SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,413
- 23,712
- Thread starter
- #161
*ROHO YAKE INADAI --- 34*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
.
.
Muda kidogo, yule polisi aliyekuwa amekaa dirishani akimtazama mwenzake, akamwona mtu fulani akiwa anakuja kumjongea mwenziwe na wale watoto. Alimtazama mtu huyo lakini hakuweza kumtambua. Mtu huyo alikuwa akiambatana na mtoto mwingine kwa pembeni yake.
.
.
Akajaribu kumshtua mwenzake, “Tazama nyuma yako! Hey! Tazama!”
.
.
ENDELEA
.
.
Mwenzake huyo alipotazama, kabla hajajitetea na bunduki yake, akanyakwa koo na kunyanyulia juu haswa kisha akaminywa kwanguvu mpaka koo lake kuanza kuchuruza damu. Bunduki ambayo huenda ingemsaidia kutetea uhai wake, ikadondokea chini.
.
.
“Hapana! Hapana!” mwenzake akatahamaki pale dirishani. Upesi akatoka kwenda kumsaidia mwenzake abaki na pumzi. Alipofungua mlango, akamnyooshea mtu yule bunduki na kumfyatulia tatu. Ajabu hazikusaidia. Zaidi yule mtu wa ajabu akamtupia mwenzake chini na kumfuata yeye kwa kasi!
.
.
Naye akamyaka shingo na kumnyanyua juu, akamminya koo na kumpasua, kisha akalichanja na kumfanya avuje damu kama sharubati toka kwenye kopo. Polisi huyo akapoteza uhai. Dubwana hilo likamtupa na kisha likapotea zake!
.
.
Baadhi ya watu wakafungua milango na madirisha kutazama. Milio ya risasi iliwaamsha na kuwapa mashaka. Wakaona maiti mbili za polisi na wale watoto wakiwa wanatembea. Kwakuwa hali ilikuwa shwari, wakatoka kwenda kutazama.
.
.
Waliwaokoa wale watoto na pia wakatoa taarifa polisi wakidhani polisi wameuawa na majambazi baada ya kurushiana risasi.
.
.
Muda mfupi, polisi wengine wakaja na kuanza kuipemua miili na kukusanya taarifa toka kwa washuhudiaji. Hawakuelewa jambo. Hakuna aliyesema amewaona hao watu waliokuwa wanapambana na polisi, lakini pia vilevile hakuna aliyetoa maelezo ya kueleweka juu ya watoto wale mapacha waliokuwa wanatembea wenyewe usiku huo.
.
.
Wakiwa kwenye mahangaiko ya kutafuta taarifa sahihi, Mama Brian akatoka akiwa amejikunyata, amejifunika blanketi, akawaambia polisi, “Mimi najua nani waliyekuwa wanapambana naye.” kwa maelezo zaidi, polisi mmoja akaongozana na Mama Brian kwenda ndani kumhoji.
.
.
“ … Mtu huyo ndiye ambaye hupoteza watoto kila siku. Polisi hao walipotaka kuwaokoa watoto hao, ndipo akajiri na kuwamaliza,” Mama Brian akaeleza. Polisi akamuuliza, “Unamjua yupoje na wapi anaishi?”
.
.
Mama Brian akanyamaza kwanza kisha akauliza, “Hata nikisema mtasadiki?”
.
.
“Usijali,” Polisi akamtoa hofu. “Unaweza tu kueleza.” basi Mama Brian akamweleza kinagaubaga ya kuwa mtu huyo ni Helo, Hernandez Lorenzo, wa miaka mingi iliyopita. Nyumba yake ipo msituni na anafanya kila anachofanya kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa mji wa Boston.
.
.
Polisi akanakili maelezo yake yote, ila yakamletea shaka kwenye kuamini. Simulizi ile ilikuwa ni ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia. Ni kwa namna gani mtu mfu akarejea na kufanya mauaji?
.
.
“Nashukuru sana.” Polisi akampatia mkono na kunyanyuka, “Naweza kwenda sasa. Au kuna cha ziada wataka kuniambia?”
.
.
Mama Brian akamjibu, “Ndio, kipo!”
.
.
“Niambie.” Polisi akasema akimpatia masikio yake kwa utulivu. Mama Brian akasema, “nendeni mkatazame kwenye korongo la kanisa …”
.
.
.
**
.
.
.
Gari la polisi lilisimama, wakashuka wanaume wawili waliovalia sare. Mmoja wao alikuwa ni yule Polisi aliyemhoji Mama Brian. Mkononi alikuwa amebebelea ngowe ya mawasiliano na bunduki ndogo. Mwenzake anayemfuatia alikuwa mikono mitupu ila viganja vyake vikiwa karibu na mkanda wake uliobebelea silaha.
.
.
Ndani ya muda mfupi, wakaonana na Padri Alfonso na Dada Magdalena, wakawafanyia mahojiano mafupi kabla ya kuwataka waongozane kwenda korongoni. Padri Alfonso akapata shaka, akauliza, “Afisa, kuna lolote lile?”
.
.
“Tunataka kupatazama!” Polisi akasema kwa amri basi Padri Alfonso na Dada Magdalena wakaongozana nao kwenda huko kwenye korongo. Walipofika, polisi hao wakangaza na kuangaza, hawakuona kitu.
.
.
“Mnaweza kutuambia mnatafuta nini ili tuwasaidie?” akauliza Padri Alfonso. Polisi akamwambia, “Usijali.” kisha wakajikokota zao kwenda kwenye usafiri wao na kutimka.
.
.
“Hamna kitu!” akasema Polisi dereva na kuongezea, “Nilijua tu mama yule atakuwa na matatizo.” wakayoyoma wakati Padri Alfonso na Dada Magdalena wakiwatazama. Walipoishilia, Padri Alfonso akauliza, “Watakuwa wameambiwa na nani kuhusu korongo lile?”
.
.
Dada Magdalena akajibu, “Si wengine bali wale waliokuja kulitembelea.” Basi Padri Alfonso akashusha pumzi ndefu na kusema, “Nadhani umefikia mwisho wao!” na mara katikati yao akasonga mtumishi mwingine. Naye alikuwa ni Dada kama yule Magdalena, akasimama kandokando yao na kuuliza, “Nami nafanyaje?”
.
.
Padri Alfonso akamtazama na kuweka mkono wake begani. Kumbe alikuwa Dada yule aliyekumbwa na kadhia na yule polisi wa mwanzoni wakiwa korongoni kuwafuata wakina Brian.
.
.
“Dada Marietta, wewe bado u mpya kabisa,” akasema Padri Alfonso. “Utafanya kazi pamoja na Dada Magdalena akuonyeshe namna ya kuenenda. Ila bila shaka usiku wa leo umekuwa mrefu sana, tuuache uende.”
.
.
Dada hao wakainamisha vichwa vyao, Padri akaenda zake.
.
.
**
.
.
Saa nane ya mchana …
.
.
Akiwa juu ya baiskeli yake, Brian alirusha macho yake huku na kule kuangazia kama kuna tangazo jipya la watoto waliopotea. Hakukuwapo, yote yalikuwa ya zamani. Mpaka anafika nyumbani hakuona tangazo lolote tofauti na yale aliyoyaona hapo kabla.
.
.
Akazama ndani na kuteta machache na Wisconsin juu ya mpango wao. Bwana huyo akamwambia kuwa siku hiyo wataenda kumtembelea Brewster majira ya usiku. Brian akauliza, “Haitakuwa hatari kutokana na yale yaliyotokea jana yake?”
.
.
Wisconsin akakuna kidevu chake na kumwambia Brian, “Hatuna muda, ni lazima tufanye hivyo. Kama tusipoyatembelea maeneo haya tukiwa na mwili wa nyama, basi itakuwia vigumu utakapoenda huko kiroho. Lazima ujue ni maeneo yapi utakayokatiza na kuyafanyia kazi.”
.
.
Basi japo kishingo upande, Brian akaridhia. Akala na kupumzika kidogo. Baadae kwenye majira ya jioni akajikwea kwenye baiskeli yake na kwenda kule kwenye makazi ya marehemu Dkt Hamill. Alipoingia, akaegesha baiskeli yake pembeni kidogo ya geti kisha akaanza kusonga kuendea jengo hilo.
.
.
Akiwa bado hajalifikia, akastaajabu kusikia sauti ya geti likifungwa. Akapata shaka. Haraka akakimbilia getini na kujaribu kulifungua. Halikufunguka. Akajaribu kwanguvu zote lakini bure, hakuweza kufungua. Akajiuliza nani kamfungia humo?
.
.
Akapigapiga geti kwanguvu akiita watu wamsaidie lakini hakuna mtu aliyemsikia wala kujali. Mpaka mikono ikawa inamuuma asifanikiwe kitu. Mara akasikia sauti nyuma yake ikimwambia, “Acha kujichosha, Brian.”
.
.
Haraka akatazama nani huyo amwongeleshaye, hamaki akamwona Brewster! Alikuwa amesimama mbele ya mlango wa jengo akiwa ameshikilia bakora ya kutembelea. Yu ndani ya suti nyeusi na kofia yake.
.
.
“ … tupo wawili tu humu, acha kusumbuka.” akamalizia na kisha akatabasamu. Brian akamuuliza, “Ni nini unataka kwangu?”
.
.
“Unajua nitakacho,” Brewster akamjibu kisha taratibu akaanza kusonga kumjongea. “Nilijitahidi sana kukuepusha na kifo, lakini …” akabinua mdomo wake. “ … hukutaka kusikia, Brian. Umekuwa mkaidi sana. Sasa mimi nifanye nini?”
.
.
Brian akamnyooshea mkono na kumwamuru, “Usinisogelee!” Brewster akaangua kicheko kisha akauliza, “Nikikusogelea, utanifanya nini, Brian?” Kabla Brian hajajibu, Brewster akiwa anatembea taratibu, akasema, “Leo ni mwisho wako. Hamna mtu wa kukusaidia, ni mimi na wewe tu … mimi na wewe, Brian.”
.
.
Brian akapiga kelele kuomba msaada. Brewster akacheka sana mpaka kushika mbavu zake. Akakohoa mara kadhaa na kusema, “Brian, acha kupoteza nguvu zako bure. Ni-me-ku-a-mbi-a …” wakati Brewster anaongea akawa anabadilika toka kwenye ubinadamu kwenda kwenye ushetani. “… u-po-na-mi-mi-tu! Ni we-we-na-mi-mi-tu!”
.
.
Uso wake ukageuka na kuwa wa mnyama. Mikono yake ikavimba na kuchomoza makucha vidoleni. Ulimi ukamtoka nje na meno yakapandana kwana kwamba tengo la miba! Miguuni akavalia kwato za ng’ombe.
.
.
Brian akaogopa sana. Akakimbia kuufuata ukuta na alipoenda mbali akajitahidi kuurukia ukuta atorokee kwa nje, lakini ukuta ulikuwa mrefu sana. Hata aliponyoosha mikono yake, hakufua dafu. Akajaribu na tena na tena. Mara mkono wake wa kuume ukafanikiwa kushika kingo ya ukuta. Akijitahidi kuunyoosha mkono wa pili, ule wa kushoto, udake ajivute, akashikwa na kuvutwa chini! Akadondoka na kulalama kwa maumivu.
.
.
Brewster akamdaka shingo na kumminya kwanguvu. Brian akaanza kutapatapa.
.
.
.
***
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
.
.
Muda kidogo, yule polisi aliyekuwa amekaa dirishani akimtazama mwenzake, akamwona mtu fulani akiwa anakuja kumjongea mwenziwe na wale watoto. Alimtazama mtu huyo lakini hakuweza kumtambua. Mtu huyo alikuwa akiambatana na mtoto mwingine kwa pembeni yake.
.
.
Akajaribu kumshtua mwenzake, “Tazama nyuma yako! Hey! Tazama!”
.
.
ENDELEA
.
.
Mwenzake huyo alipotazama, kabla hajajitetea na bunduki yake, akanyakwa koo na kunyanyulia juu haswa kisha akaminywa kwanguvu mpaka koo lake kuanza kuchuruza damu. Bunduki ambayo huenda ingemsaidia kutetea uhai wake, ikadondokea chini.
.
.
“Hapana! Hapana!” mwenzake akatahamaki pale dirishani. Upesi akatoka kwenda kumsaidia mwenzake abaki na pumzi. Alipofungua mlango, akamnyooshea mtu yule bunduki na kumfyatulia tatu. Ajabu hazikusaidia. Zaidi yule mtu wa ajabu akamtupia mwenzake chini na kumfuata yeye kwa kasi!
.
.
Naye akamyaka shingo na kumnyanyua juu, akamminya koo na kumpasua, kisha akalichanja na kumfanya avuje damu kama sharubati toka kwenye kopo. Polisi huyo akapoteza uhai. Dubwana hilo likamtupa na kisha likapotea zake!
.
.
Baadhi ya watu wakafungua milango na madirisha kutazama. Milio ya risasi iliwaamsha na kuwapa mashaka. Wakaona maiti mbili za polisi na wale watoto wakiwa wanatembea. Kwakuwa hali ilikuwa shwari, wakatoka kwenda kutazama.
.
.
Waliwaokoa wale watoto na pia wakatoa taarifa polisi wakidhani polisi wameuawa na majambazi baada ya kurushiana risasi.
.
.
Muda mfupi, polisi wengine wakaja na kuanza kuipemua miili na kukusanya taarifa toka kwa washuhudiaji. Hawakuelewa jambo. Hakuna aliyesema amewaona hao watu waliokuwa wanapambana na polisi, lakini pia vilevile hakuna aliyetoa maelezo ya kueleweka juu ya watoto wale mapacha waliokuwa wanatembea wenyewe usiku huo.
.
.
Wakiwa kwenye mahangaiko ya kutafuta taarifa sahihi, Mama Brian akatoka akiwa amejikunyata, amejifunika blanketi, akawaambia polisi, “Mimi najua nani waliyekuwa wanapambana naye.” kwa maelezo zaidi, polisi mmoja akaongozana na Mama Brian kwenda ndani kumhoji.
.
.
“ … Mtu huyo ndiye ambaye hupoteza watoto kila siku. Polisi hao walipotaka kuwaokoa watoto hao, ndipo akajiri na kuwamaliza,” Mama Brian akaeleza. Polisi akamuuliza, “Unamjua yupoje na wapi anaishi?”
.
.
Mama Brian akanyamaza kwanza kisha akauliza, “Hata nikisema mtasadiki?”
.
.
“Usijali,” Polisi akamtoa hofu. “Unaweza tu kueleza.” basi Mama Brian akamweleza kinagaubaga ya kuwa mtu huyo ni Helo, Hernandez Lorenzo, wa miaka mingi iliyopita. Nyumba yake ipo msituni na anafanya kila anachofanya kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa mji wa Boston.
.
.
Polisi akanakili maelezo yake yote, ila yakamletea shaka kwenye kuamini. Simulizi ile ilikuwa ni ya kufikirika zaidi kuliko uhalisia. Ni kwa namna gani mtu mfu akarejea na kufanya mauaji?
.
.
“Nashukuru sana.” Polisi akampatia mkono na kunyanyuka, “Naweza kwenda sasa. Au kuna cha ziada wataka kuniambia?”
.
.
Mama Brian akamjibu, “Ndio, kipo!”
.
.
“Niambie.” Polisi akasema akimpatia masikio yake kwa utulivu. Mama Brian akasema, “nendeni mkatazame kwenye korongo la kanisa …”
.
.
.
**
.
.
.
Gari la polisi lilisimama, wakashuka wanaume wawili waliovalia sare. Mmoja wao alikuwa ni yule Polisi aliyemhoji Mama Brian. Mkononi alikuwa amebebelea ngowe ya mawasiliano na bunduki ndogo. Mwenzake anayemfuatia alikuwa mikono mitupu ila viganja vyake vikiwa karibu na mkanda wake uliobebelea silaha.
.
.
Ndani ya muda mfupi, wakaonana na Padri Alfonso na Dada Magdalena, wakawafanyia mahojiano mafupi kabla ya kuwataka waongozane kwenda korongoni. Padri Alfonso akapata shaka, akauliza, “Afisa, kuna lolote lile?”
.
.
“Tunataka kupatazama!” Polisi akasema kwa amri basi Padri Alfonso na Dada Magdalena wakaongozana nao kwenda huko kwenye korongo. Walipofika, polisi hao wakangaza na kuangaza, hawakuona kitu.
.
.
“Mnaweza kutuambia mnatafuta nini ili tuwasaidie?” akauliza Padri Alfonso. Polisi akamwambia, “Usijali.” kisha wakajikokota zao kwenda kwenye usafiri wao na kutimka.
.
.
“Hamna kitu!” akasema Polisi dereva na kuongezea, “Nilijua tu mama yule atakuwa na matatizo.” wakayoyoma wakati Padri Alfonso na Dada Magdalena wakiwatazama. Walipoishilia, Padri Alfonso akauliza, “Watakuwa wameambiwa na nani kuhusu korongo lile?”
.
.
Dada Magdalena akajibu, “Si wengine bali wale waliokuja kulitembelea.” Basi Padri Alfonso akashusha pumzi ndefu na kusema, “Nadhani umefikia mwisho wao!” na mara katikati yao akasonga mtumishi mwingine. Naye alikuwa ni Dada kama yule Magdalena, akasimama kandokando yao na kuuliza, “Nami nafanyaje?”
.
.
Padri Alfonso akamtazama na kuweka mkono wake begani. Kumbe alikuwa Dada yule aliyekumbwa na kadhia na yule polisi wa mwanzoni wakiwa korongoni kuwafuata wakina Brian.
.
.
“Dada Marietta, wewe bado u mpya kabisa,” akasema Padri Alfonso. “Utafanya kazi pamoja na Dada Magdalena akuonyeshe namna ya kuenenda. Ila bila shaka usiku wa leo umekuwa mrefu sana, tuuache uende.”
.
.
Dada hao wakainamisha vichwa vyao, Padri akaenda zake.
.
.
**
.
.
Saa nane ya mchana …
.
.
Akiwa juu ya baiskeli yake, Brian alirusha macho yake huku na kule kuangazia kama kuna tangazo jipya la watoto waliopotea. Hakukuwapo, yote yalikuwa ya zamani. Mpaka anafika nyumbani hakuona tangazo lolote tofauti na yale aliyoyaona hapo kabla.
.
.
Akazama ndani na kuteta machache na Wisconsin juu ya mpango wao. Bwana huyo akamwambia kuwa siku hiyo wataenda kumtembelea Brewster majira ya usiku. Brian akauliza, “Haitakuwa hatari kutokana na yale yaliyotokea jana yake?”
.
.
Wisconsin akakuna kidevu chake na kumwambia Brian, “Hatuna muda, ni lazima tufanye hivyo. Kama tusipoyatembelea maeneo haya tukiwa na mwili wa nyama, basi itakuwia vigumu utakapoenda huko kiroho. Lazima ujue ni maeneo yapi utakayokatiza na kuyafanyia kazi.”
.
.
Basi japo kishingo upande, Brian akaridhia. Akala na kupumzika kidogo. Baadae kwenye majira ya jioni akajikwea kwenye baiskeli yake na kwenda kule kwenye makazi ya marehemu Dkt Hamill. Alipoingia, akaegesha baiskeli yake pembeni kidogo ya geti kisha akaanza kusonga kuendea jengo hilo.
.
.
Akiwa bado hajalifikia, akastaajabu kusikia sauti ya geti likifungwa. Akapata shaka. Haraka akakimbilia getini na kujaribu kulifungua. Halikufunguka. Akajaribu kwanguvu zote lakini bure, hakuweza kufungua. Akajiuliza nani kamfungia humo?
.
.
Akapigapiga geti kwanguvu akiita watu wamsaidie lakini hakuna mtu aliyemsikia wala kujali. Mpaka mikono ikawa inamuuma asifanikiwe kitu. Mara akasikia sauti nyuma yake ikimwambia, “Acha kujichosha, Brian.”
.
.
Haraka akatazama nani huyo amwongeleshaye, hamaki akamwona Brewster! Alikuwa amesimama mbele ya mlango wa jengo akiwa ameshikilia bakora ya kutembelea. Yu ndani ya suti nyeusi na kofia yake.
.
.
“ … tupo wawili tu humu, acha kusumbuka.” akamalizia na kisha akatabasamu. Brian akamuuliza, “Ni nini unataka kwangu?”
.
.
“Unajua nitakacho,” Brewster akamjibu kisha taratibu akaanza kusonga kumjongea. “Nilijitahidi sana kukuepusha na kifo, lakini …” akabinua mdomo wake. “ … hukutaka kusikia, Brian. Umekuwa mkaidi sana. Sasa mimi nifanye nini?”
.
.
Brian akamnyooshea mkono na kumwamuru, “Usinisogelee!” Brewster akaangua kicheko kisha akauliza, “Nikikusogelea, utanifanya nini, Brian?” Kabla Brian hajajibu, Brewster akiwa anatembea taratibu, akasema, “Leo ni mwisho wako. Hamna mtu wa kukusaidia, ni mimi na wewe tu … mimi na wewe, Brian.”
.
.
Brian akapiga kelele kuomba msaada. Brewster akacheka sana mpaka kushika mbavu zake. Akakohoa mara kadhaa na kusema, “Brian, acha kupoteza nguvu zako bure. Ni-me-ku-a-mbi-a …” wakati Brewster anaongea akawa anabadilika toka kwenye ubinadamu kwenda kwenye ushetani. “… u-po-na-mi-mi-tu! Ni we-we-na-mi-mi-tu!”
.
.
Uso wake ukageuka na kuwa wa mnyama. Mikono yake ikavimba na kuchomoza makucha vidoleni. Ulimi ukamtoka nje na meno yakapandana kwana kwamba tengo la miba! Miguuni akavalia kwato za ng’ombe.
.
.
Brian akaogopa sana. Akakimbia kuufuata ukuta na alipoenda mbali akajitahidi kuurukia ukuta atorokee kwa nje, lakini ukuta ulikuwa mrefu sana. Hata aliponyoosha mikono yake, hakufua dafu. Akajaribu na tena na tena. Mara mkono wake wa kuume ukafanikiwa kushika kingo ya ukuta. Akijitahidi kuunyoosha mkono wa pili, ule wa kushoto, udake ajivute, akashikwa na kuvutwa chini! Akadondoka na kulalama kwa maumivu.
.
.
Brewster akamdaka shingo na kumminya kwanguvu. Brian akaanza kutapatapa.
.
.
.
***