Sishauri sana Rais Magufuli awe ana 'disclose' mara kwa mara 'findings' za TISS publicly kwani anawaharibia

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,542
108,877
Nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuwa na taarifa nyingi na za ndani ( Nyeti ) kabisa kuhusu mambo mbalimbali ya nchi na pia nawapongeza mno TISS kwa Utendaji wao wa Kutukuka kwa sasa ila nasikitika na sishauri sana Mheshimiwa Rais awe anapenda mno kuzizungumzia hadharani katika hadhira.

Taarifa za Ugomvi wa Waziri wa Afya na Katibu Mkuu mpya wa sasa ( wote wanatoka Mkoani Tanga ), Ugomvi wa DC wa Gairo na Mbunge wa Gairo hadi wanatukanana Matusi ya Nguoni ya Viungo vya waliotuzaa ( Mama zetu Wapendwa ) pamoja na Mtifuano wa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma na DC wa Dodoma na hadi Siri za ndani kabisa juu ya Sakata zima la Dhahabu ambalo pia lipo katika Uchunguzi zaidi kwa sasa sidhani kama zilipashwa kuwa ' disclosed publicly ' katika hadhira kwani ' technically ' kabisa linawaharibia mno Watendaji wake Kiusalama TISS.

Sitaki kuamini kwamba Mheshimiwa Rais huwa hawezi Kutunza Siri labda ndiyo udhaifu wake mkubwa ila nimwombe tu sasa TISS DG Dkt. Kipilimba ajitahidi kadri awezavyo aweze ' Kumfunda ' Bosi wake hasa juu ya suala zima la Kunyamaza na kutopenda ' Kuropoka ' mambo mengine ya ndani ( Nyeti ) mbele ya Umma kwani yanaharibu misingi ya Uchunguzi na Kuudhoofisha ' Utendaji ' wa Kisiri. Nina uhakika japo ' Poti ' wangu IGP Sirro amesifiwa sana na Mheshimiwa Rais kwa ' Utendaji ' wake ila nina uhakika hata Yeye pia Kimoyomoyo hajapendezwa na jinsi Rais alivyokuwa anatiririka na anaserereka kulihadithia ' Sakata ' zima la Dhahabu.

Nawasilisha.
 
Nimemsikia na mimi hasa baada ya kueleza kila kitu kuhusu wale wafanyabishara wa madini na polisi walio kamatwa.

Akaja kueleza kuwa alikuwa anafuatilia Meseji za Ummy mwalimu na msaidizi wake jinsi walivyokuwa wanagombana.

Akaja kueleza meseji za mbunge mmoja wa ccm akitukanana na mmoja wa mke wa mtumishi wa serikali.

Akaja kueleza hazina ya dhahabu iliyopo BOT, hapa akashindwa hata kufafanua maana licha ya kujishitukia pia alionekana hana uelewa mpana kuhusu hazina ya dhahabu na faida zake kwenye uchumi

Sasa nimeelewa kwa nini analala na mafaili kwenye kitanda, kumbe ya kudukua mawasiliano ya wasaidizi wake.
 
Kutokana na maelezo yake inaonekana serikali inashirikiana na mitandao ya simu kudukua mawasiliano ya watu kitu ambacho ni very serious.

Sasa ili kuepukana na huu upuuzi, hakikisha kama una jambo la siri usipige simu au kutuma message kwa mtandao kawaida, tumia huduma kama Whatsapp au Telegram maana ipo end to end encrypted, chochote kikitokea unajua kabisa aliyekuchomea ni yule unayeongea naye.

Kama sio hivyo basi watakua wameweka mtu anayekufuatilia physically na ana mitambo mbalimbali ya kuhakikisha anajua kila unachokifanya.
 
Kutokana na maelezo yake inaonekana serikali inashirikiana na mitandao ya simu kudukua mawasiliano ya watu kitu ambacho ni very serious.

Sasa ili kuepukana na huu upuuzi, hakikisha kama una jambo la siri usipige simu au kutuma message kwa mtandao kawaida, tumia huduma kama Whatsapp au Telegram maana ipo end to end encrypted, chochote kikitokea unajua kabisa aliyekuchomea ni yule unayeongea naye.

Kama sio hivyo basi watakua wameweka mtu anayekufuatilia physically na ana mitambo mbalimbali ya kuhakikisha anajua kila unachokifanya.
Kiongozi ngazi ya mkoa mpaka taifa niliwah sikia mahal wanasema wanafatiliwa sana kila boss mfano rso anamtu anamfata kila kona bila yeye kumjua na RPC kadhalika wazir rco

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom