Simulizi ya kusisimua

Simulizi ya kusisimua

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
KIDAWA (sijivunii Uchawi)
Kipande cha 1
Na Gaooh
Simu=0654387935
Nawakaribisha wote kwa pamoja kusoma simulizi
hii ya kuvutia.
Katika makuzi yangu sikuwahi kumuona baba wala
mama, sura pekee niliyowahi kuiona pindi tu napata
fahamu za kitoto alikuwa ni bibi, tangu niweze
kuongea na kujielewa sikuona ndugu yoyote
nyumbani kwetu zaidi ya majirani tu ambao nao
walitutenga hakuna alieshirikiana nasi, japo nilifanya
juhudi kadhaa ikiwemo kukataa kula na hata
kutishia kutoroka ili tu bibi anieleze walipo wazazi
wangu lakini haikuwa rahisi wala haikuwezekana
kama nilivyotaka, naweza sema bibi ndio alikuwa
baba, mama, na hata familia nzima, Kidawa ndio
jina langu nina umri wa miaka kumi na tisa sasa
(19) nimeishi nikimtumikia bibi yangu katika kazi
zake, nilijua fika bibi yangu ni mchawi kweli ni
mchawi mara kadhaa alikuwa akiondoka usiku na
kuniacha peke yangu kitandani,na hata sikunyengine
kuondoka na mimi, nilishakula nyama nyingi sana
usiku alikuwa akileta nyama na kunilazimisha nile
zilikuwa mbichi alinilisha kwa lazima kisha nikila
ndio inakuwa furaha yake, vitendo vile vilinifanya
nizoee kiasi kwamba bibi akitoka na asiporudi na
nyama mbichi huwa namlilia,mazoea yalijenga tabia.
Usiku mmoja nikiwa nyumbani,niliandaa chakula
ulikuwa ni ugali na nyama sikujua ni nyama ya nini
bibi alireta na kunitaka niipike huku akisema kuna
wageni wake watakuja usiku huo, nilitii na kuanza
kupika saa kadhaa bibi aliingia, alikuwa peke yake
tofauti na nilivyodhania nitegemea angekuja na
wageni.
“Bibi, umerudi!” niliuliza.
“Ndio vip, chakula tayari?” nae aliuliza, hakuitika.
“ndio tayari bibi wageni wako, wako wapi?”
“Mbona wako hapa, we andaa chakula uweke
mezani ugeni wa leo ni mkubwa si kila binadamu
anaruhuskuwaona we bado mdogo kidawa ukikuwa
utawaona!”
“Hmmmm!” niliguna mana yalikuwa mapya sikutaka
kuingilia mambo ya watu niliandaa chakula kama
bibi alyoagiza na kuweka mezani sambamba na
maji ya kunawa, kisha nikaingia chumbani
kujipumzisha.
Mbali na kuwa na miaka zaidi ya kumi na tano ila
sikuwahi kwenda shule bibi hakutaka niende shule
jibpekee alilonipa ni kuwa “shule nitaenda
kufundishwa ujinga tu” hali ile ilinisumbua kipindi
cha utoto wangu nikiwaona wenzangu wakienda
shule huku wamevalia sale zao, walipendeza
kuwaangalia nilikuwa nikitamani ningekuwa mimi
sikuwa na bahati hiyo ila kwa sasa nishakuwa
mdada sitamani tena shule, nikiwa nimejilaza juu ya
kitanda cha kamba nilisiiki sauti ambayo nilitambua
fika ni ya bibi.
“Kidawa…kidawa..” niliamka kutoka kitandani na
kwenda nilipoitwa.
“Abee, Bibi”
“Ulikuwa umelala… kwani umeshakula!”
“Hapana, Bado ila sihisi njaa!”
“Kipi kimefanya usihisi njaa,”
“Hakuna chochote Bibi!”nilijibu huku nikijinyoosha.
“Leo kuna kazi tunatakiwa tukafanye pamoja ,”
“kazi?””Ndio mbona unashangaa kwani we ni mgeni
na kazi zangu!”
“hapana bibi,”
“sawa tunatakiwa tutoke sasa,” bibi alisema, hapo
yeye alikuwa kashavalia kaniki yake nyeusi,
alinivalisha na mimi kaniki nyengine, kisha alisema
tutoke nje tulitoka hapo nilishangaa kuona nyoka
mkubwa akiwa pale nje tena akiwa na mabawa,
japo tulishawahi kusafiri mara kadhaa kwa kutumia
usafiri wa aina mbali mbali ikiwemo ungo hata
farasi leo nilishangaa nilipandishwa kwenye nyoka
mwenye mabawa, sikulijali sana jambo hilo tulikwea
kisha safari ilianza, ilituchukua muda mchache
nyoka yule alitua kwenye moja ya jengo kubwa
ambalo tulitizamana nalo japo sikwenda shule ila
kusema maneno ya kiswahili niliweza, nilisema
jengo lile na kugundua palikuwa ni muhimbili,
sikuwahi waza ipo siku nitafika hapo, leo imekuwa
kama maajabu, bibi alinielekeza cha kufanya
aliniambia niking’ate kidole changu cha mwisho cha
mkono wa kushoto nami nilitii hapo nilishangaa
kuona umbo langu limebadilika sikuwa binadamu
tena nilikuwa paka bibi nae alibadilika na kuwa
pake mweusi mwenye madoa meupe shingo
aliniambia nimfate nami nilitii tukaingia wodini, mlizi
hakuwa macho wakati huo alikuwa amelala, hivyo
ikawa rahisi kupita muda wote nilikuwa
nikitetemeka juu ya muonekano wangu
ule,tuliongozana mpaka wodi ya wazazi tukaingia.
“Chagua wakike wawili!” bibi aliagiza, na mimi
nilikubali, nilikuwa nikifata maagizo ya bibi bila
kupinga nahisi haikuwa akili yangu kila alichosema
nilifanya nakumbuka siku ile tulibeba vichanga
vitano mimi nilibeba wawili yeye akachukua watatu
ambao wote tuliwachanganya ndani ya ungo kisha
kupakia kwenye nyoka tuliekuja nae na kuondoka
eneo lile, safari yetu ilitufikisha kwenye uwanja
mkubwa ambao ulikuwa kati kati ya msitu, uwanja
huo ulimea viginga vya moto sambamba na kelele
za hapa za hapa na pale wasichana waliimba na
kucheza huku wengine wakipiga ngoma wote
walikuwa wanazunguka.
“BIBi kuna nini hapa,”niliuliza.
“Tupo kwenye ibada ya kuchagua kiongozi mpya,
kiongozi wet wa zamani muda wake umeisha, leo
ndio analiwa nyama kisha nafasi yake anachukua
mtu mwengine,” bibi alinifafanulia tukio lile,
vichanga vile bibi alivipereka pale mbele kati kati ya
mduara ule aliniambia kuwa ni sadaka hivyo ni amri
wanapewa kila mmoja kuleta, wakati bibi
amepereka sadaka yake nilibaki mwenyewe
nimesimama hakuna mtu niliye mjua eneo lile
walikuwa wamama na vijana wengine walitisha jinsi
wanavyoonekana kila mmoja alikuwa yuko makini na
shughuli yake, bibi hakuwahi kurudi alicherewa
jambo hilo lilifanya usingizi uanze kunichukua
nilisinzia pale nilipokuwa nimekaa baada ya
kusimama kwa muda mrefu nilikaa mwishoni
nikaanza kusinzia, sikujua kilichoendelea eneo lile
mwishoe nilistuka nikajikuta nipo nyumbani tena juu
ya kitanda, “Bibi biibiii<” baada ya kuamka niliita
jina la bibi lakini sikuitikiwa nikahisi labda ameenda
kwenye kuni, lakini nilikumbuka kuni tayari nilikuwa
nimeleta za kutosha. “ Atakuwa ameenda wapi
mbona hakuniaga na hapa nyumbani je nimefikaje?”
nilijiuliza sikupata jibu, nilionelea ni bora niamke
kitandani nilipokuwa nimelala, niliamka na kutoka
nje kulikuwa tulivu eneo lote ni miti tu na sauti za
ndege ndio nilizisikia, nyumba yetu haikuwa karibu
na makazi wanayoishi watu wengine tulikuwa
tukikaa mbali kidogo, bibi aliwahi kunieleza kuwa
wanakijiji walimtimua baada ya kutaka kuchoma
nyumba yake ndio akaondoka na kukaa mbali
nao,sikuwa nikijua alipobibi japo nilipata fikra za
kuwa ni mtu mzima kama katoka atarudi nyumbani
mwenyewe, nilisubiri nikasubiri lakini hakurudi siku
hiyo.
Siku zilipita sikumuona bibi tena nikabaki kama
yatima sikuwa na ndugu wala rafiki upweke
uliniandama kuishi mwenyewe porini, niliamua
kuhama kule nilipokuwa naishi na bibi kisha nikarudi
sehemu ambayo wanaishi watu wengine, sikuwa na
mwenyeji pia hakuna aliekuwa akinijua, baada ya
mwendo wa hatua kadhaa nilifika kwenye moja ya
shamba ambalo lipo kando kando ya mto nilifika
pale kwa ajili ya kunywa maji, sikuwa nikijua
niendako nitafikia kwa na nani, baada ya kunywa
maji njaa nayo haikuacha kuonesha uwepo wake
nikajikalia chini ya mparachichi ambao haukuwa na
dalili ya kutoa matunda, nikiwa pale mawazo
yakiniandama kuwa wapi nitapata chakula kuistili
njaa nilikuwa nayo wakati huo ndipo alitokea
mwanamke akiwa amebeba jembe kichwani,
alionekana akitokea shamba, nilimsalimu baada ya
yeye kusimama akinisikiliza alikuwa ni mama wa
makamo nilimweleza kuwa nimepotea sijui nitokapo
wala niendapo, mama wawatu hakuwa na makuu
aliniambia kuwa niongozane nae nami nikatii hapo
nikampokea jembe alilobeba, tulifa mpaka
nyumbani aishimo, hakuwa na mume zaidi ya kuwa
na mtoto mmoja wa miaka tisa anaesoma darasa la
tatu.
“Naishi na mwanangu hapa anaitwa subira anasoma
darasa la tatu!”
Itaendelea.
Baada ya kitambo kirefu kutokana na changamoto
kadhaa sasa tumeamua kurejesha burudani kwenu
uongozi mzima wa Tungo Murua Za Kusisimua
Tungo Murua Za Kusisimua
Tunaomba ushirikiano wenu kama zamani.
like kisha share kwa wingi ili iwafikie watu wengi
pia unaweza kutag marafiki zako wapenzi wa tungo
za kusisimua
pia usisahau kuweka maoni yako tutayasoma.
 
Kipande cha 2
Na Gaooh
Simu= 0654387935
Tulipoishiaa..
nikiwa pale mawazo yakiniandama kuwa wapi
nitapata chakula kuistili njaa nilikuwa nayo wakati
huo ndipo alitokea mwanamke akiwa amebeba
jembe kichwani, alionekana akitokea shamba,
nilimsalimu baada ya yeye kusimama akinisikiliza
alikuwa ni mama wa makamo nilimweleza kuwa
nimepotea sijui nitokapo wala niendapo, mama
wawatu hakuwa na makuu aliniambia kuwa
niongozane nae nami nikatii hapo nikampokea
jembe alilobeba, tulifa mpaka nyumbani aishimo,
hakuwa na mume zaidi ya kuwa na mtoto mmoja
wa miaka tisa anaesoma darasa la tatu.
“Naishi na mwanangu hapa anaitwa subira anasoma
darasa la tatu!”
Tuendelee.
“baba yake yuko wapi?” nilihoji.
“Ni story ndefu ila baba yake subira alishafariki
miaka kadhaa iliyopita,”
“Pole sana, mama!”
“Asante mimi nimekwishapoa na maisha
yanaendelea, ila? Hujanitajia jina lako sijui waitwa
nani?” aliniuliza.
“Naitwa kidawa Mama!”
“Karibu mwanangu kama utakuwa tayari utaishi hapa
kwngu mpaka pale utakapo kumbuka kwenu, usijali
tutaishi tu hapa,”
“Nashukuru sana mama sikutegemea kama
nitakutana na mama mwema kama wewe
nimetembea porini kwa muda mrefu bila kujua wapi
nitafika kijiji nilichokuwa nikiishi nimekisahau,
nakushukuru mama Mungu akubaliki!” nilimshukuru,
nae alimwita mwanae akareta chakula nilifurahi
kukiona mana njaa iliniandamana tukala chakula na
familia ile.
Nilioneshwa sehemu ya kulala,nililala nikiwa mchovu
kiasi kwamba nilicherewa kuamka wenyeji wangu
walikuwa wameendoka tayari subira alikuwa
ameenda shule huku mama yake akienda shamba,
sikutaka kuwa mzigo niliamua kufanya usafi wa pale
nyumbani nikaosha vyombo na kuandaa chakula cha
mchana, mama aliporudi alinishukuru sana kwa
kumsaidia kazi maisha nilianza kuyafurahia yale
matukio niliyokuwa nikiyafanya na bibi sikuwa
nikiyaona tena, nilijiaminisha mambo ya uchawi
hayapo tena hata bibi nilimsahau kabisa.
Siku moja baada ya kumaliza kazi za nyumbani
niliamua niende kule nyumbani ambako nilikuwa
nikiishi na bibi nilijiandaa na safari ya kurudi,
sikujua kinirudishacho kule mana maisha mapya
yalishanivutia ya huku kwa mama subira,
haikunichukua muda mwingi nilifika mpaka pale
kwenye nyumba yetu, nilishangazwa na moshi
uliokuwa ukitoka juu ya paa ilinionesha wazi kuna
mtu anaishi ndani humo “Atakuwa ni nani? Mbona
bibi hakurudi muda mrefu hata nilipo msubiri!”
nilijiuliza kisha moja kwa moja nikajitoma ndani
kwenye uzio ambawo ulikuwa umezunguka nyumba
yetu kabla sijaufikia mlango, nilishangazwa na
nilichokiona Bibi, bibi alitoka ndani ya nyumba ile.
“Mjukuu wangu!” aliita bibi.
“Abee…bibi!” nami niliitika na kusogea pale alipo.
“Ulikuwa wapi mjukuu wangu nimekutafuta muda
mrefu, tangu siku ile tulipokwenda kwenye zile
sherehe sijakuona tena, umerudi vipi nyumbani
wakati tulienda wote kule?” alihoji, sikuwa na jibu
kwa vile nakumbuka hata mimi niklijikuta nyumbani
tu sikujua nimefikaje, nilimueleza ilivyokuwa kuanzia
nilivyojikuta nyumbani pia nilivyomsubiri hata ninapo
ishi sasa hivi kwa mama subir.
“pole mjukuu wangu, kwavile sasa hivi umepata
mwenyeji ni vizuri zaidi kisasi chetu tutakifanya
vizuri kwa kushirikiana kijiji cha ndekai
wametufanyia ubaya sana walivyotufukuza na
kuchoma nyumba yetu ni uadui tosha nilikuwa
nakujenga wewe uje ufanye kazi hiyo kwa urahisi
zaidi ila tayari naona unaelekea kwenye njia
niliyokuwa naitaka!”
“una maana gani Bibi?”
“Ni muda wa kuwatendea mabaya na maovu
wanakijijini wote wa ndekai<”
“sawa Bibi mimi ni kibaraka wako nafanya vile
utakavyo,” nilimkubalia bibi siku hiyo aliniambia
kuwa atanifanyia dawa na tambiko ambalo ndio
atakuwa amenitawaza rasmi kuwa mchawi kamili
huku akinikabidhi mkoba wa babu yangu ambaye
sikumjua.
“Leo utalala hapa nikufanyie dawa, na kukukabidhi
mkoba wa babu yako ambaye ni mume wangu,”
sikuwa na swali mara nilishachoka kuuliza maswali
ambayo hayakujibiwa na bibi.
Niliandaa chakula chetu mimi na bibi,chakula
ambacho bibi alipenda kukipika pumba za mahindi
ndio alipendelea kuzipika kama unga na nyama
ambayo mpaka leo hata uniulize ilikuwa nyama ya
nini siwezi kukujibu mana sikuwa nikijua inatoka
wapi nilijua kula tu na kuipika kama mboga, usiku
wa siku hiyo aliniambia tuongozane nilimfata mpaka
alipofika kwenye eneo ambalo lilitengwa likiwa na
makaburi, aliniambia nimsubiri ataniita nikasimama
nikimsubiri, nae aliingia katikati ya makaburi yale
akilipitia moja moja akaniita sikuwa na nguo wakati
huo nae hakuwa na nguo, yeye alikuwa ameshikilia
kibuyu pamoja na mwengo uliofanana na mkia wa
farasi, nilifika aliponiita.
“Zunguka kaburi hili huku, ukitamka yale maneno
niliyokuelekeza siku ile, kama umesahau nifatishe
ninavyotamka!” aliniambia nami nikaanza
kulizunguka kaburi lile huku nikimfatisha kama
anavyosema, yalikuwa ni maneno ya kichawi
yasioeleweka sikujua ni lugha gani ilitumika
kuyaandaa maneno yale mana hayakueleweka mimi
nilikalilishwa tu sikuwa nikiyajua, zoezi lile liliendea
mpaka pale mfu aliekuwemo ndani ya kaburi lile
akafufuka na kulala juu ya kaburi lile bibi alimchapa
na mwango yule mtu akamka mzima mzima, vile
vile akiwa amelala tuliondoka na mtu yule mpaka
chini ya mbuyu mkubwa ambao haukuwa mbali na
eneo lile.
“Leo ni siku yako mjukuu wangu,”Bibi alisema na
kunielekeza nikae chini miguu ninyooshe kuelekea
mbele, muda huo huo walitokea wazee wengine rika
la bibi wote kwa pamoja wakaanza kuimba na
kucheza kwa kunizunguka pale nilipokuwa, ile maiti
waliitenganisha vipande vipande kisha wakaweza
juu ya ungo, mzee mwengine alinisogezea chungu
ambacho kilijaa damu ndani yake sikujua ilipotoka,
pia nilishangaa matukio yale nilikuwa nikiyaona
vizuri kama nionavyo mchana hali ya kuwa ulikuwa
ni usiku tena wenye giza ilinishangaza, halikuwa
jambo geni kunywa damu hata kula nyama mbichi
tulikuwa kwa pamoja wakanivika cheo kuwa mimi
ndio mkuu wao, nilikuwa na maswali ya kumuuliza
bibi mana nilikumbuka siku ile tulienda kwenye
shereha na vitoto vichanga kwa ajili ya kumchagua
mkuubwa wao sasa iweje leo tena wanichague
mimi ndio mkubwa wao, nilibaki na swali hilo
nikijiahidi kumuuliza bibi pale tu shughuli hiyo
itakapo kwisha, hapa kuwa na watu wengi hivyo
ilichukua muda mchache tukamaliza zoezi hilo
nilijishangaa nimekuwa tofauti zaidi na mwanzo,
waliagana kisha tukarudi nyumbani kwa kupaa.
“Bibi mbona sijaelewa lile tukio pale?”
“kipi hujaelewa kidawa,”
“Iwje munichague kama mkuu wenu wakati
mlishamchagua ile siku kule?”
“Ile siku lilikuwa tukio kubwa la kumchagua
kiongozi mkubwa wa wachawi wote duniani, siku ile
kulikuwa na wachawi kutoka nchi mbali mbali, ndio
mana tulienda na nyoka kule ni nigeria sio tanzania
tukio lile hufanyika kila baada ya miaka kumi
wachawi wote huwa tuna mkuu wetu ambaye ni
mmoja mkubwa ila kuna makundi mengi hivyo kila
kundi linakuwa na kiongozi wake, ni kama serikali
kunakuwa na raisi mawaziri, wabunge,madiwani na
wenyeviti, sasa wewe ni kiongozi wa kikundi chetu
hiki na wale pale ndio watu wako ambao wataishi
wakikusikiliza wewe tu.” Bibi alinifafanulia kidogo
nikamuelewa.
Alinipa mafundisho kadhaa ikiwemo kuua kupotea
na hata kupaa alinifundisha kila kitu cha kushangaza
nilielewa vyote kwa muda huo huo, nilimuaga kuwa
narudi nyumbani kwa vile kulishakucha sikuaka
kupoteza nguvu kwa kutembea nilipotea na kutokea
nje ya nyumba ya mama subira, hakuna alieniona.
Ilikuwa ni asubuhi, si kwamba sikuweza kuingia
moja kwa moja ndani hapana niliweza ila sikutaka
kufanya vile, sikutaka kumuweka mashakani mama
subira, nikiwa pale nje mlango wa mama subira
ulifunguliwa alitoka subira alishangazwa kuniona
pale sijui ni woga sijui ilikuwa ni nini, hakutoka nje
aliingia ndani huku akiita ‘mamaa’
Itaendeleaa.
kipi kitaendeleaa usikose sehemu inayofuata.
 
Kipande cha 3
Na Gaooh
Simu=0654387935
Tulipoishiaa..
Ilikuwa ni asubuhi, si kwamba sikuweza kuingia
moja kwa moja ndani hapana niliweza ila sikutaka
kufanya vile, sikutaka kumuweka mashakani mama
subira, nikiwa pale nje mlango wa mama subira
ulifunguliwa alitoka subira alishangazwa kuniona
pale sijui ni woga sijui ilikuwa ni nini, hakutoka nje
aliingia ndani huku akiita ‘mamaa’
Tuendeleee
Hapo mama alitoka akiwa na wasi wasi na kuniona
nikiwa nimesimama.
“Kidawa!” aliita jina langu mama.
“Abeeh,”
“haya mwanangu ulikuwa wapi umetulaza macho
usiku wa kuamkia leo?” mama subira aliniuliza,
hapo nilika kimya nikimsikiliza huku nikitunga
uongo wa kumdanganya ili anielewe.
“Samahani sana mama,jana ilikuwa siku ndefu sana
kwangu niliondoka hapa nyumbani kwa ajili ya
kwenda kutembea nijue mitaa, ila nilipotea mama!”
niliongea huku machozi ya kulazimisha yakinitoka,
sikuishia hapo nilidanganya vingi mpaka kusema
nimelala chini ya mti machozi yangu ndio
yaklimuaminisha mama subira, aliamini kuwa
nimekutwa na dhahama hiyo, alinikumbatia huku
akinipa pole na kunifuta machozi.
“Usiwe unatoka mwenyewe ukiwa na shida ya
kutembea kama subira yupo mwambie akutembeze,
msituni kuna wanyama wakali mwanangu!”
nilimwitika akanikaribisha ndani, sikuwa mvivu
niliandaa chai asubuhi hiyo, subira hakwenda shule
ilikuwa siku ya mapumzikon hivyo tulijumuika
pamoja kunywa chai ile na mihogo ambayo Mama
Subira alishaiandaa, siku hiyo ilikuwa ya furaha
nilishinda nyumbani na Mama pamoja na Subira
siku kadhaa zilipita.
Baada ya kuamka nilifagia uwanja kisha kuelekea
kisimani baada ya maji ndani kuisha hivyo nilierekea
kisimani kuchota, nilikutana na wasichana kadhaa
walikuwa wakifua na wengine wakiteka maji,sikuwa
nimewaona kabla kwa vile mara nyingi mama
hakutaka niwe naenda mtoni akiogopa naweza
kupotelea huko hivyo aliniacha nifanye kazi za
nyumbani tu.
“We mshamba nani kakutuma uchote maji inamana
huoni kama ni foleni yetu,” aliongea mmoja ya wale
wasichana huku akinisogelea pale nilipokuwa
nimesimama na kushika kata.
“Samahani, si mlikuwa mmekaa pale wote unapiga
stori pia hakukuwa na mtu anaeteka hivyo ndo
mana nimekuja kuchota ningekukuta hapa
ningesubiri mpaka umalize!” nilijitetea, nilionesha
upole mbele yake, asivyona aibu alinimwagia yale
maji nusu nilikwisha anza kuyachota, wenzake
walimsema lakini hakusikia, sikujua kosa langu lipi.
“sophia huna aibu msichana wawatu ni mgeni hata
hukuwahi kumuona wewe unamparamia amekufanya
nini mpaka umtendee hayo!” wenzake walimwambia
hpo nimesimama kando nikikamua maji kwenye
kanga yangu ambayo nilitaka kuitumia kama ng’ata.
“na nyie niachane kinachowauma nini au ndio
mnaomba undugu ebu kwendeni huko,” aliongea na
msonyo ukimtoka hapo alikwisha chota tayari
akaondoka na kuwaacha wenzake pale ambao
wengine walikuwa wakifua, nikiwa nimesimama
alikuja mmoja na kunipa pole kisha kuanza
kunisaidia kuchota.
“Pole mwaya mzoee tu yule msichana anamatatizo
akishakorofishana na bwana wake basi ni visirani
tu,” alisema.
“asante nashukuru pia sijali, kwavile sijamkosea pia
simfahamu najua ni matatizo tu yake.”
“Unaitwa nani?” aliniuliza.
“Naitwa kidawa<”
“kidawa??”
“Ndio ninavyoutwa sijui wewe lako nani?”
“Mimi ukipenda waweza niita salome,”
“Oooh salome, sawa nashukuru kukufahamu acha
mi niende nyumbani mana ni muda wa kupika huu,”
“nyumbani kwenu ni wapi?, mana sikuwahi kukuona
kabla.”
“nakaa kwa mama subira!”
“Ooh, mama subira ndo nani wako?” aliniuliza huku
na yeye akichta ndoo yake kisha alipojaza akasema
tuongozane na stori zikiwa zinaendelea.
“Yule ni mama yangu mdogo, nimetoka kijiji cha
jirani!” nilimdanganya sikutaka kumweleza kila kitu,
tuliongozana mpaka kufika njia panda kila mmoja
akaelekea njia yake.
Nilifika nyumbani maji niliyatua siku hiyo mama
hakwenda shamba hivyo niliandaa chakula cha
mchana tukajumuika kula pamoja, subira
alishanizoea alinipanda kupita kiasi, muda mwingi
alipenda kucheza na mimi alipenda tufukuzane
kama watoto japo sikuwa mtu mzuri ila nilifarijika
sana maisha ya pale nyumbani, siku hiyo usiku
ulipofika nilikumbuka dharau za sophia nilimtafakari
cha kumfanya, kupitia harufu yake usiku ule ule
nilimtafuta mpaka kupajua kwao niliingia kwenye
pembe na kutekea karibu na kitanda chake
nilimkuta akiwa amelala huku ajitambui kabisa,
nilimwita bibi nae alikuja pale pale.
“Nimfanyaje huyu bibi amenikosea sana leo bila
kujua mimi nani?”
“Tumchinje~na tumle nyama,”
“Hapana bibi sitaki apotee, basi mpereke shambani
akalime umrudishe asubuhi,” nilitoa amli bibi
akamchapa na mwengo wake hapo kimvuli cha
sophia kilitoka na mwili ukabaki pale pale,
tuliongozana na bibi hadi mashambani ambako
kulikuwa na watu wengine wakilima tofauti wale
walikuwa ni misukule ambao tmewachukua jumla
jumla na kuwakata ulimi huku miili yao ikiwa
imekwisha zikwa kama migomba, huwa tukichukua
mtu msukule mwili wake unabaki kama gogo la
mgomba ambalo ndio watu huzika macho ya
kawaida ya binadamu huona ni mtu yule yule ila sisi
pamoja na baadhi ya watu wenye uwezo hasa
waganga huona picha halisi ya mwili ule pale
kitandani, sophia alijumuika na wenzake kufanya
shughuli za kulima nilimtumikisha huku nikimchapa
bakora pale tu anapoanza uvivu wa kukaa,
nilimsimamia hadi kulipokaribia kucha nikarudi nae
nyumbani tena alinibeba mgongoni nikamrudisha
kwao na mimi nikaenda kwetu hakuna aliejua kama
nilitoka kwa vile nilikuwa nikilala mwenyewe.
Hatimae kulikucha wachawi huwa mara nyingi
hatulali kama ni kulala labda mchana kwavile
shughuli zetu nyingi tunazifanya gizani, kila mtaa
haukosi wachawi kama si mmoja basi ni wawili,
siku hiyo nilikuwa na furaha sana kumsurubisha
sophia, nilienda tena kisimani kuteka maji, sikuhii
hakukuwa na watu wanaofua niliwaona tu wasichana
kadhaa wakichota maji nikajongea mpaka walipo
kabla sijafika nilishangazwa na mmoja wao kuhepa
pale walipo wenzake, hakuwa mwingine ni sophi
alichomoka moja kwa moja baada ya kuniona
nilishanganzwa nae,
“Kwani kuna nini mbona sophia amekimbia hivyo?”
mmoja wao aliuliza.
“Umemuona huyo msichana anaekuja ni mwanga
sophia amenihadithia kuwa alimuota anamlimisha
pia alipoamka asubuhi alijikuta amechoka na hata
miguuu yake ilijaa vumbi,” waliteta.
“Heeeh ndo huyu?”
“Ndio huyo huyo anaonekana mchawi kweli tizama
hata anavyotembea,” walizidi kuniteta, niliwasikia
japo sikuwa karibu nao, wachawi huwa tunambinu
tunatumia ambayo unaweza kusikia hata maongezi
ya mbali, niliwatizama wale vimbele mbele wote na
kuamaki vizuri, salome hakuwepo pale walikuwa
wasichana watatu na sophia wa nne ambaye yeye
alikimbia, nilipowakaribia wakaondoka wote bila
kuniongelesha hata nilipowasalimu walinisonya tu,
nikatabasamu na kuchota maji kisha nikaondoka
pale kurudi nyumbani.
Nilifanya kama kawaida yangu nao wale
niliwalimisha usiku mzima, kuwakomesha hapo
walianza kuniogopa mmoja mmoja hiyo ni baada ya
siku moja kuwatishia kuwa nitawapoteza wote
waache kunifatilia pia waache kunisema sema
nitawauwa na kuwatafuna mmoja mmoja, walitishika
na kuniogopa nilibaki na rafiki yangu salome tu
ambaye hakuwa akisikia maneno ya watu kuhusu
mimi alinipenda na mimi nilimpenda sikuwaza
kumfanyia ubaya wowote.
Siku moja usiku nilitembelea nyumbani kwa bibi,
aliniita akitaka kunipa kazi maalum, ambayo sikuwa
nikiijua hapo awali.
“Mjukuu wangu, mimi nataka uanze kazi,”
“Kazi gani hiyo bibi?” nilihoji.
“Nataka hapo kijijini kusizaliwe kichanga chochote,
kila mwanamke mwenye mimba uhakikishe
inaharibika kabla ya kujifungua kisha vichanga vyote
tutatumia kama kafara,” bibi alisema.
Itaendeleaa
 
Kipande cha 4
Na Gaooh
Simu=0654387935
Tulipoishiaa..
Siku moja usiku nilitembelea nyumbani kwa bibi,
aliniita akitaka kunipa kazi maalum, ambayo sikuwa
nikiijua hapo awali.
“Mjukuu wangu, mimi nataka uanze kazi,”
“Kazi gani hiyo bibi?” nilihoji.
“Nataka hapo kijijini kusizaliwe kichanga chochote,
kila mwanamke mwenye mimba uhakikishe
inaharibika kabla ya kujifungua kisha vichanga vyote
tutatumia kama kafara,” bibi alisema.
Sasa endeleaaaa…
“Bibi kazi hiyo nitaiwezaje peke yangu,”
“Huwezi kuifanya peke yako wapo watu utashirikiana
nao kuikamilisha hata mimi nitakuwepo ni muda wa
wanakijiji kulipia walichonifanyia<” alisema bibi kwa
msisitizo, nilimkubalia kisha akanipa maagizo
machache na kuniruhusu niondoke.
Niliondoka nikiwaza agizo lile, ni kweli wasichana
kadhaa niliwaona wakiwa na mimba kijijini hapo,
niliwaza jinsi watakavyoumia baada ya kupoteza
mimba zao, nilifikiria ila sikujali, tuliianza kazi ile
kila siku tulitoa mimba zaidi ya tano kwa wasichana
tofauti, japo nilikuwa mchawi ila kuna kipindi
nilihudhunika, wasichana waliokuwa wakikaribia
kujifungua tulichukua watoto na mama zao
kuwafanya misukule, kijiji kilianza kutisha kila
mmoja aliogopa, watu wengi walijua ni lana
imeingia kijijini walifanya matambiko lakini
hayakusaidia chochote watu waliendelea kupotea
kila kuitwapo leo watoto walipote na hata mimba
zilipotea.
“kidawa hivi we huogopi hii hali inayoendelea hapa
kijijini?” salome aliniuliza.
“Hali gani mbona kupo kawaida tu?”
“Inamana wewe huoni jinsi watu wanavyokufa kila
siku,”
“Hiyo si mipango ya mungu tu jamani,”
“Mipango gani ya mungu huoni kama kijiji chetu
uchawi umeshaenea sasa kwanini unapenda
kutembea usiku peke yako,”
“Kawaida mi sijali bana, mbona mi siogopi,” salome
alikuwa na wasi wasi juu ya usalama wangu ni wazi
alinipenda kweli kweli, mbali na uchawi niliopewa
na bibi ila nilionekana mpole sana machoni mw
watu hata ukiambia mimi ni mchawi uwezi kuamini
hata ukiniona waweza sema nimesingiziwa nilikuwa
mpole alafu mkarimu, tulikuwa tukiongea huku
tukielea sokoni ilikuwa siku ya mnada tulifika na
kununua mahitaji yetu wakati tunarudi walikuja
vijana wawili ambao walimsalimia salome kuonesha
wanamjua kisha wakanisalimia na mimi huku
mmoja akiniuliza jina langu, tukagawana salome
aliongozana na mmoja na mimi nikaongozana na
mmoja.
“Unajua kidawa wewe ni msichana mrembo sana,
hupaswi kuwa peke yako bila mpenzi,” alinihadaa.
“kwanini?”
“ Unapaswa uwe na watu wenye upendo wa dhati
kama mimi kisha uolewe uwe mke wa mtu lakini
ukikaa nyumbani tu watakuja waharibifu
watakuchezea chezea mwisho wakupe mimba
wakutelekeze, mi naomba niwe wako kidawa nataka
nikutunze upendeze,”aliongea maneno ambao
niliona ni ujinga ujinga tu usiona na maana.
“mbona mimi naishi tu vizuri nakula nalala wala
sina shida ya mwanaume pia hutaniweza,”
“usiseme hivyo kimfaacho mtu chake nashindwaje
kukuweza wakati unanifaa, nakuonaga siku nyingi
kidawa naogopa kukufata ila leo nimepata nafasi hii
ndio mana nimekufata nakupenda mwenzio,”
“haji mi nakuomba usinisumbue mimi si
mwanamke wa kuwa kwenye mahusiano wala si
mwanamke wa kuolewa ebu nakuomba acha
kupoteza muda wako kunidanganya mimi siwezi
kuwa na wewe.”nilimwita kwa jina lake ambalo
alijitambulisha kama anaitwa hajji.
“kidawa ukisema hivyo unaniweka katika wakati
mgumu unajua na mimi nina moyo, pia mimi
binadamu, tambua hilo,”
“bwana niachie kelele sitaki usumbufu,”” salome
kaheri mie nawahi nyumbani” niliondoka haraka
haraka sikutaka kuendelea kuwa pale, japo
nilitamani kuwa na mwanaume ila katika chama
chetu ni mwiko, nilijuafika hata nikiwa nae hawezi
kuvumilia etti aishi na mimi bila tendo, lazima
angetaka na sisi tumekatazwa kufanya tendo hilo
kwa kila atakae fanya hivyo basi huyo mwanaume
anafia hapo hapo sikutaka kumuingiza kwenye
matatizo.
Nilirudi nyumbani mama hakuwa amerudi wala
subira mama alienda shamba subira nae alienda
shule, nilianza kupika,.
“kidawa….kidawa….kidawa” ilisikika sauti pembeni
ya pale nilipokuwa nimeketi ilikuwa sauti nzito ya
kiume, niliitika nikisubiri agizo lake.
“ Tunataka kafara ya mtu wako wa karibu tunahitaji
watu watatu tu kati yao mmoja ndio umtoe sadaka
tena umtoe uhai wake wewe na umlete.”
“Sadaka gani hiyo mbona nimetoa nyingi kuna
ulazima gani nitoe watu wangu wa karibu mbona
tunakomoana,”
“Hahahahahahhahahahha, hili sio ombi tunataka
utoe mtu mmoja kati ya salome,subira au mama
yake,” alisema na kunistusha, aliposema akapotea
nilimpuuza “ Siwezi fanya hivyo!” nilijisemea,
kawaida ya uchawi ni kuwa japo utatoa kafara za
watuwengine wasiouhusu ila lazima ifike siku na
wewe utoe mtu umpendae ili nawe uone uchungu na
maumivu wayapatao wengine wengi huwa wanatoa
watoto wao, wanatoa wazazi wao na hata ndugu zao
wakaribu inakuwaga ni amri na si ombi.
Siku hiyo hata hamu ya kula sikuwa nayo ugali na
tembele la mafuta niliviangalia tu, sikujisikia kula
nilikuwa nikitafakari amri ile, “eti nitoe mtu wangu
wa karibu?”nilijiuliza, huku nikiwa na wakati mgumu
kung’amua, nilionelea bora nilale siku ilishaharibika
niliona umuhimu wa kila mmoja si salome, subira
wala mama subira wote walikuwa na umuhimu
kabla usingizi kunikuta niliendelea kujiwazia ‘sasa
watu wangu wa muhimu ikiwa sio ndugu zangu
nawatoaje watu ambao sihusiki nao!” nilibaki na
mshangao nikalala.
Nilikuja kustushwa na sauti ya mama akiniita hapo
niliamka kutoka usingizini nikatoka nje nilimkuta
akiwa na mzigo wa kuni kichwani nikamtua na
kuushusha chini, nilimpa pole na kuingia ndani
kumchukulia maji kwenye mtungi, alikunywa na
kushukuru hapo nilimwambia maji ya kuoga tayari
nimemuandalia hivyo akaoge tuje kula, subira
hakuwa amerudi.
Mama alipokuwa ameenda bafuni kuoga nami
nikiwa nimesimama alitokea mtu mbele yangu
akiwa amevaliwa nguo nyeupe juu mpaka chini huku
macho yake yakiwa yanawaka. “Kidawa,, ni lazima
utoe, ni lazima na wewe utoe na kama utakaidi amri
hii tutawatoa wote sisi wenyewe badala ya mmoja
tutachukua wote watatu, tutachukua wote watatu.”
“Hapanaaaa,hapanaaa.”nilipiga kelele.
Itaendeleaaa
kipi kitaendeleaa usikose sehemu inayofuata.
 
Kipande cha 5
Na Gaooh
Simu=0654387935
Tulipoishiaa
Mama alipokuwa ameenda bafuni kuoga nami
nikiwa nimesimama alitokea mtu mbele yangu
akiwa amevaliwa nguo nyeupe juu mpaka chini huku
macho yake yakiwa yanawaka. “Kidawa,, ni lazima
utoe, ni lazima na wewe utoe na kama utakaidi amri
hii tutawatoa wote sisi wenyewe badala ya mmoja
tutachukua wote watatu, tutachukua wote watatu.”
“Hapanaaaa,hapanaaa.”nilipiga kelele.
Sasa Endeleaa..
“Heeeeh, mwanangu hapana nini?” kumbe mama
alishatoka kuoga hivyo kelele nilizopiga aliizisikia
wakati napiga kelele mtu yule alishapotea machoni
kwangu, ilibidi nimdanganye mama tu kuwa nilikuwa
naimba, alikubali ila nilijua tu kuwa yeye ni mtu
mzima alijua kuwa nimemdanganya.
Niliandaa chakula huku nikiandamwa na mawazo
kiasi kwamba wakati napakuwa mboga nilijikuta
namwaga baada ya kuweka kwenye bakuli nikaweka
chini, mama aliona.
“kidawa unatatizo gani mwanangu mbona kama
haupo sawa?”
“’Hapana mama!”
“Unaonekana hauko sawa nambie mwanangu
kinachokusumbua?”
“Sina mama, ni maisha tu nawaza hatima ya maisha
yangu kama hivi sina ndugu zaidi yako, familia
yangu sijui ilipo yani ndio nawaza sana.”
“hupaswi kujisononesha mwanangu, mimi na
mdogo wako subira ndio familia yako mbona sisi
tunakupenda , usiwe unawaza peke yako mimi ni
kama mama yako niite mama utakavyo nami
nitaitika.” Maneno ya mama subira yalinifanya
nitokwe na machozi, nikiwaza jambo ambalo
lingeenda kutokea, chama chetu cha wachawi
kikitaka niwatoe sadaka, nilifuta machozi ambayo
yalianza kuserereka kwenye mashavu yangu, kisha
nikachukua ugali na kutenga, nilimwekea mama
ndipo alipo niuliza kuwa na mimi nimekula sikuwa
na sababu ya kumdanganya nilimweleza kuwa sikula
akanihimiza nile, nilijitahidi kumriziisha mama lakini
ugali haukupita kinywani.
“mama nimeshiba nitakula badae!” nilisema, hakuwa
na jinsi alikubali akitaka nijalimu kupika uji pengine
nitaweza kunywa, nilimwitika nikaingia ndani
nikamuacha akiwa chini ya mti ambao upo pale
nyumbani sehemu ambayo mara nyingi tunatumia
kula chakula hasa mchana na hata usiku ikibidi.
Niliingia ndani kisha nikatoka baada ya kuvaa kanga
kujifunika juu nilikuwa nimevalia gauni tu.
“Mama natoka kidogo nataka niende kwa rafiki
yangu nitarudi badae kidogo,”
“Unaenda wapi kidawa, si unaona hali yako hata
kula hujaweza alafu wataka utoke?”
“Naenda kwa kina salome mama nitarudi sio muda
mrefu,”
“Nisingependa uende, ila kwa vile umepanga
kwenda basi nenda ila kuwa makini si unajua hatari
iliyopo kijijini hapa!”
“Nitawahi kurudi mama.”nilisema kisha nikatoka,
sikuwa nikienda kwa kina salome, siku hiyo akili
haikuwa sawa nilikuwa nikielekea kwa bibi, kupata
kuwafaka wa jambo hili liniumizalo akili, sikutaka
kujichosha kwa kutembea nilitembea umbali mfupi
kisha nikaangalia kushoto na kulia hakuna mtu,
nikainama kisha kutoweka eneo lile, sekunde za
kuhesabu nilishatokea kwa bibi, wachawi huwa
tukipotea tunatumia sekunde kufika tulikodhamilia
huwa tunanuwia tundako kwa kutumia lugha zetu za
kichawi kuna maneno maalumu tunatumia ndio
yanatusaidia kukamilisha hilo, muda mwengine
tunatumia mafuta ya wanyama wakali mfano simba
na chuo hutusaidia katika shughuli zetu.
“Hivi bibi kwanini mnanifanyia hivi mimi,” niliongea
kwa hasira bila hata ya salamu ilikuwa ni baada tu
ya kutokea.
“Mjukuu wangu hilo ni agizo kutoka kwa wakubwa,
nilijitahidi kukuombea lakini wamekata wametaka
watu wako sasa mimi nitafanya nini?”
“Haijalishi bibi, ni watu wangapi nimetoa kwanini
wawatake na wale, mimi sitaweza?”
“Usiseme hivyo Kidawa, nadhani alikuambia kuwa
usipotoa kwa hiyali yako watawachukua wote
uwapendao, sasa hapo bora ni nini utoe mmoja au
uache wachukuliwe,” nilizidi vunjika moyo, bibi
hakuwa na msaada na mimi yeye anafata maagizo
kutoka kwa wakubwa zake, sikuwa na muda mwingi
niliondoka bila kuaga huku nikiwa nimefura zaidi.
Zilipita siku kadhaa sijatimiza jambo lile, walinipa
siku saba niwe tayari nimeshachagua cha kufanya,
zilipita sikukamilisha wakaniongeza tena siku saba
tena kwa vitisho,akilini nilianza kuwafikilia watu
wawili kati ya salome au subira nilipima uzito wa
kila mmoja mama subira sikutaka kumtoa kafara
hata kidogo, mwishoe nilipata jibu kuwa nimtoe
subira, niliingia mpaka chumbani anapolala na
mama hapo nikiwa nimeshika silaha ya kichawi
yenye muonekano kama kisu kirefu ambacho mpini
wake ni mfupa wa binadamu kilichongwa kama
usumali yani akikuwa kikikata pembeni bali kilikuwa
na nche tu mbele ambayo ni kali na inatoboa,
Nikiwa nimejiandaa kushusha silaha ile kumchoma
subira, mama yake alistuka kutoka usingizini huku
akikohoa nilipotea haraka haraka kabla hajaniona,
nilirudi chumbani kwangu nikitetemeka niliogopa
zaidi yanikuua mtu unayempenda lilikuwa jambo
gumu sana kulitekeleza.
Kulikucha sijaonesha tofauti yoyote, nilifanya kazi
zangu kama kawaida, siku hiyo kulikuwa kuna watu
wanapiga mbiu walikuwa wakitangaza jambo.
“Tangazo tangazo tangazo, leo kutakuwa na
mtaalamu atakuja kijijini kwetu kwa ajili ya kutatua
matatizo yanayo endelea hapa, hivyo kila nyumba
itapitiwa,” tangazo lile lilinistua sana eti
‘mataalamu’.
“Afadhali kumbe kile kikao cha jana walikwenda
kuzungumzia jambo hilo ningeenda nikajua
kinachoendelea” Mama alisema hapo nikajua
kumbe kulikuwa na kikao siku ya jana na wanakijiji
wamejadiliana kumleta mganga hapo kijijini
awatatulie matatizo yao.
“Mama kwahiyo leo wewe utabaki nyumbani au?”
“Hapana nina palizi kwavile wewe mwanangu upo
basi sio vibaya wakija wewe utawasikiliza tu
watakachofanya.” Kutokuwepo kwa mama kidogo
nilipata ahueni, nilijua nitakachofanya, uchawi
niliokuwa nao unanguvu kubwa sana, niliandaa uji
mama na subira wakanywa kisha kila mmoja
akaenda sehemu yake nikabaki peke yangu, ni kweli
baada ya saa kadhaa ngoma na kelele zililindima
mtaani nilianza kupata fukuto la mwili, mganga
alikuja mpaka pale alihangaika sana kila akijaribu ni
shoti ndio inampiga alijitahidi nilichofanya nilianza
kumchezea na yeye nilimtia bakora ambazo zilikuwa
ndio usafiri wa kumkimbiza pale alikimbia kama
mtoto mdogo asijue aliekuwa anamchapa ni
nani,sikumuacha andoke hivi hivi laah! Alikuwa na
mpambe wake ambaye ndio alimpa kazi ya
kumwaga unga akiurusha rusha huyu nilimpoteza
kwa kunyoosha mkono wangu kama namwita kisha
nikafinyanga kiganya changu mithili ya mtu
anaefinyanga tonge, huku niking’ata meno kijana
yule alipotea, mganga nae hakukaa tena pale,
alikimbia huku akibeba mkoba wake bila kuusahau.
alikuwa ni mganga ila hakukamilika uganga wake ni
wa kawaida sana.
Itaendeleaa..
 
Kipande cha 6
Na Gaooh
Simu=0654387935
Tulipoishiaaa… mganga alikuja mpaka pale
alihangaika sana kila akijaribu ni shoti ndio
inampiga alijitahidi nilichofanya nilianza kumchezea
na yeye nilimtia bakora ambazo zilikuwa ndio usafiri
wa kumkimbiza pale alikimbia kama mtoto mdogo
asijue aliekuwa anamchapa ni nani,sikumuacha
andoke hivi hivi laah! Alikuwa na mpambe wake
ambaye ndio alimpa kazi ya kumwaga unga
akiurusha rusha huyu nilimpoteza kwa kunyoosha
mkono wangu kama namwita kisha nikafinyanga
kiganya changu mithili ya mtu anaefinyanga tonge,
huku niking’ata meno kijana yule alipotea, mganga
nae hakukaa tena pale, alikimbia huku akibeba
mkoba wake bila kuusahau. alikuwa ni mganga ila
hakukamilika uganga wake ni wa kawaida sana.
Sasa Endeleaaa..
Baada ya mganga kuondoka nilirudi na kuirudisha
nyumba yetu,ilikuwa kazi rahisi kama mazinga
ombwe tu, nilianda chakula na kutoka kuelekea
kisimani, maji yalikaribia kuisha hasa ya kuoga,
hakika nilipenda kazi zangu pengine ningekuwa mke
wa mtu basi ningeitwa mama bora.
Tena ningewapenda wanangu na kumjali mume
wangu, huu uchawi naufanya lakini sio kwa mapenzi
yangu pia nilikuwa nikifanya na kujisahau muda
mwengine hata majukumu yangu sikuwa
nikiyatekeleza ipasavyo, walikuwa wakinikanya mara
kadhaa kwa kujisahau kwangu, huku wengine
wakisema nipewe muda nisihukumiwe kwa vile
walikuwa ni waelewa basi nao walielewa,na kunipa
muda wa kusahihisha makosa yangu.
Kijana yule nilimpoteza hawezi kurudi tena, huwa
tunawabadirisha watu tunaowapoteza wengine huwa
tunawabadirisha mionekano ya nyoka, wengine paka
na wengine tunawabadirisha na kuwa farasi wote
kwa ajili ya matumizi yetu, mkuu wote ndio jukumu
lake na ndio mwenye uwezo wa kubadilisha katika
mionekano tofauti, mimi huwa naweza kuwafanya
misukule tu ambao huwa tunafunga kila kitu kuanzia
jina akili na hata fikra, anakuwa anaishi hali ya kuwa
yeye ni mfu hivyo anatutumikia japo wengine
wanakuwa na akili zao za kutambua baadhi ya vitu
hasa nyumbani kwao na ndugu zake hata marafiki,
lakini huwa ni ngumu kuonekana na binadamu wa
kawaida, usiku unaficha mengi sana misukule huwa
inazunguka sana ikitanga tanga kila kona ila
hawaonekani hali ya kuwa wao wanawaona watu.
Nilitoka nikielekea kisimani mwanamke si ndio
mimi bwana utanitaka,nilitembea kwa malingo
nimeshikilia chombo changu cha kuwekea maji
huku nikijizungusha kanga mabegani kwangu kwa
ajili ya ng’ata.
“psiiiiiiiiiiii psiii” nilisikia mtu akipiga miluzi,
sikushughulika nae nilijua hainihusu, nikazidi
kujongea nikielekea kisimani.
“Kidawaaa” sauti iliita nikasimama kuangalia.
“Nisubirii” aliendelea kuonga alikuwa ni Hajji,
sikujua anataka nini wakati nilishamkatalia,
nikasimama huku ndoo nikiishikilia mkononi.
“kidawa mpenzi mbona huonekani nakutafutaga
sikuoni.”
“Mimi sio mpenzi wako!”
“Kidawa jamani mbona hutaki kuelewa hisia zangu,
mimi nakupenda mbona,”
“Kwanini huelewi, mimi sio mtu wa kuwa na
mpenzi, siruhusiwi kuingia kwenye mahusiano!”
“ Wewe ni mwanamke, kidawa ukiniambia hivyo
nashindwa kukuelewa nakuomba unikubalie
nateseka juu yako, mwenzio dhoohofuli hali kwa ajili
yako,”alinizi kunihadaa maneno amabyo niliona ni
kelele tu kwangu nilimwacha pale nikaondoka
kuelekea kisimani alizidi kunifata huku akinivuta
vuta, ghafla ulikuja upepo ambao ulimchukua haji na
kumrusha juu kisha kumtupa mbali na pale,
sikutaka iwe vile niliumia kuona anateseka bila hatia
ila ndio nitafanyaje mwenyewe king”ang’anizi
sikujishughulisha nae nikaelekea kuchota maji
wakati narudi ilibidi nibadili njia sikupita ile njia
tena, mana nilijua nikirudi na kumyuona nitamuona
huruma tu pengine nitamfata.
Nilirudi nyumbani na kutua yale maji, zilipita siku
kadhaa sikujua kiliendelea nini kwa haji ilibidi
nimtafute salome nienda hadi kwao, tulikuwa
hatujaonana kama siku tatu nzima aliniambia kuwa
yuko busy anapereka kuni mjini kuuza hivyo siku
nzima anaimaliza huko.
“Shoga umepata habari!”
“Habari gani hizo?”
“Mwenzio haji haonekani.”
“Haonekani?” niliuliza wakati nilikuwa najua
kilichomtokea.
“ndio haonekani wanasema sijui alienda shamba
hakurudi wiki sasa wamemtafuta kila mahali
hawamuoni,”
“Jamani kaka wawatu imekuaje tena au katorokea
mjini?” nilijifanya kuwa sina nianchojua .
“Labda lakini sidhani yule hapendi kuishi mjini, mi
nahisi amekutwa na maswaibu ya hapa hapa kijijini
kwetu,” taarifa ya kupotea kwa haji ilinipa simanzi
nilimuonea huruma kijana wawatu yani kunipenda
kwake tu ndio wampoteze sikuwa na la kufanya
tuliongea machache na salome kisha nikaondoka
kurudi nyumbani nilipita njia nyengine ambayo
ilikuwa nitokee nyuma ya nyumba yetu nilipoikaribia
nyumba yetu nikiwa nyuma nilisikia sauti ya mmama
akiteta jambo.
“Mama subira hapa unaishi na mwanga huyu binti
yako sio mtu mzuri, ni mchawi yani nilienda kwa
mtaalamu wangu amenipa dawa ambayo ukiipaka
unaona hata watuwasiofaa nilipaka ile siku
alivyokuja yule mtaalamu yani mwanao hii nyumba
aliipoteza yule mtaalamu hajaiona, nilimshuuhudia
kwa macho yangu akimchapa yule mganga mpaka
akakimbia.”
“wee mama sele, hayo mambo umeyatoa wapi
mwanangu mimi hana uchawi wowote”
“Hutaki kuniamini, ilikuwa kidogo tu mwanangu
wamchukue nimesaidiwa na mtaalamu ndio akanipa
na dawa” maneno yale nilijua anataka kuniharibia
hivyo ilibidi nijitokeze pale pale nae akaishiwa pozi
yani hakuendelea kuongea alizuga zuga kisha
akaaga kuondoka, niliingia ndani nikatoka na ndoo
yenye maji huku nimejifunga kanga kuonesha
naenda kuoga, ilikuwa ni zuga tu sikuwa nikienda
kuoga kama mama alivyoniona nilipoingia bafuni
nilipotea na kumtokea yule mwanamke, aliponiona
alianza kupiga kelele nilimkata kauli sauti yake
haikutoka.
“kwanini ni kimbelembele sana wewe,? inamana
wewe ndio unajua kuongea umbea sana sio,”
nilimwambia alikazana kunyoosha mikono ya
kuomba msamaha sauti haikuwa ikimtoka.
“Leo ndio mwisho wako, siwezi kusamehe”
nilisema kisha nikapiga viganja vyangu.
Itaendeleaa.
 
Kipande cha 7
Na Gaooh
Simu=0654387935
Tulipoishiaaa… kwanini kimbelembele sana wewe
inamana wewe ndio unajua kuongea umbea sana
sio,” nilimwambia alikazana kunyoosha mikono ya
kuomba msamaha sauti haikuwa ikimtoka.
“Leo ndio mwisho wako siwezi kusamehe” nilisema
kisha nikapiga viganja vyangu.
Sasa endeleaaa..
“Leo ndio mwisho wako siwezi kusamehe” nilisema
kisha nikapiga viganja vyangu, mithili ya mtu
anaepiga makofi nae akapotea pale pale nikarudi
bafuni kujimwagia maji ilikumdanganya mama
subira asijue kilichotokea, nilijimwagia makopo
kadhaa kisha maji mengine nikamwaga chini kisha
nikatoka na kurudi ndani.
Mama subira nilimuona akiwa na mawazo dhidi
yangu alionekana anataka kuniuliza jambo ila
ataanzaje, alikosa cha kuanzia hivyo alikaa kimya
huku akionekana ni mtu anaetaka kujua vitu vingi, na
mimi sikutaka ajue chochote, subira alirudi kutoka
shule nikamwandalia chakula kisha tukakaa kwenye
chini ya mti ambapo tunakaa siku zote.
“Dada leo nataka nikusomee hadithi, kwenye kitabu
chetu cha shule,”
“Unaweza kusoma?”niliuliza.
“Ndio najua, pia mwalimu alisema tukiwa nyumbani
tupendelee kujifunza kusoma zaidi,”
“Ni vizuri ebu nisomee.” Nilimwambia, nae bila
kusita akaanza kunisomea hadithi.
“Hapo zamani za kale sungura na fisi walikuwa
marafiki sana, waliishi pamoja kwa kusaidiana ila
sungura alikuwa mjanja kushinda fisi, sungura
alikuwa hapendi kwenda shamba, hapendi kufanya
kazi ila fisi alikuwa ni mkulima tena alipanda
karanga kwenye shamba lake kubwa, sungura
mwenzake akienda shamba yeye hubaki nyumbani
huku akidanganya kila siku kuwa anaumwa, ila pale
tu fisi akitoka basi na yeye hutoka kwenda shmba
kuangalia maendeleo ya mazao, sungura alikuwa
akitizama migomba na mashina ya karanga njama
zake zote zilikuwa karanga zikikomaa aanze
kuzichimba huku ndizi vijivu nazo akizipangia
kuzichuma huku hakuwahi hata kuzishughulikia,
ilipita miezi kadhaa mazao ya fisi yalianza kukomaa
hasa karanga huku ndizi nazo zikaanza kuiva, kila
siku fisi alikuta karanga zake zimeliwa, jambo lile
lilimsumbua sana huku asimjue mwizi wake, si
karanga tu hata ndizi zilikuwa zikikwanyuliwa ndizpo
siku moja aliamua ategeshe miba ya migunda
kwenye mti wa mgonga, alichukua miba mirefu kule
kwenye ncha akakuweka juu..” subira alikuwa
akinihadithia hadithi ilikuwa nzuri sana tulifurahi na
hadithi yake mwishoni aliniambia nimwambie
ujumbe uliopo ndani yake nami nikamwambia
ilikuwa furaha sana mpaka kiza kinaingia nikaelekea
jikoni kuandaa chakula cha usiku.
Jambo la kutoa mmoja katika familia lile niliamua
nilipuuzie maisha yaliendelea nikijua tayari
wamenisamehe, ila haikuwa hivyo siku isiyo na jina
walianza kuniandama, wakitaka nitoe, niliwatafutia
vichanga viwili ambavyo nilivichukua kwenye
matumbo ya mama zao vikiwa hata hazijatimiza
miezi ya kuzaliwa, wachawi pia tunauwezo wa
kuchukua matumbo ya mimba kisha tumbo
tukalijaza maji unaweza kujua kuwa unalea mimba
kumbe mtoto tulishamchukua.
Nilipereka vichanga vile lakini walikataa wakimtaka
subira, nilishikwa na hasira nikaondoka na vichanga
vile kisha nikajiweka sehemu na kuanza kuvitafuna
peke yangu havikuwa na ugumu kila kiungo kilikuwa
kilaini hata mifupa yao haikuwa imekomaa
nilivitafuta kisha nikarudi nyumbani wakati natokea
karibu na nyumbani ghafla nilimuona mama
akitokea bafuni hapo ilinibidi nijifiche asije niona na
yeye alihisi kama kuna mtu hivyo alianza kumulika
na chemli aliyoishikilia mkononi lakini hakuniona
nilipotea na kutokea kitandani kwangu, kisha
nikajifunika shuka na kujikausha kama sie mimi
nilietoka kula vichanga.
Kulikucha nikafanya shughuli zangu kama kawaida
mama nae alienda shamba, niliwaza hatima ya
maisha yangu sikuwa na jibu kuna muda nilitamani
nitoroke kuelekea mjini nikayaanze maisha mapya
ila kili nikifikiria ugumu wa maisha ya mjini
napoteza matumaini ya kuondoka kabisa, urafiki
wangu na salome uliendelea tukijaliana kama
ndugu, kuna siku niliitwa kwa bibi nami nikatii wito
tulisalimiana na bibi kisha aliniambia ni keti
anamazungumzo na mimi.
“Mjukuu wangu mimi muda wangu nimeshaumaliza,
sina muda tena wa kuishi wanataka wanichukue.”
“Wakuchukue wakupereka wapi?”
“Mjukuu wangu natakiwa niishi ulimwengi wa giza
wamesema duniani sipaswi kuishi tena hivyo
wanataka wanichukue,”
“bibi sasa mimi nitabaki na nani?”
“Kidawa wewe ni mtu mzima sasa hupaswi kuumia
kuhusu mimi,”bibi alinipa taarifa ile ambayo ilikuwa
ya kusikitisha mara nyingi ninapokwama huwa
namfata bibi kama msaada wangu sasa leo ndio
anaondoka lilikuwa ni pigo kwangu, niliamua kuuvaa
ujasiri kisha nikarudi nyumbani, asubuhi ilipofika
niliamka lakini cha kushangaza sijamsikia mama
wala subira.
“Mbona kimya au leo nimelala sana, inamana wote
wameenda shamba bila kunitaarifu, kama ni shule
leo sio siku ya shule imekuwaje,?” nilijiuliza hapo
nikaingia chumbani kwa mama baada ya kubisha
hodi, nilichokiona sikuamini macho yangu.
“Mamaaaaaaa” ukelele ulinitoka baada ya
kushuhudia nilichokiona,
Itaendeleaa
 
Kipande cha 8
Na Gaooh
Simu=0654387935
MNASOMA NI WENGI ZAIDI KULIKO MNAO
KOMENTI NA KULIKE.
Tulipoishiaaa…
“Mbona kimya au leo nimelala sana, inamana wote
wameenda shamba bila kunitaarifu, kama ni shule
leo sio siku ya shule imekuwaje,?” nilijiuliza hapo
nikaingia chumbani kwa mama baada ya kubisha
hodi, nilichokiona sikuamini macho yangu.
“Mamaaaaaaa” ukelele ulinitoka baada ya
kushuhudia nilichokiona,
Sasa endeleaaaa..
nilisisimkwa mwili mzima kwa nilichokiona, subira
na mama yake walikuwa wamelala huku viungo vyao
vikiwa vimetenganishwa na kuwekwa kwenye ungo,
niligundua ni wao kutokana na vichwa vyao
ambacho vilikuwa vikionekana taswila zao, iliniuma
zaidi, nilijiandaa kupotea ili nikalipize kwa aliefanya
hivyo, japo ni agizo nilijua siwezi pambana na
alietoa agizo hilo ila nilitaka nikamalizane na
alietekeleza, looh! Kabla sijafanya chochote ghafla
alitokea bibi kisha kunizuia nisiondoke pale.
“Mjukuu wangu hapa sio salama tena, familia yako
wameichukua, tayari wamewachinja pole sana, nawe
hupaswi kuonekana hapa.”
“Bibi mimi siwezi nataka walipie hiki walichofanya,”
“Haiwezekani kidawa wewe bado ni mdogo katika
cha hiki huna nguvu za kushindana nao,” nilipa
maumivu ambayo siku yategemea, kifo cha subira
na mama subira viliniumiza zaidi vilikuwa vifo vya
kutatanisha,iliniuma hasa nikikumbuka upendo wao
walionitendea yani vifo ndio vimekuwa malipo ya
wema wao, machozi hayakuacha kunitoa bila kujua
kuwa pale sio salama hata bibi aliponiambia, nikiwa
sijui lolote ghafla kilitokea kiumbe cha ajabu
ambacho hiki huwa kinafungiwa sehemu maalumu
kule kwenye hekalu la kichawi na pia kazi yake ni
kuua tu, baada ya kukiona nilijua kimekuja
kunimaliza kweli kilinirukia kutaka kunitafuna, looh!
Masikini bibi yangu alinisukuma pembeni kisha kile
kiumbe kinamvaa yeye na kumtia mdomoni, sauti
ya mwisho ya bibi ilikuwa ikinitaka nikimbie, mimi
ni nani nisiiskize na nina miguu nilikimbia msituni,
Nilijaribu kupotea lakini sikuwa na uwezo tena, cha
ajabu wakati nakimbia kwenye msitu nilikuwa
nikisindikizwa na sauti za vicheko, baada ya
kukimbia mita kadhaa nilijikuta mikononi mwao
walinikamata na kunifunga kamba woga ukanivaa
nani wa kunisaidia.
“Hahahaha wewe huwezi shindana na sisi, bado
wewe ni mtoto mdogo sana” walisema.
“Kipi nimefanya, mpaka mnitendee haya,”
“Inamana hujui sio, Umevunja masharti pia na ukaidi
wako wewe ni wa kupinga amri ya mkuu wetu,ni
kwamba wewe ni mkubwa kuliko yeye, haya ndio
malipo yako,”walisema sikuwa na chakuongea
nilijua nimetenda kosa pia nilijua msamaha wangu
hautanisaidia hata nikiomba, nilishashuhudia wengi
wanaovunja masharti kwa kukaidi amri adhabu yao
huwa ni kutafunwa na yule kiumbe aliemtafuna bibi.
Walinifunga kati kati ya mti huku wakinizunguka kwa
kuimba na kucheza eneo lote lilikuwa la giza
waliwasha moto wakauzungusha kama duara,
nyimbo zao hazikueleweka, sikuamini kuwa maisha
yangu yanaishia pale watu wale hawakuwa na wema
walidhamilia kunichinja.
“tunakupa siku saba tu, ya nane tutakula nyama”
walisema sikuwa na utetezi kila nilichojaribu
kusema walinipinga.
“Nipo tayari kutii masharti yenu naomba msinifanye
hivi kumbukeni mimi ni mgeni sikuwa najua hayo,
nimefanya kosa la kwanza naomba nisamehewe
hadi nikilirudia ndipo niadhibiwe,”
“hatunaga sheria hiyo kosa ni kosa unapokosea ni
adhabu tu na hakuna chaguo jengine,”
“nisameheni” nilizidi kuwaomba lakini walikuwa
wakatili nilishuhudia kwa macho yangu
wakiwachukua watu na kuwa tenganisha viungo vya
kiha walikula, japo na mimi nilikuwa miongoni mwa
wala nyama za watu ila siku hii nikajikuta nikiingiwa
na huruma hasa wale mateka wanapopiga kelele za
kuomba kusamehewa.
“upo tayari kuishi kama paka?”
“Paka??”
“Ndio unatakiwa uishi katika umbo la paka mpaka
pale utakapo kamilisha kazi,”
“Ni kazi gani hiyo?”
“Utauliza maswali au utakubali kufanya kazi hiyo ,
au upo tayari tukufanye kama wenzio.”
“hapana, nilitaka kujua ila nipo tayari”ilinibidi
nikubali kuwa paka.
“sasa ni hivi tunakurudishia nguvu zako, ila utakuwa
paka mchana kutwa hadi pale kiza kitakapo ingia
ndio utakuwa binadamu wa kawaida, kazi yako
itakuwa moja tu”
“Kazi gani hiyo,”niliuliza kwa kumkata kauli kabla
hajamaliza kuongea.
“Alafu hiki kimbelembele chako sijamaliza kuongea
unanikata maneno,”
“Nisamehe,”
“Kazi yako ni moja tu, unatakiwa kuua watu wengi
zaidi mpaka pale utakapofika kiwango
tunachokihitaji.”
“sitaki kusikia huwezi na hiyo ni amri, sio ombi”
aliongea kwa ukali hapo aliniambia kuwa tayari
natakiwa kuondoka nikatende kama walivyosema.”
nilishukuru kusamehewa sikuwa na muda wa
kusubiri niliradhimika kuondoka eneo lile, nikajaribu
kunuwia kuwa nitokee dar kweli nilitokea, nilijikuta
nipo juu ya daraja la manzese, sikuwa na sehemu
ya kwenda ilibidi nikae pale pale nikipulizwa na
upepo huku nikihesabu magari yapitayo, akilini
nikitafakari maisha yangu yatakuaje, nilidumu pale
usiku mzima mpaka kunakaribia kucha, mwangaza
wa jua ulipoanza tu kuonekana niligeuka paka tena
mweusi mwenye madoa meupe, niliogopa sana
ikanibidi nikimbie eneo lile na kuingia kwenye
vichochoro kujali uhai wangu, nilipita vichochoroni
hadi nikatokea lilipo soko la tangale nikajificha
kwenye moja ya meza ya muuza samaki wabichi,
niliishi maisha ya kutanga tanga, siku zote nilikuwa
nikitamani pasikuche kutokana na mateso ya
kubadilika kuwa paka mchana sikuwa na sehemu ya
kulala, hata kula yangu ilikuwa ya shida, baada ya
tabu zote ilinibidi nijiingize katika kazi ya bar
ambayo ilinitaka kila siku nilipoti saa moja usiku
kisha asubuhi niwe nimekwisha ondoka kazi ile
ilikuwa nzuri kwangu nilianza pata pesa kutoka
kwenye mshahara na nyengine ambazo nilikuwa
nikipewa na watu nilikuwa nikiwahudumia, sasa
nilianza kujiweza ilinibidi nitafute dalali kwa ajili ya
kupata chumba nilimtafuta usiku pia nilimwambia
akipata chumba anitaarifu nitakuja kukiangalia usiku
na hata kuhamia itakuwa usiku, yote hayo ni
kutokana na hali yangu ya kubadilika mchana,
chumba kweli kilipatikana magomeni kagera kata ya
ndugumbi nilihamia usiku baada ya kulipa kodi ya
mwaka mzima, ilikuwa nyumba ambayo
inawapangaji wengi ilikuwa na vyumba karibia kumi
na mbili japo yenye wapangaji vilikuwa kumi tu,
mwenye nyumba hakuwa akiishi hapo alikuwa ni
mtu tu wa kufata kodi yake pamoja na vikao tu kila
alipohitajika, tayari nilishanunua thamani za ndani,
nilifanya kumwagiza mtu akaniletea usiku, hakuna
aliewahi kujua mabadiliko yangu, nilipendelea mara
nyingi siku za mchana kukaa ndani na kufunga
mlango wangu bila kutoka nje wala kuonekana nje,
sikutaka rafiki mana nilijua angenisumbua tu, niliishi
kivyangu vyangu nyumbani hapo.
ITAENDELEAA..
 
SEHEMU YA 10
NA Gaooh TheAuthor
Simu =0654387935
Tulipoishia sehemu iliyopita…
“utajua tu kama bado hujaelewa,”
“Mnataka nini? kwani hawa wametoka wapi, si
tulikubaliana wawili tu,”
“Sisi kawaida yetu ni kupiga mande, huwa msichana
mmoja tunalala nae wote,”
ENDELEEA SASA..
“kwanini mnataka mnifanyie ukatili wa kijinsia,”
“Ukatili wa vipi wakati pesa umepewa si umekubali
mwenyewe,”walisema kisha wakaja kuanza kunivuta
wakitaka wanibake, hapo akili za haraka haraka
zilikuja.
“Jamani sikilizeni basi, mapenzi ni starehe
mkinibaka hamtafaidi mnaonaje aanze mmoja
mmoja wengine msubiri , mnaweza kusiamama
pembeni au maweza kukaa nje ila taa izimwe
siwezi kufanya mapenzi na taa huwa nina aibu.”
Niliwahadaa nao walivyowajinga eti wakakubali
ombi langu nilitupa taulo pembeni kisha
nikamwambia aje mmoja alafu taa izimwe kweli
alianza yule nilieahidiana nae kula bar, alipanda
kitandani baada ya mimi kupanda hapo nilitumia
uchawi wangu, kuwapoteza mmoja mmoja mpaka
wakaisha baada ya kuwapoteza, niliwasha taa kisha
nikajiangalia nikiwa sina nguo kisha nikavaa nguo
zangu, watu wale niliwa nikiwapoteza kwa kushika
vichwa vyao kila niliekamata kichwa chake alipotea
na watu wote tunaowapoteza huwa ni kama kitoweo
huk waendako, wachawi tunachukua damu na baadhi
ya viungo vya ndani kisha mabaki tunawapa
wanyama wetu.
“Kazi nzuri umefanya,” ilisikika sauti kutoka kwenye
pembe ya chumba kile huku ikinipongeza kwa
makofi.
“ukijitahidi zaidi utasamehea na utakuwa kama
mwanzo.” Ilisema hapo sikujibu chochote nilipotea
ndani pale na kutokea kwangu, nilipofioka tayari
nilikuta wamenileta chakula ambacho ni nyama
mbichi za watu pamoja na damu kama kinywaji
nilivifakamia kutokana na njaa niliyokuwa nikihisi,.
“Leo sijakuona mpenzi, nataka leo mchana nije
kwako” iliingia meseji kwenye simu yangu kutoka
kwa swedy.
“No leo siko nyumbani niko mbali kidogo kwa
dada?” niliandika na kutuma.
“Nitakufata huko huko nifahamiane nae, pia nataka
nilete mahitaji hapo kwake” swedy alikuwa
king’ang’anizi ilibidi nizime simu mana asubuhi
ilikaribia baada ya kuzima simu kulikucha nikageuka
paka, nilitoka nje kwa maajabu siku hii niliamua
zunguke mtaani nilitembea juu ya mapaa ya nyumba
na sehemu nyengine nikingia dalini kabisa hakuna
alieniona wote walihisi ni paka tu kama paka
wengine.
Asilimia sabini ya paka uwaonao jiji dar es salaam
huwa ni watu ambao mchana huwa mapaka na
usiku huwa ni watu wengine mchana watu na usiku
huwa ni mapaka, sisi wachawi tunapenda kutumia
muonekano wa paka kwa sababu paka anasiri
kubwa pia ni mnyama ambae ni rafiki wa binadamu
hana madhara yoyote japo kuna baadhi hawayapendi
ila paka popote anaingia na hata unaweza pishana
nae usimdhuru anaweza kuingia ndani kwako
ukamuacha kwa kujua anakufukuzia panya kumbe la
amekuja kwa kazi yake, paka si kama mbwa,
mmbwa huwezi ruhusu aingie ndani kwako,
Niliamua nipumzike wiki nzima nisiende kazini hata
simu sikuwasha usiku nilijibadilisha muonekano wa
paka kisha nilipotea na kutokea hospitali ya mwana
nyamara huko nilienda kwa leo moja tu, nilihasi kula
nyama ya vitoto vichanga sehemu ya kuvipata
ilikuwa ni hospitali, nilienda mapema nikajificha
chini ya uvungu kwa moja ya mzazi alikuwa akisubiri
uchungu aweze kujifungua.
“Pole mke wangu, utajifungua hivi karibuni,
nakupenda sana, mtoto wetu atareta furaha na
amani kwenye nyumba yetu,” alikuwa ni mwanaume
mmoja akiongea na mkewe muda huo kwenye wodi
ya wazazi, dakika kadhaa nesi alikuja akamtoa baba
yule kisha akampa dawa mama yule nilikuwa
nikiyashuhudia hapo nikiwa chini ya kitanda, baada
ya kutoa dawa nesi akatoka.
Hapo nikajigeuza na kuwa binadamu, yule
mwanamke alistuka akataka kupiga kelele ila
nilimuwahi sauti yake nikaichukua, yani alikuwa
akipiga kelele lakini sauti haitoki kila alipojitahidi
haitoki nilichofanya nililishika tumbo lake na mikono
yangu miwili mithiri ya mtu anaeshikilia mpira,
baada ya kulishika nilimtoa yule mtoto alafu
nikambeba na mikono yangu, tukio lile lilikuwa
kama ndoto, yani ni kama vile unaota kitu kinatokea
mfano unaota kuna msiba alafu ukiamka kweli
unapata taarifa za msiba hivyo mama yule alikuwa
kama akiota kumbe ni kweli.
Japo niliuhisi uchungu wa msichana yule, ila sikuwa
na cha kumsaidia yani abebe ujauzito miezi tisa
kisha sisi tuje tuchukue kiumbe kwa siku moja tu
loooh! Tulaaniwe wachawi, nisingefanya vile ila
sikuwa na jinsi ndio kazi niliyopewa japo niliifanya
bila mapenzi yangu, nilikuwa nikijifanya mwema
kwao huku moyoni nikiwa na kisasi ambacho
nilipanga kukikamilisha punde tu watakapo anza
kuniamini, kwa wakati huliamua kufanya kama
matakwa yao yanavyotaka huku nikijitahidi
kuwafurahisha,nilipochukua kichanga kile nilisogelea
pembe ya wodi ile ya wazazi kwa ajili ya kuondoka
kulikuwa na wazazi wengine ambao walikuwa
wamelala,niliondoka na kwenda kwenye
uongozi,kwa ajili ya kutoa kafara kiumbe kile,sikuwa
peke yangu niliungana na wenzangu kisha
tulijumuika tukala vichanga vile huku kukiwa na
sherehe ndogo ambayo huwa tunaifanya kila siku ya
jumanne, siku za jumanne ni siku mbaya vifo vingi
hutokea hasa ajali na mabalaa ni siku ambazo
wachawi tunatumia kukutana na kuabudu shetani
ambaye tunamuamini tofauti na Mungu,baada ya
kuhitimisha nilirudi nyumbani kwangu tayari usiku
wa siku nyengine ulingia niliingia ndani na kutoka
ikiwa kiza tayari kimemea, nilihisi kuchoka pia
mwili wangu uliyahitaji maji zaidi si kunywa tu hata
kuoga pia ulihitaji hapo ndio nikachukua glasi
ndogo na kumimina maji na kuyanywa kisha
nikavaa taulo langu jeusi na kumimina maji kwenye
ndoo ya kuogea nikachukua sabuni na kutoka
kwenda kuoga, nilipotoka tu mama yule alinipokea
sijui alikuwa akinisubiri ila nilishangaa tu akiwa
karibu na mlangoni kwangu amesimama mithili ya
mnazi.
“we msichana huwa unashinda wapi mbona
sikuwahi kukuona mchana yani hata asubuhi
sijawahi kukuona ukienda kuoga hivi unafanyaga
nini”
“samahani mama, hivi kuna chochote kinakuhusu
kwangu unaniuliza maswali hayo kama nani?”
“we binti nikikuuliza unatakiwa unijibu we huonekani
unakuwa wapi hata kwenye vikao haupo”
“wa kuongea na mimi ni mwenye nyumba pia mimi
kazi zangu si usiku mchana mara nyingi mchana
ndio zinakuwa nyingi usiku ndo mama naonekana
mara chache,”
“Tusijekuwa tunaishi na jambazi hapa tukaingia
matatizoni, sisi tunataka kujua ukweli wako,” alizidi
kunichokora huyu mama alionekana ni mama
mshari pia anamdomo mrefu alikuwa na watoto
watatu wote akilala nao chumba kimoja na
mumewe, alikuwa ni mama wa hali ya chini ya
kimaisha huku akijawa wivu kazi pekee
walioitegemea ni ya mumewe ambayo ilikuwa ni
fundi viatu akifanya shughuli zake huko barabani
wanapaita kagera house, hivyo stress za maisha na
umbea wake anamaliza kwa watu.
 
SEHEMU YA 10
NA Gaooh TheAuthor
Simu =0654387935
Tulipoishia sehemu iliyopita…
“utajua tu kama bado hujaelewa,”
“Mnataka nini? kwani hawa wametoka wapi, si
tulikubaliana wawili tu,”
“Sisi kawaida yetu ni kupiga mande, huwa msichana
mmoja tunalala nae wote,”
ENDELEEA SASA..
“kwanini mnataka mnifanyie ukatili wa kijinsia,”
“Ukatili wa vipi wakati pesa umepewa si umekubali
mwenyewe,”walisema kisha wakaja kuanza kunivuta
wakitaka wanibake, hapo akili za haraka haraka
zilikuja.
“Jamani sikilizeni basi, mapenzi ni starehe
mkinibaka hamtafaidi mnaonaje aanze mmoja
mmoja wengine msubiri , mnaweza kusiamama
pembeni au maweza kukaa nje ila taa izimwe
siwezi kufanya mapenzi na taa huwa nina aibu.”
Niliwahadaa nao walivyowajinga eti wakakubali
ombi langu nilitupa taulo pembeni kisha
nikamwambia aje mmoja alafu taa izimwe kweli
alianza yule nilieahidiana nae kula bar, alipanda
kitandani baada ya mimi kupanda hapo nilitumia
uchawi wangu, kuwapoteza mmoja mmoja mpaka
wakaisha baada ya kuwapoteza, niliwasha taa kisha
nikajiangalia nikiwa sina nguo kisha nikavaa nguo
zangu, watu wale niliwa nikiwapoteza kwa kushika
vichwa vyao kila niliekamata kichwa chake alipotea
na watu wote tunaowapoteza huwa ni kama kitoweo
huk waendako, wachawi tunachukua damu na baadhi
ya viungo vya ndani kisha mabaki tunawapa
wanyama wetu.
“Kazi nzuri umefanya,” ilisikika sauti kutoka kwenye
pembe ya chumba kile huku ikinipongeza kwa
makofi.
“ukijitahidi zaidi utasamehea na utakuwa kama
mwanzo.” Ilisema hapo sikujibu chochote nilipotea
ndani pale na kutokea kwangu, nilipofioka tayari
nilikuta wamenileta chakula ambacho ni nyama
mbichi za watu pamoja na damu kama kinywaji
nilivifakamia kutokana na njaa niliyokuwa nikihisi,.
“Leo sijakuona mpenzi, nataka leo mchana nije
kwako” iliingia meseji kwenye simu yangu kutoka
kwa swedy.
“No leo siko nyumbani niko mbali kidogo kwa
dada?” niliandika na kutuma.
“Nitakufata huko huko nifahamiane nae, pia nataka
nilete mahitaji hapo kwake” swedy alikuwa
king’ang’anizi ilibidi nizime simu mana asubuhi
ilikaribia baada ya kuzima simu kulikucha nikageuka
paka, nilitoka nje kwa maajabu siku hii niliamua
zunguke mtaani nilitembea juu ya mapaa ya nyumba
na sehemu nyengine nikingia dalini kabisa hakuna
alieniona wote walihisi ni paka tu kama paka
wengine.
Asilimia sabini ya paka uwaonao jiji dar es salaam
huwa ni watu ambao mchana huwa mapaka na
usiku huwa ni watu wengine mchana watu na usiku
huwa ni mapaka, sisi wachawi tunapenda kutumia
muonekano wa paka kwa sababu paka anasiri
kubwa pia ni mnyama ambae ni rafiki wa binadamu
hana madhara yoyote japo kuna baadhi hawayapendi
ila paka popote anaingia na hata unaweza pishana
nae usimdhuru anaweza kuingia ndani kwako
ukamuacha kwa kujua anakufukuzia panya kumbe la
amekuja kwa kazi yake, paka si kama mbwa,
mmbwa huwezi ruhusu aingie ndani kwako,
Niliamua nipumzike wiki nzima nisiende kazini hata
simu sikuwasha usiku nilijibadilisha muonekano wa
paka kisha nilipotea na kutokea hospitali ya mwana
nyamara huko nilienda kwa leo moja tu, nilihasi kula
nyama ya vitoto vichanga sehemu ya kuvipata
ilikuwa ni hospitali, nilienda mapema nikajificha
chini ya uvungu kwa moja ya mzazi alikuwa akisubiri
uchungu aweze kujifungua.
“Pole mke wangu, utajifungua hivi karibuni,
nakupenda sana, mtoto wetu atareta furaha na
amani kwenye nyumba yetu,” alikuwa ni mwanaume
mmoja akiongea na mkewe muda huo kwenye wodi
ya wazazi, dakika kadhaa nesi alikuja akamtoa baba
yule kisha akampa dawa mama yule nilikuwa
nikiyashuhudia hapo nikiwa chini ya kitanda, baada
ya kutoa dawa nesi akatoka.
Hapo nikajigeuza na kuwa binadamu, yule
mwanamke alistuka akataka kupiga kelele ila
nilimuwahi sauti yake nikaichukua, yani alikuwa
akipiga kelele lakini sauti haitoki kila alipojitahidi
haitoki nilichofanya nililishika tumbo lake na mikono
yangu miwili mithiri ya mtu anaeshikilia mpira,
baada ya kulishika nilimtoa yule mtoto alafu
nikambeba na mikono yangu, tukio lile lilikuwa
kama ndoto, yani ni kama vile unaota kitu kinatokea
mfano unaota kuna msiba alafu ukiamka kweli
unapata taarifa za msiba hivyo mama yule alikuwa
kama akiota kumbe ni kweli.
Japo niliuhisi uchungu wa msichana yule, ila sikuwa
na cha kumsaidia yani abebe ujauzito miezi tisa
kisha sisi tuje tuchukue kiumbe kwa siku moja tu
loooh! Tulaaniwe wachawi, nisingefanya vile ila
sikuwa na jinsi ndio kazi niliyopewa japo niliifanya
bila mapenzi yangu, nilikuwa nikijifanya mwema
kwao huku moyoni nikiwa na kisasi ambacho
nilipanga kukikamilisha punde tu watakapo anza
kuniamini, kwa wakati huliamua kufanya kama
matakwa yao yanavyotaka huku nikijitahidi
kuwafurahisha,nilipochukua kichanga kile nilisogelea
pembe ya wodi ile ya wazazi kwa ajili ya kuondoka
kulikuwa na wazazi wengine ambao walikuwa
wamelala,niliondoka na kwenda kwenye
uongozi,kwa ajili ya kutoa kafara kiumbe kile,sikuwa
peke yangu niliungana na wenzangu kisha
tulijumuika tukala vichanga vile huku kukiwa na
sherehe ndogo ambayo huwa tunaifanya kila siku ya
jumanne, siku za jumanne ni siku mbaya vifo vingi
hutokea hasa ajali na mabalaa ni siku ambazo
wachawi tunatumia kukutana na kuabudu shetani
ambaye tunamuamini tofauti na Mungu,baada ya
kuhitimisha nilirudi nyumbani kwangu tayari usiku
wa siku nyengine ulingia niliingia ndani na kutoka
ikiwa kiza tayari kimemea, nilihisi kuchoka pia
mwili wangu uliyahitaji maji zaidi si kunywa tu hata
kuoga pia ulihitaji hapo ndio nikachukua glasi
ndogo na kumimina maji na kuyanywa kisha
nikavaa taulo langu jeusi na kumimina maji kwenye
ndoo ya kuogea nikachukua sabuni na kutoka
kwenda kuoga, nilipotoka tu mama yule alinipokea
sijui alikuwa akinisubiri ila nilishangaa tu akiwa
karibu na mlangoni kwangu amesimama mithili ya
mnazi.
“we msichana huwa unashinda wapi mbona
sikuwahi kukuona mchana yani hata asubuhi
sijawahi kukuona ukienda kuoga hivi unafanyaga
nini”
“samahani mama, hivi kuna chochote kinakuhusu
kwangu unaniuliza maswali hayo kama nani?”
“we binti nikikuuliza unatakiwa unijibu we huonekani
unakuwa wapi hata kwenye vikao haupo”
“wa kuongea na mimi ni mwenye nyumba pia mimi
kazi zangu si usiku mchana mara nyingi mchana
ndio zinakuwa nyingi usiku ndo mama naonekana
mara chache,”
“Tusijekuwa tunaishi na jambazi hapa tukaingia
matatizoni, sisi tunataka kujua ukweli wako,” alizidi
kunichokora huyu mama alionekana ni mama
mshari pia anamdomo mrefu alikuwa na watoto
watatu wote akilala nao chumba kimoja na
mumewe, alikuwa ni mama wa hali ya chini ya
kimaisha huku akijawa wivu kazi pekee
walioitegemea ni ya mumewe ambayo ilikuwa ni
fundi viatu akifanya shughuli zake huko barabani
wanapaita kagera house, hivyo stress za maisha na
umbea wake anamaliza kwa watu.
 
SEHEMU YA 11
Na Gaooh TheAuthor
Simu=0654387935
Tulipoishia sehemu iliyopita.. alizidi kunichokora
huyu mama alionekana ni mama mshari pia
anamdomo mrefu alikuwa na watoto watatu wote
akilala nao chumba kimoja na mumewe, alikuwa ni
mama wa hali ya chini ya kimaisha huku akijawa
wivu kazi pekee walioitegemea ni ya mumewe
ambayo ilikuwa ni fundi viatu akifanya shughuli zake
huko barabani wanapaita kagera house, hivyo stress
za maisha na umbea wake anamaliza kwa watu.
Tuendeleee hapa..
“Au mwanga nini huyo mwambie mwambie, mtu
gani hatuoni hata rafiki wakija hata ndugu anaishije”
alidakia mwengine ambaye akikuwa akipika pale
subuleni.
“naomba tusifatiliane kila mmoja anakaa hapa kwa
kodi yake sikai bure nimelipa kodi hivyo nitapenda
zaidi kila mtu afanye mambo yake.”
“unamjibu nani hivyo ebu kuja hapa” alinivuta baada
ya kutaka kuingia ndani.
“mama nakuomba tuheshimiane?”
“Usijifanye unajua kuongea wewe wajifanya sista
duu, usafi wa hapa ndani hutaki, choni hufanyi usafi
wataka sisi vijakazi wako tufanye usafi”
“mama mbona mimi nilishaongea na mwenye
nyumba na anajua kuwa mimi sina muda wa kukaa
nyumbani kwani natoa hela za usafi kila zamu yangu
ikifika,”
“Hata kama na wewe unatakiwa ufanye usafi.”
Alizidi kuongea porojo, hapo nikampuuza na kuingia
bafuni huku nimefula nilioga haraka haraka kisha
nikarudi na kuingia ndani kwangu,hata kule
kupumzika sikutamani tena saa mbili hiyo niliamua
niende tbar kujipumzisha pamoja na kupunguza
mawazo, kweli nilienda kama kawaida siku hii
sikutaka kucheza kabisa, nilijiona mzito zaidi pia
hata kichwani sikuwa sawa, nikiwa nimekalia moja
ya viti vya pale bar huku nikipata kinywaji nilipata
mteja, si jambo geni kwangu hiyo ni moja ya kazi
yangu kulala na wanaume japo sikuendekeza sana
pia nilikuwa makini nao zaidi, mteja huyu alitaka
kulala na mimi huku akijinadi anamazo mke wake
anamsumbua hivyo anataka apate pumziko la
ubongo wake, kwavile ni kazi nilikubali kisha muda
huo huo tuliongozana guest ya Jumba La Dhahabu,
ambayo ipo karibu na sehemu ya betting hapahapa
magomeni kagera, alichagua chumba akaniambia
nitangulie kweli nilienda kwavile tulishapatana bei
alinipa ofa nzuri, nilitangulia yeye akisema anakuja
na vinywaji, nilipanda ngazi kazaa mpaka kukifikia
chumba hiko, nilikifungua nilipokelewa na madhari
nzuri ya chumba hiko chenye thamani za kitanda
kabati meza na runinga iliyopachikwa ukutani,
hakikuwa na kochi hivyo nilikaa kitandani
nikimngoja mteja wangu ambaye alisema anakuja
na vinywaji, ilikuwa saa sita ikierekea saa saba,
sikujua kinachomcherewesha ni nini?,
“Oooh, samahani mrembo wangu, nimecherewa
kidogo nilikutana na mtu ambaye tukuwa
tukifahamiana hivyo hakutaka niondoke tuliongea
kidogo ndipo nimekuja samahani sana,”
“sii kitu, umeniletea nini mana nahisi njaa,”
“Nimeleta upendacho,”
“nipendacho?”
“Ndio, nimekuletea chips na kuku mzima najua
unapenda mana wanawake wengi hupendelea,”
“Hahaha mwenzio napendaga makange au
urojo,”niliongea kwa kudeka huku kicheko
kikinitoka, kicheko cha uchokozi.
“Kwani we mpemba au mtanga,”
“Mi ndio napenda ila njaa inauma ebu tule kwanza
kisha mengine badae pia unajua mimi sitaki kulala
mpaka asubuhi natakiwa niondoke kabla
hakujakucha,”
“usifanye hivyo bana mwenzio nimepanga tukeshe,
pia kesho tushinde yani kila kitu tuletewe tukiwa
ndani,” alisema.
“Ni ngumu.” Nilijibu kwa mkato tayari ilishatafuna
yule kuku haraka haraka, nilikuwa mzoefu na nyama
si mbichi wala zilizochomwa zote zilikuwa halali
yangu hivyo kuku yule dakika za kuhesabu
nilishammaliza, mteja yule nae alianza kubwea
pombe huku na mimi nikinywa ado ado, mpaka
inafika saa nane hakuna tulichofanya ndio akataka
tukaoge nami nilitii tukaingia bafuni kuoga na
kutoka bado tuliporudi alikuwa akinywa tu huku
akininywesha alionekana wazi anataka kesho
ashinde mchana na mimi ndio mana hana haraka ya
tendo na mimi kukaa mchana siwezi, mpaka inafika
saa kumi na nusu bado tu eti ndio ananipapasa kwa
leo la kutaka tendo, nilikuwa nikimtoa mara kadhaa
mana nilijua muda huo nikisema nianze tu kufanya
nae basi tutatumia muda mrefu pia itakuwa aibu
kwangu nitakapo geuka na kuwa paka.
“nataka niondoke muda umeisha?”
“Unasemaje?”
“Nataka niondoke muda umeisha?” nilirudia maneno
yangu tena kwa msisitizo.
“Uondoke na wapi ikiwa nimekwambia leo
tutakesha pia tutashinda hapa hapa ndani,”
“Ni kwamba hutaki kunielewa ama?”
“Wewe ndio hutaki, kuelewa pia hutaki kunielewa
sasa mimi nimefuanya kazi gani usiku mzima na
wewe wataka kuondoka” aliongea na sauti yake ya
kilevi mithili ya masele chapombe alikuwa akiongea
huku akicezesha mikono na kuyumba yumba.
“samahani, kwa usalama wako nakuomba
niondoke,”niliongea kipole mana alikuwa kasimama
mlangoni baada ya kuzunguka na kitasa alikishikiria.
Kuna muda roho ya kikatili ilikuwa ikinijia kuwa
nimuue nyengine ikinijia ya huruma nimsamehe,nilio
na bora nisimfanye kitu chochote nilichofanya
niliingia chooni kwa danganya toto ya kuwa naenda
kujisaidia kweli nilipoenda ilibidi nipotelee huko
huko sikujua kilichoendelea nyuma, nilitokea ndani
ya chumba changu ambacho mara nyingi huwa
nakifunga kwa ndani nje niweka pazia refu ambalo
si rahisi mtu kujua kama sipo au nipo labda aje
afunue panzia aangalie, ila hata akiangalia hakuna
ambacho ataweza kukiona mana mlango wangu
hautumii kufuri ni kitasa cha mzungu.
Nikiwa ndani ilikuja sauti ambayo ni ujumbe kutoka
katika uongozi wa juu wakisema kuwa kuna kikao
cha wachawi, nilijiandaa kutii wito huo kisha
nikasafiri kuelekea kijijini nilitumia ungo ambao
ulinifikisha niendako.
Wazee walikuwa wamejumuika pamoja, nyimbo na
vigeregere ziliendelea ulikuwa ni usiku, siku hiyo
kijiji kizima kililemewa na mirindimo ya radi pia
mvua kubwa ilikuwa ikinyesha cha kushangaza
uwanjani pale hakukuwa na mvua yoyote wala dalili
yoyote ni sehemu ya wazi lakini imekuwa kama
ukumbi mkubwa uliefunikwa kila mahali, mvua
waliifunga sehemu hiyo.
“Mzee tengo, wewe ni mchawi wa muda mrefu
naamini unarith kutoka kwa babu yako ambaye nae
alipewa na babu yake mpaka leo na wewe
umekuwa babu, sheria zetu unapaswa na wewe
umpe mfuko mjukuu wako au mwanao kama
ulivyopewa,” yalikuwa ni mazungumzo yao
waliyokuwa wakongea ilionekan mmoja ya wazee
akikaidi jambo.
“Hapana hamuwezi nifundisha mimi, sitaki familia
yangu iendeleze huu ukafiri wenu nataka mimi ndio
niwe wa mwisho kuwa na huu uchawi wanangu
sitaki muwahusishe kabisa,”aliongea kwa kujiamni
huku akiendelea, “machungu niliyopitia katika
kupunguza familia yangu ningekuwa na watoto
wengi lakini chama hiki cha kikafiri kimenimalizia
watoto hata mke wangu kipenzi mimi siwezi
kuendeleza.” Alizidi kuongea kwa kujiamini.
“Ni wazi mzee unavunja masharti pia unakosea
mizimu yetu, maneno hayo ni kama kututusi sisi
wote,”
“Hata kama acha iwe hivyo nimechoka nahitaji
kujitoa kwenye chama hiki sasa,” sikujua nguvu
alipata wapi mzee yule kuongea vile alikuwa
tegemezi akitoa miongozo lakini leo amebadirika
hakuna alieamini, hakuendelea kusalia pale
alichukua mkongojo wake kisha kuondoka kabisa
eneo lile.
 
Sehemu ya 12
Na Gaooh TheAuthor
Simu = 0654387935
TULIPOISHIAA SEHEMU ILIYOPITAA…………….
“Hata kama acha iwe hivyo nimechoka nahitaji
kujitoa kwenye chama hiki sasa,” sikujua nguvu
alipata wapi mzee yule kuongea vile alikuwa
tegemezi akitoa miongozo lakini leo amebadirika
hakuna alieamini, hakuendelea kusalia pale
alichukua mkongojo wake kisha kuondoka kabisa
eneo lile.
SASA TUENDELEEEE HAPA…….
“Jamani hilo halikuwa kusudi la wito huu, ukaidi wa
mzee tengo ataona faida zake mi nawaomba mkae
kwa utulivu, kipindi hiki naona kuna dharau
zinaendelea miongoni mwetu mmekuwa mkidharau
chama chetu hiki ambacho ni urithi kutoka kwa
babu zetu, mila na desturi zetu mnazivunja kila
iitwapo leo,” aliongea mambo mengi mzee yule
hapo baada kumaliza kuongea na kutoa maadhimio
pamoja na kuwakaribisha wageni, tulikula na
kunywa kwa furaha kisha mimi na wasichana
wengine wawili tulipewa kazi ya kuimaliza familia ya
mzee tengo,ilikuwa ni moja ya kazi yangu ya kuua
ila walinipa wasaidizi mana walijua ugumu wa kazi
ile, kwa vile mimi sikuwa nikijua chochote niliiona
ni kazi rahisi sana tena nilijua wiki moja itakuwa
imekwisha isha, ili kutimiza kazi yangu walinipa
kikamba ambacho nilitakiwa kukivaa mguuni muda
wote ili nisijekubadilika kuwa paka hata ifikapo
mchana.
Tulipewa makazi ya kukaa tukikaribishwa na bibi
songowe akiwa kama wenyeji wetu alitupa makazi
ya kukaa kwa ajili ya kuimaliza familia ile iliyokiuka
mila na desturi, bibi songowe alikuwa mmoja ya
viongozi wa juu katika uchawi japo hakuwa mkuu ila
alikuwa ni kiongozi wa juu alitujuza ugumu wa kazi
ile huku akitaja sifa za mzee tengo pamoja na
uhodari wake na nguvu zake, wenzangu waliguna ila
mimi nilijiamini sana nikiendelea kuona ni kazi
rahisi, kuna muda nilimwambia bibi songowe kuwa
hiyo kazi waniachie niifanye ila alipingana kutaka
tuifanye kwa pamoja nikakubali kishingo upande.
Siku moja usiku niliondoka na mmoja ya wenzangu
niliotumwa nao kazi hiyo, tulifika karibu na nyumba
ya mzee tengo, hapo mimi ndio nilikuwa mstari wa
mbele tulifika mpaka kwenye nyumba yake ndipo
kila mmoja akasimama kwenye pembe yake kwa
ajili ya kuingia ndani, looh! Kwaingilika sasa kila
tukijaribu kupotea ili kuingia ndani tulijikuta nje,
haikuwa kazi rahisi baada ya kujaribu mara kadhaa
ndipo alitoka mtu ndani ya nyumba ile akiwa na
tochi huku amevaa msuli wake alikuwa mzee tengo.
“Msitake kunijalibu, mimi sijaribiwi mnataka kujua
mimi ni nani?” alikuwa akiongea kwavile tulijificha
sehemu tofauti na mwenzangu sikujua mwenzangu
anamalengo gani sehemu alipokuwepo.
“kama kweli nyie mnajiamini pia mmekuja kwa ajili
yangu ebu sogeeni karibu yangu niwaonyeshe kuwa
mimi ni nani kijijini hapa?” bila kutegemea
mwenzangu alitokeza kwa kujiamini, mzee songoro
mbali na kuwa na tochi pia alikuwa na fimbo yake
mkoni ambayo hutumia kutembelea.
Ndesi alianza kuvutaka na mzee tengo, walivutana
huku kila mmoja akiwa maejithatiti kuonesha uwezo
wake, walikuwa wakipambana kwa kutumia miyale
ambaye ilikuwa kama kamba kila mmoja akitoa ya
kwake, ndipo Ndesi aliangushwa chini huku mzee
tengo akijiandaa kumchoma na fimbo yake ambayo
iligeuka kama kisu kirefu kinachowaka, sikutaka
kusubiri hilo litokee nilijitoa nilipokuwa kwa nguvu
za ajabu nikarusha mikono kumuelekezea mzee
tengo hapo ulitoka upepo ambao ulimsukumia
pembeni kweny kibambaza cha ukuta wa nyumba
wake baada ya tukio hilo nilimchukua Ndesi
aliekuwa hoi, nikarudi nae mpaka kwa bibi
songowe.
Ndesi alikuwa amejeruhiwa sehemu kadhaa za mwili
wake, alikuwa ameungua ungua, bibi songowe
alimpokea huku akitusihi tusikate tamaa kazi bado
ngumu, alimlaza Ndesi kitandani kisha kuanza
kumkanda sehemu alizomajeraha, wenzangu
wengine walianza kuingiwa na woga kwa vile kazi
imekuwa ngumu tofauti na tulivyotegemea, mzee
tengo alibakiwa na mjukuu mmoja tu mdogo
ambaye umri wake ni miaka sita baba na mama
yake tayari walishafariki miezi kadhaa, iliyopita
hivyo mzee tengo hataki mjukuu wake aingizwe
katika uchawi alijuafika malipo ya uchawi hivyo ndio
mana anatumia nguvu nyingi kuilinda familia yake
iliyobakiwa hana mke hana watoto ni mjukuu tu
ambaye ndio kama familia sasa.
Kulipokucha asubuhi niliandaa uji pia niliandaa na
dawa ya miti shamba kwa ajili ya Ndesi, afya yake
haikuimalika hata kidogo hakuwa na nguvu hata za
kusimama, inaonesha alikuwa akishindana na nguvu
nyingi za mzee yule.
Tulitulia kama siku tatu kisha nikaenda na
mwenzangu mwengine kupambana siku hii tulienda
vizuri pia tulipewa dawa ambayo ilituongeza uwezo
tulifanikiwa kuingia ndani, hapo tukapeana majikumi
nilimwambia mwenzangu yeye amchukue mtoto
kisha mimi nitapambana na mzee tengo, nilimtaka
yeye amchukue kisha aondoke aniache mimi
ulingoni, looh! Nilimuonea huruma pale alipojaribu
kumshika mtoto yule alitupwa mbali ukutani na
shoti ambayo ni kinga mzee yule aliyoweka kwa
mjukuu wake, binti wa kuitwa masi alirushwa
mzima mzima na kugonga ukutani, hali ile ilinitisha
zaidi, mzee tengo hakuwa wa kujalibiwa alimka
kitandani kisha kuchukua fimbo yake ambayo
wakati huu ilibadilika na kuwa simba, kitendo cha
kuona vile nilijigeuza paka kisha nikajificha juu ya
paa la nyumba yake kwa usalama wangu, masikiki
Massi alitafunwa na simba yule kama kitoweo
nilishuhudia kwa macho tukio lile, liliniuma zaidi pia
sikuamini kama itakuwa vile, zoezi la kummaliza
Mzee tengo lilionekana kuwa gumu kiasi chake.
Bibi songowe siku hii alienda kutafuta dawa kwa
ajili ya ndesi ambaye amejeruhiwa tayari, mimi
nilibaki nae nyumbani kwa ajili ya kumhudumia hasa
kumsaidia pale tu alipohitaji msaada wangu nikiwa
ndani nilisikia kelele nje za sauti tena ya kiume ya
mtu anaefoka, sikuijua kabla sauti ile hapo ilibidi
nitoke nje ili kujua, looh! Mzee tengo alikuwa
uwanjani kwetu.
“Mmenitafuta sana, leo nimeamua niwafate hapa
hapa tumalizane?” alikuwa akiongea huku akipiga
makofi.
“We mzee unatafuta kwa kufia ama?”
“Unasemaje we binti mwanga,”
 
SEHEMU YA 13
NA Gaooh TheAuthor
SIMU = 0654387935
TULIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA…
“Mmenitafuta sana, leo nimeamua niwafate hapa
hapa tumalizane?” alikuwa akiongea huku akipiga
makofi.
“We mzee unatafuta kwa kufia ama?”
“Unasemaje we binti mwanga,”
ENDELEEAAA HAPAA..
“Mimi na wewe nani mwanga kama si wewe, mzee
hunaga haya wewe wala soni huogopi kuja
nyumbani kwa watu,”
“Mlivyokuwa mkija kwangu, kunisumbua mlikuwa
mnaogopa au, leo nataka tuoneshane hapa uwanjani
kwenu.” Alinitisha na maneno yake kidogo japo si
sana nilikuwa nikimuogopa mzee tengo, alikuwa
akijua uchawi wa kila aina kwa vile aliwahi kuwa
mkuu hapo nyuma pia aliwahi kwenda nchini
naigeria kuongeza ujuzi wake.
Wakati akiwa pale bahati nzuri bibi alirudi, hapo
kidogo nikapata amani, bibi alimkaribisha lakini
mzee yule hakukubali, swali lake kubwa ni kwanini
tunamfatafata.
“Ingia ndani Kidawa,”bibi songowe aliniambia
niingie ndani, nilitii nikaingia ndani, wakati naingia
mzee tengo alianza kupambana na bibi songowe,
sikuwa nimeingia ndani nilisimama mlangoni
nikitizama, mzee songowe alitoa fimbo yake ila
kabla hajatoa bibi tayari aliikamata na kuivunja hapo
mzee tengo hakupata usaidizi alipambana na nguvu
zake za kawaida ila bibi songowe alikuwa imara
zaidi, wakati wakipambana mvua na radi vilikuwa
mashabiki zao wakiwashangilia, mzee tengo baada
ya kuona anazidiwa aliamua kukimbia eneo lile.
Baada ya purukushani za nje bibi aliingia ndani hapo
tayari nilikuwa nishaingia ndani.
“Hii kazi niachieni huyu mzee si chochote kabisa?”
“Bibi utamuweza huyu,”
“uwezo wake wote upo kwenye ile fimbo akiwa
hana ile nguvu pia anakuwa nazo pungufu ngoja
mimi nikammalize yeye na familia yake leo leo.”
Bibi aliweka nadhiri jambo ambalo hakutaka lile
aliniachia maagizo ya dawa alizokwisha leta kwa
ajili ya ndesi kisha yeye akatoka kuelekea kwa mzee
tengo, baada ya bibi songowe kuondoka tulisubiri
zaidi ya saa mbili nzima hakurejea, mpaka kiza
kinaingia bado bibi yule hakurejea, nilitaka niondoke
usiku huo kwenda kujua kinachoendelea ila ndesi
alinifanya nisiondoke kwa vile hakukuwa na wa
kumuacha nae tulilala kwa wasi wasi na mashaka
tukisubiri pakuche, japo usiku wa deni haukawi
kucha ila usiku huo ulikuwa mrefu zaidi, mpaka
kulipokucha niliandaa uji haraka haraka nikanywa na
kumnywesha ndesi kisha nikatoka baada ya
kumuaga ndesi aliekuwa hana kauli kitandani,
nilijongea haraka haraka hadi nyumbani kwa mzee
tengo, hammadi! Nilichokiona baada ya kuingia
ndani haikuwa kikitazamika, bibi songowe na mzee
tengo pamoja na mchukuu wake walikuwa sakafuni,
uhai ulishawatoka niliogopa zaidi hapo sikutaka
kubaki pale ilinibidi nirudi nyumbani kumtaarifu
ndesi, nako hakukufaa kwavile hakukuwa tofauti na
nilipotoka ndesi nae hakuwa na uhai nililiaa zaidi
kwa uchungu, niliamua kuondoka kabisa bila
kufanya chochote niliamua kurudi nyumbani kwangu,
nilipotea na kutokea ndani ya chumba changu
ambacho kilijaa vumbi wakati huo nilijawa na
uchovu ikanibidi nilale.
Baada ya mchoko sambamba na mawazo niliamka,
ilikuwa jioni sikuwa na umbo la paka tena kwa vile
nilipewa kibangiri cha kuvaa mguuni ambacho
nikikivua tu basi narudi kuwa paka, nilitoka nje
nikiwa na ndoo yangu ya maji.
“Eheee, bora nimekuona,” nilipotokeza tu nje ya
panzia la chumba changu nilipokelewa hapo ikabidi
nigeuke kuangalia ni nani?.
“Hivi wewe umefanya hii nyumb ni ya baba yako
unatoka, huagi tunashituka tu hakuna mtu ndani,”
alikuwa ni mama yule yule mwenye kimbele mbele,
nilimpuuza na kuvaa ndala zangu nyekundu
zilizokuwa pembeni kwenye chumba changu
ninapowaka fagio.
“Naongea na wewe hujali sio!”
“Kwani we mama shida yako nini?, kipi
kinakusumbua mbona unanifata fata sana,”
nilimtolea uvivu ikabidi na mimi niongee.
“Hakuna asiependa kuishi kwa raha, hatujui
mwenzetu unafanya kazi gani mwisho tuje kubebwa
na polisi hata kwa kufuga majambazi,”
“Kwahiyo mi jambazi,!”
“Unaonekana mana muda ukiwepo ndani haujulikani,
muda ukitoka haujulikani yani hueleweki,”
nilichukizwa na maneno yake, nilimsonya tu kisha
nikaongea kuelekea bafuni, sikujua huyu mwanamke
anachonitafuta ni nini?, natamani sana kuchukua
maisha yake ila nawaonea huruma wanae, niliingia
bafuni nikajiswafi vizuri kisha nikarudi ndani wakati
natoka bafuni nilistushwa na sauti za vicheko tena
zikitokea chumbani kwangu walikuwa ni watoto,
nilitembea nilipokuwa nimesimama haraka haraka
kujua ni nini kipo ndani kwangu, kitendo cha kuingia
tu niliwakuta watoto wa yule mama wakiwa
wamekaa ndani kwangu tena kitandani na tv
wamewasha wakiangalia, kitu kingine walivuruga
vuruga ndani kwangu yani walitimua timua kila kitu
hapo nilishikwa na hasira niliwashika kwa pamoja
na kuwachapa makofi ambayo yalifanya sauti za
vilio ziwatoke kisha wakakimbia huku wakilia, kiza
kilishaingia walipotoka nilikifata kioo kisha
nikachagua nguo ambayo itanipendeza nikivalia
usiku huo, kabla sijavaa nguo ile, mama yule
aliingia ndani kwangu kwa jazba bila hata hodi,
alikuja na kunishika kisha kutaka kunipiga huku
akifoka kwa kuniita malaya eti siwezi kuzaa pia sijui
uchungu wa watoto kisa tu nimewaazibu wanae,
siku hii niliamua kumpatia alichotaka mama huyu
nilimsurubisha kisawa sawa aliondoka akiwa
amenywea, kipigo nilichompa kilikuwa stahili yake,
kupigana na mama yule hakukubadilisha mawazo
yangu, yalibaki vile vile nilivaa kisha nikatoka bila
kujali lolote.
 
SEHEMU YA 14
NA Gaooh Mussah
SIMU = 0654387935
LIKE KISHA SHARE ILINIPOST SEHEMU
INAYOFUATA.
TULIPOISHIAA SEHEMU ILIYOPITAAAAA..
mama yule aliingia ndani kwangu kwa jazba bila
hata hodi, alikuja na kunishika kisha kutaka kunipiga
huku akifoka kwa kuniita malaya eti siwezi kuzaa
pia sijui uchungu wa watoto kisa tu nimewaazibu
wanae, siku hii niliamua kumpatia alichotaka mama
huyu nilimsurubisha kisawa sawa aliondoka akiwa
amenywea, kipigo nilichompa kilikuwa stahili yake,
kupigana na mama yule hakukubadilisha mawazo
yangu, yalibaki vile vile nilivaa kisha nikatoka bila
kujali lolote.
TUENDELEEE HAPAA…
Nilitokeza mpaka kiduka karibu na duka la mpemba
hapo nilipata pikipiki ambayo ilikuwa ikielekea
barabarani, nilishamwambia uelekeo wangu
akanitajia bei Nilitafuta sehemu nikakaa kisha
nikaagiza kinywaji ambacho kilileta nikaanza kunywa
taratibu huku nikikisikilizia kinavyoshuka kooni.
“Mremboo,” ilikuwa sauti ya kiume.
“tukakubaliana na safari kuanza, siku hii niliamua
nibadilishe mandhali nilionelea nielekee sinza huku
fikra zangu zikinituma kuwa nende mpaka kwenye
moja ya bar nzuri iliyochangamka zaidi, kijana yule
wa bodaboda alinifikisha kwenye mja ya bar hapo
nilishuka na kumpa ujira wake akaondoka,
Mrembo upo vizuri, naweza kujiunga nawe hapo au
kuna mtu unamsubiri,”
“Aaaaahh,” nilikuwa nikijibu kwa kujing’ata ng’ata
ila kabla sijamaliza sentesi yangu akadakia.
“Kama yupo basi tukae kidogo then akitokea tu
nitaondoka kuwapisha,”
“Ooooh, sipo na mtu ninaemngoja nimekuja tu
mwenyewe,” nilijibu,
“Ni vizuri basi bila shaka naweza kujumuika nawe,”
“Karibu,” aliketi kisha kuniuliza nitakachokulaakitaka
niagize ili tuendelee kula, niliagiza nae akaagiza
tulianza kula kwa furaha huku tukipiga stori za hapa
na pale alikuwa mcheshi sana, nilifurahia siku hiyo
cha ajabu hata hakunitongoza wala kutaka namba
yangu.
“Janet, naona muda umekwenda vipi naweza
kukudrop unapokaa then na mimi nikaenda ninapo
ishi mana siwezi kukuacha hapa,”alisema.
“Usijali kuhusu mimi nitafika tu nyumbani boda
boda watanifikisha,” japo nlikataa asinipereke ila
alilazimisha zaidi kutaka kunipereka kwangu
alionesha kujali, nilimkubalia tukatoka akinishika
mkono mpaka kwenye gari yake ndogo aina ya
verosa ya rangi nyeusi nilimwelekeza kuwa naishi
magomeni kagera njia ya hotel ya nefaland
alinielewa kisha safari kuanza haikutuchukua muda
mrefu kwa vile ni usiku na hakukuwa na foleni,
sikutka apajue ninapoishi nilimwambia aniache
sehemu kisha tukaagana akaondoka, nikaelekea
kwangu kulikuwa kimya muda huo nikaingia ndani.
Asubuhi ya siku hiyo niliamka mapema asubuhi,
nikaelekea uwani huko nilimuona yule mama looh!
Hakunitazamana aliniogopa mpaka kuniangalia
hakika dozi ilimkolea, heshima ilirudi kwa mama
yule hakuwahi niongelesha tena, umbea umbea
wake wote uliisha, niliishi kipeke yangu peke yangu
bila rafiki wala ndugu kunitembelea, japo Maisha
haya ya upweke yalinichosha ila sikuwa na jinsi,
nilijua fika kuwa na urafiki wa karibu na watu ndio
ingekuwa sababu ya wao kujua kazi yangu, kazi
ambayo haina malipo tena kazi isiyojali wengine pia
bila kuwa na huruma na maumivu ya wengine.
Nilishikilia simu yangu huku nikiwa nimelala juu ya
sofa dogo la watu wawili, kichwa changu
nikikiegemeza kwenye kingo za sofa hilo huku
nikiwa nimeweka mto mkubwa ambao ulipabwa na
kitambaa kizuri cha madoa meupe na meusi,
niliingia mtandaoni nikitizama habari mpya mjini,
nilipendelea instagram kwa vile ni mtandao ambao
mastaa wengi ndipo wanakopatikana yani kama ni
mkoa kwa hapa dar si mbaya ukiuita dar es salaam,
Nilivutiwa na maisha ya watu wanavyoishi, nami
kidogo nilianza kupata hisia za kuwa mama, niliuhisi
umama nikatamani muda huo niwe na mwanangu
tunacheza pamoja au namnyonyesha niliyatamani
hayo ila ilikuwa ni ngumu kutokea,nikiwa kwenye
lindi la mawazo nilisikia hodi ikigonga mlangoni
kwangu, nilitaka nisitoke ila niliamua nitoke kujua
nani anaegonga mlangoni kwangu nilifika mpaka
mlangoni lakini haikuwa kama nilivyodhania pengine
ni hisia zangu tu, Mlangoni hapakuwa na mtu
anaegonga muda huo, Nilirudi ndani na kuanza
kufanya usafi wa chumba changu, Nilitumia saa
kadhaa kumaliza shughuli hiyo hapo ndio njaa
ilianza kunisakama tumbo nalo likikata sikuwa
nimekula kitu tangu asubuhi, Nilielekea dukani
kununua chochote ambacho kitanistili wakati huo,
nilifika mpaka kwenye moja la duka hapo nikaagiza
Pepsi big sambamba na Mkate, Baada ya kununua
nilitoka dukani pale kurudi nyumbani hapakuwa
mbali na ninapokaa, ndipo nilikutana na kijana
mtanashati ambaye alitokea tu mbele yangu.
“Samahani dada,”
“Bila samahani,”niliongea huku nikishika vizuri
mkate wangu ambao nilishika mkono mmoja na
soda
“Hivi wewe ni mwenyeji, mitaa hii?”aliuliza.
“Hapana mimi sio mwenyeji, huwa nasafiri muda
mrefu hivyo mitaa hii hata siijui vizuri, sijui ulikuwa
unasemaje,”
“Kuna sehemu nilikuwa naelekea sasa naona kama
nimepotea,”
“hmmmm,” niliguna baada ya kusema vile.
“Ila anyway, wacha mimi niendelee kuuliza pengine
nitapata mwenyeji atanijuza,”aliongea haraka haraka,
hapo nikamtizama na mimi sikutaka kujishughulisha
nae nilimjibu na kumuaga hapo nikarudi nyumbani
mawazoni nilijua tu ile ilikuwa janja janja tu za
kutaka kuniomba namba au kunitongoza mana
hakuwa na cha maana cha kuongea pale, sikumjali
nilielekea nyumbani nilipofika nilipokelewa na
watoto wa yule mama.
“Dada shikamoo,” walinisalimia kwa pamoja,
sikuwaitika nilipita kama sijawaona vile nilihisi
kama wanataka kuniletea nuksi siku hiyo mana
hawakuwahi kunisalimia hata siku moja tangu
nianze kuishi hapo.
“Dada mbona unatupita, tulikuwa tunaomba dada
utupe hata sh mia mbili tukanunue vitafunwa,”
Aliongea yule mkubwa nilimwangalia kisha nikampa
sh mia tano, ni huruma tu ndio ilinijia baada ya
kuwapa walinishukuru hapo nikaingia ndani kwangu
mana soda niliyokuwa nimeishikilia nilihisi itaanza
kupoa kabla sijainywa.
Sikuwa na muda wa kupika chai naanzaje kupika
chai yani niungue na sufuria asubuhi asubuhi
hapana, soda ile na mkate viliteremka kooni
kwangu taratiibu mithiri ya maji yateremkao
mlimani, nilijihisi nimeshiba siku hii nilitamani kufua
nguo zangu.
“sijanunu tena sabuni aaah,” nilikumbuka
kutokununua sabuni hapo nikajisonya kisha
nikaamka kuelekea dukani tena, wakati huu kabla
sijafika dukani nilimuona yule kaka tena, “Huyu tena
vipi?” nilijisemea mwenyewe baada ya kumuona
akija tena uelekeo wangu nikasimama nae
akasimama mbele yangu.
“Samahani,” alianza na samahani kama mwanzo tu
sikujua anachotaka ni kipi hasa kwangu.
“Bila samahani,” nilisema.
“Nilifanikiwa kupata nilipokuwa naelekea ila
imekuwa kama bahati kukuona tena,”
“Bahati tena??”
“Ndio ni bahati pia najilaumu najihisi
nimekosea,pengine kama ni mahakamani basi
ningehukumiwa kifungo kama si miaka mitano basi
kumi,”
“Heeeh, kwanini?” maneno yake yalinishangaza
nikahamaki.
“Yani nimekuuliza vizuri alafu nimeshindwa kutaka
kujua hata jina lako kweli nimekosea pia
najilaumu,”
 
SEHEMU YA 15
NA Gaooh TheAuthor
SIMU = 0654387935
LIKE PIA SAHRE ILI NIPOST SEHEMU INAYOFUATA
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITAA..
“Ndio ni bahati pia najilaumu najihisi
nimekosea,pengine kama ni mahakamani basi
ningehukumiwa kifungo kama si miaka mitano basi
kumi,”
“Heeeh, kwanini?” maneno yake yalinishangaza
nikahamaki.
“Yani nimekuuliza vizuri alafu nimeshindwa kutaka
kujua hata jina lako kweli nimekosea pia
najilaumu,”
SASA TUENDELEEEEEE…
“Wengine majina yetu mabaya wala hayapaswi
kujuliwa.”
“Hakuna jina baya yote mazuri mana kila jina la
mutu limebeba uhalisia wake na ndio mana mtoto
akizaliwa wazazi wake wanafikiria kuhusu jina la
kumpa huwa hawakurupuki, mfano utakuta mtoto
anaitwa Shida ukingalia historia yake utakuta
alipatikana kwa shida kubwa mpaka anazaliwa
wazazi wake walipata shida waliishi kwa tabu,”
“mhhhh,” niliguna.
“Ndio kila jina linamaana hivyo niombe tu msamaha
kama hutojali nijue jina lako kwa wakati huu,”
“Hapana nitakutajia vipi jina langu wakati sikujui
wala hunijui?”
“Hapana mdada sio kila watu ambao wapo karibu
au wanaongea kila siku walijuana tangu kuzaliwa
kwao, hapana Mungu wetu huwakutanisha watu kwa
njia mbali mbali, pengine hii ndio njia ambayo
tumepangiwa kukutanishwa,”
“hata kama ila sio rahisi kwanza nimechoka
kusimama kwa heri nawahi dukani,” nilisema na
kuanza kuongea, kaka yule hakukoma alizidi nifata.
“Basi naomba namba yako ya simu ili ukiwa na
muda tupate nafasi nzuri ya kuongea, ninayo mengi
ya kuongea nawe yalioujaza moyo wangu”
“We kaka sina simu ebu acha kunisumbua nina kazi
nyingi za kufanya, sio kila mwanamke unaemuona
basi uombe namba wengine wakupite ebu niache
ebooh!” nilimwambia hapo akasimama kama
mlingoni akaniacha niondoke sikujua hasira
zimetoka wapi ilikuwa kama ghafla niliondoka
kuelekea dukani, sabuni ndio niliifata sikutumia
muda mrefu kutoka dukani nikarudi nyumbani yule
kaka sikuweza kumuona pale tena, nilipofika
nyumbani hata kufua nilihisi kuchoka uvivu ulinishika
haswaaa.!, nilijitahidi tu nikachukua nguo
sambamba na mashuka yangu na mapanzia.
“Naona leo unafua mwanangu nikusaidie?” nilisikia
sauti wakti nimeinama nikifua hapo ikabidi
ninyanyuo uso wangu kutizama aliekuwa
akiniambuia ndipo nikakutana na yule mama.
“Hapana hata si nyingi mbona nitazimamaliza tu
kwa wakati,”nilimjibu kisha akapita na kutoka nje
alikuwa akiniogopa hata anapoongea na mimi
anaonekana kutetemeka nilisha lijua hilo hivyo na
mimi sikutaka stori nae kabisa, nilijua mwanzo wa
kuanza story nae itafanya atake kunijua zaidi na
mimi hiko kitu sipendi mtu achunguze maisha
yangu.
Wingu zito lilitanga juu ya anga, jua nalo liliwaka
kwa kiasi kidogo japo ilikuwa saa sita lakini
ilifanana na jioni, wafanya biashara wngi walijiandaa
na kusubiri mvua wengi wao wakikusanya biashara
zao mapema kwa ajili ya kufunga kwa kuogopa
mvua wengine wakiandaa maturubai ili kufunika
pale tu itakapo anza, siku hii niliamua niende
ufukweni nilikuwa na hamu ya vyakula vya ufukweni
hivyo sikuwa na budi nilidhamilia kwenda huko
zikiwa zimpita siku kadhaa, fukwe pekee iliyonijia
akilini kwa wakati huu ilikuwa ni fukwe ya jagwani,
nilionelea nikamalize siku yangu huko ilikuwa ni
sehemu nzuri kwavile kuna hoteli basi nilijua hata
pale mvua itakapo anza kunyesha nitaweza kujisitiri
kwenye hoteli hiyo.
Nilitumia usafiri wa bajaji ambao ulinifikisha kwa
wakati nilipofika nikafanya malipo kisha kuvaa
mavazi ya fukwe ambapo nilivaa chupi yangu ya
pink na sandarusi(sidilia) ya pink kisha nikakaa
kwenye moja ya viti vya kulala pembeni nikiwa na
juisi ya pera niliyoagiza, nikiwa pale niliwashuhudia
watoto kadhaa wakicheza kwenye dibwi la kuogelea
nilikuwa nikiwatizama huku nikitamani kitu kutoka
kwao, japo sikutilia manani mawazo yangu ila
nilihisi akili haikuwa yangu, katika wale watoto kuna
mmoja alikuwa akiwasukuma wenzie ndani ya maji,
nilipatwa na hasira yule mtoto nae nilimdidimiza
ndani ya maji kwa kutumia macho yangu, alipiga
kelele akiwa amekwisha kunywa lita kadhaa za
maji, wazazi wake walimfata haraka haraka kwenda
kumtoa hawakuwa mbali na eneo lile, nilichokuwa
nataka kukifanya ni tofauti na nilichofanya akili
yangu ilinituma nimtoe uhai yule mtoto ila
nilipingana nayo nilimdidimiza tu kwenye maji roho
ya huruma ilinikaa, saa zilisogea nikahisi njaa
nikasogea mpaka sehemu ya vyakula kisha
nikaagiza niliagiza sea food, yani masamaki samaki
ya baharini yaliojazwa viungo kama nyanya vitunguu
karoti na vyengine ambavyo havikupikwa kisha
nikaanza kula chakula kilikuwa kitamu kweli niliuhisi
utamu wake hapo nikawaza na kuanza kulinganisha
utamu wa chakula hiko na nyama za watu, japo
kilikuwa kitamu ila niliona nyama za watu zilikuwa
tamu zaidi hasa za watoto mbichi zilikuwa na
chumvi chumvi pia laini, niliachana na mawazo hayo
mana nilijua si akili yangu baada ya kumaliza kula
nilikaa kidogo kama nusu saa kisha nikaingia ndani
ya maji kuogelea kulikuwa na watu kadhaa wengine
na wapenzi wao wameshikana wivu ulinipita
sikuwaonea wivu japo na mimi nilitamani ingekuwa
hivyo hata ningekuwa na gao wakati huu ila mmhh
gao hanifai sitamuweza bora Kendrick wa niwe na
nani kuliko Gao wa Tia yote.
Baada ya kuridhika na maji nikajitoa kisha kuanza
kujifuta nataulo ambalo lilinikausha vizuri mwili
wangu jioni iliingia hakukuwa na mvua iliyonyesha
mchana huo mbali na wingu kutanda juu, nilivaa
nguo zangu kisha kuondokaa baada ya kuita bajaji,
sikutaka kurudi nyumbani, niliamua nifanye kazi ya
ziada mana ilikuwa ni jumanne nilichofanya
nilimulekeza yule deleva akaniache salenda
darajani.
“Huogopi si wanasema kuntisha pale kiza kiingia
pia kuna vibaka,”dereva aliongea kwa wasi wasi.
“Huo siogopagi binadamu ambao wote tunatengea
pumzi mmoja tu,”
“Hapana dada yangu mi najali usalama wako japo
wewe ni mteja wangu ila sipendi kuona ukikutwa na
baya ikiwa mimi nipo tena niache litokee,”
“Ondoa shaka we niache tu pale kuna mtu anakuja
kunichukua we usijali,” ilikuwa kama nambembeleza
yani anang’ang’aniza, kama vile usalama wa taifa
aliponifikisha alitaka eti nikae kwenye bajaji yake
mpaka huyo mtu atakapo tokea nilimwambia
aondoke huyo mtu ameshafika kweli akaondoka na
kuniacha pale nikiwa nimesimama sina hili wala lile
nilijiweka kama mtego mana nilijua tu kuna watakao
jipendekeza.
“Sister vipi,” nilisikia sauti ambayo hata sikujua
alieitoa ni nani, sikujiangaisha kuitika nikakaa
kimya.
“Si nakusalimia hunisikii au,?”aliendelea kuongea.
“Kwani lazima nikujibu si upite tu!” niliongea kwa
ukali.
“Ahaa unaleta usister duu kwenye maeneo yetu sio,
unajua mimi nani?”
“sina hata haja ya kukujua wala sia hata sababu ya
kukujua mana hakuna utakachonisaidia,”
“Niliposema tu hivyo alipiga mluzi, sijajua wa nini
ila kwa akili zangu za haraka haraka za kikubwa
nilijua anawaita wenzake
 
SEHEMU YA 16
Simu=0654387935
LIKE SHARE ILINIPOST SEHEMU INAYOFUATA.
TULIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA.
“sina hata haja ya kukujua wala sia hata sababu ya
kukujua mana hakuna utakachonisaidia,”
“Niliposema tu hivyo alipiga mluzi, sijajua wa nini
ila kwa akili zangu za haraka haraka za kikubwa
nilijua anawaita wenzake
SASA ENDELEAAAA..
Mluzi ule ulinikumbusha mbali, nilikumbuka baadhi
ya wanaume walivyokuwa wakiniita ‘phuuuu phuuuu’
kisha nikatabasamu, hapo nikasimama mithili ya
mtu anaengoja usaili wa kazi nilikuwa nimejizatiti,
japo sitatimiza kilichonipereka salenda mana leo
nilikuwa na hamu ya kula nyama hivyo niliona
sehemu ambayo itakuwa rahisi ni salenda nilipanga
nikifika pale niangushe moja ya magari yanayopita
kisha nipate nyama.
Funzo kidogo= wachawi wamepewa uwezo wa
kufanya vitu mbali mbali, na pindi wanapodhamiria
kufanya jambo lao au kumchukua mtu yoyote ni
lazima watimize mfano rahisi tu kunaweza kutokea
ajali labda gari lilijaa abilia wengi zaidi ya hamsini
hata sitini likaanguka cha kushangaza unaweza
kukuta watu wote ndani ya gari wasife wala kupata
michubuko yoyote ila mtu mmoja tu ndio utakuta
kafa, nadhani hata wewe msomaji ni shaidiwa
jambo hili kama hujashuhudia basi umewahi
kusikia.
Kijana yule alizidi kupiga miluzi huku akiniangalia
nilimuona vyema kutokana na taa zilizokuwa eneo
lile nilimuona vyema.
“We kwani unashida gani kipi unataka kutoka
kwangu,”
“We si dada wa mjini subiri,” aliongea eti akiona
ananitisha na maneno yake kumbe ndio kwanza
niliona napata nilichokifata bila kutumia nguvu wala
kuhatarisha maisha ya watu wengine wasio na hatia
yoyote, nilijaribu kuondoka ila alinivuta hapo na
wenzake wakatokea wakiwa wameshika mapanga
mikononi.
“Hahahahahaha!” nilicheka kwa sauti huku kicheko
kikijirudia rudia.
“Jimmy anaonekana anadharau sana huyu, itabidi
tukimaliza tumfanyie kama vile,”waliteta, japo
waliongea sauti ndogo ila haikuwa sababu ya mimi
kutokuisikia nilisikia.
“Kwa usalama wako weka kila kilichopo mwilini
mwako chini,” aliongea kwa msisitizo.
“Kwanza niwa katishe tu tamaa, hakuna ambacho
nitaweka chini yani hilo msahau na mfute akilini
mwenu,”
“unasemaje we malaya!”alinitusi hapo nilimpiga kofi
mmoja wao, kofi lile ndio kama liliwaamsha
walinisogelea karibu kisha jimmy akanipiga bapa la
panga kwenye mapaja yangu huku akinisindikiza na
mtama ulioniangusha chini,nikiwa pale chini niliona
wakitaka kunishika mikono yangu yani wawili
walikuja ili wanishikilie alafu mmoja nilimuona
akifungua mkanda wake kwa lengo la kutaka
kunibaka, hapo nilitumia akili za ziada nilipotea pale
kisha nikawatokea kwa nyuma huku nikicheka,
walianza kuhaha na kujaribu kukimbia, sikuruhusu
hilo litokee niliwavuta mmoja mmoja na mkono
wangu kisha kuwatupa chini, walianguka huku
wakipiga kelele, sikuona sababu ya kuangusha tena
gari tayari nilipata kafara ya siku hii ya kutoa siku ya
jumanne huwa ni siku yetu ya sadaka sio siku nzuri
kwa binadamu wa kawaida pia ni siku iliyojaa nuksi
zaidi hata biashara nyingi siku hii huwa hazitoki
vizuri.
Nilichowafanya vibaka wale sidhani kama watarudia
tena kazi hiyo huko kuzimu nilipowapereka kwani
pale nilipowaangusha chini niliwavunja vunja kila
kiungo kwenye mwili wao kwa kuwarusha juu chini
juu chini kisha niliwakata kati kati yani pande mbili
nilitumia kisu cha kichawi ambacho huwa tunakiona
kinakuja kisha baada ya kutenganisha mikono ya
kushoto na kulia hapo niliita usafiri pamoja na
chungu kikubwa ambacho nilitumbukiza nyama zao
kisha ule usafiri wa paka ukanibeba kunipereka
kwenye hekali letu la sadaka, tulijumuika tena
wachawi mbali mbali, mavazi niliyokuwa nimevaa
mwanzo niliyavua na kuvaa kaniki nyeusi
niliizungusha mwilini huku nikijifunga kitambaa
cheusi pia kichwani kwangu.
Tulisheherekea tukala na kunywa pamoja, sikuwa na
ukaribu na mchawi mwengine yoyote yani tulikuwa
tukikutana hapo tu na kufanya shughuli zetu ila ule
ukaribu wa kirafiki sikutaka kuwa nao hata kidogo,
Baada ya muda kidogo shughuli zilifika tamati kila
mmoja akaondoka pale mimi pia niliondoka ilikuwa
usiku wa saa tisha nilirudishwa nyumbani kwa
usafiri wa paka mkubwa mweusi ambaye nilikaa
kwenye shingo yake, tayari nilivaa nguo zangu na
mkoba wangu pia nilikuwa nao wale wezi
niliowafanya bucha hawakuuchukua, nilijihisi
nimechoka siku hii nilipoingia ndani nilijipumzisha
tu sikuwa na chakufanya, usingi nao ulinichukua
kisha ukasafiri na mimi mbali mawinguni na
kuniletea njozi nzurii zilizonibembeleza.
“Mshike mshike mshike,” nilizidi kukimbia huku
nguvu zikiniisha lakini bado nilijitahidi kukimbia,
sauti zile za mshike mshike nazo hazikukoma,
zilinijia sambamba kwenye masikio yangu,
walionekana ni watu wenye usongo na mimi
wakidhamilia kunikamata sikujua lengo lango, kitu
pekee kilichokuwa msaada japo ni nguvu zangu za
kukimbia mana hata uchawi ulinisaliti hata
nilipoujaribu kuutumia haukufanya chochote
nilikimbia kwenye makorongo huku mbele kukijawa
na msitu wenye giza lililomeya kila sehemu
nilimkumbuka Mungu eti nilianza kumuomba mbali
na mbaya yangu niliyotenda lakini nilimkumbuka tu,
mwanzoni zilikuwa sauti za wachache ila sasa
ziliongezeka zilikuwa ni sauti za kundi zikizomea na
kunikimbiza hata pale nilipoingia kwenye
maporomoko bado ziliendelea kunisakama, “Mungu
wangu, mungu wangu’ ndio sauti pekee iliyonitoka
kinywani, sikuwahi kujua kumbe na mimi nimuoga
namna hii, uwoga wangu ulimithilika siku hii
ambapo nilikuwa kama mtetea anekimbizwa na
jogoo.
Baada ya kukimbia maili kadhaa, nilifika sehemu
kwenye moja ya mawe makubwa hapo nilikaa, huku
pumzi ndefu zikinitoka na kuhema juu juu kama
mwana riadha japo ilikuwa ni mchana lakini msitu
huo ulikuwa na giza hata ule mwangaza wake
haukuwa mkubwa jua lilionekana kwa mbali tena
likizibwa na miti iliyokuwa mirefu zaidi, nikiwa sina
moja wala kumi na moja nilistushwa na viumbe
ambavyo vilinizunguka pale nilipokaa, cha
kushangaza macho yao yalikuwa yakiwaka taa, taa
zilizonimulika mimi,viumbe vile vilikuwa na miili
mikubwa, woga ulikaa tena nikaanza kusota kwa
kurudi nyuma ila kila ninaporudi nilikuwa nikijigonga
kwenye lile jiwe, viumbe vile vilianza kuunguruma
mithili ya simba,simba mwenye njaa asiekula wiki
nzima, hakika niliuona mwisho wangu, nikatamani
hata lile jiwe lifunguke niingie ndani iwe kama
chumba ambacho kitanisitiri na kunificha kwenye
dhahama hii kubwa.
Sikuwa na chakufanya viumbe vile vilizidi
kunisogelea,kidogo akili ilinijia sauti kubwa
ikagongwa kwenye kuta za masikio yangu zikisema
HAKUNA KUKATA TAMAA, sauti hiyo ilinipa nguvu,
nguvu iliyonituma nijitoe pale na kuamka kama sio
mimi niliamka kabla havijafika viumbe vile na
kuanza kukimbia tena jasho jingi lilitereka kwenye
kifua changu yalipomaziwa yangu, liliteremka
mpaka mgongoni, wakati nikihangaika kukimbia
viumbe vile navyo havikuwa nyuma vilinifata kwa
kasi ya ajabu huku vikiongea lugha ambayo
sikuwahi kuisikia, wala siwezi kuielewa hapo
nikatamani ningekuwa na mabawa kisha nipae
mbali na eneo hilo ila haikuwa hivyo kila
ninavyoweka jitihada za kukimbia ndio navyo
vinanikaribia.
Asie na bahati kweli habahatiki, mbali na kukimbia
kote ila niliishia kuanguka chini baada ya kukikwaa
kwenye moja ya visiki kisha nikaanguka chini hapo
viumbe vile vilikuja na kuniweka kati kati, nilizidi
kuogopa na kuuona mwisho wangu pale kilipoanza
kuvuta mguu wangu kwa lengo la kunitafuna….
 
SEHEMU YA 17
NA Gaooh TheAuthor
SIMU=0654387935
LIKE PIA SHARE NIPOST SEHEMU INAYOFUATIA..
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA…
Asie na bahati kweli habahatiki, mbali na kukimbia
kote ila niliishia kuanguka chini baada ya kukikwaa
kwenye moja ya visiki kisha nikaanguka chini hapo
viumbe vile vilikuja na kuniweka kati kati, nilizidi
kuogopa na kuuona mwisho wangu pale kilipoanza
kuvuta mguu wangu kwa lengo la kunitafuna….
ENDELEEAA SASA
Nilistuka kutoka usingizini jasho jingi likinitoa ndoto
hii iliniogofya zaidi, sikujua maana yake nini hata
usingizi ulikata niliamka huku mwili ukiwa
umechoka, tukio hili nililoota lilifanya niwaze
mwisho wangu niliwaza je siku yangu na mimi
ikifika kipi kitanikuta nilijiwazia kwa sauti, hata njaa
pamoja na kiu vilinishika nilianza na maji ambayo
nilichukua kwenye friji hayakuwa na baridi kwa vile
hakukuwa na umeme, pia hata ungekuwepo
yasingekuwa na baridi kwa vile sikuwa nimewasha
friji, nilitizama saa yangu ya mshale niliyoipachika
ukutani muda huo ilikuwa saa nne asubuhi,
niliyatamanimaji zaidi hivyo nilivua nguo zangu na
kuvaa taulo kwa ajili ya kwenda kuoga jasho lilijaa
mwilini mwangu, nilitoka nikiwa na ndoo yangu
hakukuwa na watu nje wapangaji wenzangu
walikuwa vyumbani mwao, niliingia bafuni na kuoga
dakika kadhaa nilitoka na kurudi chumbani kwangu,
nikasimama kwenye kioo kikubwa ambacho
natumia kuvaa, nilijitazama nikiwa sina nguo
nilionekana mrembo zaidi, mwili wangu ulikuwa ule
mwili wa mwanamke ambaye kila mwanaume
akimuona lazima autamani, ‘ni lini huu mwili
utakuwa mali ya mtu yani mume wangu ambaye
tutaishi na kuwa na malengo yetu’ nilijiwazia wakati
huo nikipaka mafuta, mawazo haya sikuyatilia
manani kivile niliyapuuza, siku hii sikupanga kwenda
popote nilidhamiria kukaa nyumbani muda wote
nilionelea ni bora nipumzishe mwili wangu, nilijihisi
kuchoka zaidi hata mawazo yaliniandama kuanzia
ndoto ile yenye kuogofya.
Nilivaa nguo za nyumbani siku hii niliandaa chakula
ambacho nilihasi kukila ugali dagaa na bamia la
mlenda, nilivifata gengeni ambako hapakuwa mbali
na nyumbani nilinunua mboga ikawa imebaki unga
tu,nilikuwa nimehasi kuvila hivyo siku hii ndio
ulikuwa mlo wangu, hata sabufa langu siku hii
lilipata uhai niliwasha sabufa langu na kuweka mziki
ambao ulikuwa ukipiga na mimi kuanza kuufatisha
huku nikipika, nilikuwa nikipika ndani kwangu kwa
vile ni jiko la gesi basi haikuchukua muda mboga
ziliiva, nilifata unga dukani sikuwa na wakumtuma
hivyo nilienda mwenyewe kununua unga nilinunua
unga wa dona kisha kurudi nyumbani.
Nikiwa nimekaa nasubiri uji uchemke ili niweze
kusonga, nilihisi mlango wangu ukigonga huku
nikisikia mtu akibisha hodi nilipunguza sauti ya
redio yangu kisha nikamkaribisha mtu yule alikuwa
yule mama nilimkaribisha nae akaingia, hakuwa na
watoto wake alikuwa peke yake, mwanzoni nilihisi
labda ameretwa na umbea ndani kwangu nikatamani
kumkataza asiingie ila nilimruhusu tu mana nilitaka
kujua kilichomleta ndani kwangu.
Alikaa kwenye sofa langu kuu kuu wakati huu na
mimi nilianza kusonga ugali ule kwa vile haukuwa
mkubwa nilitumia muda mchache ulikwiva nikaweka
kwenye hotpots ili usipoe, nilitaka niongee na
mgeni kwanza.
“Karibu”Nilimkaribisha tena na mimi nikakaa
kwenye kochi jengine.
“Asante mwanangu, nimekuja kukusalimia pia
nimekuja ili tumalize tofauti zetu zote,”aliongea huku
akionekana mwenye aibu, alikuwa akijishika shika
kama mtu asiejiamini.
“Kwani tunatofauti gani mama yangu mbona mimi
sina tofauti yoyote na wewe mama,”
“Najua uwezi sema, ila nakuomba uweze
kunisamehe kila nilichokukosea, mkosefu zaidi
mana nimekukosea ikiwa wewe hakuna
ulichonifanyia kibaya,”
“Kweli,” niliitika.
“Ndio mwanangu mpaka tunaadhirisha mbele ya
watoto, najua yote ni makosa yangu nakuomba
unisamehe pia sitakaa nirudie tena mwanangu”
alisema alitaka kupiga magoti ndipo nilimuwahi na
kumsimamisha, tuliendelea kuongea machache
nikamhakikishia kuwa yameisha hapo nikachukua
ugali wangu na kuweka mezani, nilipomkaribisha
hakusita nae aliukalia ugali wangu tukaanza kula
pamoja, alinipunguzia bajeti mana nilipika chakula
cha saizi yangu.
Tulipomaliza kula aliaga akaondoka, japo
nilimwambia nimemsamehe ila niliendelea kuushuku
msamaha wake niliwaza mengi pengine anataka
kuniingia au ameomba msamaha kwa manufaa yake
kuna kitu anakitaka kutoka kwangu ndio
nilichowaza, nilitoa vyombo nje kwa ajili ya kuosha
havikuwa vingi hivyo muda mchache nilimaliza hapo
nikaingia ndani niliandamwa na mchoko ila kulala
sikutamani nilihisi itajirudia ndoto ile chafu niliyoota,
nilichoamua ni kukaa tu kuangalia runinga huku
nikiweka miziki hata ile sauti ya sabufa yangu
niliiongeza ikawa kubwa zaidi kama mwanzo.
Nikiwa sina hili wala lile simu yangu ilipata uhai
baada ya kuwa kimya kwa muda, ilipata uhai na
kuanza kutoa mlio,mlio wake niliouweka hapo
niitizama kwa vile haikuwa mbali ilikuwa juu ya
meza hivyo niliweza kuitizama, namba iliyopiga
ilikuwa ngeni, nikimaanisha kwenye simu yangu
haikuwepo, nilitaka niipokee ila kuna hali ilinijia
kuwa nipokee hapo sikuipinga niliipokea na kisha
kuweka sikioni kusikiliza aliepiga anakipi cha
kusema.
“hallo” ilisikika sauti upande wa pili.
“Hallo”
“Habari kidawa umzima wewe?”
“Mimi mzima sijui wewe, pia nani mwenzangu?”
niliuliza mana sikuwa nikimjua alafu yeye ananijuaje.
“Naitwa..” kabla hajamaliza kuongea simu yake
ilikata, hata pale nilipojaribu kuimpigia haikuwa
ikipatikana niliipuuzia na kuongeza sauti ya redio
ambayo nilikuwa nimepunguza, kukaa ndani
kulinichosha hivyo niliona bora nitoke kidogo nje,
jua lilikuwa kali sana hata nje hapakuwa na sehemu
ya kukaa hivyo ilinibidi nielekee dukani kwenye moja
ya duka ambalo lipo hapa mtaani kwetu pia ndio
duka langu la siku zote nilifika pale, nikasalimiana
na muuzaji akanipa kiti nikakaa pale nje na kuagiza
soda aliniletea ilikuwa soda nyeusi, baada ya
kuniletea nae alitoka nje na kiti chengine.
“Naona leo upo nyumbani Kidawa?” aliuliza.
“ Ndio kuna wakati unapaswa kukaaa nyumbani
kupumzika, si unajua mihangaiko nayo inachosha
yani chumba changu mpaka kinanimis,”
“Hahahaha kweli haloo,mana hata mimi sikumbuki
mara ya mwisho lini nilikuona mtaani,”
“Kwani unaonaga wewe ukikaa hapo dukani macho
yote kwenye pesa, si mmetumwa hela nyie kwenu,”
“Hahahahaha, eti tumetumwa hela” alicheka hapo
hata mimi nilicheka. Siku hii niliamua nikae na
muuza duka kwa ajili ya kubadilisha mawazo,
chumba changu sikuwa nikikitamani sana, na mimi
nilianza kuuhisi ubinadamu nilitamani kuwa karibu
na watu hata nijichanganye nao.
Tuliongea mengi sana na muuza duka huyu ambaye
alikuwa akiitwa michael, alinitajia changamoto za
biashara yake, pia kipindi ambacho mauzo
yanaongezeka vyote alinielezea.
“Unajua nini Kidawa, biashara sio uchawi japo kuna
wanaotumia, biashara ni kauli na kujali, yaniMfanya
biashara kama mfanya biashara anatakiwa awe
nakauli nzuri kwa wateja wake ikiwezekana hata
kuwabembeleza awabembeleze, hivyo itafanya
waione thamani yao kiasi kwamba watakuja tena
muda mwengine, hiyo ndio siri ya biashara sisi
wachaga tunaonekana tunakasi ya kutafuta pesa
kweli ila sisi ni wabunifu pia ni watu wa kuona fursa
leo hii ukiangalia asilimia kubwa ya watu wenye
mafanikio hapa dar utakuta wachaga ni asilimia
kubwa zaidi kuliko makabila mengine,”
“Mnapenda kujisifie nyie,kama kawaida yenu.”
“Nimekwambi ukweli Kidawa, alafu vipi kuhusu
shemuji sikuwahi kukuona nae.”
“Mengine yakupite we kaka,”
“Nauliza tu Dada, si unajua kwenye uzio penyeza
rupia pengine nikabahatika,”
“Hahaha yani najitoa fahamu kabisa naolewa na
wewe Michael,”niliongea huku nikicheka wakati huo
nikimalizia soda yangu.
“kwani tuna nini wachaga,”
“Hamna kitu ila nyie ni wachumi sana, yani pia
mimi kwa sasa sipo tayari kuingia kwenye
mahusiano,” niliongea kwa ufupi huku nikimpa
chupa yake sikutaka kuendeleza mazungumzo hayo
tena, nilimuaga huku akinikaribisha kuwa nirudi tena
wakati mwingine kabla sijaondoka yule kaka alikuja
tena.
“Mamboo” alinisalimu, sikumuitika nilifanya kama
sijasikia kisha nikaondoka eneo lile kurudi kwangu,
nilifika mapaka ndani kwangu, wa huu nikajirusha
kitandani na kuvuta pumzi ndefu, muda nao
ulisogea jioni tayari ilishafika nilimka kitandani
kisha nikaelekea bafuni kuoga kutokana na jua kali
hivyo ilinibidi nikaoge tena,nilienda kuoga kisha
kurudi baada ya kumaliza niliingia ndani kwangu
kisha kuliendea kabati nilichagua nguo ambayo
nilipanga kuvaa siku hii, baada ya kuichagua
nilikiendea kioo kwa ajili ya kupaka mafuta na
kuvaa, nilipofika kwenye kioo na kuanza kupaka
mfuta kabla sijainua uso wangu nilishangaa kwenye
kioo nikiona mwili tofauti na wangu, kutokana na
wasi wasi nilimsha kichwa kutizama loooh
nilichokiona sikuamini, mzee tengo alikuwa
akionekana kwenye kioo….
 
SEHEMU YA 18
NA Gaooh TheAuthor
SIMU = 0654387935
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
nilipofika kwenye kioo na kuanza kupaka mfuta
kabla sijainua uso wangu nilishangaa kwenye kioo
nikiona mwili tofauti na wangu, kutokana na wasi
wasi nilimsha kichwa kutizama loooh nilichokiona
sikuamini, mzee tengo alikuwa akionekana kwenye
kioo….
SASA ENDELEAAA..
Niliogopa na kuanza kutetemeka, mzee tengo
alionekana kwenye kioo akiwa amefura zaidi
niliamka nilipokuwa nimekaa kwenye kitu, niliamka
ili nisimuone ila cha kushangaza mzee tengo
nilimuona tena kwenye pembe.
“Hahahaha huwezi kunikimbia we binti mdogo,”
alicheka huku akiniongelesha kwa kunitisha.
“Mzee kwani mimi nimekukosea nini?” nilimuuliza.
“hujui ulichonikosea??”alisema, hapo nilidaka taulo
lililokuwa likitaka kuanguka kwa woga.
“Wewe na wenzako ndio sababu ya familia yangu
kupotea, namiapia hili mtalipia kama mlijua
nimekufa basi hilo mnatakiwa msahau bado sijafa,”
alisema kisha akaendeleaa,”Naondoka ila
nakuhakikishia nitarudi unadeni langu pia unatakiwa
ulipe?” alisema kisha akapotea sikumuona tena
Mzee tengo ni wazi alipotea huku akiniacha na
vitisho, jambo hili lilinifikirisha kidogo, hata kule
kuvaa niliacha kabisa kisha kukaa kitandani jasho
jingi likinitiririka hali ya kuwa natoka kuoga,
nilipolaa kitandani nilijiwazia huku akili yangu
ikionekana wazi kuchoka na mambo yale, nilianza
kuunganisha dot nilikumbuka ndoto niliyoota japo
wengi wa watu huwa wanasema ndoto ni ndoto
hazina maana yoyote ila kwa sisi wachawi ndoto ya
aina ile sio nzuri hata kidogo inashiria vita pia uadui
na hata ukomo wa mtu, yani kuna jambo baya
laweza kukutokea mbeleni kama hutakuwa makini,
matukio haya mawili niliyachukulia kwa ukubwa
kisha nikayaweka kama screen kubwa mbele yangu
au kama ni maandishi basi Niliyaandika kwa herufi
kubwa zaidi kuonesha uzito wake NDOTO NA MZEE
TENGO, niliwaza masikini mie Kidawa.
Liwalo na liwe’ Niliwaza kwa sauti kisha nikaamka
nilipokaa na kuchukua ngu zangu na kuzivaa,
zilinipendeza hapo nikatabasau Mwanya mdogo
uliyokuwa kwenye meno ya chini ukaonekana vyema
kinywani mwangu,Nilijaribu kuyameza tu Mawazo
yale nikijua nitapata suruhu yake.
Niliamua nitoke wakati huo tayari kiza kilimea
angani, japo sikuwa na sehemu niliyopanga kwenda
ila nilisukumwa na kauli ya Mtembea bure sio mkaa
bure, hapo ikabidi nitoke,kutoka kutoka kweli
nilitoka hata usafiri sikuchukua nilitembea sikujua
nimepata wapi ujasiri wa kutembea wakati mara
zote huwa napendelea kupanda bajaji, miguu
haikunisali nilitembea maili kadhaa kisha nilifika
nilipokuwa naenda japo sikupanga kwenda ila
nilifika MANZESE DARAJANI nilipanda ngazi na
kufika juu baada ya kufika juu walinipokea.
“Sister mambo, nikupige moja,”
“Hapana sihitaji,”
“umependeza kubali nikupige moja itatoka vizuri
sana,” Alizidi kulazimisha mpiga picha yule wa hapa
manzese darajani alinichosha, ikabidi nikubali
nilikubali anipige picha, kisha nikaweka pozi, pozi
ambalo alivutiwa nalo akanisifia kisha akapiga,
nilijilazimisha kufurahi tu japo sikuwa na furaha
nilimlipa pesa yake kwa ajili ya kwenda kunisafishia
picha hiyo akatoka kitendo cha nusu saa alirudi
akiwa na picha ile sikuwa na haraka ya kuiangalia
niliichukua na kuweka kwenye mkoba ambao
nilikuwa nimebeba.
“Asante dada, ukihitaji picha kali za location
unaweza nicheki tu pia napiga,”alijinadi sikuwa na
story nae nikaenda kwenye moja ya ngazi kisha
nikakaa, macho yangu yakitazama magari, magari
ambayo yalikuwa yakipita kwa kasi huku honi zao
mfululizo zikisikika,zilikuwa kama mashairi ya
nyimbo sikioni mwangu huku nikitazama magari
yale sikuwa na sehemu pekee ya kutuliza mawazo
yangu zaidi ya hapo, kuna wakati nilimkumbuka
bibi,bibi alikuwa msaada wangu mkubwa kila
nilipomhitaji matatizo yangu yote ningeyamaliza na
kuyatatua kwake leo hii yuko wapi?,iliniuma sana.
Kwanini niishi kama mnyama, nisiejali wengine
maisha yangu yamekuwa kama vile mchezo,
mchezo ambao ili uendelee kucheza lazima
uwamalize wengine, filamu nzimaya matukio
mabaya na machafu niliyofanya yote yalinijia akilini
niliyaona yote kuanzia ya kumaliza watoto wa
wanakijiji mpaka kuwachinja chinja wale wezi
waliotaka kuniibia salenda, nilihisi uchungu,
uchungu ulioambatana na machozi machoni
mwangu, nilivaa uhusika wa familia zao jinsi
zilivyoumia kutoweka kwao.
Nikiwa kwenye lindi la mawazo nilistushwa na
mkono wa mtu ulionishika bega, kwa woga nilitaka
niruke mana nilistuka kama mtu alietolea usingizi.
“Sister samahani, tunaweza kukaa wote,” ndio
maneno alionitamkia nilikasirika zaidi, yani anistue
alafu aniambie ujinga huo eti anataka kukaa na
mimi.
“Nakuomba uondoke tu mana umeniharibia mood
yote ya kuwa hapa,” nilimwambia kwa ukali japo
wengine hawakusikia kwavile walikuwa mbali na
pale tulipokuwa.
“Sister nisamehe tu, tunaweza kukaa tukaongea
najua unamawazo nimekuangalia muda mrefu
unaonekana kuna jambo linakutatiza naweza
kushauri,”
“Unaonaje huo ushauri wako ukapereka hospitali
kwa wagonjwa unaweza kuwafaa kuliko kunireta
mimi,”Niliongea kwa ukali hakusikia nae alikuwa
king’ang’anizi sijui kaka zangu mnakwamaga wapi,
yani mnakuwaga bing’ang’anizi kwa wasichana
kuanzia kwenye kuomba namba yani wengine
watang’ang’ania hadi wapewe huyu kaka
aling’ng’ania hakujua mwenzio nipo kwenye hali
gani, ndipo nikachukua uamuzi, uamuzi ambayo
sikutegema kama nitauchukua, nilimtazama huyu
kaka kwa macho ya kichawi ambayo yaliwaka taa,
taa ambayo ilikuwa kama pigo kwake, nilitumia
mkono wangu kama silaha na kung’ata meno huku
nikiuvingirisha kaka huyo alinguka chini, ngazi nazo
zilimsaliti hazikumsitiri alibiringita moja kwa moja
mpaka chini kule kwenye watu ambao wanafanya
mazoezi, alipoanguka hakutamani kuwa hapo tena
aliondoka tena kwa kukimbia hakuniangalia, watu
hawakujua kilichotokea kuna ambao waliishia
kumcheka wakijua ameanguka kwa kuteleza, watu
bwana na mimi sikuwa na hamu ya kukaa tena pale
niliondoka mdogo mdogo kurudi nyumbani kwangu,
nilihisi njaa hapo ikanibidi nichukue usafiri sikuweza
kutembea tena nilichukua piki piki ambayo
ilinifikisha mtaani kwetu kwenye moja ya vibanda
vya chips, niliagiza kisha baada ya kusubiri kidogo
zilikuwa tayari hapo nikachukua na kuondoka.
Hapakuwa mbali na nyumbani, hivyo dakika kadhaa
nilifika mpaka nyumbani hapo nilikuta wapangaji
wenzangu walikuwa wamekaa, nilipotokea tu mimi
walianza kucheka, sikujua wanachocheka sikuwajali
sana mana nilijua bidamu kucheka ni kawaida yao,
nilifika mpaka pale walipo nikawasalimu hakuna
alieitika na mimi nikapita ila katika kikundi
walichokaa yule mama hakuwepo sikujua alikuwa
wapi wakati huo, sikuwajali nilikifikia kitasa cha
mlango wangu kwa vile niliwapita wakaacha
kucheka tena “Heeheeeee hallo, chezea dar wewe.”
Sikuelewa kicheko chao tena, nilitamani niondoke
hapo niingie ndani ila kitasa kiliniuangusha kila
nikijaribu kufungua kilikataa, veko vile vilinikasirisha
nikatamani nichukue hatua, cha kushukuru mlango
ulifunguka nikaingia ndani, niliwasha taa ukutani na
kukaa kwenye kochi chips zangu nikaweka mezani
na mkoba niliokuwa nimeshikilia mkononi.
Japo nilikuwa na njaa ila wakati huo hata sikuhisi
hamu ya kula, niliwaza nikaoge ila nilifikilia vicheko
vya huko nje nikashindwa kutoka, nilibaki nikiwa
sina cha kufanya ikabidi nitoe picha niliyopiga kule
darajani ili niiangalie looh! Nilipoitoa sikuamini
picha ilikuwa yangu yani kuanzia mwili na kila kitu
vilionesha ni mimi lakini sura haikuwa yangu
pichani, taswira ya paka mweusi ilionekana yani
ndio imekuwa kama uso wangu, nikaitupa chini…
 
SEHEMU YA 19
NA Gaooh TheAuthor
Simu = 0654387935
TULIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Japo nilikuwa na njaa ila wakati huo hata sikuhisi
hamu ya kula, niliwaza nikaoge ila nilifikilia vicheko
vya huko nje nikashindwa kutoka, nilibaki nikiwa
sina cha kufanya ikabidi nitoe picha niliyopiga kule
darajani ili niiangalie looh! Nilipoitoa sikuamini
picha ilikuwa yangu yani kuanzia mwili na kila kitu
vilionesha ni mimi lakini sura haikuwa yangu
pichani, taswira ya paka mweusi ilionekana yani
ndio imekuwa kama uso wangu, nikaitupa chini…
ENDELEAAA SASA
Baada ya kuitupa chini nilipiga kelele, sidhani kama
kuna aliezisikia kelele zangu, nilihisi naota ila
haikuwa vile hata nilipoiangalia tena picha ile
ilikuwa vile vile hapo sauti za vicheko zilisikika
“Hahahahahahahahaha” chumba kizima zilirindima
sikujua kama nje zilisikika ila zilikuwa kubwa kiasi
kwamba nikaziba masikio mana niliona sasa
zitatoboa ngoma za maikio yangu, nilipotoa mikono
masikioni kwangu hakukuwa na kelele tena hapo
ikabidi nitoke nje kuchungulia nilichungulia alafu
nikaingia tena ndani.
Baaada kurudi ndani nilikaa kwenye sofa
langu’inamana pale nje wale wasichana walinicheka
kwa kuwa sura yangu ni ya paka au?’ nilijiuliza
mwenyewe pasina majibu, na kama kweli uso
wangu ni wa paka mbona mpiga picha hakusema
wala kuogopa chochote,mbona hata deleva boda
boda na hata muuza chips hawakusema chochote?
Na je kama uso wangu ni wapaka wamenionaje
ikiwa wakati ule ilikuwa ni usiku’ ‘HAPANA’ nilisema
kwa sauti kubwa kisha nikaamka pale nilipokuwa
nimekaa na kukiendelea kioo ambacho kilinilaki
pale kiliponiona, chakushangaza nilipofika kwenye
kioo sura yangu haikuwa ya paka ilikuwa ile ile tu,
nikjishangaa.
Kuna kitu hapa sio bure’ nilijisemea huku niliramba
lips zangu, baada ya kuona nipo kawaida ndipo
nikakifata chakula changu japo kilisha poa ila
nilikuwa sina jinsi ilinibidi nikile hivyo hivyo kusitili
njaa niliyokuwa nayo ambayo ilianza kuonesha
uwepo wake tumboni kwangu, nilikifakamia kisha
nikashushia na maji ambao yalishuka vyema kooni
mwangu, pale pale nikajilaza kwenye kochi baada
ya kushika, shide na mchoko wa siku hiyo vilifanya
nilale kochini.
Ilipita wiki moja sikuwa na tofauti yoyote mwilini
mwangu, nilijiamini zaidi kwa vile nilijua sina
taswira ile ya pake, nilijawa na amani tele tele,
niliamua niende kijijini kule nilipokuwa naishi
mwanzo nilikumbuka mazingira yale hasa kule
nilipokuwa naishi na bibi ndio kulinisukuma zaidi
kwenda, hivyo sikuwa na jinsi japo uchawi nilionao
ungeniwezesha kufika tena haraka ila sikutaka
kufanya hivyo nilitamani nitumie usafiri wa kawaida
kama watu wengine, nilielekea ubungo asubuhi ya
siku nyengine nikachukua usafiri magari ya kwenda
kule yalikuwa ni ya mapema zaidi, pia sikutaka
kucherewa kufika ndio mana nikapanda za mapema,
gari ilianza safari yake tukiliacha jiji la Dar tulikuwa
tukielekea mbeya japo kijiji sikuwa nikikijua ila
niliamua nipande gari ili nikifika mbeya mjini basi
nitumie uchawi kufika huko, nikiwa nimekaa kwenye
siti mtu ambaye nilikuwa nae siti moja sikuwa
nikimuelewa hata kidogo, alionekana mwenye
mashaka huku akiniangalia kila saa kama vile
alikuwa akinifahamu, mara kadhaa nilimuona
akiniangalia kwa kustuka stuka.
“Wee kaka vipi?” nilimuuliza.
“A a a a a a a hamna mbona,”
“Mbona unawasi wasi kwani tatizo nini?” nilimuuliza
tena.
“Hakuna chochote dada niko sawa tu,” alijibu,
baada ya kujibu hivyo sikuongea nae tena nilitulia
nikichezea simu yangu ambayo wakati huo nilikuwa
nikiperuzi facebook nilijikita kusoma hadithi, hadithi
ambayo ilikuwa imeandikwa na Gao sijui mnamjua
ilikuwa inaitwa MAUMIVU YA JUMLA ilikuwa hadithi
nzuri ikizungumzia mahusiano yalivyoondoka na uhai
wa watu wawili, ngoja nisikuelezee sana ukipenda
utaitafuta mwenyewe, hadithi ile ilisindikiza safari
yangu ambayo njia nzima nilijikita kuisoma zaidi,
tulifika hotelini hapo watu walishuka kupata chakula
ila mimi sikushuka nilibaki ndani ya gari nikanunua
juu juu, masaa yalisogea mpaka inafika usiku ndio
tukaingia mbeya mjini kwa vile ni usiku ilinibidi
nilale kwenye vyumba vya wageni kwa vile
nilipotaka kwenda sikuwa nikipajua hivyo nilihitaji
muda zaidi wa kutulia ili kesho niweze kwenda
huko.
Ilikuwa hotel nzuri ambayo ilinihudumia vyema kwa
matakwa yangu kila nilichoagiza nilikipata,usiku huu
nilihisi upweke kukaa ndani peke yangu hivyo
ikanibidi niingie mtaani kujichanganya kidogo na
watu, nilipita mitaa kadhaa ya mji wa mbeya
niliuona utauti, utofauti na jiji la dar watu wambea
walikuwa wakipenda sana burudani nilishuhudia bar
kadha zikiwa zimejaa huku watu wakishangilia mpira
japo sikuwa mpenzi wa mpira ila shangwe na kelele
zao zilinivuta sehemu ile na mimi nikakaa
nikiangalia mpira ilikuwa timu inayovaa jezi
nyekundi na jezi za blue sikuzijua kwavile sikuwa
mpenzi wa mpira, nilikaa sehemu na kunywa kiasi
kisha nilipojihisi kutosheka ikanibidi niondoke
kurudi kwenye hotel niliyochukua mwanzo, nilipofika
niliingia na kupumzika usiku huo.
Hatimaye kulikucha siku ilibadilika nilifika yalipo
mapokezi nikakabidi chumba kisha baada ya kupata
kifungua kinywa asubuhi hiyo, nilipotoka pale
ilinibidi nitembee kidogo kisha nikafika
sehemumbayo ilikuwa na mti mkubwa ambao
haukuwa na jani lolote ulionekana umekauka ila
ulikuwa mbichi kabisa mbali na kutokuwa na jani
lolote. Nilitumia sehemu ile kupotea, kweli nilipotea
kisha nikatokea sehemu nyengine ambayo ndio
nilihisi kipindi kile ndipo nilipouwa nikiishi,
hapakuwa kama nilivyodhania kulikuwa na majani
wala dalili ya kuwa na nyumba hazikuwepo kabisa,
nilijaribu kutembea sehemu kadhaa ila kulikuwa vile
vile nilianza kuhisi labda nimeenda sehemu ambayo
sio, sikutilia manani pia sikuwa na chengine niliona
ni bora nirudi nyumbani, wakati huu sikutaka
kupanda gari niliona nitapoteza muda hivyo, niliamua
kurahisisha safari kwa vile nilijua nikisema mchana
huu nitumie uchawi kurudi nyumbani naweza
kukwama sehemu hivyo niliona ni bora nipotee
kisha nitokee mikumi ambako ndio nitapanda gari
kurudi dar, kilikuwa kitendo cha dakika kumi nilifika
stand ya mikumi morogoro, niliwahi magari
yatokayo mbeya nikapanda. Kuna muda uchawi
unarahisisha maisha ila hauna faida yoyote, hakuna
mtu aliepata utajiri kwa kutumia uchawi,wachawi
wengi hawanaga maendeleo kazi kubwa ni
kurudisha watu nyuma japo mimi ni mchawi ila sijui
hata manufaa ya kuwa mchawi japo unanirahisishia
baadhi ya vitu ila maendeleo hakuna.
Safari ya kutoka morogoro tulitumia karibuia saa
sita ndio tuliingia dar, nilishuka ndani ya gari kisha
nikapanda mwendo kasi ambao ulinishusha
manzese argentina na safari ya kwenda kwangu
ikaanza nilitembea m kadhaa mpaka nikafika.
“Mwanangu upo,”
“Nipo mama sijui wewe,”
“huonekani mwanangu sijakuona muda,”
“nipo mama mihangaiko tu,”
“Haya unatoka wapi mana hatuagani,” alikuwa ni
yule mama.
“Nilikuwa kwa rafiki yangu” nilimjibu.
“Juzi sijui jana sijui lini ile,”aliongea kwa kubabaika
babaila wambea utawajua tu.
“lini na kuna nini?”na mimi nilimuuliza nikitaka
kujua.
“Nimesahau siku, ila ulikuwa ni wewe unapita
nilisikia wakikucheka wenzio,”alisema.
“Haya walicheka nini?”
“Mi nadhani tuingie ndani tukaongee kuliko kuongea
hapa nje,” aliposema hivyo nilimkubalia nilikuwa na
shauku ya kujua sababu ya vicheko vile vya
wapangaji wenzangu, nilifungua mlango kisha
tukaingia ndani. “Eheee nambie,” nilimwambia.
“Sasa ni hivi KIDAWA wenzako pale niliwasikia
wakihadithiana eti wewe mchawi,”
“Mchawi?,”
“Ndio walikuwa wakisema kila mmoja akisema lake
wengine wakisema wewe unajiuza,” maneno ya
mama huyu yaliniumiza zaidi niliuhisi uchungu
kumbe vicheko vile walikuwa wakiniteta mimi,
tuliongea kidogo kisha akaondoka hapo nikabaki
mwenyewe, huwa sipendi kulala na jambo nilipanga
siku hii hii niwatembelee mmoja mmoja.
Japo nilitamani kuwashughulikia ila mwili ulinisaliti
nilishindwa kuamka siku hii mpaka kunakucha
sijaenda popotiliumia sana kuona sijawafundisha
adabu kwa kunifatilia na kuniteta kisha kunicheka,
CHUMA CHAO KIPO MOTONI nilijiapiza kisha
nikaamka ili nikaoge kwa vile mwili wangu usiku
sikuweza kuoga niliamka na kuangalia maji looh
sikuwa na maji ndani, maji yote tayari yaliisha
sikuwa na jinsi nilitoka nje lengo ni kuomba kwa
yule mama nilipotoka nilimuona moja ya wapangaji
wenzangu tena aliponiona alisonya na kuninyari,
sikumjali kwa vile nilijua nitakachomfanyia
hataamini, ‘Njiwa wa kwako manati ya nini, endelea
kuninyari dada’ nilijisehemua kimoyo moyo mama
yule alitoka kisha nikamuomba maji mama wawatu
hakusita alinitolea dumu zima huku akisema kuwa
nitoe madumu yangu nje ili anijazie maji, nyumba
hii ilikuwa na bomba ila ni la nje tu chooni
halikuwepo.
Baada ya kupewa maji yale nilichukua sabuni na
mswaki wangu kwa ajili ya kwenda kujiswafi,
nilikuwa nimevalia taulo, nilianza kuoga kasheshe
ilitokea wakati nikipaka sabuni sijui nilikuwa na
mkosi gani wakati napaka sabuni miguuni
nilijistukia nimekata ile kamba ambayo nilipewa
kwa ajili ya kutokugeuka paka mchana, nilishikwa
na butwaa sikuamini nilitizama chini kukiangalia ili
nikiokote nijaribu kukiunga tena, looh kinapatikana
wapi? tayari kilisha potea,wakati nikiwa kwenye
butwaa ya kutokuona kikamba kile cha mguuni,
hapo hapo sikutegemea pale umbo langu
lilipobadirika na kugeuka paka tena wakati huu
mweupe, tofauti na yule wa kwenye picha ambae
alikuwa mweusi..
 
SEHEMU YA 20
NA Gaooh TheAuthor
Simu=0654387935
TULIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
sikuamini nilitizama chini kukiangalia ili nikiokote
nijaribu kukiunga tena, looh kinapatikana wapi?
tayari kilisha potea,wakati nikiwa kwenye butwaa ya
kutokuona kikamba kile cha mguuni, hapo hapo
sikutegemea pale umbo langu lilipobadirika na
kugeuka paka tena wakati huu mweupe, tofauti na
yule wa kwenye picha ambae alikuwa mweusi..
SASA TUENDELEEEEE.
Nilijilaumu hata pale nilipotoa sauti ilisikikka sauti
ya paka ‘Nitatokaje’ndio swali niliojiuliza wakati huo
nilisogea pembeni nikiitizama ndoo ambayo ilikuwa
na maji ndani yake kwa ajili ya kuoga mimi.
Nikiwa ndani ya bafu nilisikia sauti nje wakiulizana
kama nimetoka, ‘nikiondoka humu bafuni mlango
ukiwa umefungwa, wapangaji wenzangu wataingiaje’
ni maswali tu pekee ndio nilikuwa najiuliza wakati
huo LIWALO NA LIWE niliwaza kisha nikatoweka
bafuni mule kisha kurudi ndani kwangu,Udogo wa
umbo la mnyama paka sikuweza kufanya chochote
hata kupika sikuweza, kufungua friji sikuweza
nilichofanya ni kulala tu kitandani kwangu.
Siku hii ilikuwa ndefu sana, nilitamani iishe haraka
haraka usiku ufike ila haikuwa hivyo, njaa
iliniandama kitu cha kula wakati huo sikukijua, hata
nilipotamani nitoweke mpaka sehemu yenye vyakula
niliogopa nilihofia usalama wangu pengine
ningeenda likatokea la kutokewa.
Nilikuwa nikihesabu masaa tu, nilianza
nne,tano,sita,saba,nane,tisa, kumi mpka imefika saa
kumi na mbili hapo kidogo tabasamu lilijengeka
usoni kwangu nilianza kutabasamu nikifurahia
kukaribia kwa giza ili nirudi kwenye umbo langu la
kawaida, mbali na kuisubiri kwa hamu jioni hii ila
nayo ilinihadaa eti, ilikuwa kama imesimama giza
halikuonekana dakika zake zilisogea taratiibu sana,
nilihisi kuchoka hata ile furaha ilipote hasira
zilinivaa, nilianza kupingana na hali niliyokuwa nayo
njaa ilinisukuma subira ilinichosha, hapo ndipo
nikakumbuka kuwa sikuhizi yule subira ameacha
kuvuta heri, ameanza kuvuta bangi hivyo hakunifaa
nilichofanya nilisogea lilipo friji langu kisha
nikapanda juu yake kwa kuruka hapo nikaingiza
mguu kwenye kitobo ambacho ndipo watu hutumia
kuweka mkono pale wanapofungua friji, wenzangu
mnatumia mikono eti mimi nikaweka mguu kama
mbadala wa mkono Lengo na Madhumuni eti
nifungue friji nitoe chakula kilichopo humo,
nilihangaika kwa muda bila matumaini hakuna
nilichopata zaidi ya kuchoka hata mguu ulianza
kuniuma hapo nikamua eti na mimi nitumie sasa
mkono kama binadamu wa kawaida ‘teh,the,the’
kitendo cha kujigeuza hapo ikawa kama kosa
niliparamia glasi ya maji ambayi ilikuwa juu ya
friji,glasi hakuweza kuhimili hapo ilianguka chini na
kuvunjika,kuvunjika kwake niliona kama kwa tofauti
kwani nilihisi kama inanicheka kutokana na sauti
iliyovunjika nayo, nikasonya kisha kushuka juu ya
friji wakati huu kiza kilianza kumea ndipo nikajiweka
juu ya kitanda nikisubiri mwili wangu urejee.
Hakiamungu nilihisi wazimu, muda ulizidi kusogea
nikiwa vile vile mwili wangu haukurudi eti,hapo
ikanibidi nitoweke ndani kwangu kwenda kutafuta
chakula njaa ilinikaba koo, nilitokea karibu na
sehemu ya mama muuza supu anapofanyia biashara
yake nikitegemea nitapata mafupa ambayo wateja
wake watakuwa wakiangusha na kuyatupa, nilikaa
pembeni nikisubiri ila haikuwa vile nilivyotaka
hakuna kilichotupwa hapo ikabidi nijisogeze karibu
ya pale, sikuwa nikijua kitakachonikuta kwani pale
pale nilipokea jiwe ambalo lilinipiga mgongoni
kwangu sawia, “wauuuuuuhhh’ nilitoka sauti ya
maumivu huku mbio nazo zilinitoka,japo halikuwa
jiwe kubwa ila nilihisi maumivu ambayo ndio ikawa
sababu ya kuondoka sehemu ile kabisa.
Nilizunguka mitaani nikitafuta chakula, hapo
niliokotea okoteza kila nikionacho kusitili njaa
yangu,baada ya kutosheka na maokotezo hapo
ikabidi nirudi nyumbani kutafakari cha
kufanya,haikunichukua muda tayari nilishafika
nyumbani kulikuwa kimya na giza vile vile.
Nilijutia uchawi, sikuwahi kujua kama itafika siku na
mimi nitaishi katika umbile hili la mnyama ambaye
ni paka,Jambo hili liliniumiza zaidi niliwaza wakati
huu jambo amablo nitafanya ili niachane na uchawi,
niliwaza sikuwa na jibu pia nakumbuka kwenye
moja ya viapo vyetu ni kuwa uchawi hatuwezi
kuacha ni kama vile ndoa ya kikristo yani utaishi
ukiutumikia mpaka kifo ndio kikutengenishe nao na
hata ukiamua kujitoa basi kuna mawili kama si kifo
basi ni matatizo japo wachawi wengine wanajitoa
bila vikwazo ila huu wa kwetu sio rahisi kujitia
usipokufa basi utapata malipo,malipo ambayo
utawalipia wale uliowauwa wote.
Nilitafakari jambo hili ila sauti kubwa ilinijia
kichwani, ikisema LIWALO NA LIWE, japo sauti hii
haikuwahi kunisaliti mara nyingi ilikuwa ikinijia
ikitaka nifanye maamuzi magumu.
Nilibaki na jambo hili akilini hapo ikabidi niondoke
nyumbani kwangu na kuanza maisha ya kuishi
msituni nikijilia panya kama kitoweo changu,
nilianza kumaliza siku mpaka ikafika wiki niliishi
kwa tabu maisha yale ya kulala vichakani hali ile
iliendelea kiasi kwamba hata nguvu zangu sikuwa
nazo tena, ni kwamba hata ule uchawi uliondoka ule
uwezo wa kupotea na kutokea ninapotaka sikuwa
nao tena, nilianza maisha mapya kama mnyama wa
porini looh.
Maisha haya yalinifunza kitu, niliiona ile tabu
wanayopata wanyama wa porini zile purukushani za
kukimbia nyoka na wanyama wakali wanaopenda
kula wenzao ndio zilianza na mimi kuniandama,
mara kadhaa nilitishika na nyoka waliotaka
kunifanya kitoweo adha hizi ndio zilifanya nihisi
uchungu na kuona tabu wapitiazo wanyama wadogo
wa msituni.
Siku zilizidi kusogea bila ya kupata tumaini lolote,
mpaka nikaanza kuizoea hali ile hapo nikajikubali tu
na kuanza kutafuta makazi mapya purukushani za
msituni zilinichosha hivyo niliamua nitembee umbali
mrefu mpaka nikute makazi ya binadamu ambapo
nitaweza kuishi vizuri bila hatari yoyote ile ya
kuangamizwa japo binadamu nao wanaubaya wao.
Safari yangu ilikuwa ndefu, sikupata tumaini la
kufika kule nilipodhamiria nilijiona nikitembea na
kiza safari yangu ilikuwa ndefu mpaka asubuhi bado
sikuwa nimefika mjini, nilipumzika kwa muda
nikivuta pumzi ya kuendelea na safari, baada ya
dakika kadhaa au ya muda kadhaa hapo nilianza
safari yangu tena.
Nilihisi kuchoka ila ilinibidi niendelee na safari
yangu, nikiwa safarini kelele za watu pamoja na
sauti za wanyama zilinipokea nilianza kusikia, hapo
kidogo nilipata tumaini, tumaini jipya la kuwa
nakaribia makazi ya watu nilizidi kukazana tena
wakati huu nilikimbia ili nifike kwa wakati looh! cha
ajabu sauti zile hazikuwa zikifikika yani kila
ninapojitahidi nifike ndio nazo zinazidi kusogea
mbali nami NILICHOKA nikasimama..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom