SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,803
- 25,442
- Thread starter
- #141
*ROHO YAKE INADAI --- 25*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
.
.
Hajakaa vema, Brian akamkita teke zito. Mama alishafungua mlango. Dada Magdalena akajikuta chini, gari likatimka kwa kasi!
.
.
Wakati Dada Magdalena anajikusanya chini, mara miguu ya mwanaume ikamjongea na kukoma mbele yake. Alikuwa ni Padri Alfonso. Alitazama mbele gari la wakina Brian likitokomea.
.
.
ENDELEA
.
.
Basi baada ya safari hii kudumu kwa muda fulani, Mama Brian akaweka gari kando mahali wapate kula na hata kutia mafuta garini. Walichukua kama dakika kumi na tano hapo. Wakajipakia tena kwenye gari na kuendelea na safari yao.
.
.
Wakadumu tena barabarani kwa muda wa kama lisaa, ndipo wakafika eneo walilokuwa wanaliendea, mji wa Northampton. Hapo wakatembea kwa dakika chache tu kabla hawajafika mbele ya nyumba fulani iliyo pweke. Mama Brian akazima gari na kusema. “Tumefika!”
.
.
“Ndiyo hapa?” Brian akauliza akiwa anaangaza macho yake. Punde wakamwona mwanaume aliyevalia suti nyeusi na kofia yake. Mdomoni alikuwa ameshikilia kiko chake kwa meno akijaribu kufunga mlango wake. Kuna mahali alikuwa anataka kwenda, hata mkononi mwake alikuwa amebebelea mkebe.
.
.
Mama Brian akashuka upesi na kuita, “Wisconsin!” mwanaume
yule akaacha shughuli yake na kumtazama. Ilikuwa ajabu kuwa hakumwona ilhali gari hilo lilikuwa limejiegesha karibu na makazi yake. Ila baada ya Mama Brian kujongea ndipo tukajifunza kuwa jicho lake moja la upande wa kushoto lilikuwa bovu. Yeye hutumia jicho moja tu, ambalo ameliveka miwani ya kioo kimoja.
.
.
“Hello mama!” Wisconsin akasalimu akivua kofia yake, kisha akaendelea na zoezi lake la kufunga mlango. “Samahani!” Mama Brian akasema akijitahidi kusonga karibu. Akadaka ngazi kupanda kwa upesi.
.
.
“Sisi ni wageni wako. Naomba utuskize!”
.
.
Wisconsin alipomaliza kufunga mlango wake. Akatazama jua na kisha akamtazama Mama Brian. “Samahani. Sina ratiba ya kufanya lolote leo hii, muda huu!”
.
.
“Hunikumbuki?” Mama Brian akauliza akiwa ametoa macho. Wisconsin, mwanaume mtanashati mwenye makamo ya umri wa miaka arubaini, akamtazama na kisha akabinua mdomo. “Hapana.”
.
.
“Oooh! Ndio. Tulipokuja mara ya kwanza hatukukuta … samahani, nina shida sana.”
.
.
Wisconsin akatabasamu. Akaweka mkebe wake kwenye kwapa alafu akasema kistaarabu. “Mama, mimi hufanya kazi kwa ratiba. Nina ratiba nyingine hivi sasa. Samahani sitaweza kukuhudumia.”
.
.
“Tumetoka mbali sana kuja kukuona.”
.
.
“Italia?”
.
.
“Boston!”
.
.
“Si mbali. Kama hutojali, naweza kwenda?”
.
.
“Tafadhali. Na --”
.
.
“Nazidi kukawia. Naomba niende.”
.
.
“Niambie basi muda wako. Lini unafanya kazi?”
.
.
“Keshokutwa kuanzia jua linapokuwa katikati mpaka kuzama.” Wisconsin aliposema hayo, akaenda zake. Mama Brian akabaki amesimama, anamtazama mwanaume huyo akiishilia.
.
.
“Amesemaje?” Brian akamuuliza. Yeye na Olivia walitoka ndani ya gari baada ya kumwona Wisconsin akiishilia. Mama alidaka kiuno chake akatikisa kichwa.
.
.
“Itabidi tulale huku hivi leo.”
.
.
Wakarejea kwenye gari na kutafuta ‘motel’ safi walipopata vyumba vizuri vya kulalia lakini pia huduma zinginezo zikiwa si haba. Huduma kama vile chakula na vinywaji. Moteli hii ilikuwa wazi masaa ishirini na nne kutokana na kwamba watu husafiri muda wote.
.
.
Basi baada ya kuona vyumba vyao, wakaendea mgahawa na kutulia hapo watete mawili matatu. Mezani kulikuwa na vinywaji laini, hususani sharubati.
.
.
Lakini wakiwa hapo wanateta juu ya mji ule wa Northampton, macho yao yakadakwa na taarifa runingani. Ilikuwa ni taarifa ya habari kutokea Boston.
.
.
“ … watoto nane wanaripotiwa kupotea leo katika mji wa Boston ukiwa mwendelezo wa matukio ya watoto kupotea kwa wingi kwa siku za karibuni. Sasa ndani ya siku tatu, takribani watoto kumi na tano wamekwishapotea huku karibia wote wakiripotiwa kuyoyomea ama kuonekana mara ya mwisho msituni!
.
.
Kamanda wa polisi wa mji wa Boston anathibitisha taarifa hiyo na kueleza kuwa wanaendelea kulifanyia kazi kiupelelezi zaidi. Hofu inazidi kuwatanda wazazi na vilio vinatawala majumbani.
.
.
John Bleach, KK tv!”
.
.
Mama Brian akatikisa kichwa, akasema kwa kuchoka, “wameendelea kupotea na leo.”
.
.
“Inabidi tufanye jambo haraka,” Brian akanguruma. Uso wake ulionyesha kuguswa na habari. Kwa muda kila mtu hakugusa bilauri yake ya sharubati. “La sivyo, watoto wote watatokomea. Mji mzima!”
.
.
Mama Brian akarusha macho yake nje ya vioo vya dirisha. Alikuwa anatafakuri. Japo macho yake yalikuwa yanatazama magari yakatizayo, akili yake ilikuwa inahaha ikimnyima amani.
.
.
Akasema, “Tunamhitaji sana Wisconsin.” sauti yake ilikuwa nzito kwasababu ya kubana koo lake kwa viganja vyake vyembamba ili ajipatie joto. Mhudumu akamtazama.
.
.
Alikuwa ni mwanamke mnene ndani ya sare. Mashavu yake makubwa yalikuwa mekundu yenye vidotidoti vingi rangi ya zambarau. Kidevu chake kilikuwa kimemezwa na shingo. Mdomo mdogo kana kwamba ndege.
.
.
“Umekuja kwa ajili ya Wisconsin?” mhudumu huyo akauliza. Mama Brian na wanawe wakamtazama.
.
.
“Mmekuja kwa ajili ya Wisconsin?” Mhudumu akarejea kuuliza. Mkononi alikuwa amebebelea kikombe cha udongo akikifuta kukikausha na maji.
.
.
“Ndio. Tumekuja kwa ajili yake,” Mama Brian akasema kwa kujiamini. Mhudumu yule akawatazama alafu akaendelea na kazi zake. Aliondoka pale ‘kaunta’ akaelekea ndani, jikoni. Akawaachia wageni maswali.
.
.
“Atakuwa na nini?” mama akauliza kiretorikali.
.
.
“Pengine anachakutuambia,” Brian akabashiri akiwa anatazama kule kaunta kama atamwona yule mhudumu. Kwa muda hakutokea. Alipotokea alikuwa ameshabadili sare zake, sasa amevalia nguo kama raia wa kawaida. Gauni jeusi pana.
.
.
“Tunaweza kuongea na wewe?” Mama Brian akamwomba. Mhudumu huyo akasimama akiwa anawatazama kwa mashaka. Akatikisa kichwa chake, mashavu yakacheza, kisha akaendelea zake na safari kuufuata mlango wa kutokea.
.
.
Mama Brian akanyanyuka kumfuata. Wakina Brian wakabaki wakimtazama mama yao akizungumza na yule mhudumu. Punde akarejea naye mezani.
.
.
“Hawa ni wanangu, huyu anaitwa Brian na huyu Olivia,” Mama akatambulisha kwa tabasamu. Mhudumu akaketi na kusema, “Mimi naitwa Keline.” alikuwa anaonyesha woga usoni mwake.
.
.
“Keline, kuna kitu chochote unataka kutuambia?” Mama akauliza akimtazama Keline kwa uso wa kudadisi. “… kumhusu Wisconsin. Chochote kile unachoweza kutuambia?”
.
.
Keline akatazama kwanza nje. Akarudisha macho yake madogo mezani na kisha akatazama chini. “Si mtu mwema,” akasema kwa sauti yake ndogo.
.
.
“Kwanini unasema hivyo?” Brian akauliza. “Kuna tabu yoyote?”
.
.
“Ndio … Wisconsin aliua wazazi wangu. Amenisababishia jeraha kubwa. Sitaweza kumsamehe kamwe!” macho yake yakaanza kujawa na machozi. Akavuta makamasi mepesi na kuendelea kunena, “Anasema kuwa anawasaidia watu dhidi ya nguvu za giza. Lakini yeye mwenyewe ni nguvu hizo, tena zaidi kwa maana amejiveka koti la kondoo.
.
.
Analaghai watu, na kila anayedai kumsaidia, hufa baada ya majuma matatu!”
.
.
Keline aliposema hayo akanyanyua uso wake na kumtazama Mama Brian. “Baba yangu alikufa majuma matatu baada ya kuonana naye. Naye mama ‘angu alipokwenda kumwomba msaada, naye akafa baada ya majuma matatu. Nisingependa mkapitia kwenye adha hiyo.”
.
.
Sasa Keline alikuwa anatiririsha machozi zaidi. Alitoa leso yake na kujipangusa. Akasimama na kuaga. Mama Brian na wanawe wakabaki wakimtazama mwanamke huyo akiishilia, anajifuta machozi na amebanwa na kwikwi za kilio.
.
.
Alipopotelea, Mama Brian akauliza, “Sasa tunafanyaje?” alionyesha kuchanganyikiwa.
.
.
“Tunaenda kumwona Wisconsin kesho kama tulivyokubaliana naye,” akasema Brian.
.
.
“Lakini umesikia habari zake?” Mama akauliza. Brian akatazama kwanza nyuma yake na kule mlangoni kisha akamwambia mama yake kuwa ana mashaka na Keline.
.
.
“Kwanini?” mama akauliza.
.
.
Brian akamtonya kuwa wakati Keline anaongea alifanikiwa kumtazama mkono wake wa kulia, akamwona akiwa na pete ambayo alimwona nayo Padri Alfonso wakati alipokuja kufanya sala nyumbani kwao. Hilo likamshangaza mama yake.
.
.
“Una uhakika?”
.
.
“Ndio, nina uhakika. Nimeona kwa macho yangu mwenyewe!”
.
.
Swala hilo likazua hofu miongoni mwao. Na pengine kwa kiasi fulani halikumkonga sana Mama kwenye kuliamini. Pete zi nyingi. Vipi kama ya Kelie haikuwa na mahusiano na Padri Alfonso? Aliwaza akiwa kitandani kwenye chumba cha peke yake.
.
.Ila kule dirishani, kivuli cha mtu kikakatiza. Mtu mwenye mwili mpana.
.
.
.
**
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
.
.
Hajakaa vema, Brian akamkita teke zito. Mama alishafungua mlango. Dada Magdalena akajikuta chini, gari likatimka kwa kasi!
.
.
Wakati Dada Magdalena anajikusanya chini, mara miguu ya mwanaume ikamjongea na kukoma mbele yake. Alikuwa ni Padri Alfonso. Alitazama mbele gari la wakina Brian likitokomea.
.
.
ENDELEA
.
.
Basi baada ya safari hii kudumu kwa muda fulani, Mama Brian akaweka gari kando mahali wapate kula na hata kutia mafuta garini. Walichukua kama dakika kumi na tano hapo. Wakajipakia tena kwenye gari na kuendelea na safari yao.
.
.
Wakadumu tena barabarani kwa muda wa kama lisaa, ndipo wakafika eneo walilokuwa wanaliendea, mji wa Northampton. Hapo wakatembea kwa dakika chache tu kabla hawajafika mbele ya nyumba fulani iliyo pweke. Mama Brian akazima gari na kusema. “Tumefika!”
.
.
“Ndiyo hapa?” Brian akauliza akiwa anaangaza macho yake. Punde wakamwona mwanaume aliyevalia suti nyeusi na kofia yake. Mdomoni alikuwa ameshikilia kiko chake kwa meno akijaribu kufunga mlango wake. Kuna mahali alikuwa anataka kwenda, hata mkononi mwake alikuwa amebebelea mkebe.
.
.
Mama Brian akashuka upesi na kuita, “Wisconsin!” mwanaume
yule akaacha shughuli yake na kumtazama. Ilikuwa ajabu kuwa hakumwona ilhali gari hilo lilikuwa limejiegesha karibu na makazi yake. Ila baada ya Mama Brian kujongea ndipo tukajifunza kuwa jicho lake moja la upande wa kushoto lilikuwa bovu. Yeye hutumia jicho moja tu, ambalo ameliveka miwani ya kioo kimoja.
.
.
“Hello mama!” Wisconsin akasalimu akivua kofia yake, kisha akaendelea na zoezi lake la kufunga mlango. “Samahani!” Mama Brian akasema akijitahidi kusonga karibu. Akadaka ngazi kupanda kwa upesi.
.
.
“Sisi ni wageni wako. Naomba utuskize!”
.
.
Wisconsin alipomaliza kufunga mlango wake. Akatazama jua na kisha akamtazama Mama Brian. “Samahani. Sina ratiba ya kufanya lolote leo hii, muda huu!”
.
.
“Hunikumbuki?” Mama Brian akauliza akiwa ametoa macho. Wisconsin, mwanaume mtanashati mwenye makamo ya umri wa miaka arubaini, akamtazama na kisha akabinua mdomo. “Hapana.”
.
.
“Oooh! Ndio. Tulipokuja mara ya kwanza hatukukuta … samahani, nina shida sana.”
.
.
Wisconsin akatabasamu. Akaweka mkebe wake kwenye kwapa alafu akasema kistaarabu. “Mama, mimi hufanya kazi kwa ratiba. Nina ratiba nyingine hivi sasa. Samahani sitaweza kukuhudumia.”
.
.
“Tumetoka mbali sana kuja kukuona.”
.
.
“Italia?”
.
.
“Boston!”
.
.
“Si mbali. Kama hutojali, naweza kwenda?”
.
.
“Tafadhali. Na --”
.
.
“Nazidi kukawia. Naomba niende.”
.
.
“Niambie basi muda wako. Lini unafanya kazi?”
.
.
“Keshokutwa kuanzia jua linapokuwa katikati mpaka kuzama.” Wisconsin aliposema hayo, akaenda zake. Mama Brian akabaki amesimama, anamtazama mwanaume huyo akiishilia.
.
.
“Amesemaje?” Brian akamuuliza. Yeye na Olivia walitoka ndani ya gari baada ya kumwona Wisconsin akiishilia. Mama alidaka kiuno chake akatikisa kichwa.
.
.
“Itabidi tulale huku hivi leo.”
.
.
Wakarejea kwenye gari na kutafuta ‘motel’ safi walipopata vyumba vizuri vya kulalia lakini pia huduma zinginezo zikiwa si haba. Huduma kama vile chakula na vinywaji. Moteli hii ilikuwa wazi masaa ishirini na nne kutokana na kwamba watu husafiri muda wote.
.
.
Basi baada ya kuona vyumba vyao, wakaendea mgahawa na kutulia hapo watete mawili matatu. Mezani kulikuwa na vinywaji laini, hususani sharubati.
.
.
Lakini wakiwa hapo wanateta juu ya mji ule wa Northampton, macho yao yakadakwa na taarifa runingani. Ilikuwa ni taarifa ya habari kutokea Boston.
.
.
“ … watoto nane wanaripotiwa kupotea leo katika mji wa Boston ukiwa mwendelezo wa matukio ya watoto kupotea kwa wingi kwa siku za karibuni. Sasa ndani ya siku tatu, takribani watoto kumi na tano wamekwishapotea huku karibia wote wakiripotiwa kuyoyomea ama kuonekana mara ya mwisho msituni!
.
.
Kamanda wa polisi wa mji wa Boston anathibitisha taarifa hiyo na kueleza kuwa wanaendelea kulifanyia kazi kiupelelezi zaidi. Hofu inazidi kuwatanda wazazi na vilio vinatawala majumbani.
.
.
John Bleach, KK tv!”
.
.
Mama Brian akatikisa kichwa, akasema kwa kuchoka, “wameendelea kupotea na leo.”
.
.
“Inabidi tufanye jambo haraka,” Brian akanguruma. Uso wake ulionyesha kuguswa na habari. Kwa muda kila mtu hakugusa bilauri yake ya sharubati. “La sivyo, watoto wote watatokomea. Mji mzima!”
.
.
Mama Brian akarusha macho yake nje ya vioo vya dirisha. Alikuwa anatafakuri. Japo macho yake yalikuwa yanatazama magari yakatizayo, akili yake ilikuwa inahaha ikimnyima amani.
.
.
Akasema, “Tunamhitaji sana Wisconsin.” sauti yake ilikuwa nzito kwasababu ya kubana koo lake kwa viganja vyake vyembamba ili ajipatie joto. Mhudumu akamtazama.
.
.
Alikuwa ni mwanamke mnene ndani ya sare. Mashavu yake makubwa yalikuwa mekundu yenye vidotidoti vingi rangi ya zambarau. Kidevu chake kilikuwa kimemezwa na shingo. Mdomo mdogo kana kwamba ndege.
.
.
“Umekuja kwa ajili ya Wisconsin?” mhudumu huyo akauliza. Mama Brian na wanawe wakamtazama.
.
.
“Mmekuja kwa ajili ya Wisconsin?” Mhudumu akarejea kuuliza. Mkononi alikuwa amebebelea kikombe cha udongo akikifuta kukikausha na maji.
.
.
“Ndio. Tumekuja kwa ajili yake,” Mama Brian akasema kwa kujiamini. Mhudumu yule akawatazama alafu akaendelea na kazi zake. Aliondoka pale ‘kaunta’ akaelekea ndani, jikoni. Akawaachia wageni maswali.
.
.
“Atakuwa na nini?” mama akauliza kiretorikali.
.
.
“Pengine anachakutuambia,” Brian akabashiri akiwa anatazama kule kaunta kama atamwona yule mhudumu. Kwa muda hakutokea. Alipotokea alikuwa ameshabadili sare zake, sasa amevalia nguo kama raia wa kawaida. Gauni jeusi pana.
.
.
“Tunaweza kuongea na wewe?” Mama Brian akamwomba. Mhudumu huyo akasimama akiwa anawatazama kwa mashaka. Akatikisa kichwa chake, mashavu yakacheza, kisha akaendelea zake na safari kuufuata mlango wa kutokea.
.
.
Mama Brian akanyanyuka kumfuata. Wakina Brian wakabaki wakimtazama mama yao akizungumza na yule mhudumu. Punde akarejea naye mezani.
.
.
“Hawa ni wanangu, huyu anaitwa Brian na huyu Olivia,” Mama akatambulisha kwa tabasamu. Mhudumu akaketi na kusema, “Mimi naitwa Keline.” alikuwa anaonyesha woga usoni mwake.
.
.
“Keline, kuna kitu chochote unataka kutuambia?” Mama akauliza akimtazama Keline kwa uso wa kudadisi. “… kumhusu Wisconsin. Chochote kile unachoweza kutuambia?”
.
.
Keline akatazama kwanza nje. Akarudisha macho yake madogo mezani na kisha akatazama chini. “Si mtu mwema,” akasema kwa sauti yake ndogo.
.
.
“Kwanini unasema hivyo?” Brian akauliza. “Kuna tabu yoyote?”
.
.
“Ndio … Wisconsin aliua wazazi wangu. Amenisababishia jeraha kubwa. Sitaweza kumsamehe kamwe!” macho yake yakaanza kujawa na machozi. Akavuta makamasi mepesi na kuendelea kunena, “Anasema kuwa anawasaidia watu dhidi ya nguvu za giza. Lakini yeye mwenyewe ni nguvu hizo, tena zaidi kwa maana amejiveka koti la kondoo.
.
.
Analaghai watu, na kila anayedai kumsaidia, hufa baada ya majuma matatu!”
.
.
Keline aliposema hayo akanyanyua uso wake na kumtazama Mama Brian. “Baba yangu alikufa majuma matatu baada ya kuonana naye. Naye mama ‘angu alipokwenda kumwomba msaada, naye akafa baada ya majuma matatu. Nisingependa mkapitia kwenye adha hiyo.”
.
.
Sasa Keline alikuwa anatiririsha machozi zaidi. Alitoa leso yake na kujipangusa. Akasimama na kuaga. Mama Brian na wanawe wakabaki wakimtazama mwanamke huyo akiishilia, anajifuta machozi na amebanwa na kwikwi za kilio.
.
.
Alipopotelea, Mama Brian akauliza, “Sasa tunafanyaje?” alionyesha kuchanganyikiwa.
.
.
“Tunaenda kumwona Wisconsin kesho kama tulivyokubaliana naye,” akasema Brian.
.
.
“Lakini umesikia habari zake?” Mama akauliza. Brian akatazama kwanza nyuma yake na kule mlangoni kisha akamwambia mama yake kuwa ana mashaka na Keline.
.
.
“Kwanini?” mama akauliza.
.
.
Brian akamtonya kuwa wakati Keline anaongea alifanikiwa kumtazama mkono wake wa kulia, akamwona akiwa na pete ambayo alimwona nayo Padri Alfonso wakati alipokuja kufanya sala nyumbani kwao. Hilo likamshangaza mama yake.
.
.
“Una uhakika?”
.
.
“Ndio, nina uhakika. Nimeona kwa macho yangu mwenyewe!”
.
.
Swala hilo likazua hofu miongoni mwao. Na pengine kwa kiasi fulani halikumkonga sana Mama kwenye kuliamini. Pete zi nyingi. Vipi kama ya Kelie haikuwa na mahusiano na Padri Alfonso? Aliwaza akiwa kitandani kwenye chumba cha peke yake.
.
.Ila kule dirishani, kivuli cha mtu kikakatiza. Mtu mwenye mwili mpana.
.
.
.
**