Siri mpya zafichuka kuhusu ndoa ya dk.slaa , josephine

Gumzo

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
211
7
SAKATA la ndoa ya Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa na mchumba wake, Josephine Mshumbushi limefichua siri mpya kuhusu maisha yao ya kimapenzi.
Siri hiyo, inahusu historia ya mateso aliyowahi kuyapata Dk. Slaa kutoka kwa mwanamke ambaye jina lake linahifadhiwa, kabla ya kuamua kuinua mikono na kudondokea kwa Josephine.
Imebainika kuwa wakati Slaa analo lake la kuteswa na mwanamke wake, Josephine naye ana siri inayomuumiza kutokana na yale aliyotendewa na mwanaume wake (jina tunalo), aliyekuwa naye kabla ya kutua kwa mwanasiasa huyo.

HABARI KAMILI BOFYA HAPA GUMZO LA JIJI: SIRI MPYA ZAFICHUKA KUHUSU NDOA YA DK.SLAA , JOSEPHINE
Josephine, amekiri wazi kwamba mwanaume wake aliyepita, alimtesa na kumdhalilisha kiasi cha kumfanya kuchangia mapenzi na wasaidizi wa kazi za nyumbani (ma-house girl).
Dk. Slaa, alipozungumza na mwandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwake, Tegeta, Dar es Salaam, alikiri kuteswa na mwanamke aliyewahi kuwa naye kabla ya Josephine kisha akaelekeza kila kitu kuhusu maisha yao na uhusiano wao, kizungumzwe na mchumba wake huyo.
Akieleza mambo kwa mtindo wa kuchambua, Josephine alisema, haoni sababu ya kutoolewa na Dk. Slaa, kwani anampenda kupita kiasi na kwamba kiongozi huyo alikutatanaye Dodoma akiwa amekondeana kwa mawazo kutokana na mateso ya mwanamke huyo (jina bado tunalihifadhi).
“Mimi na Dk. Slaa tulikutana bungeni. Mimi nilikuwa pale kama mtumishi wa bunge, yeye alikuwa pale kama mbunge wa Jimbo la Karatu. Uhusiano wetu ulianza kule. Sasa nimemtunza na amenenepeana watu wanaanza kumtamani. Huyu ni wangu.
“Watu wamuone Dk. Slaa hivi sasa, hapo kabla alikuwa anateseka. Hakuwa na mwili huu ambao watu wanamuona nao. Mwanamke wake wa zamani alikuwa anamnyanyasa, kila siku baba wa watu anashinda na kukesha kwa mawazo, sasa hivi katulia. Nampa huduma nzuri, nampikia mapochopocho ndiyo maana ananawiri,” alisema Josephine.
Aliendelea kusema, kama kuna watu wanaamini yeye hatafunga ndoa na Dk. Slaa, wanajidanganya, kwani wanazo haki za kimsingi za kutimiza azma yao.
“Mimi najua Slaa ana watoto aliozaa na mwanamke mwingine, hata mimi nimeishi na Slaa miaka minne na tumezaa mtoto mmoja. Nimeishi na Slaa bila ndoa kwa muda mrefu na sasa tumeamua tufunge ndoa Julai 21, mwaka huu,” alisema Josephine.
Aliendelea kusema: “Nitafurahi sana nikishatimiza hii azma ya kuolewa na Slaa. Ni mume mzuri hasa, namuomba Mungu akamilishe malengo yetu. Unajua huko nyuma niliwahi kuteswa na mwanaume, niliishi na mwanaume asiyejua thamani ya mke.
“Huyo mwanaume alikuwa anasababisha nichangie mapenzi na ma-house girl, kwani kila house girl niliyemuajiri, alitembea naye. Sasa hivi yote hayo yamekwisha. Dk. Slaa anajiheshimu, sina tena vurugu za mwanaume wangu kutembea na house girl.”
Kuhusu matarajio ya kimaisha, Josephine alisema kuwa anaamini panapo majaliwa baada ya kufunga ndoa na Dk. Slaa, wataishi raha mustarehe kwa sababu wanaelewana vizuri.
“Raha ya maisha ya ndoa ni kuelewana, ndiyo maana nasema sioni sababu ya mimi na Dk. Slaa kutofunga ndoa. Tunapendana na kuelewana sana. Dk. Slaa akiondoka kwangu, hatapata mwanamke atakayeelewana naye kama mimi. Hata mimi siwezi kumpata mwanaume wa kuelewana naye kama ilivyo kwangu na Slaa.
“Jambo pekee ninaloweza kuwaomba Watanzania ni kutuombea tufunge ndoa yetu salama, atukinge na maradhi ili tuendelee kuishi raha mustarehe na tuendelee kutetea masilahi yao,” alisema.
Aliongeza kuwa maandalizi ya ndoa yao yamekamilika na kilichobaki kwa sasa ni siku ifike ili watawazwe rasmi kuwa mke na mume.
 
mbona unawivu kiasi hiki au ulitaka uolewe wewe? tafuta mwanaume mwingine mbona chadema vidume tumejaa..

Kwanini uzinifu wa Slaa msiuone? mnaficha nini wakati Josephine mwenyewe hapo juu anasema "Nimeishi na Slaa bila ndoa kwa muda mrefu na sasa".

Kuishi bila ndoa maana yake nini kama si uzinifu na kuzaa wamezaa, utaitaje hiyo> mtoto wa nje ya ndoa? au mtoto wa haramu? sijui mnachotetea ni nini?
 
hakuzaa nje ya ndoa kazaa bila ndoa, vipi "unawashwa washwa" unamuonea wivu mwanamke mwenzio?

Kazaa nje ya ndoa. Josephine alikuwa na mumewe na talaka kaipata juzi tu. Kazaa kabla hajaachwa na mumewe wa halali na kabla hajaolewa na mwanamme mwingine, hadi hii leo bado hajaolewa.

Kwanini mnaukimbia ukweli? inawasaidia nini?
 
sipo upande wowote, ila ninachosema ni hichi"ambaye hakuwahi kuzini na mwanamke awe wa kwanza kuwahukumu hao ndugu"
wangapi wanafanya uzinzi wakiwa na ndoa zao na wengine wamewekwa ndani na vimada/wameweka ndani viserengeti boys?
Itambulike kuwa hao ni binadam na si malaika, so wana hulka zote ambazo binadam wanakuwa nazo.
Tatizo naona hapa ni personality ya slaa ndo inawafanya mzungumze sana.
By the way, ni viongozi wangapi wanazini nje ya ndoa zao na hamsemi? .
Je mtu akizini na asipogundulika na jamii, kutokugundulika kwake kumtamfanya awe hajazini?( mzinzi na mzinzi tu hata kama amefanyia uzinzi wake shimo gizani ambako hakuna aonaye.)
theme yangu ni hii wakati tunawanyooshea vidole na kusema hawa wamezini, jiulize je hujawah toka nje ya ndoa yako? Au je ni kweli wewe na huyo mwenzi wako mlishiriki ngono rasmi baada ya kufunga ndoa au kabla?
Ukipata majibu hayo jiulize swali hili tena je dr slaa ndo wa kwanza kuzini? Wamezini slaa na mashumbusi waache watajua watakavyojitetea mbele za Yesu Kristo siku ya hukumu maana wasipotubu hukumu ipo.
Hii ni JF na sio facebook, sio lazima kila kitu ukoment. Ee Mungu utusaidie kujijua.
 
sipo upande wowote, ila ninachosema ni hichi"ambaye hakuwahi kuzini na mwanamke awe wa kwanza kuwahukumu hao ndugu"
wangapi wanafanya uzinzi wakiwa na ndoa zao na wengine wamewekwa ndani na vimada/wameweka ndani viserengeti boys?
Itambulike kuwa hao ni binadam na si malaika, so wana hulka zote ambazo binadam wanakuwa nazo.
Tatizo naona hapa ni personality ya slaa ndo inawafanya mzungumze sana.
By the way, ni viongozi wangapi wanazini nje ya ndoa zao na hamsemi? .
Je mtu akizini na asipogundulika na jamii, kutokugundulika kwake kumtamfanya awe hajazini?( mzinzi na mzinzi tu hata k
theme yangu ni hii wakati tunawanyooshea vidole na kusema hawa wamezini, jiulize je hujawah toka nje ya ndoa yako? Au je ni kweli wewe na huyo mwenzi wako mlishiriki ngono rasmi baada ya kufunga ndoa au kabla?
Ukipata majibu hayo jiulize swali hili tena je dr slaa ndo wa kwanza kuzini? Wamezini slaa na mashumbusi waache watajua watakavyojitetea mbele za Yesu Kristo siku ya hukumu maana wasipotubu hukumu ipo.
Hii ni JF na sio facebook. [uko sawa mkubwa kama hauwezi kufikiri na kutoa koment iliyo na maana ni bora ukaacha ila namlaumu aliye leta maada hii huku kwenye jokes maana sio sehemu yake post mahara husika kama kweli umeamua watu washiliki]
 
Hiyo haioshi dhambi ya kuzini na kuzaa nje ya ndoa.

Hujawahi kuzini wewe, au kwa sababu mi sijui, dunia ya sasa hakuna ambaye hajazini na kama yupo awe wa kwanza kunyosha kidole(nafsi) kwa mungu kujidhihirisha
 
Hujawahi kuzini wewe, au kwa sababu mi sijui, dunia ya sasa hakuna ambaye hajazini na kama yupo awe wa kwanza kunyosha kidole(nafsi) kwa mungu kujidhihirisha

Kwa kuwa wewe unazini basi zinaa ndio imekuwa halali? soma hii:

Leviticus 20 (KJV)
10 And the man that committeth adultery with another man's wife, even he that committeth adultery with his neighbour's wife, the adulterer and the adulteress shall surely be put to death.
[h=3]Mambo ya Walawi 20:10
Na mtu aziniye na mke wa mtu mwingine, naam, yeye aziniye na mke wa jirani yake, mtu mume aziniye, na mwanamke aziniye, hakika watauawa.
[/h]
 
Hakuna njia ya kutetea wazinifu zaidi ya kuua tu.Wewe unazaa ukiwa bado kiongozi wa dini(padri),Unamchukua mke wa mtu ambae bado hakuwa amepewa talaka,Kama masharti ya yesu umeyashindwa je ya mshumbusi utayaweza.Kweli wanawake hawafikirii.Eti nimependa au njaa zako ndo zimempenda
 
Halafu wewe babu wa miaka 70 una oa kweli umefikiria au hiyo mwanamke amekushika masikio.Nakwambia sasa kama yule wa kwanza alikuwa anakunyanyasa basi huyu atakunyonga kabisa hii ni kuruka mkojo kukanyaga mavi
 
Hiyo haioshi dhambi ya kuzini na kuzaa nje ya ndoa.

Mungu angekuwa anafanya kazi kwa style ya wanadamu,hakika hakuna ambaye angejiita msafi!!
Msamaha wa dhambi upo kwa ajili ya walioanguka!!!
 
Back
Top Bottom