Sitasoma tena gazeti la Mawio

Sitasoma tena gazeti la Mawio

Ndio usisome, wengine tutasoma. Hata CHADEMA hatutaki uiamini. Sisi tutaendelea kuiamini, na tunamuunga mkono mgombea wetu Lowassa. Siyo watu mnakuja na propaganda za upuuzi kutoka CCM, halafu mnajidai ni wapenzi wa CHADEMA. Tumeshawagundua
Endelea kuamini kama wafuasi wa Kibwetele.
 
Leo nilinunua gazeti la Mawio ili kupata uchambuzi kuhusiana na Chadema kumpokea mkuu wa mafisadi na kumfanya mgombea wa urais kwa tiketi ya Ukawa. Lakini badala yake nimekutana na habari nyingi zinazoonesha kusifia na kutetea uamuzi wa fisadi huyo kuingia Chadema. Nilikuwa naliamini gazeti hili kama nilivyokuwa naiamini Chadema katika mapambano dhidi ya ufisadi. Sasa kuanzia leo sitanunua wala kusoma tena gazeti hili. Siku fisadi alipopokelewa Chadema nilichana kadi yangu ya uanachama na kuitumbukiza chooni! Sitaki kuwa sehemu ya uchafu unaoendelea hivi sasa ndani ya upinzani.

Hata usiposoma hupunguzi chochote
 
Ha hahahahahahahaha! Asante ndugu kwa kujitambua. Mungu hamfichi mnafiki kwa kweli.
Ingawa mie sie mshabiki wa Lowassa ila mwanachama wa CDM, lazima tutambue kuwa dunia tunamoishi ni dynamic. Ndiyo maana wahubiri wakuu ni Wachungaji wa Kilokole. Mapadre na makasisi wengine kwa sasa hawana mvuto kama hao Wachungaji wa Kilokole kama akina Gwajima et. al. Kwa nini wana mvuto ni kwa sababu ya uhalisia. Kawaida husema walikuwa walevi, wazinzi, majambazi etc na watu wanawaelewa na kuvutiwa nao. Mwisho wanasema kwa sasa wapo huru ndani ya Yesu ambapo sie walevi, wazinzi, majambazi hutaka kuwafuata ili tuwe huru. Kwa Mapadre huwezi kuwa mzinzi ukapata upadre hivyo wanaongelea hisia na si uhalisia wa wawahubirio.

Sasa turejee katika siasa, nadhani hakuna mchafu asiyependa kujitakasa. Kama alikuwa fisadi si haki kila wakati kumnyima fursa kwa kuangalia matendo yalopita bali tuangalia matendo yake yajayo (ingawa kuna usemi kuwa once a w.h.o.r.e always malizia.....). Angalia watawala walioingia madarakani wakiwa wasafi kama theluji, hata wabunge mwisho wa mihula yao wanakuwa mafisadi kwa kuiba raslimali za nchi. Pengine (haya ni mawazo yangu) kuwa aliyekuwa fisadi ni bora zaidi ya atakayekuwa fisadi akiingia madarakani kwani hata yeye atakuwa mwoga kuwa nikifanya hili nitajulikana. Hata umma utakuwa macho naye. Maisha ni kujaribu na kuchukua RISK.
 
Mkuu
Ndio kwanza safari inaanza
Watu wana furaha sana huku kitaaa
 

Attachments

  • 1438258840253.jpg
    1438258840253.jpg
    16.1 KB · Views: 353
kanunue Uhuru na jambo Leo ,usisahau risasi na ijumaa ya shigongo
 
Wewe gazeti lako Uhuru ndio linalokufaaa mawio tuachie sisi pole sana
 
usiponunua unadhani kampuni itakufa.ovyooo. unajua chanzo cha kuanzishwa kwa kanisa la luthelan? Unachukia mtu kwa kukaririshwa.thibitisha ufisadi wake bila kuacha shaka yoyote.
 
MzeePunch wewe kapunchike kivyako sie tunajari kushika dola kwanza kuondoa adui ccm, waliomo sio maadui wetu, adui yetu ni mfumo ulioleta umaskini.
 
MzeePunch

Usisome kabsaa Nyan ww tena unanuka mdomo toka hapa
 
Last edited by a moderator:
MzeePunch

Kwaiyo we ulitaka waandike ulichotaka wewe? Kweli we ndorobooo sibora ungejipepea nalo kuliko kuuleta huu uzi hapa.
 
Last edited by a moderator:
Huo ni uamuzi wako binafsi ambayo haina athari zozote kwa wengine.Uchaguzi wa kuwa chama gani nao ni uamuzi binafsi.uchaguzi wa kununua gaze nao ni uamuzi usiohitaji kutangazwa wala kuwa sehemu ya ushawishi habari unaoona mbaya kwako kwa wengine imetoa Elimu na ufafanuzi mpana zaidi
 
Acha kununua, nitafidia hiyo hasara mimi kwa kununua mawili mawili kila Alhamis, Naona huna akili timamu wewe....Mtu kashasema mikono yake misafi na ameeleza kuwa Rais ndiye aliyebariki sasa ulitaka Gazeti liandike nini?

Kuna kitu Nimegundua kwa Watanzania wengi, Tunakosa taarifa sahihi na tunategemea sana taarifa za kuambiwa na tunapenda sana kulishwa Umbeya hadi rohoni badala ya kuishia kinywani.
 
Lowassa mkuu wa mafisadi kivipi? Ndo matatizo ya kijifunzia siasa uzeeni, hebu kavute ugoro ulale kikongwe wewe
 
Hivi ni kwanini watu wa ccm mnapenda kujipachika uchadema?
 
Ngoja nikalitafute sasa


Sikujua hivyo. Basi, kuanzia leo sitakosa kusoma Gazeti la Mawio. Na pia nitachukua kadi ya CDM leo leo sambamba na wewe kuchana kadi ya CDM ili kuziba nafasi yako na kusiwe na pengo lolote na kura kwa wewe kujitoa. CDM na Ukawa Hoyeeeeeeeeeeee! Lowasa hoyeeeeeeeeeeeeeeeeee!
 
Back
Top Bottom