watu wameshatoa maoni yao. Kujaribu kugeuza mambo kipindi hiki kutazua balaa.
 
Kardinal Pengo anazidi kuweka pengo kubwa kati yake na Baraza la Maaskofu katoliki Tanzania. Pengo amekuwa mwanasiasa sasa.

Tofauti kubwa tunayoiona kati ya ayadi Mwadhama Lugambwa na huyu Mwadhama Pengo ni kubwa.

Mwenye jukumu la kutolea kauli au kulisemea kanisa ni mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu Tanzania ambaye ni Askofu Ngalalekumtwa wa Iringa, lakin Pengo anavyojitia kimbelembele, ipo siku ya Vatican yatamshinda, atulize mzuka hata kama Waziri Mkuu ni wa kutoka kumoja.

Atakachokiongea Pengo leo je ni kauli iliyotoka kwenye baraza la Maaskofu katoliki Tanzania au maoni binafsi? Kwa kanisa hilo maoni binafsi kwa kiongozi wa aina yako si jambo la kawaida maana wana utamaduni wa kuwa na msemaji mmoja anayetambuliwa ambaye amechagulia kwa kuongoza chombo hicho kwa kipindi cha miaka mitatu.

inavyoonekana, CCM wakiamua kumpelekea PENGO kigoli, atakubali kuoa hata kama sheria za kanisa haziruhusu kwa kuwa anawapenda CCM kuliko Mungu
 
Amemsahau Mizengo. Mufti+Kardinali wote ni Wafipa sio?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
IKUMBUKWE Card. Pengo ni kiongozi wa kanisa katoliki ila yeye siyo kanisa katoliki. Msimamo wa kanisa katoliki umetolewa na TEK.
Mufti Simba siyo Bakwata. Bakwata sina uhakika na utaratibu wao
 
Mkuu hili la kuwawekea vikwazo vya kiuchumi watumishi sio jema. Mwacheni Pengo awe huru kwa kile anachokiamini, mpingeni kwa hoja, na kama ni kweli wananchi wengi wana msimamo tofauti litadhihirika hilo kwenye kupiga kura.
hapana hapana Hayo anayoenda kuongea na sita ni mawazo yake binafsi sisi waumini hatujamtuma Bakwata walishatoa msimamo wao huko sita anacho fuata sijui ni nini. hata hivyo sina uhakika kama Bakwata ni msimamo wa waisilamu wote.

serikali haina dini sita tafadhali acha kuingiza mabo haya katika siasa utazipasua hizi dini mapande mapande mdaa si mrefu

pili nchi hii si ya wakatoliki na waisilamu tu, kuna waganga wa kienyeji, wahindu agahakani na walokole na wengine mbona unaendeleza mbini za kwatenga???
 
Wakatoliki sio wapumbavu kama wewe unaezani kutotoa dhaka na sadaka ni kumkomoa Pengo. kwa uandishi huu nakuomba sana ukatubu ndugu yangu la sivyo unaweza kupata matatizo makubwa au mtafute mchungaji wako akushauri juu ya ujumbe huu wa kujiandaa kukwamisha injili.

Haya mambo yenu ya injili wengine tunafanya tu kama formality na wala hatutishiki! kutubu? ha ha ha!
 
usitegemee viongozi wa dini kufanya au kuwaza kwa namna sahihi kila siku, nao ni binadam, pili usahihi ni ule wa wengi kama kiongozi yupo upande fulan wa mawazo basi huko ndo sahihi kulingana na yeye, sasabasi kama pengo ameunga mkono serikali mbili basi hayo ndo maonao yake na yupo sahihi kama wewe unavyojiona sahihi na serikali tatu, yeye kuwa rafiki na serikali ndio kazi yake yeye ni mtu wa kila mtu na sio kwamba asiwe rafiki ya fulani kisa anatenda mabaya, UPENDO HUJENGA YOOTE hivyo urafiki ni upendo na kupitia upendo huo ataweza kuwabadirisha kama wanatend mabaya,
note: YOU HAVE TO BE THE CHANGE YOU WANT TO SEE IN THE WORLD

Kwa hiyo kuunga mkono udhalimu ndio urafiki na upendo unaozungumzia? Unataka kuniambaoi hujui CCM wanachotaka kufanya kwenye rasimu ya katiba?
 
Back
Top Bottom