Simulizi : Ukweli Wenye Kuuma (Painful Truth)

SEHEMU YA 74

alikuwa amechoka na alishindwa kuendelea kukimbia, akaanza kumfuata mwanamke mmoja ambaye alikuwa pembeni kwenye giza pamoja na mtoto wake huku akiwa na shuka kubwa, alichokifanya ni kuingia ndani ya shuka hilo.
“Naomba unifiche....” Andy alimwambia mama yule huku akijifunika shuka lile.
Masikio yake yote yalikuwa yakisikiliza ni kitu gani ambacho kingeendelea mahali hapo. Ghafla akaanza kusikia vishindo vya watu wakija, walipofika karibu na lile eneo alilokuwa yule mama wakasimama na kuanza kumwangalia mama yule huku wakionekana kuwa na wasiwasi.
“Sisi ni mapolisi” Mwanaume mmoja alimwambia mama yule ambaye tayari woga ulianza kumshika.
Alijiona kutokuwa na jinsi, kama angeulizwa kuhusiana na Andy, mwanaume ambaye alikuwa amemficha basi ni lazima angemtaja kwani katika maisha yake alikuwa akiwaogopa sana mapolisi. Kitu cha pili ambacho alikiona kwamba ni lazima angemfichua Andy kule alipokuwa ni kwa sababu alikuwa hamfahamu hata kidogo. Asingekuwa tayari kuingia katika matatizo na wakati mtu ambaye alikuwa amemficha hakuwa akimfahamu.
Maswali mengi yakaanza kujikusanya kichwani mwake, kwa nini yule mwanaume alikuwa akikimbizwa na mapolisi? Kwa nini aliamua kumfuata yeye pale alipokuwa na kuhitaji hifadhi? Je alikuwa raia mwema au si raia mwema? Na kama alikuwa raia mwema kwa nini alikuwa akikimbizwa na mapolisi? Kila swali ambalo alikuwa akijiuliza kichwani lilimpa jibu kwamba ilikuwa ni lazima amtaje Andy ambaye alikuwa amejificha katika shuka lake.
“Kuna mtu tulikuwa tunamkimbiza, umemuona mahali hapa?” Polisi mmoja aliuliza.
“Ndio” Mwanamke yule alitoa jibu ambao lilimfanya Andy ndani ya shuka lile kupigwa na mshtuko mkubwa.

Mapolisi walionekana kuchanganyikiwa mara baada ya kufika katika barabara ya lami karibu kabisa na shule ya Sekondari ya Kiislamu ya Kinondoni na kutokumuona Andy, mtu ambaye walikuwa wakimkimbiza. Wakajaribu kuangaia huku na kule lakini wala hakuonekana machoni mwao.
Hawakujua kama Andy alikuwa amechukua daladala na kuondoka katika eneo hilo au alikuwa amevuka barabara na kuelekea upande wa pili. Kila kitu ambacho walikuwa wakijaribu kujiuliza kwa wakati huo wakakosa jibu kabisa hali iliyowafanya kukata tamaa kabisa.
Walitaka kuondoka mahali hapo ila kabla ya kuondoka wakaamua kwenda kuwauliza madereva taksi ambao walikuwa karibu na eneo lile, walijua fika kwamba madereva wale ni lazima wangejua mahali ambapo Andy alikuwa ameelekea kwa wakati huo.
“Mnamaanisha jamaa aliyekuwa na mchanganyiko wa rangi?” Dereva mmoja aliuliza.
“Ndiye huyo huyo”
“Musa alimchukua hapa kwenda nae upande ule wa Kaskazini. Sasa sijui walikuwa wakielekea mjini, Oysterbay au Coco Beach, ila Musa alimchukua” Dereva mmoja alijibu.
“Musa ndiye nani?” Polisi aliuliza.
“Dereva teksi mwenzetu wa kitengo hiki”
“Tunaweza kumpata muda gani?”
“Mmh! Labda mumsubiri mpaka atakaporudi”
“Hamna namba yake ya simu?”
“Aliibiwa wiki iliyopita. Hana hata hamu ya simu. Unacheza na Manzese nini” Dereva alijibu.
 
SEHEMU YA 75

Mapolisi hawakutaka kuendelea kuongea nao, walichokifanya ni kuacha ujumbe kwamba walikuwa wakimhitaji Musa. Wakaacha namba zao za simu ili wapigiwe mara moja katika kipindi ambacho Musa atakuwa amerudi kutoka kule alipokuwa amempeleka Andy.
Saa moja usiku mapolisi walikuwa wakipigiwa simu na kuambiwa kwamba Musa alikuwa mahali pale ambapo alikuwa akipaki gari lake. Musa alipewa taarifa kwamba alikuwa akitafutwa na mapolisi ambao walikuwa wakitaka awe mahali hapo.
Ni ndani ya dakika kumi mapolisi wakafika mahali hapo na kisha kuonana na Musa ambaye muda wote alikuwa akionekana kukosa amani kabisa, kitendo cha kufuatwa na mapolisi kilionekana kumtia wasiwasi sana.
Akaanza kuulizwa maswali kadhaa kuhusu kazi ile ambayo alikuwa akiifanya huku lengo kubwa la mapolisi wale wakitafuta kuzoeana nae hata kabla hawajamuuliza kuhusiana na Andy ambaye alikuwa amemsafirisha mchana. Walichukua dakika tano kuuliza kuhusu kazi yake na ndipo walipoanza kumuuliza kuhusiana na Andy.
“Yule jamaa mwenye mchanganyiko wa rangi?”
“Ndio”
“Alikuja hapa huku akionekana kuwa na haraka na mwingi wa wasiwasi. Nilipomuuliza kuhusiana na hali yake, aliniambia kwamba moto ulikuwa ukiteketeza ofisi yake na hivyo alikuwa akielekea kule kuokoa mafaili yake muhimu” Musa alijibu.
“Kwa hiyo ulimchukua na kumpeleka wapi?”
“Hotelini?”
“Hoteli gani?”
“Serena”
Mapolisi hawakutaka maswali zaidi, walichokifanya kwa wakati huo ni kuondoka na Musa kuelekea katika hoteli hiyo ambapo baada ya kufika wakaagiza viywaji huku macho yao yakiwa yanaangalia kila kona mahali hapo.
Kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba usiku huo wangeweza kumuona Andy na hivyo kumkamata na kumfikisha katika vyombo vya sheria kwa tuhuma za kumuua Annastazia, spika wa Bunge ambaye alikuwa akikubalika sana.
Wala hawakukaa zaidi ya dakika kumi mara mbele yao akaonekana mwanaume mmoja ambaye kwa kumuangalia tu waliweza kumgundua kwamba alikuwa Andy, walichokifanya kwa wakati huo ni kuinuka na kuanza kumfuata.
Andy alikuwa akionekana kuwa na wasiwasi, muda wote alikuwa akiangalia huku na kule huku akionekana kuwa na wasiwasi mwingi. Mapolisi wale walikuwa wakimfuata, kadri Andy alivyokuwa akipiga hatua na ndivyo ambavyo alikuwa akizidi kuongeza kasi mpaka kufikia hatua ya kuanza kukimbia.
****
Ulikuwa ni msiba mkubwa ambao ulikuwa umeikumba nchi masikini ya Tanzania. Kila mwananchi ambaye alisikia kifo cha mwanamke ambaye alionekana shupavu, Spika wa Bunge, Annastazia Kapama akashindwa kuamini kile ambacho alikuwa amekisikia.
Watu wengi wakaonekana kuwa katika nyuso zilizojaa majonzi, kifo cha Annastazia kikaonekana kushtua kila mtu. Mitaani hakukukalika hata kidogo, watu walikuwa wakikizungumzia kifo cha Annastazia ambacho kilikuwa kimetangazwa masaa mawili yaliyopita.
Gazeti la Mlalahoi ambalo lilikuwa likitoka kila jioni likawa limeandika taarifa zile ambzo zilionekana kumshtua kila mtu siku hiyo. Gazeti hilo liliuza kopi nyingi sana nchini Tanzania kutokana na wananchi kulinunua kwa wingi sana siku hiyo.
 
SEHEMU YA 76

Kila mtu alitaka kufahamu chanzo cha mauaji hayo ambayo yalikuwa yametokea chumbani kwake. Taarifa juu ya mtu ambaye alikuwa ametoka nchini Canada, Killerandy zikapatikana na hapo ndipo watu wakafahamu kwamba huyo mtu ndiye ambaye alikuwa amefanya mauaji yale.
Taarifa hazikuishia hapo, zilielezea kila kitu kwamba mtu huyo ambaye alijifanya kuwa mfadhiri alikuwa amedanganya jina, jina lake halisi alikuwa akiitwa Andy Wayne ambaye alikuwa dokta mkubwa sana nchini Marekani. Alikuwa amezaliwa na mwanamke wa Kitanzania huku baba yake akiwa mzungu kutoka nchini Marekani.
Gazeti lile likaonekana kuendelea kumvutia kila mtu. Likaeleza taarifa zaidi kwamba mwanaume huyo alikuwa amesoma shule moja na Annastazia huku wakiwa katika uhusiano wa kimapenzi. Kila mtu alionekana kuwa na hamu ya kutaka kufahamu kile ambacho kiliendelea baada ya kumaliza shule. Hakukuwa na kitu chochote ambacho kiliendelea zaidi ya watu hao kutokuonekana tena.
Hiyo ndio taarifa ambayo ilikuwa imechapwa katika gazeti hilo ambalo lilikuwa limepata habari hiyo kupitia mtandao mkubwa wa CNN ambao walionekana kufuatilia mambo mengi ya nyuma ambayo yalitokea katika maisha ya Andy.
Taarifa ile haikuwashtua Watanzania tu bali hata Wamarekani walionekana kushtuka kutokana na kile ambacho walikuwa wamekisikia na kukiona katika televisheni. Andy alikuwa ni daktari mkubwa sana ambaye alikuwa msaada mkubwa katika jamii yote ya Wamarekani, kamwe hawakutaka kumuonamtu wao akipata tatizo lolote lile, bado walikuwa wakimhitaji zaidi ya dokta yeyote yule kutokana na utaalamu wake ambao alikuwa nao juu ya magonjwa mbalimbali ya wanawake.
Watanzania wakaanza kuandamana huku wakiwa na mabango ambayo yalikuwa yakimtaka Andy akamatwe na kusfikishwa mbele ya mkono wa sheria ambako huko angeukumiwa kunyongwa au kufungwa kifungo cha maisha na kazi nzito.
“Ameuawa. Yaani mtu mzuri anauawa halafu mbaya anaachwa” Mwananchi mmoja ambaye alionekana kuwa na hasira alimwambia mwenzake.
Maandamanobado yalikuwa yakiendelea kama kawaida huku yakianza kuenea kila siku. Watu wa Morogoro wakaanza kuandamana na hata wa mikoa mingine nao wakifanya vile vile. Ndani ya masaa kumi tu, Watanzania waliokuwa katika mikoa yote nchini Tanzania wakaanza kuanamana kumtaka Andy atafutwe, akamatwe na hatimae kuhukumiwa kifo.
George alionekana kuchanganyikiwa, mara ya kwanza alipokuwa akipewa taarifa cha kifo cha mke wake alijiona kuwa kama ndondoni ambapo baada ya muda mfupi angeamka na kujikuta yupo kitandani. Masikio yake hayakuamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa mfanyakazi wa ndani, alichokifanya kwa wakati huo ni kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwake.
Garini hakuonekana kutulia hata kidogo, alionekana kuchanganyikiwa kabisa huku kila wakati akiupiga piga usukani wa gari lake. Hakujua afanye nini mara atakapofika nyumbani na kukuta kwamba kile alichokuwa ameambiwa kilikuwa ni ukweli mtupu.
Akafika nyumbani na kuanza kupiga honi. Mlinzi akaufungua mlango, kwa jinsi hali ilivyokuwa ndani ilimfanya kuona kwamba kile ambacho alikuwa
 
SEHEMU YA 77

ameambiwa simu kilikuwa na ukweli asilimia mia moja. Mapolisi walikuwa wamejazana nyumbani kwake huku gari la wagonjwa likiwa katika eneo la nyumba ile.
Kwa haraka George akateremka kutoka garini na kisha kuanza kwenda ndani. Alitembea kwa haraka haraka, machozi yalikuwa yameanza kumlenga huku kadri alivyozidi kusogea mbele na ndivyo ambavyo machozi yale yalivyoanza kumtoka na kutiririka mashavuni mwake.
Mwili wa mkewe ulikuwa kitandani huku damu zikiwa zimetapakaa kitandani, George akaanza kulia kama mtoto huku akiliita jina la mke wake ambaye alikuwa akimpenda sana. Hilo lilikuwa pigo kubwa moyoni mwake, moyo wake ulimuuma kupita kiasi, hakuamini kama kweli huo ndio ulikuwa mwisho wa kumuona mkewe ambaye alikuwa akimpenda sana.
****
Mwanamke yule bado alikuwa akionekana kuwa na wasiwasi sana, kwake mapolisi walionekana kuwa watu wa hatari kabisa ambao kila siku katika maisha yake alikuwa akiwaogopa sana. Ila pamoja na hilo, akaanza kumfikiria Andy ambaye alikuwa amemficha, kama angesema ukweli kuwa alikuwa amemfunika na shuka lake na kisha mwanaume huyo kukaatwa, angepata nini? Tena isitoshe hata wale mapolisi wasingeweza kumshtukuru.
“Mama unatuchelewesha. Umemuona wapi?” Polisi mmoja aliuliza huku akionekana kuanza kupatwa na hasira.
“Alipita hapa akiwa anakimbia. Ameelekea kule kwenye giza” Mwanamke yule aliwaambia mapolisi wale.
Hakukuwa na cha kuuliza zaidi au kusubiri kitu chochote kile, walichokifanya mapolisi wale ni kuanza kukimbia kuelekea kule ambapo walikuwa wameambiwa kwamba Andy alikuwa amekimbilia, hakukuwa na polisi yeyote ambaye alikuwa na mashaka na shuka lile ambalo lilionekana kumfunika mtu, mapolisi wote walijua kuwa mtu ambaye alikuwa amefunikwa alikuwa mtoto wa mwanamke yule.
“Wewe baba amka undoke” Mwanamke yule yule alimwambia Andy ambaye akalitoa shuka lile na kuanza kuangalia huku na kule.
“Nashukuru sana” Andy alimwambia mwanamke yule na kisha kuondoka kwa kasi mahali hapo.
Mwanamke yule akaonekana kukasirika kupita kawaida, kitu ambacho alikuwa amekifikiria kabla kilionekana kuwa tofauti. Alichokitegemea kutoka kwa Andy ni shukrani ya kiasi fulani cha fedha kutokana na kile ambacho alikuwa amemfanyia.
Kuondoka kwa Andy bila kumpatia kiasi chochote kulionekana kumkasirisha sana. Moyo wake ukaanza kujuta kwa kuamua kumficha Andy ambaye wala hakuwa msaada wowote kwake. Alikuwa akiishi katika maisha ya kimasikini, kumsaidia Andy kulionekana kumpa matumaini ya kupata japo shlingi elfu moja kwa ajili ya kunywa chai asubuhi.
Andy bado alikuwa akikimbia, moyo wake ulikuwa ukimshukuru sana mwanamke yule ambaye alikuwa amemficha na kumfanya kutokuonekana kwa mapolisi wale ambao walionekana kuwa na hasira nae. Mbio zake ziliishia barabarani ambapo akachukua teksi na kutaka kupelekwa katika hoteli yoyote ndogo.
Dereva wa teksi ile akaanza kumpeleka katika hoteli ya Jumanji ambayo ilikuwa Magomeni Mapipa. Ni mwendo wa dakika saba tu wakawa wamekwishafika. Andy akateremka na kumlipa fedha dereva teksi yule na kisha kuelekea katika hoteli ile.
 
SEHEMU YA 78

Maisha yake yakaanza katika hoteli hiyo huku akianza kufuatilia kila kitu ambacho kilikuwa kinaendelea kupitia televisheni. Picha zake zilikuwa zimebandikwa kila sehemu, alitafutwa kila sehemu lakini wala hakupatiikana. Kila gari ambalo lilikuwa likitoka nje ya jiji la Dar es Salaam lilikuwa likichunguzwa huku ulinzi mkubwa ukiwa katika uwanja wa ndege lakini napo huko wala Andy hakuonekana hata mara moja.
Mitaani bado msako ulikuwa ukiendelea, wapelelezi walikuwa wamemwagwa katika kila kona ndani ya jji la Dar es Salaam lakini wala Andy hakuweza kuonekana wala tetesi kusikika mitaani mwamba alikuwa sehemu fulani.
Mwezi wa kwanza ukapita, muda mwingi Andy alikuwa akikaa ndani tu na kama alikuwa akitoka nje basi ilikuwa ni usiku tu, tena katika muda ambao hakukuwa na watu wengi. Andy hakuwa akifanya mawasiliano ya simu na mtu yeyote yule, alikuwa akihofia sana kukamatwa.
Baada ya miezi miwili kupita, hapo ndipo alipojifikiria kuanza safari ya kurudi nchini Marekani bila kuonekana. Kwake kazi ilionekana kuwa kubwa lakini kwa kutumia fedha alijiona kufanikiwa kwa urahisi sana.
Kwa jinsi alivyokuwa akitafutwa ingekuwa ngumu sana kama angetumia ndege, usafiri ambao alikuwa akiufikiria kichwani mwake ilikuwa ni usafiri wa meli za mizigo. Hapo ndipo alipoanza harakati za kutafuta msaada huo hata kabla mambo hayajawa makubwa zaidi.
Alichokifanya ni kutoka chumbani mule hotelini na kuanza kuelekea barabarani ambapo akanunua kofia kubwa na kuivaa kichwani. Akasimamisha teksi ambayo ikaanza kumpeleka kule alipokuwa akitaka kwenda. Kusafiri salama kuelekea nchini Marekani haikuwa rahisi hata mara moja lakini kwake aliona kutokuwa na tatizo kubwa kwa sababu tu alikuwa ameishi sana nchini Marekani.
Meli ambayo alikuwa akiitaka kwa wakati huo ni meli ya mizigo ambayo ilikuwa ikielekea nchini Uingereza au nchi yoyote Ulaya. Alitaka kwanza kuelekea nchini Afrika Kusini ambapo huko angejua ni kwa jinsi gani angeunganisha safari kwani hakutaka kutumia meli moja kwa kuogopa kukamatwa.
Kwa kutumia kiasi cha fedha ambacho alikuwa nacho wala hakupata tabu kuingia bandarini. Moja kwa moja akaanza kuelekea katika sehemu ambayo ilikuwa ikihusika na mizigo ambayo ilikuwa ikiletwa kutoka nchini Ugiriki na kuanza kuongea na wahusika. Benedict hakuonekana kupata tabu sana kwani alionekana kuwa mtu kutoka nje na wala si mzamiaji.
“Sasa kwa nini unataka kutumia meli?” Kolatov, Mgiriki mwenye asili ya Urusi aliuliza.
“Najisikia tu” Andy alijibu.
“Una kiasi gani?”
“Dola elfu nne”
“Sawa. Kajiandae, safari itaanza kesho kutwa baada ya kumalizia hii mizigo iliyobakia” Kolatov alimwambia.
Benedict akaanza kurdi tena garini. Moyoni mwake alijiona kuwa mshindi kwani aliona ni lazima safari yake ya kurudi nchini Marekani ingefanikiwa. Alichokifanya ni kumtaka dereva wa taksi ampeleke daraja la Salenda huku lengo lake likiwa ni kutaka kuonana na mwanamke yule ambaye alikuwa amemsaidia kumficha na shuka katika kipindi kile alichokuwa anakimbizwa na polisi.
 
SEHEMU YA 79

“Siamini kama ni wewe” Mwanamke yule alimwambia Andy.
“Ni mimi mama”
“Nilifikiri usingerudi. Karibu” Mwanamke yule alimwambia Andy na kumkaribisha katika kibanda kidogo ambacho alikuwa akikitumia kama chumba chake.
Hapo ndipo maongezi yalipoanza. Alichokifanya Andy ni kuchukua kiasi cha shilingi laki tano na kumgawia mwanamke yule ambaye alionekana kuchanganyikiwa kwani kiasi kile cha fedha kilionekana kuwa kikubwa sana kwake.
Kwa kuwa mwanamke yule alikuwa amekabidhiwa kiasi kikubwa cha fedha, moyoni mwake akaonekana kuwa radhi mbele ya Andy kuongea kitu chochote kile, fedha zilionekana kuubadilisha kabisa moyo wake.
Muda wote wa maongezi Andy alikuwa akijitahidi kumsoma mwanamke yule aliyejitambulisha kwa jina la Sikitu huku akitaka kujua mambo mengi kuhusu maisha yake. Bi Sikitu akaonekana kuwa muwazi, hakujali kama mwanaume yule aliyekuwa mbele yake hakuwa akimfahamu au la, alichokifanya hapo ni kutaka kuhadithia historia yake ambayo ilionekana kujaa matukio mengi.
“Una moyo?” Mwanamke yule alimuuliza Andy.
“Wa nini tena?”
“Kuisikiliza hiyo stori yangu”
“Ninao”
“Sawa. Nitakapoimaliza naomba uniambie kama sisi wa wanawake wa Kitanzania tunastahili kupendwa” Mwanamke yule alisema maneno ambayo yalionekana kumshtua Andy.
“Mmmh!” Andy alijikuta akiguna.
“Mbona umeguna?”
“Subiri kwanza. Una mtoto?”
“Ninae”
“Yupo wapi?”
“Barabarani”
“Anafanya nini?”
“Ananisadia kuombaomba. Unajua nimekwishakuwa mzee sasa. Huwa sijisikii vizuri kila ninapokwenda kuomba kwenye madaladala na ndio maana ninamuachia yeye kwenda kuombaomba” Bi Sikitu alimwambia Andy.
“Sawa. Unaweza kuniambia historia ya maisha yako?” Andy alimuuliza mwanamke yule.
“Naweza. Ila sitaki kuchukua muda wako mwingi baba yangu. Historia yangu imegawanyika sehemu tatu, sehemu ya kwanza kuanzia utotoni, sehemu ya pili kuanzia ujanani na sehemu ya tatu kuanzia miaka thelathini na tano. Wapi unapotaka nianzie?” Bi Sikitu alimuuliza Andy.
“Kutokana na muda. Anzia miaka thelathini na tano” Andy alimwambia Bi Sikitu huku akionekana kutaka kufahamu kile ambacho kilitokea katika maisha ya mwanamke huyo.


Macho yangu yalikuwa wazi japokuwa kwa wakati huo nilikuwa kitandani na usiku ukiwa mkubwa sana. Mtoto wangu, Abdul alikuwa amekwishalala kutokana na kutakiwa kuamka asubuhi na mapema kuelekea shuleni.
Kwa mbali kelele za kaka yangu, Rahman na mkewe Fatuma zilikuwa zikisikika. Kelele zao za kugombana hazikuwa siku ya kwanza kusikika, mara kwa mara walikuwa wakigombana hasa Fatuma alipokuwa akirudi usiku huku akiwa amelewa.
Rahman alikuwa mwanaume mpole sana, siku zote alikuwa akiipenda familia yake. Alimpenda sana mke wake, Fatuma ambaye alikuwa akimpa kila kitu alichokuwa akikitaka katika maisha yake. Fatuma alionekana kuwa mwanamke mjinga sana, kiburi na majivuno ndio yalikuwa sehemu ya maisha yake. Alijua fika kwamba mumewe, Rahman alikuwa akimpenda sana na ndio maana alikuwa akifanya ambo ya kijinga sana kwa kuona kwamba hasingeweza kuachwa.
Rahman alikuwa mwanaume mvumilivu sana, aliona mkewe akifanya mambo
 
SEHEMU YA 80

ya kijinga lakini kamwe hakuwahi kumkaripia au kumpiga. Kwangu nilimuona Rahman kuwa mwanaume mjinga sana kwani hakukuwa na mwanaume ambaye angevumilia mambo yale ambayo alikuwa akiyafanya Fatuma.
Mimi na Rahman tulikuwa ndugu ambao tulizaliwa na wazazi wawili na tulikuwa watoto pekee katika familia yetu. Wazazi wetu walifariki kipindi kirefu kilichopita. Nilifanikiwa kupata mume, Abdallah ambaye nilizaa nae mtoto mmoja ambaye ndiye huyu niliye nae, Abdul.
Mume wangu alikuwa kila kitu katika maisha yangu, alinifanyia mambo mengi sana huku akinionyeshea upendo mkubwa na ndio maana nilizimia mara nyingi sana mara nilipopewa taarifa kwamba alikuwa amefariki mara baada ya kugongwa na gari katika kipindi ambacho alikuwa akitoka kazini.
Ndugu zake wakaonekana kuwa na ukali katika mali za ndugu yao. Kwa sababu nilikuwa na mawazo mengi sana juu ya marehemu mume wangu, wala sikuonekana kujali kuhusu mali. Ndugu zake wakafanikiwa kuchukua mali zote ambazo zilikuwa zangu na za marehemu mume wangu.
Hapo ndipo kaka yangu, Rahman alipoamua niende kuishi nyumbani kwake pamoja na mtoto wangu. Fatuma hakuonekana kuufurahia ujio wetu ndani ya nyumba ile, alituonyeshea chuki za waziwazi kabisa lakini wala sikuonekana kujali kitu chochote kile.
Maisha ambayo alikuwa akiishi Rahman na mkewe, Fatuma ndio ambayo yalikuwa yakinikasirisha sana. Nilikuwa nikiyakumbuka sana maisha ya Rahman katika kipindi cha nyuma, alikuwa mwanaume mpole sana ambaye hata wazazi wetu walikuwa wakimshangaa sana.
Fatuma ndiye ambaye alijiona kuwa kichwa cha familia, alifanya kitu chochote ambacho alikuwa akitaka pasipo kuambiwa kitu chochote kile, Katika maisha yangu nikatokea kumchukia sana Fatuma, mbaya zaidi nikatokea kuwachukia wanawake wote kwani kwangu kuyaona maisha kama yale haikuwa mara ya kwanza.
Wanawake walionekana kuwa viumbe vya ajabu sana ambavyo wala havikustahili kuonyeshewa mapenzi ya dhati, huwa tunakuwa wasumbufu sana kwa mawanaume mara tu wanapoamua kutuonyeshea mapenzi ya dhati.
Mara nyingi sana nimekuwa nikimkufuru Mungu kwa kuamua kuniumba nikiwa mwanamke, sikustahili kabisa kuwa mwanamke katika maisha yangu. Nilijiona kuwa tofauti na wanawake wengine, nilikuwa nikiishi maisha tofauti na wanawake.
Siku za kwanza hata kabla sijawa mkubwa nilikuwa nikisikia mauaji mengi tu waliyokuwa wakiyafanya wanaume juu ya wanawake, moyoni nilikuwa nikiumia sana kwani sikuwa nikitegemea kuona au kusikia mambo kama hayo lakini baada ya kukua nikaja kuona kwamba walistahili kufanyiwa mambo kama yale.
Mioyo yetu ni mioyo mikatili sana, huwa tunaweza kubadilisha hali ya mchezo muda wowote ule. Kumsaliti mtu fulani kwa sababu ya fedha wala si jambo kubwa kwetu, huwa hatuyajali maumivu ambayo watakuja kuyasikia mara baada ya kuwasaliti. Fedha ndio kitu ambacho tunakitafuta sana katika maisha yetu.
Kilipita kipindi kirefu sana hatimae Rahman akafariki katika mghahawa mmoja huko Shinyanga alipokuwa amekwenda kikazi. Kifo chake kilikuwa na
 
SEHEMU YA 81

utata mkubwa sana kwani alikuwa amewekewa sumu katika kinywaji chake.
Nilikuwa nimeshikwa sana na wasiwasi moyoni kwani tangu Rahman aondoke kuelekea Shinyanga nae mkewe, Fatuma alikuwa haonekani nyumbani na hivyo kumtilia mashaka kwamba alikuwa amehusika katika kifo hicho.
Moyo uliniuma sana na kuanza kujuta kwa nini Rahman hakuwa amemuua Fatuma tangu zamani mpaka kuja kuuawa yeye. Kifo cha Rahman ndicho ambacho kilisababisha mambo mengi katika maisha yangu na mwanangu.
Baada ya mwezi Fatuma akatufukuza katika nyumba yake. Sikuwa na ndugu yeyote ndani ya jiji la Dar es Salaam hali iliyonifanya nianze maisha ya mitaani pamoja na mwanangu. Shuleni akafukuzwa kwa kukosa ada, moyoni niliumia sana.
Japokuwa mimi ni mwanamke lakini milele nitaendelea kuichukia jinsia hii. Mwanamke ameonekana kutokuwa na mapenzi ya dhati, na hata kama atakuonyeshea mapenzi ya dhati katika kipindi hiki, baadae anaweza kubadilika na kuwa na roho mbaya hata zaidi ya shetani.
****
Bi Sikitu akashindwa kuvumilia, machozi yalikuwa yakimtoka. Alikuwa ameelezea kwa kifupi sana historia fupi ya maisha yake lakini bado ilionekana kumgusa sana. Andy alibaki akimwangalia kwa masikitiko, akapata jukumu la kuanza kumbembeleza.
Hapo ndipo Andy alipoanza kumfikiria Annastazia na kuona kwamba alistahili kumuua kutokana na kile ambacho alikuwa amemfanyia. Usaliti ukaonekana kuwa sehemu ya maisha ya wanawake wengi ambao walikuwa wakiishi nchini Tanzania. Moyo wake ukazidi kuwachukia wanawake wa Kitanzania.
Andy akainuka na kisha kuaga. Moyoni mwake kukaanza kujengeka kitu kingine, sasa akatamani kuwaua wanawake wote wa Kitanzania. Hakutaka kuwaacha wakibaki hai, alijiona kuwa na sababu ya kuua mamilioni ili aokoe mabilioni.
Chuki yake juu ya wanawake wa Kitanzania ikawa kubwa moyoni mwake. Alipofika barabarani akasimamisha teksi akapanda na kisha safari ya kuelekea hotelini kuanza. Kila mwanamke ambaye alikuwa akimuona njiani kwake alionekana kuwa mbaya na msaliti mkubwa, kiu ya kutaka kuwaua wanawake wa Kitanzania ikamkaba moyoni, hakuona sababu ya kuwaacha watu na wakati mara kwa mara walikuwa wakiwasaliti wanaume zao na kuwasababishia maumivu makali mioyoni mwao.
Alipofika hotelini, akateremka na kuanza kuelekea ndani ya jengo la hoteli ile. Kadri alivyozidi kuwaona wanawake na ndivyo ambavyo hasira zake zilipokuwa zikiongezeka zaidi na zaidi, wanawake kwake walionekana kuwa kama mashetaki ambayo hayakuwa yakistahili huruma yoyote ile maishani mwao.
Aliingia chumbani na kujipumzisha huku akipanga safari ya kuelekea Bandarini kesho kutwa na kuanza safari ya kuelekea Marekani. Akili yake haikutulia usiku huo, alikuwa akiwaza juu ya kuondoka nchini Tanzania pasipo kugundulika na mtu yeyote yule.
Alikuwa akiziona televisheni mbalimbali zikiendelea kutangaza kwamba alikuwa akitafutwa, kwa mtu yeyote ambaye angefanikisha kupatikana kwake akiwa hai au amekufa atakabidhiwa kiasi cha shilingi milioni hamsini.
Muda wote Andy alikuwa akicheka kwa kujiona mshindi kati ya washindi,
 
SEHEMU YA 82

kwake, kukamatwa kulionekana kuwa vigumu sana kutokana na mipango yake ya safari ambayo ilikuwa ikiendelea kufanyika.
****
Baharia, Kolarov alikuwa ameshtuka sana mara baada ya kumuona Andy mbele ya macho yake. Kiasi cha fedha ambacho kilikuwa kimetangazwa kwake kilionekana kuwa kikubwa japokuwa alikuwa akihitaji kiasi kikubwa zaidi.
Kadri alipokuwa akiongea na Andy, alitamani sana kuwapigia simu mapolisi na kuwaita mahali hapo wamkamate na kisha kumgawia kiasi cha fedha ambacho kilikuwa kimeahidi na kutangazwa mara kwa mara katika vyombo vya habari.
Juhudi za kumkamata Andy zilionekana kufifia machoni mwa Watanzania kutokana na Andy kuonekana kuwa mjanja sana. Serikali haikukata tamaa, bado ilikuwa ikiendelea kumtafuta Andy kwa mategemeo ya kumkamata.
“Una uhakika ni yeye?” Lilikuwa ni swali lililotoka kinywani mwa polisi mmoja ambaye alikuwa akiongea simu na Kolarov.
“Asilimia mia tatu”
“Upo wapi?”
“Mbona unakuwa na haraka hivyo? Sikiliza, nionganishe na wakubwa zako kwanza” Kolarov alimwambia polisi yule ambaye bila ubishi aliiunganisha simu ile na makao makuu ya polisi.
“Unasemaje?” Kamanda mkuu, Bwana Pawasa aliuliza kwa mshtuko.
“Ndio hivyo. Nipo nae na anataka kuondoka kuelekea nchini Marekani kwa njia za panya” Kolarov alimwambia.
“Kwa njia gani?”
“Za panya”
“Zipi?”
“Hebu acha kuuliza maswali ya kitoto. Mna milioni mia moja niwaonyeshe pa kumkamata?” Kolarov aliuliza.
“Ni kiasi kikubwa sana cha fedha. Kiasi kilichowekwa ni milioni hamsini tu” Kamanda Pawasa alimwambia Kolarov.
“Kama hamna basi poa. Mwacheni tu aondoke zake” Kolarov alisema na kukata simu.
Kolarov alibaki akitabasamu tu, alijua fika kwamba ni lazima angepigiwa simu na kuanza kubembelezwa juu ya kiasi kile cha fedha ambacho alikuwa akikihitaji. Hakuwa na wasiwasi wa mawasiliano ya simu yake kwani alikuwa akitumia mtandao wa simu wa Kimataifa ambao ulikuwa ukitumika sana na wageni wa kimataifa hasa wakubwa. Hata kama wangejaribu kusoma signal ya mahali simu hiyo ilipokuwa imepigwa, kusingekuwa na mtu yeyote ambaye angefanikiwa kupata signal.
Alichofikiria ndicho kilichotokea, baada ya dakika kadhaa simu yake ikaanza kuita, akaipokea huku tabasamu pana likiendelea kuonekana usoni mwake.
“Mmefikiria nini?” Aliuliza.
“Nimeongea na wakuu, wamekubali kukupa kiasi hicho cha fedha” Kamanda Pawasa alijibu.
“Sawa. Mnachotakiwa kufanya ni kuja na hicho kiasi cha fedha nami nitawapeni mtu huyo mnayemhitaji. Mmesikia?” Kolarov alisema.
“Sawa”
****
Alichokifanya Andy ni kuanza kuwasiliana na Dawson na kumueleza kila kitu ambacho kilikuwa kimeendelea. Dawson alionekana kushtuka sana kwani kwa mara ya kwanza ambapo aliziona taarifa zile katika magazeti na vyombo vingine vya habari alikuwa akipuuzia kwa kuona kwamba alikuwa mtu mwingine ambaye walikuwa wamefanana majina tu.
Kwa kuwa Andy alikuwa mtu muhimu sana katika maisha yake huku dawa
 
SEHEMU YA 83

zaidi zikiwa zinahitajika, Dawson akaamua kufanya kila linalowezekana kuhakikisha kwamba Andy anafika salama nchini Marekani na kuendelea na utengenezaji wa dawa za virusi aina vya Katapillar ambavyo vilikuwa vikisambaza ugonjwa wa PENINA.
“Nataka kuwaandaa vijana wangu wakufuate huko” Bwana Dawson alimwambia.
“Hapana. Wasije Tanzania. Kama itawezekana waje Afrika Kusini” Andy alimjibu.
“Hilo linawezekana. Kuna kingine?”
“Ndio. Nitahitaji sura ya bandia ambayo itakuwa imetengenezewa passport pamoja na hati zote za kusafiria” Andy alimwambia.
“Usijali. Ni ndani ya masaa mawili. Usiku huu vijana wangu watapanda ndege na kuja Afrika Kusini ambako huko utakutana nao na kisha kuanza safari ya kuja huku. Sisi ndio wazungu bwana, mtu mweusi hawezi kutusumbua” Bwana Dawason alimwambia Andy.
Mara baada ya siku ya safari kufika haraka haraka Andy akaanza kujiandaa tayari kwa kutoroka kuelekea nchini Marekani kwa kutumia meli ya mizigo iliyokuwa bandarini. Lengo lake kwa wakati huo lilikuwa ni kutaka kufika Afrika Kusini ambako angekutana na vijana wa Dawson na kisha harakati za safari kuanza huku akiwa na sura ya bandia. Kichwani mwake, mawazo yake yalikuwa juu ya safari hiyo huku mara kwa mara akimuomba Mungu Aweze kumlinda mpaka kufika salama nchini humo.
Alipofika getini, macho yake yakatua kwa Kolarov ambaye alikuwa akimsubiri na kisha kuanza kuondoka nae kuelekea katika meli ile. Kwa kuwa Kolarov alikuwa akijulikana na watu wengi hasa wafanyakazi katika bandari ile wala hakukuwa na mtu yeyote ambaye alimuuliza swali lolote lile kuhusiana na mgeni wake.
Wakafika katika meli ile na kumpeleka Andy katika chumba kimoja kilichokuwa na mizigo kadhaa huku akisingizia kisa cha kumuingiza mule ilikuwa ni sababu ya ulinzi wake. Andy hakuonekana kumtilia mashaka Kolarov, japokuwa walikuwa wamekutana kwa kipindi kichache sana lakini akajikuta akianza kumuamini.
Muda wote ule Andy alikuwa akifurahia, alijiona kuwa mshindi zaidi ya washindi, kwake, kumuua Annastazia na kisha kurudi nchini Marekani bila kuonekana ilionekana kuwa ushindi mkubwa sana. Alibaki ndani ya chumba kile kikubwa huku akiwa amewekewa magazeti mbalimbali ambayo akaanza kuyasoma.
Ni picha zake ndizo ambazo zilikuwa zimeenea kwa sana katika kila gazeti ambalo alikuwa akilisoma, watu walikuwa wakihitaji kumuona akifikishwa mbele ya sheria na kushtakiwa kwa tuhuma za kumbaka Annastazia na kisha kumuua kinyama.
Aliendelea kubaki mule chumbani kwa takribani dakika thelathini na ndipo akaanza kusikia mlango ukigongwa. Mara ya kwanza hakutaka kuufungua kwa kujua kwamba hakukuwa na mtu yeyote ambaye alikuwa akiufahamu uwepo wake ndami ya meli ile lakini aliposikia kwamba alikuwa Kolarov, akaufuata mlango na kuufungua.
Andy alibaki kuwa na mshtuko mkubwa, mwili wake ukapigwa ganzi. Macho yake yalikuwa yakiangalia midomo ya bunduki tano ambazo zilikuwa zimemuelekezea kutoka kwa mapolisi walioonekana kuwa na hasira kali.
 
SEHEMU YA 84

Andy alijiona kukamatwa kirahisi sana, kichwa chake wala hakikupata kazi ya kujiuliza ni nani alikuwa amewaelekeza mapolisi kwamba alikuwa ndani ya meli ile kutokana na Kolarov kuwa pembeni yao akimwangalia huku uso wake ukiwa na tabasamu pana na mfuko mkubwa wa kaki ulioonekana kuwa na fedha ukiwa mkononi mwake.
“Uko chini ya ulinzi” Polisi mmoja alimwambia na kisha kumsogelea na kumfunga pingu kwa nyuma.
****
Mapolisi walikuwa wakitamani kumfahamu mtu ambaye alikuwa akiwapa taarifa njema kwa wakati huo, kumkamata Andy ndicho kitu ambacho kila Mtanzania alikuwa akikitaka sana kukisikia. Kuhusu fedha wala halikuwa tatizo kubwa.
Mara baada ya Kolarov kuwapa maelekezo ya mahali alipokuwa, mapolisi wakaanza kujiandaa huku mikononi wakiwa na kiasi hicho cha fedha. Ni mwendo wa dakika kumi tu wakawa wamekwishafika katika bandari hiyo ambapo wakaingia bila kizuizi chochote kile.
Kitu cha kwanza ambacho walikuwa wakikitaka ni kuonana na mwanaume ambaye alijitambulisha kwao kwa jina la Kolarov aliyekuwa katika meli ya mizigo ya Caspian. Wakapelekwa mahali ilipokuwa meli ile na kisha kutaka kuonana na Kolarov.
“Una uhakika ni yeye?” Polisi mmoja ambaye alionekana kuwa mkuu wao alimuuliza.
“Asilimia 600”
“Sawa. Tumfuate”
“Subirini kwanza. Fedha zenyewe ziko wapi?” Kolarov aliuliza.
“Fedha kabla ya mzigo?”
“Mzigo kabla ya fedha? Nipeni kwanza. Huyu mtu yupo na wala hakimbii” Kolarov aliwaambia.
Hapo hapo polisi ambaye alikuwa na bahasha kubwa ya kaki akaitwa na kisha kumpa mkuu yule wa mapolisi bahasha ile ambayo ilikuwa na kiasi kikubwa cha fedha. Kolarov hakutaka kuhesabu kwani alikuwa na uhakika kwamba hakufanyiwa mchezo wowote mchafu.
“Bora mlivyoziweka kwenye dola kwani mmenipa urahisi mkubwa” Kolarov aliwaambia huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana.
Hapo ndipo ambapo akaanza kuingia ndani ya meli ile pamoja na wale mapolisi ambao walikuwa wamekuja mahali pale. Wala hakujisikia uchungu moyoni, kumkamatisha Andy kwa mapolisi kulionekana kuwa jambo zuri sana kutokana na fedha ambazo alikuwa amelipwa.
Hakumjua Andy kwa sana zaidi ya kumuona ona kwenye vyombo vya habari tu na ndio maana hata kama alikuwa akikamatwa, kwake wala halikuwa tatizo kubwa kutokana na akili yake kwa wakati huo kufikiria zaidi fedha.
Akaanza kuugonga mlango ule na kisha baada ya muda fulani Andy kuufungua na mapolisi kumuweka chini ya ulinzi.

Je nini kitaendelea?
Je Andy atapewa hukumu gani?
 
SEHEMU YA 85

Ilikuwa ni taarifa njema kwa Watanzania hasa mara baada ya kupewa habari kwamba mwanaume ambaye alikuwa amemuua Spika wa Bunge, Annastazia Kapama alikuwa amekamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi mkali wa polisi.
Watu wakashindwa kujizuia, wakaanza kuandamana huku wakimtaka Andy ahukumiwe kifo katika kipindi ambacho atakanyaga katika mahakama kuu ya Tanzania. Vyombo vya habari ndivyo ambavyo vilikuwa vikitangaza habari hiyo zaidi na zaidi na kufanya vyanzo vyao vya habari kusikilizwa na kununulika kupita kiasi.
Maandamano ya kumtaka Hakimu kumuhukumu Andy kifo yalikuwa yakiendelea kama kawaida. Mara ya kwanza yalikuwa yameanzia Dar es Salaam lakini kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo maandamano hayo yalivyozidi kuongezeka.
Watu wa Morogoro nao wakaanza kuandamana, Dodoma wakafuata huku nao Tanga wakishika nafasi. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo yalizidi kuenea mpaka kufika mkoani Kigoma. Katika maandamano yote hayo, mabango ambayo yalikuwa yakimtaka Andy ahukumiwe kifo ndio ambayo yalikuwa yakionekana muda wote.
Watanzania hawakutaka Andy aendelee kuishi, walimtaka auliwe kwa kunyongwa au hata kwa kuchomwa sindano iliyokuwa na sumu kali. Kifo cha Spika wa Bunge, Annastazia ambacho kilitokea wiki iliyopita kilikuwa kimewagusa sana, mioyo yao ilikataa katakata kumsamehe Andy ambaye alionekana kuwa kijana mdogo.
Ndani ya masaa mawili tu, dunia nzima ikapata taarifa juu ya kuamatwa kwa Andy. Dunia ikagawanyika, kuna wengine ambao walifurahi lakini kuna wengine ambao hawakupenda akamatwe kwani bado alikuwa akihitajika kutengeneza zile dawa zake ambazo zilikuwa zikitibu magonjwa ya moyo na mengine ndani ya mwili wa binadamu.
Mbali na Dawson, hakukuwa na mtu yeyote duniani ambaye alikuwa akifahamu kama Andy huyo ndiye ambaye alikuwa ametengeneza virusi vya Katapillar ambavyo vilikuwa vikisambaza ugonjwa hatari wa PENINA. Kwa kuwa Andy alikuwa na uraia wa Tanzania, serikali ya Marekani haikutaka kuingilia kwa chochote kile japokuwa mtu huyo alikuwa muhimu sana katika maisha yao.
Jina lake na picha zake ndivyo vilikuwa vitu ambavyo vilitawala sana katika vyombo mbalimbali vya habari. Kila mtu ambaye aliiangalia picha ya Andy alionekana kushtuka kwa sababu alionekana bado kijana mdogo sana ambaye alithubutu kunyanyua kisu na kumchoma Annastazia.
Kutokana na maandamano kuongezeka kila siku, siku ya kusomwa kwa hukumu ya Andy ikatangazwa. Kesi hiyo ikapelekwa moja kwa moja mpaka mahakama kuu tayari kwa kusomwa. Muda wote Andy alionekana kuwa na huzuni kitu kiliwapelekea watu kuona kwamba alikuwa akijuta kwa kile alichokuwa amekifanya.
“Ninawahuzunikia wanaume wa nchi hii. Hivi hawajui kwamba wanawake hawa ni wanyama na shetani wakubwa sana? Nilikuwa tayari kuwatetea lakini badala ya kuhuzunika kwamba nimekamatwa, wao ndio kwanza
 
SEHEMU YA 86

wanashangilia” Andy alisema huku akionekana kuwa na majonzi.
“Ni lazima niue mamilioni ili kuokoa mabilioni” Andy alijisemea.
Bado hali ya hewa nchini Tanzania ikaonekana kuchafuka, kila siku idadi ya watu ambao walikuwa wakiandamana ilikuwa ikiongezeka barabarani. Mapolisi walikuwa wakizidiwa nguvu na wananchi hao ambao walionekana kuwa na hasira kupita kawaida.
Wao, kiu yao ilikuwa ni kutaka kumuona Andy akihukumiwa kifo tu, ingawa siku ya hukumu ilikuwa imepangwa lakini watu waliiona siku hiyo ikichelewa kufika. Hawakutaka kumuona Andy akiendelea kuendelea kuvuta pumzi ya dunia hii.
Maandamano yaliendelea na hatimae fujo kuanza kutokea. Vibanda vilikuwa vikichomwa moto huku hata wakati mwingine mapolisi ambao walikuwa wakiwazuia katika maandamano yao wakianza kupigwa. Watu hawakutaka kusikia kitu chochote zaidi ya hukumu ya kifo tu.
Makaratasi yakachapishwa na picha za Andy kuweka huku maneno ambayo yalikuwa yakimtaka kuhukumiwa kifo yakiwa yanasomeka vizuri. Vijana wadogo ambao hawakuwa wakifuatilia kitu chochote kile nao wakapandikizwa sumu ya kutaka Andy ahukumiwe kifo.
****
Mchungaji Wayne na mkewe, Happy walionekana kuhuzunishwa na taarifa ile ambayo walikuwa wameipata kutoka katika vyombo vya habari. Hawakuamini kama kweli mtoto wao alikuwa amefanya mauaji kwa mwanamke ambaye alikuwa na uhusiano nae wa kimapenzi.
Walionekana kufahamu sababu ambayo iliwapelekea Andy kumuua mwanamke yule lakini kamwe hawakutaka kumwambia mtu yeyote sababu ile. Walichokifanya kwa wakati huo ni kuwaandaa mawakili wao ambao walionekana kuwa na uwezo wa kuwasaidia wateja wao kushinda kesi kubwa kama ile.
Wakili akapangwa na kisha kuanza safari ya kuelekea nchini Tanzania. Alichokifanya wakili yule ni kukutana na Andy na kisha kuanza kuongea nae. Aalitamani sana kumsaidia kwa nguvu zote mpaka pale ambapo angeshinda kesi ile na kurudi nchini Marekani.
“Ni kweli uliua?” Wakili Kelly aliuliza.
“Ndio” Andy alijibu.
“Kwa nini uliua?”
“Unajua wanawake hawa wajinga sana. Nimeua kwa sababu tu alinisaliti” Andy alijibu.
“Niko hapa kwa ajili ya kukusaidia Andy. Nina uhakika utatoka tu. Nitasimamia kesi yako mpaka mwisho” Andrew alimwambia Andy.
“Itakuwa vizuri sana kama ukinisaidia kwani nitafanikiwa kuifanya kazi yangu” Andy aliwaambia.
“Kazi gani?” Kelly aliuliza.
“Kazi nzito ya kuwamaliza wanawake wote wa nchi hii” Andy alitoa jibu lililoonekana kumshtua Kelly.
“Kwa nini unataka kuwaua?”
“Unajua ni bora kuua mamilioni ili kuokoa mabilioni. Nyie acheni tu. Ni bora kumpenda shetani, ukae nae chini na kuzungumza kuliko kumpenda mwananamke wa Kitanzania” Andy alimwambia.
Wakili hakutaka kuendelea kuuliza maswali japokuwa alionekana kushtushwa na maneno mazito ambayo aliyaongea Andy. Hakuonekana kujali, alichokuwa akitakiwa kukijali kwa wakati huo ni kuifanya kazi yao hiyo ambayo ilikuwa
 
SEHEMU YA 87

imemleta nchini Tanzania.
Siku ziliendelea kukatika na hatimae siku ya kwanza ya kusikiliza kesi yake ikawadia. Wananchi walikuwa wamejazana mahakamani huku kila mmoja akitaka Andy ahukumiwe kifo wa kunyongwa au kuchomwa sindano ya sumu.
Bwana Wayne na mkewe walikuwa ndani ya mahakama hiyo pamoja na binti yao, Esther. Muda wote walionekana kuwa katika hali ya mawazo kupita kawaida huku macho yao yakiwa mekundu hali iliyoonyesha kwamba katika kipindi kichache kilichopita walikuwa wakilia.
Baada ya muda fulani Andy akaanza kuingizwa ndani ya mahakama hiyo. Kila mtu ambaye alikuwa akimwangalia alionekana kumchukia, mioyo yao wala haikuwa na upendo wowote juu ya Andy kutokana na mauaji yale aliyokuwa ameyafanya ya kumuua mtu ambaye walikuwa wakimpenda kupita kiasi.
Wala hazikupita dakika nyingi, hakimu, Bi Beatrice akaanza kuingia mahakamani hapo huku watu wote wakiamriwa kusimama. Kila mtu alimwangalia hakimu Beatrice, uso wake ulionekana kuwa wa kipole sana jambo ambalo liliwafanya wananchi kuona kwamba ni lazima hakimu huyo angemuonea huruma Andy.
Siku hiyo ya kwanza Andy hakutakiwa kuongea kitu chochote kile, alitakiwa kusikiliza kesi yake tu. Kesi ikasomwa na kisha kuahirishwa mpaka baada ya wiki mbili. Hakimu akaondoka mahakamani hapo na Andy kurudishwa rumande kusikilizia siku hiyo ya kesi ambayo alitakiwa kurudishwa tena mahakamani.
Nje ya mahakama watu walikuwa wakipiga kelele za kumtaka Andy ahukumiwe kifo. Kila wakati Andy alipowasikia wanaume wakipiga kelele za kumtaka ahukumiwe kifo alibaki akihuzunika tu. Hakuamini kama wanaume ambao alikuwa na lengo la kuwatetea walikuwa wakimpinga namna hiyo kwa kutaka ahukumiwe kifo. Andy akashindwa kujizuia, machozi yakaanza kumtoka.
Andy akaingizwa ndani ya karandinga hilo na kisha kuanza kurudishwa rumande huku akisubiria siku nyingine ya kesi hiyo.
****
Kesi hiyo ya mauaji ambayo ilikuwa ikimkabili Andy ndio ambayo ilikuwa ikisikika sana katika vyombo vya habari duniani huku kila mtu akitaka kufahamu nia aina ya hukumu gani ambayo angepewa Andy, dokta mwenye jina kubwa kutoka nchini Marekani japokuwa alikuwa na uraia wa Tanzania.
Mitaani bado watu walikuwa wakiendelea kuandamana huku kadri siku zilivyokuwa zikizidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo idadi ya watu ilikuwa ikiendelea kujaa. Wanafunzi ambao walikuwa wakihitajika kwenda shuleni kusoma, hawakwenda, wanachuo ambao walikuwa wakihitajka kwenda vyuoni nao hawakwenda, waliungana na watu waliokuwa na hasira kali na Andy na kisha kuandamana nao katika zile siku ambazo zilikuwa zimepangwa maalumu kwa maandamano ya amani.
Ingawa wakili Kelly alikuwa na uhakika wa kumfanya mteja wake, Andy kushinda kesi lakini maandamano yale yakaonekana kumtia wasiwasi. Wananchi walikuwa wamehamasika kupita kawaida, kiu yao kubwa kwa
 
SEHEMU YA 88

wakati huo ilikuwa ni kutaka kumuona Andy akihukumiwa kifo au kufungwa kifungo cha maisha jela.
Siku ziliendelea kukatika na hatimae siku ya kesi kusikilizwa kwa mara ya pili kuwadia. Kama kawaida yao idadi kubwa ya wananchi ilikuwa imefurika mahakamani hapo huku kila mtu akitaka kumuona huyo Andy ambaye alikuwa amefanya mauaji yale ya kinyama.
Karandinga likaanza kuingia katika eneo la mahakama hiyo, waandishi wa habari wakajiweka tayari kwa ajili ya kupiga picha. Flashi zikaanza kuonekana mahali hapo, waandishi wakaonekana kuwa bize wakimpiga picha Andy kwa ajili ya kuziweka kwenye kurasa za mbele katika magazeti yao.
Andy alikuwa kimya huku uso wake akiwa ameuinamisha chini. Kichwani alionekana kuwa na mawazo mazito, kitendo cha kuingia mahakamani na kutaka kuhukumiwa kifo au kifungo cha maisha jela kilionekana kumuumiza. Siku hiyo napo, kesi ikaahirishwa kama kawaida hasa mara baada ya hakimu kumsomea mashitaka ambayo yalikuwa yakimkabiri. Kila kitu kilipomalizika, Andy akarudishwa katika karandika lile na kurudishwa mahabusu.
Magazeti mbalimbali bado yalikuwa yakiendelea kuuza sana kutokana na habari zilizojaa mvuto ambazo walikuwa wakiziandika huku zikiwa na vichwa vya habari ambavyo vilikuwa vikimfanya mtu kutotaka kuacha kununua magazeti hayo.
Katika kipindi hicho cha kesi hiyo ndicho kilikuwa kipindi cha biashara sana. Fulana mbalimbali ambazo zilikuwa na picha za Andy zikaanza kutengenezwa jambo ambalo kwa wale ambao walikuwa wakitaka kuzinunua wazinunue. Chuki kubwa ya watanzania juu ya Andy ilizidi kuota mizizi mioyoni mwao, walimchukia Andy kuliko mtu yeyote.
“Ni afadhari wafungwa wote jela waachiwe huru kuliko huyu mtu kushinda kesi hii” Mwananchi mmoja ambaye alionekana kuwa na hasira aliwaambia wenzake.
Bwana Wayne na mkewe, Bi Happy hawakuonekana kuwa na furaha kabisa. Kila siku walikuwa watu waliokosa amani mioyoni mwao, walizidi kumuomba Mungu aweze kumuepushia adhabu yoyote kijana wao.
Kila siku usiku walikuwa wakishikana mikono chumbani na kisha kuanza kumuombea kijana wao, Andy. Kila mmoja moyoni mwake alikuwa na uhakika kwamba Andy angeshinda kesi ile kutokana na kumuamini Mungu wao wa miujiza.
“Atashinda kesi. Naamini atashinda na maisha yake kumkabithi Yesu” Bwana Wayne alimwambia mkewe.
“Hata mimi naamini ila hii isiwe mara yetu ya mwisho kumuomba Mungu” Bi Happy alisema.
“Sawa sawa. Kila siku tutakuwa tukimuomba Mungu” Bwana Wayne alisema.
Maombi yao hayakukoma hata siku moja, kila siku alikuwa waliendelea kushikana mikono na kumuomba Mungu wao. Mbele yao waliona dhahiri Mungu kwenda kufanya miujiza na hatimae kijana wao kushinda kesi ile ngumu ambayo ilikuwa iimkabiri.
Siku zikaendelea kukatika, wiki zikaanza kusogea mpaka siku ya kesi ile kufikia. Watu kama kawaida
 
SEHEMU YA 89

yao walikuwa wamekusanyika mahakamani pale kwani waliona kwamba siku hiyo ndio ilikuwa siku ya kutangaza hukumu ile. Kutokana na wananchi kuweka shinikizo la kutaka kuiona kesi ile, kituo cha televisheni ya Taifa kikaruhusiwa kurusha moja kwa moja kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea mahakamani.
Andy akasimama kizimbani huku macho yake yakiwaangalia wazazi wake pamoja na mdogo wake, Esther. Moyoni alikuwa anaumia sana hasa kila alipokuwa akiwaangalia wanaume ambao walikuwa wamekusanyika mahali hapo.
Wakili Kelly akaanza kazi yake ya kumtetea Andy ambaye alikuwa amesimama kizimbani kimya. Wakili Kelly alionekana kuwa mjanja katika kila kitu abacho alikuwa akiongea mahali hapo huku kila mtu akiona dhahri kwamba Andy alikuwa akielekea kushinda kesi ile. Wakili Kelly aliendelea kuongea mambo mengi huku utetezi wake ukionekana kuwa na nguvu, zamu yake ilipokwisha, hakimu akaingilia.
“Tumesikiliza mambo mengi kutoka kwa wakili wa kujitegemea, Kelly. Hata kabla mahakama haijaamua kesi yako, kuna lolote ungependa kuiambia mahakama?” Hakimu wa kesi hiyo, Bi Beatrice alimuuliza Andy.
Andy akayatoa macho yake usoni mwa hakimu na kisha kuanza kuwaangalia watu ambao walikuwa wameingia ndani ya mahakama ile. Idadi kubwa ya watu ambao walikuwa ndani ya mahakama ile walikuwa wamekunja sura zao kuonyesha ni jinsi gani walikuwa na hasira juu yake.
“Mheshimiwa hakimu. Najua kwamba kila mtu ana hasira kali na mimi hasa kwa kile ambacho nimekifanya. Naomba watanzania waelewe kwamba nilifanya mauaji yale huku lengo langu likiwa ni kulipa kisasi” Andy alisema na kuendelea.
“Mara nyingi najifananisha na mkulima ambaye anatamani sana shamba lake liwe na mazao mazuri, kwangu mimi, Annastazia alionekana kama gugu, tena gugu kubwa ambalo lingeweza kuyaharibu mazao yote. Nilichokifanya kama mkulima, nikalikata gugu hilo” Andy alisema na kuendelea.
“Annastazia hakuwa mwanamke mzuri, alikuwa msaliti tena mkubwa hata zaidi ya Yuda. Nilimpenda sana mwanamke yule lakini kutokana na kuwasikiliza sana wazazi wake, akaamua kunisaliti. Niliumia sana, nilijiahidi kumuua kwa njia yoyote ile. Mara ya kwanza nilijaribu kulilipua gari lake, akanusurika na ndio maana nikaamua kumuua kwa mkono wangu mwenyewe” Andy aliiambia mahakama maneno ambayo yalionekana kumshtua kila mtu kwa kuona kuwa kumbe lile tukio la kulipuliwa kwa gari lilikuwa limefanywa na mtu huyo.
“Nimemuua Annastazia na wanawake wote kufuata baada yake kwani nimegundua kwamba wote hao wana roho kama yake. Ni bora niue mamilioni ili niokoe mabilioni mheshimiwa hakimu. Nitakapotoka hapa, nitaanza kazi yangu rasmi. Wanawake wote wa Tanzania watakuwa halali yangu” Andy aliiambia mahakama .
Kila mtu mahakamani akaonekana kushtuka. Maneno ambayo aliyaongea Andy yalionekana kumstaajabisha kila mtu aliyekuwa akiyasikia. Wakabaki
 
SEHEMU YA 90

wakimwangalia mara mbili mbili huku wakionekana kutokuamini kile ambacho alikuwa amekiongea.
Maswali mfululizo yakaanza kumiminika vichwani mwao, ilikuwaje Andy aongee maneno yale? Je alikuwa na uhakika wa kushinda kesi ile au la? Na kama alikuwa na uhakika, angeweza kutimiza kile ambacho alikuwa akikiongeakwa wakati ule? Kila maswali ambalo watu walijiuliza vichwani mwao wakakosa majibu.
“Nina kazi na wanawake wa Tanzania. Na ni lazima kazi hiyo niimalize. Nafikiri watoto ndio watakaobaki hai, ila hao wengine ni lazima niwamalize” Andy aliiambia mahakama.
“Kazi gani?” Hakimu alidakia.
“Kazi kubwa sana. Ni na uhakika kama kazi hiyo ningekuwa nimeifanya ni uhakika hata wewe usingekuwepo mahali hapa, inawezakana kwamba ungekuwa umekwishaoza kaburini” Andy alimwambia hakimu.
Hakimu akayatoa mawani yake kutoka machoni mwake na kisha kuanza kuyafuta. Maneno ambayo alikuwa ameyaongea Andy yalionekana kumchanganya, kitu ambacho alikiamua mahali hapo ni Andy kwenda kupimwa akili siku inayofuata kabla ya kesi kuendelea wiki ijayo na hukumu kusomwa.
Mahakama ikafungwa na hakimu kutoka. Minong’ono ilikuwa imetawala midomoni mwa watu ambao walikuja mahali hapo kushuhudia kesi ile. Andy akatolewa mahakamani huku akiwa katika ulinzi mzito na kisha kupandishwa kwenye karandinga kwa ajili ya kurudishwa remande ili kesho aende kupimwa akili kabla ya kesi kuendelea kwa siku ya mwisho ya hukumu.
****
“Watu wanaangamia. Dawa zinaelekea kuisha. Ninamtaka Andy mahali hapa haraka iwezekanavyo. Hata kama atakuwa akishikiliwa na mapolisi, sitojali kitu chochote. Ni ndani ya siku tatu tu, ninamtaka mahali hapa” Bwana Dawson aliwaambia vijana wake ambao aliwaajiri maalumu kwa ajili ya kumleta Andy mahali hapo.
“Sawa mkuu. Kuna kingine?”
“Ndio” Bwana Dawson alisema na kisha kuingia ndani, alipotoka alikuwa na sura ya bandia mkononi mwake na kuwapatia vijana wake pamoja na mfuko wa kaki ambao ulikuwa na dokumenti fulani ambazo aliziona kuhitajika mbele ya safari.
“Ninamtaka ndani ya siku tatu. Nitawapeni dola laki tano kuwasaidia. Kama mtaona kumpata itakuwa ngumu, tumieni risasi ili mladi tu apatikane niendelee na kazi nae” bwana Dowson alisema.
“Sawa mkuu”

Powell alikuwa mmoja wa vijana ambao walikuwa wametumwa na Bwana Dawson kwa ajili ya kumleta Andy nchini Marekani na kuendelea na mchakato wake wa kutengeneza fedha. Ilikuwa ni lazima Andy apelekwe nchini Marekani kwa ajili ya kufanya kile ambacho alitakiwa kukifanya kwa wakati huo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom