bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,095
SISTER MURCIA.
NA HEMED MAYUGU.
NO. (01).
Ni sister ambaye alikuwa na upako mkubwa na
inasadikika alikuwa na uwezo wa kuomba chochote
na mungu akamtekelezea. hata kama alikuwa na
njaa yeye alishushiwa chakuala mahara popote.
Licha ya kuwa na upeo mkubwa. syster murcia
alikwenda kuongeza elimu yake italia.
Baada ya mwaka mmoja alirudi Tanzania kutoka
masomoni.
Alipofika akapewa taarifa kuwa kuna kijiji kimoja
kinaogopwa hasa. watu wageni na watumishi wa
mungu wakienda huko wanauliwa.
Kwa kukatwa katwa mapanga na sehemu zao za siri
kuchukuliwa kwa wanaume na wanawake hubakwa
na kutupwa misituni kama chakula cha mizimu.
Mbali na hilo pia watu hao wanaamini sana imani za
kishirikina.
Baada ya maelezo hayo sister murcia aliombwa
yeye aende huko kwenye hicho kijiji cha kutisha kwa
ajili ya kuiokoa jamii hio na imani potofu imani ya
kishetani na uchawi.
Sister Murcia akakubali kuwa yeye anaweza
kulifanya hilo. kwa imani kubwa ya mungu wake.
Safari yake alikuwa ameambatana na mabint wawili.
Mercia na Alicia mabint hao walikuwa ni wanafunzi
wake. Pia alikuwepo kijana mmoja wa kiume yeye
alijulikana kwa jina la Lukas na deleva wa gari. huyu
aliitwa kwa jina la Moris. Moris ndiye pekee alikuwa
anakijua kijiji hicho. Safari ilianza ya kuelekea katika
kijiji hicho cha kutisha.
Wakiwa njiani walikutana na vitu vingi vya kutisha
kama vyungu vilivyokuwa vimetanda kila mahara
zenye njia panda, mizoga ya wanyama hasa kuku
wekundu na njiwa zilikuwa zimefungwa kwenye miti
imening'inia. Ilikuwa ni safari ya kutisha kweli muda
wote walikuwa wameshikilia Rozari zao wakiomba
mungu awafikishe salama katika kijiji hicho. Masaa
yalikwenda lakini kufikia tamati ya safari yao
ulikuwa ni mtihani mkubwa hatimaye ilitimu mida ya
saa moja za usiku hali iliamza kubadilika kabisa
sauti na miungurumo za ajabu zikaanza kusikika.
Watu wengine walianza kuogopa lakini sister murcia
aliwambia wasiogope wamtumainie mungu na
bwana aliye hai.
Wakiwa wanaendele kukisogelea kijiji hicho gari
ilizima. kupiga sitata ikagoma. Dereva akashuka na
Lucas kuangalia nini kinasumbua gari. lakini hakuon
tatizo. akaomba mercia, Alicia na sister Murcia
washuke wasaidie kuisukuma gari. Ilikuwa ni ngumu
sana kwa Alicia na Mercia kushuka kwenye gari,
mazingira yaliwatisha sana. Kwa ujasiri wa sister
murcia aliwambia vijana wake mericia na Alicia
washuke kwenye gari wasaidie kusukuma.
Kwa pamoja walishuka na kuanza kulisukuma gari,
lakini ilikuwa aisaidii gari iligoma kabisa kutoka.
Waliangaika kama Robo saa lakini hawakufanikiwa
gari liligoma liligoma.
Moris aliangalia tena kama kweli kuna tatizo lakini
tatizo halikuonekana. Wakiwa wanaangaika, kilitokea
kiumbe cha ajabu mbele yao kiumbe hicho kilikuwa
kama mtu lakini chenye mapembe. Uso wake
umetapakaa Damu. Alicia mercia na Lucas. Wote
wakakimbilia kuingia ndani ya Gari. Inje akabaki
Sister Murcia pekee.
Kiumbe kile kililisogerea gari lakini kabla akijalifikia
ulitokea moto ukakizoa na kutupilia pembezoni mwa
barabara na kukiteketeza. Hayo yote yakiwa ni
maombi ya Sister murcia. Baada ya tukio hilo
Pale pale na gari likawaka. Soster murcia akaingia
kwenye Gari na kuwambia vijana wake. "Hakuna njia
njema kama kumwamini mungu na kukaa na imani
thabiti msiyumbe shetani atawaingia kirahisi"
Baada ya kuambia hivyo wote waliitikia sawa na
gari kuondoka. waliivumilia sana safari yao ya
kutisha Usiku mida ya saa mbili na dakika 48
walifanikiwa kukifikia kijiji hicho cha kutisha.
Walilifikia kanisa la kijini hapo. Kanisa lililokuwa
njiani tu. Mazingira ya kanisa hilo yalitisha sana
kulikuwa pachafu sana mapopo ndio lilikuwa ni
makazi yao. Wanyama kama mbwa ndio yalikuwa
makazi yao. Kiujumla ilikuwa ni harufu mbaya kila
mahara ndani ya kanisa hilo. Kwa uzuri walikuwa na
taa zao wakaingia na kuangalia hali ya kanisa
ikawashinda. Wakarudi wakamuomba Dereva wa
gari(Moris), awapeleke kwa uongozi wa kijiji hicho.
Moris aliwambia hapajui na katika kijiji hicho watu
wote huwa wanalala saa moja kuanzia saa 12:30
huwa wanajifungia ndani ya nyumba zao.
Walipoangalia saa zao tayari ilikuwa imetimu mida
ya saa tatu na nusu. Baada ya kuona hivyo syster
murcia aliomba walale ndani ya gari wangoje kesho
ndio waende kuuona uongozi.
"Sister kwanini tusiende kuwaamsha"
Alicia alisema. Bint huyo aliyekuwa mdogo kuliko
wote yeye alikuwa ni muoga hasa mazingira yale
aliyaogopa kabisa. Mambo na Vitu alivyokutana
navyo njiani pindi wanaelekea ndani ya kijiji hicho
yalimtisha. Kijiji hicho kwa jina kilijulikana kwa jina
la Shimo la moto kiliogopeka sana hakuna mgeni
aliyeweza kufika huko na kudumu. Ila wenyeji tu
hata vijana waliokulia huko wakafanikiwa kutokako,
waliogopa kabisa kurudiko.
"Alicia we ni mtoto mwema wa mungu ingieni ndani
ya Gari hakika ulinzi wa mungu u juu yetu tumekuja
kuzipigania Roho za watu wapate uongofu wa
mungu"
Sister Murcia alisema.
"Sawa sister Murcia. Lakini hawa inaonekana
washagongwa mihuri ya shetani hawawezi kutoka
huko"
Alicia alisema.
"Alicia hii ni jamii ya kiafrika hata wewe, babu wa
babu yako alikuwa kama hawa je usingekuja
ukombozi juu yao kutoka kwa watu kama wewe
unazani wewe ungekuwa wapi?"
Sister murcia alimwambia Alicia
Kwa usikivu na utiifu wa mwalimu wao Alicia Lucas
na Mercia waliingia kwenye gari.
Wakala chakula chao walichokuwa ameambatana
nacho. Walipomaliza kula.
Wote kwa pamoja wakaanza kuisoma sala ya
salamu maria kisha Baba yetu uliyembinguni.
Walipomaliza kuzisoma izo sister murcia akaingoza
sala ya kulala. Vijana wake walilala lakini murcia
alitoka ndani ya gari na akatandika kitambaa chake
akakiweka kitabu chake kitakatifu cha biblia kisha
akapiga magoti na kuanza Maombi.
Hakiwa anaendelea nyuma kilitokea kikundi cha
watu.
NA HEMED MAYUGU.
NO. (01).
Ni sister ambaye alikuwa na upako mkubwa na
inasadikika alikuwa na uwezo wa kuomba chochote
na mungu akamtekelezea. hata kama alikuwa na
njaa yeye alishushiwa chakuala mahara popote.
Licha ya kuwa na upeo mkubwa. syster murcia
alikwenda kuongeza elimu yake italia.
Baada ya mwaka mmoja alirudi Tanzania kutoka
masomoni.
Alipofika akapewa taarifa kuwa kuna kijiji kimoja
kinaogopwa hasa. watu wageni na watumishi wa
mungu wakienda huko wanauliwa.
Kwa kukatwa katwa mapanga na sehemu zao za siri
kuchukuliwa kwa wanaume na wanawake hubakwa
na kutupwa misituni kama chakula cha mizimu.
Mbali na hilo pia watu hao wanaamini sana imani za
kishirikina.
Baada ya maelezo hayo sister murcia aliombwa
yeye aende huko kwenye hicho kijiji cha kutisha kwa
ajili ya kuiokoa jamii hio na imani potofu imani ya
kishetani na uchawi.
Sister Murcia akakubali kuwa yeye anaweza
kulifanya hilo. kwa imani kubwa ya mungu wake.
Safari yake alikuwa ameambatana na mabint wawili.
Mercia na Alicia mabint hao walikuwa ni wanafunzi
wake. Pia alikuwepo kijana mmoja wa kiume yeye
alijulikana kwa jina la Lukas na deleva wa gari. huyu
aliitwa kwa jina la Moris. Moris ndiye pekee alikuwa
anakijua kijiji hicho. Safari ilianza ya kuelekea katika
kijiji hicho cha kutisha.
Wakiwa njiani walikutana na vitu vingi vya kutisha
kama vyungu vilivyokuwa vimetanda kila mahara
zenye njia panda, mizoga ya wanyama hasa kuku
wekundu na njiwa zilikuwa zimefungwa kwenye miti
imening'inia. Ilikuwa ni safari ya kutisha kweli muda
wote walikuwa wameshikilia Rozari zao wakiomba
mungu awafikishe salama katika kijiji hicho. Masaa
yalikwenda lakini kufikia tamati ya safari yao
ulikuwa ni mtihani mkubwa hatimaye ilitimu mida ya
saa moja za usiku hali iliamza kubadilika kabisa
sauti na miungurumo za ajabu zikaanza kusikika.
Watu wengine walianza kuogopa lakini sister murcia
aliwambia wasiogope wamtumainie mungu na
bwana aliye hai.
Wakiwa wanaendele kukisogelea kijiji hicho gari
ilizima. kupiga sitata ikagoma. Dereva akashuka na
Lucas kuangalia nini kinasumbua gari. lakini hakuon
tatizo. akaomba mercia, Alicia na sister Murcia
washuke wasaidie kuisukuma gari. Ilikuwa ni ngumu
sana kwa Alicia na Mercia kushuka kwenye gari,
mazingira yaliwatisha sana. Kwa ujasiri wa sister
murcia aliwambia vijana wake mericia na Alicia
washuke kwenye gari wasaidie kusukuma.
Kwa pamoja walishuka na kuanza kulisukuma gari,
lakini ilikuwa aisaidii gari iligoma kabisa kutoka.
Waliangaika kama Robo saa lakini hawakufanikiwa
gari liligoma liligoma.
Moris aliangalia tena kama kweli kuna tatizo lakini
tatizo halikuonekana. Wakiwa wanaangaika, kilitokea
kiumbe cha ajabu mbele yao kiumbe hicho kilikuwa
kama mtu lakini chenye mapembe. Uso wake
umetapakaa Damu. Alicia mercia na Lucas. Wote
wakakimbilia kuingia ndani ya Gari. Inje akabaki
Sister Murcia pekee.
Kiumbe kile kililisogerea gari lakini kabla akijalifikia
ulitokea moto ukakizoa na kutupilia pembezoni mwa
barabara na kukiteketeza. Hayo yote yakiwa ni
maombi ya Sister murcia. Baada ya tukio hilo
Pale pale na gari likawaka. Soster murcia akaingia
kwenye Gari na kuwambia vijana wake. "Hakuna njia
njema kama kumwamini mungu na kukaa na imani
thabiti msiyumbe shetani atawaingia kirahisi"
Baada ya kuambia hivyo wote waliitikia sawa na
gari kuondoka. waliivumilia sana safari yao ya
kutisha Usiku mida ya saa mbili na dakika 48
walifanikiwa kukifikia kijiji hicho cha kutisha.
Walilifikia kanisa la kijini hapo. Kanisa lililokuwa
njiani tu. Mazingira ya kanisa hilo yalitisha sana
kulikuwa pachafu sana mapopo ndio lilikuwa ni
makazi yao. Wanyama kama mbwa ndio yalikuwa
makazi yao. Kiujumla ilikuwa ni harufu mbaya kila
mahara ndani ya kanisa hilo. Kwa uzuri walikuwa na
taa zao wakaingia na kuangalia hali ya kanisa
ikawashinda. Wakarudi wakamuomba Dereva wa
gari(Moris), awapeleke kwa uongozi wa kijiji hicho.
Moris aliwambia hapajui na katika kijiji hicho watu
wote huwa wanalala saa moja kuanzia saa 12:30
huwa wanajifungia ndani ya nyumba zao.
Walipoangalia saa zao tayari ilikuwa imetimu mida
ya saa tatu na nusu. Baada ya kuona hivyo syster
murcia aliomba walale ndani ya gari wangoje kesho
ndio waende kuuona uongozi.
"Sister kwanini tusiende kuwaamsha"
Alicia alisema. Bint huyo aliyekuwa mdogo kuliko
wote yeye alikuwa ni muoga hasa mazingira yale
aliyaogopa kabisa. Mambo na Vitu alivyokutana
navyo njiani pindi wanaelekea ndani ya kijiji hicho
yalimtisha. Kijiji hicho kwa jina kilijulikana kwa jina
la Shimo la moto kiliogopeka sana hakuna mgeni
aliyeweza kufika huko na kudumu. Ila wenyeji tu
hata vijana waliokulia huko wakafanikiwa kutokako,
waliogopa kabisa kurudiko.
"Alicia we ni mtoto mwema wa mungu ingieni ndani
ya Gari hakika ulinzi wa mungu u juu yetu tumekuja
kuzipigania Roho za watu wapate uongofu wa
mungu"
Sister Murcia alisema.
"Sawa sister Murcia. Lakini hawa inaonekana
washagongwa mihuri ya shetani hawawezi kutoka
huko"
Alicia alisema.
"Alicia hii ni jamii ya kiafrika hata wewe, babu wa
babu yako alikuwa kama hawa je usingekuja
ukombozi juu yao kutoka kwa watu kama wewe
unazani wewe ungekuwa wapi?"
Sister murcia alimwambia Alicia
Kwa usikivu na utiifu wa mwalimu wao Alicia Lucas
na Mercia waliingia kwenye gari.
Wakala chakula chao walichokuwa ameambatana
nacho. Walipomaliza kula.
Wote kwa pamoja wakaanza kuisoma sala ya
salamu maria kisha Baba yetu uliyembinguni.
Walipomaliza kuzisoma izo sister murcia akaingoza
sala ya kulala. Vijana wake walilala lakini murcia
alitoka ndani ya gari na akatandika kitambaa chake
akakiweka kitabu chake kitakatifu cha biblia kisha
akapiga magoti na kuanza Maombi.
Hakiwa anaendelea nyuma kilitokea kikundi cha
watu.