Simulizi: Ulimwengu Ndotoni Mwangu

Simulizi: Ulimwengu Ndotoni Mwangu

Sehemu ya 19.

Kila mmoja alitaka kuona hayo maajabu ambayo Amon aliyazungumzia, walitaka kuona kama walikuwa na jipya jingine ama yalikuwa ni mahojiano tu.
Ni dakika ya tano tu, Amon alipewa pasi na namba nane yao aliyeitwa Innocent, aliipokea pasi ile, akageuka na kukutana na mabeki wawili mbele yake, akaanza kuwasogelea kwa kasi, alikuja beki wa kwanza, alichokifanya ni kumchezea mwili tu kwamba kama anakwenda kushoto, beki akalala kushoto na yeye kupita kulia.
Alipomuona beki mwingine anakuja, haraka akampigia pasi Gideon ambaye alisimama na kumtingisha beki mwingine, alipomuona ametingishika kama alivyotaka, akaubetua mpira kwa juu, ukaenda kwa Amon, akautuliza kifuani, beki wa kwanza alipomrudia, akampiga kanzu na kubaki yeye na golikipa tu.
Mashabiki wote walisimama kushudia kilichokuwa kinafiata. Alichokifanya ni kama Ronaldinho, alimpiga mkasi mmoja tu golikipa, akaelekea kulia na yeye kupita kushoto, akabaki yeye na goli, akafunga bao safi kabisa.
Mashabiki wakalipuka kwa shangwe, hawakuamini kumuona mtu akicheza namna ile, wale waliokuwa kwenye baa, hawakutaka kusubiri, kwa burudani ile moja tu hukutakiwa kuitazama mechi kwenye televisheni tu ulitakiwa kwenda uwanjani, wakachukua simu zao na kuanza kukata tiketi harakaharaka.
Kitu alichokifanya Amon ni kumkimbilia Gideon, akamkumbatia, akamuita Innocent na wachezaji wengine na kuanza kushangilia. Ilikuwa ni dakika ya tano tu lakini tayari watu waliona kulikuwa na balaa lililokuwa linafuata.
Kupitia bao hilo la kwanza, timu ya Schalke 04 ni kama walichanganyikiwa, huyo Amon alionekana kuwa msumali wa moto, alikuwa na kasi alipokuwa akienda kushambulia, alikuwa akipiga chenga za maudhi na alijua zaidi kuuficha mpira.
Yeye na Gideon walikuwa wakionana sana, walipigiana pasi na kuwasogelea maadui kwa kasi kubwa. Wala hazikuchukua dakika nyingi, ni dakika ya kumi tu, Amon akapewa pasi, alikuwa katikati ya uwanja, akaanza kuondoka na mpira ule, alichokuwa akikifanya ni kumpiga chenga kila mchezaji aliyekuwa akija.
Alipowapiga chenga wawili, akayainua macho yake, akamuona Gideon akikimbia mbele, akamwangalia beki mwingine, akamuona akiwa sawa na Gideon, haraka sana akaipiga pasi ndefu, ilipofika kwa Gideon, alipomuona beki anakuja wanguwangu, akaugusa kidogo tu, ukampiga tobo beki, akabaki yeye na kipa, hakutaka kumsogelea, akauinua mpira, lilikuwa moja ya tukio ambalo hata kipa hakulitegemea, akashtukia mpira ukipita juu yake na kwenda wavuni.
Lilikuwa bao maridadi la pili lililofungwa na kijana mwingine wa Kitanzania. Ilikuwa ni furaha kwa kila mmoja, kocha wao alibaki akishika kichwa, hakuamini kile alichokuwa akikiona, kilimshangaza na kilikuwa kitu ambacho hakukitarajia kabisa.
Wachezaji wale wawili walionekana kuwa nuksi, hawakuwa na masihara hata kidogo, mpaka mapumziko, tayari Schalke 04 walipigwa mabao matano huku matatu yakifungwa na Amon na mengine mawili yakifungwa na Gideon.
Ndani ya chumba cha kubadilishia nguo kila mmoja alikuwa akiwaangalia kwa mshangao. Wengi walikuwa na ndoto za kucheza na Messi, Ronaldo lakini watu hao wawili walionekana kuwa sawa na wachezaji hao, Gideon alikuwa na uwezo wa Ronaldo, Amon alikuwa na uwezo wa Messi, yaani walikuwa na maajabu makubwa.
“Kila mtu atavutiwa na timu hii, ni muda wa kuonyesha maajabu,” alisema Amon huku akimwangalia kocha wake.
Hatimaye baada ya dakika kadhaa wakarudi uwanjani, uwanja ulikaribia kujaa, mashabiki waliongezeka baada ya kuona kile kilichotokea, kila mmoja alionekana kuwa na furaha isiyo kifani.
Wakasahau kwamba wao ndiyo waliokuwa wakiwachukia wachezaji hao, walisahau kila maneno mabaya waliyokuwa wametamka kwao, kila mmoja muda huo alikuwa akiwapenda, na wengi wakaanza kuimba majina yao.
Kipindi cha pili kilianza, kilikuwa ni kipindi cha maajabu mengine, walipiga mpira ambao hapakuwa na mtu aliyeamini, walionekana kuwa mwiba mkali, kwenye kila pasi waliyokuwa wakipokea walionyesha maajabu makubwa, yaani mpaka mpira unamalizika, walishinda kwa mabao nane kwa sifuri, ushindi mkubwa sana kwao. Mabao manne yakifungwa na Amon, matatu na Gideon na moja na kiungo wao mshambuliaji, Merlin.
Mechi ilimalizika, wakatakiwa kuhojiwa lakini kocha alikataa, yeye aliwachagua wachezaji wengine wa kuzungumza na waandishi lakini si hao wawili. Kwa kile kilichotokea, hata mashabiki ambao hawakuiona hiyo mechi kutokana na ubize wa kazi, wakataka kuiona kwani waliyoyasikia yalikuwa mengi na makubwa mno.
Kila aliyeiona mechi ile, aliamini kulikuwa na mengi sana yaliyokuwa yakija mbele yao, hao walikuwa wachezaji wenye hatari sana, walikuwa msumali wa moto kwa timu nyingine.
Wakati hayo yakiwa yametokea, Anita hakuwa na habari, alikuwa na kazi zake nyingine, hakutaka kuangalia mechi hiyo kwa kuwa aliamini kabisa wachezaji hao wasingefanya kile alichokitarajia. Hakutaka kuwasiliana na mtu yeyote yule kuhusu mechi hiyo.
Alipoona mechi imekwisha, haraka sana akaingia kwenye mtandao wa Livescore kuangalia matokeo. Alichokiona hakuamini, timu yake ilishinda kwa mabao nane, akafungua kuona wafungaji, moyo wake ulikuwa na furaha tele. Huku akiwa hajui ni kwa namna gani alitakiwa kufurahia, ghafla akaona simu yake ikianza kuita, haraka sana akaangalia kioo, alikuwa baba yake, akaipokea.
“Hawa watu uliwatoa wapi?” lilikuwa swali la kwanza la baba yake baada ya kupokea simu.
“Najua unajua kila kitu baba!”
“Ni wachezaji ambao sikutarajia kuwaona! Uliiona hiyo mechi?”
“Hapana! Nilikuwa naogopa!”
“Hebu itazame inarudiwa baadaye! Hii ni pesa ndefu sana, hawa wachezaji ni hatari mno!” alisema baba yake, kama mfanyabiashara, alifikiria pesa tu.
Siku hiyo habari kubwa ikawa ni Amon na Gideon, walipewa sifa ya kila aina, hawakuvimba kichwa, walichowaambia wachezaji wenzao ni kwamba kulikuwa na mengi yajayo, waendelee kuvumiliana kwani bado hawakuwa kwenye ile fomu waliyoizoea kuwa nayo.
“Yaani hamkuwa kwenye fomu?” aliuliza mchezaji mmoja.
“Ndiyo! Ila tunavyoendelea kucheza, naona tutarudi kwenye fomu yetu,” alijibu Gideon, kila mmoja aliyesikia maneno hayo alishangaa, yaani hawakuwa kwenye fomu yao walicheza vile, je, wangekuwa kwenye fomu yao wangechezaje? Kila walilojiuliza, walikosa jibu.

Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 19.

Kila mmoja alitaka kuona hayo maajabu ambayo Amon aliyazungumzia, walitaka kuona kama walikuwa na jipya jingine ama yalikuwa ni mahojiano tu.
Ni dakika ya tano tu, Amon alipewa pasi na namba nane yao aliyeitwa Innocent, aliipokea pasi ile, akageuka na kukutana na mabeki wawili mbele yake, akaanza kuwasogelea kwa kasi, alikuja beki wa kwanza, alichokifanya ni kumchezea mwili tu kwamba kama anakwenda kushoto, beki akalala kushoto na yeye kupita kulia.
Alipomuona beki mwingine anakuja, haraka akampigia pasi Gideon ambaye alisimama na kumtingisha beki mwingine, alipomuona ametingishika kama alivyotaka, akaubetua mpira kwa juu, ukaenda kwa Amon, akautuliza kifuani, beki wa kwanza alipomrudia, akampiga kanzu na kubaki yeye na golikipa tu.
Mashabiki wote walisimama kushudia kilichokuwa kinafiata. Alichokifanya ni kama Ronaldinho, alimpiga mkasi mmoja tu golikipa, akaelekea kulia na yeye kupita kushoto, akabaki yeye na goli, akafunga bao safi kabisa.
Mashabiki wakalipuka kwa shangwe, hawakuamini kumuona mtu akicheza namna ile, wale waliokuwa kwenye baa, hawakutaka kusubiri, kwa burudani ile moja tu hukutakiwa kuitazama mechi kwenye televisheni tu ulitakiwa kwenda uwanjani, wakachukua simu zao na kuanza kukata tiketi harakaharaka.
Kitu alichokifanya Amon ni kumkimbilia Gideon, akamkumbatia, akamuita Innocent na wachezaji wengine na kuanza kushangilia. Ilikuwa ni dakika ya tano tu lakini tayari watu waliona kulikuwa na balaa lililokuwa linafuata.
Kupitia bao hilo la kwanza, timu ya Schalke 04 ni kama walichanganyikiwa, huyo Amon alionekana kuwa msumali wa moto, alikuwa na kasi alipokuwa akienda kushambulia, alikuwa akipiga chenga za maudhi na alijua zaidi kuuficha mpira.
Yeye na Gideon walikuwa wakionana sana, walipigiana pasi na kuwasogelea maadui kwa kasi kubwa. Wala hazikuchukua dakika nyingi, ni dakika ya kumi tu, Amon akapewa pasi, alikuwa katikati ya uwanja, akaanza kuondoka na mpira ule, alichokuwa akikifanya ni kumpiga chenga kila mchezaji aliyekuwa akija.
Alipowapiga chenga wawili, akayainua macho yake, akamuona Gideon akikimbia mbele, akamwangalia beki mwingine, akamuona akiwa sawa na Gideon, haraka sana akaipiga pasi ndefu, ilipofika kwa Gideon, alipomuona beki anakuja wanguwangu, akaugusa kidogo tu, ukampiga tobo beki, akabaki yeye na kipa, hakutaka kumsogelea, akauinua mpira, lilikuwa moja ya tukio ambalo hata kipa hakulitegemea, akashtukia mpira ukipita juu yake na kwenda wavuni.
Lilikuwa bao maridadi la pili lililofungwa na kijana mwingine wa Kitanzania. Ilikuwa ni furaha kwa kila mmoja, kocha wao alibaki akishika kichwa, hakuamini kile alichokuwa akikiona, kilimshangaza na kilikuwa kitu ambacho hakukitarajia kabisa.
Wachezaji wale wawili walionekana kuwa nuksi, hawakuwa na masihara hata kidogo, mpaka mapumziko, tayari Schalke 04 walipigwa mabao matano huku matatu yakifungwa na Amon na mengine mawili yakifungwa na Gideon.
Ndani ya chumba cha kubadilishia nguo kila mmoja alikuwa akiwaangalia kwa mshangao. Wengi walikuwa na ndoto za kucheza na Messi, Ronaldo lakini watu hao wawili walionekana kuwa sawa na wachezaji hao, Gideon alikuwa na uwezo wa Ronaldo, Amon alikuwa na uwezo wa Messi, yaani walikuwa na maajabu makubwa.
“Kila mtu atavutiwa na timu hii, ni muda wa kuonyesha maajabu,” alisema Amon huku akimwangalia kocha wake.
Hatimaye baada ya dakika kadhaa wakarudi uwanjani, uwanja ulikaribia kujaa, mashabiki waliongezeka baada ya kuona kile kilichotokea, kila mmoja alionekana kuwa na furaha isiyo kifani.
Wakasahau kwamba wao ndiyo waliokuwa wakiwachukia wachezaji hao, walisahau kila maneno mabaya waliyokuwa wametamka kwao, kila mmoja muda huo alikuwa akiwapenda, na wengi wakaanza kuimba majina yao.
Kipindi cha pili kilianza, kilikuwa ni kipindi cha maajabu mengine, walipiga mpira ambao hapakuwa na mtu aliyeamini, walionekana kuwa mwiba mkali, kwenye kila pasi waliyokuwa wakipokea walionyesha maajabu makubwa, yaani mpaka mpira unamalizika, walishinda kwa mabao nane kwa sifuri, ushindi mkubwa sana kwao. Mabao manne yakifungwa na Amon, matatu na Gideon na moja na kiungo wao mshambuliaji, Merlin.
Mechi ilimalizika, wakatakiwa kuhojiwa lakini kocha alikataa, yeye aliwachagua wachezaji wengine wa kuzungumza na waandishi lakini si hao wawili. Kwa kile kilichotokea, hata mashabiki ambao hawakuiona hiyo mechi kutokana na ubize wa kazi, wakataka kuiona kwani waliyoyasikia yalikuwa mengi na makubwa mno.
Kila aliyeiona mechi ile, aliamini kulikuwa na mengi sana yaliyokuwa yakija mbele yao, hao walikuwa wachezaji wenye hatari sana, walikuwa msumali wa moto kwa timu nyingine.
Wakati hayo yakiwa yametokea, Anita hakuwa na habari, alikuwa na kazi zake nyingine, hakutaka kuangalia mechi hiyo kwa kuwa aliamini kabisa wachezaji hao wasingefanya kile alichokitarajia. Hakutaka kuwasiliana na mtu yeyote yule kuhusu mechi hiyo.
Alipoona mechi imekwisha, haraka sana akaingia kwenye mtandao wa Livescore kuangalia matokeo. Alichokiona hakuamini, timu yake ilishinda kwa mabao nane, akafungua kuona wafungaji, moyo wake ulikuwa na furaha tele. Huku akiwa hajui ni kwa namna gani alitakiwa kufurahia, ghafla akaona simu yake ikianza kuita, haraka sana akaangalia kioo, alikuwa baba yake, akaipokea.
“Hawa watu uliwatoa wapi?” lilikuwa swali la kwanza la baba yake baada ya kupokea simu.
“Najua unajua kila kitu baba!”
“Ni wachezaji ambao sikutarajia kuwaona! Uliiona hiyo mechi?”
“Hapana! Nilikuwa naogopa!”
“Hebu itazame inarudiwa baadaye! Hii ni pesa ndefu sana, hawa wachezaji ni hatari mno!” alisema baba yake, kama mfanyabiashara, alifikiria pesa tu.
Siku hiyo habari kubwa ikawa ni Amon na Gideon, walipewa sifa ya kila aina, hawakuvimba kichwa, walichowaambia wachezaji wenzao ni kwamba kulikuwa na mengi yajayo, waendelee kuvumiliana kwani bado hawakuwa kwenye ile fomu waliyoizoea kuwa nayo.
“Yaani hamkuwa kwenye fomu?” aliuliza mchezaji mmoja.
“Ndiyo! Ila tunavyoendelea kucheza, naona tutarudi kwenye fomu yetu,” alijibu Gideon, kila mmoja aliyesikia maneno hayo alishangaa, yaani hawakuwa kwenye fomu yao walicheza vile, je, wangekuwa kwenye fomu yao wangechezaje? Kila walilojiuliza, walikosa jibu.

Je, nini kitaendelea?
Mambo ni noma sana
 
Sehemu ya 20

Miongoni mwa mashabiki wakubwa wa mchezo wa mpira nchini Ujerumani alikuwa rais wa nchi hiyo, Bwana Simon Berbeuz aliyekuwa akishabikia timu ya Bayern Munich.
Kwenye ndoto zake za kila siku alitamani sana kuona Timu ya Taifa ya Ujerumani ikifanya vizuri kuliko timu zote duniani. Hakutaka kuona taifa jingine likiwa mbele ya taifa hilo nguri la soka duniani.
Kipindi ambacho kulikuwa na mechi baina ya Hertha Berlin na Schalke 04 alitulia kwenye kiti chake na kuanza kutazama mechi hiyo. Ilipita miezi miwili ya mateso, mateso kwa kila mshabiki wa mpira kwa sababu timu zilikuwa mapumzikoni, hapakuwa na mechi nyingine yoyote kuanzia mwezi wa sita mpaka wa nane.
Kitendo cha mechi hiyo kuwa ya ufunguzi nchini humo kila mtu alitaka kuitazama isipokuwa mashabiki wa Hertha Berlin ambao waliamini hawakuwa vizuri kutokana na kuwauza wachezaji wawili hatari kutoka kwenye timu yao.
Rais huyo aliangalia mechi kwa kipindi cha kwanza, kwa uwezo walioonyesha Amon na Gideon, alibaki akishangaa, hakuamini kama baada ya Messi na Ronaldo basi kungeibuka watu wengine waliokuwa na uwezo kama watu hao wawili. Muda mwingi alitamani kuwaona wakigusa mpira, alifurahi namna walivyokuwa wakicheza na kutengeneza mashambulizi.
Akatokea kuwapenda, kwa kile alichokiona ndicho kilichomfanya kumpigia simu Rais wa Chama cha Soka nchini Ujerumani kutaka kuzungumza naye kwani kulikuwa na jambo alilokuwa amelifikiria. Simu ikapigwa mpaka kwa Bwana Kurt Jeremiah na kuambiwa kuhusu kile alichokifikiria rais.
Ilikuwa ni lazima wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha vijana hao wawili wanapewa uraia wa Ujerumani kwa kuchezea timu ya taifa ya nchi hiyo kwani walikuwa na uwezo mkubwa na kuwaacha lilikuwa jambo lisilowezekana hata kidogo.
Hilo halikuwa na shaka ila kitu pekee alichokiomba Jeremiah ni kufuatiliwa kwa uhamiaji wa nchi hiyo kuona kama kulikuwa na watu kutoka Tanzania ambao wangekwenda huko kwa lengo la kuzungumza na vijana hao.
Hilo halikuwa tatizo, haraka sana rais akawasiliana na watu wa uhamiaji na kuzungumza nao, alichoambiwa kulikuwa na watu wawili waliokuwa wakitoka nchini Tanzania na kuingia humu Ujerumani, walikuwa ni watu wa mpira ambao walisema wanakuja kutembea na kuangalia mambo ya soka tu.
Hilo likamfanya rais kugundua lengo kubwa la watu hao kwenda nchini Ujerumani ni kwa sababu ya kuzungumza na vijana hao, hivyo ilikuwa ni lazima wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha wanawawahi wao.
Akawasiliana tena na Jeremiah na kumwambia kuhusu hilo, haraka sana Jeremiah akachukua vyumba kwenye hoteli ya Romini Royal kwa ajili ya watu hao ambao wangefika nchini Ujerumani.
Kila kitu kilichokuwa kikifanyika kilifanyika kwa siri sana, hakutakiwa kufahamu mtu yeyote yule, rais alimsisitizia hilo kwa kuwa alijua kabisa endapo Chama cha Soka Duniani, FIFA kingegundua aliingilia masuala ya mpira basi kungekuwa na uwezekano wa nchi hiyo kufungiwa.
Kila kitu kilifanyika kama kilivyopanga na mwisho wa siku Jeremiah kuwa na akina Fintani na kuanza kuzungumza nao. Alichowaambia ni kuwa wao wenyewe walitamani sana kuwa na wachezaji kama akina Amon hivyo hawakutakiwa kuwafikiria hata kidogo, kwa kuwa walionyesha uwezo mkubwa nchini Ujerumani, basi wao walikuwa na kila sifa ya kuwa raia wa nchi hiyo.
“Haiwezekani hata kidogo!” alisema Fintani huku akimwangalia Jeremiah.
“Kwa nini isiwezekane?”
“Kwa sababu wale ni Watanzania!”
“Ila hawajafikisha miaka kumi na nane, hivyo wao hawana uwezo wa kuchagua kwa sasa ni nchi gani wanataka kuichezea,” alisema Jeremiha.
“Sawa. Ila ni lazima wakachezee Tanzania!” alisema Kizota.
“Wao wakichezea Tanzania, nyie mnafaidika na nini?” aliuliza Jeremiah.
“Nchi yetu itasonga kimpira!”
“Namaanisha nyie wawili kama nyie, mtafaidika na nini?” aliuliza, wanaume hao wakaangaliana.
“Hamtofaidika na kitu! Mtaendelea kufanya kazi zetu, hata Tanzania ikivuma kisoka, nyie bado mtaendelea kuwa hapohapo, mbaya zaidi muda wenu ukiisha, watu watawatoa na kuwaweka wengine kwenye nyadhifa zenu,” alisema Jeremiah, watu hao wakaangaliana tena.
“Ni lazima mjue cha kufanya. Nina wazo moja!” alisema Jeremiah.
“Wazo gani?”
“Labda paundi laki mbili kwa kila mmoja zinaweza kubadilisha kitu fulani,” alisema Jeremiah huku akiwa kwenye tabasamu pana.
Wote wakanyamaza na kuangaliana tena, yaani hapo walipofikia, mwanaume huyo alitaka kuwahonga pesa ili waache kufuatilia suala la Amon na Gideon.
Kiasi walichoambiwa kilikuwa kikubwa mno, paundi laki mbili zilikuwa ni zaidi ya bilioni nne kwa kila mmoja, yaani walivurugwa na hawakujua ni lipi hasa walitakiwa kulifanya. Walitumwa huko kuzungumza na akina Amon lakini kwa zile pesa zilizotajwa, vichwa vyao vikapagawa.
“Chukueni pesa muondoke nazo,” alisema Jeremiah.
“Hapana! Tutashtukiwa. Akaunti zetu zitafuatiliwa,” alisema Fintani.
“Tutawaingizia pesa kwenye benki ya Euro Bank, si ipo mpaka huko Afrika?” aliuliza.
“Ndiyo!”
“Basi mtafungua akaunti huko, nitawaingizia pesa hizo, hakuna serikali yoyote ya Afrika inayoruhusiwa kuingilia akaunti za benki hii, mtakuwa salama kabisa, hizi pesa hamtakiwi kuziacha hata kidogo, zitabadilisha maisha yenu,” alisema mwanaume huyo.
Wanaume hao wakaangaliana tena, kama kulikuwa na tamaa kubwa ya kuwa mabilionea, basi kipindi hicho tamaa iliwafikia kwa kiwango cha mwisho kabisa, walizitamani hizo pesa kupita kawaida.
Wakayafikiria maneno ya Jeremiah, ni kweli hata kama wangefanya kazi ya kuwashawishi akina Amon kwa lengo la kuitumikia Tanzania, bado wao kama wao wasingenufaika kwa lolote lile, inawezekana kabisa wao wangekataa kiasi hicho basi kungekuwa na mtu fulani angekubali.
Wakachagua pesa, walichoruhusiwa ni kuonana na vijana hao, wakazungumza mambo ya kawaida na kurudi Tanzania huku wakiwa wamekwishafungua akaunti zao na kuingiziwa pesa hizo kwa siri, hapakuwa na mtu yeyote aliyejua chochote kile, hata serikali ya Tanzania nayo ilifumbwa macho kwenye pesa hizo.
***
Jeniffer aliongea na Amon na kumshawishi kwa kila kitu lakini kijana huyo alimkatalia katakata, alichomwambia ni kwamba aliipenda sana Tanzania, alikulia huko na kufanya mambo yake yote huko na ndiyo maana alitaka kuitumia timu ya taifa ya nchi hiyo.
Jeniffer alitumia uwezo wa kila namna lakini alishindwa, hilo lilimuumiza sana, alipewa kazi kubwa ya kuifanya lakini mwisho wa siku alishindwa kufanikisha kile alichoambiwa. Huyo Amon alikuwa mgumu mno kushawishika, na alikuwa tayari hata kuondoka nchini Ujerumani lakini si kukubali kuiacha Tanzania na kuitumia nchi hiyo.
Baada ya mazungumzo ya saa moja bila kufikia muafaka, hatimaye akaaga na kuondoka zake huku wakiahidiana kuonana mara kwa mara na kuzungumza zaidi kwani penzi lao lilikuwa kubwa, liliwachanganya kila mmoja.
Alipofika hotelini tu, akamtafuta Gideon na kuanza kuongea naye, alimwambia kilichotokea, jinsi Ujerumani ilivyokuwa ikimtaka kuichezea timu yao ya taifa lakini akakataa.
Gideon alimsikiliza kwa makini, alishangaa, ilikuwaje mpaka akatae kuichezea Ujerumani na wakati ndoto za kila mmoja ilikuwa ni kucheza soka la Ulaya na hata timu za taifa la nchi hizo.
“Ni vigumu sana, Tanzania ndiyo imenifanya Ujerumani inione, bila Tanzania, Ujerumani isingeniona, kubwa zaidi Mwalimu Kambarage Nyerere alituambia tuwe wazarendo wa taifa letu,” alijibu Amon.
“Daah! Yaani umekataa utaifa wa Ujerumani?”
“Kabisa!”
“Wewe utakuwa umerogwa na Chifu Mkwawa!”
“Wewe ungekubali?”
“Yaani hata nisingejiuliza mara mbili! Kwangu mimi, Tanzania imenitesa tu!” alijibu Gideon.
Hakutaka kusikia kuhusu Tanzania, maisha ya shida aliyowahi kuishi nchini humo yalitosha kabisa na ndiyo maana mara ya kwanza baada ya kufika hapo Ujerumani alichokuwa akikifikiria ni kuzamia na kuanza maisha yake mengine kabisa.
Hakutaka kusikia kuhusu Afrika, alipachukia kwa sababu kulikuwa na maisha magumu, kulikuwa na viongozi waliokuwa wakijali maisha yao lakini si maisha ya wananchi wao, hakutaka kuona watoto wake wakizaliwa na kuwa Watanzania, wapate mateso aliyopitia, ilikuwa ni lazima aondoke na kuwa raia wa nchi nyingine.
Wakati akiambiwa hayo, moyo wake ulikuwa na hamu na yeye kufuatwa na watu hao na kuambiwa hivyo, alitamani hilo litokee na bila tatizo lolote lile angekubali na hatimaye kuchezea taifa la Ujerumani.
Huku akiwa anafikiria hilo, mara simu yake ikaanza kuita na alioangalia kioo, jina la Anita likaonekana, akahisi kulikuwa na kitu, akaipokea. Alichomwambia msichana huyo ni kwamba walitakiwa kuonana kwani kulikuwa na jambo moja alitaka kuzungumza naye.
Gideon alijua ni suala la kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani, hivyo akakubaliana naye, akaondoka bila kumuaga Amon kwani alijua endapo angefanya hivyo kijana huyo angemwambia mambo kuhusu Mwalimu Nyerere mwisho wa siku kutofanya kile alichotaka kukifanya.
Wakaonana na kuanza kuongea. Siku hiyo ilimbidi Anita atumie tu uanamke wake, alikuwa akimwangalia Gideon kwa macho ya kimahaba huku akimshika huku na kule, alitaka kutumia penzi kumshawishi kijana huyo kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani kwa kuamini sifa kubwa ingekwenda kwake.
Alishikwa huku na kule, wakachukua chumba na kufanya mapenzi, alitumia nguvu kubwa sana kwa mtu ambaye hakutakiwa kutumiwa nguvu za namna hiyo kwani tayari moyo wake ulikuwa umeridhia kuichezea Ujerumani.
Baada ya kumaliza kufanya mapenzi, msichana huyo akamwambia kuhusu suala hilo tena akimwambia endapo angekubali basi tayari kulikuwa na kiasi cha paundi milioni moja kiliandaliwa kwa ajili yake.
Kwa kuwa aliahidiwa na pesa juu, kwanza Gideon akajifanya kukataa, alifanya hivyo kwa kuwa alijua Ujerumani ilikuwa ikimuhitaji mno, kwa Anita hakutaka kukubali kuona mwanaume huyo akikataa, aliendelea kumshawishi mpaka ilipofika paundi milioni mbili, kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni nne akakubaliana naye na hatimaye kumuahidi baada ya kuingiza pesa hizo kwa akaunti yake, basi mechi ijayo ya Ujerumani, angeichezea timu hiyo.
Sasa moyo wa Anita ukafurahi kwa kile kilichotokea, alitakiwa kumshawishi zaidi Amon ili kule safu ya ushambuliaji kuwe na watu hao wawili lakini hakuona kama angekubali, endao Jeniffer alimkatalia, hakuamini kama yeye angemkubalia hata kama angemwambia kuhusu pesa.
Taarifa ikatumwa mpaka kwa Bwana Jeremiah na kuambiwa kwamba Gideon alikubali lakini kwa Amon mambo yalikuwa magumu, alikataa kujiunga na timu ya taifa ya Ujerumani, aliipenda Tanzania na alitaka kuipambania na kuikuza kisoka.
Jeremiah alipoambiwa hivyo, haraka sana akawasiliana na rais wa nchi na kumwambia kilichotokea, rais alikasirika na kumwambia Jeremiah kwamba lingekuwa jambo jema kama wangemfukuza Amon nchini kwao hata kama alikuwa na uwezo mkubwa kiasi gani.
“Hilo ni gumu mkuu, hata mimi nitalikataa!” alisema Jeremiah.
“Kwa sababu gani?”
“Huyu mtu ataifanya ligi yetu ipate umaarufu zaidi, nchi itengeneze pesa, watu wavutiwe na ligi yetu! Mbona Messi aliichezea Argentina na wakati klabu yake ilikuwa nchini Hispania? Mbona hawakumfukuza? Tukisema tumfukuze, timu za Hispania ama Uingereza zitamdaka, na wakimchukua tu, basi jua watafanikiwa sana na sisi tutabaki kuwa wasindikizaji tu,” alisema Jeremiah maneno ambayo yalimuingia rais na kutulia kichwani mwake.
“Kwa hiyo tufanyeje?”
“Sisi tuangalie tu umaarufu wa ligi yetu na kutengeneza pesa kupitia hawa,” alisema Jeremiah.
“Sawa.”

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
Niwakumbushe tu kwamba simulizi hii inaendelea kupatikana WhatsApp kwa shilingi 5000 tu. Namba hizo hapo juu.
 
Sehemu ya 20

Miongoni mwa mashabiki wakubwa wa mchezo wa mpira nchini Ujerumani alikuwa rais wa nchi hiyo, Bwana Simon Berbeuz aliyekuwa akishabikia timu ya Bayern Munich.
Kwenye ndoto zake za kila siku alitamani sana kuona Timu ya Taifa ya Ujerumani ikifanya vizuri kuliko timu zote duniani. Hakutaka kuona taifa jingine likiwa mbele ya taifa hilo nguri la soka duniani.
Kipindi ambacho kulikuwa na mechi baina ya Hertha Berlin na Schalke 04 alitulia kwenye kiti chake na kuanza kutazama mechi hiyo. Ilipita miezi miwili ya mateso, mateso kwa kila mshabiki wa mpira kwa sababu timu zilikuwa mapumzikoni, hapakuwa na mechi nyingine yoyote kuanzia mwezi wa sita mpaka wa nane.
Kitendo cha mechi hiyo kuwa ya ufunguzi nchini humo kila mtu alitaka kuitazama isipokuwa mashabiki wa Hertha Berlin ambao waliamini hawakuwa vizuri kutokana na kuwauza wachezaji wawili hatari kutoka kwenye timu yao.
Rais huyo aliangalia mechi kwa kipindi cha kwanza, kwa uwezo walioonyesha Amon na Gideon, alibaki akishangaa, hakuamini kama baada ya Messi na Ronaldo basi kungeibuka watu wengine waliokuwa na uwezo kama watu hao wawili. Muda mwingi alitamani kuwaona wakigusa mpira, alifurahi namna walivyokuwa wakicheza na kutengeneza mashambulizi.
Akatokea kuwapenda, kwa kile alichokiona ndicho kilichomfanya kumpigia simu Rais wa Chama cha Soka nchini Ujerumani kutaka kuzungumza naye kwani kulikuwa na jambo alilokuwa amelifikiria. Simu ikapigwa mpaka kwa Bwana Kurt Jeremiah na kuambiwa kuhusu kile alichokifikiria rais.
Ilikuwa ni lazima wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha vijana hao wawili wanapewa uraia wa Ujerumani kwa kuchezea timu ya taifa ya nchi hiyo kwani walikuwa na uwezo mkubwa na kuwaacha lilikuwa jambo lisilowezekana hata kidogo.
Hilo halikuwa na shaka ila kitu pekee alichokiomba Jeremiah ni kufuatiliwa kwa uhamiaji wa nchi hiyo kuona kama kulikuwa na watu kutoka Tanzania ambao wangekwenda huko kwa lengo la kuzungumza na vijana hao.
Hilo halikuwa tatizo, haraka sana rais akawasiliana na watu wa uhamiaji na kuzungumza nao, alichoambiwa kulikuwa na watu wawili waliokuwa wakitoka nchini Tanzania na kuingia humu Ujerumani, walikuwa ni watu wa mpira ambao walisema wanakuja kutembea na kuangalia mambo ya soka tu.
Hilo likamfanya rais kugundua lengo kubwa la watu hao kwenda nchini Ujerumani ni kwa sababu ya kuzungumza na vijana hao, hivyo ilikuwa ni lazima wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha wanawawahi wao.
Akawasiliana tena na Jeremiah na kumwambia kuhusu hilo, haraka sana Jeremiah akachukua vyumba kwenye hoteli ya Romini Royal kwa ajili ya watu hao ambao wangefika nchini Ujerumani.
Kila kitu kilichokuwa kikifanyika kilifanyika kwa siri sana, hakutakiwa kufahamu mtu yeyote yule, rais alimsisitizia hilo kwa kuwa alijua kabisa endapo Chama cha Soka Duniani, FIFA kingegundua aliingilia masuala ya mpira basi kungekuwa na uwezekano wa nchi hiyo kufungiwa.
Kila kitu kilifanyika kama kilivyopanga na mwisho wa siku Jeremiah kuwa na akina Fintani na kuanza kuzungumza nao. Alichowaambia ni kuwa wao wenyewe walitamani sana kuwa na wachezaji kama akina Amon hivyo hawakutakiwa kuwafikiria hata kidogo, kwa kuwa walionyesha uwezo mkubwa nchini Ujerumani, basi wao walikuwa na kila sifa ya kuwa raia wa nchi hiyo.
“Haiwezekani hata kidogo!” alisema Fintani huku akimwangalia Jeremiah.
“Kwa nini isiwezekane?”
“Kwa sababu wale ni Watanzania!”
“Ila hawajafikisha miaka kumi na nane, hivyo wao hawana uwezo wa kuchagua kwa sasa ni nchi gani wanataka kuichezea,” alisema Jeremiha.
“Sawa. Ila ni lazima wakachezee Tanzania!” alisema Kizota.
“Wao wakichezea Tanzania, nyie mnafaidika na nini?” aliuliza Jeremiah.
“Nchi yetu itasonga kimpira!”
“Namaanisha nyie wawili kama nyie, mtafaidika na nini?” aliuliza, wanaume hao wakaangaliana.
“Hamtofaidika na kitu! Mtaendelea kufanya kazi zetu, hata Tanzania ikivuma kisoka, nyie bado mtaendelea kuwa hapohapo, mbaya zaidi muda wenu ukiisha, watu watawatoa na kuwaweka wengine kwenye nyadhifa zenu,” alisema Jeremiah, watu hao wakaangaliana tena.
“Ni lazima mjue cha kufanya. Nina wazo moja!” alisema Jeremiah.
“Wazo gani?”
“Labda paundi laki mbili kwa kila mmoja zinaweza kubadilisha kitu fulani,” alisema Jeremiah huku akiwa kwenye tabasamu pana.
Wote wakanyamaza na kuangaliana tena, yaani hapo walipofikia, mwanaume huyo alitaka kuwahonga pesa ili waache kufuatilia suala la Amon na Gideon.
Kiasi walichoambiwa kilikuwa kikubwa mno, paundi laki mbili zilikuwa ni zaidi ya bilioni nne kwa kila mmoja, yaani walivurugwa na hawakujua ni lipi hasa walitakiwa kulifanya. Walitumwa huko kuzungumza na akina Amon lakini kwa zile pesa zilizotajwa, vichwa vyao vikapagawa.
“Chukueni pesa muondoke nazo,” alisema Jeremiah.
“Hapana! Tutashtukiwa. Akaunti zetu zitafuatiliwa,” alisema Fintani.
“Tutawaingizia pesa kwenye benki ya Euro Bank, si ipo mpaka huko Afrika?” aliuliza.
“Ndiyo!”
“Basi mtafungua akaunti huko, nitawaingizia pesa hizo, hakuna serikali yoyote ya Afrika inayoruhusiwa kuingilia akaunti za benki hii, mtakuwa salama kabisa, hizi pesa hamtakiwi kuziacha hata kidogo, zitabadilisha maisha yenu,” alisema mwanaume huyo.
Wanaume hao wakaangaliana tena, kama kulikuwa na tamaa kubwa ya kuwa mabilionea, basi kipindi hicho tamaa iliwafikia kwa kiwango cha mwisho kabisa, walizitamani hizo pesa kupita kawaida.
Wakayafikiria maneno ya Jeremiah, ni kweli hata kama wangefanya kazi ya kuwashawishi akina Amon kwa lengo la kuitumikia Tanzania, bado wao kama wao wasingenufaika kwa lolote lile, inawezekana kabisa wao wangekataa kiasi hicho basi kungekuwa na mtu fulani angekubali.
Wakachagua pesa, walichoruhusiwa ni kuonana na vijana hao, wakazungumza mambo ya kawaida na kurudi Tanzania huku wakiwa wamekwishafungua akaunti zao na kuingiziwa pesa hizo kwa siri, hapakuwa na mtu yeyote aliyejua chochote kile, hata serikali ya Tanzania nayo ilifumbwa macho kwenye pesa hizo.
***
Jeniffer aliongea na Amon na kumshawishi kwa kila kitu lakini kijana huyo alimkatalia katakata, alichomwambia ni kwamba aliipenda sana Tanzania, alikulia huko na kufanya mambo yake yote huko na ndiyo maana alitaka kuitumia timu ya taifa ya nchi hiyo.
Jeniffer alitumia uwezo wa kila namna lakini alishindwa, hilo lilimuumiza sana, alipewa kazi kubwa ya kuifanya lakini mwisho wa siku alishindwa kufanikisha kile alichoambiwa. Huyo Amon alikuwa mgumu mno kushawishika, na alikuwa tayari hata kuondoka nchini Ujerumani lakini si kukubali kuiacha Tanzania na kuitumia nchi hiyo.
Baada ya mazungumzo ya saa moja bila kufikia muafaka, hatimaye akaaga na kuondoka zake huku wakiahidiana kuonana mara kwa mara na kuzungumza zaidi kwani penzi lao lilikuwa kubwa, liliwachanganya kila mmoja.
Alipofika hotelini tu, akamtafuta Gideon na kuanza kuongea naye, alimwambia kilichotokea, jinsi Ujerumani ilivyokuwa ikimtaka kuichezea timu yao ya taifa lakini akakataa.
Gideon alimsikiliza kwa makini, alishangaa, ilikuwaje mpaka akatae kuichezea Ujerumani na wakati ndoto za kila mmoja ilikuwa ni kucheza soka la Ulaya na hata timu za taifa la nchi hizo.
“Ni vigumu sana, Tanzania ndiyo imenifanya Ujerumani inione, bila Tanzania, Ujerumani isingeniona, kubwa zaidi Mwalimu Kambarage Nyerere alituambia tuwe wazarendo wa taifa letu,” alijibu Amon.
“Daah! Yaani umekataa utaifa wa Ujerumani?”
“Kabisa!”
“Wewe utakuwa umerogwa na Chifu Mkwawa!”
“Wewe ungekubali?”
“Yaani hata nisingejiuliza mara mbili! Kwangu mimi, Tanzania imenitesa tu!” alijibu Gideon.
Hakutaka kusikia kuhusu Tanzania, maisha ya shida aliyowahi kuishi nchini humo yalitosha kabisa na ndiyo maana mara ya kwanza baada ya kufika hapo Ujerumani alichokuwa akikifikiria ni kuzamia na kuanza maisha yake mengine kabisa.
Hakutaka kusikia kuhusu Afrika, alipachukia kwa sababu kulikuwa na maisha magumu, kulikuwa na viongozi waliokuwa wakijali maisha yao lakini si maisha ya wananchi wao, hakutaka kuona watoto wake wakizaliwa na kuwa Watanzania, wapate mateso aliyopitia, ilikuwa ni lazima aondoke na kuwa raia wa nchi nyingine.
Wakati akiambiwa hayo, moyo wake ulikuwa na hamu na yeye kufuatwa na watu hao na kuambiwa hivyo, alitamani hilo litokee na bila tatizo lolote lile angekubali na hatimaye kuchezea taifa la Ujerumani.
Huku akiwa anafikiria hilo, mara simu yake ikaanza kuita na alioangalia kioo, jina la Anita likaonekana, akahisi kulikuwa na kitu, akaipokea. Alichomwambia msichana huyo ni kwamba walitakiwa kuonana kwani kulikuwa na jambo moja alitaka kuzungumza naye.
Gideon alijua ni suala la kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani, hivyo akakubaliana naye, akaondoka bila kumuaga Amon kwani alijua endapo angefanya hivyo kijana huyo angemwambia mambo kuhusu Mwalimu Nyerere mwisho wa siku kutofanya kile alichotaka kukifanya.
Wakaonana na kuanza kuongea. Siku hiyo ilimbidi Anita atumie tu uanamke wake, alikuwa akimwangalia Gideon kwa macho ya kimahaba huku akimshika huku na kule, alitaka kutumia penzi kumshawishi kijana huyo kuichezea timu ya taifa ya Ujerumani kwa kuamini sifa kubwa ingekwenda kwake.
Alishikwa huku na kule, wakachukua chumba na kufanya mapenzi, alitumia nguvu kubwa sana kwa mtu ambaye hakutakiwa kutumiwa nguvu za namna hiyo kwani tayari moyo wake ulikuwa umeridhia kuichezea Ujerumani.
Baada ya kumaliza kufanya mapenzi, msichana huyo akamwambia kuhusu suala hilo tena akimwambia endapo angekubali basi tayari kulikuwa na kiasi cha paundi milioni moja kiliandaliwa kwa ajili yake.
Kwa kuwa aliahidiwa na pesa juu, kwanza Gideon akajifanya kukataa, alifanya hivyo kwa kuwa alijua Ujerumani ilikuwa ikimuhitaji mno, kwa Anita hakutaka kukubali kuona mwanaume huyo akikataa, aliendelea kumshawishi mpaka ilipofika paundi milioni mbili, kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni nne akakubaliana naye na hatimaye kumuahidi baada ya kuingiza pesa hizo kwa akaunti yake, basi mechi ijayo ya Ujerumani, angeichezea timu hiyo.
Sasa moyo wa Anita ukafurahi kwa kile kilichotokea, alitakiwa kumshawishi zaidi Amon ili kule safu ya ushambuliaji kuwe na watu hao wawili lakini hakuona kama angekubali, endao Jeniffer alimkatalia, hakuamini kama yeye angemkubalia hata kama angemwambia kuhusu pesa.
Taarifa ikatumwa mpaka kwa Bwana Jeremiah na kuambiwa kwamba Gideon alikubali lakini kwa Amon mambo yalikuwa magumu, alikataa kujiunga na timu ya taifa ya Ujerumani, aliipenda Tanzania na alitaka kuipambania na kuikuza kisoka.
Jeremiah alipoambiwa hivyo, haraka sana akawasiliana na rais wa nchi na kumwambia kilichotokea, rais alikasirika na kumwambia Jeremiah kwamba lingekuwa jambo jema kama wangemfukuza Amon nchini kwao hata kama alikuwa na uwezo mkubwa kiasi gani.
“Hilo ni gumu mkuu, hata mimi nitalikataa!” alisema Jeremiah.
“Kwa sababu gani?”
“Huyu mtu ataifanya ligi yetu ipate umaarufu zaidi, nchi itengeneze pesa, watu wavutiwe na ligi yetu! Mbona Messi aliichezea Argentina na wakati klabu yake ilikuwa nchini Hispania? Mbona hawakumfukuza? Tukisema tumfukuze, timu za Hispania ama Uingereza zitamdaka, na wakimchukua tu, basi jua watafanikiwa sana na sisi tutabaki kuwa wasindikizaji tu,” alisema Jeremiah maneno ambayo yalimuingia rais na kutulia kichwani mwake.
“Kwa hiyo tufanyeje?”
“Sisi tuangalie tu umaarufu wa ligi yetu na kutengeneza pesa kupitia hawa,” alisema Jeremiah.
“Sawa.”

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
Niwakumbushe tu kwamba simulizi hii inaendelea kupatikana WhatsApp kwa shilingi 5000 tu. Namba hizo hapo juu.
Kwl mambo yanazidi kuwa mazuri
 
Sehemu ya 21

Mashabiki wa Timu ya Hertha Berlin waliona kama siku hazikatiki, kitendo cha kuwa na mechi wikiendi mpaka wikiendi kwao yakaonekana kuwa mateso makubwa, hawakuamini kwamba walitakiwa kusubiri wiki nzima ndipo wangekwenda kuwaona tena Amon na Gideon wakifanya yao uwanjani.
Watu hao hawakukubali, haraka sana Jumatatu ya siku hiyo wakakusanyika kwa wingi kwenye uwanja wa mazoezi kwa lengo la kufuatilia mazoezi hayo, kila mmoja aliyekuwa mahali hapo alionekana kuchanganyikiwa, wengi wakataka kusainiwa vitabu vyao.
Amon na Gideon walionekana kubadilisha kila kitu, kwa viongozi wa timu hiyo waliona kabisa walikuwa wakienda kupata pesa nyingi na hata kocha aliamini sasa tuzo ya kocha bora wa msimu ilikuwa ikienda kwake kwa kuwa tayari alikuwa na watu waliokuwa wakimbeba kwa kuifanya timu kufanya vizuri.
Kila aliyekuwa na simu, alijitahidi kupiga picha, kila wakati walikuwa wakiimba wimbo wa timu hiyo kama kuwahamasisha kufanya vizuri kitu kilichokuwa kizuri kwa kila mchezaji.
Magazeti, mitandao na kila kitu nchini Ujerumani kilikuwa kikizungumzia kuhusu Timu ya Hertha Berlin na ule usajili wa maajabu waliokuwa wameufanya. Watu wakaacha kuizungumzia Bayern Munich na Borussia Dortmund, kwanza wakaziweka pembeni na kuuzungumzia uwezo wa watu hao wawili.
Walipambwa na kupambwa, hatimaye tetesi za kubadilishiwa uraia wao na kuwa Wajerumani zikaanza kusikika na kuandikwa kila kona.
Hizo zilikuwa tetesi nzuri kupita zote, waandishi wa habari wakaanza kuzichimba kwa uhakika lakini hawakufanikiwa kujua hasa kilichokuwa kikiendelea upande wa pili.
Kila mtu alitaka taifa lao liwe na watu kama hao, walikuwa na vipaji vikubwa mno vya kucheza mpira, kwao, kuwaacha watu hao wakaitumikie nchi kama Tanzania ilionekana kuwa tatizo kubwa mno.
Kwa Amon, hakufurahishwa na hizo tetesi, alikwishakataa kwamba hakutaka kuichezea Ujerumani, alichotaka ni kuichezea Tanzania na kuifikisha mbali na sio kule bondeni ilipokuwa.
Alijitahidi sana kumshawishi Gideon kuachana na wazo lake la kuichezea Ujerumani lakini kijana huyo alikataa, aliteseka sana Tanzania, alisema hapakuwa na mtu aliyejali maisha yake huko, sasa kwa nini arudi na asiendelee kuishi Ulaya mpaka kifo chake?
“Kwa sababu gani ulikuwa unataka kuja Ulaya?” aliuliza Amon.
“Nipate pesa! Niwe na maisha mazuri!” alimjibu.
“Hayo unayapata ama huyapati?”
“Nayapata!”
“Acha nikwambie kitu! Yaani wewe utaendelea kuwa na pesa maisha yako yote, hata ukiendelea kuwa Mtanzania, bado utaendelea kupata pesa Gideon!” alisema Amon.
“Hapana aisee! Yaani siku ukiniona narudi Tanzania, basi jua tayari nitakuwa Mjerumani. Siwezi kurudi Tanzania nikiwa Mtanzania,” alisema Gideon, kwa jinsi alivyokuwa akizungumza tu ilikuwa ni rahisi sana kujua mwanaume huyo alikuwa akimaanisha kwa kile alichokuwa akikisema.
Japokuwa kwa mara ya kwanza Amon alikataa kuichezea timu ya Taifa ya Ujerumani lakini Jeniffer hakutaka kukata tamaa, kila siku alipokuwa akizungumza na mpenzi wake na hata kuonana, alichokuwa akimwambia kilikuwa kilekile kubadilisha uraia wake na kuichezea Ujerumani.
Msimamo wa Amon haukuyumbishwa hata kidogo, alimwambia msichana huyo kwamba hakika asingeweza kulichezea taifa lolote lile zaidi ya Tanzania. Baba yake alikuwa na ndoto kubwa ya kuichezea Tanzania na kuifikisha mbali ila alishindwa baada ya kuvunjika mguu, hakutaka kuona naye akishindwa kuitimiza ndoto hiyo.
“Sawa haina shida,” alisema Jeniffer kwa sauti ya upole sana kuonyesha kukubaliana na mpenzi wake huyo.
“Haina tatizo! Naomba siku nyingine usiniambie tena kuhusu suala hili, huwa silifurahii hata kidogo,” alisema Amon.
“Usijali!”
***
Esta alikuwa akiishi maisha ya ndoto yake, kwenye maisha yake hakutaka kupenda tena mpaka siku ambayo angeona sasa imetosha na ilikuwa ni lazima kuolewa, basi angeuruhusu moyo wake kupenda tena, iwe kwa mwanaume wa mwisho tu.
Kila kitu kilibadilika baada ya kumuona huyo Edmund. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi na kila wakati alihisi kabisa huyo ndiye mwanaume aliyekuwa ameumbwa na kuletwa duniani kwa ajili yake tu.
Kwa kuwa alitokea kumpenda hatimaye akaanza kujisikia wivu, kila alipomuona amesimama na wanawake wengine ama kuzungumza nao alisikia kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake.
Hakujua Edmund alikuwa mwanaume wa nani, kila msichana aliyekuwa akizungumza naye, walizungumza kama marafiki wa kawaida tu. Alikuwa akiumia kimoyomoyo lakini na hakujua ni kwa namna gani angevumilia kwa miaka yote mitatu mpaka pale atakapomaliza.
“Ila mimi mjinga sana,” alijisemea huku akimwangalia Edmund aliyekuwa bize na mambo yake.
“Sasa kwa nini nisimfuate na kumwambia kwamba nampenda?” alijiuliza.
“Mh! Ila nitaweza mie mtoto wa Iringa kumfuata mwanaume wa Dar halafu nimwambie nampenda?” alijiuliza.
Akajiangalia.
“Halafu na haya maguo niliyovaa kama mtawa, kweli atanielewa mie? Hili lisketi langu ningelipandisha juu kidogo, miguu iliyonona ionekane, ila hivihivi, hapana hawezi kunikubali,” alijisemea, kila alipokuwa akijiangalia, aliona kabisa hakuwa na hadhi ya kutembea na mtu kama Edmund.
Edmund alikuwa mtoto wa Dar, kulipoitwa mjini, amewaona wanawake wengi wazuri, waliokuwa wakivaa kila aina ya mavazi, waliokuwa wakibadilisha mitindo ya nywele ya kila aina, wanawake waliojua kuvaa, kujipulizia manukato na kula bata.
Yaani kuwaacha hao wote na kumfuata Esta lilionekana kuwa jambo lisilowezekana kabisa kumuingia msichana huyo. Kabla ya kumfuata Edmund, kwanza akajishusha, akajiona hafai, akahisi kabisa hakustahili kuwa na mwanaume kama huyo.
“Acha niachane naye, nitamtafuta mwanaume wa ndoto zangu nikirudi Iringa. Huku Dar siwezi kwa kweli, kila mzuri ana mwenyewe,” alijisemea.
Akaamua kuachana na Edmund lakini kila siku alipokuwa akimuona moyo wake ulimwambia hiyo ndiyo nafasi ya kumfuata na kuzungumza naye. Alishindwa, hakujua ni kwa namna gani angeweza kuzungumza mbele ya macho yake.
Kwanza alikuwa msichana, mwenye aibu kubwa, kumfuata mwanaume na kumwambia alimpenda, alitaka sana kuwa naye lilionekana kuwa suala gumu sana, tangu azaliwe huko Iringa hakuwahi kumsikia mwanamke akimfuata mwanaume na kumwambia alikuwa akimpenda, sasa kwa sababu gani yeye amfuate?
“Wakati mwingine si nijitoe tu jamani!” alijiambia.
Alikuwa na moyo wa kusitasita, kumfuata Edmund lilionekana kuwa suala gumu kupita kawaida. Kila siku kazi yake ilikuwa ni kumwangalia tu, alitamani hata kuwaambia marafiki zake, hasa rafiki yake kipenzi aliyeitwa kwa jina la Lilian lakini alishindwa.
“Halafu wiki nzima hii nakuona unamwangalia sana kaka wa watu!” alisema Lilian, msichana aliyetoka mkoani Singida.
“Nani? Mimi?”
“Ndiyo! Unamtaka?”
“Walaaaa!”
“Unampenda?”
“Akuuuu!”
“Sasa mbona unamwangalia hivyo?”
“Huwa namfananisha na mtu!”
“Nani? Mpenzi wako?”
“Jamaniiiiiiiii”
“Sema! Huku Dar nasikia watu wanafunguka tu, ukimtaka mtu mwambie, ndiyo nimesikia maisha yao ya huku,” alisema Lilian huku akitoa tabasamu.
“Sasa ungekuwa wewe ungekwenda kumwambia?”
“Mwaego! Ningewezaje? Nionekane malaya!”
“Kwani kumwambia mwanaume unaonekana malaya?”
“Kwa mtazamo wa watu wengine!”
“Mtazamo wako?”
“Hebu tuachane na hayo!” alisema Lilian na kuanza kucheka, akalipotezea swali hilo kwani tayari lilionekana kuwa gumu.
Kama ni mgonjwa basi Esta alikuwa mahututi, hakujiweza kwa Edmund, ilikuwa ni sawa na mgonjwa aliyeumwa sana na hatimaye kufikishwa kwenye chumba cha ICU na kusubiri muujiza wa Mungu ili atoke na kutembea tena.
Kila siku Lilian alikuwa na kazi ya kumuuliza kama alimpenda Edmund lakini msichana huyo alikataa kwa kumwambia alikuwa akimfananisha tu. Lilian alijua kabisa rafiki yake hakuwa anajiweza kwa Edmund, hivyo alichokifanya ni kuamua kumfuata kwa lengo la kumwambia.
“Nakwenda kumwambia!”
“Kumwambia nani?”
“Edmund!”
“Kwamba?”
“Unampenda. Umeoza kwake!”
“Weeeeeeee!”
“Nakwenda!” alisema Lilian.
Hakutaka kusubiri, akainuka na kuanza kumfuata. Esta alikuwa akiogopa, alimwangalia Esta alivyokuwa akipiga hatua kumfuata Edmund, hakutaka hata kusubiri, haraka sana akainuka na kuondoka darasani haraka sana.
Aliogopa kupita kawaida, ni kama mtu ambaye alikuwa akianza kupenda kwa mara ya kwanza, ni kama alikuwa bikira kumbe haikuwa hivyo.
Kwake, kusimama mbele ya Edmund na kuzungumza naye lilikuwa jambo lisilowezekana, breki ya kwanza ilikuwa bwenini, mapigo ya moyo yalikuwa yakimdunda mno.
Huku nyuma Lilian alimfuata Edmund na kumsalimia, alikuwa peke yake, alisimama na kumwangalia usoni, alipoyapeleka macho yake mahali alipokuwa Esta, msichana huyo hakuwepo.
“Karibu!” alisema Edmund huku akimwangalia Lilian.
“Nimekaribia! Nimekuja na ujumbe wako!” alimwambia.
“Ujumbe gani?”
“Kuna rafiki yangu anakupenda sana!”
“Rafiki yako ananipenda?”
“Ndiyo! Ila anaogopa kukwambia. Naona anateseka sana juu yako, nimekuja kumsaidia,” alimwambia.
Edmund akanyamaza, akainama na kujifanya kuwa na mawazo huku kichwa chake kikifikiria ni kwa namna gani alitakiwa kumwambia msichana huyo. Kwanza hakumfahamu msichana aliyekuwa akimtaka lakini la pili alimfikiria sana Angelina.
Alimpenda msichana huyo, kwake alikuwa kila kitu, tangu akiwa shuleni alimwambia asingemsaliti lakini kuna kipindi alishindwa, alimsaliti kwa siri sana.
Kama kulikuwa na mtu aliyekuwa akimpenda chuoni hapo, hakutaka kuwa naye kwa sababu aliamini mwaka unaofuata basi naye Angelina angekuwa hapo, sasa ingekuwaje endapo angesikia mpenzi wake alikuwa na uhusiano na msichana mwingine.
“Kunipata mimi ni ngumu sana,” alimwambia Lilian.
“Kwa nini?”
“Nina mpenzi wangu!”
“Ila yeye anasema hajawahi kukuona naye!”
“Amesema yeye ama unasema wewe?” aliuliza huku akiwa na tabasamu.
“Aya! Basi tunasema sisi kwamba hatukuwahi kukuona na mpenzi wako!” alimwambia, wote wakaanza kucheka.
“Wewe una mpenzi?”
“Ndiyo!”
“Mbona hatujawahi kukuona naye?”
“Jamani! Kwani yupo hapa?” aliuliza, Edmund hakulijibu swali hilo, akacheka kidogo, kicheko kilichomfanya Lilian kujua hilo swali aliloliuliza lilikuwa sawasawa na lile lililokuwa kwa Edmund.
“Naomba umsaidie rafiki yangu, hata kuongea naye tu, inatosha,” alimwambia.
“Yupo wapi?”
“Nadhani amekimbia!”
“Amekimbia?”
“Yeah! Anakuogopa!”
“Basi naomba ukamwambie nahitaji kuzungumza naye sasa hivi!” alisema Edmund, haraka sana Lilian akaondoka.
Yeye mwenyewe hakujiamini kama ndiye aliyekuwa amezungumza maneno hayo kwa Edmund, alijiamini sana na alipoondoka moyo wake ulikuwa umetulia sasa, alikuwa kwenye wakati mgumu mno.
Alifanya hivyo kwa ajili ya rafiki yake, alimpenda, alimuona jinsi alivyokuwa akiteseka, hakutaka kuona hilo likimtokea na ndiyo maana aliamua kufanya hicho alichokifanya. Baada ya kufika bwenini, akamkuta Esta.
“Niambie imekuwaje?” aliuliza Esta harakaharaka.
“Unaitwa!”
“Na nani?”
“Edmund!”
“Kwani umemwambia kweli?”
“Ndiyo! Amesema anataka kuongea nawe!”
“Hapana! Naogopa!”
“Jikaze! Esta! Hii ndiyo nafasi, ukishindwa hii, hutoipata tena nakwambia,” alimwambia.

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
Niwakumbushe tu kwamba simulizi hii inaendelea kupatikana WhatsApp kwa shilingi 5000 tu. Namba hizo hapo juu.
 
Sehemu ya 21

Mashabiki wa Timu ya Hertha Berlin waliona kama siku hazikatiki, kitendo cha kuwa na mechi wikiendi mpaka wikiendi kwao yakaonekana kuwa mateso makubwa, hawakuamini kwamba walitakiwa kusubiri wiki nzima ndipo wangekwenda kuwaona tena Amon na Gideon wakifanya yao uwanjani.
Watu hao hawakukubali, haraka sana Jumatatu ya siku hiyo wakakusanyika kwa wingi kwenye uwanja wa mazoezi kwa lengo la kufuatilia mazoezi hayo, kila mmoja aliyekuwa mahali hapo alionekana kuchanganyikiwa, wengi wakataka kusainiwa vitabu vyao.
Amon na Gideon walionekana kubadilisha kila kitu, kwa viongozi wa timu hiyo waliona kabisa walikuwa wakienda kupata pesa nyingi na hata kocha aliamini sasa tuzo ya kocha bora wa msimu ilikuwa ikienda kwake kwa kuwa tayari alikuwa na watu waliokuwa wakimbeba kwa kuifanya timu kufanya vizuri.
Kila aliyekuwa na simu, alijitahidi kupiga picha, kila wakati walikuwa wakiimba wimbo wa timu hiyo kama kuwahamasisha kufanya vizuri kitu kilichokuwa kizuri kwa kila mchezaji.
Magazeti, mitandao na kila kitu nchini Ujerumani kilikuwa kikizungumzia kuhusu Timu ya Hertha Berlin na ule usajili wa maajabu waliokuwa wameufanya. Watu wakaacha kuizungumzia Bayern Munich na Borussia Dortmund, kwanza wakaziweka pembeni na kuuzungumzia uwezo wa watu hao wawili.
Walipambwa na kupambwa, hatimaye tetesi za kubadilishiwa uraia wao na kuwa Wajerumani zikaanza kusikika na kuandikwa kila kona.
Hizo zilikuwa tetesi nzuri kupita zote, waandishi wa habari wakaanza kuzichimba kwa uhakika lakini hawakufanikiwa kujua hasa kilichokuwa kikiendelea upande wa pili.
Kila mtu alitaka taifa lao liwe na watu kama hao, walikuwa na vipaji vikubwa mno vya kucheza mpira, kwao, kuwaacha watu hao wakaitumikie nchi kama Tanzania ilionekana kuwa tatizo kubwa mno.
Kwa Amon, hakufurahishwa na hizo tetesi, alikwishakataa kwamba hakutaka kuichezea Ujerumani, alichotaka ni kuichezea Tanzania na kuifikisha mbali na sio kule bondeni ilipokuwa.
Alijitahidi sana kumshawishi Gideon kuachana na wazo lake la kuichezea Ujerumani lakini kijana huyo alikataa, aliteseka sana Tanzania, alisema hapakuwa na mtu aliyejali maisha yake huko, sasa kwa nini arudi na asiendelee kuishi Ulaya mpaka kifo chake?
“Kwa sababu gani ulikuwa unataka kuja Ulaya?” aliuliza Amon.
“Nipate pesa! Niwe na maisha mazuri!” alimjibu.
“Hayo unayapata ama huyapati?”
“Nayapata!”
“Acha nikwambie kitu! Yaani wewe utaendelea kuwa na pesa maisha yako yote, hata ukiendelea kuwa Mtanzania, bado utaendelea kupata pesa Gideon!” alisema Amon.
“Hapana aisee! Yaani siku ukiniona narudi Tanzania, basi jua tayari nitakuwa Mjerumani. Siwezi kurudi Tanzania nikiwa Mtanzania,” alisema Gideon, kwa jinsi alivyokuwa akizungumza tu ilikuwa ni rahisi sana kujua mwanaume huyo alikuwa akimaanisha kwa kile alichokuwa akikisema.
Japokuwa kwa mara ya kwanza Amon alikataa kuichezea timu ya Taifa ya Ujerumani lakini Jeniffer hakutaka kukata tamaa, kila siku alipokuwa akizungumza na mpenzi wake na hata kuonana, alichokuwa akimwambia kilikuwa kilekile kubadilisha uraia wake na kuichezea Ujerumani.
Msimamo wa Amon haukuyumbishwa hata kidogo, alimwambia msichana huyo kwamba hakika asingeweza kulichezea taifa lolote lile zaidi ya Tanzania. Baba yake alikuwa na ndoto kubwa ya kuichezea Tanzania na kuifikisha mbali ila alishindwa baada ya kuvunjika mguu, hakutaka kuona naye akishindwa kuitimiza ndoto hiyo.
“Sawa haina shida,” alisema Jeniffer kwa sauti ya upole sana kuonyesha kukubaliana na mpenzi wake huyo.
“Haina tatizo! Naomba siku nyingine usiniambie tena kuhusu suala hili, huwa silifurahii hata kidogo,” alisema Amon.
“Usijali!”
***
Esta alikuwa akiishi maisha ya ndoto yake, kwenye maisha yake hakutaka kupenda tena mpaka siku ambayo angeona sasa imetosha na ilikuwa ni lazima kuolewa, basi angeuruhusu moyo wake kupenda tena, iwe kwa mwanaume wa mwisho tu.
Kila kitu kilibadilika baada ya kumuona huyo Edmund. Mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa kasi na kila wakati alihisi kabisa huyo ndiye mwanaume aliyekuwa ameumbwa na kuletwa duniani kwa ajili yake tu.
Kwa kuwa alitokea kumpenda hatimaye akaanza kujisikia wivu, kila alipomuona amesimama na wanawake wengine ama kuzungumza nao alisikia kitu chenye ncha kali kikiuchoma moyo wake.
Hakujua Edmund alikuwa mwanaume wa nani, kila msichana aliyekuwa akizungumza naye, walizungumza kama marafiki wa kawaida tu. Alikuwa akiumia kimoyomoyo lakini na hakujua ni kwa namna gani angevumilia kwa miaka yote mitatu mpaka pale atakapomaliza.
“Ila mimi mjinga sana,” alijisemea huku akimwangalia Edmund aliyekuwa bize na mambo yake.
“Sasa kwa nini nisimfuate na kumwambia kwamba nampenda?” alijiuliza.
“Mh! Ila nitaweza mie mtoto wa Iringa kumfuata mwanaume wa Dar halafu nimwambie nampenda?” alijiuliza.
Akajiangalia.
“Halafu na haya maguo niliyovaa kama mtawa, kweli atanielewa mie? Hili lisketi langu ningelipandisha juu kidogo, miguu iliyonona ionekane, ila hivihivi, hapana hawezi kunikubali,” alijisemea, kila alipokuwa akijiangalia, aliona kabisa hakuwa na hadhi ya kutembea na mtu kama Edmund.
Edmund alikuwa mtoto wa Dar, kulipoitwa mjini, amewaona wanawake wengi wazuri, waliokuwa wakivaa kila aina ya mavazi, waliokuwa wakibadilisha mitindo ya nywele ya kila aina, wanawake waliojua kuvaa, kujipulizia manukato na kula bata.
Yaani kuwaacha hao wote na kumfuata Esta lilionekana kuwa jambo lisilowezekana kabisa kumuingia msichana huyo. Kabla ya kumfuata Edmund, kwanza akajishusha, akajiona hafai, akahisi kabisa hakustahili kuwa na mwanaume kama huyo.
“Acha niachane naye, nitamtafuta mwanaume wa ndoto zangu nikirudi Iringa. Huku Dar siwezi kwa kweli, kila mzuri ana mwenyewe,” alijisemea.
Akaamua kuachana na Edmund lakini kila siku alipokuwa akimuona moyo wake ulimwambia hiyo ndiyo nafasi ya kumfuata na kuzungumza naye. Alishindwa, hakujua ni kwa namna gani angeweza kuzungumza mbele ya macho yake.
Kwanza alikuwa msichana, mwenye aibu kubwa, kumfuata mwanaume na kumwambia alimpenda, alitaka sana kuwa naye lilionekana kuwa suala gumu sana, tangu azaliwe huko Iringa hakuwahi kumsikia mwanamke akimfuata mwanaume na kumwambia alikuwa akimpenda, sasa kwa sababu gani yeye amfuate?
“Wakati mwingine si nijitoe tu jamani!” alijiambia.
Alikuwa na moyo wa kusitasita, kumfuata Edmund lilionekana kuwa suala gumu kupita kawaida. Kila siku kazi yake ilikuwa ni kumwangalia tu, alitamani hata kuwaambia marafiki zake, hasa rafiki yake kipenzi aliyeitwa kwa jina la Lilian lakini alishindwa.
“Halafu wiki nzima hii nakuona unamwangalia sana kaka wa watu!” alisema Lilian, msichana aliyetoka mkoani Singida.
“Nani? Mimi?”
“Ndiyo! Unamtaka?”
“Walaaaa!”
“Unampenda?”
“Akuuuu!”
“Sasa mbona unamwangalia hivyo?”
“Huwa namfananisha na mtu!”
“Nani? Mpenzi wako?”
“Jamaniiiiiiiii”
“Sema! Huku Dar nasikia watu wanafunguka tu, ukimtaka mtu mwambie, ndiyo nimesikia maisha yao ya huku,” alisema Lilian huku akitoa tabasamu.
“Sasa ungekuwa wewe ungekwenda kumwambia?”
“Mwaego! Ningewezaje? Nionekane malaya!”
“Kwani kumwambia mwanaume unaonekana malaya?”
“Kwa mtazamo wa watu wengine!”
“Mtazamo wako?”
“Hebu tuachane na hayo!” alisema Lilian na kuanza kucheka, akalipotezea swali hilo kwani tayari lilionekana kuwa gumu.
Kama ni mgonjwa basi Esta alikuwa mahututi, hakujiweza kwa Edmund, ilikuwa ni sawa na mgonjwa aliyeumwa sana na hatimaye kufikishwa kwenye chumba cha ICU na kusubiri muujiza wa Mungu ili atoke na kutembea tena.
Kila siku Lilian alikuwa na kazi ya kumuuliza kama alimpenda Edmund lakini msichana huyo alikataa kwa kumwambia alikuwa akimfananisha tu. Lilian alijua kabisa rafiki yake hakuwa anajiweza kwa Edmund, hivyo alichokifanya ni kuamua kumfuata kwa lengo la kumwambia.
“Nakwenda kumwambia!”
“Kumwambia nani?”
“Edmund!”
“Kwamba?”
“Unampenda. Umeoza kwake!”
“Weeeeeeee!”
“Nakwenda!” alisema Lilian.
Hakutaka kusubiri, akainuka na kuanza kumfuata. Esta alikuwa akiogopa, alimwangalia Esta alivyokuwa akipiga hatua kumfuata Edmund, hakutaka hata kusubiri, haraka sana akainuka na kuondoka darasani haraka sana.
Aliogopa kupita kawaida, ni kama mtu ambaye alikuwa akianza kupenda kwa mara ya kwanza, ni kama alikuwa bikira kumbe haikuwa hivyo.
Kwake, kusimama mbele ya Edmund na kuzungumza naye lilikuwa jambo lisilowezekana, breki ya kwanza ilikuwa bwenini, mapigo ya moyo yalikuwa yakimdunda mno.
Huku nyuma Lilian alimfuata Edmund na kumsalimia, alikuwa peke yake, alisimama na kumwangalia usoni, alipoyapeleka macho yake mahali alipokuwa Esta, msichana huyo hakuwepo.
“Karibu!” alisema Edmund huku akimwangalia Lilian.
“Nimekaribia! Nimekuja na ujumbe wako!” alimwambia.
“Ujumbe gani?”
“Kuna rafiki yangu anakupenda sana!”
“Rafiki yako ananipenda?”
“Ndiyo! Ila anaogopa kukwambia. Naona anateseka sana juu yako, nimekuja kumsaidia,” alimwambia.
Edmund akanyamaza, akainama na kujifanya kuwa na mawazo huku kichwa chake kikifikiria ni kwa namna gani alitakiwa kumwambia msichana huyo. Kwanza hakumfahamu msichana aliyekuwa akimtaka lakini la pili alimfikiria sana Angelina.
Alimpenda msichana huyo, kwake alikuwa kila kitu, tangu akiwa shuleni alimwambia asingemsaliti lakini kuna kipindi alishindwa, alimsaliti kwa siri sana.
Kama kulikuwa na mtu aliyekuwa akimpenda chuoni hapo, hakutaka kuwa naye kwa sababu aliamini mwaka unaofuata basi naye Angelina angekuwa hapo, sasa ingekuwaje endapo angesikia mpenzi wake alikuwa na uhusiano na msichana mwingine.
“Kunipata mimi ni ngumu sana,” alimwambia Lilian.
“Kwa nini?”
“Nina mpenzi wangu!”
“Ila yeye anasema hajawahi kukuona naye!”
“Amesema yeye ama unasema wewe?” aliuliza huku akiwa na tabasamu.
“Aya! Basi tunasema sisi kwamba hatukuwahi kukuona na mpenzi wako!” alimwambia, wote wakaanza kucheka.
“Wewe una mpenzi?”
“Ndiyo!”
“Mbona hatujawahi kukuona naye?”
“Jamani! Kwani yupo hapa?” aliuliza, Edmund hakulijibu swali hilo, akacheka kidogo, kicheko kilichomfanya Lilian kujua hilo swali aliloliuliza lilikuwa sawasawa na lile lililokuwa kwa Edmund.
“Naomba umsaidie rafiki yangu, hata kuongea naye tu, inatosha,” alimwambia.
“Yupo wapi?”
“Nadhani amekimbia!”
“Amekimbia?”
“Yeah! Anakuogopa!”
“Basi naomba ukamwambie nahitaji kuzungumza naye sasa hivi!” alisema Edmund, haraka sana Lilian akaondoka.
Yeye mwenyewe hakujiamini kama ndiye aliyekuwa amezungumza maneno hayo kwa Edmund, alijiamini sana na alipoondoka moyo wake ulikuwa umetulia sasa, alikuwa kwenye wakati mgumu mno.
Alifanya hivyo kwa ajili ya rafiki yake, alimpenda, alimuona jinsi alivyokuwa akiteseka, hakutaka kuona hilo likimtokea na ndiyo maana aliamua kufanya hicho alichokifanya. Baada ya kufika bwenini, akamkuta Esta.
“Niambie imekuwaje?” aliuliza Esta harakaharaka.
“Unaitwa!”
“Na nani?”
“Edmund!”
“Kwani umemwambia kweli?”
“Ndiyo! Amesema anataka kuongea nawe!”
“Hapana! Naogopa!”
“Jikaze! Esta! Hii ndiyo nafasi, ukishindwa hii, hutoipata tena nakwambia,” alimwambia.

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
Niwakumbushe tu kwamba simulizi hii inaendelea kupatikana WhatsApp kwa shilingi 5000 tu. Namba hizo hapo juu.
Kutongozeana na msimamo wa amon
 
Sehemu ya 22

Esta hakuwa na uwezo wa kumsogelea Edmund, bado hakuwa akijiamini hata kidogo. Alimwangalia rafiki yake huyo na kumwambia wazi hakujiamini hivyo asingeweza kumfuata Edmund na kuzungumza naye.
“Kwa hiyo utaendelea kuteseka hadi lini?”
“Lilian!”
“Nijibu kwanza!”
“Yaani!”
“Hebu twende!” alisema.
Baada ya kulazimishwa sana na kuona kweli hiyo ilikuwa nafasi yake ya kipekee, hakuwa na jinsi, ikambidi akubali na kuondoka na Lilian kuelekea huko alipokuwa Edmund.
“Ninaogopa! Lilian mwenzako naogopa!” alimwambia huku wakishuka ngazi.
“Kwani wewe ni bikira?”
“Hapana!”
“Sasa unaogopa nini? Kuna kitu gani kigeni kwako?” alimuuliza, Esta hakujibu maswali hayo, akabaki kimya, sasa wakashuka chini na kuelekea darasani, yaani japokuwa kulikuwa na joto kali Dar es Salaam lakini cha ajabu Esta alikuwa akitetemeka.
Walikwenda mpaka walipofika darasani, Esta akaangalia mbele, macho yake yakatua kwa Edmund aliyekuwa bize akifanya mambo yake, mapigo ya moyo yalikuwa juu kabisa, wakati mwingine alitamani hata kukimbia kwani kwa jinsi alivyomwangalia mwanaume huyo, alijua siku hiyo alikuwa akienda kudhalilishwa.
Wakapiga hatua mpaka alipokuwa Edmund na kumwacha Lilian azungumze, yeye ndiye alikuwa mzungumzaji mkuu mahali hapo. Alichomwambia ni kwamba aliyesimama hapo ndiye alikuwa Esta ambaye alimpenda ila aliogopa kumfuata na kumwambia ukweli.
Edmund akamwangalia Esta, ni kweli alikuwa mzuri, mwanamke fulani hivi aliyeumbika, sura ya kuvutia japokuwa kwa mbali alikuwa na ushamba fulani hivi kwani aina ya mavazi yake aliyovaa, ilikuwa ni vigumu kumuona mwanamke wa mjini akivaa hivyo.
“Esta! Mimi naitwa Edmund,” alisema Edmund huku akimwangalia msichana huyo, akampa mkono.
Kitendo cha kuushika mkono wa Edmund, Esta akahisi damu ikianza kuzunguka kwa kasi sana mwilini mwake, mapigo ya moyo yakazidi kudunda na kwa mbali kuhisi kama amepigwa na shoti ya umeme hivi.
Hakuwa na la kusema, yule mwanaume aliyekuwa akimtesa siku zote, aliyetamani sana hata kuonana naye na kuzungumza, leo hii alikuwa mbele yake, tena wakiwa wamesimama pamoja kwa lengo la kuzungumza.
“Naitwa Esta,” alisema msichana huyo, kwa mbali alionekana kuwa muoga.
“Aya niambie kile alichoniambia Lilian. Ninataka kusikia moja kwa moja kutoka kwako!” alimwambia.
Huo ulikuwa mtihani mzito kwa msichana huyo, asingeweza kumwambia alimpenda, yaani kumwambia hivyo ilikuwa ni sawa na kumtongoza, kwa mila za Kitanzania ambazo aliziamini ilikuwa ni marufuku kwa mwanamke kumtongoza mwanaume, yaani ilikuwa ni bora uzeeke bila kuolewa kuliko kuufumbua mdomo wako na kumwambia mwanaume ulikuwa unampenda sana.
Akamwangalia Lilian, kwa jicho alilomtazama tu lilikuwa lile la kuzungumza lililomwambia ‘Mwambie sasa mbona unaogopa! Nafasi hii hutoipata tena.’
“Hapana! Siwezi!” alijisemea.
Ni kweli alishindwa kumwambia jinsi alivyojisikia moyoni mwake, ulikuwa mtihani mzito kupita kawaida, alikaa kimya tu huku akijisikia aibu kupita kawaida, yaani mpaka akatamani kukimbia mahali hapo.
“Ameshindwa! Aya naomba niwaache! Kuna sehemu nawahi,” alisema Edmund, akaamua kuwaacha watu hao na kuondoka zake.
Lawama za Lilian kwa Esta zikawa kubwa, alikasirika kwa sababu tu rafiki yake alishindwa kumwambia Edmund vile alivyojisikia.
Wakati mwanaume huyo akipiga hatua kuondoka zake, Esta alitamani amsimamishe na kumwambia sasa kilekile alichomwambia amwambie lakini nafasi hiyo haikurudi tena.
Moyo wake ukawa na majuto mazito, alijiona mjinga sana kwa kushindwa kumwambia ukweli juu ya kile kilichokuwa moyoni mwake. Alitamani sana kuongea na mwanaume huyo aliyeusumbua moyo wake lakini kwa ujinga wake, akaipata nafasi hiyo akaichezea, alihisi asingeipata tena.
“Yaani umeniangusha kweli rafiki yangu!” alisema Lilian huku akimwangalia Esta, yeye mwenyewe alijiona kuzingua.
“Yaani acha tu! Nilikuwa naogopa!”
“Sasa ulikuwa unaogopa nini? Mbona unaleta habari za huko mikoani shoga’angu, hii Dar es Salaam bwana! Watu wanaishi kivyaovyao bila aibu,” alisema Lilian, naye akajifanya mtu wa Dar na wakati alitoka Singida, na alikuwa chuo mwaka wa kwanza, ila alikuwa mjanja kupindukia.
“Mimi sikufundishwa kumtongoza mwanaume!” alijitetea Esta.
“Kwani kumwambia mtu unampenda ni kumtongoza?”
“Lakini sijafundishwa hivyo!”
“Aya niambie wazazi wako walikufundisha nini!”
“Heshima!”
“Kwani kumwambia hivyo ungekuwa umemkosea heshima? Aya tazama Edmund amekwishaondoka, huko atakutana na mwanamke mwingine, atamwambia kile ulichoshindwa kumwambia, atamkubalia, watakuwa wapenzi na baadaye kuoana, halafu wewe upoupo tu kama mzimu,” alisema Lilian, kwa kile alichokifanya rafiki yake huyo hakika hakukipenda hata kidogo.
Moyo wa Esta ukanyong’onyea, kile alichokisema rafiki yake kilikuwa kweli kabisa, yaani huyo Edmund aliondoka zake, inawezekana kabisa huko angekutana na mwanamke mwingine na kumtongoza kisha kuwa wapenzi.
Akajiona mjinga miongoni mwa wajinga, akatamani dakika zirudi nyuma na kurekebisha kile alichokishindwa lakini alishindwa kufanya hivyo. Akaondoka zake na kuelekea bwenini, alipofika huko, kwanza akajilaza, kichwa chake kilikuwa na mawazo mengi tu.
Edmund alikitawala kichwa chake, hakujua ni kwa sababu gani, alihisi alilogwa, hakuwa hivyo kabla, ni kweli aliwahi kupenda lakini haikuwa kwa namna hiyo. Kipindi hicho, kile kilichokuwa moyoni mwake kilikuwa ni zaidi ya mapenzi, kilikuwa ni zaidi ya upendo.
Alimuomba sana Mungu ampatie Edmund, hakujua mwanaume huyo kama alikuwa na mtu ama la! Alichokuwa akikitaka ni kuwa naye kwa kuwa aliamini yeye ndiye alikuwa msichana pekee aliyetakiwa kuwa na Edmund.
Siku hiyo alikiri kufanya makosa, hakutaka kuona yakijirudia tena, sasa akatamani kutoka bwenini na kwenda kumtafuta Edmund mwenyewe, amuone na kumwambia kile alichoshindwa kumwambia.
Bwenini hakukukalika tena, akatoka na kuanza kuelekea nje, alishuka ngazi harakaharaka kama mtu aliyekuwa akiwahi kitu fulani cha maana sana, alitembea kama mtu aliyekuwa kwenye mashindano ya kutembea.
Alitembea mpaka sehemu ya maegesho ya magari, macho yake yakatua kwenye gari la Edmund, hilo lilimaanisha mwanaume huyo alikuwepo mahali hapo. Wala hakutaka kujichosha kwenda kumtafuta.
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kilikuwa kikubwa mno, aliamini endapo angekwenda sehemu fulani kumtafuta basi kulikuwa na uwezekano wa kupishana naye, hivyo kama kweli alitaka kuzungumza naye ilikuwa ni lazima amsubiri karibu na eneo hilo.
“Acha nikakae pale,” alisema na kuanza kupiga hatua kuelekea sehemu iliyokuwa maalumu kwa wanafunzi kukaa na kujisomea, tena akageukia upande uliokuwa na gari la Edmund.
Alitulia hapo huku akiwa na kimuemue cha kumuona kijana huyo, sasa moyo wake ulidhamiria kumwambia ukweli, ilikuwa ni lazima ateme cheche, amwambie kuhusu upendo wake kwake, jinsi ulivyomsumbua usiku kucha.
Alikaa hapo kwa dakika kama ishirini, kwa mbali akamuona Edmund akiwa anaelekea mahali lilipokuwa gari lake, haraka sana naye akasimama na kuanza kumfuata.
Mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu kama kawaida yake, alipiga hatua kumfuata lakini wakati mwingine alijiambia alikuwa akifanya ujinga sana, hakutakiwa kumfuata Edmund na kumwambia ni namna gani alikuwa akimpenda.
“Mungu nitie nguvu!” alisema Esta huku akiendelea kumsogelea mwanaume huyo.
Baada ya sekunde kadhaa akamfikia, kitu cha kwanza alichokitanguliza ni tabasamu pana ambalo aliamini ni lazima Edmund lingemchanganya na kuzungumza naye kwa uhuru zaidi.
Kama alivyotegemea, naye Edmund akatoa tabasamu pana na kuangaliana kwa sekunde kadhaa. Alishangaa kumuona msichana huyo mahali hapo, alikuwa akijiuliza alifuata nini kwani hakutetemea kabisa kumuona.
“Ni Esta vile?” alimuuliza huku akimwangalia.
“Yeah! Esta! Nilidhani ungenisahau,” alisema Esta huku akimwangalia Edmund.
“Nitamsahau vipi mwanamke anayenipenda? Nitawasahu wote lakini si wewe,” alimwambia msichana huyo maneno yaliyomfanya Esta kufurahi sana, hayohayo maneno yakamtia nguvu na kumwambia sasa nafasi ilikuwa yake, huyo Edmund alikwishalegea na kile kilichotangulia, kama mwanamke alitakiwa kufanya yake.
“Unaelekea wapi?” alimuuliza.
“Home! Unataka twende?” alimuuliza, ila swali lake lilikuwa na utani, hivyo naye hakutakiwa kulichukulia siriazi, alitakiwa kulichukulia utani kama alivyouliza.
“Yeah! Nataka twende nikalale hukohuko,” naye alitania, wote wakaanza kucheka.
Sasa kidogo wakazoeana. Kwa jinsi Esta alivyokuwa akiongea, hakuwa kama yule msichana aliyekuwa na aibu, sasa alikuwa akiongea kama msichana ambaye aliwahi kutolewa usichana wake, hivyo hakutakiwa kumuonea aibu mwanaume yeyote yule.
Waliongea kama kwa dakika tano hivi, Esta akaamua kuaga na kubadilishana namba za simu huku akimuahidi angemtafuta baada ya hapo. Hilo halikuwa tatizo, kila mmoja akafurahi na kuondoka zake.
Ni kweli Edmund alipendwa na Esta lakini kwake, mwanamke wa kwanza kabisa moyoni mwake alikuwa Angelina. Alimpenda msichana huyo, alikuwa kila kitu na muda mwingi alimuwaza kuliko kitu chochote kile.
Huyu Esta kwake hakuwa msichana mzuri wa kuwa naye, alikuwa wa kawaida sana na hakufika hata nusu ya wasichana ambao aliwahi kutembea nao. Edmund alizaliwa kwenye familia iliyokuwa na uwezo kifedha, alikutana na wasichana waliozaliwa kwenye familia kama yake wasichana warembo sana, hivyo kukutana na Esta kwake hakukumfanya kumuona mrembo kupindukia.
“Ushatoka shule?” aliuliza Edmund, aliamua kumpigia simu mpenzi wake, Angelina kwa lengo la kumfuata na kuzungumza naye kwani alimkumbuka.
“Ndiyo nipo njiani!”
“Nakuja! Nimekumisi sana!” alimwambia.
“Haina shida!”
Hayo yalikuwa maisha waliyoyazoea kuyaishi kila siku, walipenda kuonana na kusalimiana, kwa wapenzi kama wao yalikuwa maisha yaliyoyafanya mapenzi yao kudumu zaidi na zaidi.
Edmund hakutaka kuelekea nyumbani, kwanza ilikuwa ni lazima aende kumuona Angelina na ndipo hapo arudi nyumbani na kuendelea na mambo mengine. Hakuchukua dakika nyingi akafika mahali ambapo mara kwa mara alikuwa akionana na Angelina na kuanza kuongea.
Msichana huyo alionekana kuwa mrembo kila siku, alipendeza na hakuisha hamu machoni mwa Edmund. Walikaa na kupiga stori, kitu cha zaidi walichokizungumzia ni kudumisha mapenzi yao, wapendane zaidi ya walivyokuwa wakipendana kipindi cha nyuma.
“Natamani sana umalize shule uje chuo, nakuwa mnyonge sana aisee,” alisema Edmund huku akimwangalia msichana huyo.
“Ninatamani nije huko. Ninasoma sana na ninaamini Mungu ataniwezesha na kufaulu vizuri nije kukaa nawe mpenzi wangu,” alisema Angelina huku akimwangalia Edmund.
Siku hiyo walizungumza mambo mengi tu kama kawaida yao. Majira ya saa moja usiku, Edmund akaondoka na kurudi nyumbani kwao, sasa moyo wake ukaridhika, kitendo cha kuongea na mpenzi wake kikamfanya kuwa na furaha tele.
Hakutarajia kumuacha Angelina, alimpenda kwa mapenzi ya dhati, hakutaka kuona akiwa na msichana mwingine zaidi yake. Huku akiwa amezama kwenye mawazo kumfikiria mpenzi wake, mara picha ya Esta ikamjia kichwani mwake.
Msichana huyo mrembo, mpole na mwenye kaushamba fulani akaonekana kama kutaka kuchukua nafasi fulani hivi lakini kwa kuwa alikuwa na mpenzi wake ambaye walitengeneza ndoto nyingi pamoja, akaamua kuacha harakaharaka kumfikiria Esta, hakutaka kabisa aingie kichwani mwake, ni kweli alipendwa na msichana huyo lakini hiyo haikuwa sababu ya kumsaliti Angelina na kuwa na Esta.
“Kwanza wala siyo mzuri!” alisema Edmund huku akiamini kabisa kwamba kile alichokuwa akikizungumza hakikuwa kweli kabisa.

Je, nini kitaendelea?
Usikose sehemu ijayo.
 
Sehemu ya 23

Maajabu yalikuwa makubwa, kwenye kila mechi Amon na Gideon waliyokuwa wakicheza, walionyesha ni kwa namna gani walikuwa wachezaji hatari.
Bila kutarajia, baada ya kufanya mapenzi kwa siku ya kwanza, tayari Gideon na Anita wakaanza kuwa kwenye mahusiano ya siri.
Hapakuwa na mtu aliyejua kama Gideon alikuwa akitembea na bosi wa timu hiyo, kila walipokuwa wakizungumza walionekana kawaida kumbe nyuma ya pazi wawili hao walikuwa wakilala kitanda kimoja.
Kwa kipindi hicho Amon na Gideon walikuwa wakiishi hotelini, bado walikuwa wakifanyiwa mchakato wa nyumba ya kupanga. Kwa kuwa tayari alishalifaidi penzi la Gideon, Anita hakutaka kubanwa, haraka sana mchakato wa nyumba ukafanyika na wawili hao kupata nyumba kwenye mtaa wa Breonkol uliokuwa pembeni kidogo ya Berlin.
Sasa huko wakawa wanajiachia, hapakuwa na mwandishi wa habari aliyekuwa akijua kitu chochote kile, mapenzi yaliwaendesha wote wawili lakini kila siku Anita alimwambia Gideon ni lazima aonyeshe uwezo mkubwa uwanjani kwani hicho ndicho kitu pekee kilichompeleka katika timu hiyo.
Kwa kipindi hicho walikuwa vijana wa miaka kumi na saba lakini ilibaki miezi kama mitatu na kuingia miaka kumi na nane. Kwa kuwa Anita alikuwa akifahamu sana maisha ya wachezaji mpira, alichomwambia Gideon ni kuhusu kuwa na mawakala, walitakiwa kuwa na watu ambao wangewasimamia kwenye mikataba yao.
Gideon hakuwa akijua lolote lile, alichoomba ni kuunganishwa na wakala aitwaye Kenneth Paulsen kutoka nchini Denmark ili amuombe kuwa wakala wake kwenye masuala ya soka.
Paulsen alikuwa mmoja wa mawakala waliokuwa maarufu ambao walikuwa wakimiliki wachezaji wengi barani Ulaya. Mbali na mawakala maarufu kwenye soka kama Mendez na Raiola, basi mtu wa tatu aliyekuwa akifuata kwenye orodha ya mawakala hao alikuwa huyo Paulsen.
Paulsen aliijua pesa, alijua kucheza madili mengi ilimradi tu awe anaingiza pesa kwa njia alizokuwa akizifahamu yeye mwenyewe. Kila alipokuwa na mchezaji ambaye aliamini alikuwa maarufu na mwenye uwezo, alikuwa akiringa sana na kuhitaji malipo makubwa.
Timu zilizokuwa zikifanya naye biashara zilimzoea, hakuwa mwanaume mwepesi, alikuwa akijua kucheza faulo zote kwenye suala la usajili, ilikuwa rahisi kwake kukuletea mchezaji leo asubuhi, mkaongea na kukubaliana lakini inapofika usiku ukakuta kasajiliwa timu nyingine kwa sababu tu walitoa pesa ndefu kuliko wewe.
Aliwahi kuzibadilikia timu nyingi barani Ulaya, wengi hawakutaka kufanya naye biashara kwa kuwa walijua alivyokuwa na michezo mibovu lakini kwa kuwa naye alikuwa akimiliki wachezaji hatari, ilikuwa ni lazima kufanya naye tu kwani bila hivyo usingepata wachezaji wake.
“Nitampataje?” aliuliza Gideon.
“Subiri!” alisema Anita.
Haraka sana akampigia simu mwanaume huyo na kuanza kuzungumza naye, alichomwambia ni kwamba kulikuwa na ishu ya mchezaji walitaka kuzungumza lakini kwenye hilo kwanza walitakiwa kukubaliana.
Kama alivyokuwa Paulsen hata naye Anita alikuwa na tamaa ya pesa kwa kuwa alikuwa mfanyabiashara. Alitaka kumkabidhi Gideon kwake lakini mwanaume huyo alitakiwa kulipia kiasi cha euro mioni moja kwa kuamini kupitia mchezaji huyo hapo baadaye angeweza kuingia pesa ndefu.
Kwa hilo hakukuwa na tatizo, hiyo ilikuwa moja ya biashara iliyokuwa ikifanyika, yeye alinunua wachezaji vijana, aliingia nao makubaliano, baadaye aliwauza na kupiga pesa ndefu tu.
“Anajua?” aliuliza Paulsen, hakutaka kuuziwa wachezaji magarasa.
“Ni hatari sana!”
“Nani huyo?”
“Njoo utamuona!” alisema Anita.
Ni ndani ya dakika kadhaa tu Paulsen alikuwa nyumbani kwa Gideon kwa lengo la kuzungumza naye. Kitendo cha kumuona tu mwanaume huyo akapigwa na mshtuko, hakuamini kama alikuwa akiitwa na Anita kwa lengo la kwenda kuunganishwa na Gideon.
Alimfahamu kijana huyo, yeye na Amon walikuwa ni habari ya mjini, kwa kila kitu walichokuwa wakikifanya kilikuwa kikubwa, walitawala kuanzia mitandaoni, magazetini na hata kwenye televisheni.
“Mtu mwenyewe ndiye huyu?” aliuliza Paulsen.
“Ndiyo! Euro milioni mbili zipo?” aliuliza Anita.
“Zimekuwa mbili tena?”
“Kama hutaki acha nimpigie simu Mendez, najua yule hata tano atanipa,” alimwambia.
Hilo halikutakiwa kufanyika, kwake, huyo Gideon alionekana kuwa muhimu sana, kumlipa Anita kiasi cha euro milioni mbili ambazo zilikuwa ni zaidi ya shilingi bilioni nne hapakuwa na tatizo lolote lile kwa kuwa aliamini baadaye angevuna pesa ndefu na kubwa zaidi ya hizo.
Wakakubaliana kwa kuingia mkataba wa siri na kuzungumza na Gideon na kumwambia mara tu baada ya kufikisha miaka kumi na nane, basi kila kitu kitakuwa kwake, hakutakiwa kuzungumza na mtu yeyote kuhusu mikataba yake, iwe ya matangazo, viatu, picha na mingineyo, angemwachia yeye kwa kuwa aliijua biashara hiyo.
Gideon hakujua kama tayari Anita alipata mgawo wake, hakujua mambo hayo kwani hakuelewa chochote kile kilichokuwa kikiendelea kwenye mpira hasa wa Ulaya.
Wakati akisindikizwa na Anita, Paulsen akawa na uhitaji wa kuzungumza naye jambo moja ambalo alihitaji sana kusaidiwa kwa kuwa tu tayari alisaidiwa kwa Gideon.
“Jambo gani?”
“Nina euro milioni kumi hapa!” alimwambia.
“Oh! Za nini?”
“Nataka uniunganishe na yule mwenzake huyu Gideon!” alimwambia.
“Nani? Amon?”
“Ndiyo!”
“Yule kumi ndogo. Nataka kumi na mbili!” alimwambia.
“Lakini mbona unakuwa na tamaa hivi aisee!”
“Mimi tena nishakuwa na tamaa?”
“Hahaha! Kwani ukiniunganisha naye kuna nini?”
“Kwani mimi nimekataa?”
“Kumbe!”
“Tukubaliane kwenye pesa!”
“Basi haina shida.”
Kuunganishwa na Amon hapakuwa na tatizo lolote lile, alichokifanya Anita ni kumpigia simu na kuanza kuzungumza naye. Akaomba waonane nyumbani kwake kwani kulikuwa na kitu walitakiwa kuzungumza. Kwa kuwa aliheshimika, Amon akakubali na hatimaye watatu hao kuonana.
Akaanza kuzungumza naye kuhusu mambo ya mpira, kazi za mawakala na mambo mengine ya kutengeneza pesa. Alimsikiliza kwa makini sana, alipomaliza, akataka kumsikiliza Amon kile ambacho angemwambia kuhusu uamuzi wake baada ya kusikia kuhusu suala hilo.
“Nimekwishapata wakala,” alimwambia Anita, akaonekana kushtuka.
“Wakala gani?”
“Anaitwa James,” alimjibu, wawili hao wakaangaliana.
Kwenye maisha yao hawakuwahi kumsikia wakala wa mchezaji yeyote akiitwa kwa jina la James, ni kwa mara ya kwanza walimsikia kutoka kwa Amon, wakamuuliza ndiye alikuwa nani naye akajibu alikuwa kaka yake.
Hakutaka pesa zao ziende sehemu nyingine, kaka yake alikuwa na kazi ya udalali wa nyumba nchini Tanzania hivyo alitaka kuyabadilisha maisha yake na kumpa uwakala kwa ajili ya kusimamia mambo yake ya mpira.
“Ndiye nani?”
“Kaka yangu! Yeye ni wakala wangu, kama ilivyokuwa Ronaldinho kwa kaka yake,” alijibu Amon huku akiwaangalia watu hao.
“Una uhakika ataweza kukusimamia?”
“Nina uhakika! Ataweza tu. Kule Tanzania kuna madalali wenye maneno mengi sana, nadhani kaka yangu ni mmoja wa madalali hao, wanajua sana kuongea,” alimwambia.
Majibu yake yakamchosha kila mtu mahali pale, kile walichokuwa wakikitaka kikagonga mwamba, huyu Amon alionekana kufahamu mambo mengi ya mpira kuliko hata Gideon. Paulsen alihuzunika sana lakini hakuwa na jinsi, akakubali kwa kilichotokea na kuondoka zake.
Siku hiyohiyo Amon akampigia simu James na kumwambia alitakiwa kwenda nchini Ujerumani kwani kulikuwa na kitu, James hakutaka kusubiri, haraka sana akajiandaa na siku chache baadaye alikuwa nchini humo.
Alikuwa akizungumza na mdogo wake, Amon, alimwangalia, Amon alibadilika, hakuwa kama alivyokuwa, alikuwa na mwili uliojengeka sana kimazoezi, alikuwa na ngozi nzuri, yaani kwa kifupi endapo ungemuona kwa mara ya kwanza ungesema jamaa alikuwa na pesa lakini pia alikuwa na mwili wa mazoezi.
“Ninataka uwe wakala wangu!” alisema Amon huku akimwangalia James.
“Niwe wakala wako?”
“Ndiyo! Hii ni kazi ambayo itabadilisha maisha yako, maisha ya familia na hata ukoo wetu mzima,” alimwambia.
“Nitaanzaje sasa?”
“Usijali! Utafahamu kila kitu!” alimwambia.
Kwa James hapakuwa na tatizo kubwa lakini pia alitakiwa kujifunza mengi kuhusu hao mawakala, hakutaka kufanya mambo kwa kukurupuka tu, Amon akamuitia watu waliokuwa na uzoefu wa mambo hayo na kuanza kumfundisha, walitaka awe wakala mkubwa hapo baadaye.
Wakati hayo yakiendelea, mechi zilikuwa zikiendelea kama kawaida. Hertha Berlin ilionyesha maajabu, walicheza mechi kumi na mbili, walishinda mechi hizo zote, tena kwa mabao mengi huku Amon akiongoza orodha ya wafungaji bora akiwa na mabao ishirini na nne akifuatiwa na Gideon aliyekuwa na mabao kumi na sita.
Mabao hayo yakawaambia watu kuwa mtu huyo alikuwa mwiba mkali, hakuwa mtu wa masihara hata kidogo, alipokuwa mbali uwanjani alionekana kama wa kawaida ila alipokuwa akilisogelea goli alionekana kuwa msumali wa moto kwa wapinzani wake.
Ilipofika mwezi wa kwanza, hatimaye mashindano ya Afrika yalitakiwa kuanza, wakati huo nayo Tanzania ilifuzu kucheza mashindano hayo makubwa barani humo, kutokana na kuibuka kwa wachezaji wakubwa wawili, Amon na Gideon, kila mtu akataka kuyaona maajabu yake kwenye timu ya Taifa ya Tanzania.
Haraka sana kikosi kikatangazwa na wachezaji hao wawili kujumuishwa, siku hiyo Amon alitumia muda mwingi kuzungumza na Gideon kuhusu suala lake la kuichezea Tanzania lakini mwanaume huyo alikataa katakata.
Amon hakuwa na jinsi, alipelekewa watu wengi kuzungumza naye, aliwakatalia kwa kuwaambia msimamo wake mkubwa ulikuwa ni kuichezea Tanzania na si timu nyingine kwa kuwa wazazi wake wote wawili walitoka nchini humo.
Hapakuwa na mtu aliyemzuia, aliyemtaka abaki mpaka mwenyewe kukasirika, wakaamua kuachana naye na hivyo kuondoka kuelekea Tanzania ambapo baada ya kukutana na rais, basi wangezungumza kidogo na kuelekea nchini Morocco kwa ajili ya mashindano hayo.
Watanzania walishangaa kuona Amon amerudi peke yake, Gideon hakuwepo. Walihisi labda wikiendi hiyo kulikuwa na mechi kali kwani kwa mfumo wa Chama cha Soka cha Afrika, kipindi hicho mashindano yao yalikuwa yakifanyika mwezi Januari, muda ambao ligi mbalimbali barani Afrika zilikuwa zikiendelea.
“Mbona Gideon anacheza mechi ya leo Ujerumani, yeye hakuja?” aliuliza jamaa mmoja baada ya kuona kikosi cha Timu ya Hertha Berlin na kumuona Gideon.
“Hata mimi nashangaa!”
Hiyo ndiyo ilikuwa habari kubwa nchini Tanzania, kwa kitendo cha Gideon kukataa kuichezea Tanzania kilimuumiza kila mmoja. Hawakuamini kama kijana huyo aliikataa nchi yao kwa sababu ya Ujerumani, wengi walilalamika lakini mwisho wa siku wakatakiwa kukubaliana na hali hali, Gideon hakuwepo.
“Ila Amon si yupo? Huyu jamaa ni wa muhimu kuliko Gideon,” alisema jamaa mwingine.
Huo ndiyo ulikuwa ukweli wenyewe, Amon alikuwa tishio sana kuliko hata Gideon. Kuvuma kwa Gideon kulisababishwa na Amon ambaye alimpa pasi nyingi za mabao, yaani kwa kifupi Amon alikuwa na uwezo wa kutamba peke yake bila Gideon ila Gideon hakuweza kutamba bila Amon.
Kwa nchini Ujerumani, kumpata Gideon kwao ilionekana kuwa si tatizo kwa sababu mwanaume huyo alilijua sana goli, walifurahi sana japokuwa waliona furaha yao ingekamilika zaidi endapo tu wangefanikisha kumpata na Amon.
Kwa kipindi hicho kila mchezaji wa timu yoyote Afrika alikuwa akiiogopa Tanzania, kuiogopa nchi hiyo ilikuwa ni kwa sababu ya Amon tu. Mwanaume huyo alikuwa na uwezo wa kubadilisha matokeo muda wowote ule, timu ilipokuwa na matokeo mabaya, alikuwa na uwezo wa kuamua hiyo mechi.

Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 24

Angelina alikuwa bize na mambo yake, hakuwa mtu wa mpira, hata baada ya kaka yake kuelekea nchini Ujerumani hakutaka kabisa kuangalia mpira kwa kuwa hakuwa akiupenda tu. Alikuwa bize na masomo yake lakini wakati mwingine alikuwa akikutana na mpenzi wake, Edmund na kufanya mambo yao.
Wakati akiwa nyumbani kwao siku moja ya Jumamosi, mara simu yake ikaanza kuita na haraka sana akaamua kuipokea baada ya kuona mpigaji alikuwa Edmund. Mwanaume huyo aliongea huku akionekana kushangazwa na kile kitu alichotaka kumwambia mahali hapo.
“Angelina! Hivi huyu siyo yule jamaa aliyetufuata kwenye gari?” aliuliza Edmund.
“Jamaa gani?”
“Nimekutumia picha yake! Hebu mcheki,” alimwambia.
Haraka sana Angelina akainia Whatsapp kwa lengo la kuangalia picha hiyo, alipoifungua tu, macho yake yakatua kwa Amon aliyekuwa kwenye jezi ya Hertha Berlin. Moyo wake ukapiga paa, hakuamini alichokuwa akikiona. Kitu cha kwanza kabisa alitaka kufahamu kilichotokea.
Haraka sana akaifungua timu hiyo ambayo iliandikwa ndiyo aliyokuwa akichezea Amon na kuanza kuiangalia. Aliziona picha za Amon akiwa na kaka yake, Gideon wakiwa wanashangilia. Hakujua ni kitu gani kilitokea mpaka Amon kwenda nchini Ujerumani.
Hakuwa amewasiliana naye kwa kipindi kirefu, hakujua kuhusu mwanaume huyo na kaka yake alipoondoka kuelekea Ujerumani, hakuzisikia tena taarifa za mwanaume huyo. Leo hii alikuwa akionyeshwa Amon akiwa kwenye jezi ya timu hiyo, hakika ilimshangaza. Alijisahaulisha kwamba Gideon alikwishawahi kuwaambia kwamba Amon alikataa kusajiliwa mpaka asajiliwe yeye.
Hakutaka kukubali, ilikuwa ni lazima ajue kilichotokea, ni kwa sababu gani mwanaume huyo alikuwa nchini Ujerumani, je, Gideon aliamua kumuunganishia dili hilo ama ilikuwaje. Akaamua kumuuliza baba yake.
“Amon ni rafiki wa kweli kabisa,” alisema baba yake.
“Kwa sababu gani?”
“Bila yeye Gideon asingekuwa Ujerumani!”
“Kivipi?” aliuliza.
Baba yake akaanza kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea. Angelina alibaki kimya akimsikiliza, kile alichoambiwa ni kama hakikuingia kichwani mwake. Huyo Amon alimfanyia wema kaka yake kwa kuwa hakutaka kuona akiishi maisha yale aliyokuwa akiishi tena, alitaka kuyabadilisha maisha yake kwa kumwambia mkurugenzi wa timu hiyo asingehamia timu yao kama tu wasingemchukua Gideon.
Wema wa Amon ulikuwa ni kama mkuki moyoni mwa Angelina, hakuamini pamoja na kumfanyia ubaya wote huo lakini bado aliamua kumsaidia kaka yake kupata maisha mazuri, hakulipiza kisasi kama ambavyo watu wengine wangefanya.
Anita akaona haiwezekani, ilikuwa ni lazima kupata taarifa zaidi kuhusu Amon, akaanza kufuatilia kwenye mitandao mbalimbali na kugundua huyo Amon hakuwa yule aliyekuwa kipindi cha nyuma, alikuwa mtu mwingine kabisa, mwenye mafanikio, maarufu ambaye kila alipokuwa akipita mitaani, watu walitaka kusainiwa vitabu vyao.
Ilimshangaza sana, ni kama alikuwa haamini alichokuwa akikiona. Alimkumbuka Amon, vile alivyokuwa, alivyompenda na kumuumiza, hakujua kama mwisho wa siku angekuja kuwa maarufu kama alivyokuwa.
Hapo ndipo akakumbuka kile alichoambiwa na Amon kwamba piga ua ilikuwa ni lazima kuwa mchezaji mkubwa duniani, mwanaume huyo aliishi kwenye ndoto zake na muda huo alikuwa akizitimiza. Moyo wake ukaanza kujisikia hukumu, kwa kile alichomfanyia Amon sasa hapo ndiyo akaanza kujua ulikuwa ujinga mtupu.
Amon alilia sana, aliteseka kwa ajili yake, aliomba kutokuachana naye lakini hakujali, akaachana naye na mwisho wa siku kijana huyo kuwa na mafanikio makubwa. Kila kona nchini Tanzania watu walikuwa wakimfuatilia Amon, alionekana kuwa nembo ya Tanzania, vijana wengi wakatamani kufanikiwa na kuwa kama Amon.
Kwa sifa zile alizokuwa akipewa na mambo mengine kwa Angelina yalikuwa yakimuumiza, aliyasoma mitandaoni na kujikuta akiumizwa na kutamani kulia, kilichomtesa ni kwamba hakuachana na Amon kwa wema, yaani alimwacha kama kumkomoa na mwisho wa siku maisha ya mwanaume huyo yalibadilika kabisa. Huku akiwa na mawazo lukuki, mara simu yake ikaanza kuita tena, akaangalia kioo, mpigaji alikuwa Edmund, akapokea.
“Hivi ndiye yule kijana ama?” aliuliza Edmund.
“Ndiye yeye!”
“Imekuwaje tena?”
“Alikuwa anacheza mpira, nafikiri amepata nafasi kuchezea huko alipokuwa,” alimwambia.
“Daah! Jamaa ana bahati sana,” alisema Edmund na kukata simu.
Moyo wa Angelina haukuwa na furaha juu ya mafanikio ya Amon, hilo lilikuwa ni kama tusi kubwa kwake. Alimwacha kwa nia nzuri sana lakini mwisho wa siku mwanaume huyo akaanza kufanikiwa, hii ilikuwa na maana gani? Kwamba yeye alikuwa kama mkosi kwa Amon.
Alijifungia chumbani kwake akiwa kwenye majonzi makubwa, hakuwa na la kufanya zaidi ya kukubaliana na kile kilichotokea, aliamini Mungu alipanga yeye kuwa na Edmund, inawezekana mwanaume huyo aliyekuwa naye angekuwa bora kuliko Amon.
Kwa upande wa pili chuoni Edmund alikuwa akiendelea na mambo yake kama kawaida. Kwa kipindi hicho kidogo tayari alikuwa na ukaribu na Esta, msichana ambaye alimwambia alimpenda lakini kwake akaamua kupuuzia.
Walikuwa marafiki wa kawaida, walikuwa wakionana na kuendelea na mambo yao kama kawaida. Kitu kikubwa kilichokuwa kikijengeka kwa Esta ni kuwa na Edmund tu, hakutaka kuwa na mwanaume mwingine zaidi ya huyo.
Huku maisha yakiendelea, ukaribu wake na Esta ukiwa mkubwa ndipo akaanza kuona utofauti mkubwa kati ya hao wasichana wawili. Esta alikuwa msichana mwenye adabu sana, aliyekuwa akijua kumthamini mtu, mtaratibu na mambo mengine.
Kwa upande wake, Angelina alikuwa tofauti na msichana huyo kwa baadhi ya mambo. Alijua alikuwa akimpenda lakini muda mwingine msichana huyo alionekana kuwa bize na sababu kubwa ikiwa ni ubize na masomo.
Kulikuwa na mambo ambayo hakutakiwa kusema kwa msichana yeyote yule kwa sababu kulikuwa na maisha ya tofauti kila kona. Angelina alikuwa huru kusema hakuwa akipenda ugali, alikichukia chakula hicho, ama hakupenda kitu fulani.
Kwa Edmund alichukia kauli hiyo kwa sababu alipokuwa akikua, maisha yao nyumbani hayakuwa ya kitajiri kama kipindi hicho, walikuwa masikini, waliokuwa wakila chakula chochote kile ambacho baba yake alibarikiwa siku hiyo. Kwa maneno ya Esta tayari yalionyesha picha nyingine mbaya kwa upande huo.
“Ila nitamrekebisha!” alijisemea.
Wakati akiendelea kuwa na Esta kwa karibu zaidi, ukaribu wake na Angelina ukaanza kupungua taratibu, kila alipokuwa akisema yupo bize na masomo, Esta alimpa muda wake, walitoka na kwenda sehemu mbalimbali, walishikana mikono na kuishi kama wapenzi ila kila walipokuwa wakiulizwa, walisema walikuwa marafiki tu.
“Huo urafiki ndiyo mpaka kushikana mikono!” alisema Lilian huku akionekana kushangazwa na alichokiona, yule Esta aliyekuwa akimfahamu hakuwa huyo, sasa hofu juu ya Edmund ilimuondoka kabisa.
“Hata mimi nashangaa!” alisema Esta na kuanza kucheka.
Urafiki uliendelea, kila mmoja kichwani mwake alijua yeye alikuwa rafiki kwa mwenzake ila baada ya Esta kuanza kumtembelea Edmund nyumbani kwao, akajua kabisa huo urafiki ulivuka mipaka.
Wakakaa chumbani huku wakiongea mambo mbalimbali. Esta alikuwa akiyashangaa maisha ya Edmund, alikuwa mtoto wa tajiri, alikuwa vilevile kama alivyokuwa akihisi kipindi cha nyuma. Maisha yale hakutaka kuyafikiria sana, alichokitaka zaidi ni kuwa na mwanaume huyo tu.
Humo chumbani wakaanza kuangalia muvi, kila mmoja alionekana kuwa na furaha tele, walifanya mambo machache na mwisho wa siku kuanza kushikana hapa na pale na kilichotokea baada ya hapo ni kubaki watupu kama walivyotoka matumboni mwa mama zao na kuanza kufanya mapenzi.
Edmund akamsahau Angelina, hakukumbuka kama alikuwa na mpenzi wake. Aliendelea kufanya na msichana huyo hata baada ya siku hiyo. Hilo likaufanya moyo wake kuanza kubadilika, sasa akaanza kumtoa Angelina moyoni mwake na kumuingiza huyo Esta kwa kisingizio cha kujaliwa kuliko hata alivyokuwa akijaliwa na Angelina.
“Nakupenda!” alisema Edmund huku akimwangalia Esta.
“Nakupenda pia!”
Uhusiano wao wa mapenzi ukaanza kunoga, kila siku walikuwa wakionana na kufanya mambo yao mengi, baadhi ya wanachuo waliokuwa wakiwafuatilia wakajua kabisa kama watu hao walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi hivyo walitakiwa kuachwa kama walivyokuwa.
Baada ya mwezi mmoja wa mahusiano, Esta akamwambia Edmund taarifa ambayo ilimshtua sana, alisikia dalili zote za kuwa na mimba. Edmund alivyoambiwa hivyo, kwanza hakutaka kuamini, aliogopa, suala la Esta kuwa na dalili za kuwa na mimba zilimshtua kupita kawaida.
“Umepima?”
“Bado!”
“Sasa kwa nini unahisi hivyo?”
“Yaani acha tu, naona dalili zote,” alimjibu.
Edmund hakutaka kukubali, alichomwambia ilikuwa ni lazima kwenda kupima, alitaka kujiridhisha kwa kile alichoambiwa, walipokwenda hospitali na Esta kupimwa, Edmund alibaki kwenye benchi huku akiwa na mawazo lukuki.
Hakuogopa kuwa na mtoto, kitu kilichokuwa kikimnyima furaha ni Angelina tu, nini kingetokea endapo msichana huyo angegundua alimpa mimba mwanamke mwingine?
Alikaa hapo kwa dakika kadhaa hatimaye Esta akatoka kwa daktari huku uso wake ukiwa na tabasamu pana. Hakujua kulikuwa na nini, lile tabasamu hakujua lilikuwa la furaha baada ya kugundulika alikuwa na mimba ama lilikuwa la furaha kujua hakuwa na mimba.
“Kuna nini? Niambie kuna nini mpenzi!” alisema Edmund huku akimwangalia Esta.
“Nina mimba ya wiki mbili na nusu!”
“Mimba ya wiki mbili na nusu?”
“Ndiyo!”
Edmund akashusha pumzi ndefu, alimwangalia Esta, kwa jinsi alivyoonekana kuwa na furaha, alijua lingekuwa suala gumu kumwambia akaitoe mimba hiyo, sasa akatakiwa kupambana kuhakikisha mimba hiyo inabaki salama.
Hakutaka kumwambia suala la kutoa kwa kuwa angediriki kusema hivyo basi moja kwa moja msichana huyo angejua hakuwa kwenye mapenzi naye, alitaka kumtumia tu.
“Mbona unaonekana huna furaha?” aliuliza Esta huku akimwangalia Edmund.
“Hapana! Kawaida tu. Imekuwa ni sapraizi kubwa sana kwangu,” alisema Edmund.
“Oh! Sawa,” alisema.
Hakutaka kuonyesha tofauti yoyote ile, ilikuwa ni lazima kumuonyesha msichana huyo kwamba alikuwa pamoja naye, yale mawazo aliyokuwanayo alitakiwa kuachana nayo na kuanza kufikiria namna ya kumpokea mtoto huyo.
Angelina alimuumiza kichwa chake, ilikuwa ni lazima amwambie ukweli juu ya kile kilichotokea lakini hakujua angeanzia wapi. Alifikiria suala hilo kwa dakika nyingi sana lakini hakuwa na la kufanya kabisa, aliona jambo zito kubwa mbele yake.
“Ila je, ningekuwa mimi angenionea huruma? Yule msichana lazima angeniambia tu kwamba hanitaki kama alivyomfanyia yule kijana,” alisema Edmund, sasa akaanza kutafuta njia.
“Alimkataa mbele ya macho yangu, tena jamaa alikuwa akilia sana, sasa kama alifanyiwa vile, huyu mwanamke atashindwa kunifanyia mimi?” alijiuliza.
“Hakika ataweza!” akajijibu.
“Ni lazima nimwambie ukweli, hata akiumia, kimpango wake, kwanza nitakuwa namlipia kisasi yule mshikaji,” aliongeza.

Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 24

Angelina alikuwa bize na mambo yake, hakuwa mtu wa mpira, hata baada ya kaka yake kuelekea nchini Ujerumani hakutaka kabisa kuangalia mpira kwa kuwa hakuwa akiupenda tu. Alikuwa bize na masomo yake lakini wakati mwingine alikuwa akikutana na mpenzi wake, Edmund na kufanya mambo yao.
Wakati akiwa nyumbani kwao siku moja ya Jumamosi, mara simu yake ikaanza kuita na haraka sana akaamua kuipokea baada ya kuona mpigaji alikuwa Edmund. Mwanaume huyo aliongea huku akionekana kushangazwa na kile kitu alichotaka kumwambia mahali hapo.
“Angelina! Hivi huyu siyo yule jamaa aliyetufuata kwenye gari?” aliuliza Edmund.
“Jamaa gani?”
“Nimekutumia picha yake! Hebu mcheki,” alimwambia.
Haraka sana Angelina akainia Whatsapp kwa lengo la kuangalia picha hiyo, alipoifungua tu, macho yake yakatua kwa Amon aliyekuwa kwenye jezi ya Hertha Berlin. Moyo wake ukapiga paa, hakuamini alichokuwa akikiona. Kitu cha kwanza kabisa alitaka kufahamu kilichotokea.
Haraka sana akaifungua timu hiyo ambayo iliandikwa ndiyo aliyokuwa akichezea Amon na kuanza kuiangalia. Aliziona picha za Amon akiwa na kaka yake, Gideon wakiwa wanashangilia. Hakujua ni kitu gani kilitokea mpaka Amon kwenda nchini Ujerumani.
Hakuwa amewasiliana naye kwa kipindi kirefu, hakujua kuhusu mwanaume huyo na kaka yake alipoondoka kuelekea Ujerumani, hakuzisikia tena taarifa za mwanaume huyo. Leo hii alikuwa akionyeshwa Amon akiwa kwenye jezi ya timu hiyo, hakika ilimshangaza. Alijisahaulisha kwamba Gideon alikwishawahi kuwaambia kwamba Amon alikataa kusajiliwa mpaka asajiliwe yeye.
Hakutaka kukubali, ilikuwa ni lazima ajue kilichotokea, ni kwa sababu gani mwanaume huyo alikuwa nchini Ujerumani, je, Gideon aliamua kumuunganishia dili hilo ama ilikuwaje. Akaamua kumuuliza baba yake.
“Amon ni rafiki wa kweli kabisa,” alisema baba yake.
“Kwa sababu gani?”
“Bila yeye Gideon asingekuwa Ujerumani!”
“Kivipi?” aliuliza.
Baba yake akaanza kumwambia kila kitu kilichokuwa kimetokea. Angelina alibaki kimya akimsikiliza, kile alichoambiwa ni kama hakikuingia kichwani mwake. Huyo Amon alimfanyia wema kaka yake kwa kuwa hakutaka kuona akiishi maisha yale aliyokuwa akiishi tena, alitaka kuyabadilisha maisha yake kwa kumwambia mkurugenzi wa timu hiyo asingehamia timu yao kama tu wasingemchukua Gideon.
Wema wa Amon ulikuwa ni kama mkuki moyoni mwa Angelina, hakuamini pamoja na kumfanyia ubaya wote huo lakini bado aliamua kumsaidia kaka yake kupata maisha mazuri, hakulipiza kisasi kama ambavyo watu wengine wangefanya.
Anita akaona haiwezekani, ilikuwa ni lazima kupata taarifa zaidi kuhusu Amon, akaanza kufuatilia kwenye mitandao mbalimbali na kugundua huyo Amon hakuwa yule aliyekuwa kipindi cha nyuma, alikuwa mtu mwingine kabisa, mwenye mafanikio, maarufu ambaye kila alipokuwa akipita mitaani, watu walitaka kusainiwa vitabu vyao.
Ilimshangaza sana, ni kama alikuwa haamini alichokuwa akikiona. Alimkumbuka Amon, vile alivyokuwa, alivyompenda na kumuumiza, hakujua kama mwisho wa siku angekuja kuwa maarufu kama alivyokuwa.
Hapo ndipo akakumbuka kile alichoambiwa na Amon kwamba piga ua ilikuwa ni lazima kuwa mchezaji mkubwa duniani, mwanaume huyo aliishi kwenye ndoto zake na muda huo alikuwa akizitimiza. Moyo wake ukaanza kujisikia hukumu, kwa kile alichomfanyia Amon sasa hapo ndiyo akaanza kujua ulikuwa ujinga mtupu.
Amon alilia sana, aliteseka kwa ajili yake, aliomba kutokuachana naye lakini hakujali, akaachana naye na mwisho wa siku kijana huyo kuwa na mafanikio makubwa. Kila kona nchini Tanzania watu walikuwa wakimfuatilia Amon, alionekana kuwa nembo ya Tanzania, vijana wengi wakatamani kufanikiwa na kuwa kama Amon.
Kwa sifa zile alizokuwa akipewa na mambo mengine kwa Angelina yalikuwa yakimuumiza, aliyasoma mitandaoni na kujikuta akiumizwa na kutamani kulia, kilichomtesa ni kwamba hakuachana na Amon kwa wema, yaani alimwacha kama kumkomoa na mwisho wa siku maisha ya mwanaume huyo yalibadilika kabisa. Huku akiwa na mawazo lukuki, mara simu yake ikaanza kuita tena, akaangalia kioo, mpigaji alikuwa Edmund, akapokea.
“Hivi ndiye yule kijana ama?” aliuliza Edmund.
“Ndiye yeye!”
“Imekuwaje tena?”
“Alikuwa anacheza mpira, nafikiri amepata nafasi kuchezea huko alipokuwa,” alimwambia.
“Daah! Jamaa ana bahati sana,” alisema Edmund na kukata simu.
Moyo wa Angelina haukuwa na furaha juu ya mafanikio ya Amon, hilo lilikuwa ni kama tusi kubwa kwake. Alimwacha kwa nia nzuri sana lakini mwisho wa siku mwanaume huyo akaanza kufanikiwa, hii ilikuwa na maana gani? Kwamba yeye alikuwa kama mkosi kwa Amon.
Alijifungia chumbani kwake akiwa kwenye majonzi makubwa, hakuwa na la kufanya zaidi ya kukubaliana na kile kilichotokea, aliamini Mungu alipanga yeye kuwa na Edmund, inawezekana mwanaume huyo aliyekuwa naye angekuwa bora kuliko Amon.
Kwa upande wa pili chuoni Edmund alikuwa akiendelea na mambo yake kama kawaida. Kwa kipindi hicho kidogo tayari alikuwa na ukaribu na Esta, msichana ambaye alimwambia alimpenda lakini kwake akaamua kupuuzia.
Walikuwa marafiki wa kawaida, walikuwa wakionana na kuendelea na mambo yao kama kawaida. Kitu kikubwa kilichokuwa kikijengeka kwa Esta ni kuwa na Edmund tu, hakutaka kuwa na mwanaume mwingine zaidi ya huyo.
Huku maisha yakiendelea, ukaribu wake na Esta ukiwa mkubwa ndipo akaanza kuona utofauti mkubwa kati ya hao wasichana wawili. Esta alikuwa msichana mwenye adabu sana, aliyekuwa akijua kumthamini mtu, mtaratibu na mambo mengine.
Kwa upande wake, Angelina alikuwa tofauti na msichana huyo kwa baadhi ya mambo. Alijua alikuwa akimpenda lakini muda mwingine msichana huyo alionekana kuwa bize na sababu kubwa ikiwa ni ubize na masomo.
Kulikuwa na mambo ambayo hakutakiwa kusema kwa msichana yeyote yule kwa sababu kulikuwa na maisha ya tofauti kila kona. Angelina alikuwa huru kusema hakuwa akipenda ugali, alikichukia chakula hicho, ama hakupenda kitu fulani.
Kwa Edmund alichukia kauli hiyo kwa sababu alipokuwa akikua, maisha yao nyumbani hayakuwa ya kitajiri kama kipindi hicho, walikuwa masikini, waliokuwa wakila chakula chochote kile ambacho baba yake alibarikiwa siku hiyo. Kwa maneno ya Esta tayari yalionyesha picha nyingine mbaya kwa upande huo.
“Ila nitamrekebisha!” alijisemea.
Wakati akiendelea kuwa na Esta kwa karibu zaidi, ukaribu wake na Angelina ukaanza kupungua taratibu, kila alipokuwa akisema yupo bize na masomo, Esta alimpa muda wake, walitoka na kwenda sehemu mbalimbali, walishikana mikono na kuishi kama wapenzi ila kila walipokuwa wakiulizwa, walisema walikuwa marafiki tu.
“Huo urafiki ndiyo mpaka kushikana mikono!” alisema Lilian huku akionekana kushangazwa na alichokiona, yule Esta aliyekuwa akimfahamu hakuwa huyo, sasa hofu juu ya Edmund ilimuondoka kabisa.
“Hata mimi nashangaa!” alisema Esta na kuanza kucheka.
Urafiki uliendelea, kila mmoja kichwani mwake alijua yeye alikuwa rafiki kwa mwenzake ila baada ya Esta kuanza kumtembelea Edmund nyumbani kwao, akajua kabisa huo urafiki ulivuka mipaka.
Wakakaa chumbani huku wakiongea mambo mbalimbali. Esta alikuwa akiyashangaa maisha ya Edmund, alikuwa mtoto wa tajiri, alikuwa vilevile kama alivyokuwa akihisi kipindi cha nyuma. Maisha yale hakutaka kuyafikiria sana, alichokitaka zaidi ni kuwa na mwanaume huyo tu.
Humo chumbani wakaanza kuangalia muvi, kila mmoja alionekana kuwa na furaha tele, walifanya mambo machache na mwisho wa siku kuanza kushikana hapa na pale na kilichotokea baada ya hapo ni kubaki watupu kama walivyotoka matumboni mwa mama zao na kuanza kufanya mapenzi.
Edmund akamsahau Angelina, hakukumbuka kama alikuwa na mpenzi wake. Aliendelea kufanya na msichana huyo hata baada ya siku hiyo. Hilo likaufanya moyo wake kuanza kubadilika, sasa akaanza kumtoa Angelina moyoni mwake na kumuingiza huyo Esta kwa kisingizio cha kujaliwa kuliko hata alivyokuwa akijaliwa na Angelina.
“Nakupenda!” alisema Edmund huku akimwangalia Esta.
“Nakupenda pia!”
Uhusiano wao wa mapenzi ukaanza kunoga, kila siku walikuwa wakionana na kufanya mambo yao mengi, baadhi ya wanachuo waliokuwa wakiwafuatilia wakajua kabisa kama watu hao walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi hivyo walitakiwa kuachwa kama walivyokuwa.
Baada ya mwezi mmoja wa mahusiano, Esta akamwambia Edmund taarifa ambayo ilimshtua sana, alisikia dalili zote za kuwa na mimba. Edmund alivyoambiwa hivyo, kwanza hakutaka kuamini, aliogopa, suala la Esta kuwa na dalili za kuwa na mimba zilimshtua kupita kawaida.
“Umepima?”
“Bado!”
“Sasa kwa nini unahisi hivyo?”
“Yaani acha tu, naona dalili zote,” alimjibu.
Edmund hakutaka kukubali, alichomwambia ilikuwa ni lazima kwenda kupima, alitaka kujiridhisha kwa kile alichoambiwa, walipokwenda hospitali na Esta kupimwa, Edmund alibaki kwenye benchi huku akiwa na mawazo lukuki.
Hakuogopa kuwa na mtoto, kitu kilichokuwa kikimnyima furaha ni Angelina tu, nini kingetokea endapo msichana huyo angegundua alimpa mimba mwanamke mwingine?
Alikaa hapo kwa dakika kadhaa hatimaye Esta akatoka kwa daktari huku uso wake ukiwa na tabasamu pana. Hakujua kulikuwa na nini, lile tabasamu hakujua lilikuwa la furaha baada ya kugundulika alikuwa na mimba ama lilikuwa la furaha kujua hakuwa na mimba.
“Kuna nini? Niambie kuna nini mpenzi!” alisema Edmund huku akimwangalia Esta.
“Nina mimba ya wiki mbili na nusu!”
“Mimba ya wiki mbili na nusu?”
“Ndiyo!”
Edmund akashusha pumzi ndefu, alimwangalia Esta, kwa jinsi alivyoonekana kuwa na furaha, alijua lingekuwa suala gumu kumwambia akaitoe mimba hiyo, sasa akatakiwa kupambana kuhakikisha mimba hiyo inabaki salama.
Hakutaka kumwambia suala la kutoa kwa kuwa angediriki kusema hivyo basi moja kwa moja msichana huyo angejua hakuwa kwenye mapenzi naye, alitaka kumtumia tu.
“Mbona unaonekana huna furaha?” aliuliza Esta huku akimwangalia Edmund.
“Hapana! Kawaida tu. Imekuwa ni sapraizi kubwa sana kwangu,” alisema Edmund.
“Oh! Sawa,” alisema.
Hakutaka kuonyesha tofauti yoyote ile, ilikuwa ni lazima kumuonyesha msichana huyo kwamba alikuwa pamoja naye, yale mawazo aliyokuwanayo alitakiwa kuachana nayo na kuanza kufikiria namna ya kumpokea mtoto huyo.
Angelina alimuumiza kichwa chake, ilikuwa ni lazima amwambie ukweli juu ya kile kilichotokea lakini hakujua angeanzia wapi. Alifikiria suala hilo kwa dakika nyingi sana lakini hakuwa na la kufanya kabisa, aliona jambo zito kubwa mbele yake.
“Ila je, ningekuwa mimi angenionea huruma? Yule msichana lazima angeniambia tu kwamba hanitaki kama alivyomfanyia yule kijana,” alisema Edmund, sasa akaanza kutafuta njia.
“Alimkataa mbele ya macho yangu, tena jamaa alikuwa akilia sana, sasa kama alifanyiwa vile, huyu mwanamke atashindwa kunifanyia mimi?” alijiuliza.
“Hakika ataweza!” akajijibu.
“Ni lazima nimwambie ukweli, hata akiumia, kimpango wake, kwanza nitakuwa namlipia kisasi yule mshikaji,” aliongeza.

Je, nini kitaendelea?
Ubaya ubaya mapenzi yanauma acha tuhh usiombe yakukute
 
Sehemu ya 25

Kwa mwaka huo ndiyo ambapo Chama cha Soka cha Afrika, CAF kilipotengeneza pesa kubwa kwenye haki ya kurushwa kwa mechi za mashindano hayo. Kwa mara ya kwanza Shirika la Televisheni la Sky kutoka nchini Uingereza ikaamua kununua haki za kuonyesha mechi za mashindano hayo.
Hawakuwahi kufanya hivyo kwa nchi za Afrika isipokuwa kipindi kile Afrika Kusini ilipoandaa mashindano ya Kombe la Dunia, walifanya hivyo kwenye ardhi ya Afrika kwa sababu tu lilikuwa kombe la dunia, mashindano ambayo yalikuwa chini ya FIFA.
Kwa kipindi hicho walijua kabisa Amon alikuwa na jina kubwa, jina lake kwa kipindi hicho lilikuwa kama lilivyokuwa la Lionel Messi ama Ronaldo, walijua kabisa endapo wangenunua haki za kuonyesha mashindano hayo basi wangetengeneza pesa kubwa, na hivyo ndivyo ilivyotokea.
Kila mmoja alitaka kuuona uwezo wa Amon akiwa na timu ya taifa ya Tanzania. Hawakuwahi kumuona akiichezea timu hiyo ila waliuamini sana uwezo wake kwamba alikuwa akienda kufanya vizuri mno. Kila mtu ambaye alikuwa na king’amuzi nchini Tanzania, akanunua kabisa kifurushi chake kwa lengo ya kuyafuatilia mashindano hayo kwa nguvu kubwa.
Siku ambayo Timu ya Taifa ya Tanzania ilipoingia nchini Morocco, waandishi wa habari walifika kwa wingi uwanja wa ndege, kila mtu alitaka kumuona huyo Amon. Kijana huyo alikuwa na mvuto mkubwa, alipendwa na kila kona alipapatikiwa na watu waliotaka kupiga naye picha.
Alikuwa na mvuto mkubwa na watu walisema kwenye mitandao ya kijamii kwamba Amon alikuwa mtu mweusi aliyependwa zaidi ya Mohammad Ali, Barack Obama na wengine, Amon alisimama juu yao kabisa.
Wakati ndege ilipotua na wachezaji kutoka ndani ya jengo la uwanja huo, tayari waandishi walijiandaa, walikuwa uwanjani hapo kabla ya saa tatu kuanzia muda huo, walikuwa radhi kupoteza muda wao na mambo mengine lakini kitu cha kwanza walitaka kumuona huyo Amon.
Pamoja na kuwa na waandishi hao, pia hapo kulikuwa na wananchi wengi waliokuwa na lengo la kumuona Amon. Ule uwezo wake ulikuwa ni wa maajabu, walitaka kumuona na kuhakikisha kama alikuwa binadamu kweli ama kilikuwa kiumbe fulani kilichotoka sayari ya mbali.
Wachezaji hao walipoonekana tu, watu wakaanza kupiga kelele za shangwe, kila mmoja akaanza kuliita jina la Amon aliyekuwa bize kusikiliza muziki kutoka kwenye simu yake ambayo aliiunganisha na earphone zake.
Hawakufanya jambo lolote lile zaidi ya kwenda ndani ya gari lao na kuondoka mahali hapo. Amon alikuwa kimya tu, hakutaka kuzungumza na mtu yeyote, alimfikiria sana Gideon, mwanaume huyo alionekana kweli kuichukia Afrika na hakutaka kusikia lolote lile kutoka kwenye bara hilo.
Safari kutoka hapo uwanjani iliendelea kuelekea hotelini, kila mmoja alichoka na alihitaji kupumzika. Hawakuchukua dakika nyingi wakafika hotelini. Kulikuwa na waandishi kama kawaida pamoja na raia wengine waliotaka japo kumuona Amon.
Mambo hayo zamani alikuwa akiyaona kwenye televisheni tu jinsi Ronaldo na Messi walivyokuwa wakibabaikiwa na mashabiki, wengi kuhitaji wasainiwe vitabu vyao na hata kuwapiga picha kwa karibu, leo, yale yote yaliyokuwa yakiwatokea watu hao, yalikuwa yakimtokea yeye.
“Mungu ni mkubwa sana, sikuwahi kufikiria kama kuna siku ningekuja kuishi hivi,” alisema Amon huku akiwa haamini kilichokuwa kikiendelea.
Hapo hotelini walifanyiwa kila kitu, kila mmoja alionekana kuwa na furaha mno, kwanza kucheza timu moja na Amon ilionekana kuwa kama bahati. Yaani walichotakiwa kufanya ni kuonyesha uwezo mkubwa ili wapate kununuliwa na timu mbalimbali barani Ulaya.
Kucheza timu moja na Amon ilimaanisha kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakienda kuziangalia mechi ambazo wangecheza, hivyo nao walikuwa na nafasi kubwa ya kufanya makubwa na kununuliwa na timu mbalimbali.
Kila mmoja akayapania mashindano hayo, kila mmoja akataka kuonyesha uwezo aliokuwanao, hapakuwa na mtu aliyetaka kuendelea kuchezea nchini Tanzania, kila mmoja alitaka kutimka na kuelekea Ulaya.
Nafasi ya Gideon ilichukuliwa na Ramadhani Karim, mshambuliaji hatari wa Timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam. Yaani huyo ndiye ambaye alitakiwa kuwaonyesha watazamaji kwamba hawakutakiwa kumfikiria Gideon, yeye alitosha kabisa kuichukua nafasi yake.
“Rama njoo tuongee,” alisema Amon huku akimwangalia Ramadhani ambaye alikwenda na kusimama pembeni yake.
“Hii ni nafasi yako ya kuonyesha uwezo wako,” alimwambia.
“Najua sana. Ninahitaji kuonyesha kile kilicho bora kabisa, nashukuru sana kwa kuwa utakuwa msaada mkubwa kwangu!” alisema.
“Usijali! Kuna mambo mengi ya kufanya ila kubwa zaidi ni moja,” alimwambia.
“Lipi mkubwa?” aliuliza, japokuwa alikuwa na umri mkubwa zaidi ya Amon lakini hakuwa na jinsi, alimuita tu ‘mkubwa’.
“Jiamini!” alimwambia.
Amon aliyakumbuka maneno ya kocha Robben ambaye aliwaambia nchini Ufaransa walipokwenda kucheza na Lyon kwenye mechi ya kirafiki, akayatamka maneno yaleyale aliyoambiwa kwa sababu yalimjenga na kumfanya hivyo alivyokuwa.
“Nitajiamini!”
“Jiamini bwana, hiyo ndiyo silaha yako!” alisisitiza.
“Haina shida. Nitajiamini!”
“Sawa.”
Baada ya kila kitu wachezaji wakapata muda wa kulala na asubuhi ilipofika tu haraka sana wakaelekea mazoezini na kuanza kufanya mazoezi. Kulikuwa na umati mkubwa wa watu waliokuwa wakifuatilia mazoezi hayo.
Morocco ilikuwa timu mwenyeji lakini cha kushangaza Tanzania ilipata watazamaji wengi kwenye mazoezi kuliko hata nchi mwenyeji. Iliwashangaza watu wengi lakini walitakiwa kukubaliana na kile walichokuwa wakikiona kwa kuwa kulikuwa na mtu aliyeitwa Amon, mwanaume aliyekuwa na mvuto kwa wafuatiliaji wengi wa mpira.
Wanamichezo hisia zao wakazihamishia nchini Morocco, kila mtu akataka kuona kile ambacho kingefanyika kwa Amon aliyekuwa tishio. Tanzania ilipangwa kundi B kukiwa na timu kama Ivory Coast, Tunisia na Benin.
Siku ziliendelea kukatika mpaka siku ambayo watu waliisubiri ikiwadia, siku ambayo Tanzania alikuwa akifungua mechi yao ya kwanza na Tunisia. Kila mtu aliukubali uwezo wa Waarabu hao, walikuwa wazuri, wana kasi lakini kila walipomkumbuka Amon, walijua mechi hiyo inawezekana ingekuwa na matokeo ya maajabu sana.
Kwa watu wanaobeti walishindwa kuipa timu gani, kwa Tunisia, ilikuwa timu kali, tena ilitisha sana kipindi hicho, tena ilikuwa mbabe kwa Tanzania zaidi ya mara nne lakini kila walipomfikiria Amon, waliona kabisa wasipokuwa makini walikuwa wakienda kupunwa pesa zao kizembe kabisa.
“Hivi mnaona Tunisia atashindwa kumpiga Tanzania?” aliuliza jamaa mmoja, alishikilia karatasi ya kubeti.
“Tatizo moja tu, leo Tunisia anacheza na timu mbili, kwanza Tanzania na pili Amon,” alijibu jamaa mwingine.
Kila mmoja alitaka kufanya alilotaka kufanya yeye, kwenye pesa hawakuangalia utaifa, walifanya kile kitu ambacho kila mmoja aliamini kingekwenda kumfanya kupata pesa.
Mechi ilipoanza, ilianza kwa kasi kama kawaida. Uwanja ulijaza watu wengi, wengi wao walitaka kumuona Amon, jinsi alivyokuwa akicheza, walizoea kumwangalia kwenye televisheni, leo hii walitaka kumuona kwa macho yao kabisa.
Kwa jinsi alivyokuwa akicheza tu ilionyesha alikuwa tofauti na wachezaji wengine, kwa jinsi alivyokuwa akikimbia na mpira, alivyoshambulia, alivyotumia akili yake na kufunga mabao, hakuna asiyetarajia hata baada ya mechi kuona Amon akiwa amefunga mabao matatu peke yake na kuibeba Tanzania.
Hilo ndilo walilolitaka watu, walihitaji kuona Tanzania ikishinda lakini kubwa zaidi Amon akifunga bao hata moja kudhihirisha uwezo wake mkubwa kwenye suala zima la kucheza mpira.
Magazetini, mitandaoni na sehemu nyingine siku hiyo ilikuwa ni Amon tu, hapakuwa na mtu aliyeamini kama kijana huyo angeipatia Tanzania ushindi mkubwa namna hiyo tena kwa timu ngumu kama Tunisia.
Kila mtu aliliimba jina lake, alikuwa mchezaji wa kipekee kuliko wote waliokuwa kwenye mashindano hayo. Waliporudi hotelini, haraka sana akachukua simu yake na kumpigia mpenzi wake, Jeniffer kwa lengo la kuzungumza naye na kumsalimia.
“Nina habari njema!” alimwambia.
“Habari gani?”
“Nina mimba!” alijibu msichana huyo.
Kwanza Amon akakaa kimya kwa sekunde kadhaa, ni kama hakuamini kile alichoambiwa. Hakutarajia, kama kulikuwa na sapraizi basi hiyo ilikuwa ya kwanza kabisa. Jeniffer kuwa na mimba lilikuwa jambo lililomshtua kidogo kwani kama hakulitegemea.
“Ni sapraizi kubwa sana kwangu!” alisema Amon huku akionekana kuwa na furaha.
“Nimefurahi sana! Hii ni ndoto yangu ya muda mrefu nizae mchezaji mpira kama wewe,” alisema Jeniffer.
Kila mmoja alikuwa na furaha yake, walizungumza mambo mengi kwa dakika kadhaa kisha kukata simu. Amon alibaki kimya, hakuamini alichoambiwa na msichana huyo, hakika hakuamini, alifurahi sana kusikia kama mpenzi wake alikuwa na mimba.
Sasa alitarajiwa kuitwa baba akiwa na miaka kumi na nane, kwake halikuwa tatizo hata kidogo kwani aliamini kuwa na Jeniffer ulikuwa ni uamuzi sahihi alioufanya kwenye maisha yake.
Baada ya hapo mashindano hayo yaliendelea mpaka baada ya mwezi mmoja na Tanzania kujikuta wakiingia fainali na Senegal na kuchukua kombe hilo kwa mara ya kwanza huku Amon akiweka rekodi ya kufunga mabao kumi na tano kwa mashindano hayo tu.
Safari ya kuelekea nchini Tanzania kama timu ikaanza, njiani kila mmoja alikuwa na furaha tele, hawakuamini kama walifanikiwa kulichukua kombe hilo. Njiani walikuwa wakiongea mambo mengi, kila mmoja alikuwa na ndoto yake na waliamini kila mmoja angekwenda kuishi ndani ya ndoto hiyo.
Baada ya ndege kutua uwanja wa ndege, macho yao yakatua kwa umati wa watu uliofika mahali hapo kwa lengo la kuwapokea. Zaidi ya watu milioni moja waliamua kujipanga barabarani kutoka uwanja wa ndege mpaka uwanja wa taifa walipotakiwa kufikia kabla ya kuendelea na mambo mengine.
Huko, pia kulikuwa na watu wengi, uwanja ulijaa na wengine walishindwa kupata nafasi hivyo walizuiliwa nje. Wakati basi lililobeba timu ya taifa likiingia, kila mmoja akaanza kulikimbilia, wenye simu zao wakazitoa na kuanza kupiga picha.
Kila mtu aliyekuwa mahali hapo alionekana kuwa na furaha tele kwamba hatimaye ile timu iliyokwenda nchini Morocco kwa lengo la kupambana hatimaye ilikuwa ikirudi Tanzania huku ikiwa na kombe hilo kwa mara ya kwanza.
Siku hiyo ilikuwa ni furaha kwa kila mmoja, wengi hawakuamini kama kweli Tanzania ilifanikiwa kuchukua kombe hilo. Sherehe kubwa ikafanyika, wachezaji wakaonyesha mbwembwe zao na kwa sababu ligi mbalimbali Ulaya zilikuwa zinaendelea, Amon akajipanga siku inayofuata aondoke na kurudi zake Ujerumani.
Huku akiwa kwenye nyumba yake mpya iliyokuwa Mbezi Beach na kaka yake, James, wakamsikia mlinzi akizungumza na mtu ambaye alitaka kuingia ndani ya nyumba hiyo kinguvu lakini kama alikataliwa.
Hawakujua alikuwa nani, akili zao ziliwaambia inawezekana alikuwa shabiki ambaye alifika mahali hapo kwa lengo la kuzungumza na Amon, ikiwezekana hata wapige picha za ukumbusho lakini Amon alipotoka kwa lengo la kumwangalia mtu huyo, hakuamini macho yake baada ya kumuona Angelina akizozana na mlinzi, alipomuona tu, akakurupuka kutoka kule alipokuwa mlinzi na kumfuata Amon kule alipokuwa.
Msichana huyo alibadilika, hakuwa kama alivyokuwa, alipungua, alionekana kuwa na mawazo lukuki. Alikuwa akilia kilio kilichojaa kwikwi, hakujua msichana huyo alihitaji nini kwani alikwishasahau kuhusu yeye, aliamua kuishi maisha yake mapya baada ya kuachwa naye, sasa alikuja kufanya nini?
“Angelina!” aliita huku akionekana kushangaa.
Kabla ya kuzungumza kitu chochote kile, Angelina aliendelea kulia, alionekana kutia huruma, machozi yalibubujika mashavuni mwake, kwa alivyoonekana tu, alitia huruma na inawezekana alikuwa amepitia maisha magumu, yenye maumivu kupita kawaida.
Mlango ukafunguliwa, James naye akatoka, macho yake yalipotua kwa Angelina, naye alionekana kushangaa, ilikuwa msichana huyo aje nyumbani hapo na wakati alimkataa mdogo wake na kumwambia wasijuane? Tena asimjuejue?

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom