Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 20
"Kifo chako," Chonde alimjibu kijeuri. "Siwapendi vijana watundu kama wewe. Kufa, huna budi.”
"Kosa langu."
"Unapenda kufa?"
Joram alifikiri kwa makini angefanya nini kuiahirisha hukumu hiyo ya kifo. Muda. Alihitaji muda ili ikiwezekana itokee njia moja au nyingine ya kuyaokoa maisha yake. Akaanza maongezi kwa sauti ambayo aliifanya dhaifu kuliko ilivyokuwa, akimwuliza Chonde hili na lile. Chonde alikuwa mgumu wa kutoa habari kama jabali. Kati ya maneno ya kashfa na matusi kwa Joram, nchi na bara zima hakutamka neno lolote ambalo lilimfanya Joram amjue yeye ni nani na anafanya nini katika ulimwengu wa ujasusi. Alichoambulia ni zile hisia tu kwamba Chonde hakuwa raia wa kawaida.
"Umeahirisha sana kifo chako," Chonde alisema baadaye kama aliyekuwa akizisoma fikra za Joram. “Sasa iliyobaki ni kazi ndogo ya kukutoa uhai. Nitakuua kwa mkono wangu wa kushoto. Maiti yako itaokotwa kesho ikiwa imevunjikavunjika kama mtu aliyeanguka toka ghorofani. Kwa jinsi ulivyobadilika kitabia watu hawatashangaa kusikia kuwa umejirusha dirishani.”
Baada ya maneno hayo, aliinuka na kumwendea tena Joram kwa utulivu kama awali, lakini macho yake yalitangaza kitu kimoja tu, kifo.
Joram alijiandaa, akijua kuwa vita vilivyokuwa mbele yake vilikuwa vikubwa kuliko vyote alivyowahi kupambana navyo, vita vya kuitetea roho yake. Akaikusanya akili yake yote na kumsubiri Chonde kishujaa.
Mara mlango ukagongwa.
Chonde aligutuka kwa mshangao na kuutazama mlango huo. Joram hakuipoteza nafasi hiyo. Aliruka na kuufanya mguu wake utue katika shingo ya Chonde. Lilikuwa pigo ambalo Chonde hakulitegemea. Likamtia mweleka. Lakini pigo la pili alilitegemea, akalikwepa na kuachia judo ambayo Joram aliikinga. Papo hapo mlango ukagongwa tena na kufunguka ukiruhusu sura ya msichana mzuri kuingia.
Alikuwa yule msichana wa mapokezi wa hoteli ya Embassy. Alitokwa na macho ya mshangao kuona miili yenye jasho, michubuko na damu, ya wanaume hao, ikiwa tayari kuvamiana. Wote walimtazama msichana huyo, Chonde akimlaani, Joram akimshukuru. Akiwa kama hajui lipi la kufanya msichana huyo aliduwaa mlangoni, Mdomo wazi.
"Kifo chako," Chonde alimjibu kijeuri. "Siwapendi vijana watundu kama wewe. Kufa, huna budi.”
"Kosa langu."
"Unapenda kufa?"
Joram alifikiri kwa makini angefanya nini kuiahirisha hukumu hiyo ya kifo. Muda. Alihitaji muda ili ikiwezekana itokee njia moja au nyingine ya kuyaokoa maisha yake. Akaanza maongezi kwa sauti ambayo aliifanya dhaifu kuliko ilivyokuwa, akimwuliza Chonde hili na lile. Chonde alikuwa mgumu wa kutoa habari kama jabali. Kati ya maneno ya kashfa na matusi kwa Joram, nchi na bara zima hakutamka neno lolote ambalo lilimfanya Joram amjue yeye ni nani na anafanya nini katika ulimwengu wa ujasusi. Alichoambulia ni zile hisia tu kwamba Chonde hakuwa raia wa kawaida.
"Umeahirisha sana kifo chako," Chonde alisema baadaye kama aliyekuwa akizisoma fikra za Joram. “Sasa iliyobaki ni kazi ndogo ya kukutoa uhai. Nitakuua kwa mkono wangu wa kushoto. Maiti yako itaokotwa kesho ikiwa imevunjikavunjika kama mtu aliyeanguka toka ghorofani. Kwa jinsi ulivyobadilika kitabia watu hawatashangaa kusikia kuwa umejirusha dirishani.”
Baada ya maneno hayo, aliinuka na kumwendea tena Joram kwa utulivu kama awali, lakini macho yake yalitangaza kitu kimoja tu, kifo.
Joram alijiandaa, akijua kuwa vita vilivyokuwa mbele yake vilikuwa vikubwa kuliko vyote alivyowahi kupambana navyo, vita vya kuitetea roho yake. Akaikusanya akili yake yote na kumsubiri Chonde kishujaa.
Mara mlango ukagongwa.
Chonde aligutuka kwa mshangao na kuutazama mlango huo. Joram hakuipoteza nafasi hiyo. Aliruka na kuufanya mguu wake utue katika shingo ya Chonde. Lilikuwa pigo ambalo Chonde hakulitegemea. Likamtia mweleka. Lakini pigo la pili alilitegemea, akalikwepa na kuachia judo ambayo Joram aliikinga. Papo hapo mlango ukagongwa tena na kufunguka ukiruhusu sura ya msichana mzuri kuingia.
Alikuwa yule msichana wa mapokezi wa hoteli ya Embassy. Alitokwa na macho ya mshangao kuona miili yenye jasho, michubuko na damu, ya wanaume hao, ikiwa tayari kuvamiana. Wote walimtazama msichana huyo, Chonde akimlaani, Joram akimshukuru. Akiwa kama hajui lipi la kufanya msichana huyo aliduwaa mlangoni, Mdomo wazi.