Siri za nchi ni zipi (mambo ya aina gani)

Siri za nchi ni zipi (mambo ya aina gani)

Sijasema zitajwe.

Nataka kujua tu, ni mambo ya aina gani?
Mara nyingi ni mambo(au taarifa) ambayo hayatakiwi (Ni marufuku) kuwekwa hadharani (public) na yamezuiliwa kutangazwa na yanatakiwa kubaki kwa wale wachache walioaminiwa au wahusika tu.
 
Masuala ya ulinzi na usalama wa taifa , mikakati ya kijeshi, idadi halisi ya silaha, mipango ya kukabiliana na uvamizi.

Suala lingine ninalofahamu ni shughuli za kijasusi, mbinu za upelelezi, mawasiliano ya siri kati ya mashirika ya usalama.

Nb: ni kwa nchi za wenzetu tu ndiyo naelewa hayo mambo huwa ni siri.
 
Zamani Taarifa za Siri za Kiserikali zilifungwa kwenye bahasha mbili za khaki na kufungwa kwa lakiri halafu zinagongwa mhuri wa Confidential. Sijui siku hizi za kidigitali wanafanyaje.
Vitu sensitive havipitishwi kwenye digitali, ikibidi basi ni chini ya uangalizi mkubwa sana.
 
Hata mimi huwa najiuliza sana hilo swali, inawezekanaje jambo jema likawa siri kiasi cha kulindwa kwa nguvu kubwa kiasi iko wakati nchi ni yetu sote???
Adui akijua baadhi ya taarifa zako umekwisha!
Mfano, mtu akiondoka na database ya waathirika wa HIV/AIDS, .... usalama wa nchi unaweza kuwa hatarini.
Ndio maana wahuni wafanya hacking na kukimbia na mzigo kuuza
 
Adui akijua baadhi ya taarifa zako umekwisha!
Mfano, mtu akiondoka na database ya waathirika wa HIV/AIDS, .... usalama wa nchi unaweza kuwa hatarini.
Ndio maana wahuni wafanya hacking na kukimbia na mzigo kuuza
Issue ya Data za HIV excluding personal details sio Siri, acha mikwara.
 
  • Mahandaki ya makombora ya kinyuklia huko milima ya Udzungwa
  • Handaki la Ikulu linalotokomea baharini kwenye nyambizi ya raisi
  • Maafisa usalama wanaojifanya waokota makopo
  • Wauza kahawa na madafu wa TISS
  • Ongezea zingine........
 
Adui akijua baadhi ya taarifa zako umekwisha!
Mfano, mtu akiondoka na database ya waathirika wa HIV/AIDS, .... usalama wa nchi unaweza kuwa hatarini.
Ndio maana wahuni wafanya hacking na kukimbia na mzigo kuuza
Databse yote ya waathirika wa HIV/AIDS wanayo Marekani kupitia mashirika yao ya EGPAF, PEPFAR na USAID.
 
  • Mahandaki ya makombora ya kinyuklia huko milima ya Udzungwa
  • Handaki la Ikulu linalotokomea baharini kwenye nyambizi ya raisi
  • Maafisa usalama wanaojifanya waokota makopo
  • Wauza kahawa na madafu wa TISS
  • Ongezea zingine........
Hii inasaidia nini, kwenye ulimwengu wa DRONES na wananchi wasiokutaka??
 
1. Rais na mwenza wake kujamiiana.

2. Kutousema/kuutangaza mngurumo autoao kiongozi wa nchi when he/she answers the call of nature (hii huwahusu walinzi).

Na kadhalika.

adriz ze GOAT.
Sioni hapo 1-2 kama kuna kitu kinachohusiana na maslahi ya nchi bali ni faragha ya mhusika binafsi na halafu mbona hayo 1-2 watu wote hufanya?
 
  • Mahandaki ya makombora ya kinyuklia huko milima ya Udzungwa
  • Handaki la Ikulu linalotokomea baharini kwenye nyambizi ya raisi
  • Maafisa usalama wanaojifanya waokota makopo
  • Wauza kahawa na madafu wa TISS
  • Ongezea zingine........
Kwamba tuna Nuclear au?
 
Back
Top Bottom