Siri ya Mahakama ya Kadhi yafichuka

Siri ya Mahakama ya Kadhi yafichuka

Kwa hiyo unakubali kuwa hiyo technique inatumiwa na wafuasi wa wamissionary?
 
Unakosea kusema maneno kma hayo...
Mtu hutenda dhambi kwa matamanio yake ila sio kila muislam yuko hvo...
 
yaani sijawahi kuona watu wanafki kama waislam, wanaitaka sharia kishabiki tu ila kiuhalisia hawawezi kuishi maisha chini ya sharia, kila siku tunabanana nao kwenye vijiwe vya kitimoto na pombe lakini wakija hapa ndio wako mstari wa mbele kushabikia mahakama. Ahahahahaaa duuuh

Unakosea tena sana
 
CCM imelikoroga .Ni lazima ilinywe . Waislam wanadai mahakama walitoahidiwa na serikali ya CCM inayoungwa mkono kwa kiasi kikubwa na wakatoliki ,waangilikana na waluteri ;hasa viongozi wa makanisa haya. Kwa hiyo haya makanisa kupita chama chao cha Christian Councel Motion (CCM) kiliwaahidi waislam mwaka 2010 kuwa kitawapatia mahakama ya kadhi. Sasa nashangaa hao watu ndani ya CCM wanaojenga chuki za kuikataa mahakama ya kadhi.Tena kwa hoja hafifu za gharama za uendeshaji.

Na waislam nao wamezidi unafiki mabilioni ya pesa yanaliwa na mafisadi tangu awamu ya Mwinyi lakini hawajawahi hata kukemea kuhusu ufisadi unaofanya na hii serikali chonganishi.Haya mabilioni kama yangetumika vizuri yangeweza kugharamikia mahakama ya kadhi. Badala yake unamkuta mwanaharakati wa kiislam anatokwa na mapovu akisimulia memorundam of understanding(waraka wa maridhiano) tena unaohusu nchi wafadhili waliogoma kupitisha misaada yao serikalini kutokana na wizi,hivyo wakasema watakua wanasaidia makanisa yenye miradi ya huduma za kijamii.MOU haihusiani na kodi za watanzania ni sawa na MOU ya Tanzania na Kuweit ya kujenga visima na Misikit maeneo yenye waislam ni maridhiano tu na hawalazimishwi na mtu yeyote na haina athari kwa mtu yeyote.
Mahakama ya kadhi kwangu mimi naona yanafaida kwa wale watakaopata ajira lakini kwa yule atakayekuwa ni mpiga debe maskini asiye na hata kibanda cha bata hataona mabadiliko yoyote ya kiuchumi.
Tuwaache wanaotaka mahakama ya kupeana talaka na kugawana mali wapewe tu.

Wakristo jitafutieni miradi mingine ya kimaendeleo nayo ilipiwe na serikali ili ndoa ziimarike kwani umaskini ndio chanzo cha talaka na migogoro ya ndoa.

Cha msingi ni serikali kuanza kutoa ruzuku zilizo sawa kwa taasisi za dini ili wanaotaka mahakama iwe sawa na wanaotaka kuanzisha SACOSS iwe sawa.

Hakuna haja ya kugombana na waislam kwa sababu ya mahakama ya kadhi kwa kisingizio cha gharama.
 
Kama Mungu wa Israel aishivyo, Hakuna Kadhi wala Kazi Tanzania.
 
tena kipengele no 4.kuhusu 'siri ya mahakama ya kadhi kikitumika vizuri inaweza kuwa njia kuu ya kueneza imani yao kwn maeneo ambayo haipo. hili swali huwa najiuliza cpat jibu. je, kwa yale maeneo ambayo waislamu hawapo itakuwaje?
 
proisra

Umeandika meeengi kama huna ubongo vile. Sema mahakama ya kadhi ianzishwe ila ijigharamie yenyewe ingetosha. Ila ni kwanini ijigharamie yenyewe na inatoa huduma kwa wananchi? Ushani tibua na akili yako ndogo.

Inatoa huduma kwa wananchi wapi!? na kama inatoa huduma kwa wananchi kwani zilizopo zinatoa huduma kwa nani..!? na hii misikiti mnayoijenga kila kukicha mnashindwa nini kujenga hizo mahakama na mkaziendesha wenyewe? but mnawafadhili wengi wa kiarabu waombeni wawajengee kama wanavyowajengea misikiti...!!!
 
Last edited by a moderator:
To a muslim is a mater...whats we need is mahakama ya kadh...lakin hata tukipewa sio solution..nchi imeunndwa na misingi ya Berlin Conference that is...serikali...elimu na ukristo..ni kitu kimoja kwa makoloni yote...sasa hapa kwene elimu wameona aibu..waislam nao wanasoma siku hizi lakin hapa kweneUKRISTO NA SERIKALI..hapashikiki wala hapakamatiki...sie tutapiga kelele..tu lakin akina sheh Ponda watalambwa risasi na jela watakwenda...thus situation inaendelea hvyo...ukiangalia kigezo cha waislam kunyimwa mahakama ya kadhi is MINORITY..yaani sie ni wachache sana..but wasanii wameingizwa kwene katiba..wachora katuni wameingizwa kwene katiba..hivi kweli....hii sio sawasawa...anaebisha abushe tu..zamani kabla ya ukolon waislam ndio waliokua wakitumia lugha ya maandishi kuwasilian kabla ya kuja wajeruman...wapagan hawakujua kusoma wala kuandika..wajeruman walipoingia na vipengele vyao vya berlin conference waliamua kufuta shule zote za waislam na kuanzisha shule kanisa yaani SEMINARY wakawanyanyasa sana waislam..wakawafanya watumwa...mpaka waisalam wakaamua kuanzisha Resistance..kupinga dhulma walizokua wakifanyiwa waislam..akina SHEIKH ABUSHIR NA BWANA KHERI..huko Pangan tanga..Akina Suleiman wanaanzisha majimaji war..yte haya ni kupinga dhulma dhidi yao..mpaka miaka ya 1920..1960s akina marehem sheikh Sykes..na wengne wengi pale jijini tanga wanaamua kumuwezesha hyu kijana ambae anaona uchungu na waislam wamtume aende UN akapewe uhuru kwa kua nchi ikilikua under Mandatory territory..mpaka Nyerer anafuatilia uhuru huki UN kumbe nae amepandikizwa hatima yake anakataa ujenz wa chuo.kikuu cha Kiislam hapa nchini..na kuendeleza unyonyaji dhidi ya waislam na kuzidi kudidimiza maendeleo kwene miji ya waislam..ikiwemo Tanga .vuwanda vyote vikabaki magofu..kama mimi Muongo nenda tanga ukaangalie kwa macho yako hayo magofu ya viwanda.....Sasa hili swala la ukandamizaji dhidi ya uislam halita kwisha wandugu..na litaendelea mpaka siku ya kiama
 
Nitafurahi kama kuna mwana JF ataeleza muundo wa mahakama ya kadhi utakavyokuwa. Hii itasaidia kutupatia uelewa wale ambao hatujui. Vinginevyo tutabaki kutukanana tu.
Tafadhali naomba jibu.
 
Mtoa mada umenena vyema kabisa mahakama ya kadhi iwepo lakini iendeshwe kwa gharama za waislam na si kwa gharama za selikari
 
Wakatoliki ,waluteri na waangilikana kwa hili la kupinga mahakama ya kadhi hawajafikiria sawa sawa.
Ni wajibu wa serikali kusimamia vyombo vya kutoa haki ikiwa ni pamoja na mahakama ya kadhi.
Serikali ikiiianzisha mahakama hii itakua na uwezo wa kizisimamia vizuri na kuepusha migongano na vurugu miongoni mwa waislam.Na ikumbukwe kuwa waislam wakigombana wenyewe kwa wenyewe hasira zao hufika kwenye kuchoma makanisa kwa sababu kuna kundi kitatuhumu kundi lingine kuwa linatumiwa na kanisa.

Na pia hao wakristo wanaoonea huruma pesa za serikali wakumbuke kuwa kikinuka gharama za kununua mabomu na risasi ni kubwa kuliko kutoa ajira kwa waislam wenye ilm ya sharia ili watoe hukm kwa waislam wenzao kwa mambo ya kijamii.
Tena itakua ni vizuri sana kupunguza malalamiko ya kudhulumiana na rushwa za mahakama hizi za serikali zilizojaa uonevu na sheria zisizozingatia mahitaji ya kiislam katika ndoa zao.

Naunga mkono mahakama ya kadhi kwa asilimia mia moja.
 
proisra

Umeandika meeengi kama huna ubongo vile. Sema mahakama ya kadhi ianzishwe ila ijigharamie yenyewe ingetosha. Ila ni kwanini ijigharamie yenyewe na inatoa huduma kwa wananchi? Ushani tibua na akili yako ndogo.
Nawewe pia ubongo wako mfupi, nani kapinga kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi? tunachopinga ni kuwekwa kwenye katiba ya nchi. Anzisheni wenyewe kwenye nyumba zenu za ibada hakuna atakayewaingilia.
 
Huyo ni mjinga atabaki kusema anaonewa......tanzania ni nchi isiyokuwa na dini....mkisharuhusu udini,mjue kwamba hata wasukuma nao wataomba warudishiwe utawala wao wa kijadi na watemi watambuliwe kisheria.pia serikali itambue kwamba wachawi wapo na uchawi upo hivyo kuwe na mahakama ya wachawi.maana hili taifa linataka kuvurugwa na ndugu zetu waislamu masrahi.
 
Wakatoliki ,waluteri na waangilikana kwa hili la kupinga mahakama ya kadhi hawajafikiria sawa sawa.
Ni wajibu wa serikali kusimamia vyombo vya kutoa haki ikiwa ni pamoja na mahakama ya kadhi.
Serikali ikiiianzisha mahakama hii itakua na uwezo wa kizisimamia vizuri na kuepusha migongano na vurugu miongoni mwa waislam.Na ikumbukwe kuwa waislam wakigombana wenyewe kwa wenyewe hasira zao hufika kwenye kuchoma makanisa kwa sababu kuna kundi kitatuhumu kundi lingine kuwa linatumiwa na kanisa.

Na pia hao wakristo wanaoonea huruma pesa za serikali wakumbuke kuwa kikinuka gharama za kununua mabomu na risasi ni kubwa kuliko kutoa ajira kwa waislam wenye ilm ya sharia ili watoe hukm kwa waislam wenzao kwa mambo ya kijamii.
Tena itakua ni vizuri sana kupunguza malalamiko ya kudhulumiana na rushwa za mahakama hizi za serikali zilizojaa uonevu na sheria zisizozingatia mahitaji ya kiislam katika ndoa zao.

Naunga mkono mahakama ya kadhi kwa asilimia mia moja.

Wewe nawe akili zake tupu kabisa, yaani kwamaana wakigombana wanachoma makanisa ndo waogopwe wapewe mahakama yao?

Kwahiyo wapewe mahakama ya kadhi kwamaana kuna vijana wao wengi walo soma sheria wapo mtaani unaogopa wataleta vurugu? Kwani hakuna vijana wengine wasio wa imani hiyo waliosoma sheria nao wapo mtaani?

Kwahiyo wapewe mahakama ya kadhi kwamaana mahakama za serikali zina dhuluma na rushwa, kwani kwenye hizo mahakama za serikali hakuna watendaji waimani yao?
1000 digits sikudhani kuwa una akili fupi kiasi hiki.
 
Last edited by a moderator:
mnahangaika bure mahakama inakaa kwenye Katiba siyo kwenye sheria, ilishakula kwetu hiyo
 
Maelezo marefu ila UJINGA tuu ulioandika! Serikali haina dini vp mbona wasile kiapo kimya kimya wakiteuliwa kwenye nyadhifa mpya? Hujui hata kuwa UPAGANI nao ni Dini?
Tatizo ujinga wewe ndo uliokujaa, Katiba iko wazi Serikali haina dini ila inatambua kuwa wananchi wana dini zao sasa unawekaje mambo ya dini nyingine kwenye katiba wakati serikali haina dini.
 
Hii mada ya mahakama ya kadhi inaibua hisia za kidini sana, tusipoangalia tunaweza kugawanyika kwa jambo ambalo si la kimaendeleo bali la kiimani zaidi. Hakuna aliyena ushahidi usioacha shaka kwamba huko kwa Mungu kukoje. Suala hili ukijaribu kuliangalia lililetwa na wanasiasa hasa waccm ili kuwarubuni wenzetu wa kiislamu baada ya kushindwa kuwapa huduma bora za kijamii. Matokeo yake watu hawajili zaidi huduma za kijamii bali wanataka mahakama ili washitakiane na wakose muda wa kuulizia maendeleo. Hapa tulipofikia watanzania hatuna namna, kama ni mbegu sasa imeota hatuna jinsi bali kuvuna. Na kwa bahati mbaya wenzetu waislam hawataki chochote zaidi ya mahakama ya kadhi. Basi wapewe kwani hakuna jinsi bali wahakikishe mahakama hiyo ifanye kwa mujibu wa sheria za kiimani na sio tuanza kuona tena mlundikano wa kesi, majaji kuanza kula rushwa kama hizi tulizozoea.

Angalizo kwa ndugu zetu waislamu, hivi ni kweli huduma nyingine muhimu za kijamii kama maji safi, elimu, afya bora zimewatosheleza na hivyo kilichobakia ni mahakama ya kadhi tu!!? Hamuoni kama mnaipa picha mbaya jamii ya kiislamu kwamba huduma za kijamii sio kipaombele chenu bali kuna nakisi ya uadilifu kwenye jamii ya kiislamu kiasi kwamba mambo mengine si muhimu sana bali mahakama ya kadhi ili mshitakiane? Ni kweli mna upungufu mkubwa hivyo wa maadili mpaka muhitaji mahakama yenu mbali na hizi zilizopo? Kwa mazingira haya ya makundi mengine ya wananchi kukwazika na hili hitaji lenu, mna uhakika wa kuiendesha mahakama yenu kwa uadilifu wa kiimani kwa kiwango hicho, ama mnataka kuleta tena mtafuruku mwingine kwenye jamii pindi vishoka wa imani watakapoingia kwenye mahakama yenu?
 
Back
Top Bottom