stevewritter
Member
- Sep 6, 2019
- 35
- 31
🗣shunie kuja apa uendeleeSehemu ya 36
Hakuna kitu nilikuwa sipendi kama kwenda Mwanza, sio kwamba mji ule nilikuwa siupendi.
Laa! Ila nafsi yangu ilikuwa haipendi kupata kumbukumbu ya kitendo cha kuitelekeza familia yangu hospitali ya Bugando na kutimkia mjini Tabora kwa Lawalawa.
Tukio hilo lilizidi kunitesa kisaikolojia, kila wakati sauti ya mke wangu Pili ikinisihi nisiwaache ilikuwa ikijirudia. Picha ya mwanangu akiwa anateseka kitandani ikawa inajitengeneza kichwani mwangu.
Tulicheza mchezo wetu na timu ya Kigoma fc, mchezo huo tukashinda mabao matatu kwa bila, wakati magoli mawili nikifunga mwenyewe huku lile moja nikitoa asist.
Siku chache baada ya mchezo huo, kocha akatutaka wachezaji tujitayarishe kwa safari ya Mwanza kwa ajili ya mchezo wa na Igogo fc, siku hiyo kutwa nzima nilikosa raha. Kwa kweli sikupenda kabisa kufika katika jiji lile.
Siku ya pili tuliondoka na treni kuelekea Mwanza, wachezaji tulikuwa kwenye mabehwa ya daraja la kwanza. Wakati wenzangu wakicheza karata na kufurahia pamoja safarini, mimi nilikuwa peke yangu nikiwa nimezama kwenye lindi la mawazo.
“Unamuwa nini?” daktari wa timu aliniuliza.
“Hapana naifikiria mechi tu.” nilimdanganya
“Una presha?”
“Ndio, si unajua ni timu niliyotokea.”daktari yule ambaye pia alikuwa mtaalamu wa mambo ya saikolojia alianza kunijenga kiakili.
Tuliwasili Mwanza asubuhi ya siku iliyofuatia, tulifikia katika lodge moja nzuri tu ambayo kwa kweli jina lake sikumbuki vizuri. Baada ya kupumzika kidogo, niliomba ruhusa ya kutoka.
Kwa kuwa walitambua nilikuwa mwenyeji kwenye mji ule, hilo halikuwa tatizo kwao, viongozi wangu wa timu waliniruhusu.
Nilichukua gari hadi Bugando, nikaelekea hadi katika ofisi ya daktari aliyekuwa akimuuguza mwanangu. Kwa bahati nzuri nilimkuta hana wagonjwa wengi, alinikaribisha kitini na kunisikiliza:
“Unanikumbuka dokta?” nilimuliza.
“Vizuri sana, nakukumbuka. Wewe si baba wa yule mtoto aliyekuwa anaumwa kansa ya damu?”
“Naam!! ndio mimi dokta, tangu kipindi kile ndio narudi Mwanza leo.”
“Kwa hiyo huna taarifa ya kilichomkuta mwanao?” dokta aliuliza huku akiningalia kwa chati.
“Sina dokta. ”
“Yule mtoto alifariki dunia,”dokta aliniambia kwa ufupi.