"Sitaki dawa" ya Mentor ni fraud

"Sitaki dawa" ya Mentor ni fraud

Inashangaza sana aiseee....
Kiki ya kujitakia balaa..
Hivi inawezekana kweli kwa mtu kama Mentor kuleta uzi ambao unaogofya kiasi kile, eti kwakua anataka KIKI..!!?
Ebu ngoja niishie hapa aiseeee

Mkuu kwa sababu yoyote ile iwayo, sio sahihi kama kweli ni fiction.
 
Mkuu,
Ebu tufumbue macho nasisi tuzijue hizo unazo ziita sehem nyingi alizo jichanganya aiseeee...
Na unapo msemea mtu kama Mentor kutokua na ujasiri wa kusema ukweli wa kilicho msibu, hapa napata mashaka kidogo.
Kimsingi UKIMWI ni ungonjwa unao ogofya pasipo kujalisha umri, uwezo na jinsia. Hivyo kama nikweli lazima jamaa alipata mshtuko.
Na kuhusu kuleta issue yake hapa jamvini, bado naweza nikasema ni kitendo cha kijasiri tu.
Sasa wewe uliamini aliposema hataki dawa kabsaaa!!! Na amekataa kwenda kusoma kwa sababu ukimwi, labda kama afya yake ilikuwa na matatzo mengine kama ebola nk.
 
Na kaipata kweli...
Siku ya 3 leo nashindwa hata kuchangia chochote humu...narudia tu kusoma 'SITAKI DAWA'!


Nifah.PNG
 
Atakuwa bonge la kiazi. Huwezi kutafuta kick kwa ugonjwa kama AIDS bwana, si angetumia uhusika mwingine tu, tungemuelewa. Kama ni kick basi jamaa ni kiazi.

Unamkumbuka Taji Liundi?
 
Ni kweli kuna uwezekano mkubwa sana kuwa hii ni fiction. Ukisoma comment yangu ndefu kwenye ule uzi wake Mentor utaona kuwa nilionyesha mashaka yangu kuhusu ukweli wa habari yake. Nilitoa mfano wa Diagnosis iliyokuwa documented kwenye ile form yake haikuwa na uhusiano wa moja kwa moja na HIV/AIDS.

Hata hivyo, niliendelea kumpa ushauri kwa kumpa benefit of doubt.

Nafikiri nifupishe tu maelezo yangu kuwa kama kweli ile ni story ya kutunga, then amefanya kosa kubwa sana. He is very misinformed. Huyu Jamaa ni miongoni mwa watu ambao nimekuwa nikiwaona wanajitambua hapa JF. Nilimheshimu. Kwa hili, I repeat, kama ni utunzi, then nimemdharau sana. Intelligent people hawafanyi makosa ya kijinga kama hayo. Lakini kama ni mtu muelewa huwezi kutumia HIV/AIDS kama uchochoro wako wa kutokea. Alitakiwa ajue kuwa UKIMWI ni ugonjwa ambao bado global community ina-struggle kuondoa tatizo la unyanyapaa na ubaguzi kwa watu wanaoishi na VVU. Obviously, ana ufahamu mdogo na hakujishughulisha kufanya homework ili asipotoshe watu.

Mentor atakuwa ni mbaguzi kwa PLHA. Iko obvious na it seems that has subconsciously motivated him kuja na aina ile ya uzi.

If indeed he was playing with people's minds, then anatakiwa aombe msamaha. With his writing, amefanikiwa kuumiza hisia za watu, ikiwa ni pamoja na wale ambao tayari wanaishi na VVU. Kimsingi ni pigo kwenye mapambano ya UKIMWI. It is a disincentive!!

Naweka full stop hapa kwa kuomba kuwa wakuu tuweni makini na tunzi zetu. Tuwe tunafikiria nje ya box. Hata kams wakati mwingine nia zetu ni kufurahisha watu, basi tijitahidi tu tunzi zetu ziwe constructive na sio destructive.

Cheers!!!
 
Nimeimisi hii story ya ndugu yangu Mentor ambayo aliitoa tarehe 25/6/2016 kwa sababu nilikuwa kwenye majukumu mazito ya kumwagilia shamba la mapenzi. Ni hivi sasa nimepata kuisoma hii hadithi ambayo bwana Mentor kwa ustadi mkubwa ameweza kuudhihirishia umma kwamba amehathirika na ugonjwa UKIMWI.

Sijapitia comment zote maana zipo takribani 300 kuweza kudadavua kama kuna mtu aliweza kushtukia detail moja ndogo ambayo ina falsify story nzima na kuifanya kuwa ni ya uongo. Kuna sentensi kwenye story hii imeandikwa ........ "Nilifanikiwa kumaliza mapema nikatoa nakala kama walivyoelekeza; za kupeleka wizara ya elimu na za kutuma kwa barua pepe....."

Unless kama amekosea kuandika ila nimefanya confirmation na mtu wa pale wizarani na pasi na shaka amenithibitishia kabisa kwamba commonwealth scholarship zilizoombwa mwaka jana hazikupokelewa na wizara ya elimu. Hiyo tu inatosha kuifanya story hii kuwa fraud ya aina yake ambayo imetolewa kwa weledi mkubwa.

Lakini mimi binafsi sikutegemea kabisa kama bwana Mentor ambaye ni kati ya watu wenye upeo mkubwa kabisa, alishindwa vipi kudadafua ukweli wa hiyo sentensi hapo juu mpaka ije kumuumbua?

Lengo la thread yangu: Kwanza kabisa story yenyewe inasikitisha sana na najua wana JF wengi wamesikitika. Hivo basi kwa kuwa nimeweza kui falsify hii story ya Mentor napenda sasa kuchukua nafasi hii kuwaambia kwamba " Hii story ni ya uongo na ndugu yetu Mentor bado tunaye, mzima wa afya tele"....... Na wote tuseme Amen.... Mentor ni mzima na haitaji dawa kama kichwa cha thread yake kinavosema....

Kuna kikundi cha watu kinajaribu kuwachezea wenzao akili, their aim is to tyrannize JF members. They have not done it once but many times. Baada ya Mentor kuweka bandika lake wakaja na orodha ya wahanga wa Mentor. I know them and when the time comes I will divulge. X, X and X, I know the game you are playing.
 
Nilipoisoma hadithi yake, para ya kwanza tu nikajuwa ni ya kutunga nikaachana nayo.

Wajinga Ndiyo Waliwao.
 
Back
Top Bottom