Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 29.Nimeolewa na nina mtoto mmoja. Juzi nimegundua kwamba mume wangu anatembea na mmoja wa marafiki zangu. Nilimsindikiza rafiki yangu kumuona shangazi yake mgonjwa,tukiwa pale nikataka kumkumbusha mume wangu kununua baadhi ya vitu ambavyo tulikua tunahitaji nyumbani. Nikaazima simu ya rafiki yangu kwakua yangu ilikua imeisha chaji,akanipa. Nikadial namba za mume wangu bila wasiswasi,baada ya kuandika zote nikaona kwenye screen imeandikwa mpenzi. Nikajua labda nimekosea maana nilikua natoa namba kichwani kwahiyo nikadial upya,matokeo yale yale.Nikaona nipige,ikapokelewa "mambo darling" sauti ya mume wangu bila ubishi. Kigugumizi nilichopata sikuweza kutoa neno zima.Akaishia kusema "mpenzi unakatakata ngoja ntakupigia" simu ikakata. Nilichofanya nilifuta namba nilizodial alafu nikadial simu ya dada wa kazi.
Kuchungulia msg box naona zinazotoka na kwenda kwa mpenzi zimesheni. Nikamrudishia na pale pale nikaaga.Sijamuuliza yeyote kati yao wala sijaongea na rafiki yangu since.Nafikiria nini cha kufanya.Naombeni ushauri.
Kuchungulia msg box naona zinazotoka na kwenda kwa mpenzi zimesheni. Nikamrudishia na pale pale nikaaga.Sijamuuliza yeyote kati yao wala sijaongea na rafiki yangu since.Nafikiria nini cha kufanya.Naombeni ushauri.