Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Mkuu Mr. Daniel just cut ourselves out of curiousity, tunatamani kujua what happened between you and Rose. On top of that be patient on her, keshakwambia mtaendelea kujuana kadri muda uwendavyo
Ouff... Watu wameshamsahau Ester hahaha
 
Mkuu Mr. Daniel just cut ourselves out of curiousity, tunatamani kujua what happened between you and Rose. On top of that be patient on her, keshakwambia mtaendelea kujuana kadri muda uwendavyo
Ouff... Watu wameshamsahau Ester hahaha
Sasa mkuu unataka akutumie hyo hadith private au ?

Si usubili mwendelezo hapa mkuu khaaa
 
Mkuu shusha vipande vitatu leo na kesho vitatu weekend hii mkuu...tumekuwa tukifuatilia kwa ukaribu sana
 
Sasa mkuu unataka akutumie hyo hadith private au ?

Si usubili mwendelezo hapa mkuu khaaa
Mkuu ungeelewa maana rasmi ya nilichokimaanisha hapo ungetamani kuungana nami, CUT OURSELVES OUT OF CURIOUSITY aimalize hamu yetu yakujua yaliyoendelea mbeleni kati yake na Rose pia bila kusahau yaliyojiri kati yake na ESTA. Sasa wapi hapo nimetaka kujiridhisha mwenyewe binafsi?!
Fasihi ni pana sana.. Tuendelee kujifunza kwa waliokosa muda wa saa mbili hadi saa nane mchana.
 
SEHEMU INAYOFUATA................

Nilijua tu lazima urudi muda huu, tena umelewa mwenyewe kwa raha zako, kweli maskini akipata......... (Kabla hajamalizia )

Mke wangu naomba tuheshimiane, kuna njia nyingi za kuweza kumkosoa mtu ila si kumtukana , sisi binadamu tuna majina mengi Duniani. Kuna sehemu ukipita watu watakuita genius kwa sababu wanazozijua wao , wengine watakuita fala au mpumbavu, si kwamba labda Kuna kibaya umewafanyia bali Kila mmoja ana haki ya kukuchukukia anavyoona yeye .

Lakini wewe kwangu unalazimika kuniheshimu kwa asilimia nyingi, siyo kwamba siwezi kukuudhi, maudhi si ndiyo kama haya? Lakini Kuna namna ya kumkosoa mumeo. Naitwa mume Mimi ni rafiki yako, mshikaji wako lakini Nina nafasi kubwa zaidi watu wote wananiita mume wa..........

Tuheshimiane mke wangu.
nilimsema.

Sawa mume wangu, swali liko pale pale ulikuwa wapi, aliuliza.

Nilikuwa baa na marafiki zangu tukipanga na kupangia vipi Kuna Sheria nimeivunja,Nini hakipo hapa nyumbani, kila kitu kipo kwanza sioni haja ya kuendelea na maswali Hadi sasa. Nilimjibu kwa uonevu hali iliyopelekea akashindwa kuendelea kuniuliza huku akikasirika kwa kiwango Cha juu, nakumbuka alichukua kigogo fulani akanirushia kikanipata sawa sawa, ikabidi nikimbilie chumbani nikijifanya nimeumia sana .

Namjua mke wangu akikasirika, hachelewi. Kitendo Cha yeye kuniumiza kikawa ni mtego kwake., nilingia chumbani nikafikia kuoga huku nikijifanya Nina maumivu sana, ila haikuwa kweli ila niliigiza ili nimkomeshe asiwe ananiuliza uliza.

Shemeji, shemeji, ilikuwa ni sauti ya dada wa kazi akiniita kwaajili ya Chakula Cha usiku .

Hapana nyie kuleni , Mimi! Najisikia vibaya. Nilimjibu huku nikisikia akipiga hatua na kuondoka.

Dakika chache mke wangu alikuja akasukuma mlango huku akiwa kaweka mikono kiunoni,
Mume wangu Chakula tayari amka basiiiiii,

Siwezi Nina maumivu sana huku mgongoni nikiwa sawa nitakuja , tayari nilishapata pointi,aliondoka huku aliongea maneno ambayo sikumsikia vizuri ila alionesha kujuta sana, kesho asubuhi na mapema alikuja kwangu.

My husband umeamkaje, vipi unaendeleaje? Maumivu je?

Nimeamka salama japokuwa Nina maumivu sana nadhani nikiamka nitaenda hospital na Leo jumapili sidhani kama nitapata huduma kirahisi . niliongea kwa mtego.

Mmmmh mume wanguu naomba unisamehe Mimi ujue hata sijapata usingizi mwenzio, Jana hujala vile vile bado unaumwa, nisamehe baba Jack sitarudia tena,aliongea alionesha kujuta.

Mke wangu Mimi nilishakusamehe tangu jana, mpaka Sasa sijui kosa langu Nini maana umenihukumu kisa umetambua kuwa nimelewa , Sasa nikuulize, ni wapi nimevunja nikivunja Sheria, niliongea huku nikizidi kujifunika shuka .

Mimi Sina maumivu ya kwenda hospital ila nakuonya kwa Mara ya mwisho, kurushiana vitu siyo vizuri , muda wowote unaweza kupata murder case wewe, tena nikukumbushe unakumbuka ulivyomfanyia Shedy?

Kidogo umtoe jicho Sasa vipi kama angeanguka hapo nje akapoteza uhai huoni kama tungeungana mahabusu huku wewe ukikakabiliwa na kosa lisilo na dhamana, mke wangu unanitisha sana kwa naamuzi yako naomba jitahidi kujizuia na kudhibiti hasira zako vinginevyo wewe ni mfungwa mtarajiwa.

Usiseme hivyo mume wanguu (huku akitoa machozi) naomba nisamehe sirudii tena Mimi .aliongea kwa uoga.

Hapa shida siyo msamaha, tatizo ni tabia yako, Mimi nitakusamehe lakini jua wengine hawana msamaha kabisa, kwahiyo punguza hasira my wife, nilimtuliza ni wanawake tu Hawa kuharibu kitu na kukimbilia kujiliza , yaliisha.

Mume wangu naomba niende kanisani, maana tangu nijifungue sijawahi kwenda, aliongea hivyo baada ya kugundua kuwa sina maumivu kihivyo.

Usijali we nenda tu, nilimruhusu.

Walijiandaa huku Mimi nikiombea watoke nipate kuongea na simu zangu, baada ya mke wangu na dada wa kazi kwenda kanisani nilitoka ili nikapate mchemsho maeneo jirani na nyumbani kwangu maana njaa + hangover za pombe nadhani nilihitaji kuupatia mwili chochote kitu.

Aaah Daniiii afadhali nimekuona bosi wangu maana mwenzetu maisha safi kabisa naomba japo nichukue chapati mbili na chai na mimi maana hali si hali, aliongea kijana mmoja.

Sina kitu jamani hamuoni jua ni kali wanangu,?

Haaaaaa Dani, acha hizo juzi tu tumepita kwako tumeiona fence hiyooo inakaribia kuisha halafu unajifananisha na sisi acha hizo jombaa , walizidisha maneno wale vijana wahuni, ikabidi niwanunulie wanachotaka, walishukuru sana,

Dah mwanetu Dani tunashukuru sana we ndo homeboy wetu unajua Nini hunaga baya yaani, waliongea huku natamani waondoke, nikiwa naendelea kula wao walishamaliza tayari, ni vijana fulani wa mtaani pale , hawana tabia nzuri sana ila Ukiwa mjanja jitahidi kuishi nao vizuri usipende kuwakazia mlioishi uswahilini hapa nadhani mmenipata.

Oyaa braza Dani nimewasikia vijana kuwa una ujenzi huko kwako, vipi Kuna maisha. Aliuliza jamaa mmoja anayeonekana kunifahamu sana,.

Hapana Sina kazi kwasababu Kuna mtu keshachukua tenda hiyo hivyo ana vijana wake tayari anaofanya nao kazi, nilimjibu

Poa pia bro kama una mishe naomba nikuachie namba zangu za simu (huku akitaja) .

Nilimaliza kula pale Kisha nikaishika njia taratibu nikirudi nyumbani huku natafuta jina la Rose nililo sevu navyojua Mimi, simu ikionesha inaita upande wa pili.

Hello habari (niliisikia sauti yake nzuri huku mapigo ya moyo yakiongezeka)

Salama my friend umeamkaje? niliulizia hali.

Weeeeh (huku akicheka) yaani ile wine huwezi amini ilinichanganya hata vile nilivyokimbilia kwenye gari kifupi nilikuwa sijisikii poa, hivi hukunigundua? aliuliza

Hapana, Mimi nilijua labda kwakuwa muda umefika ndiyo maana ukaondoka. ila pole sana unaonekana si mtumiaji wa vitu vile, niliuliza.

Aisee umejuaje kiufupi Nina muda mrefu sijawahi kutumia kilevi, halafu kichwa changu nakijua mwenyewe, mnaitaje vile mtu asiyeziweza pombe?...

Kabla sijamjibu, niliona Kuna ugomvi mbele yangu watu wawili mwanamke na mwanaume Tena mwanamke namtambua, ikabidj niisubirishe simu ya Rose ili nione kinachoendelea hapa, alikuwa ni ESTA na jamaa mmoja wakiwa wanavutana huku ESTA akiburuzwa, huku baadhi ya wapita njia na majirani wakiwa wanaangalia ile action bila kutoa msaada.

Jamani, jamanii Kuna nini hebu tulienk kwanza mbona mnatiana aibu mtaani jua lote hili Kuna Nini kaka hebu nambie, nilimshika mkono yule jamaa mgeni machoni mwangu huku nikimbembeleza apunguze jazba .

Unajua kaka Hawa wanawake was...e sana , huyu alikuwa ni mchumba wangu muda mrefu sana ila nilisafiri , Sasa kwakuwa huko nilikokuwa nilikaa muda mrefu nimerudi na kukuta amebadilika na pia ana saloon kubwa sana maeneo ya mjini (akitaja eneo ambalo hata Mimi nilishangaa maana navyojua Mimi saloon ya ESTA haiko mbali na maeneo yale)

Muongo huyo shemeji, hakuwa mchumba wangu, Bali ni mtu nilikuwa nasali naye kanisa moja hivyo mchungaji akawa anashauri tuoane, ni ushauri tu ila hatukufikia hata level za uchumba. Kwanza Mimi hata sikumpenda huyu ni kwasababu mchungaji alikuwa ananilazimisha. aliongea kwa jeuri huku nikitambua kashaanza kujivunia uwepo wangu.

Usijali bro, we usigombane naye tumia njia tu za kistaarabu atakuelewa tu huyu , pia hapa wote mmeshakuwa na presha hivyo hakuna jibu litapatikana zaidi ya kuharibu, utajikuta unaishia pabaya.

Si wanawake, si wanaume walimtukana sana jamaa kuwa kwanza haendani na ESTA na kwanza wanawake walivyojaa kwanini amng'ang'anie mtu mmoja? nilimuhurumia mshikaji maana mtu pekee nilikuwa namtetea ni Mimi tu wengine wakimuona jamaa ni mshamba na limbukeni wa mapenzi.

Sasa na wewe ulikuwa unaenda wapi. Nilimuuliza ESTA,

Mimi nilikuwa nafuata gari ili ikanihamishe nahamia sehemu nyingine pale naona pamekaa kiswahili sana. alijibu kwa nyodo,
Nikacheka huku nikijisemea moyoni kweli pesa sabuni ya roho.

Kuepusha Shari niliondoka na yule mshikaji ambaye alionesha kuchanganyikiwa sana yaani alinasa kwa ESTA.

Kwani ESTA ana nini au hata Mimi ningetembea naye ningepagawa maana wanawake wengine ukinasa hutoki, ila siyo Mimi labda Hawa walugaluga. Nilijisemea kimoyomoyo

Bro unaonekana unafahamiana na yule ESTA. aliniuliza yule mshikaji.

Ndiyo, namfahamu ni rafiki wa mke wangu. Nilimjibu .
ila usiwaze Mimi kwakuwa namfahamu vizuri na nishajua shida yako hili niachie Mimi litakaa sawa tu nitaongea naye. Jamaa alifurahi sana

Halafu nikushauri jambo moja jitahidi sana kutumia njia ya kujishusha maana pale mlipokuwa
Mnaburuzana wenzio walisubiri tu uharibu ili wakupige au upelekwe polisi au hujui furaha ya binadamu wengi ni kuona mwenzao akiingia kwenye matatizo.

Jamaa alinielewa sana, huku tukiagana,.

Siyo kwamba nilitaka kumsaidia kweli, ila ilikuwa ni njia ya kumuweka sawa maana alikuwa kama kachanganyikiwa, hivyo mwanaume mwenzio akiwa kwenye hali ile lazima umuoneshe matumaini ni maisha tu haya.

Baada ya upepo ule kupita nikarejea kwenye calls nikipiga simu kwa Rose ila haikupatikana, nililaumu nikajilaumu, piga Mara kadhaa lakini majibu yakiwa ni sifuri.

Nilirudi nyumbani nikawasha PC yangu nikakaa nayo kitandani huku nikitafuta vitu ambavyo sikuvielewa Mara niangalie video hii Mara hii ili mradi napoteza muda

Delivery report ya sms niliyomtumia Rose ilirudi , nikajua simu yake ipo hewani, nilitoka chumbani mbio huku nikiweka simu sikioni ili nikaongelee nje simu ilipokelewa bila kusikia sauti yeyote upande wa pili,

Hadi pale nilipoongea Mimi baada ya kuigundua sauti,

Hello Mr, vipi Kuna usalama kweli, sauti Rose iliyo kwaruza kwa hofu ilisikika

Ni salama tu my friend, vipi mbona sauti ya chini hivyo.niliuliza

Unajua haya mambo ya waume za watu ndiyo maana sijawahi kutamani , yaani baada ya wewe kukata simu ghafla nikajua pengine mkeo kakustukia hivyo nilizima simu kwa muda , Sasa yote haya yanini , yaani hapa nilipo moyo wangu unaenda mbio kwa hofu . alilalamika

Ondoa Shaka kwanza ukiona nimekupigia simu jua kuwa nipo sehemu salama tu. nilimtoa hofu.

Sawaa bado, nahisi Kuna matatizo nayatafuta huwezi amini umenitisha sana tu , aliongeza.

Kwanza uko wapi my friend maana uliniambia huwa unaenda kanisani, imekuwaje unaniambia upo nyumbani tu, niliuliza

Wewe nimeamka nimechoka sana nikashindwa hata kuamka mapema nilitamani Jana unisaidie hata kuendesha gari lakini nikiogopa waume za watu, kweli walioshauri usiendeshe Ukiwa umelewa waliongea point sana Jana ndiyo nimejua maana nilikuwa kama learner. (Huku akicheka)

Ennhee na mwenzangu ilikuwaje au wenzetu mmeshazoea ?

Aliuliza akidhani na Mimi Nina gari, ndiyo asingeelewa , maana nilikuwa wa kwanza kufika hotelini huku yeye akifuata pia akawa wa kwanza kuondoka, hivyo kwenye zile parking alidhani na Mimi Nina usafiri wangu,

Sikutaka kumwambia kuwa Sina gari japo tayari kutokumiliki usafiri kulianza kuninyima Raha.

Aaaahaaa hakukuwa na shida Mimi nilifika salama tu, nilimuongopea.
Sawa kwakuwa sipo bize sana Leo ningependa tuonane nimemiss stori zako , yaani hunichoshi kukusikiliza, aliongea kwa kudeka.

Sasa tuonane wapi, nilihoji kwa pupa maana mrembo nayemuwaza Leo anaanza yeye kutaka tuonane.

ESTA Kawa matawi ya juu kwanza anahamia maeneo ya mjini, pia Kuna taarifa kuwa hata saloon kafungua nyingine tena yenye hadhi ya juu.suala la kukosa gari lishaanza kuninyima amani huenda nikawakosa watoto wakali wa mjini

ESTA ni character mkubwa kwenye hii simulizi hivyo atapotea atarudi. Nini kita jiri usikose sehemu inayofuata.

Inaendeleaa very soon............
 
Kisa cha kusisimua, ni kisa kitamu chenye mafundisho na kuburudisha pia

Nimesoma visa na stori kibao humu ziwe ni dhahania au za kweli lakini zimenipa nguvu na faraja kuwa kwenye record zilizowaweka watu kwenye wakati mgumu sipo peke yangu.

Hivyo basi na Mimi nakuja na kisa cha kweli kilichonitokea mwaka 2011. Ni kisa ambacho huwa sipendi kukumbuka na kujikumbusha Mara kwa Mara ila haina budi ni jambo lilitokea

Lazima watu wajifunze japokuwa ajali haina kinga lolote litakutokea muda wowote na mahali popote.

Kisa kinaitwa ,
MIMI NA BOSS WANGU

Kaa mkao wa kula.
Kwa hiyo hakijaanza bsi ni riwaya
 
Hii jumapili brother tolu atakua ametulia mahala na mtoto rose coz wife leo atakua kanisani
 
SEHEMU INAYOFUATA............

Maisha yaliendelea huku Kila kitu kikienda sawa kadri kilivyooangwa , nakumbuka weekend moja kama kawaida yangu ilikuwa lazima nimpigie Rose japokuwa kwa Siri ili nisije kuharibu kwa mke wangu.

Dah kwa leo nisingependa kutumia kilevi Mr kwa kweli siku ile nilipata shida sana, aliongea Rose akionesha uoga fulani.

Hapana vipo vinywaji laini mbona ? Lakini yote kwa yote kama wewe hutumii kilevi hata Mimi siwezi kutumia kwanza siyo lazima. Nilimjibu huku nikifurahi maana nimejipunguzia gharama lakini hata hivyo kulewa Kila Mara si dalili nzuri.

Enheee nipe michakato ya maisha, life linaendaje , aliuliza huku akiwa ananitazama usoni, kitu pekee ambacho niligundua toka kwa Rose ni kwamba yupo tofauti sana na wanawake wengine baadhi, yaani anajiamini sana, kumbuka siku ile ilikuwa pekee ya kuweza kumwambia ukweli kutoka moyoni mwangu Sasa nikaona kama mzani umeinama yaani anataka kunishinda.

Hivi Mr Daniel una Elimu ya level gani, samahani lakini, akionesha shauku ya kutaka kujua,

Bila samahani unapaswa kujua tu kiufupi Mimi nina Degree ya uhandisi,,huku nikimpa analyse ya shule mpaka vyuo nilivyosoma .

Safi sana Mr, vipi kuhusu kazi umeanza lini kufanya kazi pale kwenye ile kampuni ? aliuliza .

Pale hata mwaka bado sijamaliza ila nimetokea sehemu tofauti tofauti kama unavyojua kupata kazi kwenye nchi hii kunahitaji marefa, au labda uwe na mtu maarufu au mtu mzito , kwahiyo nilianza chini kabisa kwani kabla sijaanza kufanya kazi inayohusu taaluma yangu, Ila nashukuru MUNGU maisha yanaendelea. Nilimjibu

Samahani lakini, unadhani umeshatimiza ndoto zako kulingana na taaluma yako? Alizidisha maswali

Hapana , kwanza niwe muwazi hakuna anayeridhika na kipato Chake hata iweje Leo utaona mshahara ni mdogo, utapata kazi yenye mshahara fulani wa kuridhisha lakini bado utakuwa kwenye kundi la wanaolaumu kuwa bado maslahi madogo, kwakuwa Kila kiwango Cha pesa kinavyoongezeka na matumizi huongezeka. nilijibu huku nikiwa nishachoka na maswali yake

Yote kwa yote nini kinapelekea uwe unaajiriwa kwenye Private sector, maana kwenye mlolongo wa sehemu ambazo uliwahi kufanya kazi kote ni sekta binafsi, na Elimu yako inaonesha unaweza ukawa kwenye chain ya wanaofanya Kazi serikalini. aliongeza huku nikishindwa kujua kwanini anapenda sana maswali.

Kama nilivyokueleza tangu mwanzo labda sijapata watu wakuniunganisha huko, nilijibu kwa mkato.

Je, una mpango gani kupitia Elimu yako kubuni kitu ambacho kitakuwa Cha tofauti huku kikileta matokeo chanya kwenye jamii ? She's asked

Kwanza sijawahi kufikiria jambo hilo lakini pia nashukuru ni kama nimepata mwanga fulani , nikipata muda nitalifanyia kazi suala hili.

Hahaha (akicheka) tatizo bado unaamini kwenye kuajiriwa ila bado una nafasi ya kufanya chochote maana unaonekana bado kijana kama Mimi, aliongea akafanya tukacheka kwa pamoja.

Kiukweli nafurahi sana kuongea na wewe umefanya hisia zangu kuwa kwenye level za juu kabisa, Rose we ni mwanamke ambaye tayari unanikosesha amani ya moyo, hasa Kila tukikutana kama hivi nafikiri ni MUNGU tu alituunganisha , Napenda sana mwanamke bright kama wewe nashukuru kadri tunavyokutana nanoti kitu kwako , yote kwa yote Sina lolote zaidi ya kusema NAKUPENDA, nakupenda sana Rose. Niliongea kwa kumaanisha huku nikikaza uso kumtizama.

Halafu wanaume mlio kwenye ndoa sijui mpoje? Hivi Mr Mimi na wewe hatuwezi kuwa marafiki bila kuwa wapenzi, aliongea huku aiinama chini na kunifanya nizidishe mashambulizi .

Najivunia kuwa na wewe Rose najihisi mwenyewe faraja ya moyo ninapokuwa na wewe , nafurahi nikikutaja kwa jina lako, hata kama hupendi kuitwa kwa jina lako lakini nitakuita kwa jina lako ili walau kuulisha au kupoza kiu ya moyo wangu.

Mr Daniel bwana , moyo huohuo unampenda mkeo , unawezaje kupenda watu wengine? aliongea huku safari hii akibonyezabonyeza simu ambayo niligundua ilishazima chaji kabisa, hivyo alikuwa anazuga zuga tu.

Moyo ni kama taa inayowaka ndani ya sebule yako , haijalishi mtu awe mwema, muovu au jambazi , taa itamumulikia Kila mmoja kusudi atimize hitaji lake, kwahiyo huo moyo wako ni wa namna Gani? aliuliza

Kwa jinsi ulivyotoa mfano wako , unahisi Mimi ni mtu muovu au mwema? Niliuliza.

Hakujibu zaidi ya kucheka tu,.

Nikaendelea , mfano uliotoa ni mzuri ila jua moyo huongozwa na ubongo au akili timamu za kiumbehai hasa kwa sisi binadamu, hivyo ni vyema nikajua jibu langu mapema. niliongea safari hii nikionesha liwalo na liwe.

Ila Mr Daniel samahani nimeshindwa kuja na gari yangu maana niliiacha vizuri tu Jana Cha ajabu napiga start asubuhi imegoma kuwaka hivi tatizo linaweza kuwa ni Nini? aliuliza huku nikitambua ananitoa kwenye maada

Kwani inafanyaje au betri ipo down, niliuliza

Hapana nimejaribu Hadi betri ya gari la baba haijakubali kwenye gari langu wakati kwake linawasha na la kwangu kwake linawasha pia yaani hata sijui tatizo ni nini maskini sijui jumatatu itakuwaje na Sasa hivi nilivyochacha alijisemea.

Ndugu msomaji, ukisikia yaani striker yupo yeye na goli ndiyo siku ile.

Ningekuwa karibu ningeicheki , nilisema huku nikisubiri atajibu nini.

Hamna shida tunaweza kwenda kuliona maana nikiwaza jumatatu bila gari naendaje kazini napata shida sana, tulitafuta bajaji , huku nikijitahidi nisije kuonekana na mtu anayenifahamu kuna vitu mtu hupaswi kuonekana.

Naam, tulifika kwenye geti la nyumba yao akafungua geti, karibu mwaya hapa hatuna hata mlinzi ujue

Hofu yangu ilikuwa namna nitatambulishwaje kwa wazazi wake nakua Haina tabu lakini bado ilinipa ukakasi

Karibu ndani mgeni, huku akiitwa kijana wa kiume ambaye nilimkuta
Akiwa anatupatupa ngumi mithili ya wacheza boxer akiwa kwenye singilendi Cha ajabu anaonekana ni mwenye heshima sana,

Tunaomba tuangalizie juisi kwenye friji, kijana akaleta huku nikijikaza maana sikupenda kuwa maeneo yale hasa Mimi mwenye heshima zangu.

Uliniambia unakaa na wazazi wako vipi wako wapi. niliuliza

Ah samahani sikukwambia, wazazi wamesafiri wameenda Morogoro watarudi jumatatu,hata hivyo usingekuja hapa si unajua tena. Aliongea huku akicheka cheka.

Nillikunywa ile juisi kama maji Kisha nikatoka nje kuelekea kwenye gari ya Rose. akaja mpaka pale nilipo .

Kama unavyoona hili ndo gari huku nikimsaidia kufungua Bonet,nilitumia njia ya kienyeji kwa kugusisha chanya na hasi huku betri ikionesha Ina moto wa kutosha,hii si njia nzuri lakini

Hebu piga starter kwanza, nilitoa maelekezo.akawasha.
Gari ilionesha starter haina shida maana inapiga kelele ila pump haipokei,nikaomba spana ili nivagae ile kazi huku nikihofia kama haitaleta matokeo nipo mbioni kuaibika.

Nikafungua valve zote nne kwenye pump ya gari baada ya kugundua Kuna moja ni kavu hata ukipiga free pump haileti kabisa mafuta , nilifungua huku nikikuta kiraba fulani kimelika huku kikiziba kabisa njia ya kupitisha mafuta, nikamuonesha zile raba zilizolika huku nikimuuliza kuwa aliwahi kubadilisha pump maana inaonekana siyo yake , akajibu ndiyo ni mwezi uliopita alibadilisha .

Tukaangalia kwenye toolbox yake nikavikuta viraba vingi vipya vikiwa kwenye special nylon. Nikaweka na Nikafunga vile vipya

Licha ya uwepo wake lakini hakujua kinachoendelea, nikazidisha utundu kwa kufungua plugs zote na kusafisha, huku zikiwa mbwembwe tu tatizo Wala halikuwa kubwa.ili anione wa maana

Nikafunga Kila kitu, nikwambia awashe , gari hiyoo ikawaka , tulibaki tunatizamana tu huku Kila mmoja akitabasamu , hakuna aliyesema neno alitamani anikumbatie lakini akaishia kuziba USO kwa viganja vyake, niliziona movements zake alionesha kufurahi sana, tuliingia kwenye gari huku akiwa akizima na kuwasha sijui alijua tatizo litakirudia .

Akaanza kutest kwa kulitoa nje ya geti lao , majaribio ya gari la Rose yaliishia kwenye lodge moja matata, huku akiniuliza ,

Sasa huku tumekuja kufanya Nini Tena , aliuliza kwa mshangao ila nilimuamrisha apaki gari huku nikiangalia ni saa kumi kamili hata adhana iliashiria hivyo,

Nikamshika mkono tukaingia mpaka lodge tukipokelewa na mdada fulani, nikaulizia chumba , nikalipa huku akiwa kama hataki fulani hivi hata wale wahudumu waliokuwa reception walishangaa kuona ni kama watu ambao hatukuwa tumekubaliana .

Rose aliwagundua mawazo yao, kwa kuniondolea aibu akanipiga busu moja takatifu mdomoni hata sikutarajia, Kisha akatangulia mwenyewe kwenye chumba tulichoelekezwa huku akiwakata ngebe wale waliodhani labda nalazimisha mapenzi.

Rose akiwa na kaaibu fulani, huku nikigundua wote tulikutana tukiwa tumekaa muda mrefu, yaani mithili ya mchezaji ambaye kasugua benchi muda mrefu Sasa anamshawishi kocha ili awe anamuweka first eleven.

Kiufupi Rose aliupiga mwingi sana , ni fundi sana wa mipira ya pembeni, iwe kushoto au kulia halafu na dimba la Kati ndiyo kabisa anakuja juu juu huku anakukaba ukienda kwa pupa ana chenga zake za kufinya. Jamani acheni tu.magoli ya mapema sana yalipatikana kwa Kila mmoja , huku timu zikishambuliana kwa zamu mechi iliisha kwa sare ya bao tatu kwa tatu huku wachezaji tukilowa tapatapa kwenye ile derby isiyo rasmi.

Rose alikuwa daktari haswa tena anatibu maeneo mengi sana,hakuwa tu daktari wa kusomea chuoni Bali alikuwa na kipaji .

Saa mbili kasoro, tulitoka huku , jina la Mr Daniel likifa mithili ya puto lililogusa kitu chenye ncha Kali.

Na Mimi ningemwitaje Rose Sasa?

Majina wanayoitana vijana ndiyo yaliyotawala. Tukatoka huku tumekumbatiana , tukiwa wapenzi rasmi, kufika pale mapokezi uso kwa uso na ESTA akiwa na mdada mmoja ambaye anaonekana anafahamiana naye wakiwa wanakabidhiana mawigi fulani na nywele bandia pale mapokezi.

ESTA ni mtu mzima Kila kitu alikijua , akavunga kiasi Cha Rose kutojua chochote, tulitoka huku nikigeuka nyuma nikamuona ESTA akitabasamu kwa muhaho.

Nilijiona nishaharibu , nikajisemea huyu lazima atarudisha uhusiano kwa mke wangu ili amsimulie Sasa dawa yake ni kumuwahi lazima nilale , Kesho jumapili nitahakikisha namgonga huyu, kinyume na hapo ataenda kusema kwa mke wangu.

Nini kitajiri usikose sehemu ijayo
burudika.

Itaendelea......
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom