Sipendi mke wangu atumie mitandao ya kijamii

Sipendi mke wangu atumie mitandao ya kijamii

Ndiyo rafiki na wajukuu juuu. Huwezi kumbana mwenzi wako halafu uutangazie umma kuwa ni mwaminifu sana! Mwache ajichanganye lakini aushinde uovu! Usiogope ukimbana sana akiingia kwa njia za panya atafanya kile unachofikiria
Sawa mkuu,lakini kwangu mimi sitaweza kumruhusu.
 
Kama huna hela lazima uchukie mkeo kutumia social medias unaogopa atakutana na washika dau tukakusaidia majukumu.
Babu we mwenzangu hiyo hela umeipata lini wakati nakujua fika kuwa wewe ni konda na mimi ni dereva boss wetu mmoja.
 
itakuwa baadhi yetu na sio wote , ninachoamini ni kwamba miongoni mwenu mmekua na tabia ya kutaka kupambana na mwanaume. mwanaume hanuniwi.
Hata kama kakosea si eti? Ila mwanamke ananuniwa kama kawaida?
 
Kupitia mitandao atanisamehe,furaha ataipata kupitia mambo mengine. Furaha yake isigeuke kuwa kero kwangu kwasababu hata mimi nahitaji furaha.
Oohh kwahiyo unataka yeye akose furaha kwa ajili yako? Vipi na wewe kama kuna vitu havipendi kutoka kwako akikwambia utaviacha?
 
Tukisimamia nafasi zetu tunaitwa miungu watu.. Unataka tuwe legelege muanze kutuita wasenge Kama Yule jamaa alieitwa na mke wake Kama anavyodai kweny uzi Fulani
Kusimamia nafasi zenu? Yaani kuwaonea na kuwanyanyasa wake zenu ndiyo kusimamia nafasi zenu na ni nani kasema anataka muwe legelege?
 
Wewe ndiyo umekosa maarifa ya kushindwa kufanya jambo ambalo litawafurahisha wote na mkeo yaani unachojali wewe ni furaha yako tu
Wengi hutanguliza jazba,hasira na chuki. Na hasira huondoa maarifa.
 
Hapana,simzuii kutumia simu. Namzuia kujiunga kwenye mitandao ya kijamii. Kumzuia mkeo kutumia simu ni kujiingiza kwenye utumwa mkubwa usio na mfano.
Sijaona umuhimu wa mawasiliano ya simu kama ilivyo kwa wanandoa.
Km huo ni utumwa
Huoni kumzuia mitandao ya kijamii ni utumwa pia?

Kwanini huna imani nae?.unahisi nini kitatokea akitumia,.?
 
1. Sihofii lakini sipendi
2. ni haki yangu kuwa muwazi kwa mwenza wangu na kumjulisha kila nisichokipenda huenda kinaweza kupelekea ndoa kuvunjika.
3. Ishu ni mitandao ya kijamii simu ruksa kuitumia.
2.uvunje ndoa kisa mitandao zama hizi za teknolojia?..
Mfano mimi mke wa mtu niko mitandaoni saivi
Je yatosha kuvunja ndoa?.
 
Mi wangu namwacha atumie kwanza ajui Mambo mengi uwaga nacheka post zake za fb and I quote eti akitumaga picha fb anaandika " NAWATAKIA MCHANA MWEMA WANA FB"
 
Kwani kila aliyeko mjini ameshawahi kutumia mtandao wa facebook? Miaka hiyo alikuwa mwanafunzi.
Mi pia nilikua mwanafunzi miaka hio na tulikua tunashare/tunaonyeshana mitandao marafiki namna ya kutumia nk

Nashangaa katazo hili wkt mkeo ni mtu mzima

Na je ni facebook tu?
Insta?watsap?jf?snapchat?twitter?linkedin?.
 
Oohh kwahiyo unataka yeye akose furaha kwa ajili yako? Vipi na wewe kama kuna vitu havipendi kutoka kwako akikwambia utaviacha?
Eeh ndio naacha,kama nilivyoachana na mchepuko wangu kwa ajili ya kutunza heshima yake. Nimeacha tabia ya kurudi usiku sana nyumbani. Nimeacha yote hayo kwasababu alikuwa hapendi.
 
Yani nasema kiukweli toka moyoni sipendi mke wangu atumie mitandao ya kijamii.

Hata kama mimi mwenyewe natumia na anajua natumia lakini yeye sipendi nimuone anatumia hiyo mitandao.

Najua wapo watakaoniona natumia mfumo dume potelea mbali na wala sijali.
Nakubaliana na wewe.....
 
Km huo ni utumwa
Huoni kumzuia mitandao ya kijamii ni utumwa pia?

Kwanini huna imani nae?.unahisi nini kitatokea akitumia,.?
Sio utumwa kwasababu kilicho na umuhimu ni mawasiliano na njia tunayoitumia kuwasiliana ni kwa kupigia simu na kutumiana sms. Hivyo hivyo kwa ndugu zake na rafiki zake.
 
Back
Top Bottom