Simulizi: Penzi lisilo Na Mwisho

Sehemu ya 09

“Mohammed, sahau kuhusu taa za gari...mbona nishawasamehe tu,” alisema Razak huku akionekana kutokujali sana.
“Unahitaji nini?” aliuliza Aisha.
“Nakuhitaji wewe...”

“Kwa hiyo unampenda?” alidakia Mohammed kwa kuuliza swali lililomfanya Razak kuachia zaidi tabasamu.
“Twendeni sehemu kwanza...” alisema Razak.

“Wapi?” aliuliza Aisha.
“Sehemu fulani!”
“Hatuwezi kwenda mpaka utuambie wapi!”

“Aisha...mimi si mtu mbaya kwenu, niamini, naomba mnichukulie kama mtu wa kawaida,” alisema Razak kwa sauti ya kubembeleza iliyoonyesha kumaanisha alichokuwa akikisema.

“Unataka nini kwetu?”
“Niwe karibu nanyi...nimeguswa na maisha mnayoishi...”

“Kwa hiyo?”
“Nataka kuwasaidia...”
Wote watatu wakaangaliana, hawakuamini maneno aliyokuwa akizungumza Razak, kwao walimuona muongo ambaye alikuwa na jambo lake pembeni ambalo hakutaka kuliweka wazi.

Hawakukubaliana na suala hilo, walikuwa mitaani kwa miaka mingi, leo hii mtu aje na kuwaambia kwamba alitaka kuwasaidia, kukubaliana naye lilikuwa jambo gumu.

“Hapana...” alisema Aisha.
Razak alikuwa kwenye wakati mgumu, hakuweza kuaminika, ilimbidi atumie nguvu za ziada kuwaambia watu hao kwamba aliposema kuwa anataka kuwasaidia, alikuwa akimaanisha kufanya hivyo.

Je nini kitaendelea...
 
Sehemu ya 10

“Unataka nini kwetu?”
“Niwe karibu nanyi...nimeguswa na maisha mnayoishi...”
“Kwa hiyo?”
“Nataka kuwasaidia...”

Wote watatu wakaangaliana, hawakuamini maneno aliyokuwa akizungumza Razak, kwao walimuona muongo ambaye alikuwa na jambo lake pembeni ambalo hakutaka kuliweka wazi.

Hawakukubaliana na suala hilo, walikuwa mitaani kwa miaka mingi, leo hii mtu aje na kuwaambia kwamba alitaka kuwasaidia, kukubaliana naye lilikuwa jambo gumu.

“Hapana...” alisema Aisha.
Razak alikuwa kwenye wakati mgumu, hakuweza kuaminika, ilimbidi atumie nguvu za ziada kuwaambia watu hao kwamba aliposema kuwa anataka kuwasaidia, alikuwa akimaanisha kufanya hivyo.

Haikuwa kazi nyepesi, alitumia dakika arobaini na tano, tena kwa kuapa na kuapa mpaka kukubaliana naye, hivyo akawasha gari na kuondoka mahali hapo, safari iliofuata ilikuwa ni kwenda Kijitonyama.

Moyo wake ulikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli angefanikiwa kumuona msichana huyo ambaye mpaka katika kipindi hicho moyo wake ulikufa na kuoza, mbaya zaidi ulikuwa ukiogelea katika dimbwi zito la mahaba.

Kila wakati kazi yake ilikuwa ni kumwangalia Aisha kupitia kioo kilichokuwa mbele yake, uso wa msichana huyo ulikuwa mzuri, alivutia ila tatizo ni mavazi aliyokuwa ameyavaa tu.

Ukimya ulitawala kwa kipindi chote cha safari, baada ya dakika ishirini, wakafika Kijitonyama ambapo gari likasimama nje ya jumba moja kubwa na la kifahari ambalo kwa kuliangalia tu lingekufanya kugundua kwamba mtu aliyekuwa akiishi humo alikuwa na fedha nyingi.

Hakukuwa na mtu yeyote yule, akateremka na kufungua geti, akarudi garini, akaingia na kisha kuliingiza gari ndani.

Aisha, Ahmed na Mohammed walibaki wakishangaa, waliliangalia jumba lile mara mbilimbili, hawakuamini kama kweli siku hiyo wangeweza kuingia katika jumba la kifahari kama lilivyokuwa jumba hilo.

Je nini kitaendelea...
 
Sehemu ya 11

Kila alipomwangalia mwanaume yule, alimkumbuka, alikuwa yuleyule wa usiku uliopita ambaye alikuwa akiwakimbiza mapacha wale, Ahmed na Mohammed. Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwaangalia mapacha wale, je, walikuwa wamejeruhiwa? Alipowaangalia, walikuwa salama kabisa tena wote nyuso zao zilitawaliwa na tabasamu pana.

Hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, moyo wake uliogopa mno, hakumwamini mwanaume huyo ambaye alikaa nyuma ya usukani huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana, kichwa chake kikawa na maswali mengi, tena yote hayo yalikosa majibu.

“Wewe ni nani?” aliuliza Aisha.
“Naitwa Razak....unanikumbuka?” aliuliza Razak.

“Ndiyo! Si yule wa usiku uliyekuwa ukiwakimbiza hawa baada ya kukuibia taa za gari?” aliuliza Aisha swali lililowashtua mapacha wale, wakatamani kuteremka, wakahisi kwamba mtu huyo alikuja kuwakamata.

“Naomba nikaendelee na shughuli zangu jamani...” alisema Mohammed huku akitaka kuteremka.

“Mohammed, sahau kuhusu taa za gari...mbona nishawasamehe tu,” alisema Razak huku akionekana kutokujali sana.
“Unahitaji nini?” aliuliza Aisha.
“Nakuhitaji wewe...”

“Kwa hiyo unampenda?” alidakia Mohammed kwa kuuliza swali lililomfanya Razak kuachia zaidi tabasamu.
“Twendeni sehemu kwanza...” alisema Razak.

“Wapi?” aliuliza Aisha.
“Sehemu fulani!”
“Hatuwezi kwenda mpaka utuambie wapi!”

“Aisha...mimi si mtu mbaya kwenu, niamini, naomba mnichukulie kama mtu wa kawaida,” alisema Razak kwa sauti ya kubembeleza iliyoonyesha kumaanisha alichokuwa akikisema.

“Unataka nini kwetu?”
“Niwe karibu nanyi...nimeguswa na maisha mnayoishi...”
“Kwa hiyo?”

“Nataka kuwasaidia...”
Wote watatu wakaangaliana, hawakuamini maneno aliyokuwa akizungumza Razak, kwao walimuona muongo ambaye alikuwa na jambo lake pembeni ambalo hakutaka kuliweka wazi.

Hawakukubaliana na suala hilo, walikuwa mitaani kwa miaka mingi, leo hii mtu aje na kuwaambia kwamba alitaka kuwasaidia, kukubaliana naye lilikuwa jambo gumu.

“Hapana...” alisema Aisha.

Je nini kitaendelea.....
 
Sehemu ya 13

Razak alikuwa kwenye wakati mgumu, hakuweza kuaminika, ilimbidi atumie nguvu za ziada kuwaambia watu hao kwamba aliposema kuwa anataka kuwasaidia, alikuwa akimaanisha kufanya hivyo.

Haikuwa kazi nyepesi, alitumia dakika arobaini na tano, tena kwa kuapa na kuapa mpaka kukubaliana naye, hivyo akawasha gari na kuondoka mahali hapo, safari iliofuata ilikuwa ni kwenda Kijitonyama.

Moyo wake ulikuwa na furaha tele, hakuamini kama kweli angefanikiwa kumuona msichana huyo ambaye mpaka katika kipindi hicho moyo wake ulikufa na kuoza, mbaya zaidi ulikuwa ukiogelea katika dimbwi zito la mahaba.

Kila wakati kazi yake ilikuwa ni kumwangalia Aisha kupitia kioo kilichokuwa mbele yake, uso wa msichana huyo ulikuwa mzuri, alivutia ila tatizo ni mavazi aliyokuwa ameyavaa tu.

Ukimya ulitawala kwa kipindi chote cha safari, baada ya dakika ishirini, wakafika Kijitonyama ambapo gari likasimama nje ya jumba moja kubwa na la kifahari ambalo kwa kuliangalia tu lingekufanya kugundua kwamba mtu aliyekuwa akiishi humo alikuwa na fedha nyingi.

Hakukuwa na mtu yeyote yule, akateremka na kufungua geti, akarudi garini, akaingia na kisha kuliingiza gari ndani.

Aisha, Ahmed na Mohammed walibaki wakishangaa, waliliangalia jumba lile mara mbilimbili, hawakuamini kama kweli siku hiyo wangeweza kuingia katika jumba la kifahari kama lilivyokuwa jumba hilo.

Mohammed akashindwa kuvumilia, akaanza kuzunguka huku na kule, alionekana kuwa mtu mwenye furaha mno, alitamani hata Razak amwambie kwamba jumba hilo lilikuwa lao na wangetakiwa kuishi humo maisha yao yote.

“Hapa ndipo unapoishi?” aliuliza Aisha.
“Hapana! Hii ni nyumba ya mzee ambayo huwa haitumii...”
“Kwa nini?”

“Hapendi kuishi Kijitonyama, anasema kwamba ni uswahilini, huwa kuna kelele sana,” alisema Razak huku akitabasamu tu.

“Na wewe unapenda kuishi sehemu kama hizi za uswahilini?”
“Sana. Nilimwambia baba mara nyingi kwamba sipendi kuishi Osterbay lakini amekuwa hanielewi kabisa, sasa nahisi naweza kuanza maisha yangu humu,” alisema Razak.

“Kuanza maisha yako na nani?”
“Bila shaka mnasikia njaa, twendeni tukale,” alisema Razak huku akiwa amelipotezea swali aliloulizwa.

Je nini kitaendelea....
 
Sehemu ya 14

“Sabrina! Hebu niambie ukweli kabisa kabla sijarudi Dubai...” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja garini.
“Ukweli gani tena Sharifu?” alisikika Sabrina.

“Kuhusu huu uhusiano! Ni wa uhakika au kuzugia?” aliuliza Sharifu.

“Jamani! Kwani mimi nimekwambiaje?”
“Umeniambia lakini sikuelewi kabisa kuhusu huyo mtu wako! Kwanza umempendea nini hasa?”

“Nani kasema anampenda?”
“Kama ungekuwa humpendi, ungekuwa naye?”
“Hebu acha kumzungumzia huyo kinyago, tufanye yetu kwanza....”

Yalikuwa ni mazungumzo baina ya watu wawili, Sabrina na mwanaume wa Kiarabu aliyejulikana kwa jina la Sharif. Walikuwa ndani ya gari huku saa zao zikionyesha kwamba ilikuwa ni saa tatu usiku.

Mikao yao ndani ya gari hilo la kifahari ilionyesha ni kwa jinsi gani wawili hao walikuwa wamekufa na kuoza kwenye penzi zito. Muda mwingi Sabrina alikuwa akikichezea kidevu cha Sharifu kilichokuwa na ndevu za wastani.

Walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi uliokuwa mbichi kabisa. Mwanaume huyohuyo ndiye aliyemfanya msichana huyo kumuacha Razak, hakutaka kuwa naye tena kwa sababu moyo wake ulimpata mwanaume mwingine.

Uwepo wa Sharifu ndiyo uliolifanya penzi lao kuyumba, kumdharau mwanaume huyo na kila wakati kugombana. Mapenzi ya Razak aliyachoka na sasa alihitaji mapenzi mapya na ndiyo maana aliamua kuwa na Sharifu.

Sharifu alikuwa mtoto wa tajiri mkubwa nchini Dubai, chimbuko la mama yake lilikuwa nchini Tanzania, kila wakati alikuwa akifika nchini Tanzania kumtembelea mama yake, anakaa kidogo kisha kurudi Dubai ambapo huko baba yake, mzee Ashrafu alioa mwanamke mwingine.

Katika kipindi alichofika nchini Tanzania kwa mara ya tano ndipo akabahatika kukutana na msichana mrembo, aliyevutiwa naye sana ambapo akaapa kwamba kamwe hatoweza kumkosa, hata kama ingekuwa kutumia fedha, alikuwa tayari lakini mwisho wa siku awe na msichana huyo, Sabrina.

Rafiki mkubwa wa Sabrina, Minah ndiye aliyetumika kumvuta Sabrina, alimwambia mengi kuhusu mwanaume huyo, alimpamba na kumpamba mpaka msichana huyo akaingia mkenge na kutaka kuonana na Sharifu.

Siku ya kwanza alipomuona mwanaume huyo, Sharifu, Sabrina akavutiwa naye na hata pale alipotongozwa, hakukataa, alikubaliana naye na hivyo kuwa wapenzi.

Ukaribu wao ukamfanya msichana huyo kuanza kumtoa Razak moyoni mwake, akaanza dharau, hakutaka kujali wala kusikiliza, kisa kikubwa kikawa ni Sharifu.

Muda mwingi akautumia kuwa na mwanaume huyo, hakuangalia mbele, kwake, kile alichokiona ni kwamba wasingeishia kuwa wapenzi bali kuna siku wangeoana na kuishi kama mume na mke.

Mapenzi ya Sharifu yalimuendesha, hakujua ni kwa jinsi gani Razak aliumia, hakujua ni kwa jinsi gani mwanaume huyo alimtaka sana, alichojidanganya ni kuusikiliza moyo wake, unataka nini, kuwa na nani na kisha kuufuata.

Je nini kitaendelea....
 
Sehemu ya 15

“Ninakupenda Sabrina....tatizo nini?” aliyakumbuka sana maneno hayo, swali aliloulizwa ambalo mpaka kipindi hicho hakuwa na jibu lolote zaidi ya kusema kwamba hataki kuwa na Razak.

Akajitahidi kumsahau mwanaume huyo na kumuingiza Sharifu katika utawala mpya, haikuwa kazi nyepesi lakini mwisho wa siku msichana huyo alifanikiwa, alimtoa Razak na kumuingiza Sharifu ambaye hakujua historia ya maisha yake, alichokihitaji ni kuwa naye tu.

“Nitakupenda mpaka kifo changu...” alisema Sabrina huku akichezeachezea ndefu za Sharifu ndani ya gari.

“Hata mimi pia...” alisema Sharifu na kisha kumwagiana mabusu mfululizo yaliyowafanya kuingia nani ya mahaba mazito, japokuwa gari lilikuwa limepakiwa barabarani, hapohapo likaanza kunesanesa.

****
Siku hiyo walikaa mpaka usiku, kama kula, walipika na kula, na kama kubadilisha nguo, kuna kipindi walichukuliwa na kupelekwa katika duka la nguo ambapo huko wakanunua nguo na kurudi nyumbani.

Kwa Razak, kumuacha Aisha lilikuwa jambo gumu, alimpenda mno msichana huyo na hakuona kama alitakiwa kumuacha zaidi ya kuendelea kuishi naye mpaka pale ambapo wangeoana na kuishi pamoja.

Kipindi chote hicho, Aisha hakuelewa kilichokuwa kikiendelea, kwake, mwanaume yule alionekana kuwa baraka kubwa, kila kitu walichofanyiwa kwake kilionekana kuwa upendo wa kawaida tu.
“Aisha...” Razak aliamua kumuita Aisha.
“Abeee...”
“Umependeza sana...”

“Asante sana Razak...” alijibu Aisha huku akijiangalia namna alivyopendeza.

Siku hiyo, aliamini kwamba uzuri wa Aisha haukuwa ule aliokuwa ameuona kipindi cha nyuma bali alikuwa na uzuri wa ziada ambao haukuwa ukionekana kutokana na mavazi aliyokuwa amevaa.

Mavazi mapya yalimfanya kuonekana mzuri mno. Razak alichoka, muda huo alitaka kumwambia ukweli Aisha kwamba alikuwa akimpenda, hakutaka kitu kingine chochote kutoka kwake zaidi ya kuwa mpenzi wake, ufuate uchumba na hatimaye ndoa.

“Nimefanya haya yote kwa ajili yako,” alisema Razak, uso wake ulipendeshwa na tabasamu pana.

“Nashukuru sana...kwa nini umefanya hivi?” aliuliza Aisha huku akimwangalia Razak usoni kwa macho yaliyojaa aibu mno.

“Nimefanya hivi kwa sababu ninakupenda Aisha...siku ya kwanza kukutana nawe, nimehisi kitu cha tofauti sana, nimetokea kukupenda mno, sipo hapa kwa ajili ya kukuchezea, nipo kwa ajili ya kukuoa...” alisema Razak kwa sauti ya chini iliyojaa mahaba.

Aisha alishtuka, hakuamini kile alichokisikia kutoka kwa Razak, alimwangalia vizuri kuona kama mwanaume huyo alimaanisha alichokisema, hakika alimaanisha kila kitu alichoongea mbele yake.

Je nini kitaendelea.....
 
Sehemu ya 16

Huo ulikuwa mtihani mkubwa kwake, hakuamini mtu kama yeye kupendwa na mwanaume mwenye fedha kama Razak, hakutaka kuamini, moyoni, alihisi kama alikuwa akitaniwa, na Razak hakumaanisha alichomwambia.

“Unanipenda mimi?” aliuliza Aisha huku akionekana kushtuka.
“Ndiyo!”

“Umenipendea nini?”
“Aisha...kila kitu ulichokuwa nacho, nimekipenda, nimependa jinsi ulivyo, kila kitu kwa pamoja, nimekupenda,” alisema Razak.

Razak akamsogelea Aisha pale alipokuwa na kisha kuubusu mdomo wake. Mwili mzima wa Aisha ulikuwa ukitetemeka kama mtu aliyesikia baridi kali.

Wakati yote hayo yakitokea, Ahmed na Mohammed walikuwa pembezoni mwa sebule huku wakichungulia kisiri, kila kitu kilichokuwa kikendelea, walikuwa wakikiona tu.

Hapo ndipo walipojua sababu ya Razak kumtafuta Aisha kwa udi na uvumba, mpaka kufikia hatua hiyo, tayari wakajua kwamba hata wao maisha yao yangekuwa mazuri kwani kwa Aisha, wao walisimama kama ndugu zao.

“Kumbe anampenda!” alisema Ahmad kwa mshangao.

“Nilijua tu, nililigundua hilo mapema kabisa,” alisema Mohammed.

Maisha yake yalikuwa ya kimasikini, hakuwahi kupata maisha mazuri tangu alipozaliwa. Mama yake alikufa miaka mingi iliyopita, alizaliwa huku mama yake akiwa mitaani kwa hiyo hata kipindi hicho bado aliendelea kuishi hukohuko mitaani.

Hakuwa na ndugu, kama alikuwa nao hakuwa akiwafahamu kabisa. Watu wa karibu aliokuwa amezoeana nao ambao kwake walikuwa kama ndugu ni watoto wa mitaani na wale mapacha wawili ambao kwake walikuwa kila kitu.

Alimkubali Razak, hata kama mwanaume huyo alikuwa na fedha lakini naye mwenyewe moyo wake ulianza kumuingiza mwanaume huyo ila hakutaka kumwambia kwani alijua fika kwamba kuna siku tu mwanaume huyo angetamka maneno hayo.

Alipokubaliwa, Razak hakuamini, alichokifanya ni kumnyanyua Sabrina kisha kumkumbatia kwa mahaba mazito, joto la miili yao, likakutana na kujisikia tofauti, kilichotokea baada ya hapo ni kuufungua ukurasa mpya wa mapenzi.
*****

Kelele zilikuwa zikisikika kutoka ndani ya jumba moja la kifahari, watu watatu walikuwa wakibishana, mmoja alikuwa mwanaume mzee, mwingine mwanamke mzee lakini huyo wa tatu alikuwa msichana mwenye umri usiozidi miaka ishirini, huyu alikuwa Sabrina.

Mara baada ya kuanza uhusiano mpya na Sharifu, Sabrina aliamua kuwaita wazazi wake na kuwaeleza kweli kwamba alikuwa amepata mwanaume mpya na si Razak ambaye alikuwa naye tangu alipokuwa mtoto mdogo.

Wazazi wake hawakuamini kile walichokisikia, walimkubali Razak, kwao, mwanaume huyo alionekana kuwa sahihi kuwa mkwe wao, hawakutaka kuona binti yao akiwa na mwanaume mwingine tofauti na Razak.

Walitoa baraka zote kama wazazi kwa kumwambia Sabrina kwamba waliridhia kuona mwanaume huyo akimuoa binti yao, hivyo wao kama wazazi kitu pekee walichokuwa wakikisubiria kilikuwa ndoa tu.

Baada ya kupita muda fulani, leo binti yao aliwaletea habari nyingine, mpya ambayo iliwasisimua sana baada ya kuwaambia kwamba alikuwa amemuacha Razak kwa sababu alipata mwanaume mwingine mwenye mchanganyiko wa rangi aitwaye Sharifu.

Wazazi wakachanganyikiwa, hawakuamini kile alichokisikia, walimwangalia binti yao, walihisi kama alichanganyikiwa, hawakuamini kabisa kile walichoambiwa.

Walimfahamu Razak, hakuwa mwanaume machepele, alikuwa mwanaume mpole aliyejitoa kwa kila kitu, wao kama wazazi walimpenda sana, sasa kitendo cha binti yao kuwaambia kwamba aliachana na Razak kwa ajili ya mwanaume mwingine, iliwachanganya.

“Haiwezekani Sabrina....” alisema baba yake kwa sauti kubwa.

“Nimeamua baba, mtake, msitake ni lazima Sharifu anioe...” alisema Sabrina.
“Mimi si ndiye mzazi?”
“Na mimi si ndiye mtoto?”

“Utaona, hakuna ndoa hapa, huwezi kuolewa na mwanaume mchafu hata kama ana fedha kiasi gani,” alisema baba yake kwa sauti kubwa, alionekana kukasirika mpaka mishipa ya shingo kumtoka.

Je nini kitaendelea...
 
Sehemu ya 17

“Kwa nini? Kwani rangi ya ngozi ni tatizo? Ni lazima Razak anioe, hata msiposhiriki katika harusi yangu, mtajijua wenyewe...” alisema Sabrina tena akimaanisha.

Wao walikuwa Waarabu kwa asilimia mia moja kama alivyokuwa Razak, kama walivyokuwa Waarabu wengine, hata wao walitamani kumuona binti yao akiolewa na mtu ambaye alikuwa kama wao.

Hawakuwapenda watu waliochanganyika rangi, kwao, walionekana kuwa wachafu na hawakuwapa nafasi yoyote ile, kumkaribisha mtu aliyekuwa na mchanganyiko wa rangi kwao ilionekana kama laana vile.

Hiyo ndiyo sababu iliyofanya wamkatae Sharifu kwa nguvu zote. Hawakutaka kusikia chochote kuhusu mwanaume huyo, kwao, yule Razak aliyeachwa ndiye aliyeonekana kuwa wa maana kuliko huyu aliyekuwa naye kwa sasa.

“Ni lazima niolewe....” alisema Sabrina kwa sauti ya juu kabisa.
“Huolewiiii...nimesema huolewiiii...” alisema baba yake.

Sabrina hakuweza kuvumilia, japokuwa ilikuwa usiku, akaufungua mlango wa sebuleni na kuondoka zake.

Wazazi wake walihisi kwamba alikuwa akienda nje kupumzika lakini ghafla, wakasikia geti likifunguliwa, walipotoka nje kuangalia kama aliyefungua geti alikuwa Sabrina.

Hawakuweza kumuona, wakagundua kwamba msichana huyo ndiye aliyetoka, hapohapo nao wakaenda hukohuko nje, pande zote, palikuwa peupe, Sabrina hakuonekana jambo lililowatia hofu kubwa mioyoni mwao, Sabrina hakuwa mtu wa kutoka usiku kwani walifahamu kwamba kulikuwa na hatari kubwa. Wakaanza kuita lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeitikia.
*****

Razak na Aisha walikubaliana kuwa wapenzi, kuingia kwenye uchumba na mwisho kabisa kuoana. Hilo lilimfurahisha sana mwanaume huyo ila tatizo ambalo lilikuja kichwani mwake ni kwa namna gani angeweza kuwaambia wazazi wake.

Ilikuwa ni lazima kuwapa taarifa juu ya kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Alijua fika kwamba wazazi hao walimpenda sana Sabrina kwa kuwa alikuwa msichana mzuri, Mwarabu na kingine zaidi, walijua ni kwa namna gani msichana huyo alivyompenda kijana wao pasipo kuujua ukweli wa upande wa pili.

Hicho ndicho kitu pekee kilichomfanya kuwa na mawazo mengi. Hali hiyo ilimfanya Aisha kuwa na wasiwasi, akahisi kwamba kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea, akaamua kuuliza.

Je nini kitaendelea....
 
Sehemu ya 18

“Kuna nini?”
“Hakuna kitu mpenzi...”
“Ila umebadilika ghafla, hauna furaha, niambie tatizo nini,” aliuliza Aisha.
Razak hakutaka kujibu swali hilo, alichokifanya ni kumzugisha kwa stori nyingine huku akiulazimisha uchangamfu, baada ya hapo, akamwambia ajiandae kwani ilikuwa ni lazima ampeleke kwa wazazi wake kwa ajili ya kumtambulisha.

Baada ya kujiandaa, hawakutaka kupoteza muda, wakaingia ndani ya gari na safari ya kuelekea Masaki kuanza. Njiani, Razak alijitahidi kuwa muongeaji, hakutaka Aisha afahamu kitu chochote au kuona mabadiliko yoyote kwake, waliongea na kucheka sana na baada ya dakika kadhaa wakawa wamekwishafika nyumbani, wakateremka na kuelekea ndani.

Aliwakuta wazazi wake wote, alikaribishwa, wazazi hao walibaki na maswali mengi kuhusu msichana aliyeingia na Razak alikuwa nani na kwa nini alikuja naye nyumbani hapo?
Kwa kumwangalia, alikuwa msichana mrembo, aliyevutia lakini bado kwa mbali ilikuwa ni rahisi kujua kwamba hata mavazi aliyokuwa amevaa ilikuwa ni kama kulazimishwa.

Wazazi hao hawakutaka kuzungumza kitu, walijua kwamba iwe isiwe huyo msichana aliyeletwa kwao alikuwa mpenzi wa Razak ila swali pekee lililowajia vichwani mwao ni msichana Sabrina tu, alikuwa wapi? Na kwa nini Razak aliamua kuja na msichana mwingine?

Walikula na kunywa, walifurahia maisha, kwa Razak, siku hiyo hakutaka kumtambulisha Aisha kama mpenzi wake, aliwaambia kwamba alikuwa rafiki yake kipenzi aliyekuwa akiishi Magomeni, wazazi wake walifurahia, hawakuonyesha chuki yoyote ile.

Ilipofika saa kumi na moja jioni, wakaaga tayari kwa kuondoka kwani Razak aliwaambia wazi kwamba aliamua kuishi Kijitonyama kwa kuwa kulikuwa na mambo mengi binafsi alitaka kuyafanya, wazazi hawakuhoji, walikubaliana naye. Aisha alipoelekea kwenye gari tu, wakamvuta Razak.

“Razak, hebu tuambie ukweli, huyu Aisha ni nani kwako?” aliuliza baba yake.
“Ni mchumba wangu...”

“Tangu lini?” aliingilia mama yake.
“Kama wiki hivi mama...” alidanganya.
“Na vipi kuhusu Sabrina?” alidakia baba yake.

“Ni stori ndefu....”
“Ipi? Haisimuliki?”
“Inasimulika, ila inaumiza...”
“Hebu njoo huku.”

Huko, Razak alianza kuwahadithia wazazi wake kile kilichotokea, aliwaambia kila kitu tangu mapenzi yao yalipoanza kuyumba, alipokuwa akimbeleza msichana huyo kwa kumtumia meseji na hata kumpigia simu lakini msichana huyo hakuonyesha mabadiliko yoyote yale.

Hakuishia hapo, kwa kuwa alikuwa na meseji, akawapa wazisome, wote walihuzunika, hawakuamini kama msichana Sabrina ndiye yule aliyemfanyia vile kijana wao, wakatokea kumchukia sana Sabrina ila hiyo haikuwa sababu ya kumwamini sana Razak, walichokifanya ni kumpigia simu msichana huyo.

Kile walichoambiwa ndicho kilichotokea, Sabrina alibadilika, aliwajibu kiburi na mwisho kabisa kumalizia kwamba hakutaka kuwa na kijana wao kwani hakuwa chaguo lake tena.

Je nini kitaendelea......
 
Sehemu ya 19

Walisikitika lakini hawakuwa na jinsi, walitamani kumuona kijana wao akiwa na furaha hivyo kile alichoamua kuwa na msichana Aisha, kwao waliona sahihi kabisa.

“Ni lazima umuoe huyu Aisha, tena haraka iwezekanavyo...huyu Sabrina si binadamu, ni mnyama...” alisema baba yake huku akionekana kuwa na hasira mno.

“Nashukuru kwa ruhusa yenu, nitafanya hivyo mwaka huuhuu...” alisema Razak huku akiachia tabasamu pana, baada ya hapo, huyo akaondoka zake na Aisha huku moyo wake ukiwa na furaha mno, hata Aisha aliligundua hilo.

*****
“Tatizo nini Sabrina?” ilisikika sauti ikiuliza.
“Nimekuja kwako...”
“Kufanya nini tena?”
“Kulala...nyumbani wamenifukuza kwa ajili yako...”
“Umefukuzwa nyumbani kwa ajili yangu?”
“Ndiyo!”

Sabrina aliamua kwenda nyumbani kwa kina Sharifu, aliamua kukimbilia huko kwani ndipo kulipokuwa kimbilio lake. Alichanganyikiwa, kitendo cha kukataliwa kuwa na mwanaume huyo kilimuudhi na kitu pekee alichoona kustahili kukifanya ni kukimbia na kuelekea nyumbani kwa mwanaume huyo.

Moyo wake ulichanganyikiwa, alikuwa kama kichaa, wakati huo, hakuingia ndani bali alisimama getini na alikuwa akizungumza na Sharifu kwa kutumia kimashine kidogo kilichopachikwa ukutani ambapo kwa huko ndani kulikuwa na simu maalumu kwa ajili ya kuzungumza na mtu aliyekuwa ndani.

“Subiri nakuja...” alisikika Sharifu.
Sabrina alibaki akiwa amesimama nje ya geti, ilikuwa usiku sana na kila sehemu kulikuwa na ukimya mkubwa, ni sauti za mbwa ndizo zilizokuwa zikisikika kwa mbali.

Alibaki akitetemeka pale aliposimama, baridi lilimpiga ila akawa hana jinsi, ilikuwa ni lazima asubiri ili afunguliwe mlango. Wala hazikupita dakika nyingi, Sharifu akatokea mahali hapo, akalifungua geti na Sabrina kuingia ndani.
“Karibu sana...” alisema Sharifu.
“Nashukuru...”

Wakatoka mahali hapo na kwenda ndani ya nyumba hiyo. Sharifu alionekana kutokujiamini, alionekana kuwa na wasiwasi mwingi huku akiwa mtu wa mawazo mengi, macho yake hayakutulia sehemu moja, aliyapeleka huku na kule kama mtu aliyekuwa akikitafuta kitu fulani, ila alipotazamwa na Sabrina, uso wake akauwekea tabasamu pana.

Wakaingia mpaka sebuleni ambapo wakapitiliza mpaka chumbani. Sabrina alionekana kushtuka hasa macho yake yalipotua kitandani. Kilikuwa shaghalabaghala, huku kwa mbali chumba kukinukia manukato ya kike.

“Mmh!” alijikuta akiguna.
“Nini tena?”
“Mbona nasikia harufu manukato ya kike?”
“Wapi? Humu?”
“Ndiyo!”

Je nini kitaendelea.....
 
Sehemu ya 20

“Mmh! Manukato ya kike? Mbona ni yangu yanaitwa The Prince...”
“Hapana! Ni manukato ya kike, yanaitwa Cleopatra...” alisema Sabrina huku akionekana kuwa na wasiwasi mno.

“Hapana! Utakuwa umechanganya! Hebu niambie, mbona usikuusiku, imekuwaje huko?” aliuliza Sharifu huku akiwa ameingizia ishu nyingine kabisa na kuipotezea ile ya manukato.

“Nimekimbia nyumbani kwa ajili yako,” alijibu Sabrina.
“Kisa?”
“Wazazi hawakufurahia mimi kuwa nawe...”

“Haiwezekani! Kwa nini?”
“Sijui, ila hawakufurahi kabisa...nimeona bora niondoke...” alisema Sabrina.
Kwa kumwangalia tu alionyesha kuchanganyikiwa, kila alipomwangalia Sharifu, alimpenda zaidi ya alivyokuwa akimpenda hata kipindi cha nyuma.

Mwanaume huyo, kwake alikuwa kila kitu, hakutaka kumkumbuka Razak, aliuona moyo wake ukiwa na chuki juu ya mwanaume wake huyo aliyepita, mtu ambaye aliona kupanga naye maisha alikuwa huyu aliyesimama mbele yake, Sharifu.

Kwa Razak, bado alionekana kuwa na wasiwasi, hakuwa mtu huru kama ilivyokuwa kipindi wanapokuwa pamoja, kila wakati alikuwa mtu wa kuangalia huku na kule hali iliyomtia wasiwasi hata Sabrina mwenyewe.

Akahisi kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea na kitu pekee kilichokuja moja kwa moja kichwani ni kwamba mpenzi wake huyo aliingiza mwanamke ndani ya chumba hicho.
“Mbona upo hivyo?” aliuliza Sabrina.
“Nipoje?”

“Hujiamini, unaonekana una wasiwasi...una nini?”
“Hakuna kitu!”
“Umeingiza mwanamke?”
“Nani? Mimi? Hapana! Niingize mwanamke wa nini?” aliuliza Sharifu huku akijifanya kushtuka.
“Mmh! Sawa! Naomba nikaoge kwanza...”
“Hakuna tatizo...”

Sabrina hakuwa na amani, kitu pekee alichohisi ni kwamba mpenzi wake huyo alikuwa ameingiza mwanamke ndani ya nyumba. Alitaka kujua ukweli na ndiyo maana akamwambia kwamba alitaka kwenda bafuni kuoga lakini ukweli ni kwamba alitaka kufahamu kilichokuwa kikiendelea.

Alipokwenda bafuni, hakujimwagia maji bali alifungua bomba na kusimama pembeni, hapo ndipo aliposikia mlango wa chumbani ukifunguliwa, kwa harakaharaka akatoka, Sharifu hakuwepo, alikuwa ametoka.

Hakutaka kubaki chumbani, naye akatoka na kuanza kwenda sebuleni ili kuona nini kiliendelea, alipofika huko, napo hakukuta mtu. Hakukata tamaa, alichokijua ni kwamba lazima Sharifu aliingiza mwanamke ndani ya nyumba hiyo, hivyo akaenda nyuma ya nyumba hiyo ambapo huko akaanza kusikia minong’ono.
“Nusrat...nenda kwanza....” aliisikia sauti ya Sharifu.

“Ila nani ameingia?”
“Mama...”
“Usiku wote huu mpenzi...”
“Wewe nenda, nitakutafuta kesho...chukua hii hela, itakusaidia katika usafiri....” alisikika Sharifu.

Sabrina pale alipokuwa, alihisi miguu yake ikikosa nguvu, mapigo ya moyo yakaanza kumdunda kwa nguvu, hakuamini kile alichokisikia, yaani mwanaume aliyempenda, aliyempa moyo wake, leo hii aliingiza mwanamke mwingine ndani ya nyumba.

Je nini kitaendelea.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom