Jerrymsigwa
JF-Expert Member
- Jun 23, 2012
- 14,084
- 8,400
hii nchi ni balaa
http://youtu.be/6TZPdM3xn24
Skiza hiyo video, dogo kahukumiwa jana kifungo cha wiki4 jela
hii nchi ni balaa
Hayo ni matunda ya uzalendo na uongozi unaojali misingi ya haki na mgawanyo sawa wa keki ya taifa na matumizi sahihi ya rasilimali za taifa.....
Hata hapa kwetu yanawezekana endapo tu tutaamua kwa dhati kuyang'oa makupe na mafisadi ya CCM madarakani
Ni zaidi ya hayo, tupate rais dictator kama LKY ndio dawa hakuna namna nyingine
Mkuu Jerrymsigwa.
Singapore wanaruhusu wageni kufanya kazi na hata kuwa raia. Ili mradi una elimu wanayohitaji, kama Kanada au Australia.
Sisi tutakubali kuruhusu wageni wasomi waje Tanzania kufanya kazi kirahisi kuziba pengo la "highly skilled labour"?
Singapore, maraisi wawili walikuwa wenye asili ya Kihindi. Wanachaguwa mwenye uwezo siyo rangi ya mtu kuongoza.
Sisi tupo tayari kutawaliwa na Mtanzania mwenye asili ya Kihindi au Kiarabu?
Maendeleo yanahitaji zaidi ya Raisi Dikteta. Unatakiwa ujipange kielimu, kifikra na kikazi.
Pia, Raisi Dikteta mbona tulishapata kwa zaidi ya miaka 20. Alituwacha taabani na vyakula vya resheni na kuomba misaada kama leo.
Au umesahau?
Mkuu muungano wa Singapore na Malaysia uliposhidikana mwaka 1962 ndipo LKY akawa first prime minister ndipo 1965 ikawa independent democratic state. In short image ya nchi ni kiongozi, ndio maana baada ya trh 26/03/2015 umeona tofauti ya kabla ya hiyo tarehe? Imekua shida media zimekua huru, vijana kama Amos Yee anatukana ovyo ovyo kwa sababu PM wa sasa ni democratic. Dawa ni kupata kiongozi dictator tu akisema barabara inapita hapa, no discussion.
Kuhusu kutawaliwa na wahindi, asilimia 73 ni Chinese, 21 Malay na 3 ni wahindi na iliyobaki ni mix ya waasia wengine. Na historia ya hiyo nchi ni tofauti sana na sisi. Wao toka watawaliwe na wajapan 1945 mpak Brits wakaja bado palikua na mchanganyiko huo wa watu. Huwez fananisha sisi na SiNGAPORE kwa multiculturalism blaza
tunahitaji Rais anayefuata utawala wa sheria. ni madikteta wachache sana walioletea nchi zao maendeleo wengi huziingiza kwenye umaskini na vurugu.Ni zaidi ya hayo, tupate rais dictator kama LKY ndio dawa hakuna namna nyingine