Sioni umuhimu wa daraja la Aga Khan - Coco beach kwa sasa

Nimetoka Kariakoo!
Daladala limetupeleka SHAURIMOYO!
Kisha MACHINGA COMPLEX!
Then BOMA!
Kigogo round about!
Mikumi!
Tukala KUSHOTO kutokea USALAMA!
Safari ya MANZESE inaendelea!
2 Hours!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni idadi ndogo sana ya wakazi wa jiji la dar es salaam.

View attachment 972803
(under utilised bridge?).
Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.

USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.

Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.

Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.

Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.

Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.
Sasa wewe unakaa Tandale Kwa Mtogole daraja la Salender utaliona lina faida kivipi?
 
”Kuhusu eneo la Jangwani nimpongeze JPM amelizungumzia hili wakati wa Kampeni na lipo kwenye Ilani ya CCM kwamba pale Jangwani litajengwa Daraja jipya kubwa na kuutengeneza Mto wenyewe na itasaidia kuondoa changamoto ya eneo la Jangwani"- RC KUNENGE youtube.com/c/MillardAyoTza
 
”Kuhusu eneo la Jangwani nimpongeze JPM amelizungumzia hili wakati wa Kampeni na lipo kwenye Ilani ya CCM kwamba pale Jangwani litajengwa Daraja jipya kubwa na kuutengeneza Mto wenyewe na itasaidia kuondoa changamoto ya eneo la Jangwani"- RC KUNENGE youtube.com/c/MillardAyoTza
Kumbuka aliahidi milion 50 kila kijiji.
 
Kwa macho ya kawaida unaweza kufikiri lengo la daraja hili ni kupunguza foleni ya Salender Bridge na kuwaondolea wananchi wa Dar kero ya foleni. La hasha daraja hili linalojengwa kwa gharama kubwa halitapunguza foleni kwa sababu watakaotumia daraja hili ni idadi ndogo sana ya wakazi wa jiji la dar es salaam.

View attachment 972803
(under utilised bridge?).
Ukiangalia kwa jicho la tatu, lengo hasa ni kuwasaidia viongozi, mabalozi na wazungu wachache wanaoishi maeneo ya Osterbay na Masaki ambao hawazidi hata 200, labda wasikae kwenye foleni kwa muda mrefu wakichanganyika na walalahoi wa maeneo ya Mwenge, Kawe, Kunduchi, Tegeta, Boko na Bunju.

USHAURI: Kama lengo ni kupunguza foleni ya Salender Bridge ingefaa zaidi lijengwe daraja kubwa la nchi kavu kutokea maeneo ya Hananasifu au Magomeni hadi Muhimbili au Fire kuvuka bonde la Jangwani linalojaa maji kipindi cha mvua.

Daraja hili la Hananasifu - Muhimbili/Fire, lingehudumia watu wengi hasa wafanyabiashara wa Kariakoo na katikati ya jiji, ambulance, zimamoto na wafanyakazi wa kada za chini ambao ndio walio wengi, tofauti na daraja la Aga Khan - Coco beach ambalo litahudumia 'sana sana' wakazi wa Masaki na pengine kubaki 'idle' kwa kipindi kirefu.

Daraja kubwa la Jangwani si tu lingepunguza adha ya foleni ya Magomeni-Kariakoo/Posta lakini pia lingesaidia kupunguza magari yanayopita Salender Bridge.

Anyways kupanga ni kuchagua, tumechagua daraja la Coco beach kwa wadosi tukawaacha wa Mbagala wahangaike na foleni yao.

Ni ushauri na mawazo huru ya MwanaJF mzoefu Quinine.
Haujui unalolisema. Kwa taarifa yako wasafiri wengi kutoka barabara ya ALI HASSAN MWINYI na Mwai Kibaki-yaani Mwenge na njia ya chini inayopita Namanga hadi Bagamoyo ndiyo walengwa wakubwa wa daraja hili. Wataingia barabara za Masaki na Mikocheni na kukwepa foleni ya Salender bridge kupitia daraja hili. Usilolijua usilisemee
 
Umeongea ukweli mtupu ilo daraja litasaidia wakazi zaidi wa masaki,oysterbay ambao sio watz na hata kama watz basi mawaziri na viongozi wakubwa wa serikali.

Hilo daraja ni moja ya "WHITE ELEPHANT" Project za vigogo wa serikalini,wewe unadhani wakubwa wanapata wapi utajiri? Wanaanzisha miradi hewa kibao ya ufisadi na ndani ya hiyo miradi waneweka cha juu cha kufa mtu,imagine bei halisi ya Drimulaina ni usd 100m lakini sie tumenunua kwa 228m USD ina maanisha kuna watu wamepiga zaidi ya 118m usd wameweka mfukoni.

Kupunguza foleni dsm wajenge njia nyingi mbadala,sio ukitaka kwenda mwenge kwenda posta mbananane ali hassan,wajenge njia za Juu kutoka mkwajuni hadi Mwenge,wajenge njia ya juu kutoka Mikocheni viwanda ikatue mbezi beach,wajenge njia ya juu kutoka Magomeni Mtaaa mapipa ikatue Uhasibu,hapo watasaidia wakazi wengi.

Pia waharakishe Mwendo kasi kuijenga,posta to mbagala,posta to Gongo la mboto,Morocco to Mwenge to Bunju....Ilitakiwa waanze na Mwendokasi waachane kwanza na Salenda maana hilo daraja ni Pambo na 50% tu za wakubwa.
Sasa hivi unalisifia
 
Back
Top Bottom