Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,945
Mtunzi Nyemo Chilongani
Sehemu ya 01
“Nahitaji kubadilisha tairi, unaweza kunisaidia kaka?” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja akimuuliza kijana aliyekuwa amekaa pembeni kwenye tofali.
“Hakuna tatizo, kuna hela?”
“Kunisaidia tu mpaka hela?”
“Ndiyo! Hakuna msaada bila hela, hasa kwa nyie mnaomiliki magari ya kifahari! Yaani Range Rover SUV, thamani zaidi ya shilingi milioni mia moja, ushindwe hata kunitoa buku teni! Acha masihara.”
“Basi sawa! Nitakupa! Nisaidie kwanza.”
Ukimya ulikuwa umetawala sehemu kubwa ya Posta Feri, watu wachache walikuwa wamesimama pembeni kwa ajili ya kusubiri pantoni waweze kuvuka na kuelekea Kigamboni.
Muda ulikuwa umekwenda sana, ilikuwa ni saa sita usiku muda ambao si watu wengi waliokuwa wakivuka eneo hilo kwenda Kigamboni.
Gari zuri la thamani, Range Rover SUV nyeusi ilikuwa imesimama pembezoni mwa barabara ya kuingia katika kivuko cha pantoni karibu kabisa na Kituo cha Polisi cha Magogoni.
Halikuwa limeegeshwa kwa makusudi bali kutokana na tairi lake kupata pancha, dereva hakutaka kuendelea na safari, ilikuwa ni lazima kubadilisha tairi na kuweka tairi jingine kabla ya kuendelea na safari yake.
Mwanaume huyo mwenye mwenye hilo gari ambaye alikuwa Mwarabu, Razak Mahmoud alisimama pembeni ya gari hilo akimwangalia jamaa aliyekuwa akihangaika kutoa tairi la gari lake kwa ajili ya kuweka jingine.
Muda wote, Razak alionekana kuwa na haraka mno, kila wakati alikuwa akiangalia saa yake huku akitembea huku na kule, kwa kumwangalia harakahara ilikuwa ni rahisi kujua kwamba alikuwa na uharaka wa kwenda kule alipotaka kwenda.
“It’s impossible, I have to see him right now!” (haiwezekani, ni lazima nimuone sasa hivi!) alisema Razak huku akionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
Japokuwa kijana yule aliyekuwa akimsaidia alijitahidi kufanya kazi hiyo kwa haraka lakini kila alipomwangalia, aliona akiifanya kazi hiyo taratibu sana, alitamani kumuharakisha, amalize haraka ili aendelee na safari yake lakini kufanya hivyo lilikuwa jambo gumu.
“Vipi?” aliuliza.
“Ndiyo naendelea kiongozi, nitamaliza sasa hivi,” alijibu jamaa huyo.
“Hivi Kigamboni kutakuwa na bodaboda niende na kuacha gari hapa?”
“Sasa hivi?”
“Ndiyo!”
“Mmh! Sidhani, na kama zitakuwepo inabidi uwe makini tu, si unajua usiku una mambo mengi,” alisema kijana huyo.
“Kwa nini?”
“Kwani wewe unataka kwenda wapi?”
“Mji Mwema!”
“Kuna nini usiku wote huu? Au ndipo unapoishi?”
“Hapana! Kuna mtu nakwenda kumcheki mara moja,” alisema Razak.
Muda ulizidi kusonga mbele, ilipofika saa sita na dakika arobaini usiku, tayari kijana yule alimaliza kufanya kazi aliyokuwa akiifanya na hivyo kulipwa fedha aliyotaka kulipwa na kuondoka zake.
Alikuwa amekwishajiandaa tayari kwa kuvuka kivuko hicho, kitu kilichomshangaza ni kwamba bado geti lilikuwa limefungwa. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, ikambidi ateremke na kwenda kwenye kidirisha na kuuliza kilichokuwa kikiendelea, akaambiwa kwamba ilikuwa ni utaratibu wa kivuko kila ifikapo saa sita usiku, kufungwa kwa saa moja kisha baadaye safari kuendelea.
“Kwa hiyo mpaka saa saba?”
“Ndiyo!”
“Sawa.”
Je nini kitaendelea?
Sehemu ya 01
“Nahitaji kubadilisha tairi, unaweza kunisaidia kaka?” ilisikika sauti ya mwanaume mmoja akimuuliza kijana aliyekuwa amekaa pembeni kwenye tofali.
“Hakuna tatizo, kuna hela?”
“Kunisaidia tu mpaka hela?”
“Ndiyo! Hakuna msaada bila hela, hasa kwa nyie mnaomiliki magari ya kifahari! Yaani Range Rover SUV, thamani zaidi ya shilingi milioni mia moja, ushindwe hata kunitoa buku teni! Acha masihara.”
“Basi sawa! Nitakupa! Nisaidie kwanza.”
Ukimya ulikuwa umetawala sehemu kubwa ya Posta Feri, watu wachache walikuwa wamesimama pembeni kwa ajili ya kusubiri pantoni waweze kuvuka na kuelekea Kigamboni.
Muda ulikuwa umekwenda sana, ilikuwa ni saa sita usiku muda ambao si watu wengi waliokuwa wakivuka eneo hilo kwenda Kigamboni.
Gari zuri la thamani, Range Rover SUV nyeusi ilikuwa imesimama pembezoni mwa barabara ya kuingia katika kivuko cha pantoni karibu kabisa na Kituo cha Polisi cha Magogoni.
Halikuwa limeegeshwa kwa makusudi bali kutokana na tairi lake kupata pancha, dereva hakutaka kuendelea na safari, ilikuwa ni lazima kubadilisha tairi na kuweka tairi jingine kabla ya kuendelea na safari yake.
Mwanaume huyo mwenye mwenye hilo gari ambaye alikuwa Mwarabu, Razak Mahmoud alisimama pembeni ya gari hilo akimwangalia jamaa aliyekuwa akihangaika kutoa tairi la gari lake kwa ajili ya kuweka jingine.
Muda wote, Razak alionekana kuwa na haraka mno, kila wakati alikuwa akiangalia saa yake huku akitembea huku na kule, kwa kumwangalia harakahara ilikuwa ni rahisi kujua kwamba alikuwa na uharaka wa kwenda kule alipotaka kwenda.
“It’s impossible, I have to see him right now!” (haiwezekani, ni lazima nimuone sasa hivi!) alisema Razak huku akionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
Japokuwa kijana yule aliyekuwa akimsaidia alijitahidi kufanya kazi hiyo kwa haraka lakini kila alipomwangalia, aliona akiifanya kazi hiyo taratibu sana, alitamani kumuharakisha, amalize haraka ili aendelee na safari yake lakini kufanya hivyo lilikuwa jambo gumu.
“Vipi?” aliuliza.
“Ndiyo naendelea kiongozi, nitamaliza sasa hivi,” alijibu jamaa huyo.
“Hivi Kigamboni kutakuwa na bodaboda niende na kuacha gari hapa?”
“Sasa hivi?”
“Ndiyo!”
“Mmh! Sidhani, na kama zitakuwepo inabidi uwe makini tu, si unajua usiku una mambo mengi,” alisema kijana huyo.
“Kwa nini?”
“Kwani wewe unataka kwenda wapi?”
“Mji Mwema!”
“Kuna nini usiku wote huu? Au ndipo unapoishi?”
“Hapana! Kuna mtu nakwenda kumcheki mara moja,” alisema Razak.
Muda ulizidi kusonga mbele, ilipofika saa sita na dakika arobaini usiku, tayari kijana yule alimaliza kufanya kazi aliyokuwa akiifanya na hivyo kulipwa fedha aliyotaka kulipwa na kuondoka zake.
Alikuwa amekwishajiandaa tayari kwa kuvuka kivuko hicho, kitu kilichomshangaza ni kwamba bado geti lilikuwa limefungwa. Hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, ikambidi ateremke na kwenda kwenye kidirisha na kuuliza kilichokuwa kikiendelea, akaambiwa kwamba ilikuwa ni utaratibu wa kivuko kila ifikapo saa sita usiku, kufungwa kwa saa moja kisha baadaye safari kuendelea.
“Kwa hiyo mpaka saa saba?”
“Ndiyo!”
“Sawa.”
Je nini kitaendelea?