Morning_star
JF-Expert Member
- Apr 21, 2018
- 4,163
- 11,483
Nilisoma shule ya sekondari ya bweni wavulana tu. Wasichana na baadhi ya wavulana day! Karibu na bwalo la chakula kulikuwa na duka la shule! Sasa enzi hizo mimi nilikuwa miongoni mwa vijana masharobaro ambao mbele ya wasichana warembo wa day kuonekana unakula ugali maharagwe ilikuwa ni aibu.
Hivyo, mimi nilikuwa nawahi kabla ya kengere ya chakula kupigwa nachukua mfuko wa kaki na kikopo cha mafuta ya kula "superghee" (wazee wenzangu watakumbuka) naenda bwaroni nakata ugali naweka kwenye mfuko wa kaki na maharagwe kwenye hicho kikopo alafu najipitisha kwenye duka la shule kujionyesha kwa mabinti wakali kwamba natoka dukani.
Hao mabinti warembo walikuwa hawali ugali muda wa kula wanaenda duka la shule na kununua soda wakishushia na bites/keki/andazi n.k, basi! Sasa hile nafika dukani nakutana na nyomi ya warembo kama wanne hivyo kwa vile nilikuwa najulikana kwa usharobaro na vibinti vingi vilikuwa vinanikubali japo enzi hizo haya mambo ya kwichikwichi yalikuwa nadra sana na mpaka umpate lazima uwe mzoefu. Basi, wakanisimamisha wakaanza kuniongeresha na mimi namwaga swaggar za kibabe sio poa.
Sasa, huo ugali kwenye mfuko wa kaki niliwahi nikauchukua ukiwa wa moto ukaanza kulowanisha mfuko kwa chini! Duh! Nikauangalia nikaona unaanza kutokeza kutaka kudondoka nikautegemeza kwa mguu juu kidogo ya goti na kipindi hicho tulikuwa tunavaa sare ya kaptula hivyo ukagusana na ngozi moja kwa moja na kuniunguza huku story zimekolea uzalendo ukanishinda nikatoa mguu na ugali ukaanguka chini!!! 😆😂😂😂😂! Acha mabinti waanze kucheka!
Nilipigwa na butwaa kuuuokota siwezi na share yangu nimeishaichukua na nilikuwa njaa kibao! Walivyo watundu wakataka kujua kuna nini kwenye hicho kikopo cha superghee wakanipokonya na kufungua wakakuta maharagwe! I seeee! Ni ujinga lakini kwa foolish age hiyo nilipigwa na aibu! Hilo tukio lilisambaa shule nzima mpaka kesho nalikumbuka!
Hivyo, mimi nilikuwa nawahi kabla ya kengere ya chakula kupigwa nachukua mfuko wa kaki na kikopo cha mafuta ya kula "superghee" (wazee wenzangu watakumbuka) naenda bwaroni nakata ugali naweka kwenye mfuko wa kaki na maharagwe kwenye hicho kikopo alafu najipitisha kwenye duka la shule kujionyesha kwa mabinti wakali kwamba natoka dukani.
Hao mabinti warembo walikuwa hawali ugali muda wa kula wanaenda duka la shule na kununua soda wakishushia na bites/keki/andazi n.k, basi! Sasa hile nafika dukani nakutana na nyomi ya warembo kama wanne hivyo kwa vile nilikuwa najulikana kwa usharobaro na vibinti vingi vilikuwa vinanikubali japo enzi hizo haya mambo ya kwichikwichi yalikuwa nadra sana na mpaka umpate lazima uwe mzoefu. Basi, wakanisimamisha wakaanza kuniongeresha na mimi namwaga swaggar za kibabe sio poa.
Sasa, huo ugali kwenye mfuko wa kaki niliwahi nikauchukua ukiwa wa moto ukaanza kulowanisha mfuko kwa chini! Duh! Nikauangalia nikaona unaanza kutokeza kutaka kudondoka nikautegemeza kwa mguu juu kidogo ya goti na kipindi hicho tulikuwa tunavaa sare ya kaptula hivyo ukagusana na ngozi moja kwa moja na kuniunguza huku story zimekolea uzalendo ukanishinda nikatoa mguu na ugali ukaanguka chini!!! 😆😂😂😂😂! Acha mabinti waanze kucheka!
Nilipigwa na butwaa kuuuokota siwezi na share yangu nimeishaichukua na nilikuwa njaa kibao! Walivyo watundu wakataka kujua kuna nini kwenye hicho kikopo cha superghee wakanipokonya na kufungua wakakuta maharagwe! I seeee! Ni ujinga lakini kwa foolish age hiyo nilipigwa na aibu! Hilo tukio lilisambaa shule nzima mpaka kesho nalikumbuka!