Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,939
- 831,436
Pengine walikuwa na gesti humohumoHii nayo ni sheeda! Ofisi nzima mimba!
Pengine walikuwa na gesti humohumoHii nayo ni sheeda! Ofisi nzima mimba!
Tatizo la watumishi wengi katika Tassisi za umma bado hawajafahamu kuwa enzi za Awamu ya Nne zimekwisha. Walijisahau sana. Tumezoea kuona wafanyabiashara wakiwa na ukwasi mkubwa lakini kwa miaka kumi iliyopita hali ilikuwa ni tofauti kabisa. Ndio maana inakuwa vigumu sana kuwashawishi vijana wanaomaliza vyuo kuwa ajira binafsi inalipa wakati ukienda pale TRA, NIDA, SUMATRA, EWURA nk unakuwa tajiri wa kutupwa. Watu tujiulize kwanini Askari Polisi wanahonga ili kupata nafasi ya kuwa TRAFIKI pamoja na kupigwa na jua na mvua! KAMA INAVYOLIPA KUJIUNGA NA TIGO, NDIVYO INAVYOLIPA KUWA MFANYAKAZI KATIKA TAASISI YA UMMA.View attachment 319505
Baadhi ya wafanyakazi wa mamlaka ya vitambulisho(NIDA) waliokumbwa na "Operesheni tumbua majipu" walikutwa na mali nyingi "kupita maelezo" kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga.
Operesheni hiyo ambayo inatekelezwa tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, juzi ilimkumba Dickson Maimu, ambaye alikuwa Mkurugenzi wa NIDA, Joseph Makani(Mkurugenzi wa Tehama Rahel Mapande (Ofisa Ugavi mkuu)< Sabrina Nyoni (Mkurugenzi wa sheria) na George Ntalima ambaye ni Ofisa Usafirishaji. Waziri wa mambo ya ndani Charles Kitwanga alisema hatua ya kutengua na kusimamisha watumishi hao imechukuliwa baada ya uchunguzi wa hali ya juu kwenye mamlaka hiyo.
"Walipoulizwa walisema wamepata mali hizo kutokana na mikopo na mali walizonazo" alisema. Waziri huyo alisema uchunguzi zaidi unajielekeza kujua ni jinsi gani sh 180 bilioni zilitumika kusajili watu milioni 6 tu na kati yao kuwapatia vitambulisho watu milioni 2.5 tu.
Mbali na kuwaweka kando watendaji hao, Rais aliagiza vyombo mbalimbali kufanya uchunguzi wa matumizi ya fedha katika mamlaka hiyo ikiwemo TAKUKURU, PPRA na Ofisi ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali.
Chanzo: Dar es salaam wire
Andika mkuu tuokoe kodi zetu kuchezewa na wajanja, hapo kwenye mpunga usisite kunialika.Sio hivyo tu mkuu, ilitakiwa RITA, NIDA, na vitambulisho vya Taifa kuunganishwa kwa pamoja. Hizi ofisi zina Kazi zinazoshabihiana sana. Ngoja niandike proposal kuhusu hiyo kitu nami nile mpunga
Hapa karibu yetu hakuna bar... Labda kwinginekoNa kuhonga wahudumu wa baa zilizo karibu na NIDA
Si wana ofisi nyingine pale karibu na ubalozi wa ufaransa? Halafu kuna ile bar ya Gupta?Hapa karibu yetu hakuna bar... Labda kwingineko
Inaitwa Okta mkuu.Nashangaa anakanusha wakati zipo baa 3.Si wana ofisi nyingine pale karibu na ubalozi wa ufaransa? Halafu kuna ile bar ya Gupta?
Tawiree !!! Mm au hawa majizi ya NIDA?Tawiiree
Kuna watu wanajua kuitafuna hii nchi.Ukiambiwa kula nchi sio kulamba udongo ni kama hivi.Kitakuwa mali ya Jamhuri ya Tanganyika hicho
Mshana unapenda bar sio ?Kila bar ya hapa town wajua...Si wana ofisi nyingine pale karibu na ubalozi wa ufaransa? Halafu kuna ile bar ya Gupta?
Kweli kabisa aiseeKuna watu wanajua kuitafuna hii nchi.Ukiambiwa kula nchi sio kulamba udongo ni kama hivi.
pamoja na majina ya wahudumu hadi nyumba wanazoishi hahahaha
Kuna watu hawana huruma na wananchi wenzao kama fisi vile ukiwakabidhi bucha watakula mpaka lile gogo la kucharangia.Kweli kabisa aisee
Rahel Mapande (Ofisa Ugavi mkuu)< Sabrina Nyoni (Mkurugenzi wa sheria)