Pole yake, mkataa pema pabaya panamwitaKakutana na play boy
hivi amepotelea wapi jaman shemeji yanguNimemiss the_legend ukimuona mpe salaam zangu jamani
ndo nini sasa,tunaanza kuumia mapema hiviSehemu ya 29
“Razak...Razak....baridi linaniumiza...” alisikika Aisha kwa sauti ya chini.
“Baridi linakuumiza?”
“Ndiyo!”
“Subiri nikazime kiyoyozi...” alisema Razak.
Ilikuwa ni usiku wa manane, wote walikuwa wamelala chumbani, ukimya mkubwa ulitawala, dakika zilizidi kusonga mbele lakini ghafla, Aisha akashtuka kutoka kitandani, alikuwa akilia kwa maumivu makali ya tumbo yaliyomfanya kulalamika mno.
Harakaharaka Razak akainuka kutoka kitandani, akaifuata rimoti ya ya kiyoyozi na kuikizima. Bado Aisha alikuwa akilalamika kwa maumivu makali ya tumbo, Razak alishangaa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mpaka msichana huyo kulalamika kwa maumivu makali.
Kila alipouliza, hakupewa jibu zaidi ya msichana huyo kuendelea kulalamika zaidi. Razak akaogopa, akahisi kwamba kama asingefanya kitu cha ziada basi mpenzi wake angeweza kuwa kwenye hali mbaya zaidi.
“Inuka twende hospitali...” alisema Razak.
“Siwezi....naumia, tumbo linauma Razak mpenzi....nisaidie...” alisema Aisha kwa sauti ya chini iliyojaa maumivu makali.
Razak hakutaka kusubiri, alichokifanya ni kumbeba Aisha na kuanza kuelekea naye nje ya chumba kile huku lengo likiwa ni kuchukua gari na kuelekea hospitalini.
Walipofika nje, Aisha akazidi kulalamika kwa maumivu makali, baridi walilokutana nalo nje lilimtesa, akapiga kelele mpaka zikafika katika nyumba za jirani, harakaharaka Razak akaufungua mlango na kumuingiza msichana huyo ndani ya gari lake, akaelekea upande wa pili, akaufungua na kuingia ndani.
“Pole mpenzi....vumilia...” alisema Razak, akawasha gari na kuondoka mahali hapo.
Ndani ya gari, kelele zilikuwa nyingi, Razak alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani alitakiwa kufanya, alitamani kumfuata Aisha na kumbeleza lakini upande mwingine, alitamani kuliendesha gari kwa kasi kuwahi hospitalini.
Hakuchukua dakika nyingi, akawa amefika hospitali ambapo akafungua mlango huku akiwaita manesi ambao walifika na machela, wakampakiza na kuanza kuisukuma kuelekea ndani ya jengo la hospitali hiyo.
Walipofika katika chumba kilichoandikwa ‘Theatre’ akaambiwa kusubiri katika mabenchi yaliyokuwa nje, akatulia. Hapo, kichwa chake kilichanganyikiwa mno, hakujua ni kitu gani kilimsibu mpenzi wake, japokuwa ilikuwa ni usiku wa manane lakini hakuweza kupata usingizi kabisa.
Alikuwa mtu mwenye mawazo mengi, alitulia katika benchi lililokuwa nje ya kile chumba huku akionekana kuwa na mawazo mengi.
Hakuishia kukaa tu, wakati mwingine alisimama na kuanza kuzunguka huku na kule, hakika alichanganyikiwa na kilichomuumiza kichwa zaidi, Aisha alikuwa na tatizo gani?
“Tatizo nini?” alijiuliza pasipo kupata jibu lolote lile.
Watu aliowafikiria kwa kipindi hicho walikuwa wazazi wake, alitakiwa kuwapa taarifa na kuwaambia kilichokuwa kikiendelea hospitalini hapo. Muda ulikwenda sana lakini hakutaka kuacha kuwapigia ili hata kama lingetokea tatizo kubwa zaidi basi wawe na taarifa.
Akachukua simu yake na kuanza kuwapigia. Simu ikaanza kuita, iliita na kuita mpaka kukata pasipo kupokelewa. Hakujiuliza sana, alijua kwamba muda huo wangekuwa wamelala, alichokifanya ni kupiga tena simu.
“Haloo...” ilisikika sauti nzito ya baba yake, ilionyesha kabisa kama alitoka kuamka.
“Baba...Aisha amezidiwa, nimemleta hospitali...” alisema Razak kwa huzuni.
“Anaumwa nini?”
“Sijui chochote kile...”
“Mpo hospitali gani?”
“Hospitali ya Mediteranian..”
“Tunakuja...”
Simu ikakatwa na Razak kutulia kwenye benchi. Mawazo hayakumtoka na kila alipokaa, aliisikia sauti ikimwambia kwamba ni lazima mpenzi wake afariki dunia hapohapo kitandani kwani tatizo alilokuwa nalo lilikuwa kubwa mno.
Wasiwasi ukamshika lakini hakutaka kukata tamaa, kila wakati alimuomba Mungu atende muujiza na vipimo vitakavyopimwa basi ionekane hana tatizo lolote zaidi ya tumbo kuchafuka tu.
Dakika ziliendelea kukatika, baada ya dakika kadhaa, wazazi wake wakafika hospitalini hapo na moja kwa moja kuelekea kule alipokuwa. Walipomuona, walijua tu kwamba kulikuwa na tatizo, jinsi alivyoonekana, ilikuwa rahisi mno kugundua kwamba kijana wao alikuwa kwenye matatizo makubwa.
“Pole sana Razak,” alisema baba yake huku akimkumbatia, kumbatio lililomfanya kuanza kububujikwa na machozi kwa mara nyingine.
Wakakaa naye chini na kuanza kumuuliza maswali kadhaa ni tatizo gani alilokuwa nalo Aisha, hapo, akaanza kuwaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea kwamba alishtuka usiku wa manane huku akiugulia maumivu, baada ya hapo, akamchukua na kumpeleka hospitali.
“Kwa hiyo haijajulikana tatizo nini?” aliuliza mama yake.
“Bado, tangu waingie ndani, hawajatoka...” alijibu Razak.
“Ngoja tusubiri...”
Muda ulizidi kwenda, dakika zilikatika mpaka ilipofika saa kumi alfajiri, mlango ukafunguliwa na daktari mmoja wa kike mwenye koti kubwa jeupe lililokuwa na kibati kilichoandikwa Dk. Mimi kifuani kutoka ndani ya chumba hicho.
Hapohapo Razak akasimama na kuanza kumsogelea, alitaka kujua ni kitu gani kilikuwa kimeendelea lakini pia alitaka kufahamu ni tatizo gani alilokuwa nalo mpenzi wake.
“Nifuateni...”
Hawakuwa na jinsi, walichokifanya ni kuanza kumfuata Dk. Mimi ambaye alikwenda mpaka kwenye chumba kilichoonekana kuwa ofisi yake na kukaa kwenye kiti kilichokuwa nyuma ya nyumba huku akiwataka wageni wake kukaa vitini.
Kabla hajazungumza lolote, akachukua baadhi ya mafaili yaliyokuwa mezani kwake, akaandika, akashusha miwani kidogo na kuwaangalia kwa zamu huku akionekana kabisa kutaka kuzungumza kitu.
“Kwanza poleni kwa matatizo mnaliyokutana nayo....” alianza kusema Dk. Mimi.
“Asante sana, nini kinaendelea? Anaumwa nini? Atapona?” aliuliza Razak maswali matatu mfululizo.
“Tumemchunguza kwa kipindi kirefu na tumemkuta ana tatizo ambalo nashangaa ilikuwaje mpaka mkasubiri kwa kipindi kirefu mpaka tatizo kuwa sugu namna hii,” alisema Dk. Mimi.
“Tatizo gani?”
“Kwanza mpo na mgonjwa kwa kipindi gani?”
“Kama miezi miaka miwili..” alidanganya Razak.
“Katika kipindi chote hamkugundua kwamba ana tatizo lolote?”
“Hapana! Kwani kuna nini dokta?”
“Na mlikuwa mnacheki afya yake mara kwa mara?”
“Hapana!”
“Tumekuta binti yenu ana tatizo kubwa sana, lilianza kidogokidogo, likawa linakua, likakua na kukua na mwisho wa siku kuwa kubwa kabisa ambalo haliwezi kabisa kutibika,” alisema Dk. Mimi, taarifa hiyo ilimshtua kila mmoja.
“Tatizo gani?”
“Ana kansa ta utumbo mpana ambayo kitaalamu inaitwa Colon Cancer,” alijibu daktari huyo.
“Unasemaje?”
“Ndiyo hivyo! Ni tatizo kubwa sana ambalo linaua maelfu ya watu kila mwezi hapa duniani. Huwa linaanza taratibu sana, unapolipuuzia, linakua na kukua, kosa kubwa lililofanyika ni kwamba hakuangaliwa afya yake kipindi cha nyuma, ila kitu kinachosikitisha zaidi.....” alisema Dk. Mimi, hata kabla hajamalizia sentensi yake, akabaki kimya.
“Kitu gani?” aliuliza baba yake Razak, wakati huo, kijana wake alikuwa akilia tu.
“Au basi, mengine tutaongea siku nyingine...” aliseema Dk. Mimi.
“Hapana! Haiwezekani, haiwezekani utuache hewani, tuambie hicho kingine ni nini,” alisema mama yake Razak, alionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
“Tutaongea siku nyingine...” alisisitiza Dk. Mimi.
“Dokta, umetuambia kwamba Aisha ana kansa mbaya, tumekubaliana nawe, unajua ni jinsi gani tulivyoumia, naomba usituache njia panda, tuambie hilo lingine ni lipi,” alisema mama yake Razak.
“She has Terminal Cancer,” (Ana kansa isiyopona) alijibu daktari kwa sauti ya chini, hata yeye mwenyewe, alionekana kuumia sana.
“What is that?” (Ndiyo nini hiyo?)
“Hatoweza kupona, hiyo ni kansa inayoua, imesambaa sana, hatoweza kupona, ni lazima atakufa, ni ndani ya miezi mitatu tu,” alijibu daktari huku akiwaangalia wote wawili.
Hakukuwa na siku ambayo Razak alilia kama siku hiyo, ilionekana kama kuna msiba ndani ya ofisi ya daktari, alilia kwa sauti pasipo kuona kama pale palikuwa hospitali au la.
Moyo wake uliumia, hakuamini kile alichokisema daktari kwamba msichana Aisha asingeweza kupona, yaani ile kansa ilikuwa ni lazima imuue. Alitamani kuona kile alichokisikia kiwe ndoto, yaani ghafla ashtuke kutoka katika usingizini, Aisha awe pembeni yake na amwambie kwamba kila kitu alichokiota, kilikuwa ndoto tu.
Hiyo haikuwa ndoto, alijaribu kuziuma lipsi zake ili kuona kama angeshtuka kutoka usingizini lakini wapi, bado kila kitu kilichokuwa kikiendelea kilikuwa kitu halisi na hakikuwa ndoto kama alivyokuwa akihisi.
Watu wote waliokuwa ndani ya chumba kile wakaanza kumbembeleza Razak lakini hakunyamaza, alimpenda Aisha kupita maelezo, alikuwa radhi kupoteza kitu chochote katika maisha yake lakini si kumpoteza Aisha ambaye alionekana kuwa kila kitu kwake.
Kulia sana, kumbembelezwa sana hakukuweza kubadilisha matokea, ukweli ukaendelea kuwa palepale kwamba mpenzi wake alikuwa mgonjwa wa kansa ya utumbo mpana na kamwe asingeweza kupona, ilikuwa ni lazima afariki dunia.
“Siwezi kukaa....ninataka kumuona mpenzi wangu, ninataka kumuona Aishaaaaa...”
alisema Razak huku akionekana kama kuchanganyikiwa, hakutaka kubaki mahali hapo, hapohapo akasimama na kutoka nje, akaanza kukimbia kule kulipokuwa chumba alichoingizwa Aisha....wazazi wake na Dk. Mimi wakaanza kumfuata kwa mwendo wa kasi, walijua ni kwa jinsi gani Razak alikuwa amechanganyikiwa.
Je nini kitaendelea....
Tangia lini na wewe umekuwa humu?Mh! Penzi lisilo na mwisho huwa ni penzi TAMU. Raha mtindo mmoja karaha ni kidogo sana.
Tangia lini na wewe umekuwa humu?
mzima kabisa asante ila tumetupanaHuwa napita mara moja moja. Mzima weye? Wasalimie uwapendao. Mie niko bomba kabisa namshukuru Mwenyezi Mungu.
mzima kabisa asante ila tumetupana