bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,099
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 21
NA Gaooh TheAuthor
SIMU=0654387935
TULIPOISHIAA SEHEMU ILIYOPITA
Nilihisi kuchoka ila ilinibidi niendelee na safari
yangu, nikiwa safarini kelele za watu pamoja na
sauti za wanyama zilinipokea nilianza kusikia, hapo
kidogo nilipata tumaini, tumaini jipya la kuwa
nakaribia makazi ya watu nilizidi kukazana tena
wakati huu nilikimbia ili nifike kwa wakati looh! cha
ajabu sauti zile hazikuwa zikifikika yani kila
ninapojitahidi nifike ndio nazo zinazidi kusogea
mbali nami NILICHOKA nikasimama..
SASA ENDELEAAAA
“MUNGU NISAIDIE,” nilisema maneno hayo ambayo
mimi tu ndio nilielewa ila kama ungebahatika kuwa
pembeni yangu katika umbo langu hili la paka
usingeelewa nilichosema zaidi ya kusikia sauti ya
nyau tu,Mungu wetu ni mwepesi kusamehe na siku
zote anaweka njia sehemu ambayo ulidhani
hutaweza kupita ukimuomba anatimiza haijalishi
umefanya mabaya kiasi gani, hata sisi wachawi
huwa tunaomba mungu atusaidie hata waganga pia
humuomba Mungu ili wakamilishe kazi zao,
nilipoomba kwa kusema Mungu anisaidie hapo
nikaamka nikiamini nitasaidika kisha nikaanza
kuondoka tena, wakati huu sikuangalia nyuma tena
nilikuwa nikitembea kisha muda mwengine
nikikimbia ili niwahi japo jua halikuacha kunichoma
ila nilijikaza ili nitimize nilichokianza baada ya
kutembea umbali mrefu MUNGU si athumani’
nilianza kuhisi upepo ukipuliza huku mawimbi nayo
nikiyasikia, Kwa akili zangu nilijua hapo ni baharini
na kweli kulikuwa baharini wakati huu nilipotokea
kweli niliyaona maji, hapo nilimshukuru Mungu, na
kuyasogelea maji yale.
Nilitembea pembeni yake nikitafuta chochote cha
kula lkama si Samaki basi nipate hata wale wadudu
wa ndani ya Maji, baada ya kutembea kidogo
nilifanikiwa kupata hapo nilianza kula samaki yule
ambaye alikuwa ametolewa pembeni na mawimbi,
nilipommaliza nilijihisi kutosheka, sikuwa
nimekatisha adhima yangu, sikutaka kuendelea
kuishi kwa mateso tena hivi niliamua nitafute
makazi ya watu ambako nitaishi nao,
Niliondoka baharini pale sikuwa nikipajua ni bahari
gari japo inajulikana ni bahari ya hindi ila sehemu
ile sikuijua ni wapi, sauti za watoto nilizisikia,
wakikuwa wakicheza mpira juu ya mchanga huku
wengine wakiwa wamekaa ufuoni hapo wakitizama
maji na wengine wakiogelea nilipita pembeni yao,
mana nilihofia wanaweza kunidhuru nilipita mbali
kabisa kwenye njia, ufuo huo ulijawa na minazi
pamoja na makoche, eneo kubwa ilijaa miti hiyo
pamoja na miti midogo ya miba, nilifatisha njia
nikidhamiria kufika eneo wanalo ishi binadamu, hasa
nikijua wazi sehemu amabyo nitafika itakuwa ni
makazi ya familia za kivuvi yani wanaotegemea
samaki kama kitoweo na hata chanzo cha mapato
yao, KIDAWA mimi nilifika kwenye kijiji hicho
ambacho kilikuwa sio kikubwa sana kwa
kinavyoonekana POPOTE KAMBI’ ndivyo akili yangu
ilivyonituma, hata miguu na nyayo zangu zilijaa sugu
na kuwa nyeusi tii na zile kucha za mikono na
miguu zilikuwa ndefu japo sio sana, siku hii niliingia
kwenye moja ya nyumba na kujifanya mwema
sikutaka wanione nilikimbilia juu ya dari, nilitaka
nijipendekeze kwao kwa kutoa msaada wa
kukamata panya kisha nipite nazo mbele yao ili
waniamini na kunifanya kama paka wao, ndivyo akili
zangu zilinituma na mimi nilifanya hivyo.
Kule dalini japo kulikuwa na giza ila nilijitahidi
kukaa huko, nyumba hii ilionekana kusumbuliwa na
panya sana kwani hata kule dalini hawakuacha
kukimbizana kwenye miti iliyopotengeneza dali lile,
hapo ndipo nikajipa ujiko nilikamata mmoja wa
panya ambaye alikuwa mkubwa kiasi chake baada
ya kumkata nilimtuliza sikumla limng’ata hadi pale
alipokufa ndio nikamueka chini, jioni familia ile
ilijumuika alikuwa ni baba, mama na watoto wao
watatu, nilipowaona wamekaa ndipo nikashuka na
panya wangu akiwa mdomoni, nilipotokeza tu
mmoja wa wale watoto alitaka kunirushia ndala
anipige hapo nikasita hata kutembea.
“Fai muache si unaona amekamata panya
wanaotusumbua usimpige,”mama yake alisema,
hapo yule mtoto ambaye anaitwa fai ndipo akaweka
ile ndala chini na mimi nikapita kwa maringo na
panya wangu mdomoni, kutokana na kujitolea
kuwasaidi kumaliza panya walinza kuniamini wiki
moja tu ilitosha kujenga imani na familia ile
wakanifanya kama paka wao sasa shombo za
samaki pamoja na utumbo walikuwa wakinipa hata
ugali pia walinirushia na mimi nilikuwa nikila kama
paka wengine, watoto wa mama yule walipenda
kucheza nami mara nyingi walikuwa wakinifukuza
nami nikiwafukuza kama mchezo walinipa mpaka
jina tasii, tasii nililizoea jina lile kila waniitapo
niliwatiii.
Nilipata falaja kuishi maisha haya mapya japo ya
kinyama ila yalikuwa na ahueni tofauti na polini,
familia hiii ilinijari vilivyo, Siku moja fai alikuwa
akielekea sokoni ikabidi nimfate nae alipenda
nifatane nae na mimi nikamfata alifurahia eti
kwavile nilimtii kwa kila kitu hakujua kuwa mimi ni
binadamu, tulifika sokoni akanunua alichoagizwa
alininunulia embe la kuiva lilimenywa kish
akanitupia hapo nilianza kula sikuwa nimekula muda
mrefu embe, hivyo nilijiona wa thamani sana kwao
hatukuchukua muda mrefu tukarudi nyumbani nilirudi
dalini kukamata panya kila siku ilikuwa ni lazima
nikamate panya alafu kwa sifa napita na panya
mbele yao ili wajue nawasaidia.
Niliamini haya yanamwisho, kwavile hakuna lenye
mwanzo likakosa mwisho, sikuzaliwa paka siwezi
kufa nikiwa paka, Najua ni jambo gumu sana hata
wewe ukiambiwa uishi kwenye mwili wa mnyama
sidhani kama utakubali japo hata mimi sio kwa
kupenda kwangu, Nilitokomea ufuoni nikatafuta
sehemu nzuri yenye jiwe kisha nikakaa hapo
nilienda kwa lengo moja tu la kutaka msaada
nilitaka wanisaidie kunirudishia umbo langu la
kawaida nilijaribu kutumia njia kadhaa kuwaita
hazikusaidia.
“Hahahahahahahahahahahahahahaha hahahaha
hahaha,” zilikuwa ni sauti za vicheko ambazo
zilikuwa zikinicheka nilipotazama hapo kidogo
nikataka kukimbia ila nilikuwa kati kati walikuwa ni
watu ambao niliwaua kichawi kuanzia Hajji wa
kijijini mpka wale wezi, hata zile kafara tulizofanya
na bibi pamoja na vitoto ambavyo wakati huo
vilikuwa vidogo sasa eti wote wamekuwa wakubwa
nao wananichekea kisha alitokea mzee ambaye
kavalia mavazi meupe.
“Hatuna msaada na wewe, ulijisahau na kuvuka
mipaka,” “muda wa kukurudisha utakuja lakini sio
sasa, utafika muda tutakurudish aufanye kazi zetu
inavyotakiwa” mzee yule alisema huku sauti yake
ikiwa kama ya mwango yani inajirudia rudia.
Nilimuomba anisaidie niwe binadamu wa kawaida
nilijua ananisikia kila ninavyomuomba wale watu
walicheka huku yeye akinipinga na kusema siwezi
saidika kwa sasa, “hatuwezi kukusaidia mpaka
muda ufike” “ muda gani huo mnaniacha nataabika
hivi inamana nilivyowatumikia vyote ndio mnilipe
hivi’ “sina msaada nawe” alisema na kupotea na
watu wale Machozi yalinitoka, uchungu uliniandama
nikifikili kuishi hivyi mpaka huo muda wao ufike,
nilikuwa nimechanganyikiwa zaidi siku hii nilirudi
kimya kimya na kukaa dalini bila kutoka.
“Fai mbona leo sijamuona atakuwa wapi?” mama
fai alikuwa kiuliza baada ya kutokuniona siku nzima,
kila alimuuliza hapo ndani walisema hawakuniona,
mimi nilikuwa nimetulia dalini mawazo
yakiniandama, nilikuwa nikitoka usiku tu kwenda
kutafuta chakula hata panya niliokuwa nikiwapata
nilikuwa dalini bila kushuka nao walinitafuta sehemu
kadhaa bila kuniona.
Usiku mmoja nilishuka, siku hii nilipanga niondoke
nyumbani pale kabisa japo niliishi nao vizuri ila
nilihitaji kwenda mbali zaidi kupata usaidizi
mkubwa, niliondoka kimya na kufata njia ya sokoni
nikiamini nitapata bara bara ya magari, ambayo
itanipereke sehemu tofauti na hapo nilizunguka
sehemu kadhaa sikufanikiwa kuona njia ilionekana
huku nilipo ndio mwisho yani nilipotoka kule
msituni ndio kuna njia ya kwenda mji mwengine ila
huku nilipokuja ni mwisho yani kumezungukwa na
maji mbele pamoja na kushoto na kulia, nilifikilia
kurudi nilipotoka kulikuwa mbali zaidi.
NA Gaooh TheAuthor
SIMU=0654387935
TULIPOISHIAA SEHEMU ILIYOPITA
Nilihisi kuchoka ila ilinibidi niendelee na safari
yangu, nikiwa safarini kelele za watu pamoja na
sauti za wanyama zilinipokea nilianza kusikia, hapo
kidogo nilipata tumaini, tumaini jipya la kuwa
nakaribia makazi ya watu nilizidi kukazana tena
wakati huu nilikimbia ili nifike kwa wakati looh! cha
ajabu sauti zile hazikuwa zikifikika yani kila
ninapojitahidi nifike ndio nazo zinazidi kusogea
mbali nami NILICHOKA nikasimama..
SASA ENDELEAAAA
“MUNGU NISAIDIE,” nilisema maneno hayo ambayo
mimi tu ndio nilielewa ila kama ungebahatika kuwa
pembeni yangu katika umbo langu hili la paka
usingeelewa nilichosema zaidi ya kusikia sauti ya
nyau tu,Mungu wetu ni mwepesi kusamehe na siku
zote anaweka njia sehemu ambayo ulidhani
hutaweza kupita ukimuomba anatimiza haijalishi
umefanya mabaya kiasi gani, hata sisi wachawi
huwa tunaomba mungu atusaidie hata waganga pia
humuomba Mungu ili wakamilishe kazi zao,
nilipoomba kwa kusema Mungu anisaidie hapo
nikaamka nikiamini nitasaidika kisha nikaanza
kuondoka tena, wakati huu sikuangalia nyuma tena
nilikuwa nikitembea kisha muda mwengine
nikikimbia ili niwahi japo jua halikuacha kunichoma
ila nilijikaza ili nitimize nilichokianza baada ya
kutembea umbali mrefu MUNGU si athumani’
nilianza kuhisi upepo ukipuliza huku mawimbi nayo
nikiyasikia, Kwa akili zangu nilijua hapo ni baharini
na kweli kulikuwa baharini wakati huu nilipotokea
kweli niliyaona maji, hapo nilimshukuru Mungu, na
kuyasogelea maji yale.
Nilitembea pembeni yake nikitafuta chochote cha
kula lkama si Samaki basi nipate hata wale wadudu
wa ndani ya Maji, baada ya kutembea kidogo
nilifanikiwa kupata hapo nilianza kula samaki yule
ambaye alikuwa ametolewa pembeni na mawimbi,
nilipommaliza nilijihisi kutosheka, sikuwa
nimekatisha adhima yangu, sikutaka kuendelea
kuishi kwa mateso tena hivi niliamua nitafute
makazi ya watu ambako nitaishi nao,
Niliondoka baharini pale sikuwa nikipajua ni bahari
gari japo inajulikana ni bahari ya hindi ila sehemu
ile sikuijua ni wapi, sauti za watoto nilizisikia,
wakikuwa wakicheza mpira juu ya mchanga huku
wengine wakiwa wamekaa ufuoni hapo wakitizama
maji na wengine wakiogelea nilipita pembeni yao,
mana nilihofia wanaweza kunidhuru nilipita mbali
kabisa kwenye njia, ufuo huo ulijawa na minazi
pamoja na makoche, eneo kubwa ilijaa miti hiyo
pamoja na miti midogo ya miba, nilifatisha njia
nikidhamiria kufika eneo wanalo ishi binadamu, hasa
nikijua wazi sehemu amabyo nitafika itakuwa ni
makazi ya familia za kivuvi yani wanaotegemea
samaki kama kitoweo na hata chanzo cha mapato
yao, KIDAWA mimi nilifika kwenye kijiji hicho
ambacho kilikuwa sio kikubwa sana kwa
kinavyoonekana POPOTE KAMBI’ ndivyo akili yangu
ilivyonituma, hata miguu na nyayo zangu zilijaa sugu
na kuwa nyeusi tii na zile kucha za mikono na
miguu zilikuwa ndefu japo sio sana, siku hii niliingia
kwenye moja ya nyumba na kujifanya mwema
sikutaka wanione nilikimbilia juu ya dari, nilitaka
nijipendekeze kwao kwa kutoa msaada wa
kukamata panya kisha nipite nazo mbele yao ili
waniamini na kunifanya kama paka wao, ndivyo akili
zangu zilinituma na mimi nilifanya hivyo.
Kule dalini japo kulikuwa na giza ila nilijitahidi
kukaa huko, nyumba hii ilionekana kusumbuliwa na
panya sana kwani hata kule dalini hawakuacha
kukimbizana kwenye miti iliyopotengeneza dali lile,
hapo ndipo nikajipa ujiko nilikamata mmoja wa
panya ambaye alikuwa mkubwa kiasi chake baada
ya kumkata nilimtuliza sikumla limng’ata hadi pale
alipokufa ndio nikamueka chini, jioni familia ile
ilijumuika alikuwa ni baba, mama na watoto wao
watatu, nilipowaona wamekaa ndipo nikashuka na
panya wangu akiwa mdomoni, nilipotokeza tu
mmoja wa wale watoto alitaka kunirushia ndala
anipige hapo nikasita hata kutembea.
“Fai muache si unaona amekamata panya
wanaotusumbua usimpige,”mama yake alisema,
hapo yule mtoto ambaye anaitwa fai ndipo akaweka
ile ndala chini na mimi nikapita kwa maringo na
panya wangu mdomoni, kutokana na kujitolea
kuwasaidi kumaliza panya walinza kuniamini wiki
moja tu ilitosha kujenga imani na familia ile
wakanifanya kama paka wao sasa shombo za
samaki pamoja na utumbo walikuwa wakinipa hata
ugali pia walinirushia na mimi nilikuwa nikila kama
paka wengine, watoto wa mama yule walipenda
kucheza nami mara nyingi walikuwa wakinifukuza
nami nikiwafukuza kama mchezo walinipa mpaka
jina tasii, tasii nililizoea jina lile kila waniitapo
niliwatiii.
Nilipata falaja kuishi maisha haya mapya japo ya
kinyama ila yalikuwa na ahueni tofauti na polini,
familia hiii ilinijari vilivyo, Siku moja fai alikuwa
akielekea sokoni ikabidi nimfate nae alipenda
nifatane nae na mimi nikamfata alifurahia eti
kwavile nilimtii kwa kila kitu hakujua kuwa mimi ni
binadamu, tulifika sokoni akanunua alichoagizwa
alininunulia embe la kuiva lilimenywa kish
akanitupia hapo nilianza kula sikuwa nimekula muda
mrefu embe, hivyo nilijiona wa thamani sana kwao
hatukuchukua muda mrefu tukarudi nyumbani nilirudi
dalini kukamata panya kila siku ilikuwa ni lazima
nikamate panya alafu kwa sifa napita na panya
mbele yao ili wajue nawasaidia.
Niliamini haya yanamwisho, kwavile hakuna lenye
mwanzo likakosa mwisho, sikuzaliwa paka siwezi
kufa nikiwa paka, Najua ni jambo gumu sana hata
wewe ukiambiwa uishi kwenye mwili wa mnyama
sidhani kama utakubali japo hata mimi sio kwa
kupenda kwangu, Nilitokomea ufuoni nikatafuta
sehemu nzuri yenye jiwe kisha nikakaa hapo
nilienda kwa lengo moja tu la kutaka msaada
nilitaka wanisaidie kunirudishia umbo langu la
kawaida nilijaribu kutumia njia kadhaa kuwaita
hazikusaidia.
“Hahahahahahahahahahahahahahaha hahahaha
hahaha,” zilikuwa ni sauti za vicheko ambazo
zilikuwa zikinicheka nilipotazama hapo kidogo
nikataka kukimbia ila nilikuwa kati kati walikuwa ni
watu ambao niliwaua kichawi kuanzia Hajji wa
kijijini mpka wale wezi, hata zile kafara tulizofanya
na bibi pamoja na vitoto ambavyo wakati huo
vilikuwa vidogo sasa eti wote wamekuwa wakubwa
nao wananichekea kisha alitokea mzee ambaye
kavalia mavazi meupe.
“Hatuna msaada na wewe, ulijisahau na kuvuka
mipaka,” “muda wa kukurudisha utakuja lakini sio
sasa, utafika muda tutakurudish aufanye kazi zetu
inavyotakiwa” mzee yule alisema huku sauti yake
ikiwa kama ya mwango yani inajirudia rudia.
Nilimuomba anisaidie niwe binadamu wa kawaida
nilijua ananisikia kila ninavyomuomba wale watu
walicheka huku yeye akinipinga na kusema siwezi
saidika kwa sasa, “hatuwezi kukusaidia mpaka
muda ufike” “ muda gani huo mnaniacha nataabika
hivi inamana nilivyowatumikia vyote ndio mnilipe
hivi’ “sina msaada nawe” alisema na kupotea na
watu wale Machozi yalinitoka, uchungu uliniandama
nikifikili kuishi hivyi mpaka huo muda wao ufike,
nilikuwa nimechanganyikiwa zaidi siku hii nilirudi
kimya kimya na kukaa dalini bila kutoka.
“Fai mbona leo sijamuona atakuwa wapi?” mama
fai alikuwa kiuliza baada ya kutokuniona siku nzima,
kila alimuuliza hapo ndani walisema hawakuniona,
mimi nilikuwa nimetulia dalini mawazo
yakiniandama, nilikuwa nikitoka usiku tu kwenda
kutafuta chakula hata panya niliokuwa nikiwapata
nilikuwa dalini bila kushuka nao walinitafuta sehemu
kadhaa bila kuniona.
Usiku mmoja nilishuka, siku hii nilipanga niondoke
nyumbani pale kabisa japo niliishi nao vizuri ila
nilihitaji kwenda mbali zaidi kupata usaidizi
mkubwa, niliondoka kimya na kufata njia ya sokoni
nikiamini nitapata bara bara ya magari, ambayo
itanipereke sehemu tofauti na hapo nilizunguka
sehemu kadhaa sikufanikiwa kuona njia ilionekana
huku nilipo ndio mwisho yani nilipotoka kule
msituni ndio kuna njia ya kwenda mji mwengine ila
huku nilipokuja ni mwisho yani kumezungukwa na
maji mbele pamoja na kushoto na kulia, nilifikilia
kurudi nilipotoka kulikuwa mbali zaidi.