Miguel255
Member
- May 13, 2020
- 35
- 111
Tazama kwa umakini hio picha hapo juu
Bila shaka umewahi kukutana na logo hii kwenye nguo, kofia na hata mabegi. Hii kampuni inaitwa "Kappa", ni kampuni ya mavazi iliyoanzishwa 1967 huko nchini Italia.
Kama nilivyosema hapo juu, kampuni hii inajihusisha na swala zima la mavazi; kuanzia track suits, jezi za mpira na mavazi mengine kadha wa kadha.
Watu hudhani logo ya kampuni ya "Kappa" huwakilisha usawa na ushirikiano kati ya mwanaume na mwanamke. Ila si kweli, leo ngoja nikufunulie ukweli.
Mnamo mwaka 1966 mtoto wa mmiliki na founder wa kampuni ya Kappa, bwana Abramo Vitale aliingia penzini na binti mrembo sana wa huko huko Italia. Sasa siku moja alimtoa dinner mlimbwende wake na baada ya chakula hicho cha jioni Mr Abramo alichukua chumba kwenye moja kati ya hoteli ya kifahari nchini Italia.
Yeye aliamini hakuna mwanamke anayeweza kumkataa kwani tayari alishakuwa tajiri baada ya kusimamia kampuni ya baba yake iliyoitwa MCT miaka mingi nyuma. MCT ni kampumi mama ya KAPPA.
Asichokitarajia ni kwamba bibie Violet hakuwa miongoni mwa wasichana waliobabaishwa na mali za tajiri huyo.... hivyo Mr Abramo alikaziwa usiku kucha bila kupewa nyuchi.
Yaani walishinda wamegeuziana mgongo, kuanzia walipoingia mpaka wakatoka bibie hakuruhusu Mr Abramo kuigusa achilia mbali hata kuiona mali yake. Na hapo ndipo idea au wazo la kampuni ya Kappa likapatikana.
Ukiangalia vizuri hio logo utagundua mwanamme na mwanamke wamegeuziana mgongo na wote wako uchi. Sasa ile kunyimwa usiku mzima ndo inaitwa Kappa....yaani jamaa hakuambulia kitu, alitoka kappa.
Kwahiyo ukisikia mtu anasema "Mshikaji kaingia na dem geto na ametoka kapa" ujue hilo neno lilianzia kwa bwana mdogo Abramo Vitale miaka ya 60 huko.
Neno hilo linatumika hadi leo na si kwenye tendo la ndoa tu bali sehemu mbali utasikia watu wakilitumia kumaanisha hawakuambulia kitu.
Mfano:- nimesoma sana ila nimeambulia kapa
Hadi wakati mwengine mimi Miguel255 niwatakie siku njema