Tarehe 17 mwezi wa kumi mwaka 2011, mimi, bosi na mke wake tulikuwa kwenye eneo fulani tukipata Chakula Cha mchana.
Si kawaida mimi kuandamana nao ila ni kwasababu, ilikuwa ni kwaajili ya mpango maalumu yaani Mimi kutumwa kufuata mzigo fulani mkoani.
Nirudi nyuma kidogo,
Mwaka 2011, nilikuwa na wakati mgumu sana kimaisha ni baada ya mwaajiri wetu kubadili kazi kutoka kazi uinjinia na tenda za kutengeneza barabara na kuhamishia nguvu kwenye biashara hoteli ikiwa ni hatua kubwa kwake
Huku wengine tukiachwa solemba maana ikabaki tu ile
Unajua nini Dani, Mimi nitakufanyia mpango palepale mi siwezi kukuacha tumetoka mbali bwana.
Huku nikiwaza, atanifanyiaje mpango Mimi kwenye biashara hiyo mpya ikiwa Sina utaalamu kwenye eneo lolote lile, anataka kunipa kazi gani?
Ulinzi? Au niwe naelekeza watu wapi pa kupaki magari au nikawe Gardner kwenye bustani zake, hahahaha siwezi kufanya hizo kazi na haya ni maneno ananipa ili kunifariji Hana kazi ya kunipa kwa Sasa.
Basi kadri maisha yanavyoenda ndivyo ugumu wa maisha ukawa unaongezeka, kila nikihangaika kutafuta kazi ikawa ni ngumu kupita maelezo, ikafikia wakati nikamnyang'anya pikipiki kijana fulani ambaye ni mtoto wa kaka yangu binamu.
Nikachukua pikipiki yangu kwakuwa haikuwa na mkataba ikawa rahisi tu, lengo siyo niendeshe Mimi ila ilikuwa iuzwe ili inisaidie kunyoosha mambo fulani ambayo pale nyumbani yalishaanza kukaa shaghala baghala.
Ikafikia hatua, nikiangalia baadhi ya vitu mule ndani naona kama vingi halafu vimebanana, basi friji la jokoni likawa muhanga, ni sawa na mchezaji ambaye kashindwa kuonesha kiwango bora kwenye timu,
Ni kipindi ambacho mke wangu alikuwa anahuzunika sana, kwanini kuuzauza vitu, akinisihi zaidi kupambana nipate kazi maana yake nilikokuwa naelekea si kuzuri.
Mambo yalienda hivyohivyo huku nikijitahidi kujikakamua kulipa ada ya mwanangu ambaye nilimpeleka nursery ya bei kubwa, ambapo nadhani ilikuwa ni kuiga ama kufuata mkumbo maana hata kazi yangu ya mwanzo sikuwa na mshahara wa kihivyo.
Basi huku tukiishi maisha fulani ya unga nusu na robo, siku moja tukiwa kwenye Chakula Cha usiku mke wangu alivunja ukimya.
Mume wangu, mume wangu, baba Jackiiiiiii, si nakuita wewe au?
Aliuliza,
Si kwamba nilikuwa simsikii hapana Bali macho yangu yalikuwa kwenye TV ambapo yeyote angedhani labda naangalia kwa makini kinachoonesha kile, kumbe Mimi naitathmini TV yangu ilivyo kubwa yaani naona hii nikiuza sikosi laki nane Hadi milioni.
Ni TV flani za mtumba hakika kama ni TV niliipata.
Naam mke wangu, teh teh nikijichekesha.
Mke wangu aliniangalia huku akionesha kukasirishwa ila hakusema chochote kibaya
Mume wangu Mimi hapa Nina mambo mawili nataka tuzungumze,
Nikamwashiria kwa kichwa kwamba aendelee,
Akasema, jambo la kwanza hapa ni kuhusu huyu dada wa kazi, ni mtu mzuri, ana tabia nzuri na ni mchapakazi lakini tuna miezi minne Sasa hatujampa haki yake, mbaya zaidi hatuna matarajio atapewa posho yake lini, alisisitiza mke wangu.
Nikawa nimekaa kimya.
Akaendelea jambo la pili, mimi ni mjamzito..
Enheeeeeeeeeeeeeeeeeeehh
Unasemaje?
Itaendelea.....