Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa. Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.

Wewe unaye miaka minne umwelewi sisi ndio tutaelewa kwa post yako moja tu ya leo. Halafu wewe ulitaka iweje? Utongozwe? Wewe umemsimulia ya boy friend wako? Soma nae Biblia mistari ya uzinzi mfano ile ya mke wa Pharaoh kmrukia Yusuph mtoto wa Yakobo. Mwalike kwako halafu piga khanga moja - liwe na liwalo! Halafu umempenda yeye au unafukuzia hiyo mibahasha yenye mifweza zaidi?!

Nijuwavyo mimi 'walokole' wengi wako kwenye maumivu mfano kuumwa na kadhalika. Halafu walokole gani wanasakata muziki ingawaje haujasema ni muziki upi lakini yawezekana ni wa Ali Kiba.

Halafu hizi tabia za mtu upo single unaenda kwenye sherehe zinazohitaji couples hazifai.

Hivi kumbe mwanamke akipewa dinner na mifweza ya nguvu basi naye anataka kulipa kwa kumlisha mwanaume 'natural apple'?
 
Ni mlokole, inamaana haamini ngono kabla ya ndoa especially kwa mtu anaedhamiria kabisa kuwa nae. Pili kuna wakati aliniambia urafiki wetu umekuwa deep sana kiasi ambacho asingependa uvunjike.
Daah basi tena,sitii neno mamii,inamaana hapa unatuhadaa tu.
 
Wewe unaye miaka minne umwelewi sisi ndio tutaelewa kwa post yako moja tu ya leo. Halafu wewe ulitaka iweje? Utongozwe? Wewe umemsimulia ya boy friend wako? Soma nae Biblia mistari ya uzinzi mfano ile ya mke wa Pharaoh kmrukia Yusuph mtoto wa Yakobo. Mwalike kwako halafu piga khanga moja - liwe na liwalo! Halafu umempenda yeye au unafukuzia hiyo mibahasha yenye mifweza zaidi?!

Nijuwavyo mimi 'walokole' wengi wako kwenye maumivu mfano kuumwa na kadhalika. Halafu walokole gani wanasakata muziki ingawaje haujasema ni muziki upi lakini yawezekana ni wa Ali Kiba.

Halafu hizi tabia za mtu upo single unaenda kwenye sherehe zinazohitaji couples hazifai.

Hivi kumbe mwanamke akipewa dinner na mifweza ya nguvu basi naye anataka kulipa kwa kumlisha mwanaume 'natural apple'?
Sijawahi kumsimulia ya boyfriend wangu, pia sitaki kumlisha apple ila nijue where are we hearding to? Nisije ondoka kumbe ndio andiko, nibaki kumbe ninapoteza muda.
 
Inawezekana, lakini anaiomba tutoke kwa chakula kwenye hoteli nzuri, sasa kama sina mvuto mbona haoni haya kwenda na mimi in public places, pia tunakwenda wote kanisani J2.

Mama unatakiwa sasa wewe umalizie mwenyewe ingawaje sio kawaida sana kwa wanawake wa kiafrika. Sikiliza muziki huu wa Alicia Keys kuanzia dakika ya 4:40

 
Sijawahi kumsimulia ya boyfriend wangu, pia sitaki kumlisha apple ila nijue where are we hearding to? Nisije ondoka kumbe ndio andiko, nibaki kumbe ninapoteza muda.
Hapana mamii,wala hutakosea kabisa,wewe fungua moyo wako kwa yeyote umpendae ,maisha yenyewe mafupi mamii.
 
Sijawahi kumsimulia ya boyfriend wangu, pia sitaki kumlisha apple ila nijue where are we hearding to? Nisije ondoka kumbe ndio andiko, nibaki kumbe ninapoteza muda.

Basi kama ndio hivyo mweleze plan zako za maisha hususan kuwa na mwenza wa ndoa halafu usikilize kwa makini comments zake, kama hatatoa comments basi muombe comments; halafu mchomekee na yeye ya kwake ikoje ili uone kama kuna any matching.
 
Sijawahi kumsimulia ya boyfriend wangu, pia sitaki kumlisha apple ila nijue where are we hearding to? Nisije ondoka kumbe ndio andiko, nibaki kumbe ninapoteza muda.
Hata ukiamua kumlisha apple,siri itabaki ya nyie wawili tu na hakuna mungine atajua whatever what? sasa unaogopa nini? we mfunulie muyamalize na hakuna chochote kitatokea,trust me
 
Mwenzio kakupa mpunga wa nguvu na wewe mpe mzigo wa nguvu. Ukila vya watu kubali na wewe kuliwa
 
Mama unatakiwa sasa wewe umalizie mwenyewe ingawaje sio kawaida sana kwa wanawake wa kiafrika. Sikiliza muziki huu wa Alicia Keys kuanzia dakika ya 4:40


Thanks alot for this.
 
Sky eclat ujue mimi nakufatiliaga toka unidanganye you are 3... haya kwa kunificha labda ungekua wangu
 
Sasa Sky Eclat usichoelewa hapo ni kipi? Si rafiki yako kakupenda anafurahia kuongea nawe, kwenda dinner na hata kukupa mpunga wa haja. Hapo kwenye rangi nadhani uliona mtongozo huo unakuja kumbe mwenzio kwa sasa kajikita kama rafiki tu wala hajawaza mtongozo lol!

Si ajabu rafiki yako bado anakusoma kukuona weye ni binti wa aina gani, labda akisharidhika na kila kitu anachokifuatilia kwako labda tabia, maongezi yako mnapokuwa pamoja, mnapoenda kwenye dinner anakuangalia behaviour yako tangu mnapofika, mnaagiza vinywaji na vyakula, unavyokula n.k. Akishajiridhisha kwamba huyu sky Éclat ndiye mrembo niliyekuwa namtafuta siku zote na siwezi kuendelea kuishi bila huyu mrembo ndiyo atakapokuja na mtongozo.

Ukiona vipi vipi nawe kama ndiyo kishakonga moyo na akili yako basi anza wewe mtongozo au watoto wa MUJINI wanasema unajirengesha. Kila la heri maana mpaka kuja kumuanzishia uzi humu basi moyo na akili yako viko kwenye page moja kuhusu huyu njemba mlokole wa kufa mtu.



Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa. Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.
 
Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa. Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.
hivi kwanini wadada ukiwa unammwagia mpunga wa maana bila kuingiza sauti huwa wanateseka sana,kama wewe unatamani uvue nguo hadharani ili umpe mshkaji uwe huru,ajabu kweli..
 
Ningeelewa kama ingekuwa company tu, sasa na mambo ya kuniwekea pesa kwenye bahasha nayo ni company?

Ulimuuliza pesa alizokupa zilia za nini? Kama alikupa za safari ulimuuliza kakupa kama nani? Simple...
 
Jamaa ni joga.Pia mapenzi saa nyingine ni vitendo zaidi na umeviona.jiongeze
 
Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa. Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.
Sisi tunaomtumikia Bwana kutoka moyoni si mwilini,tunautaratibu wa kuwasiliana na Roho wa Bwana juu ya jambo lolote tunalotaka katika maisha yetu.Kumbuka miaka mnne Kwa Bwana ni sawa na nusu dk na nusu dk ni sawa na miaka elfu 4.
Ushauri Wangu kwako,kwakuwa na wewe umekuwa mshiriki katika eneo analoabudu yeye basi mshirikiane katika maombi,Bwana atafanya njia.
 
Back
Top Bottom