Sirro: Sitosahau Askari walipopigwa risasi Kibiti

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,544

IGP Mstaafu Balozi Simon Sirro baada ya kuagwa rasmi na Jeshi la Polisi leo Dar es salaam amesimulia tukio ambalo hatolisahau akiwa kazini ambalo amesema ni la Askari Polisi kupigwa risasi na Majambazi baada ya kushambulia kwa risasi gari la Polisi katika Kijiji cha Uchembe, Kata ya Mjawa Wilayani Kibiti, Mkoa wa Pwani.

Sirro amesema “Tuliwapata Wahusika na bahati mbaya na wao walishatangulia mbele ya haki, hili ni tukio ambalo sitolisahau, ukienda ukakuta Askari tisa wote wamepigwa risasi wamelala sio jambo dogo”
 
Asili ya kupigwa risasi kwa mkupuo ilikuwa ninini?
Ina maana wote tisa walikuwa off guard?
Waliowaua hao askari nao walikufaje wote?
Maswali ni mengi
Askari walikuwa wanaenda/wanatoka kwenye lindo walikuwa kwenye difenda la polisi ndipo mdunguaji akampiga risasi dereva wakati gari lipo kwenye mwendo likapinduka askari wakajeruhiwa ndipo walipovamiwa pale na kuanza kupigwa risasi kwa ukaribu zaidi ila kuna askari mmoja alipona baada ya kujifanya amefariki baada ya wale wadunguaji kuwafikia pale chini, hii ilikuwa kibiti miaka ya nyuma kidogo.
 
"Lisu ni zaidi ya yesu"

Hii kauli Hapana, sio sahihi, hata kusoma inasisimua, ila sababu umeandika yesu kwa herufi ndogo naamini haumaanishi Yesu ninayemfaham mimi.
Huyohuyo mnazareth anayedaiwa kusulubiwa na kufufuka baada ya kifo,misumari mitatu mguuni,na mikono akamlilia baba yake 'mbona umeniacha' wakati lisu risasi 16 mwilini na bado anagonga madem wa kibelgiji
 
Askari walikuwa wanaenda/wanatoka kwenye lindo walikuwa kwenye difenda la polisi ndipo mdunguaji akampiga risasi dereva wakati gari lipo kwenye mwendo likapinduka askari wakajeruhiwa ndipo walipovamiwa pale na kuanza kupigwa risasi kwa ukaribu zaidi ila kuna askari mmoja alipona baada ya kujifanya amefariki baada ya wale wadunguaji kuwafikia pale chini, hii ilikuwa kibiti miaka ya nyuma kidogo.
Asante sana kwa ufafanuzi
 

IGP Mstaafu Balozi Simon Sirro baada ya kuagwa rasmi na Jeshi la Polisi leo Dar es salaam amesimulia tukio ambalo hatolisahau akiwa kazini ambalo amesema ni la Askari Polisi kupigwa risasi na Majambazi baada ya kushambulia kwa risasi gari la Polisi katika Kijiji cha Uchembe, Kata ya Mjawa Wilayani Kibiti, Mkoa wa Pwani.

Sirro amesema “Tuliwapata Wahusika na bahati mbaya na wao walishatangulia mbele ya haki, hili ni tukio ambalo sitolisahau, ukienda ukakuta Askari tisa wote wamepigwa risasi wamelala sio jambo dogo”
Kwa kweli hili lilikuwa ni tukio baya, ila niliuliza Mauaji ya Polisi wetu ni Ujambazi, Ugaidi au Retaliation? Nini kifanyike kukomesha hali hii? , jeshi la polisi lilijibu mapigo with full force na kuproduce bad karma nyingine!.
P
 
Yani askari 9, wakiwa kwenye mwendo, na silaha zao wauwawe wote, wakati Lisu, mwenyewe askari wa kutosha, wataalam, risasi 40 akiwa kwenye mwendo, yupo hai.
Swali zuri sana hili! Labda wale wataalam wa 'Ukatili' wataweza kutoa ufafanuzi na mlinganisho vizuri-Wakiacha mungu wao!
 
Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Polisi Mstaafu, Simon Sirro ametaja changamoto nne alizokabiliana nazo wakati wa utumishi wake ikiwamo mauaji ya Kibiti.

Sirro ametoa kauli hiyo leo Jumatano Mei 10, 2023 wakati sherehe za kumuaga baada ya kustaafu rasmi utumishi katika kipolisi, zilizofanyika Chuo cha Taaluma cha Polisi Dar es Salaam (DPA), kilichopo maeneo ya Kurasini jijini hapa.

“Kulikuwa na changamoto ya Kibiti, ilikuwa ni shida, hata viongozi wa siasa walishindwa kwenda pale nikasema hii ni lazima nipambane nalo nawashukuru sana wananchi kwa kunipa support (ushirikiano) na mwisho nchi yetu ipo salama,”amesema Sirro.

Aidha Sirro ameyataja matukio ya unyang’anyi kwa kutumia silaha pia ilikuwa mojawapo ya changamoto wakati anateuliwa kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi na anajivunia kuiacha nchi ikiwa salama.

“Mnajua, Dar es Salaam hii watu walikuwa hawakai mpaka asubuhi (kukesha) lakini sasa hivi maduka yanafunguliwa mpaka asubuhi,”amesema Sirro.

“Mambo ya albino (mauaji ya albino) yalikuwa tatizo lakini ilipungua na pia kuliibuka vikundi vya ‘panya road’ na panya buku lakini mwisho wa siku tulienda sawa, naomba mnipigie makofi,”amemalizia hivyo akitabasamu baada ya kusema changamoto ambazo hatakuja kuzisahau.

Sirro ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe ameagwa kwa kukagua gwaride maalum la heshima ikiwa ni ishara ya kumuaga baada ya kulitumikia jeshi hilo katika nyadhifa mbalimbali kwa miaka 30.
Akiwa mwenye uso wa bashasha Sirro aliwasili kwenye viwanja vya chuo cha mafunzo cha polisi Kurasini ambapo moja kwa moja alianza kukagua gwaride hilo la heshima.

Mara baada ya kumaliza kukagua gwaride IGP Mstaafu Sirro alipanda kwenye gari maalum na kupita katikati ya askari waliokuwa wamejipanga kama ishara ya kumuaga kijeshi.

Gari hilo la wazi lilisukumwa na makamishna waandamizi wa polisi ikiwa ni ishara ya kumuaga rasmi kiutoka kwenye utumishi wa jeshi hilo ambalo kimsingi amemaliza utumishi wake toka machi mwaka huu.

Baada ya shughuli hiyo ya kijeshi kukamilika Mkuu wa Jeshi la Polisi, Camilius Wambura alimkabidhi Sirro kadi ya kustaafu jeshi hilo inayomtambulisha kwa sasa kama raia.

Akiipokea kadi hiyo Sirro amewaonyesha waandishi wa habari akisema, “Nimepewa kadi hii ya kustaafu jeshi la polisi sasa hivi mimi ni raia ambaye ninategemea kupata huduma kutoka katika jeshi hili.”

Mbali na kadi hiyo IGP Wambura amemkabidhi Sirro gari jipya aina ya Toyota Land Cruiser Prado TX kama zawadi ya kustaafu kulitumikia jeshi hilo.

MWANANCHI
 
Back
Top Bottom