Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Hapo Kuna mboga inataka kumwagika,, shukran kwako mkuu
 
SEHEMU INAYOFUATA......

Tuliagana na Shedy huku kukiwa hakuna maelewano, ni kwamba kila nililoliuliza sikujibiwa ipasavyo,

Majibu yalikuwa mepesi, tuliachana huku wakiingia, kwenye gari lao Toyota RAV4 wakiwa kwenye Mabishano makali hasa kile alichokisia mkewe tayari aligundua jambo,

Niliwasindikiza kwa macho, huku gari yake ikiwa inapandisha kilima fulani inatoa moshi na muungurumo mkubwa sana.

Nilicheka peke yangu,nikajisemea
Yaani huyu kuwa na hii gari ndiyo imekuwa fimbo ya kuweza kutuumiza sisi, kwahiyo anapita majumbani mwetu akitongoza wake wa watu kisingizio hii gari.

Kwa gari gani, hii ambayo inaonekana CC zimeshuka, halafu rejeta yenyewe inachemsha si kafika hapa kafungua boneti naona mvuke umetanda,

Gari hii ukute walitaka kupima chuma chakavu akajikuta anafunikwa na udalali wake wa pupa , nikitaka kununua gari hata leo nanunua hata kwa mtu , kwanza Nina uzoefu mkubwa wa magari nishaendesha sana siwezi kuuziwa mkweche Mimi baada ya muda fulani alinipigia simu akiniomba radhi nikiwa bado nipo palepale waliponiacha.

Nikaipokea .

Ila we Shedy nitakutafuta nishajua ukweli wote malaya mshamba wewe usiyejua kutongoza, unadhani mwanamke gani angekukubalia wakati unaenda kumvunjia heshima mumewe ,hivi wewe wa kumtongoza shemeji yako wewe?

Hapana kaka, hata Mimi nilimshangaa mkeo kunidhuru ila sikuwa na lengo baya.

Muongo wewe,acha upuuzi nimekustahi mbele ya mkeo ili asijue mengi lakini jua kuwa tukikutana Mimi na wewe hakuna maelewano umenikosea sana. Nikakata simu

Hapa Sasa sikuwa na masihara hata mke wangu sikuwa na Imani naye moja kwa moja,

Nikafika nyumbani pitiliza Hadi chumbani,mke wangu kuona ujio wangu alikuja .la kuniuliza aliuliza akajibiwa,

Mke wangu hiyo laki moja aliyoitoa Shedy iko wapi,niliuliza huku wangu ukimtisha mke wangu,

Mmmmh makubwa,hiyo hela ipo Mimi sikuipokea, anayo dada wa kazi vipi nimuite ailete, aliuliza.

Hapana, subiri kidogo hata hivyo Nina maswali kwako nadhani uliniambia ila sikukujibu kwakuwa sikuwa na maelezo ya pande mbili lakini pia hili suala sitaki mama yangu alijue liishie hapa hapa chumbani.
Nilisema.


Mume wangu kama nilivyokwambia ,kwanza hakuna maelezo zaidi ya niliyokupa,
Alijibu mke wangu.

Sasa we ulijuaje kuwa ana nia ya kukutongoza na yule ni shemeji yako,niliuliza,

Hey baba mbona maswali yako siyaelewi, kwahiyo Mimi ningeshindwaje kuelewa Hilo Jambo,kubwa zaidi ,aliongea mengi lakini nikamjibu kuwa kama nahitaji kupumzika,bado alikaa sebuleni,halafu wakati hayo yakiendelea dada wa kazi hakuwepo nikagundua kuwa yule pale ,kajificha makusudi huenda anajua kinachoendelea

Nikamtoa shem shedy kwa nguvu, lakini sababu iliyopelekea nimpige ni baada ya kunishika mkono eti niingie kwenye gari lake tuongee zaidi.

Nilimsifu mke wangu kimoyomoyo,ila nikajifanya sijaridhika na majibu yake.

Nikatoka nje,nikaongea na mama mambo fulani akikazana kuwa yeye anataka kuondoka,hata hivyo wao walienda huko nje ya mji wao na dada walienda kuchukua dawa fulani ili nioge,

Mwanangu wewe bado siku mbili tu ukaripoti huko kwa maboss wako wapya tumeona si vyema ukaenda kazini Ukiwa mwepesi.

Haaaaaa mamaaaaa mtakuja kutapeliwa bure ,nyie si wenyeji wa mji huu mmemjuaje huyo mtu mama yangu,niliuliza kivivu.

Tunamfahamu tangu aje hapa ana miaka mitatu tu,we humfahamu yule baba ambaye alikuwa anapata kifafa miaka ile Ukiwa unasoma shule ya msingi,walimpeleka hospitali za kila aina lakini ilishindikana hadi pale walipompeleka kwa mganga wa jadi ikaonekana ana majini/maruhani ya kiganga anatakiwa afunguliwe ,ili awe mganga na yeye,

Tangu hapo ugonjwa wake alipona na akaendelea na utaalamu wake huku akiwa na wateja sana hata hivyo Kuna miaka mitatu au minne alichukuliwa na tajiri mmoja aje aizindike nyumba yake,ndipo alipokwama huku kwakuwa aliona Kuna wateja zaidi,na hata namba zake za simu tunazo siku nyingi ndiyo maana ikawa rahisi,mama alisema.

Nikaishia kushangaa tu,kwanza huyu jamaa namjua tangu kijijini kwetu, na pia sifa za uwepo wa mtaalamu mkubwa pale pembeni ya mji nilikuwa nazo Ila sikujua kuwa ni yeye hasa ukizingatia Mimi si muumini wa hao watu.

Kumbe Ukiwa na maruhani mtu unaweza kupiga hela eeeh,niliuliza kiutani,

Ndiyo huoni anasaidia watu,mama alijibu

Sasa mama kama haya yanasaidia mbona mkiwa makanisani huwa mnayakemea yamtoke muhusika?

Hebu toka zako huko yaani we Dani hata hukui yaani tukaishia kucheka tu,

Sasa hii dawa mama,naifanyaje?

Hiyo ukaoge,ukienda ukienda kuoga nuizia kabisa mambo unayohitaji na usiyoyahitaji yaani kemea vitu vyote vibaya ni Mara moja tu Haina kurudia,alisema dada yangu.

Nikarudi chumbani nikaiweka mahali safi kabisa kwenye droo,nikarudi sebuleni,kwakuwa huko nje watu walikuwa bize na mambo yao nikaona ni wakati wa dada wa kazi kuongea na mimi nikamwita.

Naomba kujua kipindi Nina matatizo,mke wangu alipiga mtu.

Yaani Mimi Nina matatizo na yeye anatafuta matatizo,hebu nieleze ilikuwaje maana aliyepigwa ni rafiki yangu.niliuliza

Kiukweli shemu, yule rafiki yako sijui yupoje,alikuja hapa mchana akamuulizia dada,nikasema hayupo.
Lakini baada ya nusu saa,
Alirudi Tena,nikamuuliza unamtaka wa nini akasema, wewe una matatizo kwahiyo anataka waende wote ili wakusaidie,akaniachia laki moja kwamba nimpe dada akirudi Kisha akaondoka.

Baadaye akarudi Tena ,Mara ya tatu ilikuwa saa moja jioni dada akiwa hajarudi ,safari hii akawa anashuka kwenye gari, anataka kuingia ndani
Nikamzuia nikimwambia dada anakataza watu kuingia na Sasa ni usiku hutakiwi kuingia humu ndani.

Lakini alinitolea lugha Kali kwamba ,

Yeye hapa ni kama kwake,alisimamia nyumba hii kipindi inajengwa, kuanzia tofali na vifaa vyote alileta yeye,akanitukana nikajimbilia chumbani kwangu,

Baada ya muda kidogo dada akarudi, wakasalimiana, wakawa wanaongea vizuri tu,lakini dada nilimsikia akisema yule rafiki yako kaja usiku kufanya Nini kwetu,

Akajibu atulie kwanza atamwambia,

Ndipo dada alipoanza kumsukuma atoke nje, na walipofika nje nikasikia yule rafiki yako akilalamika ameumizwa ,akaondoka.

Siku hiyo dada nilimtengea Chakula hakula huku akiwa anatukana sana ,na akawa anaongea peke yake.

Ningekuua malaya wewe, kwahiyo kama umetembea na ESTA, unadhani utanipata na Mimi kwanza nilikuwa nakuheshimu sana kumbe wewe ni bure kabisa, alimalizia dada huku akienda kulala chumbani bila hata kuoga,

Asubuhi ilipofika,nilimpa hela nilizopewa Jana na yule rafiki yako,alizikataa huku akinilaumu nilipokea za nini nikamwambia nililazimishwa tu,

Akasema nikae nazo mpaka mwaka utakaporudi.

Inaendeleaa........

Bado mbichi hii
 
SEHEMU INAYOFUATA....

Nilisikia maelezo yale yalikuwa hayajaachana sana na ya mke wangu nikaamua kudili na mambo mengine ya maana.

Asubuhi saa kumi na moja nilikuwa bafuni nikitimiza masharti ya ile dawa, Ndiyo.

Ilinilazimu kufanya hivyo wengi wape .

Nikamaliza Kila kitu kikawa poa kabisa ,

Nilishinda pale kutwa nzima huku mama akinambia anahitaji kuondoka mkoani, lakini nikwambia abaki kwanza kwa sababu ambazo nilizijua Mimi.

Sasa mwanangu hali yako unaijua huna kazi ya maana , familia ishakuwa kubwa wote sisi tunakuangalia wewe huoni kama tutakuongezea mzigo?

Nilicheka kwa kuguna,

Halafu mume wangu unajua mama kama alikuja na mahindi hapa yapo stoo kule hata hatujasaga . Sikutaka kusimuliwa nikainuka nikazama mpaka stoo nikaona Kuna karibu debe nne za mahindi na maharage nilicheka kwa kumuhurumia mama na familia yangu,

Nilitulia huku machozi yakinilenga bila kujijua,

Kwahiyo ye mama baada ya kusikia Kuna matatizo huku akaona abebe na Chakula kabisa masikini.

Kweli UPENDO wa kweli hutoka kwa mama,

Wabarikiwe akina MAMA wote.

Nilitoka nje nikaungane nao ,

Mume wangu hayo machozi ya Nini Tena,? Mke wangu aliuliza.

Labda vumbi za huko stoo nilikotoka lakini ukweli niliujua mwenyewe huku mke wangu akinifuta machozi kwa kanga yake

MAMA, niliita, akaniitika

Niwe mkweli nashukuru kwa msaada wenu wote kwenye hii familia Kila mmoja amecheza vizuri sana kwenye nafasi yake, lakini niwaahidi tu kuwa nitajitahidi kufuata ushauri wenu , kuliko kuliko kuziishi falsafa zangu ambazo zimeniumiza kwa namna nyingi, naahidi kuwa mwaminifu na MUNGU awape maisha marefu.

Aminaaa, waliitikia kwa pamoja huku huku Kila mmoja akitabasamu kwa furaha.

Lakini mama, mmekuja na mizigo mingi ya vyakula, lakini Mimi Sina njaa ndogo ndogo hata mkae hapa mwaka mzima kutakuwa na shida zingine tu lakini siyo Chakula.

Hapana mwanangu, hatutoi kitu au zawadi kwa mtu kwakuwa ana shida, Bali tunatoa kwa UPENDO tu, Wala hakuna shida , hata wewe siku pitia dukani nunua hata miwani ya elfu mbili tu, najua maboss wengi wanapenda miwani,

Mpelekee mfanyie kama saprazi, atafurahi sana, anaweza kujaribu kuivaa hata mbele yako. Kitendo Cha kuivaa tayari mtakuwa mmebadilishana UPENDO.

Kumbuka anaweza asiivae kwasababu labda anayo ya gharama zaidi au anavaa iliyopimwa, lakini kikubwa umempa.

Japo zingatia aina ya watu, mtu mwingine unaweza kufanya naye kazi Hana nyota na wewe siku ukimpa zawadi yoyote , utaonekana unataka kumroga na kujikuta unapoteza kazi yako.

Nilimwelewa sana MAMA.

Hata hivyo Dani una hela gani wewe familia yenyewe naiona inavyoongezeka, alisema hayo huku akisimama na kuondoka

Tuliangaliana Mimi na mke wangu tukacheka,

Aliendelea kufanya kazi mbalimbali pale home huku akiwa kaipendezesha nyumba kwa kulima majani yote yaliyoizunguka nyumba nilifurahi sana. Masaa yalikatika hamu ya kwenda kuripoti ofisi mpya huku wakinihakikishia ajira ya maana zilinitia hamu, taratiiiibu nikaanza kusahau yaliyopita, kitu pekee kilichoongezeka ni kwamba safari nilikuwa nakula kama mchwa yaani njaa Kila saa naisikia.

Nikiwa nimetulia nilipokea simu kutoka kwa bosi wa kiume huku nikigundua huenda hajarudi nchini maana namba ilikuwa na code za South Africa , ni simu nilizitegemea lazima zitapigwa kama siyo yeye basi mkewe, au yeyote kwenye ile kampuni,

Nikaipokea nikaiweka sikioni.

Hujambo mwanangu,

Ilisikika sauti toka upande wa pili, nikamjibu kwa heshima zote.

Akaendelea..

Najua Kila kilichotokea kwa upande wako, hata hivyo hakuna haja ya kunieleza chochote badala yake urudi kazini, sawa mwanangu?

Aliongea kwa kuweka kituo, nikamjibu, lakini Mimi naumwa nipo hospital kwahiyo nikiwa sawa nitakuja tu boss wangu,

Akanijibu sawa.

Sikuwa naumwa, nilidanganya nilitaka kujipa nafasi ya kwenda kwenye kampuni mpya ambayo, niliona kabisa Ina masilahi kwangu

Wakati nikiwaza hayo. Simu iliita tena Safari ni mke wa boss, nikaipokea

Bila hata salamu, akauliza

Uko wapi tulo upo wapi mwanangu aliongea kwa sauti ya chini bila breki,

Upo hospital gani nije kukuona mwanangu.

Nikamjibu kuwa nipo mbali ni nje ya jiji hata hivyo asijali nipo sawa tu.

Basi Kama una mtu mwaminifu unaweza kumtuma aje huku Kuna bakshishi yako, itakusaidia tolu.

Anapenda sana kuniita tulo/tall kwakuwa Mimi ni mrefu lakini pia Kuna akina Daniel watatu kwenye kampuni huku Kila mmoja aliitwa kwa namna yake ili tuwe tunatambulika haraka.

Halafu huyu boss naye kuniita mwanangu ana maana gani wakati fulani akisherehekea sikukuu yake ya kuzaliwa si niligundua nimempita mwaka mmoja?

Najua anamuiga mumewe, kwakuwa huwa ananiita hivyo hata hivyo siyo mbaya kwakuwa anaishi na mzee si mbaya akatuita wanae.

Niliwaza sana kuwa hii kampuni siitaki hata kuisikia, ni kiburi baada ya kuwa Nina mchongo mwingine.

Laiti ningejua,

Nilikaa pale huku nikiwa jikoni nikiwahimiza dada yangu na yule dada wa kazi kuwa mbona mpaka muda huu chakula bado.

Walinishangaa sana jinsi navyopenda kula siku hizo,

Wakati naendelea kutizama maeneo kuzunguka nyumba yangu huku nikipiga hesabu pindi nikiianza kazi kitu Cha kwanza ni kuanza na fence,..

Ndiyo, ilikuwa kipaumbele baada ya nyumbani kwangu kugeuka kilabu Cha pombe mtu anakuja kama kilabuni, Kuna wale wavuta bangi waliokuwa wanaitaka TV si nilishtuka Hawa hapa uwanjani, pia shedy si nasikia alijitapa kabisa hii nyumba kaisimamia yeye, yote haya ni kukosa fence nitaweka bonge la geti na nitafuga na mbwa.

Nilisema kwa uchungu na hasira nikikumbuka namna Shedy alivyokula hela zangu baada ya kumpa tenda aniletee mawe na tofali, kwakuwa sikuwa na ujuzi na tripu za mawe, mchanga, na tofali nikajikuta natumia hela nyingi sana namshukuru fundi ujenzi ambaye tulikaa chini akanipa bei za Kila kitu, kumbe ilikuwa very cheap yaani, lakini sikusema kitu kwake baada ya kugundua yeye huwa ana tamaa za kidalali mpaka kwa washkaji zake eti,

Lakini Leo hii anajitapa eti Nini kum.......... Nilitukana kimoyomoyo

Wakati nikiwaza hayo, alipita ESTA. Akakaribishwa vizuri na mke wangu Huku akidai alikuja kutupa pole.

Dah pole sana shemeji yangu, aliongea huku nikiwaza wanawake bwana kama nisingefahamishwa na mke wangu juu ya shida yake ningeshalala naye.

Sasa shemu vipi kuhusu kazi,hujarudi kazini, aliuliza ESTA

Aaaaaa pale Mimi mwenyewe walivyonidharau na kunisumbua, siko radhi mume wangu arudi pale, alisisitiza mke wangu.

Hapana shemu usijali Kuna kampuni fulani(nikaitaja jina)watu wake walikuja mpaka nyumbani wakidai wananihitaji hata hivyo ni kesho tu natakiwa nikaripoti .Niliongea kwa majigambo

Weeee shemu, unajua kuwa hiyo kampuni ni ya yule boss wako huyu huyu, mi naijua

Yaani hii ya Sasa hivi uliyokuwa unafanya kazi ni kampuni mtoto wa ile, hii inaongozwa na mke mdogo wa boss, halafu hiyo ambayo inakuhitaji inaongozwa na mtoto waboss,

Ni hivi huyo boss wako makazi yake ni south Africa anakoishi mke mkubwa , huyo unayemuita ni boss wako wa kike alikuwa mfanyakazi kwenye kampuni ya kwanza. Akaolewa na boss na kupewa asimamie hii ya sasa,

Alimalizia ESTA.

Nikagundua ndiyo maana wale mafundi wa pale huwa wananiambia na kunitambia kuwa wao wanahudumia kampuni mbili,

ESTA akaendelea....

Na huyo boss wako wa kike ni msimamizi tu bado watoto wa mwenye Mali ndiyo wamiliki sema Mara nyingi hawakai hapa Tanzania.

Sikumpinga ESTA kwakuwa ni moja kati ya madada wa mjini wanaojua vitu vingi, Mimi natoka mkoani naingia kwenye huu mji najiunga kwenye kanisa moja maarufu hapa mjini, namuona ESTA ni mtu ambaya kwake kulishakucha zamani wakati si wengine ndiyo tunazisaka ajira.

Hivyo sikushangaa yeye kujua mambo mengi, aliaga na kuondoka pale nyumbani huku Mimi na mke wangu tukiwa na maswali mengi tukihisi tunategwa.

Sasa itakuwaje, usichoke bado mbichi,

Simulizi inaitwa

Mimi na boss wangu.

Unataka kujua ni boss gani,

Wakiume au wakike.

Itaendelea.................
 
Samahani wakuu,
Kwa wale wafuatiliaji wa mkasa wangu ni kwamba.

1.Sijalazimishwa na mtu kuleta hiki kisa hapa

2.Sitaongozwa Wala kuamrishwa na mtu namna na muda wa kupost.

3.Sitalazimika kufupisha stori kisa Kuna mtu inamchosha.pia Sina muda maalumu wa kuileta hapa

4.kuna simulizi chungu mzima humu jamiiforum zimeandikwa na waandishi mahiri,waweza kujikita zaidi huko

5.hiki siyo kisa cha kufikirika,ni kisa cha kweli hivyo stori italetwa kama ilivyo.

6Mimi si mwandishi mzuri,tusameheane pale yanapojitokeza makosa, typing error n.k
 
Samahani wakuu,
Kwa wale wafuatiliaji wa mkasa wangu ni kwamba.

1.Sijalazimishwa na mtu kuleta hiki kisa hapa

2.Sitaongozwa Wala kuamrishwa na mtu namna na muda wa kupost.

3.Sitalazimika kufupisha stori kisa Kuna mtu inamchosha.pia Sina muda maalumu wa kuileta hapa

4.kuna simulizi chungu mzima humu jamiiforum zimeandikwa na waandishi mahiri,waweza kujikita zaidi huko

5.hiki siyo kisa cha kufikirika,ni kisa cha kweli hivyo stori italetwa kama ilivyo.

6Mimi si mwandishi mzuri,tusameheane pale yanapojitokeza makosa, typing error n.k
Poa man tumekupata
 
Samahani wakuu,
Kwa wale wafuatiliaji wa mkasa wangu ni kwamba.

1.Sijalazimishwa na mtu kuleta hiki kisa hapa

2.Sitaongozwa Wala kuamrishwa na mtu namna na muda wa kupost.

3.Sitalazimika kufupisha stori kisa Kuna mtu inamchosha.pia Sina muda maalumu wa kuileta hapa

4.kuna simulizi chungu mzima humu jamiiforum zimeandikwa na waandishi mahiri,waweza kujikita zaidi huko

5.hiki siyo kisa cha kufikirika,ni kisa cha kweli hivyo stori italetwa kama ilivyo.

6Mimi si mwandishi mzuri,tusameheane pale yanapojitokeza makosa, typing error n.k
na tilia mkazo hata ukiileta kisa kingne mwakan bdo tutkisubria kwa hamu
usiwe na hark taratibu mwandish
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom