Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,937
- Thread starter
- #81
Sehemu ya 27
Sabrina alikuwa akitetemeka, joto lilikuwa likiongezeka mwilini mwake, hakuamini kile alichokuwa akikisoma katika notebook aliyokuwa nayo ambayo aliitoa katika chumba cha Sharifu.
Kitabu kile kilikuwa na majina ya wanawake aliotembea nayo Sharifu, walikuwa wanawake kadhaa na yeye mwenyewe kukiri kwamba wote hao aliotemba nao hakuwa akiwapenda, alitaka kuwaumiza kama yeye alivyoumizwa na msichana wake wa kwanza, Shamsia.
Moyo wake uliwaka kwa hasira, alijikuta akikitupa notebook ile na kujilaza kitandani.
Alishindwa kuvumilia, kilichokuwa kimetokea kwake kilikuwa dharau kubwa, yaanii ampende mwanaume kwa mapenzi yote halafu mwisho wa siku aseme kwamba alitaka hakuwa akipendwa bali kuchezewa, hakika yalikuwa ni maumivu makubwa ambayo hakutarajia kuyapata.
Hasira iliyowaka moyoni mwake, ikayaondoa mapenzi aliyokuwa nayo kwa Sharifu, alimchukia ghafla, kitu pekee alichokitaka ni kumuua mwanaume huyo na kisha yeye kufungwa, hata kama angefungwa kifungo cha maisha, sawa, kama ni kunyongwa, napo ingekuwa sawa ila si kumuacha mwanaume kama Sharifu aendelee kuishi.
Hakutaka kuondoka chumbani pale, alibaki akilia, alimsubiri Sharifu kwa hamu kubwa, alitaka mwanaume huyo atakapokuja basi amchome kisu na kumuua humohumo chumbani, na kama itawezekana, basi hata na yeye ajiue pia.
Aliendelea kumsubiri Sharifu, hakutulia chumbani, mara atoke, mara aingie, alipokumbuka kwamba hakuwa na kisu cha kufanyia mauaji, harakaharaka Sabrina akaondoka chumbani na kuelekea jikoni, huko akachukua kisu na kurudi chumbani.
“Nitakuua Sharifu...nitakuua Sharifu....” alisema Sabrina huku akilia kama mtoto.
Alikumbuka vilivyo kwamba alimuacha mwanaume ambaye aliamini kwamba angemuoa, akaangukia katika penzi la Sharifu ambaye leo hii eti alisema kwamba yeye alikuwa msichana wa kupita, yaani kumuumiza kama kisasi cha yeye kuumizwa na msichana mmoja huko Dubai, hakika hakutaka kusubiri, hakutaka kuona mwanamke mwingine anaumizwa baada yake, ilikuwa ni lazima amuue huyo Sharifu.
Dakika zilizidi kusonga mbele, masaa yalikatika lakini Sharifu hakutokea nyumbani hapo. Hiyo haikuwa kawaida kabisa, alimfahamu mwanaume wake, hakuwa mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, huwa anapokwenda kwa marafiki zake kucheza mchezo wa Darts, hurudi nyumbani haraka na kukaa naye.
Siku hiyo hali ilikuwa tofauti kabisa, hakujua kama Mungu alizungumza na Sharifu na kumpa taarifa kama kule nyumbani alimsubiri kwa hamu ili amuue au la, kwani kuchelewa kwake huko hakikuwa kitu cha kawaida kabisa.
“Ngoja niimpigie simu,” alisema na hapohapo kuchukua simu yake.
Akampigia, simu haikuita sana, ikapokelewa na sauti ya Sharifu kusikika upande wa pili.
Japokuwa ilikuwa ngumu lakini Sabrina alijikaza kwa kuongea kwa furaha, aliilazimisha furaha yake huku akiamini kabisa kwamba moyo wake ulikuwa na kidonda kikubwa kabisa tena huku akiwa na hamu kubwa ya kumwaga damu.
“Mpenzi...” aliita Sabrina.
“Niambie mpenzi! U mzima?” aliuliza Sharifu upande wa pili.
“Nipo poa...unarudi saa ngapi?” aliuliza Sabrina.
“Muda si mrefu...”
“Basi fanya haraka kipenzi, nimekumisi sana...”
“Kweli?”
“Ndiyo! Nataka nikuone, nikupe mapenzi motomoto mpaka upagawe...” alisema Sabrina.
“Nakuja fasta.....”
“Nakupenda mpenzi...”
“Nakupenda pia.”
Baada ya mazungumzo hayo machache, Sabrina akakata simu. Hapohapo kilio kikubwa kikaanza kusikika, hasira alizokuwa nazo hakuweza kuzivumilia, zilimkaba kooni kiasi kwamba kwa jinsi alivyokuwa akitetemeka, hali ile iliongezeka zaidi.
Harufu ya damu ikaanza kusikika puani mwake, hakuona sababu ya kumuonea huruma mwanaume huyo, alichokiona kuwa suluhisho, kumpa furaha moyoni mwake ni kumuua tu.
Baada ya dakika thelathini, akaanza kusikia muungurumo wa gari kutoka nje, harakaharaka akachungulia dirishani, akauona mwanga wa gari lililokuwa likipiga honi, hakuwa na wasiwasi, akajua dhahiri kwamba mtu aliyekuwa kwenye gari alikuwa Sharifu, hivyo harakaharaka akaanza kutoka ndani na kuelekea huko getini, amfungulie mlango, akiingia ndani tu amuue na yeye kujiua.
Akaanza kuelekea getini.
****
Sharifu alikuwa mtoto wa tajiri mkubwa aliyekuwa akiishi Dubai, alitembelea magari ya kifahari, alikuwa akiringa kwa sababu alipata kila kitu alichokitaka kutoka kwa baba yakee, alipewa fedha nyingi ambazo zote hizo alizitumia kwa kutembea na wanawake mbalimbali ambao kwa kifupi aliwaita mademu zake.
Jina lake likawa kubwa katika kumbi nyingi za starehe hapo Dubai, alijukana kila kona kwa kuwa hakuwa na mkono wa birika, kwa mtu aliyekuwa akihitaji kiasi fulani cha fedha, kwake hakukuwa na tatizo, alimpa, hasa wasichana.
Baadaye alipoamua kwenda kwa mama yake aliyekuwa akiishi nchini Tanzania katika jiji la Dar es Salaam, baba yake akamnunulia jumba kubwa lililomgharimu zaidi ya milioni mia saba, fedha halikuwa tatizo, kiasi hicho kilitolewa haraka sana.
Alipofika tu ndani ya nyumba hiyo, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kumuita mtaalamu wa IT na kumfungia kamera ndogo chumbani kwake ambazo hujulikana sana kwa jina la CCTV.
Kamera hizo zilifungwa kila kona, kuanzia sebuleni, ukumbini, bafuni, chooni mpaka chumbani. Hakuwa mtu wa kujiamini, alijua jinsi watu walivyo kwamba mara unapogundulika umetoka kwenye familia ya kitajiri, kitu cha kwanza kufanya ni kukuteka na kuhitaji kiasi kikubwa cha fedha.
Alihitaji kujua kila kitu kilichokuwa kikiendelea nyumbani kwake kupitia katika laptop aliyokuwa nayo, tena aliunganisha mpaka kwenye simu yake. Hata kama alikuwa mbali kiasi gani, kupitia vifaa vyake hivyo alijua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea nyumbani.
Mara baada ya kugombana na Sabrina, alijua fika kwamba ni lazima msichana huyo atafanya kitu kibaya kwani baada ya ugomvi ule wa kumfumania, msichana huyo alibadilika, akawa mtu wa hasira ambaye hakutaka kuzionyesha hasira zake hadharani, yaani alikuwa akiwaka moto moyoni mwake, nje, alijilazimisha kutoa tabasamu pana.
Siku ambayo Sabrina alipanga kumuua kwa kumchoma kisu, alikuwa akifuatilia kila hatua, alimuona msichana huyo akiwa kitandani amejipumzisha, hakuonekana kuwa na furaha kabisa na dalili zilionyesha kwamba alikuwa akilia sana.
Baada ya kukaa kwa kipindi fulani, akatoka ndani ya chumba kile na kuelekea jikoni. Kote huko, Sharifu alikuwa akifuatilia kwa ukaribu, aliona hatua kwa hatua mpaka msichana huyo alipochukua kisu na kwenda nacho chumbani.
“Mmh!” Sharifu alijikuta akiguna.
Hakuishia hapo, aliendelea kufuatilia kwa karibu kabisa, alitaka kuona nini kingetokea baada ya hapo. Alimuona Sabrina akielekea kitandani kwake, alionekana kuwa na hasira na hisia zake zikamwambia kwamba kile kisu kiliandaliwa kwa ajili yake.
Akamuona Sabrina akichukua simu na kuanza kumpigia, japokuwa sauti yake ilisikika vizuri lakini picha aliyokuwa akiiona, haikuwa nzuri kabisa, ilionyesha kwamba alikuwa na hasira kali, tena alikuwa radhi kufanya jambo lolote lile.
“Nakuja...” alisema kwenye simu na kuikata.
Alichokifanya ni kuwapigia simu marafiki zake, aliwaambia kila kitu kinachotakiwa kufanywa kwani hakutaka kurudi tena nyumbani kwake, kwa jinsi hali ilivyokuwa, ilikuwa ni lazima aondoke zake kwani vinginevyo, huyu Sabrina hakuwa mtu tena, alikuwa ni mnyama mwenye hasira kali ambaye kila wakati alikuwa akimuwinda.
“Nyie nendeni, fanyeni kama nilivyowaambia...” alisema Sharifu.
Je nini kitaendelea...
Sabrina alikuwa akitetemeka, joto lilikuwa likiongezeka mwilini mwake, hakuamini kile alichokuwa akikisoma katika notebook aliyokuwa nayo ambayo aliitoa katika chumba cha Sharifu.
Kitabu kile kilikuwa na majina ya wanawake aliotembea nayo Sharifu, walikuwa wanawake kadhaa na yeye mwenyewe kukiri kwamba wote hao aliotemba nao hakuwa akiwapenda, alitaka kuwaumiza kama yeye alivyoumizwa na msichana wake wa kwanza, Shamsia.
Moyo wake uliwaka kwa hasira, alijikuta akikitupa notebook ile na kujilaza kitandani.
Alishindwa kuvumilia, kilichokuwa kimetokea kwake kilikuwa dharau kubwa, yaanii ampende mwanaume kwa mapenzi yote halafu mwisho wa siku aseme kwamba alitaka hakuwa akipendwa bali kuchezewa, hakika yalikuwa ni maumivu makubwa ambayo hakutarajia kuyapata.
Hasira iliyowaka moyoni mwake, ikayaondoa mapenzi aliyokuwa nayo kwa Sharifu, alimchukia ghafla, kitu pekee alichokitaka ni kumuua mwanaume huyo na kisha yeye kufungwa, hata kama angefungwa kifungo cha maisha, sawa, kama ni kunyongwa, napo ingekuwa sawa ila si kumuacha mwanaume kama Sharifu aendelee kuishi.
Hakutaka kuondoka chumbani pale, alibaki akilia, alimsubiri Sharifu kwa hamu kubwa, alitaka mwanaume huyo atakapokuja basi amchome kisu na kumuua humohumo chumbani, na kama itawezekana, basi hata na yeye ajiue pia.
Aliendelea kumsubiri Sharifu, hakutulia chumbani, mara atoke, mara aingie, alipokumbuka kwamba hakuwa na kisu cha kufanyia mauaji, harakaharaka Sabrina akaondoka chumbani na kuelekea jikoni, huko akachukua kisu na kurudi chumbani.
“Nitakuua Sharifu...nitakuua Sharifu....” alisema Sabrina huku akilia kama mtoto.
Alikumbuka vilivyo kwamba alimuacha mwanaume ambaye aliamini kwamba angemuoa, akaangukia katika penzi la Sharifu ambaye leo hii eti alisema kwamba yeye alikuwa msichana wa kupita, yaani kumuumiza kama kisasi cha yeye kuumizwa na msichana mmoja huko Dubai, hakika hakutaka kusubiri, hakutaka kuona mwanamke mwingine anaumizwa baada yake, ilikuwa ni lazima amuue huyo Sharifu.
Dakika zilizidi kusonga mbele, masaa yalikatika lakini Sharifu hakutokea nyumbani hapo. Hiyo haikuwa kawaida kabisa, alimfahamu mwanaume wake, hakuwa mtu wa kuchelewa kurudi nyumbani, huwa anapokwenda kwa marafiki zake kucheza mchezo wa Darts, hurudi nyumbani haraka na kukaa naye.
Siku hiyo hali ilikuwa tofauti kabisa, hakujua kama Mungu alizungumza na Sharifu na kumpa taarifa kama kule nyumbani alimsubiri kwa hamu ili amuue au la, kwani kuchelewa kwake huko hakikuwa kitu cha kawaida kabisa.
“Ngoja niimpigie simu,” alisema na hapohapo kuchukua simu yake.
Akampigia, simu haikuita sana, ikapokelewa na sauti ya Sharifu kusikika upande wa pili.
Japokuwa ilikuwa ngumu lakini Sabrina alijikaza kwa kuongea kwa furaha, aliilazimisha furaha yake huku akiamini kabisa kwamba moyo wake ulikuwa na kidonda kikubwa kabisa tena huku akiwa na hamu kubwa ya kumwaga damu.
“Mpenzi...” aliita Sabrina.
“Niambie mpenzi! U mzima?” aliuliza Sharifu upande wa pili.
“Nipo poa...unarudi saa ngapi?” aliuliza Sabrina.
“Muda si mrefu...”
“Basi fanya haraka kipenzi, nimekumisi sana...”
“Kweli?”
“Ndiyo! Nataka nikuone, nikupe mapenzi motomoto mpaka upagawe...” alisema Sabrina.
“Nakuja fasta.....”
“Nakupenda mpenzi...”
“Nakupenda pia.”
Baada ya mazungumzo hayo machache, Sabrina akakata simu. Hapohapo kilio kikubwa kikaanza kusikika, hasira alizokuwa nazo hakuweza kuzivumilia, zilimkaba kooni kiasi kwamba kwa jinsi alivyokuwa akitetemeka, hali ile iliongezeka zaidi.
Harufu ya damu ikaanza kusikika puani mwake, hakuona sababu ya kumuonea huruma mwanaume huyo, alichokiona kuwa suluhisho, kumpa furaha moyoni mwake ni kumuua tu.
Baada ya dakika thelathini, akaanza kusikia muungurumo wa gari kutoka nje, harakaharaka akachungulia dirishani, akauona mwanga wa gari lililokuwa likipiga honi, hakuwa na wasiwasi, akajua dhahiri kwamba mtu aliyekuwa kwenye gari alikuwa Sharifu, hivyo harakaharaka akaanza kutoka ndani na kuelekea huko getini, amfungulie mlango, akiingia ndani tu amuue na yeye kujiua.
Akaanza kuelekea getini.
****
Sharifu alikuwa mtoto wa tajiri mkubwa aliyekuwa akiishi Dubai, alitembelea magari ya kifahari, alikuwa akiringa kwa sababu alipata kila kitu alichokitaka kutoka kwa baba yakee, alipewa fedha nyingi ambazo zote hizo alizitumia kwa kutembea na wanawake mbalimbali ambao kwa kifupi aliwaita mademu zake.
Jina lake likawa kubwa katika kumbi nyingi za starehe hapo Dubai, alijukana kila kona kwa kuwa hakuwa na mkono wa birika, kwa mtu aliyekuwa akihitaji kiasi fulani cha fedha, kwake hakukuwa na tatizo, alimpa, hasa wasichana.
Baadaye alipoamua kwenda kwa mama yake aliyekuwa akiishi nchini Tanzania katika jiji la Dar es Salaam, baba yake akamnunulia jumba kubwa lililomgharimu zaidi ya milioni mia saba, fedha halikuwa tatizo, kiasi hicho kilitolewa haraka sana.
Alipofika tu ndani ya nyumba hiyo, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kumuita mtaalamu wa IT na kumfungia kamera ndogo chumbani kwake ambazo hujulikana sana kwa jina la CCTV.
Kamera hizo zilifungwa kila kona, kuanzia sebuleni, ukumbini, bafuni, chooni mpaka chumbani. Hakuwa mtu wa kujiamini, alijua jinsi watu walivyo kwamba mara unapogundulika umetoka kwenye familia ya kitajiri, kitu cha kwanza kufanya ni kukuteka na kuhitaji kiasi kikubwa cha fedha.
Alihitaji kujua kila kitu kilichokuwa kikiendelea nyumbani kwake kupitia katika laptop aliyokuwa nayo, tena aliunganisha mpaka kwenye simu yake. Hata kama alikuwa mbali kiasi gani, kupitia vifaa vyake hivyo alijua ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea nyumbani.
Mara baada ya kugombana na Sabrina, alijua fika kwamba ni lazima msichana huyo atafanya kitu kibaya kwani baada ya ugomvi ule wa kumfumania, msichana huyo alibadilika, akawa mtu wa hasira ambaye hakutaka kuzionyesha hasira zake hadharani, yaani alikuwa akiwaka moto moyoni mwake, nje, alijilazimisha kutoa tabasamu pana.
Siku ambayo Sabrina alipanga kumuua kwa kumchoma kisu, alikuwa akifuatilia kila hatua, alimuona msichana huyo akiwa kitandani amejipumzisha, hakuonekana kuwa na furaha kabisa na dalili zilionyesha kwamba alikuwa akilia sana.
Baada ya kukaa kwa kipindi fulani, akatoka ndani ya chumba kile na kuelekea jikoni. Kote huko, Sharifu alikuwa akifuatilia kwa ukaribu, aliona hatua kwa hatua mpaka msichana huyo alipochukua kisu na kwenda nacho chumbani.
“Mmh!” Sharifu alijikuta akiguna.
Hakuishia hapo, aliendelea kufuatilia kwa karibu kabisa, alitaka kuona nini kingetokea baada ya hapo. Alimuona Sabrina akielekea kitandani kwake, alionekana kuwa na hasira na hisia zake zikamwambia kwamba kile kisu kiliandaliwa kwa ajili yake.
Akamuona Sabrina akichukua simu na kuanza kumpigia, japokuwa sauti yake ilisikika vizuri lakini picha aliyokuwa akiiona, haikuwa nzuri kabisa, ilionyesha kwamba alikuwa na hasira kali, tena alikuwa radhi kufanya jambo lolote lile.
“Nakuja...” alisema kwenye simu na kuikata.
Alichokifanya ni kuwapigia simu marafiki zake, aliwaambia kila kitu kinachotakiwa kufanywa kwani hakutaka kurudi tena nyumbani kwake, kwa jinsi hali ilivyokuwa, ilikuwa ni lazima aondoke zake kwani vinginevyo, huyu Sabrina hakuwa mtu tena, alikuwa ni mnyama mwenye hasira kali ambaye kila wakati alikuwa akimuwinda.
“Nyie nendeni, fanyeni kama nilivyowaambia...” alisema Sharifu.
Je nini kitaendelea...