Sehemu ya 08
Kila alipomwangalia mwanaume yule, alimkumbuka, alikuwa yuleyule wa usiku uliopita ambaye alikuwa akiwakimbiza mapacha wale, Ahmed na Mohammed.
Kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuwaangalia mapacha wale, je, walikuwa wamejeruhiwa? Alipowaangalia, walikuwa salama kabisa tena wote nyuso zao zilitawaliwa na tabasamu pana.
Hakuelewa ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea, moyo wake uliogopa mno, hakumwamini mwanaume huyo ambaye alikaa nyuma ya usukani huku uso wake ukiwa kwenye tabasamu pana, kichwa chake kikawa na maswali mengi, tena yote hayo yalikosa majibu.
“Wewe ni nani?” aliuliza Aisha.
“Naitwa Razak....unanikumbuka?” aliuliza Razak.
“Ndiyo! Si yule wa usiku uliyekuwa ukiwakimbiza hawa baada ya kukuibia taa za gari?” aliuliza Aisha swali lililowashtua mapacha wale, wakatamani kuteremka, wakahisi kwamba mtu huyo alikuja kuwakamata.
“Naomba nikaendelee na shughuli zangu jamani...” alisema Mohammed huku akitaka kuteremka.
Je nini kitaendelea....