Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,170
Mtunzi Nyemo Chilongani SEHEMU YA 01
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2005, mwaka ambao nilimaliza kuchukua Diploma yangu ya Uandishi wa habari katika Chuo cha Uandishi cha DSJ (Dar es Salaam School of Journalism) kilichokuwa Mtaa wa Bungoni, Buguruni jijini Dar es Salaam.
Katika kipindi hicho nilikuwa na furaha sana kwa sababu ndoto zangu ambazo nilijiwekea katika maisha yangu niliziona kuanza kutimia katika muda mchache ujao.
Katika kipindi chote ambacho nilikuwa katika chuo hicho nikipata elimu yangu, kichwani mwangu kulikuwa na ndoto nyingi, ndoto za kuwa mwandishi mkubwa ambaye ningekuja kuheshimika na jamii yote, mwandishi ambaye ningeweza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta zote za uandishi nchini Tanzania.
Kila nilipokuwa nikimwangalia mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Charles Hilary, nikajiona nikizidi kupata nguvu zaidi za kusoma kwa sana, nilitamani sana kuwa kama yeye katika maisha yangu.
Nilikuwa na kiu sana ya kuwa mwandishi bora na kisha kutafuta nafasi ya kutangaza katika shirika lolote kubwa la Habari kama la BBC, CNN, Al Jazeera au shirika lolote ambalo lilikuwa likitambulika kimataifa.
Hapo ndipo ambapo nilipofikiria kitu kimoja ambacho nilitakiwa kufanya, kitu ambacho kingekuwa cha hatari sana katika maisha yangu.
Nakumbuka siku hiyo mara baada ya kutoka katika ‘field’ yangu niliyoifanyia katika kituo cha utangazaji cha Global TV, nikarudi nyumbani na kutulia chumbani kwangu.
Siku hiyo sikuonekana kuwa na furaha kabisa, kichwa changu kilikuwa kikifikiria ni kwa namna gani ningeweza kuwaambia wazazi wangu kuhusu kile nilichokuwa nikikifikiria kichwani mwangu.
Kiukweli nilihitaji sana ushirikiano kutoka kwa wazazi wangu, wao ndiyo walikuwa watu sahihi ambao kamwe wasingeweza kunishauri kitu kibaya.
Nilitulia chumbani kwangu kitandani, hakukuwa na siku ambayo niliwaona wazazi wangu wakichelewa kurudi nyumbani kama siku hiyo.
Muda wote macho yangu yalikuwa yakiangalia saa yangu ya mkononi, nilitamani sana waingie nyumbani hapo na kuwaambia kile nichokuwa nimepanga kuwaambia.
Nakumbuka ilikuwa mwaka 2005, mwaka ambao nilimaliza kuchukua Diploma yangu ya Uandishi wa habari katika Chuo cha Uandishi cha DSJ (Dar es Salaam School of Journalism) kilichokuwa Mtaa wa Bungoni, Buguruni jijini Dar es Salaam.
Katika kipindi hicho nilikuwa na furaha sana kwa sababu ndoto zangu ambazo nilijiwekea katika maisha yangu niliziona kuanza kutimia katika muda mchache ujao.
Katika kipindi chote ambacho nilikuwa katika chuo hicho nikipata elimu yangu, kichwani mwangu kulikuwa na ndoto nyingi, ndoto za kuwa mwandishi mkubwa ambaye ningekuja kuheshimika na jamii yote, mwandishi ambaye ningeweza kuleta mabadiliko makubwa katika sekta zote za uandishi nchini Tanzania.
Kila nilipokuwa nikimwangalia mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Charles Hilary, nikajiona nikizidi kupata nguvu zaidi za kusoma kwa sana, nilitamani sana kuwa kama yeye katika maisha yangu.
Nilikuwa na kiu sana ya kuwa mwandishi bora na kisha kutafuta nafasi ya kutangaza katika shirika lolote kubwa la Habari kama la BBC, CNN, Al Jazeera au shirika lolote ambalo lilikuwa likitambulika kimataifa.
Hapo ndipo ambapo nilipofikiria kitu kimoja ambacho nilitakiwa kufanya, kitu ambacho kingekuwa cha hatari sana katika maisha yangu.
Nakumbuka siku hiyo mara baada ya kutoka katika ‘field’ yangu niliyoifanyia katika kituo cha utangazaji cha Global TV, nikarudi nyumbani na kutulia chumbani kwangu.
Siku hiyo sikuonekana kuwa na furaha kabisa, kichwa changu kilikuwa kikifikiria ni kwa namna gani ningeweza kuwaambia wazazi wangu kuhusu kile nilichokuwa nikikifikiria kichwani mwangu.
Kiukweli nilihitaji sana ushirikiano kutoka kwa wazazi wangu, wao ndiyo walikuwa watu sahihi ambao kamwe wasingeweza kunishauri kitu kibaya.
Nilitulia chumbani kwangu kitandani, hakukuwa na siku ambayo niliwaona wazazi wangu wakichelewa kurudi nyumbani kama siku hiyo.
Muda wote macho yangu yalikuwa yakiangalia saa yangu ya mkononi, nilitamani sana waingie nyumbani hapo na kuwaambia kile nichokuwa nimepanga kuwaambia.