Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Simulizi: Mimi na Boss Wangu

Handle your feelings,do something else ujisahaulishe na hii ataileta kwa right time for him and convenience, kasome Ile mash marrow experiments.tangiapo akimaliza ndani ya Wiki ama siku tatu utakuwa umeshasahau huu utamu unakupelekesha.just have handle with your limbic brain system
Jack Daniel
Mzee baba tuokoe na hii alosto
 
Poa poa mkuu. Umenifunza jambo. I am sorry ndugu yangu nimefuta. Peace kaka mkubwa
Hongera mkuu.
Napenda sana mtu anayekiri kakosea ili maisha yaendelee. Tumezaliwa, tunaishi na tutakufa.

Hapa katikati kwenye maisha Kuna mengi sana ya kuyazingatia ili tu uishi vizuri na walimwengu.

Jitahidi sana ukikasirika usiropoke neno, litakuponza baadaye.

Hata ukifurahi sana, usiahidi chochote, maana wapo waliofurahishwa na mambo fulani wakajikuta wanaropoka na kuahidi vilivyo nje ya uwezo wao.
 
SEHEMU INAYOFUATA........

Niliipokea simu ya Shedy, na kuiweka sikioni,

Halo kaka u mzima, pole na matatizo, lakini ni kwamba naomba tuonane, chonde chonde kaka ni mazungumzo na wewe

Aliongea bila kunipa nafasi Wala sikumjibu kitu.

Ila huyu ananitafuta Tena ananitafuta haswa, nilijitahidi kutokuonesha dalili za unyonge huku nikirudi kwenye kikao chetu na kuwaaga Mama, mke wangu kuwa najipumzisha ndani kidogo,

Mama akaniambia nipumzike ila muda kidogo ana mazungumzo na mimi.

Niliingia chumbani nikiwa kwenye PC yangu na search vitu mbalimbali ambavyo pengine sikuwa na vielewa kutokana na mawazo kuhusu tabia aliyoionesha Shedy.

Ni rafiki yangu, tuna historia nzuri tangu utotonj, tumeshirikiana mambo mengi,

Ni mdogo kwangu nikiwa nimemzidi miaka minne, kipindi nasoma shule fulani ya seminary kule mkoani kipindi wazazi wakiwa wamelenga niwe padri, niliishindwa ile shule nikiwa form three,

Nikarudi nyumbani hapa nikatafutiwa shule nyingine ya kawaida ya serikali nikaanza kidato Cha kwanza upya tukiwa na Shedy, nilikuwa nafanya vizuri sana kwenye masomo ukizingatia from form three to form one, nilitesa sana huku nikipata marafiki wengi kulingana na kuonekana genius.

Kama ni suala la mademu ilikuwa rahisi sana kiasi Cha Kila mtu kunitaka nimtafutie demu,

Lakini rafiki wa kweli alikuwa Shedy, kwanza hakuwa na akili kivile, halafu alikuwa mvivu sana, hali iliyopelekea niwe nakuwa naye sambamba kwenye discussion mbalimbali.

Kubwa aliloliweza pale shuleni ni biashara alikuwa anauza vitu huku vidogo vidogo Kama vyakula akakuza mtaji wake Hadi kufikia kuuza madaftari ambayo yalikuwa adimu sana kuanzia mtaani Hadi shuleni lakini yeye alikuwa nayo

Nakumbuka aliwahi kupewa kichapo toka kwa wanafunzi wa form six baada ya kuwapelekea mzigo fulani na wao kwa ubabe wakata kumdhulumu dogo akawa hajakubali wakampa kichapo , kama si Mimi niliyemuamulia sijui ingekuwaje.

Familia yangu ilikuwa ya kanisani, kwahiyo Kila jumapili hakuna aliyekosa kwenda kanisani huku mshua akinihimiza zaidi Mimi labda kwakuwa nilikuwa mtoto pekee wa kiume,kwahiyo nilichungwa kiaina

Na Mimi nikaona isiwe tabu nitakuwa naenda na Shedy kanisani ,kwa Mara ya kwanza Shedy anaingia kanisani aligundua fursa kibao hasa biashara zinazoendelea kule nje,miwa,na vitu vingine kibao.

Ikawa jumapili iliyofuata alikuwa na mazaga kibao ,asitambue kwanza hairuhusiwi
Lakini yeye alikomaa licha ya kupigwa mkwara lakini akawa anauza kwa Siri.

Nakumbuka tukiwa form four ,ile ya zamani siyo ya Sasa bado watoto
Nilienda nyumbani kwao nikamkuta ana baiskeli mbili aina ya swala .

Akinambia Kuna mzee mmoja kampa amuuzie kwakuwa yule mzee alistaafu kazi yake ya udaktari akaamua kuuza baadhi ya vitu ili aende kwao, lakini kabla Shedy hajauza yule mzee aliondoka na familia yake , hatukuwaona Tena.

siku si nyingi baiskeli zikauzwa na hakukuwa na simu kwamba angewapa taarifa kwaiyo ikawa imekula kwao, nakumbuka alikuwa na vijihela kiasi Cha kumzalisha mmoja wa mabinti pale kijijini kwetu
Ambaye ndiye mke wake Hadi leo

Mitihani ilikaribia, wakufaulu tulifaulu tukaendelea mbele ya safari huku Mimi nikimfurahisha sana baba yangu mkubwa aliyeko huku mjini kiasi Cha kunitafutia shule nzuri kiasi chake tofauti na kayumba za mkoani,

Nikaachana na Shedy kwa kipindi kirefu kwakuwa yeye alifeli

Cha ajabu tukakutana hapa mjini nikiwa form six yeye akiwa kajikita zaidi kwenye vijibiashara ambapo kwanza nilikuwa namuonea huruma sana nilimuona akiteseka tu

Lakini MUNGU si mwanadamu, alianza kung'ara huku mtaji wake ukikua huku Mimi nikiendelea na Elimu ya juu,

Alikuwa wa kwanza kuoa baada yakujiona mambo yake safi akaamua kumfuata mwanamke aliyemzalishaga huko mkoani, ilafungwa ndoa safi ya kanisani huku Mimi nikijitoa kwa asilimia Themanini kuhakikisha Kila kitu kipo sawa,

Na nilikuwa mmoja wa viongozi wa moja ya makanisa ya hapa mjini kulingana na historia yetu kuwa watu wa kanisa,

Maisha yaliendelea nikawa natafuta kazi Sasa, ili na Mimi niwe kwenye ramani ya maisha nikafanikiwa kupata kazi ya kumuendesha boss fulani wa kiarabu.

Kutokana na kuwa sikuwa na familia hela niliyokuwa nalipwa ilitosha kufanya vitu vingi sana, huku nikijua kabisa lazima nitafute kazi ya heshima ili nikaitendee haki taaluma yangu

Tatizo tulilopishana na mwarabu yule ni udini, alilazimisha niingie msikitini wakati Mimi mkiristo niliyesimikwa licha ya ndugu zake kumshauri kuwa aachane na Mimi tufanye kazj iliyotuunganisha bado ye alikomaa kiasi Cha kuniahidi eti nitamuoa Binti fulani walikuwa wanakaa naye alikuwa shombeshombe fulani

Kama nisingekuwa na msimamo ningesilimishwa lakini nilivizia nikambandua yule Binti Kisha nikaendelea na kazi zingine tuliachana na yule mzee baada ya kuumwa akapelekwa huko kwao

Nikatafuta kazi nyingine ya maana kabisa, nikirudi kwa Shedy ni kwamba ni rafiki yangu wa kitambo ila sasa aliyakanyaga hayawani yule.

Kwahiyo yeye kuwa na hela na magari ndiyo aje kumtongoza mke wangu,?

Usikute alifanikisha analotaka sema labda tu mke wangu anajitetea Lakini sipaswi kumhukumu mke wangu Hawa wanawake ni dhaifu sana
Yaani kukaa wiki mbili tu ndani rafiki yako wa damu anakuharibia kama ningekaa mwaka ndani,

Si angehamia kwangu kabisa.

Sema nitamkomesha ila napaswa kuwa makini kwakuwa naweza kuharibu nikaishia pabaya wakati wamenichokoza.

Sikutaka kukutana naye,

Mume wangu unawaza Nini taani unawaaaaaza baba Jack achana na hizo habari zimepita tuangalie mengine, aliongea mke wangu Huku akiwa anachagua nguo fulani toka kwenye kabati akidai zingine zinambana kwakuwa tumbo lilishakuwa kubwa,

Hivi ni miezi mingapi niliuliza

akajibu ni miezi sita, hata hivyo nimemuomba mama wifi abaki,

Hamna kwani si tunaye dada wa kazi Kila kitu kitakuwa poa wewe hao waache waende tu mkoani,

Mume wanguuuuuu, kwanza ungejua huyu dada wa kazi kanikera basi tu sema nilikuwa kwenye heka heka ya tatizo lako nikawa sijapata muda wa kumsema, na kwa Sasa Bora aende tu kwasababu Kuna siku nilikuwa natoka mjinj kwa bosi wako nikamkuta kamkaribisha Shedy mpaka ndani wakati nilishamkataza ni marufuku kuwakaribisha marafiki wa mume wangu Kama yeye hayupo. Lakini pia alipewa laki moja na Shedy eti itatusaidia mimi nilishajua lengo lake nikanwambia airudishe na sidhani kama kairudisha

Cha ajabu shemeji Shedy akawa anakataa kutoka nje mpaka nilipotishia kumuitia mjumbe ndiyo akatoka, kwanza ngoja nimwite dada wa kazi akuelezee

Na ukionana na Shedy ana alama au kidonda usoni Mimi ndiyo nilimpiga na kibao Cha Nazi baada ya kuwa mbishi hataki kutoka nyumbani kwangu,

Sikutaka kusubiri nikampigia simu tukutane baa fulani lakini siyo kwake nadhani alinielewa sikutaka kuonesha utofauti,

Tulikutana akiwa yupo na mkewe.

Kabla hata Shedy hajaanza kuongea ,
Mkewe akaanza kuwaka, kwanza shemeji pole na matatizo, wewe ni ndugu yetu tumetoka mkoa mmoja ila mkeo alichomfanyia mume wangu sikupenda Tena sijapenda haswaaa

Hebu mtazame, mume wangu si angemsababishia upofu,/ukilema

Nilimtuliza Kisha nikataka nimsikilize mwanaume mwenzangu.

Ujue braza Dani ilikuwaje,

Siku uliyopata matatizo wewe hakuna aliyejua upo wapi mkeo akawa na mashaka huku wivu ukimjaa akihisi labda upo kwa wanawake

Akanipigia simu nifanye upelelezi+kusaidia utafutwe ila baada ya masaa mawili alipiga simu mwenyewe kuwa kapata taarifa kuwa umeshikiliwa na maaskari baada ya wewe kupoteza mzigo hata hivyo , ila hakujua upo kituo gani

Hata hivyo mke wangu aliniruhusu nije nyumbani kwako, ili nipate kuzungumza naye kwa kina zaidi.

Je, ulimpigia simu kuwa unahitaji kuonana naye?

Niliuliza.

Hapana, nilitambua wazi ni namna gani shem alivyochanganyikiwa nikaona isiwe tabu ngoja nifike tu.

Kwani mume wangu si ulidai ulipiga simu, mkewe alimuhoji,

Ndiyo ila haikupatikana.

Nikanote kitu,.

Akaendelea

Nilipofika nyumbani kwako nilimkuta dada wa kazi akanikaribisha,

Ukaingia mpaka sebuleni, niliuliza

Hapana nilikuwa kwenye gari langu

Sawa halafu ikawaje,

Baada ya muda kidogo kama saa mbili usiku, shemu alirudi alifurahi kuniona tukaongea mawili matatu Cha ajabu sijui Nini kilimpata akaanza kunisukuma , eti nitoke nikashangaa Nini kimempata shemu matatizo yako yamemchanganya namna hii

Nilipojaribu kumtuliza alichukua kitu ambacho si kukijua nahisi ni chuma akanipiga nacho usoni nilikimbilia kwenye gari huko nikiwa naomba MUNGU nisije sababisha ajali maana damu zilikuwa zinavuja sana.

Ndiyo mimi nahisi yule mdogo wangu mimba inampeleka vibaya maana kama kuzaa wote tumezaa Tena ye ndo kwanza anatafuta mtoto wa pili watu wengine tunakaribia kuacha kabisa.

Hawezj kuniumizia mume wangu yule kujifanya kachanganyikiwa ili ionekane anakupenda sana au vipi

Mbona Mimi mume wangu na kazi zake za udalali huko mahabusu kukaa ni kama kwake lakini sijawahi kujifanya naumizwa kiuwendawazimu kama alivyofanya mkeo, Tena nikwambie shemu urafiki wako na mume wangu atakaye uwa ni mkeo wewe kabla hata hujaoa ulikuwa unakuja hapa tunakula, tunafurahi, lakini mnaenda kuachana na mume wangu kisa ni huyo mkeo nikwambie ukweli,

Aliongea yule mke wa Shedy kiukali kiasi Cha kufuta lipstick zake,

Lakini nilimtuliza huku, nikiwa njia panda Ina maana mke wangu alinidanganya, au kweli mimba yake inampa hasira, niliwaza moyoni.

Nikauliza, lakini Shedy wewe laki moja mke wangu ulitaka kumpa ya Nini?

Tena ulimpa dada wa kazi ili aifikishe kwa boss wake,

Haaa Mimi nilikuwa namsaidia tu, alijibu,

Weewe mume wangu, we siku ile nilikuomba elfu thelathini tu niongezee nipeleke kwenye marejesho ukadai hauna, hiyo laki uliitoa huko ya Nini?

Haya tufanye una huruma sana, mbona hukunishirikisha kama ambavyo tulishauriana mambo mengine, alifoka mke wajamaa

Ambaye ana mdomo sana na namjua suku nyingi.

Tena Mimi kifupi niwe mkweli mke wangu ndo akaunti yangu ndogo ukiacha akaunti zingine,
Hela ya kula tu mpaka Mimi napata matatizo alikuwa na zaidi ya milioni tatu, niliongea kwa ukali kidogo baada ya kunote jambo lingine.

Unajua mume wangu sikuelewi, aling'aka mke wa jamaa.


Itaendelea........
Ndio ndio
 
SEHEMU INAYOFUATA...........

Nilitulia ofisini huku tayari nikiwa nimevurugwa si kidogo,

Sasa itakuwaje kumbe yule dogo ana ukaribu na madam, Sasa hospital tenaaaaa..... Nilipanga na kupangua huku nikishindwa kupata jibu kamili, hata muda wa lunch ulipofika sikuweza hata kula maana tayari nilikuwa na hofu kubwa.

Niliomba ruhusa ya masaa mawili ili nielekee hospital ya taifa ambako niliambiwa na MADAM tukutane,
Nilipofika nilikuta baadhi ya ndugu wa yule kijana, wakiwa naye nje kabisa tayari kwa kuondoka naye, nilichogundua ni kwamba dogo Wala hakuumia lengo ilikuwa anitengenezee msala.

Niliwasalimia wote huku wengine wakiitikia kwa sauti ya chini, lakini Kuna mama mmoja alianza kunitolea lugha chafu.,

Yaani umeshindwa kumuua jana, ukasikia bado yuko hai na anapumua ukaona Bora uje ummalizie kabisa,
Haya muue huyo hapo. Fanya lolote mwanaume wewe. alibwata sana yule mama huku kama mjuavyo umati kwenye ile hospital nikaona Bora niondoke tu, wakati najiandaa, kutoka nilidakwa na maaskari waliovaa kiraia huku vitambulisho vyao vikiniaminisha.

Hivi kumbe ni huyu jamaa, mbona hata hafanani na kupiga mtu , ujue kidogo nibishe yaani Wala huwezi kumdhania,

alikuwa ni afande mmoja ambaye alikuwa akimuuliza mwenzake kama ni Mimi.

Sasa bwana Daniel, tunaomba utwambie tairi za gari ya jamaa ulipeleka wapi, maana tulichogundua ni kwamba Kuna watu uliwapanga mje mmvamie dogo, halafu mkamwibia, maana wakati wewe ukimburuza Kuna vijana uliwaandaa kwaajili ya kukamilisha mpango wenu, haya tuambie vifaa viko wapi.
aliuliza afande aliyekuwa anaendesha gari ndogo hivi vi crown.

Kwa uzoefu wangu sijawahi kuulizwa maswali njiani nyie tufike kituoni Kisha mengine yatafuata, niliwajibu kijeuri huku simu yangu ambayo tayari waliichukua wao, ikaita.

Afande Ommy, hii simu ya hiri jambazi inaita huenda ni majambazi wenzie wanampigia, alisema Afande ambaye tulikaa siti za nyuma Mimi na yeye, kucheck jina la mpigaji ni Rose, aisee moyo ukiniuma sana

Yule afande akapokea simu huku akiweka loud speaker na kuniamrisha niongee.............

Hello my vipi tena, nasikia Kuna maaskari wamekuja hapo ofisini kwako wakikuulizia, inaonekana hawana Nia njema na wewe , kwani Kuna Nini kimetokea , unaniumiza ujue, aliongea Rose bila hata salamu.

Tayari wameshani arrest ila tutaongea, baada ya kugundua Niko nao akakata simu.

Huyu unamwitaje kwanza maana anavyoongea ni kama mke wako, na ulivyomsevu ni tofauti.

Atakuwa ni malaya wake tu huyo, au anashirikiana naye kwenye wizi, waliongea kwa kupokezana wale maafande huku wakiwa wameniudhi pakubwa.

Hatimaye tulifika kituo fulani ambacho sikujua kwanini wamechagua kituo kile, tulishuka kwenye Lile gari huku ukali wa majamaa ukiongezeka (Wana sifa Hawa maaskari basi tu)

Kushuka nilimkuta MADAM akiwa na wapambe kadhaa , pamoja na wale ambao niliwaacha hospital pamoja na yule kijana niliyempiga, nikagundua kumbe ndiyo maana walikuwa wananizungusha lengo lilikuwa Hawa watangulie kufika.

Haya vua mkanda, vua viatu halafu una viatu vya gharama kweli, ulivipiga wapi maana we una mbinu sana kwenye kuiba. aliongea yule afande niliye sikia akiitwa Ommy, au Omari

Hapana naomba nimsikilize kwanza akiongea upuuzi namwacha hapa hapa , aliongea madam ambaye kwa uzito wake anaheshimika sana kwahiyo akasikilizwa,.

Enhee hebu tuambie ilikuwaje maana Mimi ninavyokujua nimeshangaa, tumefanya mambo mangapi wewe tolu, Hadi imefikia tunaishi kirafiki sana , kwanini ulimpiga huyu mtoto sisemi kwakuwa yupo na Mimi, ni kwamba hata angekuwa mtu hapaswi kujichukulia Sheria mkononi.
aliweka kituo.

Kwanza samahani madam kwa usumbufu wote, lakini pili nikushukuru kwa kuweza kunipa nafasi ya kusikilizwa Kabla sijawekwa lockup, story iko hivi.. nikawasimulia yote kuanzia uwepo wa dada yangu Hadi anauzoea mji na kuanza kurubuniwa sisemi kwamba lilikuwa ni kosa dada yangu kuwa na mwanaume tatizo ni utaratibu uliotumika,

Kama huyu kijana angekuwa anamtaka Dada yangu kiheshima yasingetokea yote haya...
. Kabla sijamaliza

Lakini wewe jamaa unasema Dada yako aliaga anaenda mkoani ila yeye Ndiye akaenda kwa huyu jamaa hivyo Mimi sioni kosa lake huyu, kifupi alifuatwa mwenyewe, aliongea mmoja wa maaskari akimtetea yule dogo kwamba Hana kosa.

Kipande hiki madam alikielewa sana, inaonekana alivyoelezwa ni tofauti na maelezo yangu.

Ni kweli ulikuwa na mwanamke kwa kipindi Cha wiki nzima, aliuliza MADAM akimgeukia yule Dogo.
Akajibu kwa kutingisha kichwa.

Jamani ndugu zangu naombeni Hawa niwasuluhishe mwenyewe, maana wote wapo upande wangu maana mzizi nimeshaupata , alizungumza madam, akiwaambia wale maaskari.

Sasa mama sisi tumeshamuweka kwenye detension , kuhusu shambulio na wizi wa vifaa vya gari la mlalamikaji, Sasa unavyosema utamaliza mwenyewe naona si vizuri maana, kweli inaonekana bwana Daniel alikasirika kuhusu dada yake, lakini swali, kwanini achukue sheria mkononi? Huoni hii ni jinai mama, aliongea afande Fulani ambaye alikuwa na cheo Cha koplo Huku akijichekesha chekesha kwa kumuogopa Mama.

Hapana afande naomba nieleweke hivyo, aliongeza MADAM Kisha tukaondoka.

Safari iliishia kwenye mgahawa Mmoja Huku tukifika kwa mafungu maana wengine walipanda daladala kwakuwa gari ya MADAM ilitosha watu wachache, tulisuluhishana Huku ikionekana gari ya dogo walifungua ni wale marafiki zake, lengo siyo wamuibie lengo wanizidishie kosa, kwa hiyo ikaonekana wazi tairi zote zipo hivyo Madam akaamrisha zikarudishiwe .

Tuliagana huku madam akinionya sana, kuhusu kudhibiti hasira zangu akidai tungekuwa hatujuani mimi na yeye tungeongea mengine.na pia kama yatajirudia ataweka ujuwani pembeni

Nilifurahi yale matatizo kuisha huku nikitazama saa ikionekana ni saa tatu usiku, nikampigia mke wangu ambaye huwa anakereka sana kuhusu kurudi usiku.huku nikimsimulia kwa kifupi mkasa wangu.

Nilifika nyumbani, siku hiyo nikipokelewa vizuri sana na mke wangu, licha ya kuwa alikuwa bado kanuna kutokana na vibao nilivyomzaba Jana yake, lakini kusikia nilikuwa polisi, alihuzunika sana,.

Yaani Leo mke wangu, kama asingekuwa yule boss wangu, mngesikia Niko mahabusu, yaani mbona ingekuwa balaa.

Mmmh mume wangu ujue nafsi yako tayari imejenga urafiki na vituo vya polisi, naiona hiyo evil spirit ikikuandama tayari, hebu jaribu kufanya hata maombi mume wangu Kuna roho si nzuri kwa upande wako, tatizo hata kanisani mume wangu umekuwa mvivu, lakini pia nilikuonya Jana kuwa unalotaka kufanya utapoteza haki hako bure tu.

Hebu fikiria baada ya kugundua kuwa dada yako yupo, sehemu fulani wewe ungeripoti polisi huku ukiwasaidia kuwajulisha mahali alipo mtuhumiwa huoni kama ingekuwa heko kwako yaani hao maaskari unaosema walikuwa wakikukejeli Leo pengine ungekuwa nao Jana mkimfuata huyo mtuhumiwa.

Pole sana mume wangu, ulinipiga Jana umeniumiza, ni mzazi nahitaji UPENDO na ukaribu wako, lakini bila kujiuliza Mimi ni nani ulirusha kibao hadi nilishangaa ni huyu huyu mume wangu kweli, ona Sasa yaani umeponea kwenye tundu la sindano sijui ingekuwaje, yaani Mimi tena na mtoto mgongoni, mahot pot na chupa za chai huku nikitafutiza wadhamini eti upate dhamana hivi unajisikiaje mume wangu!

Unanionea sana halafu mume wangu ni mpole, mcheshi mnyenyekevu yaani hata marafiki zangu Kuna muda wanakumwagia sifa Hadi naweka wivu lakini unaanza kubadilika mambo ambayo ulitakiwa kuyafanya ujanani unafanya ukubwani , si umechelewa tu kupata watoto wewe pengine ungekuwa na mjukuu. aliongea mke wangu huku nikiwa simpingi kwa lolote, aliongea kweli tupu, japo nilitamani niwajue hao marafiki zake wanaonimwagia sifa.maana nilishakuwa wa moto.

Kesho asubuhi ya Jumanne nilipiga suit fulani ya kijivu huku nikipiga tai fulani , hata nilivyopanda kwenye daladala Baadhi ya abiria wasiowavumilivu wakasema hata wewe kiongozi unapanda humu , au unaigiza movie.

Nilishuka huku nikisindikizwa na kejeli, mnamuona Boss eti sababu kavaa hiyo suti Hawa ni matapeli wa mjini huenda, hata anapolala hapajulikani, wengine wakiniita Yahya wakifananisha alivyoimba Lady Jay Dee, walimwengu bwana.

Nilifika ofisini huku, yule dada ambaye niko naye ofisini akinishangaa,

Mr, yaani hata siamini Jana Kuna PT(yaani gari la polisi) lilikuja hapo nje waliingia ndani wakakukosa , yaani nilikosa amani kabisa, mbaya Zaidi sikuwa na salio nikupigie, ili nikustue , bahati nzuri Da Rose alinitafuta ikabidi nimuelekeze kuwa akupigie ili akustue kuwa unatafutwa,.

Lakini alinipa jibu kuwa umeshakamatwa, hatukuwa na namna Mr,. yaani ingekuwa huna mke tulipanga tukutafute tungejua tu upo kituo gani ila tulihofu tusijegongana na mke wako. tutasema sisi ni akina nani, alisema yule Binti.

Sasa na wewe , si mngekuja tu mnamwambia kuwa sisi tunafanya kazi ofisi Moja, kifupi ni heshima tu kwake kwani kungekuwa na ubaya gani, nilimtega .

Weweee mwenzangu hatungeweza sisi,. Aliongea yule Binti huku nikifikiria jambo kuwa kwani dada yake kashamwambia kuwa yuko karibu na Mimi, ila huwenda maana hata umri hawajaachana sana pengine huwa wanaambizana .
nilijisemea.

Halafu Mr Daniel uliwasiliana na Dada maana tangu jana hata leo asubuhi alinipigia, akiulizia maendeleo yako, hebu mtafute mtoe hofu basi, aliongea yule Binti almaarufu kwa jina la Janet. ni la Binti Fulani kana nyodo sana na utoto mwingi sana , hata waliomleta kwenye ofisi yangu walilenga apate uzoefu fulani.

Nikapiga simu baada ya kuona nishafanya setup ya mambo yangu.

Haloo my, habari za asubuhi. nilimsabahi kwa uchangamfu Rose.

Hata siamini kama ni wewe haya nambie imekuwaje, aliuliza

Nilimwambia mwanzo mwisho huku nikimdanganya kwa asilimia tisini , sikutaka ajue mambo yangu hasa suala la kumpiga mtu maana ningejishushia heshima yangu.

Basi Sawa , usiku wa jana nilikuwa zamu hata hivyo leo niko free tunaweza kuonana baada ya kazi ili nikupe pole? aliongea Rose

Huku mwili ukinisisimka kutokana na ile kauli niliyoambiwa,

Haina shida Haina shida, nilimkatisha ili mdogo wake asielewe mambo yetu,
Nilipiga kazi huku Kila saa nikimuwaza Rose, namna atakavyonipa pole kutokana na misukosuko ya jana iliyonipata.
Kiufupi Rose alishanipenda tayari.

Siyo kupendwa bure lakini, ni kwamba Mimi ni mhongaji mzuri nikiwa nazo , hizi miatatu mianne kwangu kawaida.

Mida fulani ya mchana nilipokea simu toka kwa mke wangu, akiniagiza vitu fulani,

Sasa mume wangu, Leo uwahi kidogo Nina mazungumzo na wewe , lakini pia Kuna muda ESTA alinipigia simu eti ana mazungumzo na Mimi, hata sijui anataka kuongea Nini na miye nilitaka anipe hata utangulizi kidogo ila kadai atakuja hapa hapa, alimalizia Mke wangu.

Nilikauka kama nimepigwa electric shock maana baridi si baridi na joto si joto, sikumjibu kitu mke wangu.

Nikakata simu yake ili nimpigie ESTA huku nikiwa nusu kwa nusu nimchane kuwa ole wake nisikie kile alichokiona siku ile, au nimtongoze, yaani nimwambie tukutane somewhere, sikuweza kuopt kitu muda ule. Nilikuwa njia panda.

Itaendelea.............................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom