Sitta autamani Urais 2015

Superman

JF-Expert Member
Mar 31, 2007
5,695
1,696
Please note: Huu si Mkenge wa April's Fools Day. Akili zako changanya na za Mbayuwayu!

Source 1:
Sitta atangaza nia kuwania urais ‘akiombwa' | FikraPevu.com

Source 2:
Sitta kugombea Urais 2015

Source 3:http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=28475 (Sitta: Ninafaa Urais)

* ATAKA KUONGOZA MIAKA MITANO AWAACHIE VIJANA


Na Sheilla Sezzy, Mwanza

MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao mwaka 2015 na kutamba kuwa ana nafasi nzuri kutokana na sifa alizojijengea ndani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Sitta alitaja sifa hizo kuwa ni pamoja ile ya kuwa mteule wa rais, kwa awamu zote nne za uongozi taifa, tangu Tanzania ilipotaka uhuru wake, Desemba 9 mwaka 1961.

Spika huyo mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , alisema kwa sasa anawasikiliza wananchi kama wataona anafaa na haoni ubaya wowote wa kushika nafasi hiyo ya juu katika uongozi wa taifa kwa miaka mitano tu na kuwaachia vijana waendelee.

"Mimi nawasikiliza wananchi kama wataona nafanana na rais wanayemtaka, basi nitachukua maamuzi kwa wakati huo. Sioni ubaya wowote kama wakiniachia kuongoza nchi hii hata kwa miaka mitano halafu niwaachie vijana waendelee,"alisema Sitta.

Alisema kuwa ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2014, kila kitu kitakuwa wazi na haweza kukataa majukumu atayopewa na wananchi wake kwani anatambua wanamuamini kwamba ana uwezo wa kuchapa kazi.

Sitta ambaye pia ni Mbunge Urambo Mashariki na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa( NEC) ya CCM, aliyasema hayo jana muda mfupi kabla ya kupanda jukwaani kufunga kampeni za udiwani za CCM, Kata ya Kirumba.

Mwanasiasa huyo ambaye umaarufu wake umepanda kwa kasi katika miaka ya hivi karubuni kutokana na msimamo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi ndani ya CCM, alitamba kuwa amefanya mambo mengi ndani ya Serikali ya CCM, ambayo yamesaidia kuleta mageuzi makubwa nchini.

Alisema kadri siku zinavyokwenda rais wa Tanzania atajulikana kwa matendo yake na kubainisha kuwa mtu mbaya hawezi kubadilika kuwa mzuri kwa kipindi kifupi.

"Sioni sababu ya mtu kuutafuta urais wakati wananchi wanaona na wanajadili kila siku ni rais wa aina gani wanayemuhitaji kutokana na mahitaji yao,"alisema

Alisema anachofanya kipindi hiki ni kutimiza wajibu wake na wananchi ni mashahidi kila nafasi anayopewa, anatimiza wajibu wake ipasavyo na kusisitiza kuwa amefanya mengi yanayoonekana machoni pa watu na kudhihirisha kwamba ni kiongozi bora.

Akizungumzia umri wa urais, alisema mijadala kuwa vijana hawawezi kuongoza haina msingi. Alifafanua kuwa kiongozi mzuri ni yule mwenye uwezo wa kuwaongoza wananchi na kuwaletea maendeleo.

Alisema rais anachaguliwa na wananchi hivyo maamuzi yote ya nani anafaa kwa nafasi hiyo na umri upi, ipo mikononi mwa wananchi wenyewe.

Katika hatua nyingine Sitta, aliwashangaa wanasiasa wanaopigana vijembe majukwaani na kueleza kwamba tabia ya kumtukana mtu mmoja mmoja, haina maana yoyote.

Aliwashauri viongozi wa CCM kutojibu mapigo ya wapinzani na kuwataka kutumia busara kila wanapokutana na kauli chafu kwani nia ya kudumisha amani ya nchi.

Alionya kuwa amani ya nchi ikitoweka, itakayobebeshwa lawama ni CCM na Serikali yake.

"Kauli nyingi za majukwaani zinachochea chuki miongoni mwa wananchi, matokeo yake zinaweza kuibua machafuko na waathirika watakuwa wananchi wenyewe, tena wale wasio na uwezo wa kujiokoa,'' alisema Sitta.

Alisema kuwa katika miaka 50 ya utawala wa CCM, kuna mambo mengi yamefanyika na kwamba wapinzani hawana haja kubeza kwani yanaonekana kwa macho.

Alisema kuwa katika mafanikio hayo, kuna mengi yamefanywa na Rais Jakaya Kikwete, mfano mzuri ni kampuni tano za madini kulipa kodi na wananchi kuanza kufaidika na rasilimali za nchi yao.

Hofu ya mahasimu wake

Akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali katika Tamasha Vyombo vya Habari lililofanyika wiki iliyopita kwenye Ukumbi Msasanki Beach, Dar es Salaam, Sitta alieleza kuwa anashangazwa na watu wanaoweweseka wakisikia anataka kuwania urais mwaka 2015.

"Nashangaa watu wanapata kiwewe kusikia nataka kuwania urais, kuwania urais ni haki ya kila Mtanzania na Watanzania ndiyo watakaoamua nani ni mzuri na atawafaa," alisema Sitta na kushangiliwa na waliohudhuria tamasha hilo.

"2015 tunataka kuwa na mwelekeo mzuri, nikiwa na maana mambo ya hongo, ubadhirifu hatutaki yawe na nafasi, alisema Sitta na kuongeza:

Alisema watu wanatumia fedha nyingi kusaka urais na hata wengine kutumia ndumba kwa kwenda Mlingotini, Bagamoyo, kwa nia ya kutaka uongozi na matokeo yake wanaposhinda lengo lao la kwanza linakuwa kurudisha fedha walizotumia.

Source:
Sitta kugombea Urais 2015

MY TAKE:
Kwa Changamoto za leo ambayo Nchi Yetu inazo, bado Mh. Samuel Sitta hana uwezo wa kuleta mageuzi ya Kimaendeleo katika Tanzania. Alipata mafasi kamili kama Kiongozi wa moja Mhimili kamili wa Kikatiba kama Spika wa Bunge kusimamia kuondoa uovu kikamilifu pamoja na Ufisadi Mwingine lakini akaamua kukumbatia uovu kuinusuru serikali yake ya CCM.

Japo anaweza kuwa anakubalika na baadhi, Mzee Sitta hawezi kuwa udhubutu wa kutupa Tanzania tunayoiota, na hata huko Wizara ya Afrika ya Mashariki bado hatujaziona cheche zozote.
 
Kwa upande wangu nasema hakuna ccm kama sita,afadhari yeye anaweza kuliko hao wengine,labda tumpe magufuri tatizo tu huwa hatupendi kuambiwa ukweli

Lakini ccm ya leo sitta ama magufuri ndio wanaweza angarau kutusogeza
 
Hana akili! angekuwa mjanja angepigania kuwepo kwa mgombea binafsi, sasa anafikiri atapitia wapi? Kwa hicho chama chake hawampitishi. Akisumbua sana ataondolewa kwa zengwe lile lile la zamu ya kina mama na Asha Migiro atasimamishwa. Labda arudi CCJ.
 
Kwa upande wangu nasema hakuna ccm kama sita,afadhari yeye anaweza kuliko hao wengine,labda tumpe magufuri tatizo tu huwa hatupendi kuambiwa ukweli

Lakini ccm ya leo sitta ama magufuri ndio wanaweza angarau kutusogeza

Magufuli naye asingekuwepo hapo alipo kama sio nafasi yake kwa jinsi alivyojijenga kwa wananchi. Na ili agombee lazima apitishwe na chama, tatizo "wenye chama walioshika hatamu" hawamtaki. Na mbaya zaidi amejiingiza mno kutangaza chama badala ya wa utendaji wa serikali, hivyo basi amelipunguza kundi la kati lililokuwa likimuunga mkono.
 
Sitta yuko sahihi kuweka wazi nia yake hiyo,tatizo ni mfumo uliopo ndani ya CCM,uongozi wa mtandao! angalau kidogo ana uthubutu wa kuzungumzia yale mabovu ya ndugu zake!
 
Hana akili! angekuwa mjanja angepigania kuwepo kwa mgombea binafsi, sasa anafikiri atapitia wapi? Kwa hicho chama chake hawampitishi. Akisumbua sana ataondolewa kwa zengwe lile lile la zamu ya kina mama na Asha Migiro atasimamishwa. Labda arudi CCJ.

Hana ubavu! Akiwa Spika wa bunge hakututendea haki hata kidogo! aliuzima mjadala wa Richmond kidikteta, je alihongwa ahadi ya kugombea Urahisi 2015? huyu mtu ni hatari sana!
 
Watanzania kama tunataka rais mzalendo basi ni huyu!NA KUWEKA WAZI MAPEMA NI KUJIAMINI KWA UADILIFU,WANAOJIFICHA SIO WAADILIFU NDIO MANA WANAOGOPA KUJITOKEZA MAPEMA,HONGERA MZEE SIX,JAPO SAFARI HII NI ZAMU YA ZANZIBAR SIJUI ITAKUWAJE TUTAJUA MBELE!
 
Dah!Leo nakuwa mzito sana kukubaliana na habari yeyote ile maana nyingi ni za kusherehekea sikukuu ya wajinga!Kama ni kweli haya basi yetu macho tu!!
 
Samuel Sitta ni mtu ambaye ameitumikia serikali ya CCM zaidi ya nusu ya Umri wake wote, na yeye alikuwa mwanamtandao.Inasikitisha sana watu kuhadaiwa eti Sitta anapinga ufisadi, Sitta anatumia neno ufisadi kwa maslahi ya kisisiasa na pia kuwachafua wapinzani wake kisiasa. Si ndo huyu Sitta alipopata nafasi ya kuwa kiongozi wa serikali bungeni povu lilimtoka kuwashambulia na kuwadharilisha wapinzani,na kuitetea serikali na chama kwa kuviita "waadilifu" na wasikivu? mnaomshabia huyu gamba opportunist ni vema muangalie na mtathmini misimamo yenu ya kisisiasa.
 
Samuel Sitta ni mtu ambaye ameitumikia serikali ya CCM zaidi ya nusu ya Umri wake wote, na yeye alikuwa mwanamtandao.Inasikitisha sana watu kuhadaiwa eti Sitta anapinga ufisadi, Sitta anatumia neno ufisadi kwa maslahi ya kisiasa na pia kuwachafua wapinzani wake kisiasa. Si ndo huyu Sitta alipopata nafasi ya kuwa kiongozi wa serikali bungeni povu lilimtoka kuwashambulia na kuwadharilisha wapinzani,na kuitetea serikali na chama kwa kuviita "waadilifu" na wasikivu? mnaomshabia huyu gamba opportunist ni vema muangalie na mtathmini misimamo yenu ya kisiasa.
 
Samuel Sitta ni mtu ambaye ameitumikia serikali ya CCM zaidi ya nusu ya Umri wake wote, na yeye alikuwa mwanamtandao.Inasikitisha sana watu kuhadaiwa eti Sitta anapinga ufisadi, Sitta anatumia neno ufisadi kwa maslahi ya kisiasa na pia kuwachafua wapinzani wake kisiasa. Si ndo huyu Sitta alipopata nafasi ya kuwa kiongozi wa serikali bungeni povu lilimtoka kuwashambulia na kuwadharilisha wapinzani,na kuitetea serikali na chama kwa kuviita "waadilifu" na wasikivu? mnaomshabia huyu gamba opportunist ni vema muangalie na mtathmini misimamo yenu ya kisiasa. Even if it is a fools day We cannot be fooled by cheap politics of Sitta and co.
 
Source: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=28475

Sitta: Ninafaa urais

Imeandikwa na Grace Chilongola, Mwanza; Tarehe: 31st March 2012

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema ana vigezo vya kuwa Rais wa Tanzania kutokana na kutimiza wajibu wake vizuri kwa miongo minne iliyopita, kwa kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali.

Alisema hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari mjini hapa, muda mfupi kabla ya kwenda kufunga kampeni za udiwani katika kata ya Kirumba ambapo alisema amefanya mambo mengi katika Serikali ya CCM yaliyoleta mageuzi makubwa.

Sitta, ambaye kati ya mwaka 1967 na 1969 alikuwa Meneja wa Caltex Oil, na baadaye kushika nyadhifa mbalimbali zikiwamo Katibu wa CCM mikoa ya Iringa na Kilimanjaro, Mbunge, Mkuu wa Mkoa na Waziri, alisema Rais ajaye wa Tanzania atajulikana kwa matendo yake na kusema mtu mbaya hawezi kubadilika kuwa mzuri kwa muda mfupi.

"Sioni sababu ya mtu kuutafuta urais wakati wananchi wanaona na wanajadili kila siku ni Rais wa aina gani ambaye wanamhitaji kutokana na mahitaji yao," alisema Waziri Sitta ambaye pia alipata kuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

Alisema yuko tayari kwa majukumu ambayo atapewa na wananchi kwa kuwa wanamwamini kuwa na uwezo wa kufanya kazi na kwamba yeye atawasikiliza kama wataona anafaa na kuchukua uamuzi.

Alisema katika kipindi hiki anachokifanya ni kutekeleza wajibu wake na wananchi wenyewe wanaona kuwa kila nafasi anayopewa anafanya kazi ipasavyo na kudai kuwa vipo vitu vingi ambavyo amefanya na vinaonekana machoni mwa watu ambavyo vinamfanya kuwa kiongozi bora.

Akizungumzia umri wa urais, alisema mijadala kuwa vijana au wazee hawawezi kuongoza haina msingi wowote na kusema kiongozi mzuri ni mwenye uwezo wa kuongoza wananchi na kuwaletea maendeleo.

Aliendelea kusema kuwa, Rais anachaguliwa na wananchi kwa hiyo uamuzi wote wa nani awe rais na kwa umri gani yako mikononi mwa wananchi wenyewe. Desemba atafikisha umri wa miaka 70.

Katika hatua nyingine, Sitta alishangaa viongozi wa siasa ambao wanapigana vijembe katika majukwaa ya mikutano ya hadhara na kusema tabia hiyo si nzuri.

Alisema kauli za majukwaani zinawatia wananchi hasira.
 
superman mambo? (i come in peace today...lol?)

Leo mi nimegundua habari nyingi kwenye magazi ni urongo mtupu
 
MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao mwaka 2015 na kutamba kuwa ana nafasi nzuri kutokana na sifa alizojijengea ndani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).

Sitta alitaja sifa hizo kuwa ni pamoja ile ya kuwa mteule wa rais, kwa awamu zote nne za uongozi taifa, tangu Tanzania ilipotaka uhuru wake, Desemba 9 mwaka 1961.

Spika huyo mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , alisema kwa sasa anawasikiliza wananchi kama wataona anafaa na haoni ubaya wowote wa kushika nafasi hiyo ya juu katika uongozi wa taifa kwa miaka mitano tu na kuwaachia vijana waendelee.

“Mimi nawasikiliza wananchi kama wataona nafanana na rais wanayemtaka, basi nitachukua maamuzi kwa wakati huo. Sioni ubaya wowote kama wakiniachia kuongoza nchi hii hata kwa miaka mitano halafu niwaachie vijana waendelee,”alisema Sitta.

Alisema kuwa ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2014, kila kitu kitakuwa wazi na haweza kukataa majukumu atayopewa na wananchi wake kwani anatambua wanamuamini kwamba ana uwezo wa kuchapa kazi.

Sitta ambaye pia ni Mbunge Urambo Mashariki na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa( NEC) ya CCM, aliyasema hayo jana muda mfupi kabla ya kupanda jukwaani kufunga kampeni za udiwani za CCM, Kata ya Kirumba.

Mwanasiasa huyo ambaye umaarufu wake umepanda kwa kasi katika miaka ya hivi karubuni kutokana na msimamo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi ndani ya CCM, alitamba kuwa amefanya mambo mengi ndani ya Serikali ya CCM, ambayo yamesaidia kuleta mageuzi makubwa nchini.

Alisema kadri siku zinavyokwenda rais wa Tanzania atajulikana kwa matendo yake na kubainisha kuwa mtu mbaya hawezi kubadilika kuwa mzuri kwa kipindi kifupi.

“Sioni sababu ya mtu kuutafuta urais wakati wananchi wanaona na wanajadili kila siku ni rais wa aina gani wanayemuhitaji kutokana na mahitaji yao,”alisema

Alisema anachofanya kipindi hiki ni kutimiza wajibu wake na wananchi ni mashahidi kila nafasi anayopewa, anatimiza wajibu wake ipasavyo na kusisitiza kuwa amefanya mengi yanayoonekana machoni pa watu na kudhihirisha kwamba ni kiongozi bora.

Akizungumzia umri wa urais, alisema mijadala kuwa vijana hawawezi kuongoza haina msingi. Alifafanua kuwa kiongozi mzuri ni yule mwenye uwezo wa kuwaongoza wananchi na kuwaletea maendeleo.

Alisema rais anachaguliwa na wananchi hivyo maamuzi yote ya nani anafaa kwa nafasi hiyo na umri upi, ipo mikononi mwa wananchi wenyewe.

Katika hatua nyingine Sitta, aliwashangaa wanasiasa wanaopigana vijembe majukwaani na kueleza kwamba tabia ya kumtukana mtu mmoja mmoja, haina maana yoyote.

Aliwashauri viongozi wa CCM kutojibu mapigo ya wapinzani na kuwataka kutumia busara kila wanapokutana na kauli chafu kwani nia ya kudumisha amani ya nchi.

Alionya kuwa amani ya nchi ikitoweka, itakayobebeshwa lawama ni CCM na Serikali yake.

“Kauli nyingi za majukwaani zinachochea chuki miongoni mwa wananchi, matokeo yake zinaweza kuibua machafuko na waathirika watakuwa wananchi wenyewe, tena wale wasio na uwezo wa kujiokoa,’’ alisema Sitta.

Alisema kuwa katika miaka 50 ya utawala wa CCM, kuna mambo mengi yamefanyika na kwamba wapinzani hawana haja kubeza kwani yanaonekana kwa macho.

Alisema kuwa katika mafanikio hayo, kuna mengi yamefanywa na Rais Jakaya Kikwete, mfano mzuri ni kampuni tano za madini kulipa kodi na wananchi kuanza kufaidika na rasilimali za nchi yao.

Hofu ya mahasimu wake

Sitta alieleza kuwa anashangazwa na watu wanaoweweseka wakisikia anataka kuwania urais mwaka 2015.

"Nashangaa watu wanapata kiwewe kusikia nataka kuwania urais, kuwania urais ni haki ya kila Mtanzania na Watanzania ndiyo watakaoamua nani ni mzuri na atawafaa," alisema Sitta

"2015 tunataka kuwa na mwelekeo mzuri, nikiwa na maana mambo ya hongo, ubadhirifu hatutaki yawe na nafasi, alisema Sitta na kuongeza:

Alisema watu wanatumia fedha nyingi kusaka urais na hata wengine kutumia ndumba kwa kwenda Mlingotini, Bagamoyo, kwa nia ya kutaka uongozi na matokeo yake wanaposhinda lengo lao la kwanza linakuwa kurudisha fedha walizotumia

E-mail: meezy@youngmaster.co.tz
 
superman mambo? (i come in peace today...lol?)

Leo mi nimegundua habari nyingi kwenye magazi ni urongo mtupu

Haaaa haaa Mkuu wangu mimi niko poa kabisa ndo kwanza nimetia timu DSM.

Mkuu mbona mimi nakufahamu miaka sana na wala sina issue na wewe kabisa. Napenda tu unavyosimamia hoja unazoziamini.

Kama uko Bongo, let us meet in one of the days. Naona AshaDii kule kishawafunga kamba wengi.

Niaje habari ya Sitta kuweka hadharani nia yake ya kuwa kuishi makazi ya sasa ya Baba Mwana-Asha?
 

MY TAKE:

Kwa Changamoto za leo ambayo Nchi Yetu inazo, bado Mh. Samuel Sitta hana uwezo wa kuleta mageuzi ya Kimaendeleo katika Tanzania. Alipata mafasi kamili kama Kiongozi wa moja Mhimili kamili wa Kikatiba kama Spika wa Bunge kusimamia kuondoa uovu kikamilifu pamoja na Ufisadi Mwingine lakini akaamua kukumbatia uovu kuinusuru serikali yake ya CCM.

Japo anaweza kuwa anakubalika na baadhi, Mzee Sitta hawezi kuwa udhubutu wa kutupa Tanzania tunayoiota, na hata huko Wizara ya Afrika ya Mashariki bado hatujaziona cheche zozote.
Mkuu Superman, tafuta thread ya Mzee Mwanakijiji aliyouliza, "Wapiganaji Walioko CCM, Wanapigania Nini?". https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...naji-walioko-ccm-wanapigania-nini-hasa-2.html

Nilisema hivi kuhusu hawa wanaojiita wapiganaji.

Mzee Mwanakijiji, hao makamanda dhidi ya ufisadi wamegawanyika makundi mawili, miongoni mwao wamo wanapinga ufisadi kwa sababu wanauchungu wa dhati na umasikini wa Watanzania ambao ufisadi umechangia kuongezeka kwa umasikini na unaendelea kuitafuna nchi na utaendelea kwa miaka kadhaa ijayo.

Kundi la pili ni la wapinga ufisadi wanaopigania nafsi zao, wanahasira kwa sababu nao wanataka share yao kwenye huo mkate na nafasi zikiwakalia vazuri, nao watafisidi vile vile hivyo nawaweka kundi moja na mafisadi tuu.Kwa mtazamo huo kuna makamanda wenye uchungu na makamanda mafisadi.

Swali ni jee ndani ya CCM, wanapigania nini?. Jibu langu la jumla ni kuwa wanapigania nafsi zao just for survival na wakishapata uhakika wa survival baada ya 2010, mtawashuhudia nao wakifisidi ushahidi ni 'time will tell'.

Kitu kibaya zaidi kuhusu baadhi ya hawa makanda ambacho mtakishuhudia ni kwa baadhi yao kuwapigia magoti mafisadi ili kuwanusuru na panga la CCM kupitishwa kugombea 2010 na wakishapitishwa, wataungana na kuwa kitu kimoja kwa ajili ya kuweka mikakati ya 2015.

Baadhi watakao piga magoti ni wale ambao nguvu ya mafisadi kuhakikisha hawateuliwi na CCM kugombea itatumika, na wakisha toswa na CCM, watatamani kukimbilia upinzani sio ili kuendeleza mapambano, bali kujaribu kuokoa mkate wao wa kila siku na nawahakikishieni, kama mafisadi watamwaga fedha kuhakikisha makamanda hawapiti, na wakihamia upinzani, ndio kwanza sasa chama kitamwaga mapesa zaidi kuhakikisha hakishindwi.

Baadhi ya makamanda watapigwa chini na hapo ndipo itakuwa mwisho wa habari yao, kitakachofuatia ni kwenda kuwalamba miguu mafisadi kwa kurejea CCM wakiwa wametahayari kama alivyofanya yule kinara wa kundi la G-55.

Hizi harakati za kujipambanua kwa pamoja na kuzungukiana majimbo ya wapiganaji zamu kwa zamu huku wakitoa michango ya shilingi 500,000 walizopewa na mshitiri, wakisindikizwa na ka 'kipindi maalum' ndani ya taarifa za habari (no 10min news clip) ya kwenye TV ya mshitiri, hizi ni nyimbo tuu za shangwe na mapambio ya kujinusuru na panga la uteuzi wa CCM mwaka 2010, baada ya hapo kutakuwa hawana hili wala lile.

Sibezi juhudi za makamanda, bali mbinu zilizotumika kuwapambanua bungeni tukianzia kwenye ripoti ya Richmond iliyotumika kumchapa bakora EL kwa kumuhukuma bila kupewa fursa ya kusikilizwa, hivyo ukamanda wao unapimwa ni kwa kiasi gani wanaweza kuzungumza kwa jazba na mapokezi makubwa makubwa kuashiria wananchi wanawakubali.

Wapiganaji wa kweli ni wale ambao wako tayari to take risk kwa kusimama mbali na uvundo kuwathibitishia watanzania kuwa huku tuliko chama kimetekwa na mafisadi, hivyo baada tuu ya kuvunjwa Bunge mwakani, wataonyesha waliposimama na wananchi watawachagua kwenye chama chochote watakacho simama nacho na hawa ndio watakuwa wapiganaji wa kweli kweli.

Wale makamanda wanaopigania nafsi zao, mtawatambua kwa kutokubali kurski nafasi zao ndani ya CCM ambako mafisadi wana upper hand. Hawa watasubiri mpaka watakapo temwa na CCM ndipo waje upande wa pili kujaribu kamari ya upinzani, hawa ndio watakao kwenda na maji kwa sababu upinzani Tanzania ni kwenye baadhi tuu ya maeneo, kuna maeneo mengi CCM inachaguliwa sio kwa sababu imekubalika sana, bali kwa sababu ya mazoea tuu na kukosekana kwa elimu ya uraia.

Kuna sehemu hata akisimamishwa mgombea kiazi vipi, atapita tuu.Kwa vile CCM ina wenyewe, na baadhi ya wenyewe hao ndio hao hao mafisadi na wengine wao ndio hao makamanda, hapa ni mwendo wa mwenye kisu kikali ndie anayekula nyama, na ili ukubaliwe kula nyama ni lazima uchague upande, either with us, or against us, maadamu wenye guvu ni mafisadi, mwenye nguvu mpishe, hao makamanda watajikuta kuliko kuriski loosing, wakijua hawawezi kuwashinda, watatumia formular ya 'if you can't beat them, join them' watajiunga nao na wote wakuwa kwenye tenga moja la samaki, na wote watakuwa ndio hao hao.
 
Back
Top Bottom