Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #121
SEHEMU YA 91
Mikakati kabambe ikaandaliwa, vijana nane wakatafutwa, vijana ambao hawakuwa na hata na chembe yoyote ya woga, vijana ambao walikuwa na uzoefu mkubwa wa kutumia bunduki wakati wowote na sehemu yoyote bila kuogopa kitu chochote kile.
Vijana nane tayari walikuwa wamekamilika na kitu ambacho kilifanyika ni kuanza kusafiri kuelekea Tanzania. Kwa kuwa walitumia usafiri wa ndege ya kukodi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana Dawson wala hawakutumia muda mrefu angani wakawa wamekwishafika Tanzania.
Walichokifanya mahali hapo ni kuchukua vyumba katika hoteli ya The Cape na kisha kupumzika. Usiku hawakulala, kitu ambacho walikuwa wakikifanya ni kukusanyika katika chumba kimoja na kuanza kupanga mipango juu ya namna ya kumchukua Andy na kuanza kurudi nae nchini Marekani.
Nchi ya Tanzania wala haikuwaogopesha hata kidogo kwani kwao waliuona ulinzi wa nchi hiyo kuwa ndogo sana na hivyo kuwapa nafasi kubwa sana ya kumchukua Andy salama salimini. Kikao chao cha siri kilichukua dakika thelathini, kila mmoja akaelekea chumbani mwake huku wakimuacha Powell ndani ya chumba kile.
Hawakutaka kuchelewa, siku iliyofuata wakakodi gari moja kwa moja kuanza kuelekea katika sehemu ambayo waliiona kufaa kwa kufanya tukio moja muhimu ambalo walitakiwa kulifanya kwa wakati huo huku wakiwa na bunduki zao zilizokuwa zimejaa risasi.
“Na vipi kuhusu Michael?” Shawn aliuliza
“Amekwishafika jana usiku kwa kutumia boti ile ile ya bosi iendayo kasi. Kinachosubiriwa ni sisi tu” Powell alijibu.
“Na umekwishamwambia wapi pa kuonana?”
“Ndio. Kuna ufukwe unaitwa Coco ambapo hapo ndipo tutakapokutania na kuanza safari yetu. Natumaini hii itakuwa kazi nyepesi sana” Powell alisema huku wakiwa wanaingia eneo la Mnazi Mmoja ikiwa imetimia saa moja na nusu asubuhi.
****
Watanzani walikuwa wakizidi kumiminika ndani ya mahakama kuu ya Tanzania kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya kesi hiyo ya mauaji ambayo inamkabili Andy ambayo ilikuwa imevuma kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwili.
Kila mtu alikuwa akitamani hakimu amhukumu kifo Andy kwa kile ambacho alikuwa amekifanya kwa kumuua Spika wa Bunge la Tanzania, Bi Annastazia Kapama. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walizidi kuongezeka mahakamani hapo kiasi ambacho watu wengine wakazuiliwa na kutakiwa kusimama nje ya mahakama hiyo.
Kama kawaida, waandishi wa habari walikuwa wakiendelea na kazi yao ya kupiga picha na kuandika mambo mbalimbali ambayo yalikuwa yakiendelea mahali hapo. Ingawa karandinga ilitakiwa kuingia hapo saa mbili kamili asubuhi hiyo lakini watu waliiona karandinga hiyo ikichelewa kufika mahali hapo.
Mikakati kabambe ikaandaliwa, vijana nane wakatafutwa, vijana ambao hawakuwa na hata na chembe yoyote ya woga, vijana ambao walikuwa na uzoefu mkubwa wa kutumia bunduki wakati wowote na sehemu yoyote bila kuogopa kitu chochote kile.
Vijana nane tayari walikuwa wamekamilika na kitu ambacho kilifanyika ni kuanza kusafiri kuelekea Tanzania. Kwa kuwa walitumia usafiri wa ndege ya kukodi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana Dawson wala hawakutumia muda mrefu angani wakawa wamekwishafika Tanzania.
Walichokifanya mahali hapo ni kuchukua vyumba katika hoteli ya The Cape na kisha kupumzika. Usiku hawakulala, kitu ambacho walikuwa wakikifanya ni kukusanyika katika chumba kimoja na kuanza kupanga mipango juu ya namna ya kumchukua Andy na kuanza kurudi nae nchini Marekani.
Nchi ya Tanzania wala haikuwaogopesha hata kidogo kwani kwao waliuona ulinzi wa nchi hiyo kuwa ndogo sana na hivyo kuwapa nafasi kubwa sana ya kumchukua Andy salama salimini. Kikao chao cha siri kilichukua dakika thelathini, kila mmoja akaelekea chumbani mwake huku wakimuacha Powell ndani ya chumba kile.
Hawakutaka kuchelewa, siku iliyofuata wakakodi gari moja kwa moja kuanza kuelekea katika sehemu ambayo waliiona kufaa kwa kufanya tukio moja muhimu ambalo walitakiwa kulifanya kwa wakati huo huku wakiwa na bunduki zao zilizokuwa zimejaa risasi.
“Na vipi kuhusu Michael?” Shawn aliuliza
“Amekwishafika jana usiku kwa kutumia boti ile ile ya bosi iendayo kasi. Kinachosubiriwa ni sisi tu” Powell alijibu.
“Na umekwishamwambia wapi pa kuonana?”
“Ndio. Kuna ufukwe unaitwa Coco ambapo hapo ndipo tutakapokutania na kuanza safari yetu. Natumaini hii itakuwa kazi nyepesi sana” Powell alisema huku wakiwa wanaingia eneo la Mnazi Mmoja ikiwa imetimia saa moja na nusu asubuhi.
****
Watanzani walikuwa wakizidi kumiminika ndani ya mahakama kuu ya Tanzania kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya kesi hiyo ya mauaji ambayo inamkabili Andy ambayo ilikuwa imevuma kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwili.
Kila mtu alikuwa akitamani hakimu amhukumu kifo Andy kwa kile ambacho alikuwa amekifanya kwa kumuua Spika wa Bunge la Tanzania, Bi Annastazia Kapama. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walizidi kuongezeka mahakamani hapo kiasi ambacho watu wengine wakazuiliwa na kutakiwa kusimama nje ya mahakama hiyo.
Kama kawaida, waandishi wa habari walikuwa wakiendelea na kazi yao ya kupiga picha na kuandika mambo mbalimbali ambayo yalikuwa yakiendelea mahali hapo. Ingawa karandinga ilitakiwa kuingia hapo saa mbili kamili asubuhi hiyo lakini watu waliiona karandinga hiyo ikichelewa kufika mahali hapo.