Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,007
- 9,873
MWANAMKE mmoja Moshi Mkimbu (40) mkazi wa Kijiji cha Ndulungu Tarafa ya Ndago Wilaya ya Iramba mkoani Singida ameuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali na mume wake aitwaye Juma Shabani.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ACP) Stella Mutabihirwa akizungumza na waandishi wa habari leo aamethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo lilitokea Julai 18, 2021 katika kitongoji cha Misughaa na kuwa mtuhumiwa alikamatwa na atafikishwa mahakamani kujibu shitaka lake.
Mutabihirwa alisema kuwa uchunguzi wa awali wa Jeshi la polisi umebaini kuwa chanzo kikubwa cha mauaji hayo ni ugomvi wa kifamilia pamoja na ulevi baada ya marehemu kudai pesa za mahindi yaliyouzwa kwa ajili ya ada ya mtoto shuleni, ndipo mume wake huyo alianza kumshambulia kwa kumpiga na fimbo na kitu chenye ncha kali na kusababisha kifo cha mke wake.
Michuzi Blog
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida Kamishna Msaidizi (ACP) Stella Mutabihirwa akizungumza na waandishi wa habari leo aamethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo lilitokea Julai 18, 2021 katika kitongoji cha Misughaa na kuwa mtuhumiwa alikamatwa na atafikishwa mahakamani kujibu shitaka lake.
Mutabihirwa alisema kuwa uchunguzi wa awali wa Jeshi la polisi umebaini kuwa chanzo kikubwa cha mauaji hayo ni ugomvi wa kifamilia pamoja na ulevi baada ya marehemu kudai pesa za mahindi yaliyouzwa kwa ajili ya ada ya mtoto shuleni, ndipo mume wake huyo alianza kumshambulia kwa kumpiga na fimbo na kitu chenye ncha kali na kusababisha kifo cha mke wake.
Michuzi Blog