Simulizi ya kusisimua

Simulizi ya kusisimua

SEHEMU YA 50
NA GAOOH
SIMU 0654387935
Ilipoishiaaa sehemu iliyopitaa
"Unasemaje naomba uniambie vizuri, mbona
sikuelewi?"Rafiki yake john aliekuwa akiniambia na
yeye alionekana kuchanganyikiwa hata ongea yake
haikuwa ya kueleweka naye alionekana
kuchanganyikiwa.
"Kidawa mumeo ameumia vibaya...."Alianza
kuniambia lakini hakumaliza akaacha kuongea huku
machozi Yakimtoka..
ENDELEAAAA SASAAA
Nilitaka kuingia ila nilizuiwa nikaishia pale nje,
nilijaribu kumhoji kilichotokea ila alishindwa
kuongea zaidi ya kulia tu, nilikosa cha kufanya na
mimi nilikaa sehemu nilihisi kuchoka zaidi, dakika
kadhaa chumba kile ambacho ndio shemeji
alichosema kinamo john ndani yake kilifunguliwa
kisha kitanda kilichotundikwa drip la damu pamoja
juu kilipitisha, nilitaka niangalie ila nilizuiwa manesi
na madaktari walikizunguka kisha wakatoka nje na
kuingiza kwenye gari, walikuwa wakimwamisha,
shemeji nae aliamka akiwa amechanganyikiwa, gari
iliondoka pale kuelekea upande wa kushoto ambako
kuna jengo kubwa la jakaya kikwete, sikujua
kilichoendelea daktari alituita mimi na shemeji,
akatuuliza maswali kadhaa nabkutupa maelezo
anapoperekwa john alisema wanampereka moi kle
ndio atapata huduma stahiki nilikuwa sijui
kilichotokea.
Kwa kufuta machozi na kulia kwa kufina fina alianza
kunisimulia kilichotokea hapo nikikuwa makini
nikimsikiliza.
"Shemeji leo wakati tuko kazini kule bandarini john
aliomba kumsaidia derava anaetoa mizigo kwenye
kontena na kile kigari maaulum alikubaliwa kwa vile
alipenda kuwasaidia wengine, siku hii yule dereva
hakuwepo hivyo john aliamua akatoka mizigo, ni
kweli aliweza na alijitahidi kutoa kwa usahihi.."alipo
fika hapa alinyamaza na kuanza kulia.
"Samahani tunaomba mrudi nyumbani mgonjwa
wenu yupo ICU hamwezi kumuona madaktari
wanapambania uhai wake bado,"alisema nesi
mmoja akimkatisha asiendelee kunisimulia hapo
tuliondoka na kwenda mpka kwenye mabanda
ambayo watu wanapumzika nikiyafuta machozi yake
yaliokuwa yakisarauka mashavuni kwake, tulifika
mpka pale na kukaa ila akili haikutulia ikabidi
tuelekee moi huku tukiikumbuka namba ya ward
tuliyoelekezwa, hatukutumia muda mrefu tulifika
pale hapo tukaa nje tukisubiri, madaktari waliingia
na kutoka.
"Hamruhusiwi kumuona bado hali yake sio nzuri
haweze kutoka ICU leo wala kesho,"alitupa taarifa
nesi na kuondoka na kweli tukishinda hapo
sikunzima bila kula hatukuruhusiwa kumuona John,
shemeji alinieleza kuwa john amepata jeraha
kichwani pia baadhi ya viungo vyake pia vimekutwa
na mkandamizo wa ajali aliyoipata akiwa katika kazi
ya kumsaidia dereva, alisema kuwa lilikuwa kama
jambo la kushangaza kwavile john hakuwahi tamani
kuendesha vigari vile pia aliladhimisha sana
kuendesha hivyo wakamkubaria. Niliumia sana
kusikia hivyo nilijiona mtenda zambi mkubwa
kwavile nimemkosea Mungu pakubwa kiasi kwamba
maisha yangu yamejawa na huzuni na machozi
nahisi sistahili kupata fulaha hata chembe.
Bila kujua hali ya John tulikuwa tukienda hospital
kila siku jibu tunalopewa kuwa john bado hatuwezi
kumuona ni siku tatu sasa ndipo dokta alituita
ofisini kwake.
Baada ya salamu ndipo alitupa maelezo mafupi
huku akitutia moyo.
"Mke wa john si ndio wewe kwanza poleni sana
kwa tatizo lililomkuta ndugu yenu, au mume wako
najua ni mipango ya Mungu huwezi kujua kusudi la
Mungu, ila naomba niwape pole kwa mara nyingine,
sehemu ambayo john ameumia kuna mambo karibia
matatu au mawili anaweza kutana nayo la kwanza,
John anaweza kupona ila akapoteza kumbu kumbu
yani akasahau kila kitu ambacho aliwahi kufanya au
alichowahi kukutana nacho kutokana na
mahalialipoumia yani ubongo umepata hitirafu
kubwa kitaalamu tunaita... Nimesahau kidogo jina
lake ila sana sana ni kupoteza kumbu kumbu zote,
cha pili anaweza pona ila mwili mzima ukapooza
viungo vyote, cha tatu anaweza kupoteza uhai
kabisa, najua ni hakuna cha afadhali kati ya hivyo ila
timu yetu ya madaktari bingwa wanaendelea
kupambana na uhai wa John tumuombee dua kwa
uwezo wa mungu atapona, usilie Mrs John"dokta
alitoa maelezo nilishindwa stahmili maneno yake
hapo machozi yalinitoka bila kutarajia nikayafuta
dokta akaendelea kunipa matumaini kisha alituomba
turudi nyunbani kwa vile john yupo katika chumba
cha wagonjwa mahututi anatumia mipira kula
pamoja na kupumua.
Tulimsikiza dokta, hapo ndio na sisi tulianza safari
kuja kila siku na kuondoka marafiki zake mbali
mbali nao walikuja kuangalia mandeleo yake zilipita
wiki mbili ndipo tukaruhusiwa kumuona john
nilifurahi taarifa ya kumuona john wangu tuliingia na
kumkuta kitandani akiwa amelala tu huku kichwani
akivalishwa kifaa kama helmet sijui kinaitwaje
sijasoma mimi sijui jina lake, john alikuwa kimya
mipira tu ndio ilionekana mdomoni kwake, macho
akiwa amefumba ilikuwa nafasi ya upendeleo
hatukuruhusiwa kumuona dokta alitufanyia
upendeleo kwa vile tumekuwa tukizunguka muda
mrefu bila kujua anaendelea, sikuacha kulia mbele
ya john kilio cha uchungu kilinitoka vilivyo.
Dokta alitutoa ndani hapo siku hii nilirudi nyumbani,
mapema nilijaribu kumshukuru mungu pamoja na
kumuomba amrejeshe john kama zamani, nilifanya
maombi., hata hamu ya kula sikuwa nayo kila
nikijitahi nipike hamu ya kula haiji nilishazoea kula
na john mara zote niliishia kumwaga chakula tu na
kunywa chai tupu, chakula kilikuwa hakimezeki.
Nilianza kwenda kanisani nikiamini ndio sehemu
sahihi ambayo nitasaidika, kwenda kwangu kanisani
kdogo upekwe ulianza kupungua hata muda wa kula
nilipakua sahani mbili yangu na ya john kisha
nakula yangu huku nikifanya kama john yupo karibu
yangu hata kulala nikifanya hivyo hivyo nilipanga
mito sehemu moja kisha kuifanya kama john.
Siku moja nilienda hospital hapo ilikuwa ni baada
ya kupita siku moja sijaenda hivyo siku hii niliamua
niende, nikifika hadi kwenye chumba alicholazwa
john pale nje nilikuwa sielewi kwa vile walionekana
watu tofauti wakiingia ndipo nikaenda kwa dokta
nawe sikumkuta ikibidi nikaulize mapokezi jibu
nikilopewa sikuamini pia likinishangaza zaidi.
"Mgonjwa wako amehamishiwa mloganzila"alinijibu
hivyo.
"Mloganzila ndio chumba gani mbona mi najua
alikuwaga chumba kile pale"nikimwambia nikiwa na
wasi wasi nisipajue mloganzila ni wapi.
"We dada, mgonjwa wako ameperekwa hospital ya
mloganzila hapa hayupo,"alizidi kunichanganya.
"Amehamishwa vipi sasa mbna sijapewa taarifa, na
huko alikohamishwa ni wapi,?"nikiuliza maswali
mfurulizo lakini hakunijibu nikahisi ananioima imani
nikaenda kukaa pale pale nikiwa nimepanga jambo
la kufanya dakika kadhaa nikiw pale ndipo
nikamuona muuguzi akiingia looh, sikusubiri
niliingia nae humo humo yeye akiwa kabeba kibaketi
kilichoonekana na mikasi nilipoingia nikakimbilia
kuangalia pale looh john hakuwepo, nusura nipige
kelele bahati nzuri dokta aliniona akaniwahi kunitoa
huku akifoka na kuniambia watu hawaingii huku,
nilihisi kurukwa na akili ila nikiwa pale nje ndipo
simu yangu ilipata uhai na kuanza kuita niliitizama
namba ilikuwa ngeni sikujishughulisha nayo nilibofya
kitufe cha kuzimia simu japo sikuizima nilifanya
hivyo kutoa sauti iliyokuwa ikitoka ikabidi nirudi
tena mapokezi ila kabla sijafika simu iliita tena
hapo ikabidi niipokee wakati huu nilipopokea
nikaisikia sauti ambayo haikuwa ngeni masikioni
mwangu.
"Samahani shem John tumemhamishia huku
mloganzila hivyo chukua bajaji hapo utamwambia
akulete huku."alisema kisha simu ilikatwa hakutaka
kuniruhusu niongee, nilichukizwa na jambo hilo yani
amemhamisha john bila kuniambia Nilitoka hima
hima mpka kufika nje hapo niliona bajaji
zilizojiweka kwa ajili ya safari nilipanda moja.
"Samahani kaka naomba unipereke hospital ya
mlugunzela,"
"Mlugunzela ndio wapi,?"
"Si hospitali,"
"Ni mloganzila ndio panaitwa hivyo,"
"Aah mimi sipajui ila si bora umeelewa basi
nipereke huko,"nilimwambia akanitajia nauli ya mpka
kufika huko nilimwambia pesa sio tatizo bora nifike
tu.
Safari ilikuwa ndefu tukivipita vituo kadhaa mpka
kufika huko, ilikuwa hospital kubwa kwa kiasi chake
nikampigia simu rafiki yake John akanielekeza
sehemu alipo deleva bajaji alinifikisha mpka pale
hapo akalipwa pesa yake na kuondoka alinipa
maelekezo kadhaa huku akinianbia john anapata
nafuu pia huku tunaruhusiwa kumuona maneno yake
kidogo yalipunguza hasira nikizokuwa nazo,
tukaingia hapo moja kwa moja alinipereka
alipolazwa john, huku pia alikuwa akipumua kwa
kutumia mashine pia kichwani alikuwa na mabendeji
mengi yaliozunguka kichwa chake, nilikaa pembeni
yake nikimuangalia tu huku nilijaribu kumuongelesha
ila hakuna kikichoonesha uwepo wake hakika
alikuwa nusu binadamu nusu mfu, furaha yangu
ilikuwa kumuona john nilijitahidi kufanya maombi
nikimuombea kwa mungu apone haraka hatimae
tulimaliza mwezi mluganzila, siku moja nikiwa
nimekaa nimeshika mkono wa John uliokuwa
umebanwa na kibanio kidoleni, nilimshikilia huku
nikigusa kifua chake na mkono wangu mwengine
john alikuwa kimya, nikiwa nimemshika alianza
kuchezesha kidole chake ndipo nilipopiga kelele
nikimuita daktari niliamka kabisa na kutoka nje
nikimuita daktali nae alikuja akiwa na vifaa vyake
alianza kumpima john dakika kadhaa mapigo ya
moyo ya john yalianza kupungua kabisa, nilitizama
kwenye mashine amabyo ilikuwa pembeni yake
ikionesha mapigo yake ya moyo, daktari alinitoa
ndani pale nisijue kinachoendelea rafiki john nae
akikuwa pale hapo ndio dokta aliniita baada ya
kutoka ndani, akiniambia nimfate ofisini kwake.
"Nimekuita hapa peke yako nakuomba uwe na
ujasiri,"dokta alisema hapo nilikaa kimya
nikmsikiliza.
"Kidawa,"
"Abee,"
"Pole sana kidawa,"
"Pole ya nini dokta,"
"John hatupo nae tena, pole sana Kidawa."dokta
alisema, sikumwelewa nikimuomba arudie tena.
"John amefariki Kidawa"dokta alirudia hapo ikawa
ndio kama amenipandisha kichaa changu, nikipiga
kelele, nikatoka nje nikikimbia sikujua ninachofanya
nilijikuta nikiongea vitu visivyoelewka hapo nikaanza
kuvua nguo looh, kabla sijamaliza iliyopo ndani
nikishikiliwa na watu walionifunga kamba ilionkana
wazi nimechizika sikuwa nikielewa ninachofanya.
Nilizidi kupiga kelele nikitaka waniachie nikaingizwa
kwenye gari, nilirusha rusha miguu lakini haikusaidia
kamba ilinikamata vyema.
MWISHO

Safi sana... Bonge la story...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom