Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #441
*MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN -- 19*
*Simulizi za series*
Phares alipotelea ndani akimuacha Rhoda anamtazama. Mwanamke huyo alipoteza kama dakika tatu kufikiria, akiwa amesimama.
Alitoka zake ndani kwenda kumtafuta kibaraka wake, kuna mambo alitaka ayaweke sawa. Baada ya punde alimpata, wakasogea kando pasipo na watu.
“Nimeshaongea naye,” alisema Rhoda. “Ila bado sijapata kujua msimamo wake haswa kwenye hili jambo.”
“Kwahiyo tunafanyaje?” akauliza kibaraka. Mwanaume mlinzi mwenye mwili wa mapambano.
“Inabidi tuendelee kumtia hamasa,” alisisitiza Rhoda. “Kama tukimuacha, anaweza akapoteza hili jambo akilini mwake.”
“Sawa.”
“Jitahidi. Nadhani hujasahau kama kuna pongezi kubwa ndani ya hili.” Kibaraka alitikisa kichwa chake kuridhia. Rhoda aliaga akiahidi wataonana kesho, ila kuna jambo mwanaume akalikumbuka.
Alimuita Rhoda akamwambia kwa sura yenye ukakamavu. “Keshokutwa kuna wito wa baraza.”
Rhoda akapigwa na bumbuwazi. “Kweli?”
“Ndio.”
“Umepata wapi hizo taarifa? Mbona Phares hajaniambia.”
“Nakaa, nakula na kulala humu kasrini. Natambua kila korido.”
Rhoda aliinamisha chini kichwa chake akitafakari. Hili jambo lilikuwa ni nyeti na muhimu.
Inampasa ahakikishe kwamba Phares anabakia madarakani, la sivyo, haja zake zote zitakuwa zimekoma. Na kama kuna sehemu ya kuhakikisha hilo, basi ni barazani.
Ila hana nafasi yoyote kwenye baraza. Ni kwa namna gani mawazo na mapendekezo yake yakatasikilizwa na kutiliwa maanani? Anapata mashaka.
“Namjua mzee mmoja tu wa baraza, anaishi nyumba ya tatu mashariki ya kasri hili. Unawafahamu hao wengine?”
“Ndio, nawafahamu. Hawana muda mrefu barazani.”
“Kivipi naweza kuwajua?”
“Kwa kumtumia huyo unayemjua. Ana ushawishi mkubwa barazani kwa uzoefu wake.”
Macho ya Rhoda yalisadifu akili yake inayotatua mawazo. Aling’ata lips kisha akaliza vidole vyake.
“Tuonane kesho.” Aliondoka upesi akishikilia gauni lake lisimkinge kutembea. Alikwea mgongo wa farasi wake mweupe aliyekuja naye, akapotea eneo hilo la utawala.
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
.
.
“Tokea amenikabidhi sijaona chochote. Ndege hasogei na hakuna linalotukia. Nashindwa kuelewa.” yalikuwa maneno ya Sultan aliyekuwa amejilaza kwenye kitanda kikubwa, pembeni yake akiwa na mwanamke mwembamba mrembo, mke wake wa tatu.
Yalikuwa ni majira ya jioni, hali ya baridi ikipuliza kwa mujibu wa vipindi vya msimu. Sultan pamoja na mkewe walikuwa wamejifunika shuka zito la manyoya lililokuwa linajitahidi kwa kiasi kikubwa kupambana kuwapa joto.
Mandhari yalikuwa yanavutia, vitu vikiundwa na madini ya silva ama vumbi la dhahabu. Chumba kilikuwa kinameta. Nadhani si vema kujadili gharama ya samani hizo kwakuwa zaweza kutupa mishtuko ya moyo.
Mwanamke huyu, mke wa tatu wa Sultan, alikuwa mrembo haswa. Japokuwa hakuwa ametia kiungo chochote usoni mwake, bado alikuwa anavutia. Macho yake kama ya mtu aliyetoka usingizini. Mdomo wake, mdogo mwekundu, ni kana kwamba anabusu muda wote. Nywele zake ndefu nyeusi ya bendera zilikuwa zinamsumbua kiuno.
Macho yasikulaghai, mwanamke ni ndani. Hata kama awe ameumbwa siku Mungu hana msongo wa mawazo, kama ndani ni shetani, uzuri wake unakuwa vumbi peponi.
Mwanamke huyu anamtazama Sultan, kisha anapeleka vidole vyake vilaini kumchezea chezea mwanaume huyo ndevu.
“Pole sana mpenzi wangu,” anasema kwa sauti ya puani. “Sasa umepanga kufanya nini?” aliuliza kiudadisi. Sultan alisafisha koo lake na kutulia kwanza kwa sekunde sita kabla ya kufungua lips zake kavu kusema:
“Nitamfunda adabu, naona ananichezea. Kesho nitatuma jeshi langu likamtie nguvuni. Nitachoma dhana zake zote na kumtia ndani ajifunze.”
Mke akatabasamu kwa mbali. “Sasa kama ukimkamata na kumfunga, utapataje hicho kitu unachokitafuta?” Aliuliza kwa sauti ya upole iliyobembeleza masikio ya Sultan, ila swali hilo lilikuwa gumu, Sultan hakuwa na jibu.
“Sijui nafanyaje. Naelekea kukata tamaa sasa.”
Mwanya huu ulikuwa adhimu kwa mke huyu wa tatu. Alishusha mikono yake mpaka kwenye kifua cha Sultan, akawa anachezea nywele za mwanaume huyo akimtazama kana kwamba chakula kitamu kinachomtesa kwa harufu.
“Mpenzi, huna haja ya kukata tamaa,” alinong’oneza na kuendelea: “Ulifanya makosa kutonishirikisha. Laiti kama ningelikuwa nalijua, ungelishapata kito chako hicho cha thamani.”
Sultan hakuwa amemueleza mke huyu kama anachotafuta ni mkufu, bali kito fulani cha thamani. Baada ya hiyo kauli alimtazama mwanamke huyu kwa macho ya kuguswa, akauliza:
“Ungelifanyaje?” Mwanamke akatabasamu.
“Ningelitimiza wajibu wangu kama mkeo, kwa kukushauri namna ya kupata mwarobaini wa tatizo.”
Sultan alikaa kimya, asitie neno. Kwa muda kidogo kulikuwa kimya, ila mke akiendelea kukanda kifua cha mumewe katika namna lainishi.
“Najua hupendi nikimuongelea mke wako wa kwanza, ila jua ya kwamba Karim ana kiburi cha udugu nawe. Anajua hata asipofanya yanayokupendeza, damu ya mkeo itamlinda. Kama mke wako angelitumia ushawishi wake kwa nduguye, haya yangekuwa historia.”
Bado kulikuwa kimya kwa Sultan.
“Hakuna mtu yeyote mwenye uwezo kumzidi Karim maili za mbali sana pande zote za dunia toka kwenye kasri yako. Haingii akilini kuniambia ameshindwa.”
Hapo Sultan akaguna kuashiria kukubali. “Inahitaji theluthi tu ya uwezo wa Karim kupata hicho kito,” aliendelea kusema Mke huyu wa tatu.
“Auhitaji jeshi, wala vita. Naomba unipe nafasi hiyo nami nijaribu kukusaidia. Pengine naweza leta matokeo chanya.” Sultan alinyamaza kwa dakika kama moja. Alikuwa anatafakari. Alitazama dari kana kwamba anaona ramani. Alishusha pumzi ndefu, akamtazama mkewe kwa macho yaliyojawa uchovu.
“Nisingependa kukubebesha shida zangu ...”
“Hapana!” mke akadakia upesi. “Ni faraja kwangu kumhudumia na kumsaidia mtu ninayempenda.”
Ni kama vile mawazo yalimtinda zaidi Sultan. Aliwaza, ila mwishowe akaamua.
“Sawa, unaweza ukanisaidia.” Mke alimbusu shavuni na kumshukuru. Baada ya lisaa limoja, Sultan alijiandaa na kuondoka akirejea kasrini. Alipoyoyoma, mke huyu naye alijiandaa upesi, akiwa ameongozana na walinzi wake wanne, alikwea farasi wake na kuanza safari ya kuelekea kaskazini ya mbali na makazi yake.
Alikuwa amevalia gauni refu zito, jeupe kwa rangi. Kola yake ilikuwa na mawe madogo madogo mengi yenye rangi ya dhahabu. Juu ya gauni hilo alivalia koti kubwa lenye manyoya mengi ya mnyama. Nywele zake ndefu alikuwa amezibana. Uso wake usiwe na kikolombwezo chochote, ila alipendeza. Miguu yake mirefu ilikuwa imefunikwa na viatu imara vya ngozi.
Safari yake ilidumu kwa masaa manne, alifika ikiwa ni usiku. Mbele ya nyumba ndogo yenye chumba kimoja na sebule, ila ikiwa imefumwa kwa ustadi. Mlango wake ulikuwa mkubwa, madirisha madogo. Bomba kubwa refu la kutoa moshi lilikuwa linatazama angani.
Mke huyo wa tatu wa Sultan aliwaamuru walinzi wake wangojee hapo nje wakati yeye akienenda ndani. Walinzi wakatii. Aliugonga mlango mara tatu akiita bibi. Punde mlango ukafunguliwa na mzee wa makamo ya umri wa miaka hamsini na ushee.
Nywele zake zilikuwa nyeusi, mvi za kutafuta. Alikuwa amejitanda shuka kubwa lililofunika mwili wake wote kuanzia shingoni mpaka miguuni. Uso wake ulifanana na wa mgeni wake. Japo alikuwa mzee, hakuwa haba kwenye kujitunza.
Alijikuta anatabasamu punde tu alipomwona mgeni. Alimkumbatia na kumkaribisha ndani kwa furaha.
“Umenikumbuka mjukuu wangu, mbona muda huu?”
“Nina shida, bibi,” alisema mke wa tatu wa Sultan. “Nimeshindwa kuvumilia mpaka usiku ukome.”
“Shida gani hiyo? Ni kuhusu Sultan?”
“Ndio.”
“Umefanya nini tena? Sina nguvu ya kukimbizana barabarani kwenda kuwasuluhisha, mjukuu wangu.”
“Sio hivyo, bibi. Kuna kitu nataka unisaidie. Ni muhimu sana. Lina uzito sawa na lile ulilowahi fanya miaka miwili nyuma.”
Kabla ya miaka hiyo miwili nyuma, mke huyu wa Sultan hakuwa kitu mbele ya jamii. Hakuna aliyekuwa anamjua wala kumheshimu zaidi tu ya kutamaniwa na wanaume mbalimbali, aliowaona wa hovyo.
Siku moja Sultan akiwa anakatiza maeneo ya karibu na bibi huyo aliyekuwa anaishi na mke huyu wa tatu wa Sultan, ndipo maisha yalipobadilika. Bibi huyu akiwa anafahamu fika mjukuu wake ni mrembo, na Sultan angevutiwa naye, basi anaamua kutumia ulozi.
Anasema maneno kadhaa akiwa ameshikilia pindo la gauni lake chakavu, basi Sultan anakatiza kando kando ya kisima alipokuwapo mjukuu wake akifua nguo. Na kutokana na joto la kipindi hicho, binti huyo alikuwa amevalia nguo nyepesi iliyoonyesha umbo lake zuri.
Sultan alisimamisha msafara wake akaagiza aitiwe mwanamke huyo aliyemuuliza maswali kadhaa kisha akaondoka. Baada ya siku moja, vibaraka wa Sultan walitumwa kwenda kumtwaa mwanamke huyo na hayo mengine yote yakawa historia. “Mjukuu wangu, unanitisha,” alisema bibi. Mjukuuye akamshika mkono.
“Si kikubwa, bibi. Kuna kitu Sultan anakitaka. Kinamnyima furaha na amani kabisa. Endapo nikimsaidia kupata kitu hicho, ni wazi nitakuwa nimeteka nafasi kubwa ya moyo wake. Mtoto wangu anaweza akarithi kiti cha utawala.”
Bibi aliukunja uso wake.
“Kitu gani hicho?”
“Ni kito fulani cha thamani. Je bibi una namna yoyote ambayo inaweza ikasaidia kukipata na huku kipo mbali na himaya yetu?”
“Inawezekana, ila kuna baadhi ya mambo inabidi kwanza yawekwe sawa.”
“Yapi hayo?”
“Punguza hamu, mjukuu wangu. Bila shaka leo unalala huku. Pumzika, tutayajenga.”
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Baada ya kufuatilia kwa takribani siku nzima pasipo mafanikio, ikiwa ni usiku sasa, vikongwe watatu wa Tanashe wanafika kwenye mpaka wa mashariki wa himaya yao. Walidumu hapo kwa muda mchache kabla hawajagundua nyayo za binadamu.
Nyayo hizo zilikuwa ni za mguu wa kike. Walizitazama wasichukue muda mrefu kuugundua ukweli mchungu, nyayo zile zilikuwa za mtu wanayemtafuta, si mwingine bali Malkia. Hakuna mwenye nyayo kama zile Tanashe nzima.
“Ameshaondoka, imewezakanaje?” aliuliza kikongwe mmoja. Nyuso zao zilijawa na huzuni.
“Sijui ni nini kilitokea. Siju ni nini kimempa uhai?” Kulikuwa kimya kwa muda kidogo kabla mmoja hajauliza:
“Itakuwa tulifanya makosa kumlaza na mkufuwe. Hakuna kingine kilichompa uhai zaidi ya mkufu ule. Ule ni mkufu wake na hatukufanikiwa kuchukua kibali hicho kwasababu ya Faki.”
Kukawa kimya tena kidogo. Upepo ulikuwa unapuliza, giza lilikuwa limetanda.
“Kwanini hatukumuona upesi kwenye rada zetu na ilhali alikuwa ndani ya Tanashe? Au atakuwa alitoka nje ya himaya hii tukiwa kwenye mapambano?”
“Yote yanawezekana. Kama bado alikuwa ndani ya Tanashe wakati tunamsaka, basi itatuwia vigumu sana kumrudisha mikononi mwetu. Maana itakuwa inamaanisha hatuna uwezo wa kumuona tena. Sijui uwezo huo ameutoa wapi?”
Akadakia mwingine:
“Na Sijui atakuwa ameelekea wapi? Kufanya nini?”
Walitamani sana kufahamu lakini haikuwezekana. Hawakujua kwa wakati huo Malkia alikuwa juu ya farasi aliyemkwapua hatua chache baada ya kutoka Tanashe akielekea himaya ya masonara.
Mwanamke huyo kifuani alikuwa amebebelea mkufu. Ngozi yake ilikuwa laini inayong’ara. Uso wake ulikuwa na uhai. Nywele zake zilikuwa ndefu, nyeusi. Alikuwa ni yule Malkia! Malkia wa Goshen tuliyekuwa tunamfahamu, mzuri atakayekufanya uache shughuli zako kumtazama.
Alikuwa amedumu kwenye safari hii kwa masaa kadhaa, na sasa alikuwa anaingia msituni kabla hajaumaliza na kudaka jangwa. Alipomaliza msitu huo mpana wenye miti na mandhari ya kuogofya, alimuacha farasi hapo atumie miguu yake kusema na jangwa.
Hakugeuza shingo nyuma kutazama alipotoka. Hakuwa na dalili hata ndogo za kuogopa. Baridi kali lililokuwa linampiga lilimfanya ajikunyate, lakini si kusitisha safari yake. Alizamisha miguu yake ndani ya mchanga na kuichomoa. Hakuchoka.
Safari yake inakuja kukoma katikati ya usiku. Alisimama kana kwamba aliona jambo. Alichota mchanga akaujaza kiganjani mwake kisha akaumwagia mbele yake kama hatua moja, mara shimo kubwa likatokea hapo. Lilikuwa ni lile lililommeza Zura.
Malkia alirusha macho yake ndani ya shimo hilo, hakuona kitu. Kulikuwa ni totoro haswa. Alisimama hapo kama anayechambua kiza anachokiona. Mara akajirusha kuzama humo ndani!
Kishindo kiliashiria amefika chini. Alikuwa haonekani kabisa. Hakukuwa na mwanga wowote ule. Punde baada ya kishindo hicho, sauti ya farasi inasikika. Sauti hii haikomi baada ya mara moja, inaendelea zaidi na zaidi. Inakuwa kelele sasa.
Malkia anasogea taratibu, vishindo vyake vya miguu vinasema. Haichukui muda mrefu, kidani chake cha mkufu kinawaka, sasa anaona anapopakanyaga, anaona pia anapoelekea. Ila mbele bado ni kiza. Haoni komo la shimo.
Anatembea kama hatua nane akiangaza, mara anasikia vishindo vya watu vikikatiza upesi, anasimama! Anaminya kidani cha mkufu wake na mara kunakuwa giza totoro. Alitembea hatua mbili, akaachia kidani hicho, mara mwanga ukachipuka haraka. Uso kwa uso Malkia akaona kundi la watu wa ajabu mbele yake!
Tabasamu linamtoka usoni.
.
.
.
.
.
.
.
****
.
.
LAKO JICHO!
.
.
.
.
*Simulizi za series*
Phares alipotelea ndani akimuacha Rhoda anamtazama. Mwanamke huyo alipoteza kama dakika tatu kufikiria, akiwa amesimama.
Alitoka zake ndani kwenda kumtafuta kibaraka wake, kuna mambo alitaka ayaweke sawa. Baada ya punde alimpata, wakasogea kando pasipo na watu.
“Nimeshaongea naye,” alisema Rhoda. “Ila bado sijapata kujua msimamo wake haswa kwenye hili jambo.”
“Kwahiyo tunafanyaje?” akauliza kibaraka. Mwanaume mlinzi mwenye mwili wa mapambano.
“Inabidi tuendelee kumtia hamasa,” alisisitiza Rhoda. “Kama tukimuacha, anaweza akapoteza hili jambo akilini mwake.”
“Sawa.”
“Jitahidi. Nadhani hujasahau kama kuna pongezi kubwa ndani ya hili.” Kibaraka alitikisa kichwa chake kuridhia. Rhoda aliaga akiahidi wataonana kesho, ila kuna jambo mwanaume akalikumbuka.
Alimuita Rhoda akamwambia kwa sura yenye ukakamavu. “Keshokutwa kuna wito wa baraza.”
Rhoda akapigwa na bumbuwazi. “Kweli?”
“Ndio.”
“Umepata wapi hizo taarifa? Mbona Phares hajaniambia.”
“Nakaa, nakula na kulala humu kasrini. Natambua kila korido.”
Rhoda aliinamisha chini kichwa chake akitafakari. Hili jambo lilikuwa ni nyeti na muhimu.
Inampasa ahakikishe kwamba Phares anabakia madarakani, la sivyo, haja zake zote zitakuwa zimekoma. Na kama kuna sehemu ya kuhakikisha hilo, basi ni barazani.
Ila hana nafasi yoyote kwenye baraza. Ni kwa namna gani mawazo na mapendekezo yake yakatasikilizwa na kutiliwa maanani? Anapata mashaka.
“Namjua mzee mmoja tu wa baraza, anaishi nyumba ya tatu mashariki ya kasri hili. Unawafahamu hao wengine?”
“Ndio, nawafahamu. Hawana muda mrefu barazani.”
“Kivipi naweza kuwajua?”
“Kwa kumtumia huyo unayemjua. Ana ushawishi mkubwa barazani kwa uzoefu wake.”
Macho ya Rhoda yalisadifu akili yake inayotatua mawazo. Aling’ata lips kisha akaliza vidole vyake.
“Tuonane kesho.” Aliondoka upesi akishikilia gauni lake lisimkinge kutembea. Alikwea mgongo wa farasi wake mweupe aliyekuja naye, akapotea eneo hilo la utawala.
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
.
.
“Tokea amenikabidhi sijaona chochote. Ndege hasogei na hakuna linalotukia. Nashindwa kuelewa.” yalikuwa maneno ya Sultan aliyekuwa amejilaza kwenye kitanda kikubwa, pembeni yake akiwa na mwanamke mwembamba mrembo, mke wake wa tatu.
Yalikuwa ni majira ya jioni, hali ya baridi ikipuliza kwa mujibu wa vipindi vya msimu. Sultan pamoja na mkewe walikuwa wamejifunika shuka zito la manyoya lililokuwa linajitahidi kwa kiasi kikubwa kupambana kuwapa joto.
Mandhari yalikuwa yanavutia, vitu vikiundwa na madini ya silva ama vumbi la dhahabu. Chumba kilikuwa kinameta. Nadhani si vema kujadili gharama ya samani hizo kwakuwa zaweza kutupa mishtuko ya moyo.
Mwanamke huyu, mke wa tatu wa Sultan, alikuwa mrembo haswa. Japokuwa hakuwa ametia kiungo chochote usoni mwake, bado alikuwa anavutia. Macho yake kama ya mtu aliyetoka usingizini. Mdomo wake, mdogo mwekundu, ni kana kwamba anabusu muda wote. Nywele zake ndefu nyeusi ya bendera zilikuwa zinamsumbua kiuno.
Macho yasikulaghai, mwanamke ni ndani. Hata kama awe ameumbwa siku Mungu hana msongo wa mawazo, kama ndani ni shetani, uzuri wake unakuwa vumbi peponi.
Mwanamke huyu anamtazama Sultan, kisha anapeleka vidole vyake vilaini kumchezea chezea mwanaume huyo ndevu.
“Pole sana mpenzi wangu,” anasema kwa sauti ya puani. “Sasa umepanga kufanya nini?” aliuliza kiudadisi. Sultan alisafisha koo lake na kutulia kwanza kwa sekunde sita kabla ya kufungua lips zake kavu kusema:
“Nitamfunda adabu, naona ananichezea. Kesho nitatuma jeshi langu likamtie nguvuni. Nitachoma dhana zake zote na kumtia ndani ajifunze.”
Mke akatabasamu kwa mbali. “Sasa kama ukimkamata na kumfunga, utapataje hicho kitu unachokitafuta?” Aliuliza kwa sauti ya upole iliyobembeleza masikio ya Sultan, ila swali hilo lilikuwa gumu, Sultan hakuwa na jibu.
“Sijui nafanyaje. Naelekea kukata tamaa sasa.”
Mwanya huu ulikuwa adhimu kwa mke huyu wa tatu. Alishusha mikono yake mpaka kwenye kifua cha Sultan, akawa anachezea nywele za mwanaume huyo akimtazama kana kwamba chakula kitamu kinachomtesa kwa harufu.
“Mpenzi, huna haja ya kukata tamaa,” alinong’oneza na kuendelea: “Ulifanya makosa kutonishirikisha. Laiti kama ningelikuwa nalijua, ungelishapata kito chako hicho cha thamani.”
Sultan hakuwa amemueleza mke huyu kama anachotafuta ni mkufu, bali kito fulani cha thamani. Baada ya hiyo kauli alimtazama mwanamke huyu kwa macho ya kuguswa, akauliza:
“Ungelifanyaje?” Mwanamke akatabasamu.
“Ningelitimiza wajibu wangu kama mkeo, kwa kukushauri namna ya kupata mwarobaini wa tatizo.”
Sultan alikaa kimya, asitie neno. Kwa muda kidogo kulikuwa kimya, ila mke akiendelea kukanda kifua cha mumewe katika namna lainishi.
“Najua hupendi nikimuongelea mke wako wa kwanza, ila jua ya kwamba Karim ana kiburi cha udugu nawe. Anajua hata asipofanya yanayokupendeza, damu ya mkeo itamlinda. Kama mke wako angelitumia ushawishi wake kwa nduguye, haya yangekuwa historia.”
Bado kulikuwa kimya kwa Sultan.
“Hakuna mtu yeyote mwenye uwezo kumzidi Karim maili za mbali sana pande zote za dunia toka kwenye kasri yako. Haingii akilini kuniambia ameshindwa.”
Hapo Sultan akaguna kuashiria kukubali. “Inahitaji theluthi tu ya uwezo wa Karim kupata hicho kito,” aliendelea kusema Mke huyu wa tatu.
“Auhitaji jeshi, wala vita. Naomba unipe nafasi hiyo nami nijaribu kukusaidia. Pengine naweza leta matokeo chanya.” Sultan alinyamaza kwa dakika kama moja. Alikuwa anatafakari. Alitazama dari kana kwamba anaona ramani. Alishusha pumzi ndefu, akamtazama mkewe kwa macho yaliyojawa uchovu.
“Nisingependa kukubebesha shida zangu ...”
“Hapana!” mke akadakia upesi. “Ni faraja kwangu kumhudumia na kumsaidia mtu ninayempenda.”
Ni kama vile mawazo yalimtinda zaidi Sultan. Aliwaza, ila mwishowe akaamua.
“Sawa, unaweza ukanisaidia.” Mke alimbusu shavuni na kumshukuru. Baada ya lisaa limoja, Sultan alijiandaa na kuondoka akirejea kasrini. Alipoyoyoma, mke huyu naye alijiandaa upesi, akiwa ameongozana na walinzi wake wanne, alikwea farasi wake na kuanza safari ya kuelekea kaskazini ya mbali na makazi yake.
Alikuwa amevalia gauni refu zito, jeupe kwa rangi. Kola yake ilikuwa na mawe madogo madogo mengi yenye rangi ya dhahabu. Juu ya gauni hilo alivalia koti kubwa lenye manyoya mengi ya mnyama. Nywele zake ndefu alikuwa amezibana. Uso wake usiwe na kikolombwezo chochote, ila alipendeza. Miguu yake mirefu ilikuwa imefunikwa na viatu imara vya ngozi.
Safari yake ilidumu kwa masaa manne, alifika ikiwa ni usiku. Mbele ya nyumba ndogo yenye chumba kimoja na sebule, ila ikiwa imefumwa kwa ustadi. Mlango wake ulikuwa mkubwa, madirisha madogo. Bomba kubwa refu la kutoa moshi lilikuwa linatazama angani.
Mke huyo wa tatu wa Sultan aliwaamuru walinzi wake wangojee hapo nje wakati yeye akienenda ndani. Walinzi wakatii. Aliugonga mlango mara tatu akiita bibi. Punde mlango ukafunguliwa na mzee wa makamo ya umri wa miaka hamsini na ushee.
Nywele zake zilikuwa nyeusi, mvi za kutafuta. Alikuwa amejitanda shuka kubwa lililofunika mwili wake wote kuanzia shingoni mpaka miguuni. Uso wake ulifanana na wa mgeni wake. Japo alikuwa mzee, hakuwa haba kwenye kujitunza.
Alijikuta anatabasamu punde tu alipomwona mgeni. Alimkumbatia na kumkaribisha ndani kwa furaha.
“Umenikumbuka mjukuu wangu, mbona muda huu?”
“Nina shida, bibi,” alisema mke wa tatu wa Sultan. “Nimeshindwa kuvumilia mpaka usiku ukome.”
“Shida gani hiyo? Ni kuhusu Sultan?”
“Ndio.”
“Umefanya nini tena? Sina nguvu ya kukimbizana barabarani kwenda kuwasuluhisha, mjukuu wangu.”
“Sio hivyo, bibi. Kuna kitu nataka unisaidie. Ni muhimu sana. Lina uzito sawa na lile ulilowahi fanya miaka miwili nyuma.”
Kabla ya miaka hiyo miwili nyuma, mke huyu wa Sultan hakuwa kitu mbele ya jamii. Hakuna aliyekuwa anamjua wala kumheshimu zaidi tu ya kutamaniwa na wanaume mbalimbali, aliowaona wa hovyo.
Siku moja Sultan akiwa anakatiza maeneo ya karibu na bibi huyo aliyekuwa anaishi na mke huyu wa tatu wa Sultan, ndipo maisha yalipobadilika. Bibi huyu akiwa anafahamu fika mjukuu wake ni mrembo, na Sultan angevutiwa naye, basi anaamua kutumia ulozi.
Anasema maneno kadhaa akiwa ameshikilia pindo la gauni lake chakavu, basi Sultan anakatiza kando kando ya kisima alipokuwapo mjukuu wake akifua nguo. Na kutokana na joto la kipindi hicho, binti huyo alikuwa amevalia nguo nyepesi iliyoonyesha umbo lake zuri.
Sultan alisimamisha msafara wake akaagiza aitiwe mwanamke huyo aliyemuuliza maswali kadhaa kisha akaondoka. Baada ya siku moja, vibaraka wa Sultan walitumwa kwenda kumtwaa mwanamke huyo na hayo mengine yote yakawa historia. “Mjukuu wangu, unanitisha,” alisema bibi. Mjukuuye akamshika mkono.
“Si kikubwa, bibi. Kuna kitu Sultan anakitaka. Kinamnyima furaha na amani kabisa. Endapo nikimsaidia kupata kitu hicho, ni wazi nitakuwa nimeteka nafasi kubwa ya moyo wake. Mtoto wangu anaweza akarithi kiti cha utawala.”
Bibi aliukunja uso wake.
“Kitu gani hicho?”
“Ni kito fulani cha thamani. Je bibi una namna yoyote ambayo inaweza ikasaidia kukipata na huku kipo mbali na himaya yetu?”
“Inawezekana, ila kuna baadhi ya mambo inabidi kwanza yawekwe sawa.”
“Yapi hayo?”
“Punguza hamu, mjukuu wangu. Bila shaka leo unalala huku. Pumzika, tutayajenga.”
.
.
.
.
.
.
***
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Baada ya kufuatilia kwa takribani siku nzima pasipo mafanikio, ikiwa ni usiku sasa, vikongwe watatu wa Tanashe wanafika kwenye mpaka wa mashariki wa himaya yao. Walidumu hapo kwa muda mchache kabla hawajagundua nyayo za binadamu.
Nyayo hizo zilikuwa ni za mguu wa kike. Walizitazama wasichukue muda mrefu kuugundua ukweli mchungu, nyayo zile zilikuwa za mtu wanayemtafuta, si mwingine bali Malkia. Hakuna mwenye nyayo kama zile Tanashe nzima.
“Ameshaondoka, imewezakanaje?” aliuliza kikongwe mmoja. Nyuso zao zilijawa na huzuni.
“Sijui ni nini kilitokea. Siju ni nini kimempa uhai?” Kulikuwa kimya kwa muda kidogo kabla mmoja hajauliza:
“Itakuwa tulifanya makosa kumlaza na mkufuwe. Hakuna kingine kilichompa uhai zaidi ya mkufu ule. Ule ni mkufu wake na hatukufanikiwa kuchukua kibali hicho kwasababu ya Faki.”
Kukawa kimya tena kidogo. Upepo ulikuwa unapuliza, giza lilikuwa limetanda.
“Kwanini hatukumuona upesi kwenye rada zetu na ilhali alikuwa ndani ya Tanashe? Au atakuwa alitoka nje ya himaya hii tukiwa kwenye mapambano?”
“Yote yanawezekana. Kama bado alikuwa ndani ya Tanashe wakati tunamsaka, basi itatuwia vigumu sana kumrudisha mikononi mwetu. Maana itakuwa inamaanisha hatuna uwezo wa kumuona tena. Sijui uwezo huo ameutoa wapi?”
Akadakia mwingine:
“Na Sijui atakuwa ameelekea wapi? Kufanya nini?”
Walitamani sana kufahamu lakini haikuwezekana. Hawakujua kwa wakati huo Malkia alikuwa juu ya farasi aliyemkwapua hatua chache baada ya kutoka Tanashe akielekea himaya ya masonara.
Mwanamke huyo kifuani alikuwa amebebelea mkufu. Ngozi yake ilikuwa laini inayong’ara. Uso wake ulikuwa na uhai. Nywele zake zilikuwa ndefu, nyeusi. Alikuwa ni yule Malkia! Malkia wa Goshen tuliyekuwa tunamfahamu, mzuri atakayekufanya uache shughuli zako kumtazama.
Alikuwa amedumu kwenye safari hii kwa masaa kadhaa, na sasa alikuwa anaingia msituni kabla hajaumaliza na kudaka jangwa. Alipomaliza msitu huo mpana wenye miti na mandhari ya kuogofya, alimuacha farasi hapo atumie miguu yake kusema na jangwa.
Hakugeuza shingo nyuma kutazama alipotoka. Hakuwa na dalili hata ndogo za kuogopa. Baridi kali lililokuwa linampiga lilimfanya ajikunyate, lakini si kusitisha safari yake. Alizamisha miguu yake ndani ya mchanga na kuichomoa. Hakuchoka.
Safari yake inakuja kukoma katikati ya usiku. Alisimama kana kwamba aliona jambo. Alichota mchanga akaujaza kiganjani mwake kisha akaumwagia mbele yake kama hatua moja, mara shimo kubwa likatokea hapo. Lilikuwa ni lile lililommeza Zura.
Malkia alirusha macho yake ndani ya shimo hilo, hakuona kitu. Kulikuwa ni totoro haswa. Alisimama hapo kama anayechambua kiza anachokiona. Mara akajirusha kuzama humo ndani!
Kishindo kiliashiria amefika chini. Alikuwa haonekani kabisa. Hakukuwa na mwanga wowote ule. Punde baada ya kishindo hicho, sauti ya farasi inasikika. Sauti hii haikomi baada ya mara moja, inaendelea zaidi na zaidi. Inakuwa kelele sasa.
Malkia anasogea taratibu, vishindo vyake vya miguu vinasema. Haichukui muda mrefu, kidani chake cha mkufu kinawaka, sasa anaona anapopakanyaga, anaona pia anapoelekea. Ila mbele bado ni kiza. Haoni komo la shimo.
Anatembea kama hatua nane akiangaza, mara anasikia vishindo vya watu vikikatiza upesi, anasimama! Anaminya kidani cha mkufu wake na mara kunakuwa giza totoro. Alitembea hatua mbili, akaachia kidani hicho, mara mwanga ukachipuka haraka. Uso kwa uso Malkia akaona kundi la watu wa ajabu mbele yake!
Tabasamu linamtoka usoni.
.
.
.
.
.
.
.
****
.
.
LAKO JICHO!
.
.
.
.