Sioni haja ya kukutana, Naona haja ya kufuata Katiba

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,239
113,612
Toka Freeman Mbowe atoke jela/ gerezani, ameshakutana na Rais Samia mara kadhaa sasa.

Bado sijui na sielewi kwa nini hasa wamekuwa wakikutana kutana.

Ni kweli kuwa Mbowe alikamatwa na kufungwa kimakosa.

Mtu yeyote aliye na chembe ya akili kwenye ubongo wake analijua hilo.

Kwenye nchi zilizostaarabika, mtu anayekamatwa na kufungwa kimakosa huwa anastahili kulipwa fidia ya usumbufu alioupata na muda alioupoteza.

Lakini nchi yetu hii iliyo ni jamhuri na ndizi, hakuna cha fidia. Unaswekwa jela kwa amri ya Rais, unatolewa kwa amri ya Rais. Halafu baadaye Rais huyo huyo anakuita nyumbani kwake ukanywe juisi na kutafuna karanga na biskuti, na wewe unaenda. Ngoma inaisha.

Kwa watu tulio wahalisia wa mambo na tusiopenda kuyafanya mambo marahisi yawe magumu, mara nyingi huwa tunapenda kufuata taratibu zilizopo.

Kwa msingi huo, mimi sioni sababu wala tija yoyote kwa hawa CHADEMA kukutana kutana na Rais mara kwa mara.

Kinachohitajika kwa sasa ni Rais na chama chake kilichopo madarakani kufuata tu katiba iliyopo, basi.

Kama katiba inayotumika sasa inaruhusu vyama vingi vya siasa viwepo na inaruhusu vyama hivyo kufanya shughuli zake nchini kwa mujibu wa sheria, basi na viachwe vifanye hizo shughuli.

Hakuna haja wala sababu ya kuvizuia. Katiba inaruhusu. Kwa nini wewe uende kinyume na katiba na kuvizuia?

Yaani kuna mambo mengine ni marahisi tu lakini baadhi ya watu hupenda kuyafanya yawe changamani.

Fuateni katiba. Acheni kuonea watu. Ni hivyo tu.

Lipi lililo gumu katika hayo?
 
Ikifuatwa katiba si chama ndio kinakufa kabisa cha kijani!!unafikiri mikutano ya hadhara ikiruhusiwa kuna mtu atatka kujua MAMA yupo wapi leo badala ya Mbowe leo anahutubia wapi!!!na hakuna atakaye fuatilia mikutano ya mama na atafunikwa na chama chake!!!
 
Kwa msingi huo, mimi sioni sababu wala tija yoyote kwa hawa CHADEMA kukutana kutana na Rais mara kwa mara.

Kinachohitajika kwa sasa ni Rais na chama chake kilichopo madarakani kufuata tu katiba iliyopo, basi.
Wewe Nyani Ngabu uwashauri CHADEMA kama nani? Wapumbavu mna enjoy kuona kuna mivutano ya kisiasa. Mbowe alikuwa jela anateseka peke yake, mambo yamekwisha anafanya siasa za kistaarabu hamtaki. Anzisha na nyinyi vyama vyenu mje mdai Katiba kwa namna mnavyotaka.

Katiba haijawahi kuwa suluhisho la kila kitu popote duniani. Hata USA mbona tunaona blacks wanavyopuuzwa licha ya Katiba kuwapo
 
Ikifuatwa katiba si chama ndio kinakufa kabisa cha kijani!!unafikiri mikutano ya hadhara ikiruhusiwa kuna mtu atatka kujua MAMA yupo wapi leo badala ya Mbowe leo anahutubia wapi!!!na hakuna atakaye fuatilia mikutano ya mama na atafunikwa na chama chake!!!
Chama kitakufa kama hakina sera bora. Hakitakufa kwa kufuata katiba.
 
Wewe Nyani Ngabu uwashauri CHADEMA kama nani? Wapumbavu mna enjoy kuona kuna mivutano ya kisiasa. Mbowe alikuwa jela anateseka peke yake, mambo yamekwisha anafanya siasa za kistaarabu hamtaki. Anzisha na nyinyi vyama vyenu mje mdai Katiba kwa namna mnavyotaka.

Katiba haijawahi kuwa suluhisho la kila kitu popote duniani. Hata USA mbona tunaona blacks wanavyopuuzwa licha ya Katiba kuwapo
Blacks wanapuuzwaje licha ya katiba kuwepo?
 
Siasa zetu ngumu sana.

Top officials wa vyama wanakutana.

Hawaweki agenda public.

Wala hawatuambii walichokubaliana.

Angalau basi wangekua hata wanafanya press kila baada ya hiyo mikutano.

Ila kama wanajadili maswala ya biashara zao basi wasiwe wanatuwekea hizo taarifa za mikutano yao publicly bila kutuambia agenda za mikutano na nini wamekubaliana.
 
Mkuu
Yule mzee aliharibu sana nchi
So ili tutoke huko yanatakiwa mazungumzo kama haya, ili maza acute baadhi ya hata zile sheria zilizokua zinapitishwa kwa hati za dharura bungeni
Katiba ifuatwe tu.

Hakuna kilicho kigumu hapo!
 
Toka Freeman Mbowe atoke jela/ gerezani, ameshakutana na Rais Samia mara kadhaa sasa.

Bado sijui na sielewi kwa nini hasa wamekuwa wakikutana kutana.

Ni kweli kuwa Mbowe alikamatwa na kufungwa kimakosa.

Mtu yeyote aliye na chembe ya akili kwenye ubongo wake analijua hilo.

Kwenye nchi zilizostaarabika, mtu anayekamatwa na kufungwa kimakosa huwa anastahili kulipwa fidia ya usumbufu alioupata na muda alioupoteza.

Lakini nchi yetu hii iliyo ni jamhuri na ndizi, hakuna cha fidia. Unaswekwa jela kwa amri ya Rais, unatolewa kwa amri ya Rais. Halafu baadaye Rais huyo huyo anakuita nyumbani kwake ukanywe juisi na kutafuna karanga na biskuti, na wewe unaenda. Ngoma inaisha.

Kwa watu tulio wahalisia wa mambo na tusiopenda kuyafanya mambo marahisi yawe magumu, mara nyingi huwa tunapenda kufuata taratibu zilizopo.

Kwa msingi huo, mimi sioni sababu wala tija yoyote kwa hawa CHADEMA kukutana kutana na Rais mara kwa mara.

Kinachohitajika kwa sasa ni Rais na chama chake kilichopo madarakani kufuata tu katiba iliyopo, basi.

Kama katiba inayotumika sasa inaruhusu vyama vingi vya siasa viwepo na inaruhusu vyama hivyo kufanya shughuli zake nchini kwa mujibu wa sheria, basi na viachwe vifanye hizo shughuli.

Hakuna haja wala sababu ya kuvizuia. Katiba inaruhusu. Kwa nini wewe uende kinyume na katiba na kuvizuia?

Yaani kuna mambo mengine ni marahisi tu lakini baadhi ya watu hupenda kuyafanya yawe changamani.

Fuateni katiba. Acheni kuonea watu. Ni hivyo tu.

Lipi lililo gumu katika hayo?
FAM ni kada mtiifu wa CCM aliyepewa kazi ya kuwa mwenyekiti wa CHADEMA
 
Maza anataka Mbowe asimkazie 2025 ila baada ya hapo atafungua miango yote ya upinzani
 
Back
Top Bottom