Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 41 & 42
kuvutia kila macho ya mwanamume. Kwa hiyo, tafadhali leo pitapita madukani ununue kila vazi ambalo litakustahili. Usijali bei. Kumbuka pesa tunayo."
Nuru alizipokea na kumuuliza, "Na wewe huhitaji nguo mpya?"
"Nahitaji. Hata hivyo, sina haraka. Wanaume huwa hawatazamwitazamwi kama wanawake."
"Najua unahitaji muda wa kuwa peke yako," Nuru alimwambia. "Endelea baba, siwezi kukuzuia."
Mara tu Nuru alipoondokaJoram aliingia kazini. Alifungua begi lake na kutoa nyaraka za Chonde ambazo alitumia kila njia, kuzielewa. Akatoa kitabu ambacho alikipata kwa taabu sana kinachoeleza mbinu mbalimbali za kusoma maandishi ya mafumbo.
Akaketi na kuanza kutumia kitabu hicho kuyasoma tena maandishi ya Chonde. Haikuwa kazi ndogo. Ilihitaji muda mrefu na utulivu mkubwa. Alichofanikiwa ni kupata mwongozo ambao ulieleza namna ya kukifungua kile kisanduku. Akakifungua bila tabu yoyote.
Ndani mlikuwa na vijigololi kumi na viwili. Joram alikiinua kimoja na kukitazama kwa makini. Katikati ya kigololi aliona vidude vilivyokuwa vikichezacheza mfano wa saa za electronic. Alikitazama kigololi kwa makini akijaribu kutafuta umuhimu wake, hakuupata. Chini ya vigololi hivyo Joram alipata ramani ambayo alipoikunjua alikuta kuwa ni ya Jiji la Dar es Salaam. Ramani hiyo ilionyesha majengo maarufu kama Ikulu, vituo vya kijeshi, mabenki, na kadhalika. Vitu vyote hivyo vilikuwa vimewekewa namba za kirumi kuanzia moja na kuendelea. Namba ya jengo la benki kuu iliyoungua ilikuwa imewekewa alama ya x kwa wino mwekundu.
Mara baada ya kuona hayo Joram alipatwa na wasiwasi. Alihisi kuwa, kwa namna moja ama nyingine, Chonde alihusika na moto ulioteketeza Benki Kuu. Hofu yake kubwa ilikuwa zile hisia kuwa alama zilizofuata ambazo zilikuwa hazijawekwa x kwa wino mwekundu zilikuwa katika orodha zikisubiri, jambo ambalo lingeleta maafa na madhara makubwa kwa nchi na wananchi. Zaidi, ingekuwa ushindi mkubwa kwa maadui wa taifa. Hivyo, kwa mara nyingine, alifanya sherehe moyoni kushangilia kifo cha Chonde.
Kisha alifunga sanduku hilo kikamilifu na kuirudia meza ambayo aliinamia na kuanza kujifunza tena mbinu za kuyasoma maandishi hayo kwa makini zaidi.
Alikuwa hajatulia vizuri mlango ulipofunguka ghafla na Nuru kuingia huku macho yake yakiwa mekundu kwa mchanganyiko wa hasira na mshangao. Alisimama akitweta na kumtazama Joram kwa namna ya mtu ambaye hakujua la kusema.
"Usiniambie kuwa kuna mtu aliyekuvamia kwa nia ya kukunajisi mchana wote huu," Joram alimwambia kwa dhamira ya kumfariji.
"Acha mzaha Joram. Sikutegemea kama ungekuwa mtu wa kufanya kitendo kama kile."
Joram aliinua uso wake kumtazama.
"Kufanya nini?"
"Kuiba".
"Kuiba?"
Nuru akamkazia jicho la hasira. "Usijifanye hufahamu. Dunia nzima sasa inafahamu. Kwa kweli, sikutegemea kabisa. Imenishangaza kukuona katika televisheni ukitangazwa kama mtu hatari ambaye ameweza kuiba fedha za kigeni ambazo nchi yake inazitegemea kama dawa." Akasita akamtazama kwa chuki ambayo ilichanganyika na mshangao, "Kwanini ulifanya hivyo, Joram?"
***
"Bado siamini kama amefanya hivyo," mtu mmoja alikuwa akifoka pia, akiwa kaketi katika kundi la watu wenye hasira na mshangao kama yeye. Mabega yao yalikuwa yakimeremeta kwa nyota ambazo zilipamba magwanda yao kudhihirisha madaraka yao.
"Amefanya, lakini siamini kama Joram ni mtu wa kutenda kitendo cha aibu kama hiki. Jambo la kusikitisha zaidi ni jinsi habari hiii ilivyovuja kiasi cha kuyafikia masikio ya adui zetu. Leo nimesikia habari hizo na Afrika Kusini," Kombora aliendelea kulalamika.
"Ujerumani pia imetangaza afande," mtu mmoja aliongeza.
"BBC vilevile," mwingine aliongeza.
"Unaona, basi? Unaona habari mbaya zinavyosafiri upesiupesi? Pamoja na kwamba Joram ametuasi kimsimamo tulikuwa na haki ya kumsetiri kwasababu ya vitendo vyake vya nyuma. Sasa nadhani hatuna tunachoweza kufanya. Maji yamekwishakumwagika, hayazoleki. Lililopo ni kutafuta uwezekano wa kumpata na kurudisha pesa zote, hasa za kigeni."
"Hilo ndio tatizo mzee," msaidizi wake mmoja alijibu. "Taarifa za mwisho zinathibitisha kuwa hayupo kabisa hapa nchini. Kuna dalili kuwa ametorokea nchi jirani kwa ndege ya kukodi."
"Lazima, lazima apatikane," Kombora alisisitiza. "Pesa alizochukua ni nyingi sana na zinahitajika sana. Hana haki ya kuzifuja kwa starehe zake binafsi. Wasiliana na nchi jirani zote. Wasiliana na Interpol. Waarifu kuwa tunamhitaji Joram kwa hali na mali. Maadamu siri imekwishafichuka, hakuna haja ya siri tena."
kuvutia kila macho ya mwanamume. Kwa hiyo, tafadhali leo pitapita madukani ununue kila vazi ambalo litakustahili. Usijali bei. Kumbuka pesa tunayo."
Nuru alizipokea na kumuuliza, "Na wewe huhitaji nguo mpya?"
"Nahitaji. Hata hivyo, sina haraka. Wanaume huwa hawatazamwitazamwi kama wanawake."
"Najua unahitaji muda wa kuwa peke yako," Nuru alimwambia. "Endelea baba, siwezi kukuzuia."
Mara tu Nuru alipoondokaJoram aliingia kazini. Alifungua begi lake na kutoa nyaraka za Chonde ambazo alitumia kila njia, kuzielewa. Akatoa kitabu ambacho alikipata kwa taabu sana kinachoeleza mbinu mbalimbali za kusoma maandishi ya mafumbo.
Akaketi na kuanza kutumia kitabu hicho kuyasoma tena maandishi ya Chonde. Haikuwa kazi ndogo. Ilihitaji muda mrefu na utulivu mkubwa. Alichofanikiwa ni kupata mwongozo ambao ulieleza namna ya kukifungua kile kisanduku. Akakifungua bila tabu yoyote.
Ndani mlikuwa na vijigololi kumi na viwili. Joram alikiinua kimoja na kukitazama kwa makini. Katikati ya kigololi aliona vidude vilivyokuwa vikichezacheza mfano wa saa za electronic. Alikitazama kigololi kwa makini akijaribu kutafuta umuhimu wake, hakuupata. Chini ya vigololi hivyo Joram alipata ramani ambayo alipoikunjua alikuta kuwa ni ya Jiji la Dar es Salaam. Ramani hiyo ilionyesha majengo maarufu kama Ikulu, vituo vya kijeshi, mabenki, na kadhalika. Vitu vyote hivyo vilikuwa vimewekewa namba za kirumi kuanzia moja na kuendelea. Namba ya jengo la benki kuu iliyoungua ilikuwa imewekewa alama ya x kwa wino mwekundu.
Mara baada ya kuona hayo Joram alipatwa na wasiwasi. Alihisi kuwa, kwa namna moja ama nyingine, Chonde alihusika na moto ulioteketeza Benki Kuu. Hofu yake kubwa ilikuwa zile hisia kuwa alama zilizofuata ambazo zilikuwa hazijawekwa x kwa wino mwekundu zilikuwa katika orodha zikisubiri, jambo ambalo lingeleta maafa na madhara makubwa kwa nchi na wananchi. Zaidi, ingekuwa ushindi mkubwa kwa maadui wa taifa. Hivyo, kwa mara nyingine, alifanya sherehe moyoni kushangilia kifo cha Chonde.
Kisha alifunga sanduku hilo kikamilifu na kuirudia meza ambayo aliinamia na kuanza kujifunza tena mbinu za kuyasoma maandishi hayo kwa makini zaidi.
Alikuwa hajatulia vizuri mlango ulipofunguka ghafla na Nuru kuingia huku macho yake yakiwa mekundu kwa mchanganyiko wa hasira na mshangao. Alisimama akitweta na kumtazama Joram kwa namna ya mtu ambaye hakujua la kusema.
"Usiniambie kuwa kuna mtu aliyekuvamia kwa nia ya kukunajisi mchana wote huu," Joram alimwambia kwa dhamira ya kumfariji.
"Acha mzaha Joram. Sikutegemea kama ungekuwa mtu wa kufanya kitendo kama kile."
Joram aliinua uso wake kumtazama.
"Kufanya nini?"
"Kuiba".
"Kuiba?"
Nuru akamkazia jicho la hasira. "Usijifanye hufahamu. Dunia nzima sasa inafahamu. Kwa kweli, sikutegemea kabisa. Imenishangaza kukuona katika televisheni ukitangazwa kama mtu hatari ambaye ameweza kuiba fedha za kigeni ambazo nchi yake inazitegemea kama dawa." Akasita akamtazama kwa chuki ambayo ilichanganyika na mshangao, "Kwanini ulifanya hivyo, Joram?"
***
"Bado siamini kama amefanya hivyo," mtu mmoja alikuwa akifoka pia, akiwa kaketi katika kundi la watu wenye hasira na mshangao kama yeye. Mabega yao yalikuwa yakimeremeta kwa nyota ambazo zilipamba magwanda yao kudhihirisha madaraka yao.
"Amefanya, lakini siamini kama Joram ni mtu wa kutenda kitendo cha aibu kama hiki. Jambo la kusikitisha zaidi ni jinsi habari hiii ilivyovuja kiasi cha kuyafikia masikio ya adui zetu. Leo nimesikia habari hizo na Afrika Kusini," Kombora aliendelea kulalamika.
"Ujerumani pia imetangaza afande," mtu mmoja aliongeza.
"BBC vilevile," mwingine aliongeza.
"Unaona, basi? Unaona habari mbaya zinavyosafiri upesiupesi? Pamoja na kwamba Joram ametuasi kimsimamo tulikuwa na haki ya kumsetiri kwasababu ya vitendo vyake vya nyuma. Sasa nadhani hatuna tunachoweza kufanya. Maji yamekwishakumwagika, hayazoleki. Lililopo ni kutafuta uwezekano wa kumpata na kurudisha pesa zote, hasa za kigeni."
"Hilo ndio tatizo mzee," msaidizi wake mmoja alijibu. "Taarifa za mwisho zinathibitisha kuwa hayupo kabisa hapa nchini. Kuna dalili kuwa ametorokea nchi jirani kwa ndege ya kukodi."
"Lazima, lazima apatikane," Kombora alisisitiza. "Pesa alizochukua ni nyingi sana na zinahitajika sana. Hana haki ya kuzifuja kwa starehe zake binafsi. Wasiliana na nchi jirani zote. Wasiliana na Interpol. Waarifu kuwa tunamhitaji Joram kwa hali na mali. Maadamu siri imekwishafichuka, hakuna haja ya siri tena."