Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #101
SEHEMU YA 74
alikuwa amechoka na alishindwa kuendelea kukimbia, akaanza kumfuata mwanamke mmoja ambaye alikuwa pembeni kwenye giza pamoja na mtoto wake huku akiwa na shuka kubwa, alichokifanya ni kuingia ndani ya shuka hilo.
“Naomba unifiche....” Andy alimwambia mama yule huku akijifunika shuka lile.
Masikio yake yote yalikuwa yakisikiliza ni kitu gani ambacho kingeendelea mahali hapo. Ghafla akaanza kusikia vishindo vya watu wakija, walipofika karibu na lile eneo alilokuwa yule mama wakasimama na kuanza kumwangalia mama yule huku wakionekana kuwa na wasiwasi.
“Sisi ni mapolisi” Mwanaume mmoja alimwambia mama yule ambaye tayari woga ulianza kumshika.
Alijiona kutokuwa na jinsi, kama angeulizwa kuhusiana na Andy, mwanaume ambaye alikuwa amemficha basi ni lazima angemtaja kwani katika maisha yake alikuwa akiwaogopa sana mapolisi. Kitu cha pili ambacho alikiona kwamba ni lazima angemfichua Andy kule alipokuwa ni kwa sababu alikuwa hamfahamu hata kidogo. Asingekuwa tayari kuingia katika matatizo na wakati mtu ambaye alikuwa amemficha hakuwa akimfahamu.
Maswali mengi yakaanza kujikusanya kichwani mwake, kwa nini yule mwanaume alikuwa akikimbizwa na mapolisi? Kwa nini aliamua kumfuata yeye pale alipokuwa na kuhitaji hifadhi? Je alikuwa raia mwema au si raia mwema? Na kama alikuwa raia mwema kwa nini alikuwa akikimbizwa na mapolisi? Kila swali ambalo alikuwa akijiuliza kichwani lilimpa jibu kwamba ilikuwa ni lazima amtaje Andy ambaye alikuwa amejificha katika shuka lake.
“Kuna mtu tulikuwa tunamkimbiza, umemuona mahali hapa?” Polisi mmoja aliuliza.
“Ndio” Mwanamke yule alitoa jibu ambao lilimfanya Andy ndani ya shuka lile kupigwa na mshtuko mkubwa.
Mapolisi walionekana kuchanganyikiwa mara baada ya kufika katika barabara ya lami karibu kabisa na shule ya Sekondari ya Kiislamu ya Kinondoni na kutokumuona Andy, mtu ambaye walikuwa wakimkimbiza. Wakajaribu kuangaia huku na kule lakini wala hakuonekana machoni mwao.
Hawakujua kama Andy alikuwa amechukua daladala na kuondoka katika eneo hilo au alikuwa amevuka barabara na kuelekea upande wa pili. Kila kitu ambacho walikuwa wakijaribu kujiuliza kwa wakati huo wakakosa jibu kabisa hali iliyowafanya kukata tamaa kabisa.
Walitaka kuondoka mahali hapo ila kabla ya kuondoka wakaamua kwenda kuwauliza madereva taksi ambao walikuwa karibu na eneo lile, walijua fika kwamba madereva wale ni lazima wangejua mahali ambapo Andy alikuwa ameelekea kwa wakati huo.
“Mnamaanisha jamaa aliyekuwa na mchanganyiko wa rangi?” Dereva mmoja aliuliza.
“Ndiye huyo huyo”
“Musa alimchukua hapa kwenda nae upande ule wa Kaskazini. Sasa sijui walikuwa wakielekea mjini, Oysterbay au Coco Beach, ila Musa alimchukua” Dereva mmoja alijibu.
“Musa ndiye nani?” Polisi aliuliza.
“Dereva teksi mwenzetu wa kitengo hiki”
“Tunaweza kumpata muda gani?”
“Mmh! Labda mumsubiri mpaka atakaporudi”
“Hamna namba yake ya simu?”
“Aliibiwa wiki iliyopita. Hana hata hamu ya simu. Unacheza na Manzese nini” Dereva alijibu.
alikuwa amechoka na alishindwa kuendelea kukimbia, akaanza kumfuata mwanamke mmoja ambaye alikuwa pembeni kwenye giza pamoja na mtoto wake huku akiwa na shuka kubwa, alichokifanya ni kuingia ndani ya shuka hilo.
“Naomba unifiche....” Andy alimwambia mama yule huku akijifunika shuka lile.
Masikio yake yote yalikuwa yakisikiliza ni kitu gani ambacho kingeendelea mahali hapo. Ghafla akaanza kusikia vishindo vya watu wakija, walipofika karibu na lile eneo alilokuwa yule mama wakasimama na kuanza kumwangalia mama yule huku wakionekana kuwa na wasiwasi.
“Sisi ni mapolisi” Mwanaume mmoja alimwambia mama yule ambaye tayari woga ulianza kumshika.
Alijiona kutokuwa na jinsi, kama angeulizwa kuhusiana na Andy, mwanaume ambaye alikuwa amemficha basi ni lazima angemtaja kwani katika maisha yake alikuwa akiwaogopa sana mapolisi. Kitu cha pili ambacho alikiona kwamba ni lazima angemfichua Andy kule alipokuwa ni kwa sababu alikuwa hamfahamu hata kidogo. Asingekuwa tayari kuingia katika matatizo na wakati mtu ambaye alikuwa amemficha hakuwa akimfahamu.
Maswali mengi yakaanza kujikusanya kichwani mwake, kwa nini yule mwanaume alikuwa akikimbizwa na mapolisi? Kwa nini aliamua kumfuata yeye pale alipokuwa na kuhitaji hifadhi? Je alikuwa raia mwema au si raia mwema? Na kama alikuwa raia mwema kwa nini alikuwa akikimbizwa na mapolisi? Kila swali ambalo alikuwa akijiuliza kichwani lilimpa jibu kwamba ilikuwa ni lazima amtaje Andy ambaye alikuwa amejificha katika shuka lake.
“Kuna mtu tulikuwa tunamkimbiza, umemuona mahali hapa?” Polisi mmoja aliuliza.
“Ndio” Mwanamke yule alitoa jibu ambao lilimfanya Andy ndani ya shuka lile kupigwa na mshtuko mkubwa.
Mapolisi walionekana kuchanganyikiwa mara baada ya kufika katika barabara ya lami karibu kabisa na shule ya Sekondari ya Kiislamu ya Kinondoni na kutokumuona Andy, mtu ambaye walikuwa wakimkimbiza. Wakajaribu kuangaia huku na kule lakini wala hakuonekana machoni mwao.
Hawakujua kama Andy alikuwa amechukua daladala na kuondoka katika eneo hilo au alikuwa amevuka barabara na kuelekea upande wa pili. Kila kitu ambacho walikuwa wakijaribu kujiuliza kwa wakati huo wakakosa jibu kabisa hali iliyowafanya kukata tamaa kabisa.
Walitaka kuondoka mahali hapo ila kabla ya kuondoka wakaamua kwenda kuwauliza madereva taksi ambao walikuwa karibu na eneo lile, walijua fika kwamba madereva wale ni lazima wangejua mahali ambapo Andy alikuwa ameelekea kwa wakati huo.
“Mnamaanisha jamaa aliyekuwa na mchanganyiko wa rangi?” Dereva mmoja aliuliza.
“Ndiye huyo huyo”
“Musa alimchukua hapa kwenda nae upande ule wa Kaskazini. Sasa sijui walikuwa wakielekea mjini, Oysterbay au Coco Beach, ila Musa alimchukua” Dereva mmoja alijibu.
“Musa ndiye nani?” Polisi aliuliza.
“Dereva teksi mwenzetu wa kitengo hiki”
“Tunaweza kumpata muda gani?”
“Mmh! Labda mumsubiri mpaka atakaporudi”
“Hamna namba yake ya simu?”
“Aliibiwa wiki iliyopita. Hana hata hamu ya simu. Unacheza na Manzese nini” Dereva alijibu.